Home


  • Namba Zetu Za Malipo

    Namba za malipo ya vitabu:

    Namba za lipa

    TIGO PESA: 19016638 Jina ni SONGAMBELE CONSULTANTS

    M-PESA: 5564517 jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

    Namba za kawaida

    AIRTEL MONEY: 0684408755
    TIGO PESA: 0655 848 392
    M-PESA: 0745 848 395

    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    NB: Kama namba ya malipo anatumiwa mtu ambaye yuko nje ya nchi. Iandikwe Kwa kuanza na +255

    Kwa hiyo namba zinazotumwa nje ya nchi zitakuwa
    Airtel money: +255 684 408 755
    TIGO PESA: +255 655 848 392
    M-PESA: +255 745 848 395

    KOTE Jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Kama malipo yatakuwa yanafanyika kupitia benki.

    Yafanyie kupitia

    1. CRDB BANK: 0150770710200
    2. NMB BANK: 22110047274

    Kote jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

  • Wasiliana na Godius Rweyongeza Sasa

    Habari yafuatayo ni mawasiliano Unayoweza kutumia kumpata GODIUS RWEYONGEZA

    Simu: +255 (0) 684408755

    Whatsap: +255 (0) 755848391

    Email: songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu vyake wasiliana Moja kwa Moja na +255 (0) 684408755 (more…)

  • Fedha Chanzo Chake Ni Thamani

    Wachezaji Lionel Messi na Ronaldo wanacheza dakika 90 uwanjani na wanalipwa kiasi kikubwa Cha fedha kuliko wachezaji wengine.

    Unadhani kwa nini wanalipwaa kiasi kikubwa hivyo? Ni kwa sababu ya thamani yao wanayotoa.

    Kitu chenye thamani kubwa kinauzwa kwa bei kubwa ukilinganisha na kitu chenye thamani ya ndogo.

    Kama unataka kupata fedha basi unapaswa kuwa tayari kutoa thamani kwa watu.

    Labda unajiuliza, thamani ni kitu gani? Na Mimi nawezaje kuongeza thamani kwa watu.

    Iko hivi, ebu chukulia sasa hivi umetoka nje na umekutana na sura ngeni mtaani kwako. Mgeni akakuuliza, naomba kujua kwa mzee Daudi. Na wewe Daudi unamjua ni mzee pale nyumba ya tatu kutoka UNAPOKAA.. ukasema ngoja nimpeleke huyu jamaa mpaka kwa mzee Daudi…

    Kwa upande wako unakuwa umetoa thamani…
    Huyu jamaa alikuwa na shida na na umemwonesha kwa mzee Daudi, na shida yake imeisha.

    Tungekuwa sehemu nyingine, basi ilibidi akulipe jero kwa kitendo cha kukuuliza kwa mzee Daudi ni wapi na buku ya kumwonesha kwa mzee Daudi….Hahah

    Ulivyomfikisha yule jamaa kwa mzee Daudi amefurahi, kuthibitishwa kwamba amepata thamani kutoka kwako.

    Hivyohivyo kwa fedha, fedha ni matokeo ya thamani unayotoa..

    Unataka watu wakulipe? Toa thamani..
    Ukitatua matatizo ya watu, unakuwa umetoa thamani.
    Ukisogeza huduma karibu yao, unakuwa umeongeza thamani.

    Kwa hiyo badala ya kukazana kuikimbiza fedha, kazana kutoa thamani kwanza. Fedha itakuja tu.

    Sijui umenielewa….

    Kama umenielewa kaangalie video hii YouTube kwanza, Kisha SUBSCRIBE

    anyaway, tuendelee..

    Si umewahi kusikia habari za fuata nyuki ule asali. Unajua kwa Nini Watu wanawafuafa nyuki mbali na kuwa nyuki ni wakali..

    Kwa sababu nyuki wanatoa thamani kubwa kiasi hakuna MTU anayeweza kuitega mgongo.

    ukizalisha thamani nzuri watu watakuwa tayari kukufuata hata Kama upo kijijini. Kwani nyuki huwa tunawafuata wapi?

    Hakuna nyuki wenye mzinga Kariakoo… Mizinga yote ipo misituni Ila tunawafuata tu. Rafiki yangu, zalisha thamani…

    Bado tuko pamoja? Basi mpaka hapa Sina shaka utapendaa kitabu changu cha KUTOKA SIFURI MPAKA KILELENI. Kitabu hiki Ni 20,000 tu na unatumiwa popote ulipo duniani.

    wasiliana na 0755848391 kukipata.

    Umekuwa nami
    Godius Rweyongeza kutoka SONGAMBELE CONSULTANCY
    0755848391
    Morogoro-Tz

  • Fanya Yafuatayo Kuepuka Kuwa Miongoni mwa Walalamikaji

    Moja ya kitu rahisi sana ni kulalamika. Kila mtu anaweza kukifanya. Lakini kitu kigumu kufanya ni vitendo na kuonesha matokeo.

    Sasa siku ya leo, nataka uepukane na malalamishi ili mwisho wa siku uwe mtu wa kuleta matokeo ambayo wewe mwenyewe unayatamani

    Unajua kwa Nini Watu wanalalamika?

    Kwa sababu kuna matokeo mazuri wanayataka ila  wanataka mtu mwingine awasaidie kupata hayo matokeo. Kwa hiyo, wanataka MTU mwingine azalishe matokeo na siyo wao.

    Mtu anataka kupata afya njema, anawalaumu wazungu kwa kuleta vyakula vya makopo.

    Mtu anataka utajiri na fedha, anailaumu serikali kwa kutokutoa hela. Wakati fedha chanzo chake ni thamani.

    Sasa badala ya kulaumu, sikiliza. Kuwa mtu wa kuzalisha matokeo.

    Kwanza, kuwa na malengo ambayo unayafanyia kazi. Zama kwenye kufanyia kazi malengo yako na sahau Mambo mengine

    Pili, kabla ya kulaumu jiulize wewe umezalisha matokeo gani. Kila utakapojiuliza swali hili, utakuta kwamba unalazimika kukazana na malengo yako zaidi kuliko kulaumu MTU mwingine

    Tatu, fahamu kuwa maisha ni wajibu wako. Hakuna mtu mwingine ambaye anaweza kupiga push-up kwa ajili yako.

    Nne, usifuatilie maisha ya watu wengine. Kadiri unavyofuatilia maisha ya watu wengine, ndivyo unavyojinyima fursa ya kufanyia kazi malengo yako.

    Tano, Mara zote kuwa mtu wa kujifunza na kusoma vitabu. Jifunze , jifunze jifunze.

    Kila la kheri.

    Umekuwa nami
    Godius Rweyongeza kutoka SONGAMBELE CONSULTANCY
    0755848391
    Morogoro-Tz

  • Usikubali Kuendelea Kubaki Hivyo hivyo

    the simba mentality
  • Njia Mpya Ya Kutengeneza Utajiri Tanzania

    Kwa kila sekunde inayopita, mtandao wa google unapokea maombi 40,000. Hawa ni watu mbalimbali wanaotafuta majibu ya maswali yao kwenye mtandao huu.
     
    KWA NINI WATU WANATAFUTA MAJIBU GOOGLE?
    Moja ni kwa sababu majibu waliyonayo hayatoshelezi hivyo wanatafuta suluhisho jipya.

    Pili, kwa sababu hawajawahi kupata suluhisho la swali hilo kabisa maishani mwao. Hivyo njia pekee ni kukimbilia Google kuona kama kuna mtu ambaye anaweza kutoa suluhisho.

    SASA HILI LINA MAA GANI KWAKO?
    Hii maana yake kwamba, ukiweza kujibu swali moja tu kati ya hayo 40,000 ambayo yanaulizwa  kila sekunde basi utakuwa umeweza kuwasaidia watu kupata kile WANACHOTAKA.

    Na kumbuka kwamba, unaweza kupata kitu chochote unachotaka kama utawasaidia watu kupata kile WANACHOTAKA.

    Wewe, hapo ulipo umebeba majibu ya maswali ya baadhi ya watu. Kwa nini hutaki kuyatoa ili uwasaidie.

    Ebu chukua hatua leo uanze kujibu walau swali la mtu mmoja kuanzia siku hii ya leo.

    USIBANIE HAYO MAJIBU UMEPEWA WEWE KWA AJILI YANGU. Nisaidie mimi kujibu maswali yangu ili nikulipe.

    Asante Sana.

    Kitabu hicho unachokiona kwenye picha ni nakala tete (soft copy), na kinapatikana kwa 10,000 tu. Kichukue leo ili kikupe msingi wa kuanzisha kitu kitakachotoa majibu ya maswali ya watu.


    Lipia kwa nambari 0755848391 jina Godius Rweyongeza Kisha nitumie ujumbe wenye neno BIASHARA ili nikutumie kitabu

    Usisahau pia kuingia YouTube Leo na kuangalia video hii yenye masomo matatu ya kibiashara.

    Karibu sana

  • Leo ikiwa Ni siku ya Idd napenda kutoa ofa kwa mtu mmoja tu ambaye atajiunga na kozi yangu ya UANDISHI

    Eid Mubarak Kwako rafiki yangu

    Kozi ya kipekee ambayo inadumu kwa siku 30 Ina Mambo mengi ndani yake.

    Kwa kawaidaa gharama ya kozi hii huwa ni laki mbili (200,000). Ila kwa ofa ya leo. Mtu mmoja tu ambaye atalipia 120,000/- nitamuunganisha kwenye hii kozi.

    Ukiwa ndani ya hii kozi utapata

    • Utajifunza mbinu za kitabu chako kuanzia mwanzo mpaka mwisho
    • Nitakusimamia na kusoma kazi zako unazoandika kila siku na kukupa mrejesho wa kuziboresha
    • Nitakufungulia blogu ya bure.
    • Utajifunza mengi kutokana na yale wanayoandika wenzako na maoni nitakayokuwa natoa kuhusu kazi za wenzako.
    • Utapata kitabu Cha JINSI YA KUWA MWANDISHI MBOBEVU NDANI YA SIKU 30 bure.
    • Utapata jarida lenye hatua 15 za kufuata ili kuandika magazetini.
    • Utapata mafunzo ya audio zaidi ya 10. Yakiwemo mahojiano na waandishi wakubwa hapa nchini.

    Uko tayari?

    Basi wasiliana nami kwa 0755847391 Sasa hivi

    First come. First Served

    NB: hii ni nafasi ya kipekee ya kufundishwa uandishi, na kutimiza ndoto yako ya siku nyingi ya kuwa mwandishi.

    Wahi sasa hivi Tena bora ubonyeze HAPA TU KUWAHI KIKASHANI

  • MAISHA YA NYOTA TANO

    Leo nimesikiliza audiobook ya kitabu cha Oprah Winfrey. Nimejifunza mengi sana ila hapa kuna kimoja tu ambacho ningependa na wewe ukijue.
    Oprah anasema kwamba, unaweza kuishi maisha ya nyota tano hata   hauna pesa sasa. Sio lazima ulale kwenye hoteli zenye viyoyozi ndio uanze kuishi maisha ya aina hii. Ebu ona

    ukiamka asubuhi na mapema. Basi jipe nyota tano kwa ushindi huo.

    ukitoka nje ukavuta pumzi na kufanya tafakari pamoja na kunywa maji. Jipe nyota tano kwa kitu hicho kikubwa.

    Ukisoma kitabu, kurasa kadhaa, jipe nyota tano, maana hilo ni jambo kubwa.

    ukiwahi kazini, jipe nyota tano pia.

    ukimpigia ndugu, mke, mme, mzazi simu na mkaongea hadi mkacheka kiasi unasikia kichwa kama kinauma. hiyo ishara ya wewe kupata nyota tano kwenye hilo.

    Yaani kiufupi ni kwamba. Maisha ya kila siku ukiyaishi vizuri sana. Basi utakuwa unaishi maisha ya nyota tano.

    Bila shaka utakuwa umeona ilivyo rahisi kuishi maisha ya nyota tano.

    Je, wewe leo umeishi maisha ya nyota tano?

    Nashauri usome au usikilize audiobook ya kitabu hiki hapa. imebeba mambo mazito na muhimu kwa maisha yako.

    kila la kheri.

    Kitabu kinaitwa WHAT I KNOW FOR SURE.
    Mwandishi Oprah Winfrey

    makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.
    Tembelea pia www.songambeleblog.blogspot.com

    kuna makala nzuri mimeweka.

    kwenye youtube pia usikose kuangalia video hii. https://youtu.be/LrBROehGr64

    nyingine zaidi zinakuja.
    cha kufanya wewe SUBSCRIBE ili uwe wa kwanza kupata video hizi

    haya twende https://youtu.be/LrBROehGr64

  • VITENDO VIZIDI MANENO

    Dunia ina tabia ya kukupatia kitu kama utaonesha nia, kuwa wewe ungependa kupata hicho kitu. Huwa ninapenda kuwaambia watu kuwa, hata kama ni bahati itakukuta njiani unatembea wala sio chumbani kwako ukiwa umelala.

    Kwa hiyo, wewe kama unahitaji kupata bahati maishani mwako basi kuwa tayari kuweka kazi inayoendana na bahati unayotaka. Bahati unaitengeneza wewe mwenyewe na vitendo vyako ndivyo vinapaswa kuonesha hilo.

  • Leo najisikia kutoa ofa. Sema Toa Ofa basi 😂😂😂

    Hii ofa ni ya kipekee kwa ebooks zangu ambazo watu wanapenda sana.

    Ebooks hizi ni

    1. MITAJI 8 ILIYOKUZUNGUKA NA JINSI YA KUITUMIA
    2. KIPAJI NI DHAHABU: Jinsi ya kugundua, kunoa na kuendeleza Kipaji
    3. NGUVU YA WAZO (The power of an idea): How An Idea Can Change The World. Jinsi Wazo kinachoweza kubadili Dunia

    Thamani ya ebooks, hizi Ni kubwa Sana. Ila unajua Nini? Nataka nikupe wewe ofa ya kupata ebooks hizi kwa 12,000/- tu.

    Changamkia fursa hii ya kipekee sasa. Lipia kwa 0755848391 jina ni GODIUS RWEYONGEZA.

    BAADA YA HAPO UTANITUMIA UJUMBE ILI NIKUTUMIE EBOOKS HIZI.

    Karibu

    By
    Godius Rweyongeza
    www.songambele.co.tz
    0755848391

  • THE SIMBA MENTALITY

    Karibu sana kwenye makala ya leo. Ni makala ndefu kidogo. Kwa wale wasiopenda kusoma vitu virefu sana hii ya leo inaweza isiwe makala ya aina yako. Ila wale ambao wanapenda kuzama ndani na kujifunza vitu kwa kina vilivyotafitiwa na kutafitika, basi vuta kiti maana unachoenda kujifunza hapa ni kitu kikubwa sana.

    Kwa siku nyingi sana nimekuwa nikipanga kuandika makala yenye kichwa hiki cha The Simba Mentality. Nadhani mara ya kwanza kupata wazo la aina hii, ilikuwa kipindi nasoma wasifu wa Kobe Bryant, unaoitwa The Mamba Mentality.

    Kwenye wasifu huu, Kobe Brayant ameeleza safari yake kimichezo tokea akiwa shule ya upili (high school) mpaka anastaafu. Ni kitabu kizuri sana. na sote tunajua kwamba Kobe alishatangulia mbele ya haki, tangu mwaka 2020, hivyo, kitabu hiki, ndio kimebaki kama alama ya kumkumbuka na kujifunza kutoka kwake, sambamba na video na mafunzo kadhaa yanayozunguka mtandaoni. Unaweza kutazama video ya uchambuzi wa kitabu chake kwenye channel yangu ya youtube hapa chini. hakikisha umesubscribe pia.

    Nakumbuka mwanzoni nilipanga kabisa niandike kitabu kinachoitwa The Simba Mentality, ila sasa leo nimeona kwanza nikudoletee makala hii. Kama utaipenda, unaweza kuniambia niiongezee nyama zaidi, ili pengine nitengeneze kitabu.

    Siku siyo nyingi kwenye mtandao wa youtube nilikutana na video iliyokuwa ikiwaonesha simba waliokuwa njiani. Kilikuwa ni kikosi kikubwa cha Simba, ambao walilala katikati mwa barabara na hivyo, kusababisha magari yaliyokuwa yanatokea kila upande kukwama kwa muda, kila mwenye gari alijitahidi kupiga honi kadiri alivyoweza ili labda kuwaongopesha hawa wanyama na kuwafanya wasogee, ila hakuna mnayama hata mmoja ambaye alitoka.

    Sote tumewahi walau kisikia stori za simba. maana nikisema, sote tumewahi kumwona simba ana kwa ana, hapa tutaanza kutafutana., labda kumwona kwenye royal tour tu

    Simba ni mnyama wa mwituni ambaye pia anajulikana kama mfalme wa nyika. Anafahamika kwa ukali wake na uwezo wake maridadi wake kuwinda. Mpaka tulipokuwa wadogo tulikuwa tumamwimba,

    Tulikuwa tunaimba hivi

    KIONGOZI: Watoto wanguu ee

    WOTE: Ee

    Kiongozi: Mimi mama yenu

    WOTE: Ee

    Kiongozi: Sina nguvu tena

    WOTE: Ee

    Kiongozi: Za kuua simba

    WOTE: Ee

    Kiongozi: Simba ni mkali

    Wote: Eeh

    Kiongozi: Aliua mama,

    WOte: Ee

    Kiongozi: Akaua mama

    Wote: Ee

    Kiongozi: Sasa kimbieni

    Wote: Makelele ya shangwe……

    Naam, nimekurudisha utotoni ee.

    Huyu ndiye simba. Nakumbuka nyumbani jina maarufu la mbwa, ni simba. Mbwa wengi wa nyumbani ambao nimewahi kuwaona majina yao wanaitwa simba. Hii yote ni kwa sababu kila mtu anapenda mbwa wake awe na ukali kama simba. Na hata siku hizi kuna watu wanajiita majina ya wanyama.

    Kama nilivyokudokeza tangu mwanzo kuhusu kitabu cha Kobe Brayant ambaye pia alikuwa anajiita Black MAMBA. Watu wengine wanajiita majina ya wanyama kama yeye, likiwemo jina la simba, chui,…

    Nadhani kila mtu anajaribu kutafuta jina ambalo litamtambulisha vizuri, kulingana na tabia alizonazo. Ila jina SIMBA, nadhani wengi wanalipigania.

    Sidhani kama kuna mtu ambaye anapenda aitwe panya, kunguru, au nguchiro. Hii yote ni kuonesha kwamba kila mtu anataka kuonekana kwamba ana ustadi wa hali juu kwenye kile anachofanya.

    Sasa simba ana kitu gani cha kipekee ambacho kinamtofautisha na wanyama wengine.

    Zifuatazo hapa chini ni sifa muhimu za simba ambazo zinamfanya kuwa mfalme wa nyika.

    Fedha ya kupata ebook yenye andiko lote la THE MAMBA MENTALITY utaituma kwa namba 0755848391 Jina ni GODIUS RWEYONGEZA

  • Je, Kuna Haja Ya Kuendelea Kusoma Wakati Ajira Hakuna?

    Jana kupitia Temino ya Clouds FM niliongea na wanachuo wote hapa nchini, huku nikiwasisitiza juu ya umuhimu wa kutumia bumu lao la chuo vizuri maana kuna maisha baada ya chuo.

    Waendeshaji wa kipindi hicho ambao ni Harris Kapiga pamoja na Advovate Henry Mwinuka nao walisisitiza pointi muhimu sana kwa kusema kwamba kila mwaka kuna wahitimu zaidi ya laki nane ambao wanahitimu na miongoni mwao, ni wahitimu elfu themanini tu ambao wanapata ajira. Huku wahitimu laki saba na elfu ishirini wakibaki bila ajira. Na hizi usifikiri ni takwimu za kubahatisha. Hapana, ebu angalia screenshot hizi hapa chini

    Hii nimeitoa kwenye tovuti ya bunge la Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania. Kama hujaweza kuona vizuri, ebu yasome hayo maneno hapa chini

    Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa taarifa ya Serikali, kila mwaka takribani Wahitimu laki nane, kwa mwaka, na wanaoajiriwa ni elfu arobaini peke yake, kwa hiyo laki saba na sitini wanabaki mtaani. Ningependa kujua Serikali ina Mkakati gani wa ziada, kwa sababu Mkakati uliopo umeshindwa kukidhi vigezo vya kuweza kuwaajiri vijana wengi ambao wamehitimu? Ni Mkakati gani wa ziada ambao Serikali inao kwa ajili ya kuwasaidia Vijana hawa ambao wengi wako mtaani?

    Screenshot nyingine hii hapa

    hii nimeitoa kwenye tovuti ya gazeti la habari leo. Iliandikwa tarehe 28.12.2021

    Sasa swali la mmoja aliyesikia huo ujumbe lilikuwa ni hili hapa

    Habari bro mm naitwa mtima nimekusikia kwenye kipindi cha chimbo clouds FM mm nilikua naomba ushauli kama ajira ni chache je kunahaja ya kusoma maana unaweza kusoma na usipate ajira alafu ukawa umepoteza mda mm ni mwanafunzi naelekea kujiunga na kidato cha tano

    Kama unavyoona hapo. Leo ninaenda kuwa najibu swali la je, kuna umuhimu wowote ule wa mtu kuendelea kusoma wakati ajira hamna? Kuna umuhimu wowote kweli, au ndio bora ukaanze biashara kabla hata ya kupoteza fedha na muda?

    Eti kwa mfano wewe kwa maoni yako unasemaje?

    Kwenye hili siendi kuongea sana, badala yake napenda kwanza nikupe stori.

    Mwaka 2017 nikiwa chuoni, nilitaka kuacha chuo. Siriazi, nilitaka niache chuo, ili niende nikaanzishe biashara.

    Niliongea na rafiki zangu na kuwapa taarifa kuwa ninaenda kuacha chuo, na baadaye nikaongea na wazazi ambao hawakupenda uamuzi huo kabisa. Wazazi wangu walikuwa wachungu kwenye hili kuliko hata mwimba.

    Baadaye nikaongea na mshauri mmoja ambaye alinipa ushauri, ambao ningependa niutoe kwako pia.

    Aliniambia hivi, Godius huna haja ya kuacha chuo na kwenda kuanzisha biashara. Badala yake pambana na vyote viwili. Anzisha biashara na soma chuo. Ukifanikisha kufanya vyote viwili ukiwa chuoni, utakuwa shujaa.

    Kwangu huu ushauri niliupokea kwa mikono miwili, hivyo niliamua kukomaa na chuo na wakati huohuo nilianzisha biashara na kukomaa nayo.

    Kwa hiyo kwanza kabisa ningependa kukwambia kwamba, USIACHE KUSOMA. SOMA KWA BIDII NA UFAULU. ILA SASA FIKIRI NJE YA MASOMO. Na hapa sasa ndipo nataka nikupe mbinu na vitu ambavyo huwezi kuvipata sehemu nyingine.

    Labda tujiulize ni nini lengo la shule? Je, ni kukaririsha watu vitu wasivyovielewa? Ukiniuliza mimi nitakwambia hivi

    #1. LENGO LA ELIMU NI KUTENGENEZA WATU AMBAO WANAWEZA KUTAFSIRI KILE WANACHOJIFUNZA KWENYE MAISHA YA KAWAIDA

    Nakumbuka siku moja niliwahi kumsikia mkuu wa chuo cha SUA akihoji watafiti kuwa je, hizo tafiti mnazofanya zinawasaidiaje wananchi wa kawaida? Unaone ee.

    lengo la elimu siyo kwamba ukariri kile unachojifunza darasani. Badala yake ni kwamba, uweze kutafsiri kile unachojifunza na kukileta kwenye maisha ya kawaida.

    Nakumbuka tukiwa mwaka wa pili pale chuoni. Tulisoma kozi moja inaitwa SPICE PRODUCTION (uzalishaji wa viungo) Viungo si unavijua? Mambo ya iriki, tangawizi, karafuu…Mambo ya Pemba hayo yahe…

    Hii kwangu ndio ilikuwa ni kozi ya kipekee iliyokuwa na vitu vingi ambavyo nilikuwa napenda. Niliona kuna vitu vingi ndani yake ambavyo ningeweza kuvitumia kwenye maisha ya kawaida ya kila siku. Na hivyo, nikawa nimeamua kwamba baada ya chuo, nitakuwa nashughulika na uzalishaji na usindikaji wa viungo. Kwa hiyo, nikawa nimeona fursa kutokana na kile nilichokuwa nimejifunza na sasa hivi nimefungua kampuni inayohusika na uzalishaji wa viungo.

    Laiti ningeacha chuo nikiwa mwaka wa kwanza, hiki kitu nisingekaa nikakisoma mwaka wa  pili. Na sijui sasa hivi kampuni yangu ingekuwa inahusika na nini

    Kwa hiyo, endelea kusoma, ila sasa jiulize kwenye kile ambacho unajifunza darasani, unawezaje kukitumia kwenye maisha ya kwaida ya kila siku. Huku mtaani, kuna watu wana shida na wanategemea wasomi wazitatue, siyo kwamba wasomi watatatua hizi shida kwa kuwapa hela. Hapana, bali kwa kuwaletea suluhisho sahihi.

    Wewe hujawahi hata kumsaidia bibi kizee huko kijijini ambaye simu yake imejifunga tu, labda watoto walikuwa wanaichezea, ila kwa sababu hajui kiingerereza haelewi wapi pa kubonyeza. Mara paap akaileta kwako, ukasoma soma vitu viwili vitatu, ukaifungua akafurahi? Hujawahi? Mimi huwa inanitokea sana, na hiyo huwa inanipa picha kwamba hata matatizo mengine yanayokumba watu huku mtaani, ukiyatatua, watu watafurahi hivi hivi….

    Kwa hiyo, kila mara unapaswa kuwa unajiuliza  nasoma chuoni. Lakini, hawa uliowaacha nyumbani kwenu. Wanawezaje kunufaika na hiki ninachosoma. Je, kuna namna ambavyo wanaweza kunilipa kutokana hiki ninachosoma kama ipo. Basi zama ndani, ukijue hicho kitu. Ili baadaye uje ukigeuze hicho kitu kuwa biashara.

    Hivi Geometry ndio elimu ya maumbo ee…

    Au basi siyo lazima uelewe kila kitu, vingine utaelewa siku ya mtihani…Hahaha

    Ila ninachotaka kukwambia ni kwamba, Ben Carson anasema kaka yake aliona fursa kwenye hiyo elimu ya maumbo na akaamua kuitumia kwenye maisha ya kawaida ya mtaani.

    Hiki ni kitu ambacho shuleni walimu wako hawakwambii, ila ukweli ni kwamba, kwa kila unachojifunza unapaswa kuangalia namna ambavyo unaweza kukitumia kwenye maisha ya kawaida ya huku mtaani. Maana huku, ndio kuna maisha yenyewe…

    Siyo kila kitu kitakufaa wewe, na haipaswi kuwa hivyo, unahitaji kitu kimoja tu ambacho unaweza kutumia huku mtaani, vingine waachie wengine.

    Sijui unanielewa….

    Kama umenielewa basi, vuta pumzi kidogo wakati mimi nakunywa maji hapa….

    Kafanyaje huyu?

    #2. Imani ni yangu kuhusu chuo ni kwamba, chuo kipo kwa ajili ya kuandaa watu ambao watakuja kuajiri baadaye

    Hii ni imani yangu na ni msimamo wangu, hata ukiniamsha saa nane usiku, na kuniuliza ebu niambie kazi za shule na vyuo ni vipi.

    Nitakwambia vyuo vinapaswa kuandaa watu ambao watakuja kutengeneza ajira baadaye.

    Kwa nini? Na kwa jinsi gani?

    Kwa sababu elimu wanayoitoa shuleni, inapaswa kutafsiriwa kwenye maisha ya kawaida ya huku mtaani. Kwa hiyo kama kila mwanachuo, akitoka chuoni na kitu kimoja amnacho anaweza kupambana nacho huku mtaani, ataweza kuwasaidia hata wale aliowaacha nyumbani.

    Sasa kinachotokea sasa hivi ni kwamba wale waliosoma, wanarudi tena nyumbani na wanaanza kuwategemea wale waliowaaacha.

    Hiki kitu unaweza usiambiwe na walimu wako, lakini unapaswa ukijue. Jua kabisa kwamba unaposoma, hata kama mwalimu wako anakwambia soma bidii ili uje upate ajira. WEWE badili hilo liwe kwamba nasoma kwa bidii ili nije niajiri.

    #3. Lengo la elimu ni kukusaidia kutengeneza konekisheni.

    Iko hivi, unapokuwa unasoma kwanza unakutana na watu wengi. na kila mtu ana kipaji chake na uwezo wake. sasa hili ndilo lengo la shule. Kwamba liwakutanishe watu wenye vipaji vyenu, halafu muone namna ambavyo mnaweza kuunganisha vipaji vyenu kwa manufaa makubwa.

    Ila sasa hili halitokei kwa sababu, vipaji na uwezo havipewi kipaumbele kwenye mfumo wa elimu uliopo. Ndio maana mtu anasoma mpaka chuo kikuu, lakini ukiumuuliza kipaji chake hajui.

    Lakini, ukiweza kukutana na watu ambao wana vipaji na mkaweza kuunganisha nguvu kwa pamoja. YAANI, kiufupi mkaendana au mkaivana, basi ujue mtaweza kufika mbali.

    Halafu konekisheni haiishii kwa wanafunzi wenzako tu, hata kukuunganisha na walimu wako na hata watu wenye fikra za tofauti kabisa na wewe. Hii yote inakusaidia wewe kuuona ulimwengu katika namna ya kipekee na kuchukua maamuzi sahihi.

    Kuna konekisheni ambazo unaweza kuzitengeneza wakati wa kusoma zikaja kukusaidia baadaye. Pengine wewe kwenye kusoma umependa kuzama zaidi kwenye mambo ya uzalishaji wa viungo (spices) kama mimi. Na mwezako amependa kuzama kwenye sheria. Baadaye huyu mwanasheria anaweza kukusaidia wewe wakati unaajiri kwenye kuweka mikataba.

    Hata kama utamlipa, lakini kwa kuwa ni miongoni kwa konekisheni ambayo uliwahi kuitengeneza wakati unasoma, basi utakuwa na uhakika kwamba hapa nasaidiwa na mtu sahihi. Na siyo magumashi, anaweza pia kukusaidia kupooza bei kidogo…

    Hiki kitu ninachosema hapa unaweza usikielewe vizuri, lakini ulimwengu wa sasa umeanza kuonesha kuwa kweli hiki kitu kinafanya kazi kweli.

    Mfano mzuri tu, siku hizi mtandaoni kuna hivi vitu tunvyoviita aplikesheni.

    Unaweza kukuta kuna aplikesheni labda inayohusika na masuala ya uhasibu. Kama THL (watu wa THL mkisoma hapa, mnitumie vocha maana nimewarusha hewani leo)

    Sasa kutengeneza aplikesheni kama hii ya THL inayohusika na utunzaji wa kumbukumbu za kihasibu, kunahitaji walau muunganiko wa watu wa aina mbili.

    Kwanza ni wahasibu

    Na pili ni watalaamu wa teknlojia.

    Hizi ndizo konekisheni zenyewe, ambazo unaweza kuzipata ukiwa shuleni. Kwa hiyo wewe wakati unasoma, unaweza kugundua kwamba mtu fulani yuko vizuri kwenye kitu fulani, na mimi niko vizuri kwenye hiki kitu, basi tukiungana na kuunganisha haya maujuzi yetu, tunaweza kutengeneza kitu fulani ambacho kitakuwa na manufaa kwenye jamii.

    Mimi ni daktari, na jamaa mwingine ni mtalaamu wa teknolojia, tunaweza kuunganisha udaktari na teknojia tukawasaidia watu wengi zaidi.

    Daah, hapa nimemkumbuka jamaa mmoja. Ofcourse kinyozi. Hivi anaitwa kinyozi au fundi kinyozi, au basi…

    Huyu jamaa alikuwa anataka kuunganisha utalaamu wake wa kunyoa na teknoljia. Yaani, kwamba ukienda saloon kwake anachukua namba yako, ukishaondoka tu kuna mfumo wa kiteknolojia unakutumia ujumbe wa kukushukuru kwa kuweza kufika ofisini kwake kunyoa, baada ya wiki mbili mfumo huo unakukumbusha urudi kunyoa maana zimepita siku tangu unyoe…

    Sasa mtu kama huyu anahitaji konekisheni. Anahitaji kuunganishwa na mtu mwenye uelewa wa haya mambo ili amwezeshe kutengeneza mfumo wa aina hii…

    Sijui unanielewa? Kama umenielewa mpaka hapo, gonga cheers!

    #4. naamini kwamba chuo kipo kwa ajili ya kukupa maarifa sahihi unayoyahitaji kwenye maisha ya baada ya chuo.

    #5. shuleni na chuo ni kwa ajili ya kukufundisha wewe kusoma na kuandika, sasa jukumu lako baada ya kumaliza shule ni kujiendeleza kwenye kusoma na kuandika.

    Shuleni unafundishwa kusoma na kuandika. Si ndio? Tatizo la watu wengi wanapomaliza shule, ndio wanaona kwamba hakuna haja ya kusoma tena. Hawajifunzi kitu chochote kipya.

    Kitu hiki kinawafanya waendelee kuwa na maarifa yaliyopitwa na wakati. Sikiliza. Shuleni unafundishwa kusoma na kuandika. Ila sasa kwenye maisha ya kawaida ya huku mtaani unapaswa kusoma na unapaswa kuandika pia.

    Ebu fikiri amtu aliyesomea kompyuta mwaka 2010. Kama mtu huyu hajajiendeleza kuongeza maarifa na kujifunza zaidi, lazima tu ameshapitwa na wakati. unajua kwa nini? kwa sababu kompyuta zinabadilika kwa kasi, na na kuna vitu vingine vinazidi kugunduliwa sasa hivi.

    Mtu aliyosoma kompyuta 2010 atakuwa hakujifunza mambo ya roboti kama yalivyo sasa hivi. lakini kama wewe ukiwa ni mtu wa kujiupdate na kujifunza zaidi kila siku. Hata baada ya chuo, hutahangaika, maana utakuwa unapata ujuzi na kuelewa kinachoendelea. Na utakuwa unaweza kutumia hiki kitu unachojifunza kwenye maisha ya kawaida.

    Hayo ndiyo nilivyokuwa nayo moyoni kuhusu chuo na wqnachuo kwa leo. Nina mengi Ila sasa nikiyabwaga hapa tote, hayataleta maana. Nadhani siku nyingine jamaa akinichokoza kwabkuniuliza swali kamablanleo nitaandikia ena Kitu kingine.

    Ila jamani nisitize. Endelea kusoma, soma kwa bidii ila fikiria nje ya ajira. Kama umenielewa share makala hii na watu wengine ili nao wanufaike.

    Mpaka wakati mwingine

    Mimi ni Godius Rweyongeza kutoka SONGEMBELE CONSULTANTANCY

X