Home


  • Kwa nini unajipunja hivyo?

    Wahaya wana usemi unaosema hivi, “endirira ekagaba emikira yayeyebwa”. Ukiniuliza tafsiri yake sijui ila nitakupa stori😂😂.

    Inasemekana hapo zamani za kale kulikuwa na mkutano wa wanyama. Kitu kikubwa kwenye mkutano huo ulikuwa ni ugawaji wa mikia.

    Mnyama aliyepewaa jukumu la kuwagawia wanyama wengine mikia ni mnyama mmoja ambaye kwa kihaya anaitwa NDIRIRA. Kiswahili chake sikijui aisee😂😂. Anayejua ataniambia baadaye nirekebishe🙈🙈.

    Sasa mnyama NDIRIRA aligawa mikia kwa wanyama wote. Wengine akawapa mikia mirefu, wengine akawapa mikia ya saizi ya kati na wengine mikia mifupi.

    Halafu, mikia ikaisha….

    Mwisho wa siku yule mnyama alijisahau, akawa amebaki na kitu kilichokuwa hakieleweki ni mkia au siyo mkia….

    Akaambulia hicho tu…

    Sasa kwa nini nimeandika hivi leo.
    Nataka nikwambie kuwa usijipunje. Una ndoto kubwa, zifanyie kazi na kitakachokuwezesha wewe kufikia hizi ndoto kubwa ni mwongozo sahihi.

    Mwongozo huu ndio nimeuandika kwenye kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO.

    Hakikisha unapata mwongozo huu wa kipekee sana, utakaokusaidia wewe kuzifanyia kazi ndoto mpaka kuzifikia. Usipopata mwongozo utakuwa unajipunja.

    Mwongozo huu unapatikana kwa 20,000/-.

    Utatuma fedha kwa 0755848391 jina ni GODIUS RWEYONGEZA halafu utaniambia uko wapi ili uweze kutumiwa kitabu hiki.

    Gharama kidogo za usafiri zitaongezeka kulingana na eneo ulipo.

    Umekuwa nami
    Godius Rweyongeza
    www.songambele.co.tz
    0755848391
    Morogoro-Tz

  • Vitu Vinne Ambavyo Hakuna Mtu Anaweza Kufanya Kwa Niaba Yako

    Kwanza hakuna mtu ambaye anaweza kupenda familia yako kwa ajili yako. Ni jukumu lako kuhakikisha unaijali na kuipenda familia yako.

    Pili hakuna mtu mtu anaweza kutunza afya yako kwa ajili yako, jukumu la kutunza afya yako ni la kwako.

    Tatu ni juu yako kuhakikisha kuwa unatunza fedha zako vizuri. Hakuna mtu ambaye anaweza kufanya hili kwa niaba yako.

    Nne, ni kuongeza maarifa. hakuna mtu anaweza kusoma na kujifunza kwa niaba yako. Ni wewe ambaye unapaswa kufanya hivyo.

    soma zaidi: Hii ni kazi anbayo huwezi kuajiri mtu kuifanya kwa niaba yako

  • Audiobook ni nini?

    Audiobook ni kitabu kilichosomwa. Yaani, kitabu kilekile ambacho ungekaa chini na kukisoma kwa siku au wiki. Zamu hii kinakuwa kimesomwa na kuwekwa kwenye mfumo wa sauti.

    Hivyo, unaweza kukisikiliza popote pale ulipo.

    Muda mwingine unaweza kukuta majukumu yamekubana, hivyo ukasikiliza audiobook vizuri tu bila ya shida yoyote wakati unaendelea na majukumu yako mengine kama kufua, kupika, au majukumu mengine yanayoruhusu usikilize audiobook.

    Muda mwingine wakati unasafiri kwenye gari yako unaweza kusikiliza audiobook yako vizuri tu.

    Audiobook ni kitabu ila kwa mfumo wa sauti.

    Kinakusaidia kupata mengi ndani ya muda kidogo. Na unaweza kukisikiliza mara nyingi kadiri uwezavyo.

    Sasa hapa tunayo audiobook ya kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO. Unaweza kuipata hii kwa  kwa elfu kumi tu (10,000/-)

    Kupata audiobook ya kitabu Cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO lipia 10,000/- kwa 0755848391 jina ni GODIUS RWEYONGEZA. Utapata audiobook bila kuchelewa.

  • Huu Ndio Ulevi Pekee Ambao Unapaswa Kuwa Nao

    Rafiki yangu mpendwa, najua umekuwa unasikia kuwa ulevi ni noma! Ulevi ni hatari. Mimi mwenyewe siyo kwamba napinga hili. Hapana, nakubaliana nalo kwa asilimia zote, ukweli ni wamba ulevi ni hatari kwa afya yako.

    Watu wanajiiingiza kwenye aina mbalimbali za ulevi. Kuna ambao wanaingia kwenye ulevi wa pombe, wengine madawa ya kulevya, wengine mitandao ya kijamii na hata wengine umalaya.

    Sasa siku ya leo napenda nikwambie aina mpya ya ulevi ambao unapaswa kujihusisha nao. Na ulevi huu ni ulevi wa kufanya kazi kwa bidii.

    Hii ndi oaina pekee ya ulevi ambayo inaweza kukusogeze mbele na kukufanya wewe uweze kufika mbali maishani mwako. Hakuna aina nyingine ya ulevi ambayo inaweza kukuletea maendeleo tofauti na aina hii tu ya ulevi. Kwa hiyo, kama unataka kufanya makubwa rafiki yangu, zama kwenye ulevi wa kufanya kazi kwa  bidii.

    Hii ndio aina pekee ya ulevi ambayo ninaweza kukushauri ujihusishe nayo rafiki yangu. aina pekee ya ulevi ambayo inaweza kukuletea maendeleo.

    umeshasoma kitabu changu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO? Hiki ni kitabu ambacho kitakufanya ufikiri kwa ukubwa lakini pia uanze kuzifanyia kazi ndoto zko kwa bidii kubwa,

    Kkupata kitabu hiki wasiliana na 0755848391

    Fanya hivyo sasa hivi.

    Umekuwa nami

    Godius Rweyongeza

    0755848391

    Morogoro-Tz

    Kwa maswali, maoni au booking: songambele.smb@gmail.com

  • Niweke Fedha zangu benki Kama akiba au niwekeze kwenye CRDB Mzigo Flexi?

    Juzi kuna mtu alinipigia simu. Alikuwa ameniakiliza kupitia TEMINO YA CLOUDS FM. Swali lake lilikuwa moja tu na hakuwa na kitu kingine cha ziada

    Alitaka kujua kipi ni Bora, Kati ya kuweka fedha yake benki au kuwekeza kwenye CRDB Mzigo flexi!

    Unajiuliza kwani CRDB MZIGO FLEXI ni nini?

    Huu ni aina ya uwekezaji ambapo unaikopesha benki ya CRDB fedha, halafu yenyewe inawekeza kwenye miradi mbalimbali baadaye inakupa faida ya asilimia 9. Kwa mwezi, baada ya miezi mitatu, sita au kwa mwaka.

    Haya ni makubaliano ambayo mnaingia Kati yako wewe na CRDB, kwa hiyo fedha yako unapoiweka huku inakuwa salama na wanapaswa kukulipa wewe kiasi cha fedha mlichokubaliana.

    Kama umesoma kitabu changu cha MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE utagundua Kuwa Hii Ni aina ya HATIFUNGANI.

    Kama hujasoma kitabu changu hiki cha kipekee ngoja nukupitishe tu kwa haraka.

    Kuna aina mbili za hatifungani:

    Hatifungani za serikali (ambapo wewe unaweza kuikopesha serikali hela yako kwa makubaliano ya kuwa ikurudishie hela yako pamoja na hiyo faida ya kila baada ya muda fulani ambapo mara nyingi huwa ni kuanzia miezi sita, miaka mitatu, kumi na hata ishirini au ishirini na tano.

    Hatifungani za serikali huwa zinatolewa na benki kuu ya taifa (BOT).

    Pia Kuna hatifungani za makampuni ambapo unaweza kuikopesha kampuni fedha zako kwa makubaliano hayohayo Kama unayoyafanya kwa serikali.

    Sasa CRDB mzigo Flexi. Nadhani itakuwa flexible Ila wamefupisha 😂😂 ni hatifungani ila za kampuni.

    Tofauti kati ya hisa hatifungani

    Jamani jamani! Ambao hamjasoma kitabu cha MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE mnakosaa mengi. Niseme nisiseme!

    Tofauti kubwa iliyopo Kati ya hisa na hatifungani ni kwamba ukinunua hisa za kampuni fulani, wewe unakuwa ni sehemu ya mmiliki wa kampuni husika.

    Lakini ukinunua hatifungani, unaikopesha kampuni. Kuna tofauti kubwa hapo.

    Hiki kitu kinamaanisha kuwa endapo kampuni itafilisika Kama wewe ni mmiliki wa hisa kwenye Kampuni, hutapata chochote maana wewe mwenyewe ni mmiliki wa ile kampuni iliyopata hasara.

    Ila kama umeikopesha kampuni (umenunua hatifungani), hiyo ni stori nyingine kabisa.

    Yaani, kampuni itakazimika kuuza rasilimali zake zitakazokuwa zimebaki Kama majengo na uwekezaji mwingine ili kukulipa wewe.

    Any way, sasa baada ya kueleza hayo yote kwa kina ndio sasa nataka nikueleze nilivyomjibu yule mtu wangu wa juzi.

    Kumbuka aliuliza

    Niweke Fedha zangu benki Kama akiba au niwekeze kwenye CRDB Mzigo Flexi ?
    Yule mama aliendelea kuniambia kuwa alikuwa na milioni kama tatu hivi na ile fedha alikuwa anaiweka kwa ajili ya mwanae ambaye yupo darasa la saba sasa.

    Nilimwambia hivi, kulinganisha na riba inayotolewa kwenye akaunti za benki, hata kama ni akaunti ya mtoto, ni vigumu sana kupata riba ya asilimia 9 kwa mwaka. Ikizidi sana, sana, itakuwa asilimia nne. Hapo imezidi.

    Ila kwa riba ya asilimia 9 ukilinganisha na akaunti ya kawaida ya benki Ni Bora tu kuweka fedha zako huku utakapopata riba ya asilimia 9.

    Nikaweka kituo. Nikamwambia achukue kitabu cha MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE. Baada ya dakika tano tu, nikaona Mpesa inasoma hivi

    9ES67XC1Z imethibitishwa mnamo tarehe 27/5/22 1:23 PM, toa 30,000 kutoka kwa…

    Alikuwa ametuma fedha kwa ajili ya vitabu viwili. Kwanza ni kitabu Cha NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA na
    ebook ya MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE pamoja na nauli ya kumtumia kitabu.

    Sasa hivi anaendelea kusoma vitabu vyake.

    Ebu na wewe hakikisha unapata nakala laini ya kitabu cha MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE kwa 5,000/- tu. Tuma fedha kwa 0755858391 jina ni GODIUS RWEYONGEZA.

    Kumbuka hiki ni kitabu pekee kitakachokufundisha wewe uwekezaji kwenye HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE kwa namna ambayo hujawahi kujifunza.

    Naamimi sasa umeelewa CRDB mzigo Flexi ni Nini na tofauti take na akiba ya kawaida.

    Pata nakala yako, wasiliana na 0755848391

  • Tofauti Ya Thamani Ya Hisa Na Bei Ya Hisa

    Huyu ni msomaji wa kitabu changu cha MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE

    Habari ya leo. Siku ya leo ningependa kujibu swali la mtu mmoj amabye amesoma kitabu changu cha MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE.

    Anauliza swali hivi, samahani kuna kitu sijakikujua hapo, tofauti kati thamani yahisa na bei ya hisa

    Kwa hiyo hapa kitu cha kujibu ni je, thamani ni nini? na bei ni kitu gani?

    kwa kawaida thamani ya hisa huwa ni sawa ni bei ya ya hisa ya wakati  husika. Kwa hiyo, kama hisa zinauzwa kwa shilingi 500, hiyo ndiyo itakuwa thamani yake pia.

    Kitu hiki pia ndio kinatumika kupima utajiri wa watu. kwa mfano ukisikia wanasema bilionea fulani ana utajiri wa bilioni kadhaa ni kulingana na bei ya hisa kwenye soko la hisa, ambayo ndio inatuletea thamani ya utajiri wake.

    Kwa mfano, ukifuatilia orodha ya mtajiri hapa duniani. Utagundua kwamba utajiri wao unakuwa unapanda na kushuka kila mara. Kinachofanya utajiri wao ushuke au kupanda siyo kitu kingine bali ni kupanda na kushuka kwa hisa. Kadiri hisa zinavyopanda au kushuka bei, ndivyo utajiri wao unapanda na kushuka.

    Hili suala la kupanda na kushuka kwa bei ya hisa huwa linatokana na jinsi watu wanavyonunua na kuuza hisa zao.

    Ikumbukwe kuwa hisa ni bidhaa zilizo sokoni, kama zilizyo bidhaa nyingine.  Tuchukulie mfano wa kawaida tu wa nyanya sokoni. Kuna kipindi nyanya zinakuwa adimu na hivyo bei yake inakuwa juu. Na kuna kipindi nyanya zinakuwa nyingi sokoni na hivyo bei yake inakuwa chini. Hivyohivyo, kwenye suala zima la hisa.

    Kupanda na kushuka kwake huwa kunategemea na jinsi ambavyo watu wanauza na kununua. Wanunuaji wakiwa wengi, maana yake kuna uhitaji, hivyo ambavyo thamani ya hisa itapanda na kadiri wauzaji wanavyokuwa wengi maana yake uhitaji ni mdogo na thamani ya hisa inashuka.

    Thamani halisi ya hisa.

    Hizo thamani za hisa zote huwa zinatokana na mihemko ya wanunuaji. Maana yake, watu ndio wanaweza kufanya thamani ya hisa ipande au kushuka. Hata hivyo, ukitaka kujua thamani halisi kabisa ya hisa unapaswa kutumia taarifa za ndani ya biashara.

    Na yenyewe inapatikana kwa kuchukua rasilimali zote za kampuni kisha unatoa madeni yote ambayo kampuni inadaiwa, halafu unagawa kwa idadi ya hisa zote zilizo sokoni.

    Thamani ya hisa =Rasilimali zote za kampuni (thamani kwa shilingi au dola)- madeni yote ya kampuni ÷ Idadi ya hisa zote zilizo sokoni

    Kama kampuni tayari imeshaingia kwenye soko la hisa, taarifa hizi unaweza kuzipata kwa kufuatilia taarifa zake za mwaka au mhura husika.

    Kama ndio inaingia mara ya kwanza kwenye soko la hisa utazipata kwenye ripoti yake inayotolewa kwa umma. Hata hivyo, utafiti binafsi unahitajika kwenye hili.

    Kama bado hujasoma kitabu changu cha MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE, nashauri sana usome kitabu hiki.

    Kitabu kingine cha nyongeza ni kitabu cha NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA

    Unaweza kupata vitabu hivi kwa kuwasiliana na 0755848391

    Fanya hivyo sasa hivi.

    Umekuwa nami

    Godius Rweyongeza

    0755848391

    Morogoro-Tz

    Kwa maswali, maoni au booking: songambele.smb@songambele

  • Kama Wewe Ni Shabiki Wa Yanga au Simba Hakikisha Umesoma Hapa

    Jana ilikuwa ni mechi ya simba na Yanga. Ni moja ya mechi zinagusa watu wengi kwa hapa Tanzania. Kuna watu hawashabikii timu yoyote ile hapa duniani, isipokuwa simba au Yanga.

    Sasa leo nilikuwa nikifikiri kuhusu hili nikawakumbuka rafiki zangu ambao wanahangaika kuandika vitabu. Wanahangaika na hawajui kitu gani wanaweza kuandikia. Nikasema ngoja leo niwaambie kitu.

    Kama wewe unajiuliza ni shabiki wa yanga au simba na unajiuliza ni aina gani ya kitabu unaweza kuandika. Ebu kuanzia leo hii tuandikie kitabu kuhusu ushabiki wako na timu yako.

    Ebu tuambie kwa nini unaipenda Simba au YANGA. Ilikuwaje mpaka ukaipenda simba au Yanga.

    Kwa nini mpaka leo hii wewe unaendelea kuishabiki hii timu

    Nini mpango wako kwa siku za mbeleni juu ya hii timu?

    Je, ushabiki wako nje ya hizi timu ukoje?

    Je, huwa unatumia kiasi gani kwa mwaka kwa ajili ya hii timu? Iwe ni kuangalia mechi, kutoa michango n.k

    Kuna mambo mengi san asana ya kuandika kuhusu simba na yanga tu, ambayo ni kitabu tosha.

    Nadhani kitabu chako unaweza kukiita. MIMI NI YANGA AU SIMBA DAMU.

    Au USHABIKI WANGU DHIDI YA SIMBA au YANGA NI MPAKA KIFO

    Au hata unaweza kusema NIMEFUNGA NDOA NA SIMBA au NIMEFUNGA NDOA NA YANGA. hahah

    Ni mapendekezo tu. lakini hii yote ni kutaka kukuonesha kwamba unaweza kuandika kitabu kuhusiana na hili nab ado tukasoma kitbu chako.

    Kwa hiyo kuanzia leo hii usije ukasema kwamba mimi sina cha kuandika na wala sijui nianzie wapi. Aznia hapohapo.

    Tukutane siku nyingine

    Kwa maswali, maoni au booking: songambele.smb@gmail.com

    Umeshapata nakala yako? Wasiliana na 0755848391

  • Mtaka cha uvunguni

    Leo nimemkumbuka jamaa mmoja niliyesoma naye shule ya msingi na baadaye sekondari. Huyu jamaa alikuwa anapenda maisha mazuri sana, ila alikuwa hataki kufanya kazi ili kuyapata hayo maisha mazuri.

    Alikuwa anapenda kufanya kazi kwenye ofisi nzuri ila alikuwa hapendi kupitia kwenye ule mchakato wa kumfikisha kwenye hiyo ngazi. Hivi kweli kitu kama hiki kinawezekana kweli

    Yaani, itokee tu siku moja upo kwenye gari unaendeshwa kwenda kazini. unafika ofisini watu wanakuita bosi, bosi, bosi. Unasaini tu na kuondoka bila kufanya kitu chochote…Linawezekana hili kweli…

    Sidhani hata kama mabosi wenyewe wanafanya hivi..

    Kanuni ya asili ni kwamba, ili upate vinono, sharti ukubali kuvilipia gharama.

    Mtaka cha uvunguni sharti ainame.

    Huwezi kutaka kuishi maisha mazuri, wakati wewe mwenyewe  Kwa hiyo, ondoa huo mtazamo wako uliokuwa nao.

    • jua kitu unachotaka kwenye maisha, ila sasa kuwa tayari kulipa gharama ili uweze kukifikia.
    • fanya kazi kwa bidii. Waru wanaweza kukushind kwenye vitu vingine vyote. Wanaweza kukushinda kwenye kipaji, watu wanaweza kukushinda kwenye kujituma, ila wasikushinde kwenye kuchapa kazi kwa bidii. Chapa kazi kwa bidii mpaka kieleweke
    • Onesha kazi yako Haitoshi tu wewe kusema kwamba u mbunifu. Au kusema kwamba una kipaji, bila kuonesha kazi yako. Onesha kazi zako kwa watu. Watu wataziona hizo kazi, na hapo sasa ndipo wataamua kuwa wazichukue hizo kazi au la. Ila usichoke kuonesha kazi zako. Onesha kazi zako mara zote
    • na kutokea hapo sasa, ndio siku moja utajikuta upo kwenye gari unaendeshwa, upo kwenye ofisi wenye kiyoyozi na mengine mengi.

    Mimi nakuamini sana ila unapaswa pia kufanya kazi, ili hayo yote unayoyatamani yaje kwenye uhalisia.

    Umeshapata nakala zako. Kama bado wasiliana na 0755848391 ili utumiwe nakala zako popote pale ulipo duniani.

  • Hii ni kazi anbayo huwezi kuajiri mtu kuifanya kwa niaba yako

    Unaendeleaje rafiki yangu wa ukweli. bila shaka kila kitu kinaenda vizuri upande wa huko. Siku ya leo ningependa nikujuze kazi mbili ambazo huwezi kumwajiri mtu kuzifanya kwa niaba yako. Na kazi hizi siyo nyingine bali ni

    Moja kufikiri. Hiki ni kitu ambacho huwezi kumwajiri mtu ili akifanye kwa niaba yako. Badala yake ni kwamba unapaswa ukifanye wewe mwenyewe bila kujali unapitia hali gani. kufikiri kwa ajili ya kesho yako, ni jukumu lako na hakuna mtu ambaye anaweza kufanya hilo kwa niaba yako.

    Kufikiri kwa ajili ya kesho ya kampuni au biashara yako, ni jukumu lako na hakuna mtu mwingine ambaye anaweza kufanya hicho kitu kwa niaba yako.

    Kwa hiyo kuanzia leo hii, fahamu kuwa huu ni wajibu wako, na hakikisha kwamba unaufanyia kazi..

    Pili ni kupanga ratiba yako. Hili ni jukumu lako jingine ambalo huwezi kumwajiri mtu kulifanya kwa niaba yako. Wewe mwenyewe unapaswa kuwa tayari kulifanya. Kila mwishoni mwa wiki unapaswa kutenga muda maalumu ambapo utaipangilia wiki yako. Muda ambapo utafanya na kukamilisha majukumu ya wiki ijayo. Na kila siku jioni unapaswa kupanga ratiba ya kesho yako. Kiasi kwamba ukiamka tu asubuhi, basi unaanza kuifanyia kazi hiyo ratiba kama ambavyo umeipangilia.

    Sikiliza kitu kimoja, kama huwezi kupangilia ratiba yako kwa ufanisi na ubora unaotakiwa, unapaswa kujua kwamba majukumu yako utayafanya hovyohovyo. Sasa kazi ni kwako. je, upo tayari kufanya majukumu yako hovyohovyo au utaanza kupangilia ratiba yako kiufanisi?

  • Mapambano yanaendelea!

    Kwenye Moira wa MIGUU, timu huwa haishindi wa kufunga goli dakika ya kwanza. Hata timu ukifunga goli dakika ya kwanza. Bado huwa haitangazwi Kuwa imeshinda.

    Badala yake Ni mchezo huwa unaendelea mpaka dakika ya 90.

    Na wewe fahamu kuwa mapambano yanaendelea. Hujafaulu kwa sababu ushindi wa muda mfupi uliopata. Huu ushindi huo wa muda ukupe NGUVU ya kuendelea mbele ila siyo kukufanya ubweteke.

    Mapambano yanaendelea.

    Imeandikwa na Godius Rweyongeza
    0755848391
    Morogoro-Tz

    For booking: songambele.smb@gmail.com

X