-
Njia Mpya Ya Kupakua Vitabu Mtandaoni
Kwa wale wanaopata shida kupakua vitabu Mtandaoni. leo nimekuja na suluhisho. hakikisha unaagalia video hii Mpaka mwisho. BONYEZA HAPA KUIANGALIA
Hii video Ni muhimu Sana, hakikisha unaiangalia kila la kheri.
-
Nani anapaswa kusoma vitabu na kwa nini
Kuna MTU kaniuliza swali hili, Nani anapaswa kusoma vitabu na kwa nini
Jana kwa upande wangu imekuwa Ni moja ya siku moja bize Sana. niliamka saa nane usiku, nililala saa sita usiku. Na hapa nipo ikiwa Ni saa kumi alfajiri nimeahaamka.
Ninachotaka kukwambia siku ya leo siyo kuamka mapema, Bali kusoma vitabu.
Ninaamka mapema hivi kila siku, ikiwa Ni lengo la mimi kupata muda wa ziada wa kujifunza na kusoma vitabu.
Ikumbukwe sisomi kwa ajili ya mitihani, wala sisomi ili kupata cheti chochote.Labda kujibu swali lako vizuri zaidi nipende tu kusema kwamba MTU yeyote ambaye anajua kusoma na kuandika anapaswa Kuwa msomaji wa vitabu.
Bila kujali wewe unafanya kazi ya kupiga debe
Ni machinga
Ni mfanya usafi kwenye kampuni au mkurugenziUnapaswa kujijengea utaratibu wa kusoma vitabu. Vitabu vitakujenga na vitabu vitakuwa na uwezo wa kukutoa hapo ulipo Mpaka uweze kufika unapotaka.

Pata ebook Hii bure ili ujifunze umuhimu wa kusoma vitabu. Jaza taarifa zako hapa chini Kuna sababu nyingi kwa nini unapaswa kusoma vitabu, lakini sababu kuu ni kwamba unapaswa kusoma vitabu kwa sababu vitakufumbua macho na kukuonesha yale ambayo huwezi kuyaona kama ingekuwa husomi vitabu.
-
Ushauri Huu Haufanyi Kazi Kwenye Uwekezaji

Mara kwa mara utasikia watu wanakwambia Kuwa unapaswa kuanza kwanza, mambo mengine utayajua wakati unaendelea na safari.
Hicho kitu kinafanya kazi vizuri sana na nimekuwa nikikitumia kwa siku nyingi . Ila Sasa siku ya leo ningependa nikuongezee ushauri muhimu hasa kwa upande wa uwekezaji.
Kwenye uwekezaji Ni muhimu kwako kufanya utafiti wa kina Kabla hujaamua Kuwa utawekeza kwanza na mengine utajua mbele ya safari.
Utafiti Ni muhimu Sana kwenye suala zima la uwekezaji. Ni muhimu ufanye utafiti na kuhakikisha Kuwa umejiridhisha na uwekezaji unaoufanya.
Kila la kheri.
-
App Itakayokusaidia Kutuma SMS baadaye, kupiga simu kwa wakati na kudai hela zako😂😂
Katika makala ya leo tunaenda kuona namna ya kuandaa ujumbe leo na ukautuma siku ya krismasi au mwaka mpya. HutahItajika kuuandika tena au kuutuma tena
Tutaona namna ya kupanga kumpigia siku za mbeleni na ukampigia kwa uhakika bila kukosa hata dakika 1
Tutaona namna ya kupangilia watu wa kuwasiliana nao.
Tutaona njia nzuri ya kukukumbusha kufanyia kazi majukumu yako na kuyafanikisha na mengine mengi.Kwa wale waliojiunga na emali list yangu watakumbuka kuwa huwa nawatumia ujumbe wa kuwapokea ambao huwa
Unawaahidi kuendelelea kuwashirikisha vitu mbalimbali vya kuwasaidia kupitia makala na mafunzo ambayo ninatoa kwa njia ya baruapepe. Na hiki ni kitu ambacho nimekuwa nikikifanyia kazi. Kama wewe hujajiunga na email list yangu, hakikisha unafanya hivyo kwa KUBONYEZA HAPA 👇🏿 na kujaza taarifa zako kamili.Hiki kitu huwa nakifanyia kazi mara kwa mara na leo napenda kukuletea app ambayo inaweza kukusaidia SMS siku za mbeleni.
Mfano tuseme, nataka nikuandalie ujumbe mzuri wa kheri ya krismasi.
Ila Sasa nataka niuandae ujumbe huu uje kwako siku ya krismasi Ila nataka niuandae Leo hii tarehe 18.12.2022. na ninataka ujumbe huu uje kwako tarehe 25.12.2022 saa moja asubuhi.
Kwa kutumia app hii inawezekana.Au tuseme kwamba tumeongea leo tarehe 17 na umeniambia nikupigie tarehe 31 Disemba saa kumi na mbili na nusu jioni kabla hujaenda kwenye mkesha wa mwaka mpya.
Halafu nikaongea na mwingine akaniambia nimpigie tarehe 23 asubuhi saa mbili. Nikawa na orodha ya watu ishirini na kila mtu Anataka mimpgie kwa muda wake, saa yake na tarehe yake. Utakumbukaje?Utaandika kwenye diary si ndio? Kuandika Kwenye diary ndio suluhisho la Watu wengi Ila tatizo muda mwingine unaweza kusahau, na linapokuja suala la muda Kuna watu wengi ambao utajikuta huwapigii kwa wakati.
Siku ya leo nina app ambayo nimekuwa naitumia na imekuwa inanisaidia kutuma SMS muda, saa na dakika ninapotaka.
Imekuwa pia inanikumbusha kuwapigia watu muda, saa na dakika tulipokubaliana.Tuseme nataka nikutumie wewe ujumbe Leo saa kumi jioni. Lakini muda huu ninapoandika makala hii ni saa kumi na moja asubuhi. Hapa ninachofanya naandika ujumbe wako kama ifutavyo hapa chini
Habari yako [JINA LAKO], nakukumbusha kuwa leo jioni saa mbili tutakuwa na kikao cha Cha pamoja kwa njia ya mtandao wa zoom. Nakutakia maandaalizi mema kwa ajili ya kikao, tafadhali hakilisha unawahi.
Halafu usisahau kutuma Ile laki tatu ya kozi tetu inayoendelea. Malipo yote yafanyike kwa namba ya simu 0755848391 jina ni GODIUS RWEYONGEZA.
Enewei, huu ujumbe ninaweza kuuandaa Sasa na ukaja kwako baadaye leo jioni. Au siku yoyote ya tukio.

Ninaweza kuandaa ujumbe huu na kuupanga uje kwako kwa kutumia APP inayoitwa DO IT LATER. Lakini Kuna mengine zaidi ya haya ambayo ningependa ujue kutoka kwenye hii APP.
Vifuatavyo Ni vitu Tisa ambavyo app inaweza kukusaidia kufanya
- KUKUKUMBUSHA KUPIGA SIMU
Mfano, tumeongea Sasa hivi na umeaniambia nikupigie tarehe 2.2
Tukimaliza kuongea tu kwenye simu yakokitajitokeza kitu Kama hiki.

App inavyoonekana baada ya kuwa umempigia mteja. Unaweza kuamua kumtumia ujumbe au kuweka reminder kwamba ikukunbushe lini utampigia tena Hapo nitachagua sehemu ya Call na Kisha nitapanga lini ningependa kuongea na wewe. Ambapo kwa upande wako Ni tarehe 2.2.2023
Hiyo tarehe ikifika , muda na saa tukivyokubaliana. App itanikumbusha nikupigie.

Wakati naendelea kuandika makala hii, app ilinikunbusha nimpigie Godius Rweyongeza. Hahah 
kama aPp imekukumbusha umpigie mu, lakini unaona umebanwa huwezi kumpigia kwa wakati huo. Unaweza kubonyeza SNOOZE kisha ukachagua lini utampigia 2. KUTUMA SMS BAADAYE
Nadhani tangu mwanzo nimeliongelea hili. App hii inaweza kunisaidia kuandaa ujumbe wa kuja kwako tarehe, muda, saa na dakika ninayotaka au tulivyokubaliana.3. KUTUMA SMS kwa mtu kwa kwa kurudia.
Tuseme kwa mfano, birthday yako ni tarehe 1.1. kila mwaka.
Halafu Mimi nataka kila tarehe 1 Januari niwe nakutumia ujumbe wa kukutakia kheri ya siku ya kuzaliwa. Lakini nahisi naweza kusahau, au sitaki niwe naurudia kuandika ujumbe huohuo kila mwaka. Naweza kuandaa ujumbe leo ambao utakuja kwako tarehe 1 Januari na utakuwa unakuja kwako kila mwaka tarehe moja Januari.
Ujumbe unaojirudia kila wiki. Sihitajiki kurudia kuandika ujumbe huu kila wiki. Ikifika jumapili, wenyewe unaenda hewani. Kama umekuwa unapata changamoto ya ndugu kukwambia kwamba
Ooh unajua huwa hautupigiagi.
Ooh hata hutusalimii, siku hizi unalinga. Ngoja nikwambie kitu, kuanzia leo hawapaswi kukwambia huwasalimii.Wachukue hao ndugu zako wote. Waweke kwenye grup maalumu, Kisha waandalie ujumbe wa kuwatakia wikendi njema na panga ujumbe huo uwe unaenda kwao kila jumamosi saa nne asubuhi. Umemaliza. Ujumbe huo utakuwa unaenda kwao kila jumamosi asubuhi maisha yako yote, mpaka siku utakapoamua kubadilisha hilo.

App inanikumbusha nimpigie kila alhamisi ya mwisho wa mwezi Ni hivyo tu.
5. KUANDAA SMS NYINGI ZA KWENDA KWA MTU ILA ZIKAENDA KWA NYAKATI TOFAUTI
Unaweza kuandaa sms nyingi za kwenda mtu na ZIKAENDA kwa NYAKATI tofauti.Mfano unaweza kuandaa sms ya kwanza ya kwenda kwa MTU yenye ujumbe huu.
Habari, tunakushuru Sana kwa kununua simu mpya aina ya…. Siku ya leo.
Tumefurahi Sana kukuhudumia siku ya leo na tunakutakia kila kheri. Je, kuna Jambo lolote ungependa kuongea kuhusiana na huduma yetu? Kama unalo tafadhali usisite kutuambia, ahadi yetu Ni kwamba maoni utakayotoa tutayafanyia kazi.Asante Sana na karibu kwa maoni.
Siku ya pili ukaandaa ujumbe wa kwenda kwa mtu huyuhuyu unaosema hivi
Habari ya tangu jana, Sina shaka umeshaanza kutumia simu yako uliyonunua kwetu sisi….. Unaoionaje?
Unaweza kuandaa jumbe nyingi na za kutosha kwenda kwa mtu yuleyule au kikundi cha watu. Mtu/watu unaweza hata kuwaandalia jumbe za mwaka mzima au hata miezi mitatu au minne ijayo.
Kwa kutumia app hii hutasahau birthday za wateja wako au watu wako wa karibu maisha yako yote. Wewe unaweza kusahau Ila app haitasahau, itakuwa inawatumia jumbe na wataona unawajali kweli.
5. UNAWEZA KUITUMIA APP KAMA ALARM
Hapa app itakukumbusha majukumu yako ya muhimu ya kufanya6. APP INAWEZA KUTUMA SMS KWENYE WHATSAP
Mimi nimeijaribu kwa upande wa WhatsApp. App haifanyi kazi vizuri hasa pale unapokuwa unataka kutuma jumbe kwa watu wengi, Ila kitu kimoja Cha uhakika Ni kwamba kama umeandaa ujumbe wa kwenda kwa mtu mmoja, utaenda. Ni uhakika utaenda.Ila pia unapaswa kuwa mtandaoni.
7. APP INAWEZA KUKUONESHA WATU AMBAO IMEAHAWATUMIA UJUMBE NA AMBAO IMEAHINDWA KUWATUMIA
Kama kuna watu IMESHINDWA KUWATUMIA ujumbe, labda kutokana na kuwa simu yako ilikuwa imezima. App itakuonesha watu wa Aina hiyo. Na utaweza kuwarudia.Ila pia app itakuonesha watu ambao wamekamilishwa kwa kutumiwa jumbe au kupigiwa.

App ikionesha missed call baada ya mtubkunipigia na kunikosa. 8. APP ITAKUSAIDIA KUWAKUMBUSHA WANAOKUDAI WAKUTUMIE HELA YAKO😂😂
Natania tu japo ni ukweli.9. APP INA UWEZO WA KUTAJA JINA LA MTU NA KUFANYA MENGINE MENGI.
Kama unatuma ujumbe kwa wengi na ungependa kila mtu atajwe jina lake. App ina huo uwezo.
Na mengine mengi sana…

Ukitumia hii code wakati unatumia app. Itataja jina la mhusika kwenye ujumbe mfupi hata kama hukuandika jina hilo Cha kufanya sasa. Ningependa nikushike mkono kwa kukupa maelezo ya kina juu ya namna ya kuitumia app hii. Sitaki upate shida hata kidogo. Nipo hapa kukusaidia.
NB: utapaswa kulipia 50,000/- ambapo utaelekezwa na kufunzwa kila kitu kuhusiana na app hii. Wewe mwenyewe utaipenda. Gharama utakayolipa kufundishwa ni ndogo kulinganisha na mengi utakayopata.
Kama upo tayari kupata mafunzo na kushikwa mkono ili uelekeze kila kitu kihusu hii app. Lakini pia upo tayari kulipia 50,000 basi jiunge na kundi la whatsap hili hapa chini. Au tuwasiliane kwa 0755848391
https://chat.whatsapp.com/KyTsb41sK6e8R0oC6qEHGFKaribu sana
Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.
Godius Rweyongeza ni mwandishi wa vitabu zaidi zaidi ya 20. Na ni mwendeshji wa mtandao wa Songambele. Amekuwa akiandika kwenye huu mtandao huu tangu mwaka 2016. Kitabu chake cha Kutoka Sifuri Mpaka Kileleni kimekuwa #1Best Seller kwa muda sasa kwenye mtandao wa GETVALUE
Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.
Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.
Mtandaoni, vitabu vyake unaweza kuvipata kupitia mtandao wa GETVALUE kwa KUBONYEZA HAPA
- KUKUKUMBUSHA KUPIGA SIMU
-
STRIVE MASIYIWA
STRIVE MASIYIWA
Strive Masiyiwa ni bilionea wa Zimbambwe ambaye alizaliwa mwaka 1961 huko nchini Zimbambwe. Alikulia nchini Zimvambwe na baadaye alienda kusoma masomo ya chuo kikuu nchini Uingereza akisomea uhandisi. Baada ya masomo Strive Masiyiwa kama walivyokuwa watu wengine wazalendo wa kipindi kile alirudi nchini mwake kwa ajili na kuanza kufanya kazi na shirika la mawasiliano, akiajiriwa Kama mhandisi
Masiyiwa anasema kwamba, kila mara alipokuwa akitoka kazini alikuwacna mazoea ya kukutana na marafiki zake baa ili wapate moja baridi, moja moto.
Siku moja katika maongezi na rafiki zake alipendekeza kuwa watenge kiasi kidogo Cha fedha, yaani na wawe wanaweka kiasi hicho kama akiba kwenye akaunti Yao ya benki. Alipendekeza wazo hili kwa watu 10 Ila waliochukua hatua na kuweka akiba walikuwa wawili tu.
Mpaka hapo tunajifunza kuwa unaweza kuwa na marafiki wengi, Ila kumbe hao marafiki siyo wale wa kushirikiana na wewe katika upambanaji Bali wanakuwa marafiki wa bata tu! Ukiwa na mmarafiki wa Aina hii, mafanikio kwako yanakuwa magumu kwa sababu hawafikirii nje ya boksi, na hata pale wanapokuwa na wazo hawachukui hatua.
Sisi kama mabilionea mafunzoni tuna mengi ya kujifunza kutoka kwake. Kuanzia namna unavyoweza kuanzia chini kabisa, ambapo Masiyiwa anasema kwamba kwake hakuna kilichobadilika, unaanza na kile ulichonacho, unafanya kinachowezekana ili mwisho wa siku uweze kufanya yasiyowezekana.
kuja kwenye kukuza mtaji, kuja kwenye kujenga timu.
Kuja kwenye kwenye kupambania ndoto, kusaidia watu na kutoa na vitu vingine.Asilimia kubwa ya vitu ambavyo tunafanya Sasa hivi Masiyiwa alivipitia miaka mingi iliyopita.
Kadiri ya Forbes Masiyiwa Ni bilionea namba 1012
Utajiri wake ni Dola bilioni 3
Utajiri wake mkubwa unatoka kwenye mitandao ya simuAmbapo anamiliki zaidi ya 50% ya kampuni ya Econet Wireless
-
Makosa ambayo watu hufanya wanapotaka KUONGEZA chanzo kingine Cha kipato

Utakuwa umegundua kuwa wiki hii nimekuwa nikikushirikiaha nakala zinazoeleza ni kwa namna gani unaweza KUONGEZA chanzo kipato Cha ziada.
Sasa Leo napenda kukwambia kuwa bado sijamaliza nilichokusudia kukwambia. Kwenye hii makala ya leo ningependa ujue makosa ambayo watu hufanya wanapotaka KUONGEZA chanzo kingine Cha kipato. Makosa yenyewe ni
Kosa la kwanza wanaanzisha chanzo kwenye eneo ambalo wenyewe hawajui.
Kisa mtu kasikia kitu fulani kinalipa au kisa kaona mtu akifanya biashara fulani na ana MAFANIKIO, Basi utakuta kwamba na yeye anakimbilia kutaka kuwekeza huko au kuanzisha biashara ya aina hiyohiyo huku akiwa haijui Kwa undani. Ninachotaka kukwambia siku ya Leo ni kuwa unapaswa kuanzisha chanzo cha kipato kwenye eneo ambalo wewe mwenyewe tayari unalijua. Ninaposema unalijua simaanishi kwamba uwe umeshahawahi kulifanyia kazi, Bali uwe umelifanyia utafiti wa kina.
Siyo kisa umesikia eti kuna crypotocurency na wewe unakimbilia huko.
Au kisa eti unasikia mavi ya tembo ni dili na wewe unakimbilia kutafuta mavi ya tembo.Kuwa makini!
Kosa la pili ni kutojua chanzo husika kitakuwa kinaingiza kipato kwa muda gani.
Kila chanzo cha kipato huwa kinaingiza kipato kwa nyakati tofauti. Ni muhimu kwako kujua chanzo cha kipato kitakuwa kinaingiza fedha baada ya muda gani.Hatifungani huwa zinaingiza kipato kila baada ya miezi sita
Kuna kampuni hisa zake huwa zinatoa gawio kila baada ya miezi sita na nyingine kila mwaka. Hayo yote unapaswa kuyajua.
Uwekezaji kwenye miti huwa unatoa kipato baada ya muda mrefu. Kumbe basi ni jukumu lako kujua vizuri aina ya chanzo cha kipato na kitakuwa kinagiza kipato baada ya muda gani.Unahitaji kuwa na mchanganyiko. Vyanzo vinayoingiza kipato kila siku au kila wiki na vyanzo vinavyoingiza kila mwezi, baada ya miezi kadhaa na vile vya muda mrefu.
Kama ndio unaanza wekeza zaidi kwenye vyanzo vinavyotoa kipato kila siku au kila wiki au kila baada ya siku chache.
Kosa la tatu ni kubeti. Kuna wengi wanaofikiri kuwa kubeti ni chanzo, cha kipato. Vijana wengi wamenasa kwenye huu mtego. Hawafanyi kazi wala kujituma wakitegemea kubahatisha.
Rafiki yangu, maisha hayabahatishwi. Yana kanuni zake, zipo wazi kabisa.
Ukizifuata utafika mbali kabisa.Ndiyo maana tunaziongelea kwenye hii blogu kila mara.
Kosa la nne ni kuanzisha chanzo Cha kipato kinachohitaji usimamizi mkubwa wenyewe wakiwa hawapo.
Kuna vyanzo ambavyo vinahitaji usimamizi mkubwa mwanzoni. Kosa ambalo watu hufanya ni kuanzisha vyanzo vinavyohitaji usimamizi mkubwa mwanzoni huku wao wakiwa wapo mbali.
Mfano mtu anaanzisha chanzo chake cha ziada kwenye kilimo biashara huku yeye akiwa mbali. Kilimo kina mambo mengi ambayo nyuma ya pazia yanahitaji kufanyiwa kazi, kumbe basi kitu kama hiki unahitaji ukianzishe ukiwa karibu ili kufanya usimamizi wa karibu.
-
Siri Hii Wanayoijua Matajiri Unapaswa Kuijua Pia

Tujifunze kwa bahari
Kila mwaka huwa kuna mito na vijito ambavyo huwa huwa vina maji na baadaye hukauka. Wakati mito hivi na vijito, vikikauka, bahari huwa haikauki hata siku moja.
Unajua kwa nini bahari huwa haikauki, moja ya kitu ambacho huwa kinafanya bahari isikauke ni kwa sababu huwa inapokea maji kutoka kwenye vyanzo vingi. Kadiri ambavyo vyanzo hivi huwa vinaleta maji kwenye bahari ndivyo bahari huwa inazidi kuwa na uhakika wa kutokauka hata siku moja.
Hiki kitu kikufundishe na wewe kuwa, kadiri ambavyo utakuwa na vyanzo vingi vya kipato, ndivyo ambavyo utakuwa na uchumi imara na usioyumba kuliko pale unapokuwa unategemea chanzo kimoja cha kipato.
Sifa kuu ya matajiri
Sifa kuu ambayo matajiri wanayo Ni sifa ya kuwa na vyanzo zaidi ya kimoja. Richard Branson ambaye ni mmoja wa matajiri wakubwa hapa duniani, anasemekana kuwa na vyanzo 42 vinavyomwingizia kipato. Na hapa ninaposema vyanzo 42 vinavyomwingizia kipato, simaanishi kipato tu cha kawaida, Bali kipato haswa kilichoshiba.Kila mtu kuna sehemu anaanzia
Rafiki yangu na wewe Kuna sehemu unaanzia kwenye maisha, lakini usikubali kibaki hapohapo ukiwa na chanzo hichohicho. Una unwezo wa kukuza kipato chako zaidi ya hapo. Ongeza Vyanzo vya kipato walau uwe navyo zaidi ya kimojaSOMA ZAIDI
- Baadhi Ya Vyanzo Vya Kipato Ambavyo Unaweza Kuwa Navyo
- Kwa Nini Unahitaji Kuwa Na Vyanzo Vingi Vya Kipato
Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.
Godius Rweyongeza ni mwandishi wa vitabu zaidi zaidi ya 20. Na ni mwendeshji wa mtandao wa Songambele. Amekuwa akiandika kwenye huu mtandao huu tangu mwaka 2016. Kitabu chake cha Kutoka Sifuri Mpaka Kileleni kimekuwa #1Best Seller kwa muda sasa kwenye mtandao wa GETVALUE
Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.
Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.
Mtandaoni, vitabu vyake unaweza kuvipata kupitia mtandao wa GETVALUE kwa KUBONYEZA HAPA
-
Baadhi Ya Vyanzo Vya Kipato Ambavyo Unaweza Kuwa Navyo
1. Ajira
Hiki ni chanzo maarufu ambacho wengi huwa wanakuwa nacho. Chanzo hiki huwa kinaingiza kipato (ujira) kila baada ya muda fulani (siku,wiki au mwezi). Kwa MTU yeyote ambaye hana sehemu ya kuanzia hakikisha walau unaanzia kwenye ajira.Ukipata ajira hakikisha unaifanya kwa uaminifu na kwa kujituma. Maana ajira inaweza kukupelekea wewe kupata vyanzo vingine zaidi.
2. Kitabu
Naamini wewe utakuwa na uzoefu mkubwa ambao wengine wanatamani kuupata kutoka kwako. Uzoefu huu unaweza kuuweka kwenye kitabu na watu wakasoma hiki kitabu.Kama wewe umekuwa unafuga ng’ombe kwa miaka kumi sasa, tayari una uzoefu wa kutosha wa kuandika kitabu kuhusu ufugaji wa ng’ombe. Utumie uzoefu huu, kuandika kitabu. Kuna watu watapenda kusoma kitabu chako.
Leo hii unaposoma hapa, Kuna MTU sehemu anajiuliza naweza kuanza kufuga ng’ombe wa kisasa. Nini kinahitajika? Napaswa kuepuka Nini? Napata wapi ndama wa kuanza nao? MTU huyuhuyu anaendelea kujiuliza, hivi ng’ombe huwa wanachanjwa? Kila baada ya muda gani? Kwa Nini?
Na wewe una uzoefu huu, Tena wa miaka mitatu, mitano au kumi na zaidi. Kwa Nini usiandike kitabu?
Naomba unisikilize, kaa chini andika kitabu ili watu waweze kunufaika na uzoefu wako huu.
Japo watu watapaswa kununua kitabu chako ili wanufaike, ila ubora ni kwamba baada ya hawa watu kusoma kitabu chako, watakushukuru sana kwa namna ulivyowasaidia.
Unajiuliza unawezaje kuanza kuandika kitabu? Pata nakala ya kitabu cha JINSI YA KUWA MWANDISHI MBOBEVU. Nakala laini ni 5,000/- tu. Tuma fedha kwa namba ya simu 0755848391 jina ni GODIUS RWEYONGEZA.
Kitabu ni chanzo cha kipato ambacho unakitengeneza mara moja na kinaendelea kuwepo kwa miaka yote. Watu wanaendelea kununua kile ulichoandika miaka kadhaa iliyopita.
Mfano ukiandika kitabu mwaka ujao wa 2023 na ukakimaliza na kuanza kukiuza. Kitabu hicho kitaendelea kuwafaa watu hata mwaka miaka kumi, ishirini, hamsini na zaidi.
Kuna mtu atanunua kitabu hichohicho ulichoandika mwaka 2023, atakinunua mwaka 2035. Kazi yako ya Mara moja tu, itakulipa maisha yako yote. Hiki ni chanzo kizuri cha kipato ambacho unapaswa kukitengeneza.
Cha kushangaza utasoma hapa na kutikisa kichwa bila kuchukua hatua ya kuanza kuandika kitabu.
Enewei,
Ngoja mimi nikuacheIla matokeo yako ya kesho yanaathiriwa na uamuzi unaofanya sasa hivi. Na uamuzi unaofanya Sasa hivi Ni au upate kitabu cha JINSI YA KUWA MWANDISHI MBOBEVU kwa shilingi 5,000/- au la uache!
Kwa uamuzi wowote ule utakaochukua, fahamu kuwa una madhara kwenye kesho yako. Sasa je, upo tayari kuiharibu kesho yako kwa sababu hutaki kuchukua hatua ya kupata KITABU hiki?
Changamka sasa. Lipia 5,000/- upate kitabu Cha JINSI YA KUWA MWANDISHI MBOBEVU, ili ujifunze namna ya kutengeneza mfereji wako mwingine wa kipato.

Katika ulimwengu wa leo unaweza kuandika kitabu na kukiuza kwa njia ya mtandao. Kwa hiyo, ukatoa kitabu kwa gharama ndogo. Kumbe tofauti na wengine wanavyofikiri kuchapa lazima uwe na fedha nyingi, bado kuna uwezekano wa wewe wa kuchapa na kuuza kitabu kwa njia ya mtandao.
3. Kozi
Kama kilivyo kitabu, kozi pia ukiiandaa inadumu kwa muda mrefu. Unaiandaa Mara moja ila inadumu kwa muda mrefu huku ikikuingizia kipato.Labda unajiuliza Kati ya kitabu na kozi, niandae kipi? Nashauri uandae kitabu kwanza, Kisha uandae kozi.
Nazungumzia uwekezaji kwenye hisa, hatifungani na vipande. Huu ni uwekezaji muhimu sana ambao wewe rafiki yangu unapaswa kuhakikisha kwamba umeufanya.
4. Uwekezaji
Yees, na Mimi ninapozungumzia uwekezaji siongelei Mambo ya Bitcoin, sijui crypto currency au sijui nini?Ni uwekezaji ambao ni uhakika kuwa unaweza kukuingizia kipato hata Kama umelala? Kama hujawahi kuingiza kipato ukiwa umelala, hakikisha unachukua uamuzi Tena leo, wa kuanza kuwekeza kwenye HISA, hatifungani na vipande.

5. Biashara
Biashara chanzo kingine Cha kipato ambacho kwenye ulimwengu wa Sasa Ni CHANZO ambacho lazima uwe nacho. Hata kama umeajiriwa, bado unahitaji kuwa na biashara yako ambayo itakuwa unaiendesha kwa pembeni hata kama ni ndogo.Sote tunajua kuwa mshahara huwa haubadiliki mara kwa mara. Lakini kipato kwenye biashara hakina ukomo. Unaweza kukuza kipato chako kadiri uwezavyo. Hivyo, nakushauri na wewe uhakikishe unakuwa na biashara yako.
6. Kamisheni
Kamisheni ni kipato unachopata kutokana na mauzo ya vidhaa fulani ambayo siyo yako au kwa kuwaelekeza watu wanunue vidhaa fulani. Hii ni Aina ya kipato ambayo Unaweza kuifanyia kazi pia.Mfano, mimi Sasa hivi nalipa kamisheni ya asilimia 40 pale unapomleta mteja akanunua Audiobooks au softcopy zangu. Kumbe mteja mfano akinunua Audiobook ya kitabu cha NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA, ambayo kwa Sasa naiuza 10,000/-
Wewe unapata 4000/-. Just kwa kumweleza mteja tu aje kununua kwangu na akanunua.
Kwa ambaye angependa tufanye kazi pamoja kwenye hili, hakikisha tunawasikia kwenye WhatsApp yangu leo.
BONYEZA HAPA 👇🏿 kuchati nami
https://wa.me/message/3PMZSAFONLHAP1Karibu sana
7. Mrabaha
Mrabaha ni malipo unayopata kutokana na kazi ya sana au kazi ya kubunifu.Wasanii wa muziki huwa wanalipwa mrabaha kwa kazi zao kutumiwa kwenye vyombo vya habari na maeneo mengine. Mchoraji pia anaweza kupata mrabaha kutokana na kazi yake ya kuchora.
Mwandishi anaweza kupata mrabaha pale kitabu/ kazi yake inapochapwa na kuuzwa. Na kampuni za uchapishaji.

Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.
Godius Rweyongeza ni mwandishi wa vitabu zaidi zaidi ya 20. Na ni mwendeshji wa mtandao wa Songambele. Amekuwa akiandika kwenye huu mtandao huu tangu mwaka 2016. Kitabu chake cha Kutoka Sifuri Mpaka Kileleni kimekuwa #1Best Seller kwa muda sasa kwenye mtandao wa GETVALUE
Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.
Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.
Mtandaoni, vitabu vyake unaweza kuvipata kupitia mtandao wa GETVALUE kwa KUBONYEZA HAPA
-
Viashiria Vinne Vya Uhuru wa kweli. Kama hauna hivi vitu jua huna Uhuru..

Leo Ni tarehe 9 Disemba, ni siku uhuru hapa nchini Tanzania. Sikupanga kuandika chochote kuhusiana na uhuru, ila ngoja niandike haya machache kuhusiana na uhuru wako binafsi.
Watu wengi huwa wanachanganya kuwa kwa kuwa nchi iko huru Basi na wao wako huru. Siyo kweli, Kuna viashiria ambavyo vinaweza kuonesha kuwa wewe uko huru au hauko huru. Vifuatavyo Ni viashiria muhimu vinavyoonesha kuwa wewe uko huru.
Ukiona viashiria hivi vinakupiga chenga, basi pambana ili uweze kupata Uhuru wako
Kiashiria namba moja ni Uhuru wa kazi.
Uhuru wa kazi ni pale Ambapo unakuwa hulazimiki kufanya kazi ili uingize kipato. Lakini pia unakuwa unafanya kazi unayoipenda na siyo kufanya kazi unayolazimishwa kufanya. Labda nikuulize unaipenda kazi unayoifanya?Uhuru wa kazi haumaanishi kwamba uwe mzembe. Mimi Ni mwumini mzuri Sana wa kufanya kazi kwa bidii. Mara zote na siku zote hakikisha unajituma kwenye Kazi, ila fanya kazi unayoipenda.
Kiashiria namba 2 ni Uhuru wa fedha
Wazungu huwa msemo unaosema fuck you money. F*ck you money ni kiwango Cha fedha ambacho ukiwa nacho hakuna mtu yeyote anaweza kukuzuzua. Hiki ni kiasi Cha pesa ambacho ukiwa nacho hata bosi wako akizingua unaweza kumwambia f*ck you!
Kwa kusema hivi simaanishi uanze kutoa matusi kwa watu, Ila hiki ni kiasi Cha fedha ambacho ukiwa nacho, kinakupa uhuru.
Watu wengi huko makazini hawana Uhuru wa kuongea. Wana hoja nzuri ila wanashindwa kuzitoa kwa sababu wanahofia zinaweza kukataliwa na hivyo wakafukuzwa kazi.
Muda mwingine bosi anazingua au anawalazimisha kufanya vitu kinyime na vile wanavyoamini, lakini bado wanafanya kwa sababu hawana fedha, maana wakimpinga hawama kazi, hivyo hawana hela.
Kama bado hujawa na kiasi cha pesa cha kukufikisha kwenye kiwango cha f*ck you money, jua bado unapaswa kuendelea kupambana ili upate uhuru wako, maana sasa hivi huna uhuru.
Kiashiria namba tatu ni uhuru wa muda. Yaani, kwamba unakuwa na Uhuru wa kupangilia ratiba zako. Una Uhuru wa kwenda popote bila kuathiriwa na kitu chochote.
Je, unao uhuru wa muda?Kiashirikia namba nne Ni uwezo wa kuingiza fedha hata kama umelala.
Kama huwezi kuingiza fedha hata kama umelala jua bado hujawa na uhuru. Unapaswa kupambana kuhakikisha kwamba unaweza kuingiza fedha hata kama umelala. Inawezekanaje? Ndio inawezekana kupitia uwekezaji na kuwa biasharaHakikisha umesoma kitabu changu cha MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE ili ujifunze mbinu za uwekezaji ambazo zitakusaidia wewe kuingiza fedha ukiwa umelala?
Je, ni Uhuru upi ambao hauna?
Hauna Uhuru wa kazi. Basi soma kitabu cha JINSI YA KUONGEZA THAMANI YAKO (softcopy 10,000/-)Hauna Uhuru wa muda? Soma kitabu cha KUTOKA SIFURI MPAKA KILELENI (Hardcopy 12,000/-) na softcopy 7,000/-
Hauna Uhuru wa kazi? Soma kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO na NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA. Kila kitabu Ni 20,000/-
Hauna Uhuru wa fedha. Soma kitabu cha MAAJABU YA KUWEKA AKIBA na kitabu Cha MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE 20,000/-
Hivyo, ni vitabu muhimu ambavyo unapaswa kusoma kama unataka kupata Uhuru wa kweli.
Unapenda nikupe ofa siku ya leo ya Uhuru? Ndio inawezekana. Bonyeza hapa
Kisha andika OFA YA UHURU!BONYEZA HAPA: https://wa.me/message/3PMZSAFONLHAP1
Nitakupa ofa ya kitabu unachotaka siku ya leo.
Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.
Godius Rweyongeza ni mwandishi wa vitabu zaidi zaidi ya 20. Na ni mwendeshji wa mtandao wa Songambele. Amekuwa akiandika kwenye huu mtandao huu tangu mwaka 2016. Kitabu chake cha Kutoka Sifuri Mpaka Kileleni kimekuwa #1Best Seller kwa muda sasa kwenye mtandao wa GETVALUE
Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.
Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.
Mtandaoni, vitabu vyake unaweza kuvipata kupitia mtandao wa GETVALUE kwa KUBONYEZA HAPA
-
Kwa Nini Unahitaji Kuwa Na Vyanzo Vingi Vya Kipato

Unahitaji Kuwa na vyanzo vingi vya kipato
Moja ya Kitu Cha muhimu ambacho unahitaji kuhakikisha umekizingatia ni kuwa na vyanzo vingi vya kipato. Labda swali la kwanza la kujiuliza ni je, vyanzo vingi vya kipato maana yake nini?
Vyanzo vingi vya kipato, Ni pale unapokuwa unaingiza kipato kwa njia zaidi ya moja. Yaani, siyo tu unakuwa unategemea njia moja ili kupata fedha, bali unakuwa na uhakika wa kuingiza kipato kupitia vyanzo mbalimbali. Vyanzo hivyo vinaweza kuwa ni
1. Ajira yako
2. Ujuzi wako
3. Uwekezaji
4. Biashara
4. Kamisheni
5. Mrabaha n.k
Kwa nini unahitaji kuwa na chanzo zaidi ya kimoja cha kipato.
Rafiki yangu, hiki Kitu cha kuwa na chanzo zaidi ya kimoja cha kipato, hakifundishwi shuleni na hata majumbani. Hii ni elimu ambayo MTU unajiongeza kwa kuhakikisha unakuwa nayo huku mtaani. Ila ni elimu ya lazima na wala siyo hiyari.
Kuna sababu nyingi za kwa nini unapaswa kuwa na vyanzo vingi vya kipato.
Kwanza ni kwa sababu ya mabadiliko ambayo huwa yanatokea. Hiki kitu kinaweza kufanya baadhi ya vyanzo vya kipato visikuingizie kipato. Mfano mfumuko wa bei ambao umetokea mwaka huu, kwa namna moja au nyingine unakuta kwamba unaathiri kipato chako, pia. Unakuta kwamba fedha uliyokuwa nayo haitoshi kukuwezesha wewe kununua bidhaa husika. Ndio maana unahitaji kuhakikisha kwamba unakuwa na chanzo kingine Cha kipato
SOMA ZAIDI: Mfumuko wa bei maana yake nini?
Pili, ni Kujijengea kinga. Kama unakitegemea na chanzo kimoja tu cha kipato ili uingize fedha, unakuwa unapotea rafiki yangu. Kwa sababu inaweza kutokea siku moja ambapo chanzo hicho kikawa hakijaingiza kipato kama inavyostahili. Hiki Kitu kitakufanya wewe ukwame kufanikisha malengo yako. Lakini unapokuwa una chanzo zaidi ya kimoja, huo ndio unakuwa ni mwanzo wa wewe kupiga hatua Kubwa kimaisha. Kwa sababu chanzo kimoja Cha kipato kinapokwama, kingine kinakuwa tayari kufanya kazi kwa ajili yako na kuhakikisha kwamba kimekuinua zaidi.
Tatu, Huwa Kuna mabadiliko ya hapa na pale ambayo huwa yanatokea karibia kwenye kila sekta, ambayo huwa yanapelekea aidha kipato kushuka au hata muda mwingine kukoma kabisa. Ninachoshauri rafiki yangu Ni wewe kujiwekea Kinga kwa kuhakikisha unakuwa na chanzo zaidi ya kimoja Cha kipato.
Nne, ili kuingiza fedha kwa nyakati tofauti. Chanzo maarufu ambacho watu wanacho ni ajira. Ajira huwa inaingiza fedha kwa MTU mara moja kwa mwezi, mwishoni mwa mwezi, lakini unaweza kuwa na vyanzo vingine ambavyo vinaweza kukuingizia kipato tofauti na ajira na hivyo kukupa uhakika zaidi.
Tano, kufanya mishahara yako ikutane. Imezoeleka miongoni mwa wafanyakazi kuwa mishahara huwa haikutani, vyanzo vingi vya kipato vina uwezo wa kuifanya mishara yako iweze KUKUTANA.
Sita, vyanzo vingi vya kipato, vina uwezo wa kukufanya ufanye uwekezaji. Kama mshahara pekee ulikuwa haukutoshi, sasa vyanzo vingi vya kipato, vinakuwezesha wewe kufanya uwekezaji pia. Chanzo kimoja kinaweza kutumika kwa ajili ya uwekezaji na chanzo kingine kikasaidia kwenye matumizi ya hapa na pale ya kila siku
Sifa ya vyanzo vingi vya kipato
Kuna watu baada ya kusikia kuwa wanapaswa kuwa wanapaswa kuwa na vyanzo vingi vya kipato wameenda kichwakichwa na kujikuta waanzisha vyanzo vingi vya kipato, ilimradi tu wameanzisha Sasa zifuatazo Ni sifa za vyanzo vya kipato.
Kwanza, vyanzo vyako vinapaswa kuwa kwenye sekta tofauti. Yaani, usitegemee sekta moja tu kwa ajili ya kukuingizia kipato. Mfano kipindi Cha Corona Kuna baadhi ya sekta zilikwama au kufungwa kabisa, lakini kipindi hichohicho sekta nyingine zilizidi kukua na kuwa na kuwa Bora ZAIDI. Sasa kwa MTU ambaye anategemea sekta Moja kwa ajili ya kuingiza kipato, na Kama sekta hiyo iliyumba basi, ni wazi kuwa MTU huyu Atakuwa aliyunva pia.
Kwa hiyo basi, vyanzo vyako visiwe kwenye sekta moja.
Kama ni kampuni au biashara, usiwe na bidhaa moja tu, maana Kuna baadhi ya bidhaa huwa zinauzika Sana kipindi fulani. Sasa ikitokea unategemea chanzo kimoja Cha kipato na kipindi hicho chanzo hicho kikakwama, Basi Ni wazi kuwa na wewe utakwama.
Pili, Vyanzo vyako visikutegemee wewe kufanya kazi ili viingize kipato vyanzo vyako vyote rafiki yangu havipaswi kuwa vinakutegemea wewe kufanya kazi moja kwa moja ili uingize kipato.
Ndio chanzo kimoja au viwili vinaweza Kuwa vinakutegemea wewe kufanya kazi moja kwa moja, ila kama unavyojua rafiki yangu. Kufanya kazi huwa juna ukomo. Unafanya kazi na unachoka. Kumbe basi, baadhi ya vyanzo vya kipato havipaswi kuwa vinakutegemea wewe ufanye kazi moja kwa moja ili uingize kipato. Vingine vinapaswa kuwa na uwezo wa kukuingizia kipato hata kama hufanyi kazi. Vingine unapaswa kufanya kazi Mara moja na vikulipe milele. Mfano mzuri ni Kama kuandika kitabu. Ukiandika kitabu, unafanya kazi Mara moja, Ila kipato kinachotokana na kazi hiyo ya Mara moja kinakuwa cha kudumu maisha yako yote.
Au kutengeneza video kama YouTube. Ukishaitengeneza video hii ndio unakuwa umeitengeneza.Makosa kwenye vyanzo vingi vya kipato
Kosa la kwanza huwa ni kuanzisha vyanzo vyote vya kipato kwa wakati mmoja.
Kutegemea na Aina ya chanzo Cha kipato, baadhi ya vyanzo vya kipato haviwezi kuanzishwa kwa wakati mmoja. Kuna baadhi ya vyanzo vinapaswa kuanzishwa kwa nyakati tofauti, ili kukupa wewe mwanya wa kujenga chanzo kimoja kwa uhakika kwanza.Kosa la pili huwa Ni kuchanganya hela kutoka kwenye kila chanzo. Wengi wanapopokea hela kutoka kwenye vyanzo mbalimbali huwa wanazichanganaya na kuzitumia bila ya mwelekeo wowote. Hivyo basi, nashauri uwe na utaratibu wa kutofaytisha hela zinazotoka kwenye chanzo kimoja na hela zinazotoka kwenye chanzo kingine.
Na ikiwezekana kabisa uwe na malengo kwamba fedha itakayotoka sehemu fulani, nitaielekeza kwenye kufanyia kazi Jambo fulani wakati fedha ambayo itatoka kwenye chanzo kingine utafanya jambo jingine.
Tatu ni kutoa hela kwenye chanzo kimoja na kuiweka kwenye chanzo kingine.
Ni wazi kuwa pale unapoakzisha chanzo fulani Cha kipato, unakuwabunaweka fedha. Ila inabidi ifikie hatua ambapo wewe utakuwa huweki fedha, badala yake chanzo kiwe kinakupa wewe kipato.
NI VYANZO KIASI UNAPASWA KUWA NAVYO.
Hili nalo neno! Tafiti mbakimbali zimeonesha kuwa vyanzo vinne mpaka vitano, vinatosha sana kukufanya uishi maisha mazuri.Kumbe basi idadi yako ya kwanza ya vyanzo vyako vya kipato ipiganie iwe nne mpaka saba. Na Hivi viwe vyanzo vya uhakika.
Mpango wako wa kuongeza kipato Cha ziada mwaka 2023 ukoje? Unafanyaje ili kuhakikisha unakuwa na chanzo kingine Cha ziada?Karibu kwenye Semina ya kufungua mwaka 2023. Semina hii itaendeshwa kwa njia ya mtandao na imelenga kuhakikisha inakupa wewe mbinu za kuongeza kipato chako mara mbili mpaka mara kumi zaidi.
Semina hii itadumu kwa siku 15 kuanzia Januari 15 mpaka tarehe 30.
Kwa siku zote hizo 15 utalipia 15,000/- tu.Unataka kuongeza kipato chako Mara mbili mpaka Mara kumi zaidi ndani ya mwaka 2023, Basi jiunge kwenye Semina hii.
Kwa maelezo zaidi tuma ujumbe kwenda 0755848391 au
Jiunge kweye kundi letu la WhatsApp Sasa kwa kubonyeza hapa
https://chat.whatsapp.com/FbzmwEVkObKIuqeR4pIZmuKaribu sana
Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.
Godius Rweyongeza ni mwandishi wa vitabu zaidi zaidi ya 20. Na ni mwendeshji wa mtandao wa Songambele. Amekuwa akiandika kwenye huu mtandao huu tangu mwaka 2016. Kitabu chake cha Kutoka Sifuri Mpaka Kileleni kimekuwa #1Best Seller kwa muda sasa kwenye mtandao wa GETVALUE
Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.
Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.
Mtandaoni, vitabu vyake unaweza kuvipata kupitia mtandao wa GETVALUE kwa KUBONYEZA HAPA