-
Usikose mara mbili
Rafiki yangu, kwenye makala ya jana nilikusisitiza kitu kimoja muhimu sana. Kitu hiki ni kufanya kila unachofanya kwa msimamo, na kwa mwendelezo. Kama hukusoma hii makala, rudi hapa uisome kwa umakini mkubwa.
Msimamo na mwendelezo.
Kitu hiki ni kutokuacha kufanya kitu husika zaidi ya mara mbili. Ikitokea kuna siku umeshindwa kufanikisha kitu fulani ambacho umepanga kufanya, basi walau kesho yake usishindwe kufanya hivyo.
Usikose mara mbili. Kosa leo ila siyo na kesho pia.
Pambana kadiri ya uwezo wako kuhakikisha haukosi kufanya jambo ulilopanga kufanya mara mbili mfululizo.
Kama umepanga kuweka akiba, pambana uwezavyo usiache kuweka akiba mara mbili mfululizo. Kama umepanga kuwekeza, pambana kadiri iwezekavyo ushindwe kufanya hivyo mara mbili mfululizo.
Ukiona umekosa siku ya kwanza, kufanya jambo fulani. Ukaona na siku ya pili pia hujaweza kufanya hivyo, basi ujue wazi kuwa hutaweza kuwa na mwendelezo kwenye jaambo lako na itakuwa vigumu kwako kuweza kufikia mafanikio makubwa
Sasa swali la pekee ambalo n ingependa kukuacha nalo siku ya leo ni kwamba, ni kitu gani ambacho umekuwa unatamani kufanya kwa mwendelezo? Na ni kwa namna gani unaenda kukifanyia kazi kuanzia sasa hivi?
Tukutane kwenye makala ya kesho
-
Msimamo na mwendelezo
Rafiki yangu moja ya kitu cha muhimu sana kwa wewe unayetaka kufanya makubwa ni kuwa na mwendelezo kwenye kitu ambacho unafanya. Wengi huwa wanaweza kufanya kitu mara moja, ila siyo kwa mwendelezo. Wewe unahitaji kuwa na mwendelezo kwenye kazi na shughuli zako zote unazofanya.
Ukianzisha kitu, usikifanye mara moja tu. Bali kifanye kwa mwendelezo kwa siku nyingi zinazofuata. Mafanikio ya kweli yapo kwenye kufanya vitu kwa mwendelezo ba siyo kufanya mara moja tu.
Wengi huwa wanaweza kuanza kuweka akiba, ila siyo wote wanaweza kuwa na mwendelzo kwenye kuweka akiba.
Wengi huwa wanaweza kuanza kufanya mazoezi, ila siyo wote ambao huwa wanakuwa na mwendelezo kwenye kufanya mazoezi. Wengi huwa wanaweza kuanza kunoa vipaji vyao, ila siyo wote ambao huwa wanakuw ana mwendelezo kwenye hilo.
Na kwa sababu tu ya kukosa mwendelezo wengi huwa wanaishia kujishangaa kwa nini hawapati matokeo na mafanikio makubwa. Kumbe kinachowafanya wasipate mafanikio makubwa ni kwa sababu hawana mwendelezo kwenye kufanya kile ambacho wanaamua kufanya.
Sasa rafiki yangu naomba nikwambie kitu kimoja muhimu sana. Kwa kitu chochote ambacho utachangua kufanya mwaka huu, hakikisha kwamba unakuwa na mwendelezo. Usifanye kitu na kuishia njiani. Bali kifanye kwa msimamo na kwa muda mrefu.
Tukimwangalia mtu kama Warren Buffet ambaye amekuwa anawekeza tangu ana miaka 11 mpaka leo hii, tunachojifunza kwake ni kwamba amekuwa anawekeza kwa mwendelezo na kwa msimamo.
Tukisoma historia ya mtu kama Kobe Brayant tunagundua kwamba alikuwa anaamka mapema na kuanza kufanya mazoezi, na anachelewa kulala. Na hii ndiyo ilikuwa ratiba ya kila siku. Unachogundua hapo ni mwendelezo.
Au hata ukisikia Michael Jordan anasema kwamba, nimeshindwa mara nyingi sana ndiyo maana nashinda. Ni kwa sababu anakuwa na mwendelezo.
Wewe pia kuwa na mwendelezo kwenye kitu ambacho unafanya.
Usifanye kitu mara moja tu.
Usifanye mara mbili. Hapana
Fanya kwa mwendelezo na kwa msimamo. Kwa muda mrefu bila kuacha.
Makala hii imeandikwa name rafiki yako wa ukweli.
Godius Rweyongeza
Tuwasiliane sasa kwa namba ya simu 0755848391
Karibu sana
-
Mwezi januari unaisha, umeulaani au umeubariki? Umekuwa wenye Baraka kwako au wenye karaha?
Rafiki yangu mpendwa, nichukue nafasi hii kukupongeza sana kwa kuumalizia mwezi wa Januari. Najua wazi kuwa haujawa mwezi rahisi, hivyo nikupongeze sana kwa hilo.
Mwezi januari unapofikia tamati, ningependa kwa pamoja tufanye tafakari kuhusiaa na mwezi huu wa kipekee. Mwisho wa siku tujiulize kuwa mwezi huu umeubariki au umeualaani? Umekuwa wenye Baraka kwako au wa karaha?
Kila mwaka huwa kuna mwezi Januari na kila mwaka kuna mwezi Disemba.
Na sote tunafahamu kwamba kuna majukumu ambayo yako mbele yetu.
Kwa wengi tunajua kwamba ukifika mwisho wa mwaka na hasa sikukuu, kuna sherehe. Kwa wengi matumizi ya pesa huwa yanakuwa juu. Huwa yanahusisha kusafiri kutoka mkoa mmoja kwenda mwingine kitu ambacho huwa kinaongeza gharama za matumizi na kuzifanya kuwa kubwa zaidi
Kwa kuwa huwa ni sikukuu huwa tunaenjoy, lakini wakati huohuo ni kama huwa tunasahau majukumu yetu ya muhimu.
Majukum ya januari. Kwa upande mwingine ni kwamba Januari ni mwezi wa kipekee pia. kwa kuwa watoto huwa wanafunga shule disemba yote, januari baada ya sikukuu kuisha, huwa ni muda wa watoto kurudi shule sasa ili wasome.
Na hapa ndipo swali langu la kwanza linapojikita leo. Januari inapoisha umeibariki au umeilaani?
Najua unajua wazi kwamba una watoto wako. Labda mmoja au wawili, watatu n.k
Hiki siiyo kitu ambacho mimi napaswa kukufundisha si ndio?
Lakini pia unajua wazi kwamba watoto hawa wanapaswa kwenda shule Januari au la! Kwa mfano leo hii unaposoma hapa, unajua mwakani kwamba wanao watakuwa wanaenda shule au watakuwa hawaendi. Kama watakuwa wanaenda maana yake maandalizi ya mapema yanatakiwa kufanywa kuanzia leo hii. Changamoto ya watu wengi ukiwaambia wafanye maandalizi ya ada ya mtoto mwkani wanaona ni kitu cha ajabu sana. Wengi wataishia kukwambia siku bado. Lakini sasa unabaki unajiuliza. Bado nini? Sasa mtu huyuhuyu subiri ifike januari.
Ndiyo anaanza kukwambia Januari ni ngumu na hizi ada za watoto. Sasa kwa maneno hayo unakuwa unaibariki Januari au unakuwa unailaani? Je, watoto wako unakuwa unajivunia kuwa nao au unalaumu?
Yaani, ni kama vile hao watoto kuna mtu aliwaleta kwako ghafla na kukuamuru kwamba kuanzia leo hii hawa ni watoto wako, walee. Lakini kumbe watoto umewazaa mwenyewe, umewalea mwenyewe na sasa hivi kukosa kwako mipango ndiyo unaanza kuilaani Januari, na hata watoto wako unaanza kuwaona kama karaha? Haya ni ya kweli? Ebu jirekebishe bwana kuanzia mwaka 2025.
Ujue kama unaweka malengo, huwa kuna malengo ambayo yanajirudia kila mwaka. Lengo la kulipa ada kila januari liweke kama lengo ambalo linajirudia kila mwaka.
Pengine badala ya kusubiri kulipa ada Januari, unaweza kuwa unailipa mapema. Disemba au novemba.
Nakumbuka mwishoni mwa mwaka jana nilikutana na mama mmoja aliyekuwa anajiandaa kwenda uchagaani kwa ajili ya likizo. Lakini kabla ya kufanya maandalizi ya kitu chochote, kitu cha kwanza alichofanya ilikuwa ni kuhakikisha amelipa ada zote za watoto.
Siku hiyo nilikutana naye njiani anatabasamu, ikabidi nimuulize kulikoni, ndipo aliponiambia kuwa nimelipa ada zote za watoto, hapa hata nikienda nyumbani nikajisahau nikatumia hela zote, nitakuwa bado na uhakika wa ada za watoto kuwa zimelipwa.
Nilichojifunza kwa mama huyu ni kwamba, badala ya kusubiri mpaka Januari uanze kulalamika kuhusiana na watoto wako, ANZA KUANDAA HIZI ADA MAPEMA. Kisha jipange kuhakikisha kwamba unailipa mapema kabla hujaila.
Unapolalamika kuhusiana na kulipa ada Januari wakati ni wajibu wako. Ni kama unakuwa unaona karaha kuwa watoto wako. Ni kama unakuwa unawalaani kuwa bora wasingezaliwa.
Makala hii imeandikwa na
GODIUS RWEYONGEZA
Unaweza kuwasiliana naye kwa simu 0755848391
-
Hii Kozi Nayo Inalipa Vizuri Sana; Sema Watu Hawaijui Tu
Moja ya kitu ambacho wazazi bado wanawaambia watoto ni kwenda kusomea kozi au kitu fulani kwa sababu wanahisi kinalipa. Mzazi anamwambia mwanae akasomee uhasibu kwa sababu yeye anahisi unalipa kuliko vitu vingine vyote, au anadhani mtoto wake atapata ajira.
Nafikiri ushauri wa namna hii ulikuwa ni ushauri halisi miaka kadhaa iliyopita, ila leo hii hauwezi kuwa bado ni ushauri halisi. Kwenye ulimwengu wa leo kuna mabadiliko mengi ambayo tayari yanatokea na sisi tunayaona.
Ujio na uwepo wa AI umepindua karibia kila kitu, vitu vingi ambavyo mwanzoni tulikuwa tunadhani haviwezi kufanywa na mashine leo hii tunashuhudia kwa macho yetu vikifanywa na mashine.
Kuna watu wanahudumiwa migahawani na akili bandia
Kuna mashine zinapika chakula
Kuna mashine zinatibu wagongwa
Kuna mashine ziko vizuri kwenye kufanya hesabu na zinakupa ushauri mzuri kutokana na takwimu ulizonazo.
Kwa lugha ya vijana naweza kusema kwamba disco limevamiwa na mmasai. Hakuna kozi, au kitu chochote ambacho unafikiri kwamba mwanao anaweza kusomea ambacho hakiwezi kufanywa na mashine. Kama mashine zinaweza kufanya ulinzi ambao kwa miaka mingi uliaminiwa mikononi mwa polisi na jeshi unadhani zitashindwa kulima, kumwangilia au kuzuia wadudu shambani?
Kama kuna sehemu ambazo hazina mashine basi ujue pengine watu wanaofanya kazi kwenye eneo husika hawajaanza kuzitumia au hawajafuatilia kujua kama zipo. Lakini ni suala la muda tu hizo mashine wataanza kuzitumia.
Sasa kwenye ulimwengu unaobadilika kwa kasi hivyo, ni vigumu sana kumwambia mwanao kwamba nenda shuleni usome kozi fulani kwa sababu inalipa zaidi
Mimi kwa maoni yangu naona huu ni ushauri wa kizee. Badala yake mzazi unapaswa kumshauri mwanao.
- Aendeleze kipaji, elimu au kitu chochote ambacho roho yake inapenda. Afanye kitu roho inapenda, ila siyo kufanya kitu ambacho analazimishwa kufanya. Kumbuka hiki kitu anaenda kukifanya kwa miaka mingi inayokuja mbele yake. Na kama hiki kitu akikifanya vizuri, nakuhakikishia kwamba hatakosa hela ya kula. Kuna watu wapo tayari kumlipa, endapo atakuwa anafanya hicho kitu kwa bidii na kwa nguvu zake zote.
- Mwanao afahamu wazi kuwa kufanya kazi kwa bidii kunalipa sana. Kunaweza kumkutanisha na wafalme, hata kama siyo mfalme.
- Aaminike. Katika ulimwengu ambapo watu wanasema kwamba uswahili na utanzania umetawala. Katika ulimwengu ambapo mtu anaweza kukuahidi kitu na asikifanyie kazi. Katika ulimwengu ambao mtu anaweza kuwa na haraka na kazi ila akazungushwa licha ya kwamba amelipia. Mwambie mwanao aaminike. Mwambie kwamba akimwambia mtu njoo kesho uchukue kazi yako, iwe ni kesho kweli na asirembe mwandiko kwenye hilo. Nakuhakikishia kitu kimoja cha uhakika kwamba, mwanao ataweza kupata soko la uhakika miongoni mwa watu kuliko pale akisomea hicho kitu ambacho unadhani kwamba atalipwa vizuri huku akiwa hafanyi kazi kwa bidii.
- Ndiyo yake iwe ndiyo yake na hapana yake iwe hapana yake. Akisema neno, ahakikishe analitimza. Atalipwa zaidi ya mtu mwingine yeyote, nakuhakikishia.
- Ajenge sana ujuzi wa kuwasiliana. Sisi ni watu na tutaendelea kuwa watu. Hata kama zinakuja mashine,. Haziondoi utu wetu. Bado nitapenda kuhudumiwa kiutu. Kuna vijana wamesomea kozi nzuri sana, wanajua vitu haswa, ila hawajui kuhudumia watu na hawajui kuongea vizuri na wateja. Ninvyoandika hapa, jana kompyuta yangu ilipata shida, nikaipeleka kwa fundi. Fundi huyu yuko vizuri sana kwenye kutengeneza hizi mashine, ila changamoto yake ni moja tu, uwezo wake wa kuwasiliana na watu ni mdogo sana. Huwa ninamtumia kwa sababu tu, ANAIWEZA KAZI. Iila kwa mfano akitokea mtu ambaye anaiweza kazi kama yeye na anajua kuongea vizuri na watu, anajali n.k. nakuhakikishia huyu fundi naweza kumhama ndani ya usiku mmoja tu. Kwa sababu utu bado tunaupenda. Ni kupitia kuwasiliana ndiyo tunajua namna unavyojali utu wa watu au la! Mwambie mwanao ajifunze sana kuwasiliana na watu itamsadia kwenye kazi yake
- Mwmabie mwanao pamoja na hicho ambacho anataka kusomea au kufanyia kazi, ajifunze kuuza pia. kwenye uliwengu wa leo, kuuza ni lazima. Kujua kitu bila kujua kuuza ni kazi bure. Lazima ajue namna ya kuwashawishi watu wngine ili wawezekununua kitu hicho.
- Mwambie pia mwanao kwamba hata baada ya kuwa amemaliza masomo asiache kujifunza. Kwake kujifunza kuwe ni kila siku. Atenge muda asome kitabu, atenge muda ajifunze kozi mtandaoni. Katika ulimwengu ambao unabadilika kwa kasi. Kujifunza ni tiketi muhimu ya yeye kuendelea kuwa mbele na kufanya makubwa. Mwambie kamwe asiache kujifunza.
- Mwambie kwamba muda ni mali. Aache na dhana ya kwamba hakuna haraka barani afrika, badala yake ajali muda siku zote. Apangilie ratiba zake vizuri na azifuate. Akimwambia mtu kwamba tukutane saa 10 ahakikishe kwamba hiyo saa 10 ameweza kukutana naye kwelikweli.
Kuna mengi ya kumwambia ila kwa sasa mwambie azingatie hayo. Nakuhakikishia kuwa mwanao ataweza kufanya makubwa kwenye ulimwengu huu unaobadilika kuliko tu wewe kumwambia kwamba akasomee kozi fulani kwa sababu inalipa, bila kumwambia vitu vya ziada kama hivi.
Imeandikwa na Godius Rweyongeza
Unaweza kuwasiliana na mwandishi kupitia namba ya simu 0755848391
-
JICHANGAMOTISHE
Uliwahi kufanyika utafiti kwa madereva waliokuwa wanaendesha taxi zao kwenye jiji la LONDON, moja ya kitu cha kipekee sana kilichogundulika kwa madereva hawa wa jiji la LONDON ilikuwa ni kwamba ubobgo wao ulionekana kuwa imara sana, ukilinganisha na madereva wengine ambao walikuwa hawaendeshi magari yao kwenye mazingira yenye barabara nyingi na idadi kubwa kama London.
Ikagundulika kwamba kwamba, kumbe changamoto za kuendesha gari kwenye mazingira yenye idadi kubwa, barabara nyingi, kona nyingi na vingine vingi, vilifanya ubongo wa watu kuwa imara zaidi.
Leo nataka niongee na wewe rafiki yangu ambaye siku zote huwa unaogopa changamoto na vikwazo. Unaviona kama jela vile. Ukweli ni kuwa changamoto na vikwazo ambavyo unakutana navyo kila mara vipo kwa ajili ya kukuimarisha. Vinakupa somo jipya kwenye maisha ambalo kama ukilifanyia kazi utazidi kuwa imara zaidi na utaweza kufanya makubwa.
Vikwazo vinaibua ukuu uliolala ndani yako. hivyo, usiogope unapokutana na vikwazo, bali vipende vikwazo, vikumbatie.
Huwa napenda kuwaambia watu kuwa vikwazo ni kama darasa. Ukishavuka darasa unaona maswali ya darasa la nyuma ni rahisi. Lakini ukweli ni kuwa kuna wakati maswali hayahaya yalikuwa yanakugalagaza, ila kwa sababu hukuyakimbia ndiyo maana sasa hivi ukiangalia nyuma unaona ni rahisi sana.
Hivyo, na wewe usiogope vikwazo, nakuhakikishia kuwa utakapokuwa umeweza kuvuka hivi vikwazo. Utaangalia nyuma na kuona kwamba ni rahisi sana kuvuka hivi vikwazo, utaangalia nyuma na kusema kwamba, mbona hapo ni rahisi?
Lakini usipovuka hivi vikwazo, utabaki kusema kikwazo fulani ni kigumu sana.
Na hata wengine utawaambia kwamba haiwezekani kuvuka kikwazo fulani, utawaambia kwamba haiwezekani kwa sababu, wewe mwenyewe ulishindwa kuweka juhudi kuvuka hicho kikwazo kwa wakati husika.
Ni kikwazo gani ulichonacho kwa sasa hivi? Je, ni kikwazo cha kuweka akiba? Unaona kwamba ukiweka akiba, hela haitoshi? Hiki kinaweza kuwa kikwazo kwa sasa hivi, ila fanya kitu kimoja, amua kwamba liwalo na liwe. Mimi nitaweka akiba tu. Kama nitakutana na changamoto au kikwazo chochote, nitapambana mpaka nishinde. Nakuhakikishia kuwa utashinda na kuna siku utaangalia nyuma na kuona kwamba MBONA HAPO NI RAHISI TU?
Pengine kikwazo chako ni kwenye kufanya KIPAJI CHAKO KIJULIKANE. Hilo ndilo jambo ambalo unapaswa kuwa unalipambania. Lipambanie kwa nguvu zako zote, na kamwe usirudi nyuma. Kuna siku utaangalia nyuma na kusema kwamba MBONA HAPO NI RAHISI tu, utaweza kusema hivyo kwa sababu tu, uliweza kuvuka kikwazo ambacho kilikuwa mbele yako kwa wakati husika. Hukutaka kubaki nyuma na wala kukwamishwa na mtu au kitu chochote.
Kwa leo tuishie hapa
Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.
Tuwasiliane kwa 0755848391
-
Huhitaji kusubiri mpaka uwe na kila kitu
Ni mara nyingi sana watu huwa wanasubiri mpaka wawe na kila kitu ili waweze kuanza kuanza kufanyia kazi malengo yao, ndoto zao, au kitu ambacho wanafikiria. Mtu haanzi hiyo biashara kwa sababu anasubiri mpaka aweze kupata kila rasilimali ambayo anafikiri anahitaji. Mtu haanzi kufanyia kazi hicho kipaji chake kwa sababu anasubiri mpaka awe na kila kitu ili aweze kufanyia kazi hicho kipaji chake.
Kusubiri mpaka uwe na kila kitu ili uweze kufanyia kazi malengo na ndoto zako kunaweza kukufanya usianze kabisa. Unakuwa ni sawa na mtu ambaye anasubiri ashibe ili aanze kula. Huwa hatuanzi kula tunapokuwa tumeshiba, bali huwa tunaanza kula hata kama hatujashiba. Wewe pia anza kufanyia kazi malengo na ndoto zako bila kuchelewa.
Unachohitaji kujua ni wapi unaelekea.
Ni rasilimali gani ulizonazo ambazo unaweza kuanza nazo. Hili pia ni muhimu kwa sababu, huwezi kuanza kufanyia kazi malengo na ndoto zako kubwa kama hauna kila rasilimali, unaweza kuanza kufanyia kazi malengo na ndoto zako kwa rasilimali hizo hizo kidogo ulizonazo. Ukweli ni kuwa uhaba wa rasilimali, ndiyo huwa unatengeneza kampuni imara na watu imara. Muda mwingine uwepo wa kila rasilimali huwa unafanya watu wanabweteka na hata wanashinda kutumia vizuri hizo rasilimali. Lakini rasilimali zinapokuwa haba, maana yake ni kwamba hao watu wanaongeza juhudi na bidii katika kuhakikisha kwamba wanatumia kile kidogo walichonacho kufanya makubwa.
Mfano wa nchi ambayo ilionesha uwezo wa kufanya makubwa kwa kutumia rasilimali kidogo ilizokuwa nazo ni Japani. Baada ya vita ya pili ya dunia, Japani ilikuwa kwenye hali mmbaya. Hali yake ya uchumi ilikuwa chini, miji yake miwili mikubwa ilikuwa imelipuliwa na mabomu.
Lakini bado katika mazingira haya, viongozi hawakuachakuota ndoto kubwa ambazo wangeweza kuzifanyia kazi. Hatimaye walianza kuzifanyia kazi.
Kufikia miaka ya sabini na themani, Japani iliingia miongoni mwa nchi ambazo zilikuwa na uchumi mkubwa sana hapa duniani. Lakini hii yote ilitokana na uwezo wa kutumia rasilimali haba ambazo zilikuwepo. Kumbe hii ndiyo kusema kwamba, ukiwa na rasilimali fulani kwa uhaba basi usiogope. Jifunze namna bora ya kuzitumia hizo rasilimali chache kwa ubora, ili ziweze kuleta manufaa makubwa.
INAWEZEKANA KUFANYA MAKUBWA KWA KUTUMIA RASILIMALI CHACHE ULIZONAZO.
Unahitaji pia kujua ni watu gani unaambatana nao. Ukiambatana na watu sahihi, watakuonesha wewe namna unavyoweza kuanza kwa kutumia rasilimali zako hizo. Kumbuka kuwa wengi unaowafahamu leo hii kama watu waliofanya makubwa hawakuwa watu ambao walikuwa wana kila kitu walipoanza. Walianza kufanya kwa kutumia rasilimali ambazo walikuwa nazo, baadaye wakaendelea kuboresha na kukuza kile walichokuwa wanafanya.
-
Maswali Mawili Ambayo Unapaswa Kujiuliza Kila Siku
Rafiki yangu, kuna maswali mawili mazuri sana ambayo unapaswa kuwa unajiuliza kila siku. Haya maswali yatakufanya utafakari juu ya mambo mengi ambayo unafanya kila siku na namna gani unaweza kuendelea kuifanya hii dunia kuwa sehemu bora kabisa kuwahi kutokea.
Maswali haya tunayapata kutoka kwa Benjamin Franklin ambaye alikuwa ni mmoja wa wanasiasa, mvumbuzi na mwanadipolomasia wa Marekani. Ni masawli ambayo alikuw anajiuliza miaka hiyo, na aleo hii bado tunaweza kujiuliza hayo maswali na tukapata matokeo mazuri pia kwenye maisha yetu.
Swali la kwanza kabisa ambalo Benjamin Franklina alikuwa anajiuliza lilikuwa ni ni je, ni kitu gani ambacho ninaenda kufanya leo kikawa msaada kwa watu wengine leo?
Tunapojiuliza swali hili tunaondoka kwenye dhana ya kujifikiria sisi wenyewe kwanza. Badala yak e tunaanza kuwafikiria wengine kwanza. Mpaka hapo unaweza kuwa unajiuliza, hivi kwa nini napaswa kuwafikiria wengine badala ya kuanza kujifikiria mimi mwenyewe. Ukweli wa hili tunaweza kuupata kwa kuisikiliza nukuu ya Zig Ziglar inayosema kwamba, unaweza kupata chochote unachotaka kama utawasaidia wengine kupata wanachotaka. HiI NDIYO Kusema kwamba kuwafikria wengine ni namna moja ya kujififikiria wewe kwanza. Maana unaweza kupata chochote unachotaka, ila kikubwa unapaswa kuwa tayari kuwasaidia wengine kwanza.
Ebu tuone mfano wa mtu ambaye anafungua duka mtaani kwako. Huyu mtu anapofungua duka maana yake kuna kitu choa tofauti ambacho anakuwa tayari ameshaona, hakipo au kinalegalega. Inawezekana unapoenda dukani kwenye duka zilizopo kununua bidhaa huzipati zote sehemu moja, unalazimika kununua bidhaa moja hapa na nyingine pale. Sasa huyu jamaa anaweza kuwa amaeona hilo gepu na hivyo, akaamua kulitumia vizuri sana. Badala ya wewe kwenda duka fulani, ukanunua bidhaa moja, kisha ukalazimia kwenda duka jingine ili kununua bidhaa nyingine, yeye anakuunganishia bidhaa zote kwa pamoja. Ukienda kwake unaweza kununua kila bidhaa unayotaka. Hii maana yake nini? Hii maana yake ni kwamba amekusaidia wewe kupata unachotaka. Ni kitu gani unataka, unataka bidhaa za nyumbani, lakini hutaki uchovu wa kuzunguka zunguka huku na kule ukinunua bidhaa moja hapa na nyingine pale. Unataka ukitoka nyumbani na hela yako uende sehemu moja ununue bidhaa zako kisha uondoke.
Lakini pia inawezekana huyu ameshaona fursa, ya huduma bora. Inawezekana watu waliopo wanatoa huduma, ila siyo huduma bora na yakuaminika. Mteja anaweza kwenda kununua kitu, wanaanza kukufokea na wanakuona kama mtu mwenye shida. Huyu akafungua duka, akaamua kwamba wewe mteja ndiye mfalme. Wewe ndiye mwanzo na mwisho. Akaanza kuwahudumia vizuri wateja wake.
Kumbe rafiki yangu swali hili moja tu la kujiuliza kila siku, linakufungulia fursa kibao. Ni swali muhimu sana ambalo unapaswa kuwa unajiuliza kila siku bila ya kuacha. Naamini utaanza kulifanyia kazi moja bila ya kurudi nyuma.
Soma zaidi:
- Maswali Manne Muhimu Unayopaswa Kujiuliza Baada Ya Kusoma Kitabu
- NJE YA KUMI NA NANE: fikiri, Hoji Na Uliza Maswali Katika Ulimwengu Ambao Hautaki Uwe Hivyo.
- Iambie dunia kile unachotaka kufanya, ila kwanza kioneshe hicho kitu
Swali la pili ambalo unapaswa kujiuliza ni swali Ni kitu gani bora nimeweza kufanya siku ya leo kwa ajili yaw engine?
Unapaswa kujiuliza hili swali jioni kabla ya kulala. Usilale kabla hujajiuliza hili swali, na ikitokea kwenye kujiuliza hili swali umegundua kwamba siku hiyo hujafanya kitu, basi itumie nafasi hiyo kufanya kitu hata kama ni kidogo.
Kuna siku moja nilijiuliza hili swali, nikagundua kwamba mbali na kwamba siku hiyo nilikuwa bize tokea asubuhi mpaka jioni, lakini sikuweza kufanya kazi ya yoyote ya kuwasaidia watu wengine. Nilichofanya japo nilikuwa tayari nimechoka, nilichukua muda kidogo na kuandika makala fupi nzuri sana ambayo watu wengine wangeweza kusoma na kupata kitu cha kufanyia kazi. Na hivyo kwa namna hiyo nikawa nimeweza kufanya kitu chenye mchango kwenye hii dunia.
Rafiki yangu, kamwe usiache kujiuliza haya maswaili mawili kila siku. Isipite siku ambayo hujajiuliza haya maswlai, utagunduakwamba unazidi kuwa bora zaidi kwenye kazi zako na unaimarika.
SOMA ZAIDI:
- Kitabu cha NGUVU YA KUCHUKUA HATUA YA KWANZA ni kitabu ambacho kila mtu anapaswa kusoma
- Vita Ya Maisha Anashinda Mtu Anayefikiri Anaweza
- Kitu Kimoja Ambacho Hakuna Mtu anaweza Kukifanya Kwa Niaba Yako
Nikutakie kila la kherii kwenye kufanyia kazi haya ambayo tunajifunza
Makala hii imendikwa na Godius Rweyongeza
Unaaweza kuwasiliana na mwandishi kupitia namna ya simu 0755848391
Mwandishi yuko Morogoro, nchini Tanzania
-
Kitu Ambacho Kinaua Biashara Nyingi
Kuna utafiti ambao ulifanyika, na ulikuja na majibu ya kitofauti kidogo ambayo huwezi kuyategemea. Utafiti huu ulihusisha wateja, wafanyakazi pamoja na viongozi wa kampuni na biashara mbalimbali.
Lengo la utafiti huu lilkuwa ni kuona ni kwa namna gani kampuni au taasisi zinatoa huduma bora kwa wateja. Asilimia kubwa ya viongozi wa kampuni zilizofanyiwa utafiti walisema kwamba wanatoa huduma bora kwa asilimia 95%. Walijiona kwamba wako vizuri kwenye kutoa huduma kwa wateja.
Aidha walipoulizwa wafanyakazi waeleze kiwango chao cha kutoa huduma kwa wateja, walisema kwamba, wanatoa huduma bora kwa asilimia 75.
Kitu cha kushangaza kilikuja pale walipoulizwa wateja wanaonunua kwenye kampuni au taasisi husika. Hawa walisema kwamba huduma wanayopata kwenye kampuni au taasisi husika ni ya viwango vya asilimia 8% tu.
Kumbe wakati viongozi kwenye kampuni husika walikuwa wanajiona vizuri, wakati wafanyakazi walikuwa wanajiona vizuri, wateja walikuwa bado wanaona kwamba kuna mambo mengi ambayo hayajakaa sawa ambayo watu hao wanapaswa kurekebisha. Kitu hiki inawezekana kinatokea kwako pia. unaweza kuw aunajiona vizuri kwenye huduma kwa wateja au kwenye biashara yako, lakini badala ya kujiona kwamba uko vizuri sana. Jichukulie kwamba kuna mambo mengi ambayo hujafanya na unapaswa kuyafanya.
Jione unatoa huduma kwa asilimia 8 tu
Rafiki yangu, badala ya kujiona kwamba unatoa huduma bora kwa asilimia 95 au 75, jione unatoa huduma kwa asilimia 8, kisha kazi yako iwe ni kuangalia ni kwa namna gani unaweza kutoka kwenye hiyo asilimia 8 na kwenda mpaka asilimia 95 na zaidi. Usijione umefika, jione bado unapaswa kuendelea kupambana kushinda muda wote.
-
Kuwa Mwanafunzi wa KUDUMU
Dr. Myles Munroe ni mmoja watu ambao walikuwa wamefanikiwa sana kwenye sekta ya maendeleo binafsi. Kazi zake nyingi zimegusa maisha ya watu wengi enzi za uhai wake mpaka leo hii. Siku moja alikuwa anaeleza namna alivyoenda kwenye duka la vitabu na kununua kitabu cha zaidiya dola 125. Dola 125 ni zaidi ya laki mblii na nusu za Tanzania.
Msaidizi wake alishangaa kuona kwamba Dr. Myles Munroe amenunua kitabu cha gharama kubwa hivyo. Kwa nini unatumia gharama kubwa hivyo kununua kitabu kimoja tu? Kw anini usitumie hii hela kufanya vitu vingine kama kununua nguo? Hapo ndipo Dr. Myles Munroe alipomwambia msaidizi wake kwamba, hiii ndiyo tofauti inayotutofautisha mimi na wewe. Ndiyo maana mimi ni kiongozi na wewe ni mfuasi. Unajua kwa nini alimwambia hivyo? Alimwambia hivyo kwa sababu alijua wazi mazuri yaliyo kwenye vitabu ambavyo msaidiz wake alikuwa bado hayajui.
Ukweli ni kuwa kwenye maisha ya kila siku ni kwamba unapaswa kuwa mtu ambaye anajifunza bila ukomo. Wekeza nguvu na muda wako kwenye kujifunza mara kwa mara bila ya kuchoka. Kamwe usifikie hatua ambapo utajiona kwamba umejifunza na umeju akila kitu kwenye maisha yako. kila mara unapaswa kuwa unaendelea kujifunza bila ya kukoma. Kujifunza ni tiketi ya wewe kufanya makubwa. Kujifunza kunakufanya unaona mbali kuliko pale ambapo unakuwa hujifunzi.
Kwenye haya maisha, kubali watu wakuite mzembe, ila siyo kwenye vitu viwili. Kwanza usikubali kuitwa mzembe kwenye kufanya kazi kwa bidii, na usikubali kuitwa mzembe kwenye kujifunza. Hivi ni vitu viwlii ambavyo unapasw akuwa unavipambania kila siku, bila ya kuacha na bila ya kujali kitu gani ambacho kinatokea kwenye maisha yako. hakikisha mara zote unapambana kushinda kila siku kwenye haya maeneo mawili.
Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza
unaweza kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza kwa Kujiunga naye hapa
-
HITIMISHO LA KILA MAKALA
Najua kuwa ungependa kupata ushauri wa karibu zaidi moja moja kwa moja kutoka kwangu.
Nitafute tuone ni lini nitakuwa na muda, ili nikupangie ratiba ya kuongea na wewe. Utalipia kiasi kidogo tu.
Saa moja ni laki moja mazungumzo kwa njia ya mtandao.
SAA MOJA NI LAKI MBILI NA NUSU MAZUNGUMZO YA ANA KWA ANA. Malipo yanafanyika kwanza, kisha unapewa tarehe (appointment) tutakapoweza kuongea.
Tumia namba ya simu +255 755 848 391 kuwasiliana nami.
Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza ambaye anaishi Morogoro nchini Tanzania.
Unaweza kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza kupitia youtube channel yake hapa
Kwa ushauri niandikie songambele.smb@gmail.com
Kupata vitabu ambavyo ameandika Godius Rweyongeza, wasiliana naye kwa +255 684 408 755 na orodha ya vitabu vyenyewe unaweza kuiona HAPA. Chagua unachopenda, kisha twanga, +255 684 408 755
Kujiunga na programu yetu ya uandishi. Wasiliana na +255 678 848 396
For Consultation only: +255 755 848 391 au godiusrweyongeza1@gmail.com