Home


  • Jinsi Ya Kufungua akaunti ya mfuko wa FAIDA (FAIDA FUND)

    Juzi niliandika makala kuhusu mfuko wa FAIDA (FAIDA FUND). Swali ambalo nilipokea kutoka kwa wengi waliosoma makala hii lilikuwa ni kwa namna gani naweza KUFUNGUA akaunti kweye mfuko huu wa FAIDA.

    KITU hiki kimenisukuma nikuandalie Makala nyingine kukuonesha ni kwa namna gani unaweza KUFUNGUA akaunti kwenye mfuko huu wa FAIDA. Unajua unawezaje kufungua akaunti.

    Fanya yafuatayo.

    BONYEZA *152*00# kwenye simu yako.

    Kisha chagua namba 1 kama inavyoonekana hapo chini

    Baada ya hapo chagua namba 6 Kama inavyoonekana hapo chini

    kisha chagua namba 1 tengeneza akaunti ya binafsi.

    Baada ya hapo utaweka majina yako kamili

    Kisha utaweka tarehe, mwezi na mwaka wa kuzaliwa

    Ukibonyeza hapa, kuna hatua zaidi, utapata. Zifuate Mpaka mwisho ili ukamilishe kusajili akaunti yako.

    Ukishasajiri akaunti yako, endelea mbele kwa kuhakikisha unaweka kiasi kisichopungua elfu kumi kwenye akaunti. Kwa kufanya hivyo, utakuwa umefungua akaunti.

    kila la kheri

    Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.

    Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.

    Mtandaoni, vitabu vyake unaweza kuvipata kupitia mtandao wa GETVALUE kwa KUBONYEZA HAPA

  • Kitu Kimoja Kinachopaswa Kukufanya Usome Vitabu Vya Hardcopy badala ya Softcopy

    Rafiki yangu, linapokuja suala la softcopy au hardcopy watu wamekuwa wanakuwa na mtazamo tofauti. Wapo wanaopendelea hardcopy na wapo wanaopendelea softcopy na wengine wanapendelea audiobook kama huyu hapa

    Kwa upendeleo wowote atakaokuwa nao mtu, hakuna ambaye anakuwa sahihi wakati mwingine akiwa hayuko sahihi. Kitu kikubwa sana ni kupata maarifa yaliyo kwenye kitabu na kuyafanyia kazi.

    Ila siku ya leo ninapenda nikwambie sababu hii moja ambayo inapaswa kukusukuma wewe kupata vitabu vya nakala ngumu au audiobook na siyo softcopy.

    Na sababu hii ni kwamba, kama una watoto au mtoto mdogo. Hii ni sababu kubwa kwa nini unapaswa kununua vitabu vya nakala ngumu au vitabu vilivyosomwa (audiobook).

    Ili unielewe vizuri hapa naomba nieleze kwa undani kidogo, mtoto mdogo ana tabia ya kuiga kile ambacho mzazi anakuwa anafanya.

    Unapokuwa unasoma kitabu kwenye simu, mtoto anakuwa hajui kama unasoma kitabu au husomi kitabu. Kitu hiki kinamfanya mtoto awe anapenda kushika simu. Ila unapokuwa unasoma kitabu cha kushikika (hardcopy), mtoto anakuwa anaona. Kitu hiki kinamfanya mwanao apendelee zaidi kushika kitabu cha nakala ngumu na hivyo kumjengea tabia ya kuanza kusoma vitabu mapema.

    Hivyo, kama wewe ni mzazi, sambamba na kusoma vitabu vya nakala laini (sofcopy/ebooks), hakikisha unakuwa na nakala ngumu kadhaa pale nyumbani kwako. Pale ambapo utakuwa na mtoto,  usisome kitabu kwenye simu, badala yake soma kitabu cha nakala ngumu.

    Mpe na mtoto kitabu ashike, ili aanze kuzjenga tabia ya kusoma vitabu mapema sana.

    Unatakiwa pia kupenda vitabu vya kusikiliza unapokuwa na mtoto. Kwanza inasaidia kumwongezea mtoto misemo ya ziada. Na tafiti zinaonesha kwamba watoto wanaokuwa wanaojifunza misemo mingi, huwa wanajiamini mbele ya watu kuliko ambao wanakuwa na misemo kidogo. Lakini pia watoto wanaokuwa na misemo mingi huwa ni wawasilishaji wazuri wa mada. Ssa wewe hupendi mwanao awe mwasilishaji mzuri wa mada? Naamini wewe ni kama mimi, na ungependa mwanao awe gwiji wa kuongea na kuwasilisha mada mbele za watu kwa kujiamini na bila uoga wowote.

    Watu wengi huwa wanapenda pale ambapo huwa wanaona  mtoto mdogo anasimama mbele ya watu na kuongea kwa kujimini. Wengi hupiga makofi na kumpongeza kwa namna ambavyo wanaweza, ikiwa ni pamoja na kutoa zawadi ya pesa.

    Naamini na wewe unaweza kumlea mwanao hivyo, kwa kuanza kumjengea misingi sahihi sasa hivi.

    Nakutakia siku njema

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.

    Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.

    Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.

  • Jinsi ya kupata matokeo ya tofauti mwaka 2023

    Kuna kitu kimoja nakijua kuhusu wewe rafiki yangu. Na kitu hiki ni kwamba mwaka 2023, ungependa kupata matokeo ya tofauti. Matokeo ya tofauti kwenye kila eneo ambalo utakuwa ukilifanyia kazi.

    Kama unataka kupata matokeo ya tofauti mwaka 2023, basi hakikisha kwamba unakuwa tayari kufanya vitu vya tofauti. Yaani, vitu ambavyo hujawahi kufanya siku za nyuma.

    Huwezi kutegemea kupata matokeo ya tofauti mwaka 2023, huku ukiwa unaendelea kufanya vitu vile vile bila ya kubadilika.

    Ni lazima uwe tayari kufanya hivi vitu vya tofauti, labda swali la kujiuliza ni vitu gani vya tofauti ambavyo naweza kufanya mwaka 2023 vikanipa matokeo ya tofauti.

    VIfuatavyo ni vitu vitatu vya tofauti ambavyo unaweza kufanya mwaka 2023, vikakupa matokeo ya tofauti kwenye kipato chako, kwenye uwekezaji, kwenye afya yako, kwenye watu unaokutana nao na kwenye kila kitu unachofanya. Kiufupi kama unataka kuufanya mwaka 2023, uwe mwaka wa baraka na kila kitu utakachogusa basi kibadilike kuwa dhahabu, basi hakikisha kwamba unafanyia kazi yafutayo.

    Kwanza hakikisha kwamba una malengo ambayo unayafanyia kazi. rafiki yangu, bila malengo makubwa mwaka 2023, hutaweza kutoboa. Kwa hiyo, kama kuna kitu ambacho unapaswa kuanza nacho mwaka 2023, basi ni kuhakikisha kwamba unaanza kwa kuweka malengo. Weka malengo na yafanyie kazi.

    Pili, kuwa tayari kuchukua hatua. Rafiki yangu, bila ya kuchukua hatua, malengo uliyojiwekea hayataweza kutimia. Ni lazima uwe tayari kuchukua hatua hata kama ni kidogo.

    Wengi hufikiri kwamba ili wafanikishe malengo yao, basi wanapaswa kusuburi siku moja ya mwisho wa mwaka ambapo malengo yao yatatimia, ukweli ni kwamba malengo makubwa huwa hayatimii kwa siku moja ya mwisho wa mwaka. Badala yake yale unayokuwa unayafanya kila siku, kila kukicha ndiyo yanakupelekea wewe kwenye kufanikisha malengo yako au kufeli kwenye kufanyia kazi malengo yako. Ndio maana nimekuandalia kitabu murua kabisa cha NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA. Ukipata kitabu hiki, utajifunza na kuona ni kwa namna gani unaweza kufanyia kazi malengo makubwa kwa kuanza kidogo kidogo.

    Mambo madogo madogo unayoyafanyia kazi leo hii, yana uwezo wa kukuletea matokeo makubwa. Hakikisha kwamba unapata nakala ya kitabu hiki cha kipekee leo hii. Nakala yako ni 20,000/- tu. na utatumiwa popote pale utakapokuwa nchini.

    Tatu ni kukaa na watu sahihi. Watu sahihi rafiki yangu watakufanya uweze kupiga hatua na kufika mbali. Hivyo basi, kama unataka kuufanya mwaka 2023, uwe  mwaka wa kipekee hakikisha kwamba unaungana na timu ya watu sahihi. Kuna timu ya watu sahihi ambayo unahitaji kujiunga nayo mwaka 2023, na timu hii ni ya watu ambao wamejiunga na semina ya kufungua mwaka 2023. Ukijiunga na timu hii utakutana na watu sahihi ambao wana mtazamo chanya kama wewe.

    hawa wote utakutana nao, endapo tu utajiunga na semina ya kufungua mwaka 2023.

    Karibu kwenye semina hii ya kipekee sana.

    Kila mwanzo mwa mwaka na katikati mwa mwaka huwa Kuna semina ambayo huwa naiendesha.

    Mwakani wakati wa kufungua  mwaka mpya tunatarajia kuwa na semina ya kufungua mwaka ambayo itafanyika kuanzia tarehe 15.

    Na itadumu kwa siku 15 mfululizo. Semina hii ya kipekee ambayo itafanyika kwa njia ya mtandao, inalenga kukupa maelezo ya kina yatakayokusaidia kuuanza mwaka mpya kwa mtazamo sahihi na kuuweza kuufanikisha kwa viwango vikubwa sana. Semina hii inaitwa JINSI YA KUONGEZA THAMANI YAKO 2023.
    Kwenye Semina hii utajifunza Mambo
    1. Namna ya kuongeza thamani yako
    2. Namna ya kuongeza kipato chako mara mbili mpaka mara kumi zaidi
    3. Njia za kuweka malengo na kuyafanyia kazi kwa usahihi ndani ya mwaka 2023.
    3. Nguvu ya vitu vidogo kwenye kuongeza thamani yako binafsi na mengine mengi

    Hii Ni semina ya siku 15 mfululizo ambayo imeshiba mambo ya msingi sana yanayokufaa wewe na yatakayokusaidia wewe kuuanza mwaka kwa usahihi na kupiga hatua na kufika mbali.

    Katika siku hizi 15 utapata masomo 15 yaliyoandaliwa kwa kina na ambayo yatakusaidia wewe kuanza KUONGEZA THAMANI YAKO ndani ya mwaka 2022.

    Ni matarajio yangu kuwa baadaa ya semina hii, utakuwa na mbinu za kukusaidia wewe kuongeza thamani yako binafsi na kipato chako walau Mara mbili zaidi

    Hakikisha kwamba haukosi Semina hii, ya kipekee sana

    Semina itafanyika lini?
    Itaanza tarehe 15 Januari na itadumu kwa siku 15

    Semina itafanyika wapi?
    Semina itafanyika mtandaoni (WhatsApp) kwenye kundi maalumu la WhatsApp.

    Je, Kuna ada ya kujiunga na Semina.
    Ndiyo ada ipo. Ada ya semina ni 15,000/- tu. Kwa kila mshiriki kwa siku zote za semina.
    Mwisho wa kulipia ni tarehe 10 Januari.

    Njoo uuanze mwaka wako kwa kiusahihi na kwa kupata mwongozo utakaokusaidia kuufanyia kazi mwaka mpya kutokea kwenye nafasi nzuri.

    Kuthibitisha ushiriki wako. Tuma malipo yako kwenye Namba ya simu 0755848391 jina ni GODIUS RWEYONGEZA.

    Karibu sana

    Whatsap group la semina: https://chat.whatsapp.com/FbzmwEVkObKIuqeR4pIZmu

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza
    Unaweza kusoma makala na mafunzo yake zaidi kwenye blog yake ya SONGAMBELE (www.songambele.co.tz)

  • Faida Tatu KUBWA unazopata pale unapowekeza kwenye hisa

    Kitabu hiki kinapatikana kwa elfu tano tu (sotfcopy0
    Kitabu hiki kinapatikana kwa elfu tano tu (sotfcopy)

    Rafiki yangu, umewahi kuwaza kwamba ukiwekeza kwenye hisa utanufaika na kitu gani?

    Kuna faida nyingi za kuwekeza kwenye hisa, ila kwenye hii makala ya siku ya leo ningependa kuongelea faida mbili kubwa kwa haraka

    Faida ya kwanza ya kuwekeza kwenye hisa ni kupata ongezeko la thamani.  Ongezeko la thamani ni pale unaponunua hisa kwa bei ya chini na baadaye kuja kuiuza kwa bei ya juu.

    Mfano mwaka, 2022 hisa za CRDB zilikuwa zinauzwa na kununuliwa kwa bei ya shilingi 150. Sasa hivi hisa hizohizo zinauzwa shilingi 380. Hii ndio kusema kwamba aliyenunua hisa kipindi hicho cha mwaka 2020 kwa shilingi 150, sasa hivi kila hisa yake ina thamani ya shilingi ya 380. Kumbe hapa kila hisa ina ongezeko la thamani la shilingi 230 na zaidi.

    Na hiyo ni pesa ambayo imeongezeka bila ya wewe kutoa jasho wala kufanya kazi yoyote ile. Ulichofanya wewe ni kuwekeza fedha yako tu.

    Hii ndiyo faida kubwa ambayo watu wanaomiliki hisa huwa wanaipata.

    Faida nyingine ambayo utaipata kama utamiliki hisa ni  GAWIO. Gawio ni faida ambayo wanahisa wanapata. Faida huwa inapatikana kulingana na wingi wa hisa ambazo mtu anakuwa anamiliki kwenye kampuni husika. Kumbe basi, hisa ni kitegauchumi ambacho kila mtu anapaswa kuwa nacho na anapaswa kukimiliki.

    3. Hisa ni kipimo cha utajiri. Leo hii dunia inamfahamu Elon Musk kama tajiri mkubwa duniani. Ila tajiri huyu siyo kwamba ana mabilini yote ya fedh mfukoni. Utajiri wake uko kwenye hisa anazomiliki kwenye makampuni ya TESLA, SPCAEX na makampuni mengine. Kumbe hisa, ni kipimo cha utajiri wa mtu husika. Na wewe tunaweza kupima utajiri wako kwa kuangalia vitegauchumi ulivyo navyo ikiwa pamoja na hisa unazomiliki..

    Rafiki yangu, kama bado hujawa na kitega uchumi hiki cha kipekee basi hakikisha kwamba unakuwa nacho.

    PATA KWANZA NAKALA YA KITABU CHA MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE. Hiki kitabu kitakupa mwongozo wewe wa kuweza kuanza kuwekeza kwenye hisa, hatifungani na vipande.

    Kitabu hiki kinapatikana kwa elfu tano tu (sotfcopy0
    Kitabu hiki kinapatikana kwa elfu tano tu (sotfcopy)

  • Njoo Uongeze Kipato Chako Mara Mbili Zaidi Mwaka 2023

    Kuna kitu kimoja nilicho na uhakika nacho juu yako rafiki yangu…Kitu hiki ni kwamba, ungependa kuongeza kipato chako walau mara mbili zaidi ndani ya mwaka 2023! Na hiki ni kitu ambacho ningependa kukusaidia ukifanikishe ndani ya mwaka 2023!

    Kuanzia tarehe 15 januari 2023, tutakuwa na semina ya kufungua mwaka mpya 2023, lengo kubwa la semina hii, ni kukupa mbinu za kukusaidia wewe kuweza kuongeza kipato chako walau mara mbili zaidi ya kilivyo sasa.

    Kwa mbinu tutakazoona kwenye hii semina, ni uhakika kwamba unaenda kuongeza kipato hako walau mara mbili zaidi ndani ya mwaka 2023!

    Hii semina siyo ya kukosa hata kidogo.

    Semina hii itaanza tarehe 15  januari na itadumu kwa siku 15 mfululizo.

    Gharama ya semina hii ni 15,000/- tu. sawa na shilingi elfu moja kwa kila siku ambayo utahudhuria semina. Ili kuhudhuria semina hii ya kipekee utapaswa kulipia hiki kiasi cha shilingi 15,000/- tu. namba ya malipo ni 0755848391 jina ni GODIUS RWEYONGEZA. Ukifanya malipo, utakuwa umethibitisha ushiriki wako kwenye semina

    Wahi sasa maana nafasi kwenye hii semina ni chache kwa watu maalumu tu!

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.

    Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.

    Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.

  • Mfuko wa FAIDA (FAIDA FUND): Unawekeza au Huwekezi?

    Watumishi Housing Investment (WHI) wameanzisha mfuko wa uwekezaji wa pamoja ambao wanauita MFUKO WA FAIDA au kama unaielewa vizuri lugha ya kigeni basi unasema FAIDA FUND. Mfuko wao ni mfuko ulio wazi (open-endend). Kama bado hujasoma kitabu changu cha maajabu ya kuwekeza kwenye hisa, hatifunagni na vipande lazima tu utakuwa unajiuliza mfuko ulio wazi maana yake ni nini?

    Mfuko ulio wazi ni mfuko ambao pale unapotaka kununua vipande meneja wa mfuko anakutengenezea vipande vyako. Na pale unapotaka kuuza vipande meneja wa mfuko ananunua vipande vyako.

    Yaani, tuchukilie mfano, mimi naanzisha mfuko wa uwekezaji wa pamoja. Na watu mnakusanyika kununua vipande, labda kipande kimoja ni shilingi mia moja. na watu wa kwanza, mnanunua vipande elfu moja (1000). Mfuko hapo hapo utakuwa na vipande elfu moja. Labda baada ya siku kumi za kununua vipande anatokea mmoja ambaye anataka kuuza vipande vyake 200. Anauza vipande na mimi meneja wa mfuko nanunua hivyo vipande na kumpa hela yake. Mfuko unabaki na vipande 800. Wakati kesho yake anatokea mwingine ambaye anataka kunununua vipande mia tano. Na huyo anaunua vipande na hivyo vipande vya mfuko sasa vinakuwa 1300/-.

    Kwa hiyo, mfuko ulio wazi huwa una sifa ya kuongezeka kwa vipande pale wanunuaji wanaponunua na kupungua kwa bei pale wauzaji wanapouza.

    Mfuko ulio wazi (open ended) ni tofauti kabisa na mfuko uliofungwa (closed ended) ambao wenyewe huwa una idadi ya kamili ya vipande, na idadi hiyo huwa haiongezeki wala kupungua. Kama mfuko una vipande 1000. Vinabaki kuwa hivyo hivyo tu miaka yote. Ili ununue vipande kwenye mfuko uliofungwa, lazima awepo mtu anayeuza. Na ili uuze, lazime kuwepo anayenunua. Utagundua kitu hiki ni tofauti na mfuko ulio wazi ambao meneja wa mfuko ndiye ananunua au kukuuzia vipande. Kama huelewi, hakikisha unapata kitabu changu cha MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE kwa 20,000 tu, nakala ngumu, na 10,000 tu nakala laini (softcopy).  Kipate kitabu hiki kwa ajili ya kuongeza maarifa zaidi pia kuhusu eneo hili la uwekezaji.

    Kitabu hiki kinapatikana kwa elfu tano tu (sotfcopy0
    Kitabu hiki kinapatikana kwa 20,000/- tu

    Mimi niache niendelee mbele kuuongelea mfuko wa FAIDA ulioanzishwa na WHC.

    Mfuko upo chini ya WHI ambao wamesajiliwa na kisheria chini ya soko la mitaji (CMSA).

    Madhumuni ya mfuko

    •   Mfuko huu   ni    mpango    ulio    wazi unaotoa fursa nyingine ya uwekezaji kwa Watanzania hasa wa kipato cha kati na cha chini kupitia uwekezaji katika vipande ili kupata mapato shindani kupitia ukuaji wa mitaji.

    • Kuwajengea watanzania utamaduni wa kuwekeza katika Masoko ya Fedha na Mitaji na kuweka akiba.

    Anayestahili kuwekeza kwenye huu mfuko

    Mfuko huu unatoa mwanaya wa mtu yeyote, (ambaye ni mtanzania au wa nje ya nchi) kuwekeza kwenye mfuko huu. Lakini pia taasisi kama benki, mifuko ya pension, taasisi za kiserikali,  taasisi zisizo za kiserikali, taasisi za kijeshi, makampuni n.k.

    Kiwango cha chini cha kuwekeza kwenye mfuko huu

    Kiwango cha chini cha kuwekeza kwenye huu mfuko ni elfu kumi, pale unapofungua akaunti mara ya kwanza. Baada ya kufungua akaunti, unaweza kuendelea kuwekeza zaidi kwenye huu mfuko kwa kuongeza kiwancho cha chini kabisa cha shilingi elfu tano.

    Kiwango cha juu cha kuwekeza

    Hakuna kiwango cha juu cha kuwekeza. Kwa hiyo, kama una mabilioni ya kuwekeza, unaweza kuyawekeza bila shida yoyote kwenye huu mfuko. Lakini bado kama huna mabilioni makubwa sana, unaweza kuendelea na utaratibu wako wa kuwekeza kwenye huu mfuko kadiri utakavyojiwekea, kwa kuweka kiwango cha chini kabisa cha elfu tano (5,000/-) kila utakapohitaji kuwekeza.

    Gharama za kujiunga na mfuko (Entry load)

    Kwa kawaida huwa ukitaka kununua hisa, huwa kuna gharama ambayo mtu unalipia ili kununua hisa. Na pale unapotaka kuuza hisa zako, kuna gharama ambazo unakatwa. Hizi gharama kwa Kiswahili tunaweza kuziita tozo za kiujiunga (entry load) au tozo za kujitoa (exit load).

    Wakati wa kujiunga na mfuko huu au wakati wa kujitoa kwenye huu mfuko, hakuna gharama yoyote ile ya kujiunga au kujitoa.

    Thamani ya kipande

    Thamani ya mwanzo ya kipande ni Tsh 100/=. Hii itatumika wakati wa mauzo ya awali na baada ya hapo kipande kitauzwa kulingana na thamani halisi.

    Ambapo kipande kitapanda au kushuka kulingana na mwenendo wa soko kwa wakati husika.

    NB: Mpaka sasa hivi mfuko upo kwenye hatua za awali za kuuza vipande vyake. Hivy, kama unasoma ujumbe huu kabla ya tarehe 31 Disemba, unaweza kununua vipande kwa bei ya awali ya vipande.

    Ukwasi

    Uuzaji wa vipande utafanyika kila siku baada ya mienzi mitatu tangu kumalizika kipindi cha mauzo ya awali. Mfuko utatuma malipo ya mauzo ya vipande ndani ya siku tatu za kazi baada ya kupokea maombi katika Makao Makuu ya Watumishi Housing Investments. Fedha za mauzo zitatumwa moja kwa moja katika akaunti ya benki ya mwekezaji au simu ya mkononi iliyosajiliwa.

    Sera za uwekezaji kwenye mfuko

    Mfuko utawekeza katika masoko ya fedha kwa asilimia 100%. Kiwango cha uwekezaji katika masoko ya fedha na Dhamana kitalenga kupata mapato makubwa katika soko.

    Muda wa kuendesha mfuko

    Mfuko huu ni wa kudumu kwa mujibu wa Waraka wa Makubaliano.

    Faida za kikodi

    Kwa mujibu wa sheria za nchi,mgawanyo wa mapato ya Mfuko yamesamehewa kodi ya mapato kwa wawekezaji.

    Hayo ni baadhi ya mambo ambayo nimekuandalia kuhusu  mfuko huu.

    NB: 1. Kabla hujachukua hatua ya kuwekeza kwenye huu mfuko, nashauri uhakikishe umesoma kitabu changu cha MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE ili uweze kuelewa zaidi dhana ya uwekezaji.

    2. Mwandishi wa makala hii hauhusiki kwa vyovyote vile na faida au hasara utakayopata kutokana na uwekezaji utakaoufanya kwenye huu mfuko. Ni muhimu kuhakikisha kwamba umepata ushauri wa watalaam kabla ya kufanya uwekezaji.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.

    Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.

    Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.

  • SEMINA YA KUFUNGUA MWAKA: Karibu kwenye Semina ya kufungua mwaka 2023

    Kila mwanzo mwa mwaka na katikati mwa mwaka huwa Kuna semina ambayo huwa naiendesha.

    Mwakani wakati wa kufungua  mwaka mpya tunatarajia kuwa na semina ya kufungua mwaka ambayo itafanyika kuanzia tarehe 15.

    Na itadumu kwa siku 15 mfululizo. Semina hii ya kipekee ambayo itafanyika kwa njia ya mtandao, inalenga kukupa maelezo ya kina yatakayokusaidia kuuanza mwaka mpya kwa mtazamo sahihi na kuuweza kuufanikisha kwa viwango vikubwa sana. Semina hii inaitwa JINSI YA KUONGEZA THAMANI YAKO 2023.
    Kwenye Semina hii utajifunza Mambo
    1. Namna ya kuongeza thamani yako
    2. Namna ya kuongeza kipato chako mara mbili mpaka mara kumi zaidi
    3. Njia za kuweka malengo na kuyafanyia kazi kwa usahihi ndani ya mwaka 2023.
    3. Nguvu ya vitu vidogo kwenye kuongeza thamani yako binafsi na mengine mengi

    Hii Ni semina ya siku 15 mfululizo ambayo imeshiba mambo ya msingi sana yanayokufaa wewe na yatakayokusaidia wewe kuuanza mwaka kwa usahihi na kupiga hatua na kufika mbali.

    Katika siku hizi 15 utapata masomo 15 yaliyoandaliwa kwa kina na ambayo yatakusaidia wewe kuanza KUONGEZA THAMANI YAKO ndani ya mwaka 2022.

    Ni matarajio yangu kuwa baadaa ya semina hii, utakuwa na mbinu za kukusaidia wewe kuongeza thamani yako binafsi na kipato chako walau Mara mbili zaidi

    Hakikisha kwamba haukosi Semina hii, ya kipekee sana

    Semina itafanyika lini?
    Itaanza tarehe 15 Januari na itadumu kwa siku 15

    Semina itafanyika wapi?
    Semina itafanyika mtandaoni (WhatsApp) kwenye kundi maalumu la WhatsApp.

    Je, Kuna ada ya kujiunga na Semina.
    Ndiyo ada ipo. Ada ya semina ni 15,000/- tu. Kwa kila mshiriki kwa siku zote za semina.
    Mwisho wa kulipia ni tarehe 10 Januari.

    Njoo uuanze mwaka wako kwa kiusahihi na kwa kupata mwongozo utakaokusaidia kuufanyia kazi mwaka mpya kutokea kwenye nafasi nzuri.

    Kuthibitisha ushiriki wako. Tuma malipo yako kwenye Namba ya simu 0755848391 jina ni GODIUS RWEYONGEZA.

    Karibu sana

    Whatsap group la semina: https://chat.whatsapp.com/FbzmwEVkObKIuqeR4pIZmu

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza
    Unaweza kusoma makala na mafunzo yake zaidi kwenye blog yake ya SONGAMBELE (www.songambele.co.tz)

  • Maisha ndiyo hayahaya rafiki yangu

    KIPAJI NI DHAHABU
    Rafiki yangu, nimeandika kitabu. Kinaitwa KIPAJI NI DHAHABU. Ili kupata kitabu hiki, wasialiana na mi kwa 0755848391 sasa

    Rafiki yangu wa ukweli, moja ya kitu ambacho watu huwa wanafanya kwenye maisha yao ni kusubiri kila kitu kiwe sawa ili waweze kufanyia kazi malengo na ndoto zao. Ila ninachotaka kukwambia rafiki yangu ni kwamba, hakuna hata siku moja ambayo kila kitu kitakaa sawa kwa ajili ya kukusubiri wewe ufanyie kazi malengo yako. Maisha ni haya haya, hivyo, unachopaswa kufanyia malengo na ndoto zako sasa hivi katika hali hii hii unayopitia. Ukweli ni kwamba rafiki yangu ukiendelea kusubiri kila kitu kikae sawa, hiyo siku haitakuja kufika.

    Fanyia kazi malengo yako katika hali hiyohiyo.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.

    Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.

    Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.

  • Bei kisiwe kigezo cha wewe kuuza

    Moja ya dhana ambayo watu huwa wanatumia kwenye kuuza ni kuuza kwa bei ya chini. rafiki yangu, nataka kukwambia kitu kimoja muhimu sana, kwamba mara zote usishindane kwa bei. Maana kadiri unavyopunguza bei, mara zote utakuta kwamba kuna mtu anawezakupunguza bei zaidi yako.

    Hivyo, bei kisiwe ndiyo kigezo pekee cha wewe kuuza.

  • Wafanyakazi na mfumuko wa Bei

    hisa na nguvu ya vitu vidogo  kuelekea mfanikio makubwa
    hisa na nguvu ya vitu vidogo kuelekea mfanikio makubwa

    Kila tarehe 1 mwezi Mei. Macho na masikio yote ya wafanyakazi huwa yapo kwa kiongozi mkuu wa nchi kuona kama atawaongezea mshahara.

    Unajua kwa nini huwa wanataka ongezeko la mshahara? Ni kwa sababu kile kipato wanachokuwa nacho mwanzoni kinakuwa hakitoshi kuwafanya wamudu mahitaji ya kila siku. Hivyo, ongezeko la mshahara likiwepo kweli, linaweza kuwa suluhisho, japo kwa kiasi fulani. Lakini kesi hii haiishii hapo, hii kesi ni kubwa na mahakama haitoshi, ndio maana tunaendelea mbele mpaka tupate suluhisho😋😋

    Utakumbuka kwenye makala ya jana tuliongelea juu ya suala zima la mfumuko wa bei. Lakini mwisho wa siku tuliona ni kwa namna gani unaweza kuukwepa mfumuko huu wa bei kwa kufanya uwekezaji.

    Sasa siku ya leo nataka tuone uhusiano uliopo Kati ya mshahara na mfumuko wa bei na kwa nini kila mwaka wafanyazi huwa wanaomba ongezeko la mshahara. Lakini kama  kawaida yangu, sitakuacha hivihivi, maana lengo langu siyo tu kuliongelea tatizo pekee, bali kukupa suluhisho.

    Kabla sijaenda mbali zaidi. Naomba niwashukuru wale wote wanaosoma makala zangu na kunipa mrejesho. Na hasa wanaoenda mbali zaidi na kusapoti kazi zangu kwa kununua. Nyie ndio mnawezesha ujio wa makala nyingine zaidi kama hizi. Asante sana

    Sasa ili tuweze kuelewa kwa kina zaidi kwa nini wafanyakazi wanakuwa wanahitaji ongezeko la mshahara, inabidi uelewe kwa kina dhana ya mfumuko wa bei kama nilivyoieleza jana.

    Mfumuko wa bei huwa unatokea kila mwaka, na serikali kupitia benki kuu ya Tanzania (BoT) huwa inatangaza mfumuko wa bei kwa mwaka huo umekuwa ni kiasi gani. Ila mshahara huwa hauongezeki kila mwaka, kumbe basi kama mfumuko wa bei unaongezeka kila mwaka na mashahara hauongezeki kila mwaka, basi hapo Kuna shida sehemu……..

    Jana nilisema kwamba mfumuko wa bei ni pale Ambapo uwezo wa fedha kufanya manunuzi unapungua japo fedha inabaki ileile.
    Mfano kama ulikuwa na elfu moja mwanzoni mwa miaka 2000 ulikuwa na uwezo wa kununua nguo za kutokelezea mtaani. Ila leo hii elfu  huwezi kununua nguo ya kudamshi kwa elfu moja hiyohiyo😂😂.

    Elfu moja imebaki ileile, Ila uwezo wake wa kufanya manunuzi umepungua.

    Tuchukulie unalipwa mshahara wa laki moja. Na mwaka huu mfumuko wa bei ni asilimia 4.4 kama ulivyoripotiwa. Tazama jedwali hapo chini

    Kama mwwka huu  mfumuko wa Bei ni 4.4 na wewe mshahara wako ni laki moja. Maana yake mshahara utapokea uleule Ila utakuwa umepungua uwezo wa kufanya manunuzi kwa asilimia 4.4.

    Asilimia 4.4 ya mshahara wa laki moja ni 4400.

    Kumbe basi, Kama mwaka jana mshahara wako wa laki moja ulikuwa unakutosha kuishi vizuri.
    Mwaka huu hautakutosha kwa sababu ya mfumuko wa bei. Mshahara wako utabaki uleule ila utakuwa umepungua uwezo wa kufanya manunuzi kwa asilimia 4.4 sawa na shilingi 4400/-

    Kumbe basi ndio maana wafanyakazi wanakuwa wanahitaji ongezeko la mshahara.  Ili walau like ongezeko la mshahara lifidie kile kilichopungua kutokana na mfumuko wa bei.

    Kama mfanyakazi ana matumizi sawa na mshahara wake. Na mfumuko wa bei ni asilimia 4.4. anahitaji, ongezeko la mashara linaoendana na mfumuko wa bei ili asiingie kwenye mikopo ili kukidhi mahitaji yake. lakini endapo, hakutakuwa na ongezeko la mshahara, maana yake huyu mfanyakazi, atapaswa kukopa kiasi cha walau shilingi 4400/- ili kuongezea kufidia mfumuko wa bei uliotokea. Na hapo atakuwa ameanza kuingia kwenye madeni.

    Hiki kitu ndicho huwa kinawafanya wafanyakazi waombe ongezeko la mshahara zaidi.

    sasa mfanyakazi anaweza kufanyaje ili kuondokana na hali hii?

    Kwanza ni kuhakikisha kwamba anapata elimu sahihi, kuhusu mfumuko wa bei.

    Pili ni kuanza kufanya uwekezaji. maana njia pekee ya kuukwepa mfumuko wa bei ni kuwekeza sehemu ambayo inaweza kukupa mrejesho mkubwa kuliko mfumuko wa bei wenyewe.

    na kwenye hili nimekua nakushauri walau kuwekeza UTT, kwenye mifuko ya uwekezaji wa pamoja. Unajiuliza, mfuko wa pamoja ni nini? UTT ni kitu gani? Naanzaje kuwekeza kwenye UTT na maswali mengine kama hayo? basi, tuwasiliane kwa 0755848391 ili uweze kupata nakala ya kitabu chako. Karibu sana.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.

    Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.

    Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.

X