Home


  • Kwa Chochote Unachofanya, Jitoe Kwa Asilimia 100 Labda Kuchangia Damu Tu!

    Niendelee kukutakia wewe na familia yako sikukuu njema

    Rafiki Yangu, kwa kazi au suala lolote ambalo unafanya. Jitoe kwa asilimia 100 kwenye kufanya hiyo kazi. Usijibakize nyuma na wala usikubali kitu chochote kile kikukwamishe. Weka nguvu zako, muda wako na akili zako kwenye hicho kitu.

    Ngoja nikwambie kitu.

    Ebu siku moja jaribu kufanya kitu kimoja na mawazo yaliyogawanyika.

    Mfano huku unaandika kama hapa, na wakati huohuo unajibu jumbe. Ni ukweli usiopingika kuwa itakuchukua muda kuandika na kukamilisha andiko lako kuliko pale ambapo ungekuwa umeweka nguvu zako na muda wako wote kwenye jambo moja kwa kwati huo.

    Hivyo basi rafiki yangu, chagua kufanya kitu kimoja kwa nguvu zako zote, kwa akili zako zote na bila kupepesa macho. Wekeza kila kitu sehemu moja.

    SOMA ZAIDI: Jinsi Kufanya Kazi Kwa Bidii Kunavyoweza Kukukutanisha Na Wafalme

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza

    Jipatie vitabu vya Godius Rweyongeza kwa kuchagua HAPA.

    Wasiliana nami wasap hapa

    Hakikisha umepata kitabu cha RASILIMALI ZA WATU WENGINE, ni kitabu kizuri kwa ajili yako. wasiliana na 0755848391 au 0745848395 sasa

    Makala ya kesho itawekwa kwenye blogu ya SONGAMBELE ambayo unaweza kuifikia kupitia www.songambele.co.tz na itawekwa kwenye channel ya telegram pia ambayo unaweza kuifikia kwa KUBONYEZA HAPA

     

  • USHINDI NI LAZIMA

    Rafiki yangu, tukiamia kwamba tunataka kufanikiwa. Hatuna mbafala wa Hilo. KITU pekee kinachotakiwa ni sisi tupambane mpaka USHINDI ufikiwe.

    Hakuna mbafala wa USHINDI.

    Kama tunapaswa kufanya mazoezi zaidi, basi tutafanya mazoezi zaidi. Ila USHINDI ni LAZIMA.

    Kama tunatakiwa kujitoa tutafanya hivyo, maana USHINDI ni LAZIMA.

    Siku ya Leo, jiulize ni USHINDI Gani wa lazima ulio mbele Yako? Upambanie sasa. Kumbuka. USHINDI ni LAZIMA.

    SOMA ZAIDI: NI LINI HUWA TUNASEMA MTU AMEANZA KUPATA USHINDI?

  • KESHO BORA INATENGENEZWA LEO

    Rafiki yangu mpendwa salaam. NIchukue nafasi hii kukupongeza kwa siku hii nyingine ya kipekee. Je, wajua kuwa kesho bora inatengenezwa kwa maamuzi sahihi unayofanya siku ya leo?

    Tunapoizungumzia kesho bora, siyo tu tunazungumzia mabadiliko ya kalenda, bali tunazungumzia mabadiliko ya kimaisha ambayo yatakuwa yametokea kwa upande wako.

    Matokeo mazuri utakayokuwa nayo miaka kadhaa ijayo, yanaandaliwa leo. Inawezekana leo hii mambo yakawa hayako sawa kwa upande wako. Ila hilo haliondoi nguvu na umuhimu wa kusema kwamba mambo mazuri na kesho yako nzuri inaweza kuandaliwa leo hii.

    Ili kujenga kesho bora, ni muhimu kufahamu kwamba huwa hakuna mafanikio ya ghafla. Mafanikio yoyote unayotaka ni mchakao ambao unapaswa kuwa nao kuufuata, hivyo basi, kesho yako bora itaweza kujengwa kama utawez akuwa na mchakato mzuri ambao unaufufta na kuufanyia kazi. NI ukweli usiopingika kuwa ili kujenga kesho bora inayomeremeta unapaswa kuanza kuiandaa leo.

    Pengine unajiouliza ni kwa namna gani naweza kuiandaa kesho bora leo hii?

    #1. Maamuzi bora unayofanya leo yanaweza kuwa chaChu ya kutengeneza kesho bora. Maamuzi haya yanaweza kuwa ya kuwekeza muda, nguvu, pesa uliyonayo leo, maarifa n.k

    Maamuzi haya yanaweza kuwa ya kuanzisha biashara. Yanaweza kuwa maamuzi ya kuweka akiba au kufanya uwekezaji. Kwa vyovyote vile leo hii unapaswa kufanya maamuzi kuilelekea kesho bora.

    Inawezekana maamuzi haya yakawa magumu sana kwako.  Inawezekana maamuzi haya yakaambatana na maumivu, ila ni ukweli usiopingika ni kwamba  usiogope kufanya maamuzi haya. Yafanye maana, usipofanya maamuzi ya kesho unayohitaji, ukakubali kulipa gharama hata kama muda mwingine inaumiza, ni ukweli usiopingika kwamba hiyo keshoa bora itabaki kuwa ndooto tu.

    Inawezekana leo hii ukafanya maamuzi ya kuweka akiba, lakini wakati huu unaamua kukweka akiba, kipato chako kikawa hakitoshi. Na muda mwinigine inawezekana uhkawa unaweka akiba ila unashawikishika kutumia akiba yako. ukweli ni kuwa jipe muda na usirudi nyuma. Kubali kulala njaa siku nyingine hata kama una akiba umeiweka. Ili mwishowe, hii akiba iweze kukusaidia kwenye kufanikisha malengo ambayo umeweka.

    Maamuzi bora ya kesho yako unayofanya leo yaambatanae na vitendo. Nakumbuka mara kwa mara nimekuwa nasikia watu kuwa hawana mtaji, ila unakuta mtu analalamika miaka nenda miaka rudi shida hiyohiyo. Badala ya kuchukua hatamu ya maisha na kuanza kutengeneza kesho bora ambapo watakuwa na mtaji, wanaendelea kulalamika. Ngoja ni kwambie kitu rafiki yangu, kesho bora, inajengw akwa misingi mizuri ya kuamua na kuchukua hatua.

    #1. Weka malengo

    Kamwe usiishi bila ya malengo, kama hutakuwa na malengo rafiki yangu kila kitu ambacho kitakuja mbele yako kinaenda kuwa ndiyo malengo yako. hivyo, ni muhimu sana kwako kuyhakikish akmwab amara zote unakuw ana malengo ambayo unayafanyi akazi na malengo haya unayasimamia kwa dhati na kwa nguvu kubwa. Nakwambia hivi kwa sababu kuna wakai baada ya kuwa umeweka malengo unaweza kujikuta unataka kuacha kuyafanyia kazi. Jikita kwenye kuyafanyia kazi malengo yako mar azote. Malengo yako  yakufanye uwe bize muda woate nbadal;a ya kuwa bize na mambo ambayo siyo sawa na siyo sahiahi kwako n aka wka maendele ya kesho yako bora.

    #3.  Jifunze kila siku

    Rafiki yangu, kila siku jifunze. Iko hivi, kesho bora inaandaliw akwa kuwa na maarifa sahihi pia. maarifa ni moja ya kitu cha muhimu sana kuelekea kesho bora. Hata vitabu vitakatifu kama biblia vinayapa kipaumbele. Mfalme kama Suleimani, anaonakena akiomba kupata maarifa kwanza kabla y akitu kingine chochote. Hii ndiyo kusema kwamba wewe usiipuuzie nguvu ya maarifa. Maarifa yana nguvu kubwa sana.

    Isitokee siku ukasema kwamba unajua kila kitu. Kila siku kwako iwe ni siku ya kujifunza upya.

    #4. Heshimu muda wako

    Baada ya kuwa umepanga aratiba yakp hakikisha kwamba unaheshimu muda wako wa kazi na hufanyi mambo menine yasiyoendana na kazi uliyokusudia kufanya  kwenye ratiba yak o rasmi.

  • Uvaaji wa headphones ni faida kwa wavaaji au ni hasara?

     

    Tunaishi kwenye dunia ya kipekee sana. Mara paap, headphones hizo hapo tunazo na tunatamba nazo. Unaweza kuzivaa kwenye daladala
    Kwenye usafiri wowote wa umma au wa binafsi
    Ukiwa unatembea
    Na hata ukiwa ofisini au nyumbani.

    Leo nataka tujadiliane kwa pamoja kwamba uvaaji huu wa hizi headphones ni wa faida au hasara

    Ni jambo la wazi kuwa uvaaji wa headphones una faifda zake lakini pia umeambatana na hasara kadhaa.Haya yote nataka tuyaangalie kwa jicho la tai aliye juu angani na angalia vitu kama vilivyo bila ya kupepesa macho.

    IKo wazi kwa mfano kwamba ukiwa kwenye mazingira yenye kelele nyingi, ukiwa na headphone zinakusaidia sana kundelea na majukumu yako. Nakumbuka wakati nipo chuoni, NILIKUW NA UWEZO WA KUENDELEA NA MAJUKUMU YANGU HATA KAMA NILIKUWA NIMEZUNGUYKWA NA WATU WENYE MAKELELE kwa sababu tu nilikuwa nimevaa headphone.

    Kuna kipindi fulani unahitaji usikilize jambo au taarifa ambazo hutaki upande wa pili usikie. na hapa ndipo headphone zinafanya kazi nzuri sana.

    Aidha kwenye suala zima la kujifunza kwangu, huwa napenda kuzivaa na kusikilza vitabu vya sauti. Yaani audioooks kama hizi ambazo unaweza kuzipata hapa. Kila ninapopita na headphone zangu, ninakuwa ninapata maarifa bila shida yoyote ile.

    Wengine pia wanapenda kuzivaa wakati wa kufanya mazoezi, kitu hiki kinawafanya wanaua ndege wawili kwa jiwe moja.

    Hata hivyo kuna mazingira tunazivaa kupitiliza. Mfano, unakuta mtu anapanda kwenye usafiri. muda wote wa safari (labda kutoka Morogoro kwenda Dar) amevaa headphone tu.! je, hii ni faida au hasara?

    Ukiniuliza mimi nitakwambia hii ni hasara. unajua kwa nini? Umekaa kwenye treni au gari au ndege, hujasalimiana na mtu wa karibu yako. HUjajua ni nani n.k.

    • Halafu wewe huyohuyo kila siku unaomba uweze kukutana na watu wazito, unadhani utakutana nao kivipi? watashuka kutoka mbinguni? Hapana, inawezekana konekisheni unazozitafuta umeshapishana nazo mara nyongi tu kwa sababu ya kutozitumia. au kwa kuwa bize muda wote.

      USHAURI WANGU: Ukipanda usafiri au ukiwa kwenye mazingira ya watu, weka pembeni headphone hata kwa muda kwa ajili ya kusalimiana na watu. Usisafiri na mtu kwa saa mbili, bila kumjua vizuri. Unaweza kukuta huyo ni mteja mzuri wa bidhaa zako, unaweza kukuta anakuja kuwa msambazaji wa bidhaa zako, unaweza kukuta anakuwa mshirika wako muhimu na pengine anaweza asiwe chochote. Lkini haya yote yatawezekana kwa wewe kuhakikisha unakuwa na mazungumzo na huyu mtu

      SOMA ZAIDII: JINSI YA KUANZISHA MAZUNGUMZO NA MTU YEYOTE

    Fanya Kitu Hiki Kimoja Tu Kwenye Biashara Yako (Funzo Kutoka Kwa Makampuni Makubwa Kama Google, Facebook Na Amazon)

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza

    Jipatie vitabu vya Godius Rweyongeza kwa kuchagua HAPA.

    Wasiliana nami wasap hapa

    Hakikisha umepata kitabu cha RASILIMALI ZA WATU WENGINE, ni kitabu kizuri kwa ajili yako. wasiliana na 0755848391 au 0745848395 sasa

    Makala ya kesho itawekwa kwenye blogu ya SONGAMBELE ambayo unaweza kuifikia kupitia www.songambele.co.tz na itawekwa kwenye channel ya telegram pia ambayo unaweza kuifikia kwa KUBONYEZA HAPA

  • Kama huwezi kupaa, kimbia

    RAFIKI yangu mpendwa salaam, nichukue nafasi hii kukupongeza kwa kazi nzuri unayofanya.

    Moja ya kitu ambacho kimekuwa kinawakwamisha watu wengi kuandika ni kwa sababu hawana vifaa vya kuandikia. Ukweli ni kuwa muda mwingine si kwamba unahitaji kuwa na vifaa vya kipekee sana ili uandike, bali unapaswa uanze kuandika kwa kutumia vifaa ulivyonavyo.

    ANZA KUANDIKA kwa kutumia simu yako. Asilimia kubwa ya watu wanamiliki simu. Wewe kama mwandishi, itumie simu yako kuandika. weka app za kutumia kuandika kwenye simu yako, kama app ya Google docs kisha anza kuandika.

    HARIRI kitabu chako kwa kutumia simu yako. Baada ya kuandika, anza kuhariri kitabu chako kwa kutumia simu yako hiyohyo.

    Tengeneza Kava kwa kutumia simu. App ya Canva inaweza kukusaidia kwenye kutengeneza kava na hata kwenye kupangilia kitabu chako.

    SANIFU kitabu chako kwa kutumia simu yako pia. Inawezekana kutumia simu yako kwenye kusanifu maudhui na mwonekano wa ndani ya kitabu pia.

    Lakini pia kama una vifaa zaidi ya simu unaweza kuvitumia rafiki yangu.

    Ninachoweza kukwambia ni kwamba kwenye kuandika, tumia kile ulichonacho.

    Kama huna simu, andika kwenye daftari.

    kama huna tablet, tumia simu

    kama huna kompyuta, tumia tablet.

    ila kwa vyovyote vile usiache kuandika.

    Ningependa tu kukuuliza swali moja, ni lini utaweza KUANDIKA KITABU CHAKO NA KUKIKAMILISHA?

    SOMA ZAIDI: Vitu 50 Ambavyo Hupaswi Kuchukulia Poa

  • UNAMUONA DADA HUYO?

    UNAMUONA DADA HUYO?

    Wengi huwa likija suala zima la kuandika kitabu huwa wanapenda kuniuliza kuwa ni wapi wanaweza kupata wazo la kuandika kitabu.

    NImekuwa nikieleza mara kwa mara namna ya kupata wazo la kuandika kitabu.

    Na moja ya njia ambayo unaweza kutumia kwenye kupata wazo la kuandika kitabu ni ikama alivyofanya huyo dada hapo juu.

    Yaani, mazingira na matukio ambayo yanatokea unaendana nayo hivyohivyo

    Kwa dada huyo ambaye ni dancer, kitendo cha yeye kukutwa na kadhia ya kuanguka, amegeuza hiyo kuwa mwendo mpya wa kucheza. HIvyo hivyo kwangu mimi na wewe.

    matukio yanayotokea kwenye mazingira yetu yanaweza kugeuzwa kuwa chanzo cha kuandika.

    tunaweza kuyatumia kuandika kitabu, makala au andiko 

    lolote ambalo tunaona kwamba linafaa. Hivyo, usiogope rafiki yangu. kuwa utapata wapi wazo la kuandika. wazo la kuandika unalo hapo.

    Dada huyo amepata wazo la kutengeneza mwenendo mpya wa kucheza kutokana na tukio la kutaka kuanguka.

    Na mimi  nimepata wazo la kuandika makala hii baada ya kuangalia video yake

    wewe pia unaweza kupata wazo la kuandika kitabu chako kutokana na makala hii.

    Kama bado unajiuliza uandike nini, usiwe na wasiwasi, hakikisha unapata kitabu cha JINSI YA KUWA MWANDISHI MBOBEVU, unaweza kujipatia nakala yako popote pale ulipo kwa shilingi 30,000/- tu.

    Au unaweza kujipatia pakeji nzima ya vitabu vya uandishi.

    Pakeji hii inahusisha vitabu vifuatavyo.

    1. JINSI YA KUWA MWANDISHI MBOBEVU

    2. SEHEMU KUU MUHIMU ZA KILA KITABU

    3. ANDIKA KITABU CHAKO KAMA SMS

    4. MWANDISHI NI MUUMBAJI

    Hii ni pakeji kamili ya vitabu vya uandishi ambayo unapaswa kuwa nayo. Kuipata ni rahisi sana. Tuwasiliane kwa 0655848392

    image1758192352437.png

    Hivi ni vitabu ambavyo unapaswa kuhakikisha kwamba unavipata.

    Wengi huwa likija suala zima la kuandika kitabu huwa wanapenda kuniuliza kuwa ni wapi wanaweza kupata wazo la kuandika kitabu.

    NImekuwa nikieleza mara kwa mara namna ya kupata wazo la kuandika kitabu.

    Na moja ya njia ambayo unaweza kutumia kwenye kupata wazo la kuandika kitabu ni ikama alivyofanya huyo dada hapo juu.

    Yaani, mazingira na matukio ambayo yanatokea unaendana nayo hivyohivyo

    Kwa dada huyo ambaye ni dancer, kitendo cha yeye kukutwa na kadhia ya kuanguka, amegeuza hiyo kuwa mwendo mpya wa kucheza. HIvyo hivyo kwangu mimi na wewe.

    matukio yanayotokea kwenye mazingira yetu yanaweza kugeuzwa kuwa chanzo cha kuandika.

    tunaweza kuyatumia kuandika kitabu, makala au andiko 

    lolote ambalo tunaona kwamba linafaa. Hivyo, usiogope rafiki yangu. kuwa utapata wapi wazo la kuandika. wazo la kuandika unalo hapo.

    Dada huyo amepata wazo la kutengeneza mwenendo mpya wa kucheza kutokana na tukio la kutaka kuanguka.

    Na mimi  nimepata wazo la kuandika makala hii baada ya kuangalia video yake

    wewe pia unaweza kupata wazo la kuandika kitabu chako kutokana na makala hii.

    Kama bado unajiuliza uandike nini, usiwe na wasiwasi, hakikisha unapata kitabu cha JINSI YA KUWA MWANDISHI MBOBEVU, unaweza kujipatia nakala yako popote pale ulipo kwa shilingi 30,000/- tu.

    Au unaweza kujipatia pakeji nzima ya vitabu vya uandishi.

    Pakeji hii inahusisha vitabu vifuatavyo.

    1. JINSI YA KUWA MWANDISHI MBOBEVU

    2. SEHEMU KUU MUHIMU ZA KILA KITABU

    3. ANDIKA KITABU CHAKO KAMA SMS

    4. MWANDISHI NI MUUMBAJI

    Hii ni pakeji kamili ya vitabu vya uandishi ambayo unapaswa kuwa nayo. Kuipata ni rahisi sana. Tuwasiliane kwa 0655848392

    image1758192352437.png

    Hivi ni vitabu ambavyo unapaswa kuhakikisha kwamba unavipata.

  • Kama Isingekuwa Pesa, Ungekuwa Unafanya Unachofanya sasa

    Ndugu Godius Rweyongeza
    Ndugu Godius Rweyongeza

    Anaandika GODIUS RWEYONGEZA

    Wasiliana naye wasap hapa

    Mwaka juzi taarifa zilisambaa mtandaoni kwamba mchungaji mmoja huko nchini Uganda ameacha uchungaji baada ya kushinda milioni 100 kupitia kubeti. Kwa maneno yake huyu mchungaji alisema kwamba alikuwa anafanya kazi ya uchungaji kwa sababu hakuwa na fedha.

    Hiki kinatafakarisha sana. Kumbe tuna watu wanafanya vitu ambavyo hawapendi, na kila siku wanalazimika kwenda kufanya shughuli wanazofanya ila moyoni mwao hawapendi hivyo vitu.

    Je, wewe umo?

    Mtu mmoja alisema kwamba biashara za kitanzania ni ngumu sana. Kwa sababu pale biashara zinapoanza kupata faida inayoeleweka, ndipo watu wanataka kupata pesa zao na kuondoka kwenye biashara hizo badala ya kurudisha faida kwenye biashara. Kumbe kitu cha kwanza kilichokuwa kimewapeleka kwenye biashara hiyo si kutoa huduma, siyo kutatua matatizo yanayowakumba watu, bali ni pesa.

    Sasa swali llangu kwako siku ya leo ni kwamba kama isingekuwa pesa, je, unachofanya sasa hivi ungekuwa unakifanya? Najua utanza kusema sasa nitaishije bila yakuwa na pesa. Ni ukweli usiopingika kuwa pesa ni muhimu na inahitajika sana.

    Ila unatakiwa kupenda unachofanya.

    Kupenda unachofanya ni hatua moja mbele ukilinganisha na pale unapofanya usichokipenda.

    Kuna siku unaweza kuwa siku hiyo hujisikii kufanya kazi. Ila ukiwunapenda unachofanya utaendelea kupambana.

    SOMA ZAIDI: Kauli Yenye Nguvu: Ni bora Ufe Ukiwa unafanya unachopenda…

    Sasa kwenye makala ya leo tujadiliane vitu vitano vinavyopaswa kukusukuma kufanya kazi au biashara. Hii siyo kwa sababu hatutambui umuhimu wa fedha. Itambulike umuhimu fedha. lakini kwa hapa tuzungumzie hili. 

    sababu ya kwanza ni kutimiza kusudi lako. kila mmoja ana kusudi kubwa ambalo limemfanya awepo hapa duniani. 

    1. Kutimiza kusudi la kuwepo hapa duniani

    Kila mtu ameumbwa kwa kusudi fulani. Kazi au biashara unayofanya inapaswa kuwa sehemu ya kutimiza kusudi hilo. Unapofanya kazi kwa kuelewa kwamba unatekeleza wito wa maisha yako, hutachoka kirahisi, wala hutafanya mambo kwa kubahatisha.

    2. Kuwahudumia watu na kutatua changamoto

    Biashara na kazi yoyote yenye mafanikio makubwa inasimama juu ya msingi wa kutatua matatizo ya watu. Ukizingatia kusaidia na kuhudumia wengine, thamani yako itaongezeka, na kwa hakika pesa zitaingia kama matokeo.

    3. Kujenga historia

    Kila siku unayofanya kazi au biashara, unajenga hadithi yako ya maisha. Je, utataka watu wakikukumbuka waseme uliishi tu kwa ajili ya kutafuta fedha, au watasema ulileta mabadiliko makubwa? Kufanya kazi kwa lengo la kuacha alama ni nguvu ya pekee ya kukusukuma kila siku.

    4. Kukuza vipaji

    Kazi na biashara ni shule kubwa zaidi ya maisha. Inakupa nafasi ya kutumia kile kilicho ndani yako na pia kujifunza zaidi. Unapoliona hilo kama msukumo, utathamini kila changamoto na fursa kama nafasi ya kukua na kuwa bora.

     

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza

    Jipatie vitabu vya Godius Rweyongeza kwa kuchagua HAPA.

    Wasiliana nami wasap hapa

    Hakikisha umepata kitabu cha RASILIMALI ZA WATU WENGINE, ni kitabu kizuri kwa ajili yako. wasiliana na 0755848391 au 0745848395 sasa

    Makala ya kesho itawekwa kwenye blogu ya SONGAMBELE ambayo unaweza kuifikia kupitia www.songambele.co.tz na itawekwa kwenye channel ya telegram pia ambayo unaweza kuifikia kwa KUBONYEZA HAPA

     

     

  • Biashara ni Mkakati, Wa Kwako Ni Upi?

    Biashara huwa zinakuwa na mkakati wa biashara. Inawezekana wewe mwenyewe hujui kwamba una mkakati kwenye biashara, lakini kutoujua mkakati huo, haimaanishi kwamba haupo. Upo tu, tena umejaa tele. 

    Mkakati wa biashara tunaweza kuuona kwenye namna unavyofanya shughuli zako kwenye biashara yako. Sasa swali ni je, mkakati wa biashara unapaswa kugusa kitu gani na kitu gani?

    Washiriki wa semina ya Godius Rweyongeza
    Washiriki wa semina ya Godius Rweyongeza

    Kwenye biashara, mkakati wa biashara unaweza kuwa

    1.  KIla mmoja kwenye biashara kujua anachopaswa kufanya na lini kinapaswa kuwa kimekamilika na kukifanya kwa bidii, 
    2. Kila mmoja anapaswa kuwa anashambulia muda wote. Hakuna timu ya mpira wa miguu ambayo huwa inashinda kwa kulinda lango bali kwa kushambulia.
    3. Kuwa bora kwenye eneo fulani, bidhaa moja au huduma moja ambayo utafahamika kwayo kabla hujaanza kuzalisha bidhaa nyingine au huduma nyingine.
    4. Ni muhimu sana kwenye biashara kuhakikisha kwamba unatafuta njia ambayo ni bora, haraka, urahisi na ya uhakika kwa wateja.
    5. kwenye biashara kampuni zina watu wanaojituma kwenye kazi. Wanatumia neno kama sisi. Wanaona kampuni kama mwendelezo wao. na hawafikirii kwamba hiyo siyo kazi yangu.
    6. Kwenye biashara kila mara unaangalia namna ya kumshangaza mteja kwa kumpa huduma bora, ya haraka ya uhakika na 
    7. Kwenye biashara unatakiwa kulijua soko lako na kutengeneza mbinu za uhakika za kulifikia hili soko lako bila shida yoyote.

    hii ni baadhi ya mikakati muhimu sana unayoweza kuwa nayo.

    Ni mkakati upi unaenda kuanza nao siku ya leo?

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza

    Jipatie vitabu vya Godius Rweyongeza kwa kuchagua HAPA.

    Wasiliana nami wasap hapa

    Hakikisha umepata kitabu cha RASILIMALI ZA WATU WENGINE, ni kitabu kizuri kwa ajili yako. wasiliana na 0755848391 au 0745848395 sasa

    Makala ya kesho itawekwa kwenye blogu ya SONGAMBELE ambayo unaweza kuifikia kupitia www.songambele.co.tz na itawekwa kwenye channel ya telegram pia ambayo unaweza kuifikia kwa KUBONYEZA HAPA

  • SIAFU: Viumbe Wadogo Akili Nyingi. Mambo 12 Ya Kujifunza

    Wiki hii nimealikwa kufundisha kwenye kongamano la wanawake, jiandikishe na wewe uweze kuwepo

    Moja ya viumbe ambao wanatafakarisha sana ni siafu. ni viumbe wadogo lakini wanafanya mambo makubwa. Leo hii nataka tuzame kwenye namna wanavyofanya kazi na masomo ambayo tunaweza kujifunza kwa viumbe hawa wadogo, viumbe wadogo wanaofanya makubwa.

    1. Kufanya kazi, wanafanya kazi mpaka usiku. Viumbe hawa sijajua huwa wanalala saa ngapi, ila wanafanya kazi mchanana usiku.

    Hiki ni kitu cha kwanza kabisa tunachojifunza kutoka kwa hawa viumbe, kufanya kazi. Unakuta mtu anafanya kazi kwa saa nane tu, anaangalia tamthiliya saa zingine nane na kulala. Lakini kama unataka kufanya makubwa lazima uwe tayari kufanya kazi zaidi ya hapo. Tumeona kwa mfano, mabilionea wengi wameripoti kufanya kazi kati ya saa 12 mpaka 16 na wachache mpaka saa 18 kwa siku. Yaani, huu ni muda ambao mtu anaweka kazi tu. Ukweli ni kuwa kama unataka kufanikiwa na kufanya makubwa ni wewe kufanya kazi kama wanavyofanya waliofanikiwa. Hii ni siri kubwa sana unayotakiwa kuifahamu. Vile vitu wanavyofanya watu waliofanikiwa, wewe fanya kama wao. Nakuhakikishia kitu kimoja cha ukweli kwamba, utaweza kwenda mbali. Na kama kuna kitu cha kwanza kabisa cha kuanza nacho, basi anza na kufanya kazi.

    Mafunzo ya biashara na uchumi
    Mafunzo ya biashara na uchumi na Ndugu Godius Rweyongeza

    SOMA ZAIDI: KAMA UNATAKA KUFANIKIWA, KUBALI KULIPA GHARAMA

    2. Wakiamua jambo lao hawashindwi. Sisi tuliokulia vijijini tunawajua, wanakuamsha hata kama ni saa 5 usiku au saa 9 kwa sababu umelala kwenye njia waliyoplan kupita. Hapo kumbuka umelala ndani, ila wanapenya na wanaingia na wanakuamsha.

    Ninyi wengine mliokulia MJINI tupisheni, Unajua usingizi wa saa Tisa unavyonoga na hasa ukiwa mtoto, sasa muda ambao ndiyo umeanza kufurahia huo usingizi, siafu wanataka kupita na wewe unazingua umelala njiani kwao.  Unaonekana kikwazo, Na wao huwa hawana dogo, Kila jambo hata kama ni dogo wanalifanya kwa ustadi MKUBWA kama ambayo wangekuwa wanafanya kubwa. Kuna mtu eti unakuta anasema hii kazi siyo Ile ninayoipenda nifaifanya tu kwa sababu ya pesa, ikitokea kazi nzuri naacha naenda huko. Kajifunze kwa Hawa siafu.

    Hawafanyi jambo lolote kwa udogo. Wakiamua ndiyo wameamua. Huwa hawana cha kurudi nyuma

    3. Wakiamua jambo lao hawana Cha kuwazuia. Wanavuka mpaka mto wenye maji yanayotiririka kwa Kasi. Unaweza kwenda sehemu, maji yanaaptita kwa kasi ila waoa ndiyo wanavuka hapo bila stress. tayari wanajenga daraja lao na wanasonga mbele. Hiki kitu kinanikumbusha ule usemi wa Napolleon Hill unaosema kwamba lolote ambalo akili yako itaamua na kushikilia basi lazima italifikia. Kumbe na wewe ukiamua hakuna kinachoweza kukushinda. Inawezekana vizuri tu.

    SOMA ZAIDI: Unataka kufanya vitu vya tofauti? Siri hii hapa

    4. Wanapasiana taarifa kwa spidi kubwa. Ukiwaangalia siafu vizuri wakati wanaenda sehemu, kuna siafu ambao huwa wanaenda mbele na kuna ambao huwa wanarudi nyuma. Na hata ikitoea kwenye msafara wao ukawatibua kidodo, hawarudi nyuma wote, kuna wachache ambao huwa wanarudi nyuma kutoa taarifa kwa haraka kwamba huku kimenuka. Jiandae. Hili ni jambo muhimu sana la kuzingatia. Kwenye biasahra ili biashara yako iweze kwenda hatua ya ziada, lazima mawasiliano yawe ni ya hali ya juu, yawe ni ya haraka.

    Kwenye mahusiano, ili yaweze kudumu, lazima mawasiliano yawe mazuri. Mawasiliano ni njia bora ya kufanya makubwa, kupeana taarifa za msingi. ni ufunguo muhimu wa jambo lolote la maana unalotaka kufanya.

    SOMA ZAIDI: Jifunze Mawasiliano

    5. Ushirikiano kwao ndiyo KITU kinachowafanya kuwa tishio. Mchwa mmoja kama mchwa mmoja Haogopeshi na hawezi kufanya MAAJABU, hawezi kuvuka mto, ila wakiwa wengi hata nyoka anasubiri. Hawana Ile ya kusema Mimi ni jeshi la mtu mmoja, ujue kwanza binafsi Huwa siwapendi watu wanaosema kwamba wao ni jeshi la mtu mmoja, kwa sababu ni vigumu kwa mtu yeyote kuwa jeshi la mmoja. Ni vigumu sana. Unajua kwa Nini. Ili uwe jeshi la mtu mmoja labda uwe unaishi kwenye kisiwa, iwe kwamba wewe unapika chakula Chako mwenyewe, unajisafirisha mwenyewe, unalima mwenyewe kwa mbegu ulizotengeneza mwenyewe.

    Ukiona mtu anasema yeye ni jeshi la mtu mmoja ujue kabisa anajiamdalia njia ya kuangamia.

    Kwanza hakunaga JESHI ambalo tena unaweza kusema ni la mtu mmoja. JESHI NI NI JUMLA YA WATU. Hivyo huwezi kusema wewe ni jeshi wakati uko peke Yako. Sharti muwe wengi.

    SOMA ZAIDI: Dhana ya jeshi la mtu mmoja, je ni dhana halisi au tunahitaji kufikiri nje ya boksi?

    6. Ukimchokoza mmoja umewachokoza WOTE. Kama walikuwa wanafanya kazi wataacha hiyo kazi wakushambulie kwanza, halafu watarudi kuendelea na kazi. Hawacheki na yeyote. Hapa tunajifunza kitu muhimu sana, USHIRIKIANO. Tunapofanya kazi, tufanye kazi kwa ushirikiano. Tuwe kitu kimoja, kauli ya mmoja wetu iwe ni kauli ya wote.

    7. Hawana muda wa umbea. Haijalishi umewakasirisha kiasi Gani, wakishamaliza kukusambulia, hawakai kijiwemi na kunywa kahawa.  Wanaendelea na kazi yao ya mwanzo na kamwe hawajawahi kusahau kazi Yao.

    8. Wanafanya kazi wanayopenda. Hili siwezi kulithibitisha sana, ila moyoni ninashawishika kusema hivyo, unajua kwa Nini…kwa sababu huwezi kufanya kazi usiyoipenda kwa muda mrefu hivyo tena kwa kujituma. Hili ni somo ambalo na sisi tunapaswa kuondoka nalo, kwamba, tupende tunachofanya. Mtu mmoja aliwahi kusema kwamba ukifanya kazi unayopenda hutahisi kama unafanya kazi kamwe. Naye Albert Einstein alisisitiza hili aliposema kwamba, ukikaa na msichana unayempenda kwa saa mbili, utadhani ni dakika mbili. Lakini ukikaa kwenye jiko la moto kwa dakika mbili, utadhani ni saa mbili.

    Na mimi namalizia kwa kusema kwamba penda unachofanya.

    SOMA ZAIDI: FANYA UNACHOPENDA

    9. Kikwazo kwao ni njia. Huwezi kuwazuia siafu kwa kuwawekea kikwazo. Kwao kikwazo ni namna ya kusema kwamba endelea.  Kwenye maisha yetu ya kila siku pia tusiogope kikwazo. Ni ukweli usiopingika kwamba vikwazo vipo na vitaendelea kuwepo. Vikwazo kwetu isiwe changamoto, bali iwe ni njia. 

    10. Hawasubiri kusimamiwa, hawana kiongozi ila kazi zao zinajulikana. Kama kuna kitu kikubwa sana cha kujifunza kutoka kwa hawa siafu ni utendaji kazi wao. Wana mfumo wao mzuri unaohahakikisha kwamba majukumu yao yanaendelea kufanyika na kukamilika. Hiki ni kitu muhimu sana kwenye maisha na hasa kwenye biasahra. Kwamba uwe na namna ya kufanikisha kila majukumu bila kujali kitu gani kinatokea. Bila kujali nani yupo au nani hayupo kwenye biashara. Unaweza kuwaua baadhi ya siafu, lakini hakuna jukumu lolote la msingi kwao ambalo linakwama.

    Biashara yako inapaswa kuwa hivi. Iendelee kwenye hali zozote.

    Lakini pia wewe uwe kiongozi mwenyewe na kila mmoja awe kiongozi. Ufanye kazi na watu wanaoweza kujisimamia wao, siyo wale ambao lazima wasimamiwe au uwe nyuma yao muda wote ili waweze kufanya kazi. 

    SOMA ZAIDI: Usijilinganishe Na Wengine

    11. Wanatunza akiba. Hawajisahau. kuna wakati siafu huwa hawaonekani. Wakati wa mvua sana, au wakati wa jua kali. Wanajichimbia wanapojua wao wakila na kunywa. Kitu kikubwa tunachokiona kutoka kwao ni KUWEKA AKIBA. Wanaweka akiba mara zote wakati wa mavuno, sisi pia tuendelee kuweka akiba mara zote.

    SOMA ZAIDI: MAMBO MUHIMU KUHUSU KUWEKA AKIBA

    12. Ukizubaa umekwisha. Siafu hawana dogo, hata kaka kazi Yao ni ndogo, ila lazima waifanye kwa UKUBWA. Kuna walevi walikaa kwenye njia zake kesho yake wakakutwa wamekufa, maana Hawa wadudu hawana dogo au kama nilivyosema mwanzoni hawacheki yeyote.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza

    Jipatie vitabu vya Godius Rweyongeza kwa kuchagua HAPA.

    Wasiliana nami wasap hapa

    Hakikisha umepata kitabu cha RASILIMALI ZA WATU WENGINE, ni kitabu kizuri kwa ajili yako. wasiliana na 0755848391 au 0745848395 sasa

    Makala ya kesho itawekwa kwenye blogu ya SONGAMBELE ambayo unaweza kuifikia kupitia www.songambele.co.tz na itawekwa kwenye channel ya telegram pia ambayo unaweza kuifikia kwa KUBONYEZA HAPA

     

  • MTAJI:Kila Kitu Unachohitaji Kujua

    Ndugu Godius Rweyongeza akifundisha semina kwa wafanyabiashara. Wasiliana naye wasap kwa KUBONYEZA hapa

    Kwenye kitabu chake Cha MAISHA NI MTIHANI, Fr. Faustine Kamugisha anatupa tafakuri moja nzuri sana. Anasema maisha ni MTIHANI. Ukiwa na chakula ni MTIHANI, usipokuwa nacho ni MTIHANI pia. Ukioa ni MTIHANI na usipooa ni MTIHANI pia. Ukiwa na ndugu ni MTIHANI ila usipokuwa nao ni MTIHANI pia.

    Fr. Kamugisha kaainisha vitu ambavyo ni MTIHANI, na ukiangalia unaona kweli maisha ni MTIHANI, yaani KITU chochote ukiwa nacho tayari ni MTIHANI ila usipokuwa nacho ni MTIHANI pia.

    Tukichukukie mfano wa ndugu au marafiki, ukiwa nao ni mtihani. Ila pia usipokuwa nao ni mtihani mkubwa pia.

    Kwenye andiko langu la Leo ninazungumzia zaidi kuhusu MTAJI. Naam, MTAJI wa kuanzisha biashara, ukiwa nao ni mtihani, ila usipokuwa nao ni mtihani pia😁.

    SOMA ZAIDI: MITAJI 21 ILIYOKUZUNGUKA NA JINSI YA KUITUMIA

    Jinsi Ya Kupata Mtaji Wa Biashara

    Iko hivi kuna Watu wana changamoto kwamba wanashindwa kuanzisha biashara kwa sababu hawana MTAJI. Na kuna Watu wanashindwa kuanzisha biashara kwa sababu wana MTAJI. Hivi vitu ukivitafakari unaweza kuona kama masihala, ila ndivyo ukweli ilivyo. Nimewahi kueleza siku za nyuma kuwa Biashara Ni Zaidi Ya Mtaji PESA. Ila kwa mantiki ya makala ya leo, tujikite kwenye MTAJI PESA, na hata tukiongelea MITAJI mingine ambayo siyo pesa, mwisho wa siku tuone ni kwa namna gani inaweza kugeuzwa kuwa pesa? Hivyo, popote pale nitakapotumia neno mtaji kwenye makala hii, ifahamike kama Pesa ya kuanzisha biashara.

    Sasa swali ni kwamba nifanyeje ikiwa Sina MTAJI Ili niweze kupata MTAJI?

    Ukweli ni kuwa kama hauna MTAJI haupaswi kuogopa. Inawezekana kwa wewe kupata MTAJI vizuri tu endapo utaanza kutumia vitu ulivyonavyo Sasa hivi. Kwenye makala hii, vitu hivi sitavieleza kwa undani sana, ila kwa haraka nitakushauri ukasome kitabu cha NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA, ambacho sehemu ya tatu ya kitabu hiki, inaeleza kwa undani mitaji 21 iliyokuzunguka na jinsi unavyoweza kuitumia. Hivyo hapa ninaenda kutaja baadhi ya mitaji unayoweza kuanza kutumia mara moja.

    Moja Anza kutumia NGUVU ZAKO mwenyewe. Tafuta kazi yoyote halali unavyoweza kufanya kwa kutumia NGUVU Yako ukalipwa. Naomba ieleweke kwamba huwezi kukosa kila kitu, ukose mtaji PESA na ukose nguvu. Tumia ulichonacho kwanza (NGUVU) kupata ambacho hauna (MTAJI FEDHA). Na hata wahenga wetu waliwahi kusema kwamba mtaji wa maskini ni nguvu zake mwenyewe. chukua hiyo.

    Pili, tumia kipaji chako kulipwa. KIPAJI CHAKO NI DHAHABU. unachotakiwa kufanya ni kukitumia kipaji chako. Tena kwenye ulimwengu wa leo imekuwa rahisi sana kuonesha kipaji chako kuliko muda mwingine wowote, vitu ambavyo hapo zamani za kale vilikuwa vinaonekana kama haviwezekani, kwenye ulimwengu wa leo wa intaneti vimewezekana vizuri sana. Tumia mitandao ya kijamii kuonesha kipaji chako. Kama utakitumia vizuri, kitakulipa.

    Tatu tumia muda wako vizuri. Wahenga wetu walishatuambia kwamba muda ni mali. na kama muda huu ukitumiwa vyema maana yake unaweza kukuinua na kukusogeza sehemu nzuri. Moja ya kufahamu ni kwamba hakuna mtu mwenye muda wa kufanya kila kitu. Hivyo, ukiongea vizuri na watu unaweza kutumia muda wako kufanya baadhi ya vitu vyao na wao wakakulipa. Inawezekana mtu ana kipato kizuri, lakiini hana muda wa kuosha gari lake, wewe ukamsaidia kwa hilo, inawezekana mwingine ana kipato kizuri lakini hana muda wa kuandaa chakula kizuri kwa ajili ya afya yake na familia yake, wewe ukamsaidia kwenye hilo. Muda wako ni mali utumie vizuri. Na hata kama sasa hivi huna jambo kubwa linalokuingizia kipato kupitia muda wako, angalia vitu vidogo unavyoweza kuanza kuvifanyia kazi mara moja vikakulipa sasa au hata baadaye.

    SOMA ZAIDI: Jinsi ya Kuanzisha Biashara Kubwa Kwa Mtaji Kidogo

    Nne ni Ujuzi au uzoefu wako. Una ujuzi fulani, umekuwa unajua namna ya kuandaa matangazo ya kuweka mtandaoni, unajua kuendesha mitandao ya kijamii kwa manufaa, unajua kuhariri video au makala, unajua  kupamba, unajua kufundisha au chochote kile unachojua. Hicho ni pesa. Kiufupi ni kwamba mwenye ujuzi halali njaa. Kama una ujuzi na unalala njaa, kosa lako haujajua namna ya kuufanya ujuzi wako ukulipe, jifunze hilo. Na hapa nashauri ukasome kitabu cha KIPAJI NI DHAHABU ile sura ya tano, ya sita na ya nane pamoja na kitabu cha TENGENEZA PESA KWA KUUZA UNACHOJUA. Utanishukuru baadaye. Wasiliana na huyu akupe nakala yako. 0755848391 AU 0745848395 sasa hivi.

    Tano ni konekisheni ulizonazo. Hizi zitumie pia kupata mtaji, konekisheni ulizonazo unaweza kuzitumia kupata mtaji, au watu hao wakakuunganisha na wengine ambao wanaweza kuwa watu wenye manufaa kwako. Konekisheni zako ukizutumia vizuri zitakuinua kwa sababu hata baada ya kuanzisha biashara, utahitaji kutumia konekisheni zako kupata wateja. Kwenye makala ya kesho, nitaeleza zaidi juu ya suala zima la konekisheni. Usiikose, jiunge hapa ili kupata kiti cha mbele, ikitoka tu wewe unayo. JIUNGE HAPA

    Sasa kwenye hiki kipengele ninaishia hapa, kupata makala na mafunzo zaidi kuhusu MITAJI ILIYOKUZUNGUKA NA NAMNA UNAVYOWEZA KUITUMIA KWA MANUFAA, HAKIKISHA UNASOMA KITABU CHA NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA. 

    Ndugu Godius Rweyongeza akifundisha misingi ya kusimamisha biashara Imara
    Ndugu Godius Rweyongeza akifundisha misingi ya kusimamisha biashara Imara

    Swali nifanye biashara Gani endapo Nina MTAJI kidogo?

    Yes, ikitokea kwenye vitu ambavyo nimeainisha hapo mwanzo umevifanyia kazi na umeanza kupata MTAJI, Sasa unafanya biashara Gani na huu MTAJI kidogo.

    Ukweli ni kuwa ni biashara za kufanya kwa MTAJI huuhuu kidogo ni nyingi. Naweza nisiweze kuzitaja zote hasa kwenye makala hii ila nashauri uangalie vitu vifuatavyo kwenye hiyo biashara unayotaka kuanzisha.

    Moja, iwe biashara ambayo unaweza kuanzia kwa MTAJI kidogo

    Pili, iwe biashara ambayo itaingiza pesa KILA siku. Kwa vile MTAJI wako BADO ni kidogo, siahauri tuanze kufanya biashara ambayo itashikilia MTAJI wako kwa muda mrefu, badala yake iwe biashara ambayo unaweza kuuza kwa haraka na kupata Hela Kisha ukairudisha kwenye biashara.

    TATU, iwe biashara Kutoka kwenye sekta ambayo inapendwa na wengi. Kwa MTAJI kidogo ulio nao huna jeuri la kuanzisha biashara kwenye eneo ambalo utahitaji kutumia NGUVU kubwa kuwashawishi Watu, inatakiwa kiwe KITU ambacho Watu wamezoea na wewe utantumia NGUVU kidogo kuwaeleza Watu.

    NNe iwe biashara ambayo gharama za uendeshaji ni ndogo. Kwa kuanzia, usianzishe biashara ambayo utatakiwa kutumia gharama kubwa za uendeshaji kama ulipaji wa kodi, vifaa, watu, n.k Anza na biashara ambayo gharama zake za uendeshaji ni ndogo tu.

    Tano, anzisha biasahara ambayo unaweza kufanya hata katika mazingira ya nyumbani au siyo mbali na nyumbani. Yaani, isiwe biashara ambayo utaanza tena kusafiri umbali mrefu. Kumbuka unaanza na kile ulichonacho sasa, kisha unafanya yanayowezekana sasa kabla y akuja kufanya yasiyowezekana.

    Sita, iwe bishara ambayo unaweza kuongeza au kupunguza mtaji muda wowote. Mfano biashara ya matunda, leo unaweza kuwa na mtaji wa kununua matunda tenga moja, kesho ukanunua tenga mbili. Kesho kutwa mtaji ukipungua unauza tenga moja kama kawaida.

    saba iwe ni biashara inayohitaji ujuzi ulio nayo tayari, na si biashara ambayo inakuhitaji uanze kusoma sana kwanza.  Kumbuka unapaswa kuanza Na Ulichonacho kwanza

    Nane iwe ni biashara unayoweza kutangaza kwa gharama kidogo. Kama unavyojua kila biashara inahitaji ufanye masoko. Sasa wewe huhitaji kuanzisha biashara ambayo itakugharimus ana kwenye masoko. Iwe ni biashara ambayo unaweza kufanya masoko ya gharama nafuu kama wasap status, kutumia profile yako ya facebook, ambayo unaweza kutangaza kwa gharama za chini ambazo unazimudu na ziko ndani ya uwezo wako kwa sasa.

    Siku siyo nyingi nimeanza kulima uyoga, sehemu ya matangazo niliyofanya ilikuwa ni kutengeneza bango kwenye karatasi za kawaida, na kubandika maeneo yaliyokuwa na watu niliokuwa nawalenga. Matangazo haya ambayo hayajagharimu zaidi ya elfu mbili kutengeneza, tayari yananiletea watu wa maana kabisa. Hii ndiyo kusema kwamba baadaye nikitengeneza mengine, nitapata wateja wengi zaidi.

    SOMA ZAIDI: Unawezaje Kujiajiri kwa Mtaji Kidogo?

    Tisa, Iwe ni biashara ambayo inaleta wateja mara kwa mara. Siyo mteja akinunua mara moja ndiyo imeisha. Iwe ni biasahra ambayo mteja akinunua leo anaweza kununua tena baada muda fulani. Nikienda kunyoa leo, siyo zaidi ya wiki mbili zijazo nitalazimika kwenye kunyoa. Nikinunua maziwa leo, nitayahitaji na kesho, nikinunua majiya kunywa asubuhi naweza kuyahitaji mchana au jioni. Biashara za namna hii nzuri kwa kuanzia.

    Kumi, iwe ni biashara ambayo inaweza kukua. Kumbuka lengo la kuanzisha biashara ni kwamba siku moja unataka kuwa mkubwa kibiashara, iwe ni biashara inayoweza kukua zaidi ya unayoianzisha hapo. Kwamba unaanza na kuuza mayai trei moja, baadaye unauza tano, baadaye unauza trei 1000 na kuendelea. 

    Hakikisha pia unapata kitabu cha MAMBO 55 YA KUZINGATIA KABLA YA KUANZISHA BIASHARA. Kipate kwa kuwasiliana nami kwa simu 0755848391 au tumia 0745848395

    Sasa je, ikiwa una MTAJI mkubwa ni biashara ipi unaweza kufanya?

    Ukweli ni kuwa KANUNI za kuanzisha biashara ni zilezile hazijabadilika. Misingi ya kusimamia biashara ni ileile haijabadilika pia. Muhimu unapoanzisha biashara ya namna hii hakikisha

    Moja unaangalia eneo lenye tatizo na uhitaji wa watu. 

    pili, angalia tatizo ambalo linawasumbua sana watu na wewe unaweza kulitatua

    tatu, angalia biashara ambayo inafanyika ila inafanyika kiholela, wewe unaweza kuweka ubunifu wako na kuifanya kitalaam na kibobevu zaidi. Inawezekana inafanyika na ina wateja ila wanaoifanya hawana nguvu ya mtaji ya kuleta bidhaa zinazotakiwa kwa wateja kwa wakati kwako hii inaweza kugeuzwa kuwa fursa.

    SOMA ZAIDI: 

    Ifahamu kanuni ya copycat

    Ni muhimu sana kufahamu kwamba kwa biashara yoyote unayoianzisha ndani ya miezi sita kuna watu wataona biashara hiyo inafaa na wao watakuwa tayari kuianzisha. 

    SOMA ZAIDI: WAZO LA BIASHARA AINA HII LAHUWEZI KULIPATA

    Kazi ya kufanya leo

    Leo nataka nikupe kazi muhimu sana. Zunguka mtaani na notebook, kisha angalia biashara zinazofanyika. andika kila bango la kila biashara unayoona. 

    Kisha jiulize ni biashara gani unaweza kufanya, ni biashara ipi inafanyika kwa kawaida mimi naweza kuiongezea ubunifu?

    Hakikisha umepata kitabu cha RASILIMALI ZA WATU WENGINE, ni kitabu kizuri kwa ajili yako. wasiliana na 0755848391 au 0745848395 sasa

    Makala ya kesho itawekwa kwenye blogu ya SONGAMBELE ambayo unaweza kuifikia kupitia www.songambele.co.tz na itawekwa kwenye channel ya telegram pia ambayo unaweza kuifikia kwa KUBONYEZA HAPA

X