Home


  • kuomba msamaha ni bora

    kuomba msamaha ni bora

    Rafiki yangu ukikosea usiogope kuomba msamaha. Sisi kama binadamu huwa tunakosea, na ukigundua umekosea unajirudi, unakaa chini, unaweka mkakati mpya kisha unasongambele.

    Usije ukatumia kipengele cha kuomba msamaha kama sehemu ya kufanya makosa yanayojirudia.  Simamia mambo ya msingi, simamia haki. Ikitokea umekosea. jisahihishe na Songambele.

  • Tofauti kati ya ISBN na hakimiliki, USIJICHANGANYE

    Habari,

    Kinacholinda kitabu siyo ISBN, kinacholinda kitabu ni Hakimiliki.

    Hakimiliki ni tamko la kisheria linalompa mwandishi au mzalishaji wa kazi ya kiubunifu haki ya kipekee ya kutumia, kunakili, kuchapisha, au kusambaza kazi yake. Hii ina maana kwamba mtu mwingine hawezi kutumia au kuchapisha kazi hiyo bila ruhusa ya mwenye hakimiliki.

    Kwa upande mwingine, ISBN (International Standard Book Number) ni namba ya utambulisho wa kitabu inayotumika kibiashara. ISBN husaidia maduka, maktaba, na wachapishaji kutambua na kufuatilia vitabu kwa urahisi, lakini haiwezi kulinda kazi yako kisheria.

    Kwa hiyo, ukimaliza kuandika kitabu, hakikisha kwanza ISBN maana ni rahisi kuipata, lakini kabla ya kutoa kitabu au mara tu baada ya kutoa kitabu, hakikisha unapata hakimiliki.

    Kumbuka: ISBN ni namba ya utambulisho wa kitabu, lakini Hakimiliki ni kinga ya mwandishi.

    Kwa Tanzania ISBN inatolewa na Maktaba ya taifa. Na hakimiliki inatolewa na COSOTA

    Kwa maelezo zaidi kuhusu jinsi ya kupata hakimiliki au ISBN kwa kazi yako, wasiliana nasi Songambele Consultants kupitia:


    WASAP   bonyeza HAPA


    📞 0655 848 392

     

  • Kwa Chochote Unachofanya, Jitoe Kwa Asilimia 100 Labda Kuchangia Damu Tu!

    Niendelee kukutakia wewe na familia yako sikukuu njema

    Rafiki Yangu, kwa kazi au suala lolote ambalo unafanya. Jitoe kwa asilimia 100 kwenye kufanya hiyo kazi. Usijibakize nyuma na wala usikubali kitu chochote kile kikukwamishe. Weka nguvu zako, muda wako na akili zako kwenye hicho kitu.

    Ngoja nikwambie kitu.

    Ebu siku moja jaribu kufanya kitu kimoja na mawazo yaliyogawanyika.

    Mfano huku unaandika kama hapa, na wakati huohuo unajibu jumbe. Ni ukweli usiopingika kuwa itakuchukua muda kuandika na kukamilisha andiko lako kuliko pale ambapo ungekuwa umeweka nguvu zako na muda wako wote kwenye jambo moja kwa kwati huo.

    Hivyo basi rafiki yangu, chagua kufanya kitu kimoja kwa nguvu zako zote, kwa akili zako zote na bila kupepesa macho. Wekeza kila kitu sehemu moja.

    SOMA ZAIDI: Jinsi Kufanya Kazi Kwa Bidii Kunavyoweza Kukukutanisha Na Wafalme

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza

    Jipatie vitabu vya Godius Rweyongeza kwa kuchagua HAPA.

    Wasiliana nami wasap hapa

    Hakikisha umepata kitabu cha RASILIMALI ZA WATU WENGINE, ni kitabu kizuri kwa ajili yako. wasiliana na 0755848391 au 0745848395 sasa

    Makala ya kesho itawekwa kwenye blogu ya SONGAMBELE ambayo unaweza kuifikia kupitia www.songambele.co.tz na itawekwa kwenye channel ya telegram pia ambayo unaweza kuifikia kwa KUBONYEZA HAPA

     

  • USHINDI NI LAZIMA

    Rafiki yangu, tukiamia kwamba tunataka kufanikiwa. Hatuna mbafala wa Hilo. KITU pekee kinachotakiwa ni sisi tupambane mpaka USHINDI ufikiwe.

    Hakuna mbafala wa USHINDI.

    Kama tunapaswa kufanya mazoezi zaidi, basi tutafanya mazoezi zaidi. Ila USHINDI ni LAZIMA.

    Kama tunatakiwa kujitoa tutafanya hivyo, maana USHINDI ni LAZIMA.

    Siku ya Leo, jiulize ni USHINDI Gani wa lazima ulio mbele Yako? Upambanie sasa. Kumbuka. USHINDI ni LAZIMA.

    SOMA ZAIDI: NI LINI HUWA TUNASEMA MTU AMEANZA KUPATA USHINDI?

  • KESHO BORA INATENGENEZWA LEO

    Rafiki yangu mpendwa salaam. NIchukue nafasi hii kukupongeza kwa siku hii nyingine ya kipekee. Je, wajua kuwa kesho bora inatengenezwa kwa maamuzi sahihi unayofanya siku ya leo?

    Tunapoizungumzia kesho bora, siyo tu tunazungumzia mabadiliko ya kalenda, bali tunazungumzia mabadiliko ya kimaisha ambayo yatakuwa yametokea kwa upande wako.

    Matokeo mazuri utakayokuwa nayo miaka kadhaa ijayo, yanaandaliwa leo. Inawezekana leo hii mambo yakawa hayako sawa kwa upande wako. Ila hilo haliondoi nguvu na umuhimu wa kusema kwamba mambo mazuri na kesho yako nzuri inaweza kuandaliwa leo hii.

    Ili kujenga kesho bora, ni muhimu kufahamu kwamba huwa hakuna mafanikio ya ghafla. Mafanikio yoyote unayotaka ni mchakao ambao unapaswa kuwa nao kuufuata, hivyo basi, kesho yako bora itaweza kujengwa kama utawez akuwa na mchakato mzuri ambao unaufufta na kuufanyia kazi. NI ukweli usiopingika kuwa ili kujenga kesho bora inayomeremeta unapaswa kuanza kuiandaa leo.

    Pengine unajiouliza ni kwa namna gani naweza kuiandaa kesho bora leo hii?

    #1. Maamuzi bora unayofanya leo yanaweza kuwa chaChu ya kutengeneza kesho bora. Maamuzi haya yanaweza kuwa ya kuwekeza muda, nguvu, pesa uliyonayo leo, maarifa n.k

    Maamuzi haya yanaweza kuwa ya kuanzisha biashara. Yanaweza kuwa maamuzi ya kuweka akiba au kufanya uwekezaji. Kwa vyovyote vile leo hii unapaswa kufanya maamuzi kuilelekea kesho bora.

    Inawezekana maamuzi haya yakawa magumu sana kwako.  Inawezekana maamuzi haya yakaambatana na maumivu, ila ni ukweli usiopingika ni kwamba  usiogope kufanya maamuzi haya. Yafanye maana, usipofanya maamuzi ya kesho unayohitaji, ukakubali kulipa gharama hata kama muda mwingine inaumiza, ni ukweli usiopingika kwamba hiyo keshoa bora itabaki kuwa ndooto tu.

    Inawezekana leo hii ukafanya maamuzi ya kuweka akiba, lakini wakati huu unaamua kukweka akiba, kipato chako kikawa hakitoshi. Na muda mwinigine inawezekana uhkawa unaweka akiba ila unashawikishika kutumia akiba yako. ukweli ni kuwa jipe muda na usirudi nyuma. Kubali kulala njaa siku nyingine hata kama una akiba umeiweka. Ili mwishowe, hii akiba iweze kukusaidia kwenye kufanikisha malengo ambayo umeweka.

    Maamuzi bora ya kesho yako unayofanya leo yaambatanae na vitendo. Nakumbuka mara kwa mara nimekuwa nasikia watu kuwa hawana mtaji, ila unakuta mtu analalamika miaka nenda miaka rudi shida hiyohiyo. Badala ya kuchukua hatamu ya maisha na kuanza kutengeneza kesho bora ambapo watakuwa na mtaji, wanaendelea kulalamika. Ngoja ni kwambie kitu rafiki yangu, kesho bora, inajengw akwa misingi mizuri ya kuamua na kuchukua hatua.

    #1. Weka malengo

    Kamwe usiishi bila ya malengo, kama hutakuwa na malengo rafiki yangu kila kitu ambacho kitakuja mbele yako kinaenda kuwa ndiyo malengo yako. hivyo, ni muhimu sana kwako kuyhakikish akmwab amara zote unakuw ana malengo ambayo unayafanyi akazi na malengo haya unayasimamia kwa dhati na kwa nguvu kubwa. Nakwambia hivi kwa sababu kuna wakai baada ya kuwa umeweka malengo unaweza kujikuta unataka kuacha kuyafanyia kazi. Jikita kwenye kuyafanyia kazi malengo yako mar azote. Malengo yako  yakufanye uwe bize muda woate nbadal;a ya kuwa bize na mambo ambayo siyo sawa na siyo sahiahi kwako n aka wka maendele ya kesho yako bora.

    #3.  Jifunze kila siku

    Rafiki yangu, kila siku jifunze. Iko hivi, kesho bora inaandaliw akwa kuwa na maarifa sahihi pia. maarifa ni moja ya kitu cha muhimu sana kuelekea kesho bora. Hata vitabu vitakatifu kama biblia vinayapa kipaumbele. Mfalme kama Suleimani, anaonakena akiomba kupata maarifa kwanza kabla y akitu kingine chochote. Hii ndiyo kusema kwamba wewe usiipuuzie nguvu ya maarifa. Maarifa yana nguvu kubwa sana.

    Isitokee siku ukasema kwamba unajua kila kitu. Kila siku kwako iwe ni siku ya kujifunza upya.

    #4. Heshimu muda wako

    Baada ya kuwa umepanga aratiba yakp hakikisha kwamba unaheshimu muda wako wa kazi na hufanyi mambo menine yasiyoendana na kazi uliyokusudia kufanya  kwenye ratiba yak o rasmi.

  • Uvaaji wa headphones ni faida kwa wavaaji au ni hasara?

     

    Tunaishi kwenye dunia ya kipekee sana. Mara paap, headphones hizo hapo tunazo na tunatamba nazo. Unaweza kuzivaa kwenye daladala
    Kwenye usafiri wowote wa umma au wa binafsi
    Ukiwa unatembea
    Na hata ukiwa ofisini au nyumbani.

    Leo nataka tujadiliane kwa pamoja kwamba uvaaji huu wa hizi headphones ni wa faida au hasara

    Ni jambo la wazi kuwa uvaaji wa headphones una faifda zake lakini pia umeambatana na hasara kadhaa.Haya yote nataka tuyaangalie kwa jicho la tai aliye juu angani na angalia vitu kama vilivyo bila ya kupepesa macho.

    IKo wazi kwa mfano kwamba ukiwa kwenye mazingira yenye kelele nyingi, ukiwa na headphone zinakusaidia sana kundelea na majukumu yako. Nakumbuka wakati nipo chuoni, NILIKUW NA UWEZO WA KUENDELEA NA MAJUKUMU YANGU HATA KAMA NILIKUWA NIMEZUNGUYKWA NA WATU WENYE MAKELELE kwa sababu tu nilikuwa nimevaa headphone.

    Kuna kipindi fulani unahitaji usikilize jambo au taarifa ambazo hutaki upande wa pili usikie. na hapa ndipo headphone zinafanya kazi nzuri sana.

    Aidha kwenye suala zima la kujifunza kwangu, huwa napenda kuzivaa na kusikilza vitabu vya sauti. Yaani audioooks kama hizi ambazo unaweza kuzipata hapa. Kila ninapopita na headphone zangu, ninakuwa ninapata maarifa bila shida yoyote ile.

    Wengine pia wanapenda kuzivaa wakati wa kufanya mazoezi, kitu hiki kinawafanya wanaua ndege wawili kwa jiwe moja.

    Hata hivyo kuna mazingira tunazivaa kupitiliza. Mfano, unakuta mtu anapanda kwenye usafiri. muda wote wa safari (labda kutoka Morogoro kwenda Dar) amevaa headphone tu.! je, hii ni faida au hasara?

    Ukiniuliza mimi nitakwambia hii ni hasara. unajua kwa nini? Umekaa kwenye treni au gari au ndege, hujasalimiana na mtu wa karibu yako. HUjajua ni nani n.k.

    • Halafu wewe huyohuyo kila siku unaomba uweze kukutana na watu wazito, unadhani utakutana nao kivipi? watashuka kutoka mbinguni? Hapana, inawezekana konekisheni unazozitafuta umeshapishana nazo mara nyongi tu kwa sababu ya kutozitumia. au kwa kuwa bize muda wote.

      USHAURI WANGU: Ukipanda usafiri au ukiwa kwenye mazingira ya watu, weka pembeni headphone hata kwa muda kwa ajili ya kusalimiana na watu. Usisafiri na mtu kwa saa mbili, bila kumjua vizuri. Unaweza kukuta huyo ni mteja mzuri wa bidhaa zako, unaweza kukuta anakuja kuwa msambazaji wa bidhaa zako, unaweza kukuta anakuwa mshirika wako muhimu na pengine anaweza asiwe chochote. Lkini haya yote yatawezekana kwa wewe kuhakikisha unakuwa na mazungumzo na huyu mtu

      SOMA ZAIDII: JINSI YA KUANZISHA MAZUNGUMZO NA MTU YEYOTE

    Fanya Kitu Hiki Kimoja Tu Kwenye Biashara Yako (Funzo Kutoka Kwa Makampuni Makubwa Kama Google, Facebook Na Amazon)

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza

    Jipatie vitabu vya Godius Rweyongeza kwa kuchagua HAPA.

    Wasiliana nami wasap hapa

    Hakikisha umepata kitabu cha RASILIMALI ZA WATU WENGINE, ni kitabu kizuri kwa ajili yako. wasiliana na 0755848391 au 0745848395 sasa

    Makala ya kesho itawekwa kwenye blogu ya SONGAMBELE ambayo unaweza kuifikia kupitia www.songambele.co.tz na itawekwa kwenye channel ya telegram pia ambayo unaweza kuifikia kwa KUBONYEZA HAPA

  • Kama huwezi kupaa, kimbia

    RAFIKI yangu mpendwa salaam, nichukue nafasi hii kukupongeza kwa kazi nzuri unayofanya.

    Moja ya kitu ambacho kimekuwa kinawakwamisha watu wengi kuandika ni kwa sababu hawana vifaa vya kuandikia. Ukweli ni kuwa muda mwingine si kwamba unahitaji kuwa na vifaa vya kipekee sana ili uandike, bali unapaswa uanze kuandika kwa kutumia vifaa ulivyonavyo.

    ANZA KUANDIKA kwa kutumia simu yako. Asilimia kubwa ya watu wanamiliki simu. Wewe kama mwandishi, itumie simu yako kuandika. weka app za kutumia kuandika kwenye simu yako, kama app ya Google docs kisha anza kuandika.

    HARIRI kitabu chako kwa kutumia simu yako. Baada ya kuandika, anza kuhariri kitabu chako kwa kutumia simu yako hiyohyo.

    Tengeneza Kava kwa kutumia simu. App ya Canva inaweza kukusaidia kwenye kutengeneza kava na hata kwenye kupangilia kitabu chako.

    SANIFU kitabu chako kwa kutumia simu yako pia. Inawezekana kutumia simu yako kwenye kusanifu maudhui na mwonekano wa ndani ya kitabu pia.

    Lakini pia kama una vifaa zaidi ya simu unaweza kuvitumia rafiki yangu.

    Ninachoweza kukwambia ni kwamba kwenye kuandika, tumia kile ulichonacho.

    Kama huna simu, andika kwenye daftari.

    kama huna tablet, tumia simu

    kama huna kompyuta, tumia tablet.

    ila kwa vyovyote vile usiache kuandika.

    Ningependa tu kukuuliza swali moja, ni lini utaweza KUANDIKA KITABU CHAKO NA KUKIKAMILISHA?

    SOMA ZAIDI: Vitu 50 Ambavyo Hupaswi Kuchukulia Poa

  • UNAMUONA DADA HUYO?

    UNAMUONA DADA HUYO?

    Wengi huwa likija suala zima la kuandika kitabu huwa wanapenda kuniuliza kuwa ni wapi wanaweza kupata wazo la kuandika kitabu.

    NImekuwa nikieleza mara kwa mara namna ya kupata wazo la kuandika kitabu.

    Na moja ya njia ambayo unaweza kutumia kwenye kupata wazo la kuandika kitabu ni ikama alivyofanya huyo dada hapo juu.

    Yaani, mazingira na matukio ambayo yanatokea unaendana nayo hivyohivyo

    Kwa dada huyo ambaye ni dancer, kitendo cha yeye kukutwa na kadhia ya kuanguka, amegeuza hiyo kuwa mwendo mpya wa kucheza. HIvyo hivyo kwangu mimi na wewe.

    matukio yanayotokea kwenye mazingira yetu yanaweza kugeuzwa kuwa chanzo cha kuandika.

    tunaweza kuyatumia kuandika kitabu, makala au andiko 

    lolote ambalo tunaona kwamba linafaa. Hivyo, usiogope rafiki yangu. kuwa utapata wapi wazo la kuandika. wazo la kuandika unalo hapo.

    Dada huyo amepata wazo la kutengeneza mwenendo mpya wa kucheza kutokana na tukio la kutaka kuanguka.

    Na mimi  nimepata wazo la kuandika makala hii baada ya kuangalia video yake

    wewe pia unaweza kupata wazo la kuandika kitabu chako kutokana na makala hii.

    Kama bado unajiuliza uandike nini, usiwe na wasiwasi, hakikisha unapata kitabu cha JINSI YA KUWA MWANDISHI MBOBEVU, unaweza kujipatia nakala yako popote pale ulipo kwa shilingi 30,000/- tu.

    Au unaweza kujipatia pakeji nzima ya vitabu vya uandishi.

    Pakeji hii inahusisha vitabu vifuatavyo.

    1. JINSI YA KUWA MWANDISHI MBOBEVU

    2. SEHEMU KUU MUHIMU ZA KILA KITABU

    3. ANDIKA KITABU CHAKO KAMA SMS

    4. MWANDISHI NI MUUMBAJI

    Hii ni pakeji kamili ya vitabu vya uandishi ambayo unapaswa kuwa nayo. Kuipata ni rahisi sana. Tuwasiliane kwa 0655848392

    image1758192352437.png

    Hivi ni vitabu ambavyo unapaswa kuhakikisha kwamba unavipata.

    Wengi huwa likija suala zima la kuandika kitabu huwa wanapenda kuniuliza kuwa ni wapi wanaweza kupata wazo la kuandika kitabu.

    NImekuwa nikieleza mara kwa mara namna ya kupata wazo la kuandika kitabu.

    Na moja ya njia ambayo unaweza kutumia kwenye kupata wazo la kuandika kitabu ni ikama alivyofanya huyo dada hapo juu.

    Yaani, mazingira na matukio ambayo yanatokea unaendana nayo hivyohivyo

    Kwa dada huyo ambaye ni dancer, kitendo cha yeye kukutwa na kadhia ya kuanguka, amegeuza hiyo kuwa mwendo mpya wa kucheza. HIvyo hivyo kwangu mimi na wewe.

    matukio yanayotokea kwenye mazingira yetu yanaweza kugeuzwa kuwa chanzo cha kuandika.

    tunaweza kuyatumia kuandika kitabu, makala au andiko 

    lolote ambalo tunaona kwamba linafaa. Hivyo, usiogope rafiki yangu. kuwa utapata wapi wazo la kuandika. wazo la kuandika unalo hapo.

    Dada huyo amepata wazo la kutengeneza mwenendo mpya wa kucheza kutokana na tukio la kutaka kuanguka.

    Na mimi  nimepata wazo la kuandika makala hii baada ya kuangalia video yake

    wewe pia unaweza kupata wazo la kuandika kitabu chako kutokana na makala hii.

    Kama bado unajiuliza uandike nini, usiwe na wasiwasi, hakikisha unapata kitabu cha JINSI YA KUWA MWANDISHI MBOBEVU, unaweza kujipatia nakala yako popote pale ulipo kwa shilingi 30,000/- tu.

    Au unaweza kujipatia pakeji nzima ya vitabu vya uandishi.

    Pakeji hii inahusisha vitabu vifuatavyo.

    1. JINSI YA KUWA MWANDISHI MBOBEVU

    2. SEHEMU KUU MUHIMU ZA KILA KITABU

    3. ANDIKA KITABU CHAKO KAMA SMS

    4. MWANDISHI NI MUUMBAJI

    Hii ni pakeji kamili ya vitabu vya uandishi ambayo unapaswa kuwa nayo. Kuipata ni rahisi sana. Tuwasiliane kwa 0655848392

    image1758192352437.png

    Hivi ni vitabu ambavyo unapaswa kuhakikisha kwamba unavipata.

  • Kama Isingekuwa Pesa, Ungekuwa Unafanya Unachofanya sasa

    Ndugu Godius Rweyongeza
    Ndugu Godius Rweyongeza

    Anaandika GODIUS RWEYONGEZA

    Wasiliana naye wasap hapa

    Mwaka juzi taarifa zilisambaa mtandaoni kwamba mchungaji mmoja huko nchini Uganda ameacha uchungaji baada ya kushinda milioni 100 kupitia kubeti. Kwa maneno yake huyu mchungaji alisema kwamba alikuwa anafanya kazi ya uchungaji kwa sababu hakuwa na fedha.

    Hiki kinatafakarisha sana. Kumbe tuna watu wanafanya vitu ambavyo hawapendi, na kila siku wanalazimika kwenda kufanya shughuli wanazofanya ila moyoni mwao hawapendi hivyo vitu.

    Je, wewe umo?

    Mtu mmoja alisema kwamba biashara za kitanzania ni ngumu sana. Kwa sababu pale biashara zinapoanza kupata faida inayoeleweka, ndipo watu wanataka kupata pesa zao na kuondoka kwenye biashara hizo badala ya kurudisha faida kwenye biashara. Kumbe kitu cha kwanza kilichokuwa kimewapeleka kwenye biashara hiyo si kutoa huduma, siyo kutatua matatizo yanayowakumba watu, bali ni pesa.

    Sasa swali llangu kwako siku ya leo ni kwamba kama isingekuwa pesa, je, unachofanya sasa hivi ungekuwa unakifanya? Najua utanza kusema sasa nitaishije bila yakuwa na pesa. Ni ukweli usiopingika kuwa pesa ni muhimu na inahitajika sana.

    Ila unatakiwa kupenda unachofanya.

    Kupenda unachofanya ni hatua moja mbele ukilinganisha na pale unapofanya usichokipenda.

    Kuna siku unaweza kuwa siku hiyo hujisikii kufanya kazi. Ila ukiwunapenda unachofanya utaendelea kupambana.

    SOMA ZAIDI: Kauli Yenye Nguvu: Ni bora Ufe Ukiwa unafanya unachopenda…

    Sasa kwenye makala ya leo tujadiliane vitu vitano vinavyopaswa kukusukuma kufanya kazi au biashara. Hii siyo kwa sababu hatutambui umuhimu wa fedha. Itambulike umuhimu fedha. lakini kwa hapa tuzungumzie hili. 

    sababu ya kwanza ni kutimiza kusudi lako. kila mmoja ana kusudi kubwa ambalo limemfanya awepo hapa duniani. 

    1. Kutimiza kusudi la kuwepo hapa duniani

    Kila mtu ameumbwa kwa kusudi fulani. Kazi au biashara unayofanya inapaswa kuwa sehemu ya kutimiza kusudi hilo. Unapofanya kazi kwa kuelewa kwamba unatekeleza wito wa maisha yako, hutachoka kirahisi, wala hutafanya mambo kwa kubahatisha.

    2. Kuwahudumia watu na kutatua changamoto

    Biashara na kazi yoyote yenye mafanikio makubwa inasimama juu ya msingi wa kutatua matatizo ya watu. Ukizingatia kusaidia na kuhudumia wengine, thamani yako itaongezeka, na kwa hakika pesa zitaingia kama matokeo.

    3. Kujenga historia

    Kila siku unayofanya kazi au biashara, unajenga hadithi yako ya maisha. Je, utataka watu wakikukumbuka waseme uliishi tu kwa ajili ya kutafuta fedha, au watasema ulileta mabadiliko makubwa? Kufanya kazi kwa lengo la kuacha alama ni nguvu ya pekee ya kukusukuma kila siku.

    4. Kukuza vipaji

    Kazi na biashara ni shule kubwa zaidi ya maisha. Inakupa nafasi ya kutumia kile kilicho ndani yako na pia kujifunza zaidi. Unapoliona hilo kama msukumo, utathamini kila changamoto na fursa kama nafasi ya kukua na kuwa bora.

     

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza

    Jipatie vitabu vya Godius Rweyongeza kwa kuchagua HAPA.

    Wasiliana nami wasap hapa

    Hakikisha umepata kitabu cha RASILIMALI ZA WATU WENGINE, ni kitabu kizuri kwa ajili yako. wasiliana na 0755848391 au 0745848395 sasa

    Makala ya kesho itawekwa kwenye blogu ya SONGAMBELE ambayo unaweza kuifikia kupitia www.songambele.co.tz na itawekwa kwenye channel ya telegram pia ambayo unaweza kuifikia kwa KUBONYEZA HAPA

     

     

  • Biashara ni Mkakati, Wa Kwako Ni Upi?

    Biashara huwa zinakuwa na mkakati wa biashara. Inawezekana wewe mwenyewe hujui kwamba una mkakati kwenye biashara, lakini kutoujua mkakati huo, haimaanishi kwamba haupo. Upo tu, tena umejaa tele. 

    Mkakati wa biashara tunaweza kuuona kwenye namna unavyofanya shughuli zako kwenye biashara yako. Sasa swali ni je, mkakati wa biashara unapaswa kugusa kitu gani na kitu gani?

    Washiriki wa semina ya Godius Rweyongeza
    Washiriki wa semina ya Godius Rweyongeza

    Kwenye biashara, mkakati wa biashara unaweza kuwa

    1.  KIla mmoja kwenye biashara kujua anachopaswa kufanya na lini kinapaswa kuwa kimekamilika na kukifanya kwa bidii, 
    2. Kila mmoja anapaswa kuwa anashambulia muda wote. Hakuna timu ya mpira wa miguu ambayo huwa inashinda kwa kulinda lango bali kwa kushambulia.
    3. Kuwa bora kwenye eneo fulani, bidhaa moja au huduma moja ambayo utafahamika kwayo kabla hujaanza kuzalisha bidhaa nyingine au huduma nyingine.
    4. Ni muhimu sana kwenye biashara kuhakikisha kwamba unatafuta njia ambayo ni bora, haraka, urahisi na ya uhakika kwa wateja.
    5. kwenye biashara kampuni zina watu wanaojituma kwenye kazi. Wanatumia neno kama sisi. Wanaona kampuni kama mwendelezo wao. na hawafikirii kwamba hiyo siyo kazi yangu.
    6. Kwenye biashara kila mara unaangalia namna ya kumshangaza mteja kwa kumpa huduma bora, ya haraka ya uhakika na 
    7. Kwenye biashara unatakiwa kulijua soko lako na kutengeneza mbinu za uhakika za kulifikia hili soko lako bila shida yoyote.

    hii ni baadhi ya mikakati muhimu sana unayoweza kuwa nayo.

    Ni mkakati upi unaenda kuanza nao siku ya leo?

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza

    Jipatie vitabu vya Godius Rweyongeza kwa kuchagua HAPA.

    Wasiliana nami wasap hapa

    Hakikisha umepata kitabu cha RASILIMALI ZA WATU WENGINE, ni kitabu kizuri kwa ajili yako. wasiliana na 0755848391 au 0745848395 sasa

    Makala ya kesho itawekwa kwenye blogu ya SONGAMBELE ambayo unaweza kuifikia kupitia www.songambele.co.tz na itawekwa kwenye channel ya telegram pia ambayo unaweza kuifikia kwa KUBONYEZA HAPA

X