Home


  • Namba Zetu Za Malipo

    Namba za malipo ya vitabu:

    Namba za lipa

    TIGO PESA: 19016638 Jina ni SONGAMBELE CONSULTANTS

    M-PESA: 5564517 jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

    Namba za kawaida

    AIRTEL MONEY: 0684408755
    TIGO PESA: 0655 848 392
    M-PESA: 0745 848 395

    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    NB: Kama namba ya malipo anatumiwa mtu ambaye yuko nje ya nchi. Iandikwe Kwa kuanza na +255

    Kwa hiyo namba zinazotumwa nje ya nchi zitakuwa
    Airtel money: +255 684 408 755
    TIGO PESA: +255 655 848 392
    M-PESA: +255 745 848 395

    KOTE Jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Kama malipo yatakuwa yanafanyika kupitia benki.

    Yafanyie kupitia

    1. CRDB BANK: 0150770710200
    2. NMB BANK: 22110047274

    Kote jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

  • Wasiliana na Godius Rweyongeza Sasa

    Habari yafuatayo ni mawasiliano Unayoweza kutumia kumpata GODIUS RWEYONGEZA

    Simu: +255 (0) 684408755

    Whatsap: +255 (0) 755848391

    Email: songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu vyake wasiliana Moja kwa Moja na +255 (0) 684408755 (more…)

  • Njia Mpya Ya Kujenga Tabia Kwa Haraka

    Leo nataka nikwambie kitu kikubwa ambacho kitakusaidia wewe kuweza kujenga tabia mpya kwa haraka. Ebu fikiria tabia yoyote ile ambayo ungegependa kujenga miashani mwako. Ni tabia gani nzuri ambayo kwa siku umekuwa unatamani kuwa nayo?

    Je, ni kusoma vitabu?

    Je, ni kuandika

    Je, ni kufanya mazoezi?

    Au kuweka akiba?

    Ni kitu gani haswa unataka uwe nacho ila sasa umekuwa unashindwa?

    Je, ni kuboresha na kujenga mahusiano mazuri na mwenza wako?

    Leo nataka nikwambie hivi. unaweza kujenga tabia mpya au kufanya kitu chochote kile ulichokuwa unatamani kufanya maishani mwako kwa kutumia kanuni ndogo tu ya dakika mbili.

    Na dakika mbili siyo dakika nyingi sana rafiki yangu.

    Ebu kwa mfano sasa hivi unavyosoma hapa. chagua kitu kimoja ambacho ungependa kufanyia kazi kisha kifanyie kazi sasa hivi unavyosoma hapa. acha kwanza kusoma hapa kifanyie kazi kisha urudi kumalizia.

    Unaona eeh.

    Badala ya kubaki na ndoto kubwa ya kuwa mwandishi na kuendelea kutamani kuwa mwandishi, kaa chini uandike ndani ya dakika mbili. ukiandika sentensi mbili. zinatosha na ni za kwako. Kesho utaongeza nyingine mbili na kesho kutwa utaongeza nyingine mbili. ukiweza kuandika kwa mwaka mzima, siyo siri hizi dakika mbili zitakusaidia hata kuandika kitabu kikubwa tu.

    Bado unabisha tu. Ebu fanyia kazi hii kanuni ya dakika mbili kwa mwezi huu mmoja tu halafu utanipa mrejesho.

    Kama ni mazoezi badala ya kusubiri upate masaa mawili ya kufanya mazoezi. Amka sasa hivi nenda hapo mbele ya uwanj na ufanye mazoezi ndani ya dakika mbili tu. au unaweza kufanyia hata hapo chumbani kwako kwa dakika mbili tu. dakika mbili siyo nyingi na wewe huwezi kushindwa kufanyia kazi kitu kwa dakika mbili tu.

    Kama ni kuboreshamahusiano yako, tumia kanuni hii hii ya dakika mbili. tumia dakika mbili kuandika vitu viwili unavyopenda kwa mwenza wako. Kushukuru kwa kizuri alichokufanyia na hata kuongea naye.

    Unaona eeh. Dakika mbii siyo nyingi sana, na zinaweza kukusadia wewe kufanya makubwa.

    Ikitokea umepanga kufanyia kazi kitu fulani ila mzuka ukapanda ukakifanya kwa dakika zaidi ya hapo, basi. Ila hata mzuka usipopanda ukitumia hizo dakika mbili tu. inatosha.

    Nadhani hata hii makala umeisoma kwa dakika mbili. kama siyo basi, maana mwenyewe nilidhamiria uisome kwa dakika mbili tu.

    Tukutane wakati mwingine

    Ni mimi

    Morogoro-Tz

    0755848391

  • Kwa nini wazazi wanawalazimisha watoto kusoma kozi wanazopenda wao

    Kila mwaka kikifika kipindi cha wahitimu wa kidato cha sita kuomba vyuo, huwa napokea simu za vijana ambao wanalazimishwa na wazazi kwenda kusomea kozi wasizopenda.

    Unakuta kijana anataka akasomee uhandisi, mzazi anataka akasomee human resources.

    Sasa leo kwa ufupi tu nataka niseme kwa nini, wazazi wanakuwa hivyo:

    Moja ni kwa sababu ilikuwa ndoto ya mzazi, ikamshinda sasa anaisukuma kwa mwanae.
    Unakuta mzazi wako alikuwa na ndoto ya kuwa daktari ila udaktari ukamshinda, akaapa kuwa nitahakikisha mwanangu anakuwa daktari. Sasa bila kujali wewe unaupenda au huupendi, utakuta anakulazimisha ukausome.

    Kitu hiki siyo sahihi. Kama wewe ni mzazi unapaswa kufahamu kuwa jukumu lako siyo kumchagulia mwanao kozi ya kusoma Bali kumwongoza na kumwacha achague mwenyewe.

    Wazazi wengi huwa wanatumia nguvu waliyonayo kama wazazi kuwalazimiaha watoto kuchagua kozi wanazotaka waaome. Na muda mwingine kuwatishia watoto kuwa endapo wataenda kinyume watawaadhibu kwa kuwanyima ada.

    Mzazi kama mzazi unapaswa kuwa shabiki kwa kile anachofanya mwanao na anachopenda kufanya.

    Kama wewe ulikuwa na ndoto za kusomea kitu fulani Ila ilashindikana, basi. Hiyo imepita, mwache na mwanao apambane na hali yake.

    Pili ni kwa sababu, ya walivyowaona ndugu wengine.
    Unakuta mzazi kamwona ndugu au rafiki yake amesomea kitu fulani na anatamani hicho kitu, basi analazimisha na mwanae asomee hicho kitu.

    Unachopaswa kufahamu mzazi ni kuwa ukiona ndugu au rafiki amesomea kazi fulani na anaifanya inamlipa, jua kasomea kitu anachopenda. Na wewe mwache mwanao akasomee anachopenda.

    Kitu kingine Ni kwamba, ajira inayolipa leo, haitakuwa inalipa kesho. Hivyo, Leo unaweza kumwambia mwanao kasomee kozi fulani inalipa Sana. Ila kesho kozi hiyohiyo ikawa haina dili kwenye soko la ajira….

    Ndio maana nawashauri vijana wengi waaomee kile wanachopenda wenyewe.


  • Kozi gani nzuri ya Kusoma chuo inayolipa

    Sikumbuki ni mara ngapi watu wamekuwa wakinitafuta kwa ajili tu kuniuliza kozi gani ambayo mtu akisoma itamlipa. Nimejitajidi kujibu swali hili kadiri ninavyoweza kwa kila mtu, Sasa leo nataka nijibu swali hili mwanzo na mwisho.

    ujumbe niliopokea kutoka kwa mmoja wa wafuatiliaji wa kazi zangu

    Jibu la swali hili halina exception. Haijalishi umehitimu kidato Cha nne na unataka kwenda chuo au umehitimu kidato Cha sita na unatakiwa kwenda chuo. Kama swali lako unajiuliza ni kozi gani inayolipa basi soma hapa uone.

    Zamani ulikuwa hivi, ulitakiwa kwenda shuleni, kusoma kwa bidii ili baadaye yje uajiriwe serikalini! Serikalini ndipo kulikuwa na uhakika wa ajira maana ulipoajiriwa huko kulikuwa na uhakika kuwa utafanya kazi mpaka unastaafu na hatimaye ungepata kiiunua mgongo na kwenda zako kifurahia maisha. Siku hizi Mambo YAMEBADILIKA.

    Kuna kipindi udkaktari ulikuwa dili sana. Hivyo, kusoma tu udkatari kulikufanya wewe uwe kwenye nafasi nzuri ya kutoboa.
    Wanafunzi wengi walikimbizana na kusoma udkaktari na masomo yanayohausiana na udaktari, hata kama hawakuwa na ule moyo wa kutibu.  Nadhani ndio maana kulitokea madkatari waliokuwa wanapasua kichwa badala ya mguu…Natania tu!!
    Lakini siku hizi madkatari nao wapo mtaani wanasugua benchi.

    chanzo: Jamii Forums

    Baadaye uanasheria ulivuma. Kama ulitaka kuajiriwa ulipaswa kuwa mwanasheria. Siku hizi wanasheria nao wanasugua benchi mtaani, hawana ajira.

    Ualimu nao kuna kipindi ulitamba sana. Kama ulitaka kuajiriwa ulipaswa kusoma ualimu. Juzi kuna mtu nilikuwa naongea naye akaniambia amesomea ualimu Ila sasa ajira ameamua kwebda kusomea umeme…..

    Sasa sijui huko kwenye umeme atapata AJIRA….

    Ebu kwanza niache ninywe maji….au niagize soda utalipia wewe 😂😂.

    Sasa Kwa nini Ushauri Huu Haufanyi Tena Kazi?

    Jibu Ni moja tu. Zama Zimebadilika…

    Kabisa. Ushauri wa nenda shuleni, kasome kwa bidii utaajiriwa serikalini umepitwa na wakati. Ulikuwa Ni ushauri wa Zama za viwanda. Mtu yeyote ambaye aliutumia ushauri huu kipindi hicho alitoboa Ila kwa ukiutumia ushauri huohuo, unatoboka mwenyewe…

    Nifanyeje Sasa? Nisome kozi gani itakayonipa ajira. Ukweli ni kwamba kozi inayolipa kwa sasa ipo moja tu ila yenyewe haupaswi kuisoma kwa mkumbo wa kuajiriwa.  Nakuomba sasa uangalie video hii hapa chini ambapo nimeeleza kwa kina kozi inayolipa zaidi kwenye zama hizi

  • Mjasiriamali ni nani

    Siku hizi kumekuwepo na wimbi kubwa la vijana wanaojiajiri. Hiki ni kitu kizuri, hata hivyo wengi wamekuwa wanadhani kujiajiri tu kunakufanya uwe mjasiriamali.

    Kwa wengine ujasiriamali umekuwa unahusishwa na kutengeneza bidhaa kama vile sabuni, vitenge, viatu vya kimasai…..

    Ukiwa unatengeneza hivyo vitu, wewe ni mjasiriamali. Kama hutengenezi hivyo vitu wewe siyo mjasiriamali. Kitu ambacho siyo kweli?

    Ujasiriamali unaanza kwa kutatua tatizo lililopo kwenye jamii. Lakini haushii hapo…
    Kutengeneza bidhaa ni sehemu moja. Unaweza kutengeneza bidhaa Ila bidhaa hizo kuuzwa unakuwa bado hujafaulu.

    Wengi wamekuwa wanategeneza bidhaa Ila sasa wanashindwa kuziuza. Ujasiriamali wa kweli upo kwenye vitu viwili.

    Kutengeneza bidhaa ya kweli au kutoa thamani kubwa na
    Kuuza.

    Unaweza kutengeneza bidhaa Ila kama hujui kuiuza utabaki unaijua mwenyewe.

    Kwa hiyo kama wewe unatengeneza vitenge, viatu vya kimasai au sabuni, usiishie tu kujiita mjasiriamali kwa sababu umejua kutengeneza hizo bidhaa. Nenda kaziuze kwa watu

    Ukienda kuuza bidhaa zako ndio utagundua kuwa kazi kubwa haipo kwenye kutengeneza bidhaa bali kuuza.

    Kwa hiyo mjasiriamali Ni mtu AMBAYE anatatua changamoto za watu na kuwauzia watu suluhisho.

  • Siri Mbili Za kuwa Kiongozi Bora Kutoka Kwenye Kitabu Cha My Story Cha Sheikh Mohammed bin Rashid Al Maktoum

    1.Siri ya kuwa Kiongozi Bora kuwasikiliza watu wako na kuwa karibu na watu wako.

    Mwandishi anasema kwamba hiki Ni kitu ambacho alijifunza kutoka kwa babu yake na alikuja kukifanyia kazi yeye mwenyewe kwenye maisha yake.

    Ukiwa karibu na watu wako ni rahisi kujua matatizo yao na hivyo kujua wanataka Nini?

    2. Unapaswa kubadilika la sivyo mabadiliko yatakubadilisha. Huu ni usemi ambao aliusema kwenye hotuba yake mwaka 2004 wakati akihutubia viongozi wa nchi za kiarabu.

    Miaka 60 na 70 nchi nyingi za kiarabu zilifanya mapinduzi ya kivita. Na wote waliokuwa wanafanya mapinduzi kuna aina  fulani ya maisha walikuwa wanataka. Wengi walikuwa wanaona viongozi hawatendi haki na wananchi wanaonewa. Lakini baada ya wao kuingia madarakani walisahau hilo na kuanza kufanya yaleyale ambayo wao walikuwa hawataki.

    Na hapo ndipo aliwaambia kuwa BADILIKA au la sivyo mtabadilishwa.

    Hapa Kuna somo kubwa sana kwetu. Watu wengi huwa wanapenda kuhubiri mabadiliko Ila wao wenyewe huwa hawapo tayari kubadilika.

    Ngoja nikwambie kama unataka mabadiliko, basi anza wewe kubadilika la sivyo utabadilishwa.

    Kama ungependa kupata kitabu hiki jaza taarifa zako hapa chini, nitakutumia kwako bila kuchelewa

    Kila la kheri
    Umekuwa nami
    Godius Rweyongeza
    0755848391
    Morogoro-Tz

  • [eBOOK MPYA] NGUVU YA KUTOA (THE MAGIC OF GIVING)

    Utangulizi

    Rafiki yangu kuna nguvu kubwa sana katika kutoa. Hii ni tabia ambayo unapaswa kujifunza na kuifanyia kazi kila siku. Nadhani utakuwa umewahi kusikia kuwa matajiri wana hadi mashirika ambayo yanahusika na utoaji. Kwa mfano, Bill Gates ana shirika la GATES AND MELINDA FOUNDATION. Elon Musk ana shirika la MUSK FOUNDATION na mabilionea wengine pia wana mashirika au tasisi zinahousika na utoaji au la wamejiunga moja kwa moja na shirika la Bill Gates au shirika jingine ambalo wao wameona linawafaa. Hii ni kwa sababu kutoa kuna nguvu kubwa sana kwenye maisha.

    Kwa asili ni kwamba, kadiri unavyotoa ndivyo unapokea zaidi. haupungukiwi chochote kile unapotoa. Ndio maana unaona kwamba mabilionea wanaotoa, wanazidi kuwa mabilionea zaidi na zaidi. Kutoa kwao hakuwafanyi washindwe kuendelea kukua zaidi. kwa hiyo kama ulikuwa unaamini kuwa ukitoa labda utaishiwa, siyo kweli.

    Hivyo na wewe anza kujenga utaratibu wa kutoa. Hakikisha kwamba kwako haipiti siku bila ya wewe kuwa umetoa kitu chochote kile hata kama kitu hicho ni kidogo. unaweza kununua hata mfuko wa pipi na kila siku ukawa unatoa pipi moja tu kwa mtu mmoja kwa mwezi mzima. Na siyo kwamba utoe kwa mtu huyo huyo huyo kila siku. Bali kila siku toa kwa mtu yeyote kitu. Hii itaimarisha misuli yako ya kutoa. Mwanzoni unapoanza utaratibu wa kutoa kwa watu, kinakuwa ni kitu kigumu lakini kadiri unavyoendelea misuli yako inazidi kuimarika na hivyo unajikuta kwamba unaweza kutoa vizuri tu bila shida yoyote.

    Sasa hili suala la kutoa linaweza kuwa linakuchanganya kidogo. wewe unaweza kuwa unaona kwamba hauna kitu cha kutoa. Au pengine unasubiri mpaka pale utakapokuwa milionea au bilionea ili utoea. Ila ukweli ni kwamba hakuna binadamu ambaye ni masikini kiasi cha kukosa kitu cha kutoa. Hivyo, katika ngazi yoyote ile ulipo, una uwezo wa KUTOA

    Ninatoa nini sasa wakati sina fedha?

    Na hapa ninapozungumzia kutoa simaanishi kwamba, utoe fedha peke yake. Fedha ni kipengele kimojawapo cha kutoa kwa watu. Ila kuna vitu vingine ambavyo unaweza kutoa ikiwa ni pamoja na muda wako, nguvu zako, furaha yako, kuwasaidia watu kutengeneza maisha bora na utajiri, kuwaburudisha watu kwa kipaji chako, kuwashirikisha wengine maarifa, makala na vitabu n.k

  • 1. UCHAMBUZI WA KITABU CHA THE 5 SECOND RULE

    Una sekunde tano tu za kuanza kufanya kitu. Kitabu cha the 5 second rule kinakuonesha nguvu ya sekunde tano katika kufanya majukumu yako na kuepuka kughairisha.

    Kama umelala kitandai na alarm ya kuamka ikalia. Hesabu tano, nne, tatu, mbili, moja, kisha toka kitandani..

    Kwenye kitabu hiki Mel Robbins anaenda kukuonesha namna ambavyo utaepuka kughairisha majukumu yako ya kila siku. Ebu BONYEZA hapa chini kufuatilia uchambuzi mpaka mwisho

  • Kitu Ambacho Hakuna Mtu Yeyote Anaweza Kufanya Kwa Ajili Yako

    Pigana kwa ajili ya ndoto zako maana hakuna mtu yeyote ambaye anaweza kufanya hivyo kwa ajili yako. Hakuna mtu wa aina hiyo.

    unajua kwa nini?

    Kwa sababu hakuna mtu AMBAYE anaweza kuiona ndoto yako kwa usahihi Kama ambavyo wewe mwenyewe unaiona. Wewe ndiwe unaona ndoto yako kwa usahihi.

    Pili, kama wewe mwenyewe tu utashindwa kupambana kwa ajili ya ndoto zako, usitegemee kwamba kutakuwa na mtu mwingine ambaye anaweza kupambana kwa ajili yako.

  • KITABU CHA KISWAHILI CHA BURE

    Abraham Lincoln aliwahi kunukuliwa akisema kuwa, rafiki yangu wa kweli ni yule ambaye atanipa kitabu.

    Nadhani huu usemi una maana kubwa katika ulimwengu wa leo kuliko hata alipousema.
    Ebu fikiria katika ulimwengu wa sasa ambapo kila mtu anapenda kupewa simu mpya na ya kisasa kama zawadi.
    Ulimwegu ambapo watu wanapenda kupewa zawadi ambazo ukifungua utaonekana kwa nje kuwa wewe ni wa viwango!

    Je,  ukipewa zawadi ya kitabu si ina maana kubwa zaidi?

    Kwa kulitambua hilo,  nimeona ni vyema kabisa na wewe nikupe zawadi ya kitabu changu pendwa cha Kiswahili. Kipate hapa

  • Jinsi Ya Kupakua Vitabu Bure Mtandaoni-2

    Kama umekuwa unajiuliza unawezaje kupakua vitabu mtandaoni, leo nimekuja na maelekezo yanayojieleza moja kwa moja kuonesha namna ambavyo unaweza kupakua vitabu mtandaoni.

    Kuna video ya kwanza ambayo ilitangulia hii.
    Kwa hiyo unaweza kutumia video hii ya kwanza au ukatumia video hii ya pili.

    Ila sana sana nashauri utumie hii ambayo nimekushirikisha hapa.

    Kila la kheri.

X