-
Kiongozi ni mtu wa aina gani?
Kwa watu wengi akitajwa kiongozi au mtu yeyote yule anayeitwa kiongozi basi wanafikiria kwamba kiongozi ni mtu mwenye cheo. Kama rais, waziri, mkurugenzi au cheo chochote kikubwa.
Kama hauna cheo wewe siyo kiongozi. Ninachoweza kusema hapa ni kwamba watu wanachanganya kati ya cheo na uongozi. unaweza ukawa na cheo ila ukawa siyo kiongozi. Na unaweza ukawa usiwe na cheo ila ukawa ni kiongozi.
Kwa hiyo sasa kiongozi ni nani?
Kiufupi ni kwamba kila mtu anapaswa kuwa kiongozi. Kiongozi wa maisha yake mwenyewe. Na sifa moja kubwa ya kiongozi ni kujisimamia. Hivyo, kama wewe unaweza kujisimamia na kufanya majukumu yako bila ya kuhitaji kusimamiwa basi ujue kwamba wewe ni kiongozi.
Kama hujaweza kujisimamia kwenye baadhi ya majukumu ambayo unafanya, basi ujue kwamba unapaswa kubadilika ili uanze kujijengea sifa za kuwa kiongozi.
Kuna vitu unaweza kuanza kukjisimamia kuanzia leo hii na vikakufanya kuwa kiongozi.
Kwa mfano huhitaji kuwa kiongozi ili kuamka asubuhi na mapema.
Huhitaji kuwa kiongozi ili uweze kusema ukweli na kuwa mwaminifu.
Huhitaji kuwa kiongozi ili uweke akiba
Huhitaji kuwa kiongozi ili ufanye kazi kwa bidii
Na hizo ni baadhi ya sifa ambazo kiongozi anapaswa kuwa nazo, na wewe huhitaji kuwa hata kiongozi ili uwe na hizo sifa.
umeshapata kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO?
kama bado, basi jipatie nakala yako sasa hivi, wasiliana na 0755848391
-
Uchambuzi wa kitabu cha Think And Grow Rich (Mambo 50 Ya Kujifunza)
Kitabu: THINK AND GROW RICH
Mwandishi: Napoleon Hill
Mchambuzi: Hillary Mrosso
Kupata kitabu cha THINK AND GROW RICH BONYEZA HAPA Whatever your mind can conceive and believe it can achieve.
- Mafanikio yote yanaanzia kwenye mawazo, na ukiyaamini mawazo yako na kuyafanyia kazi utayaona mafanikio yako.
- Mafanikio mara zote yanakuja kwa wale wanaofikiria mafanikio kwenye fikra zao au mawazo yao.
- Mwandishi wa kitabu hiki ni Napoleon, ambaye inasemekana ndie mtu mwenye ushawishi zaidi kuwahi kutokea duniani, hasa kwenye masuala ya fedha, utajiri na biashara.
- Utajiri sio mara zote utapimwa kwa wingi wa fedha. Utajiri unajumuisha, afya njema, mahusiano mazuri, na mwenendo mzuri wa maisha.
- Ili kupata unachokitaka katika maisha unahitaji kuwa na matamanio dhabiti ndani yako, matamanio na tamaa kali ya kufanikiwa ndio itakusaidia kuchukua hatua.
- Unahitaji dhamira ya dhati kabisa na uvumilivu mkubwa ili kufikia na kuyaona mafanikio yako.
- Hakuna mafanikio yatakuja bila gharama za kuumia, kupoteza, kushindwa, kukataliwa au kuchukiwa.
- Unahitaji kuwa kinganganizi kweli ili kufikia malengo na mafanikio unayotaka, kifedha, kiuchumi, kifamilia nk.
- Katika safari yako ya mafanikio, unahitaji sana imani, mani itakusukuma na kukupa matumaini ya kuendelea mbele pale mambo yanapoonekana magumu.
- Imani ni muhimu sana katika safari ya mafanikio maana itakufanya uendelee kuamini ndoto zako na kuzipigania kwa uvumilivu.
- Katika kanuni na fomula za kufanikiwa kwenye maisha ya kifedha na kiuchumi ni kutokata tamaa, kamwe usikate tamaa kuufikia mafanikio yako.
- Kuwa na tamaa ya kupata mafanikio, penda kupata mafanikio unayoyataka na utayafikia licha ya changamoto zitakazojitokeza.
- Inawezakana kushindwa na kuambiwa haiwezekani mara moja au zaidi ya mara moja, kama ndani yako kuna ule moto na matamanio ya kufikia ndoto zako, endelea kuzifanyia kazi na kuzipigania.
- Kushindwa kwako jambo hakutafsiri kushindwa kwa wengine, au ndivyo itakavyokuwa kwa wengine.
- Kama umeshindwa wewe umeshindwa wewe, usitengeneze iwe sheria kuwa kwa kuwa wewe umeshindwa iwe hivyo kwa wengine kushindwa pia.
- Kumbuka siku zote wewe ndio mwamuzi wa hatima yako, maisha yako ya sasa na baadaye yanaathiriwa zaidi na wewe mwenyewe.
- Chukua hatua juu ya maisha yako, jipe jukumu la asilimia 100 la kuwajibika na maisha yako. Usimwachie mwingine maisha yako kama vile hayakuhusu.
- Tengeneza maisha bora unayoyataka na unayoyafurahia kuyaishi. Kuwa na mpango wa kila siku wa kuboresha maisha yako.
- Hakuna atakayeishi maisha yako badala yako, hakuna anayeweza kuyabadili maisha yako bila wewe mwenyewe kuamua, imiliki hatima yako.
- Amua mawazo yako yatawaliwe na hisia nzuri za mafanikio, utajiri, fedha na haki. Hayo yote yapo ndani ya uwezo wako kuyaruhusu na kuyatawala.
- Kumbuka pia unaweza kuruhusu mambo hasi na hisia za hofu, kushindwa, magonjwa na kukata tamaa vikatawala mawazo yako. Amua kwa dhati ni mambo gani unataka yatawale na yachukue sehemu kubwa ya fikra zako na mawazo yako.
- Chochote kitakachotawala mawazo, hisia na fikra zako kwa kiasi kikubwa hicho ndio kitakuwa rahisi kufanyiwa kazi na kutokea kwenye maisha yako, mfano kama ni fedha, utajiri, afya, Imani, upendo, chuki, hasira, vyote hivyo vinaweza kukaa ndani ya mawazo ya mtu na vina athiri mwenendo wake wote.
- Kama umeamua kulivalia njuga suala la mafanikio yako, basi fanya hivyo na jiweke kwenye msitari wa mbele kabisa wa mapambano ama ufanikiwe ama ukufe, kusiwe na uwezekano wowote wa kurudi nyuma au kukata tamaa. DO or DIE.
- Ukiamua kuingia kwenye njia ya mafanikio na kupata utajiri, akili, mwili, roho, nafsi na kila kitu ndani yako kinatakiwa kutambua jambo moja tu, ni kupambana hadi kufikia mafanikio hayo.
- Ondoa uwezekano wowote wa kurudi nyuma na kukata tamaa, kushindwa kunaweza kutokea lakini kukata tamaa hakutakiwi kutokea, pambana ufikie ndoto zako au ufe ukizipambania lakini sio kukata tamaa.
- Usitoe ruhusa kwa mawazo au akili yako kuleta hisia za kukata tamaa kwenye mapambano ya kufikia mafanikio yako ya kifedha, kielimu, kiuchumi au kiafya, pambana mpaka pumzi yako ya mwisho.
- Choma madaraja yote, ziba njia zote zitakazokufanya ufikirie kutoroka uwanja wa vita, salia uwanja wa vita ukipambania ndoto zako, hatima yako na uhai wako kwa nguvu zako zote.
- Weka mipango imara na madhubuti ya kufikia mafanikio yako ambayo haitajali utashindwa mara ngapi ili kufikia ndoto zako.
- Panga na weka mipango ya kuvumilia na kuendelea kung’ang’ania kubakia katika njia ya mafanikio yako.
- Kutamani tu hakutakuletea matokeo, panga, weka mikakati na fanyia kazi mipango hiyo hadi ilete matokeo uliyotamani, fanyia kazi matamanio yako.
- Matamanio yako ni vizuri yakachanganyika na imani na hisia kali za kukufanya uchukue hatua hata kama mazingira ni magumu, hata kama hakuna hamasa yoyote.
- Imani ina mchango mkubwa sana katika kutuletea utajiri, usipuuze imani katika safari yako ya mafanikio.
- Unajua hakuna ukomo kwenye fahamu zetu, isipokuwa ukomo tuliojiwekea wenyewe. Jipe ruhusa na ruhusu ufahamu wako kufikiri makubwa ili uchukue hatua kubwa zitakazo kuletea mafanikio makubwa.
- Utajiri na umasikini vyote vinaanzia au vinazalishwa na mawazo. Chagua mawazo unayotaka kazalisha katika fikra zako.
- Hakuna kinachoingia kwenye mawazo yetu bila sisi wenyewe kutoa ruhusa hiyo, toa ruhusa kwa mawazo chanya ya mafanikio kuingia katika fikra zako nafahamu zako.
- Maarifa pekee hayaleti utajiri wala fedha, kinacholeta utajiri na fedha ni matumizi ya maarifa uliyojifunza au kusikia. Fanyia kazi maarifa au elimu uliyoipata ili ilete matokeo.
- Onyesha maarifa yako kwa njia ya matendo, matendo yana nguvu na ushawishi zaidi, tekeleza unachojifunza.
- Maarifa bora hayataleta maisha bora kama huyatatekeleza. Uwe mtendaji wa neno usiwe msikiaji tu.
- Panga kabisa tena kwa kumaanisha kuwa utakachojifunza utakifanyia kazi, utaweka kwenye matendo unachojifunza, au maarifa unayopata.
- Thamani ya maarifa ipo pale unapoamua kuiweka kwenye matendo au kutekeleza. Jiahidi nafsi yako kuwa utaanza kufanyia kazi maarifa, ujuzi na elimu uliyoipata.
- Utofauti kwenye maisha unakuja pale unapoamua kufanyia kazi maarifa au elimu uliyoipata. Jitofautishe na wengine kwa kuwa mtendaji zaidi.
- Jifunze kila siku kuboresha ujuzi wako, pata maarifa ya kutosha kuhusu utalamu wako, itakufanikisha sana.
- Nidhamu ni muhimu sana katika safari ya mafanikio. Kama huna nidhamu huwezi kufika kwenye mafanikio yako.
- Nidhamu binafsi ndio kazi kubwa ambayo itakugharimu sana kuifanya.
- Tunahitaji nidhamu kwenye kila eneo la maisha yetu, nidhamu ya fedha, nidhamu ya muda, nidhamu ya kuendelea kufanyia kazi malengo yetu.
- Moja ya kazi kubwa unatakiwa kuifanya kwenye maisha yako ni kujizuia, kujidhibiti, kujitawala na kujiweza. Kama utafanikiwa kujitawala na kujiweza, basi umefanikiwa.
- Sio vizuri kuwapa wengine jukumu la kukusimamia, kukudhibiti ili uwe na nidhamu, jipe wewe mwenyewe hili jukumu liwe ndio jukumu la maisha yako yote.
- Kabla hujaanza kusimamia na kuwaongoza watu wengine, jisimamie, jimiliki, na jiongoze wewe mwenyewe kwa mafanikio kwanza.
- Uhuru wa kweli upo pale unapoweza kujidhibiti, kujizuia na kujitawala. Utumwa ni pale unapokosa utawala na udhibiti kwenye maisha yako binafsi.
- Dhibiti na tawala kila eneo la maisha yako, kifedha, afya, hisia, mapenzi, kazi, chakula, nk. Ukiweza kudhibiti mambo hayo utakuwa na maisha huru yenye afya na furaha.
SOMA ZAIDI: Uchambuzi wa Kitabu: The Psychology of Money: Mambo 94 niliyojifunza katika kitabu hiki.
Kitabu hiki kina mambo mengi sana ya msingi kwa ajili ya kuboroesha maisha yetu, hakifai hata kuchambua maana kila kilichoandikwa ni mafunzo muhimu sana. Nashauri kila mtu akisome kitabu hiki ili aboreshe maisha yake na ya watu wengine. .
-
Jinsi Ya Kufanikisha Ndoto Zinazohitaji Fedha Nyingi

Kwenye video ya leo kupitia channel yetu ya YouTube nimeeleza kwa kina ni namna gani unaweza unaweza kupata na kutunza fedha ya kukusaidia Kufanikisha ndoto yako kubwa. Je, upo tayari kwa ajili ya hiki? Ebu tazama video yenyewe hapa
Hakikisha umejiunga na mfumo wetu wa kupokea makala maalumu kikashani mwako kwa kujaza taarifa zako hapa chini.
usisite kuagiza nakala ya kitabu chako cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO ili uweze kutumiwa popote pale ulipo. Kupata nakala ya kitabu hiki, wasiliana nami kwa 0755848391
For bookings: songambele.smb@gmail.com
-
Huu ndio utaratibu mzuri ambao unapaswa kuujenga kuanzia mwezi huu
Moja ya sifa ya watu wanaofanya makubwa kwenye hii dunia ni tabia ya kujifunza. Hii ni tabia moja muhimu ambayo inaweza kukusaidia wewe kufanikisha mambo makubwa kwenye hii dunia. Kama bado unajiuliza ni kwa jinsi gani kusoma kunaweza kukusaidia wewe, chukua hatua. Utoe mwaka mmoja ambapo utajifunza kila siku. Kisha linganisha huo mwaka na miaka mingine ya nyuma ili uweze kuona utofauti.
Baada ya mwaka mmoja, linganisha mwaka wako huo mmoja ambao ulikuwa unasoma vitabu na ile miaka ambayo ulikuwa husomi. Kusoma ni jambo la muhimu sana kwenye maisha yako ya kila siku, kama kula kulivyo muhimu kwenye maisha yako ya kila siku.
Kwa hiyo, anza kujijengea utaratibu wa kusoma vitabu kuanzia leo hii. Lakini, haupaswi kuishia hapo tu. Badala yake unapaswa pia, kujenga utaratibu mzuri wa kununua walau kitabu kimoja kila mwezi. Kila unapopokea mshahara, hakikisha kwamba, unatoa kiasi fulani kwa ajili ya tu ya kununua vitabu au kitabu. Hiki kitu kidogo tu, kinaweza kukusukuma na kukufikisha mbali.
Fedha yako ya kununua kitabu, inaweza kuwa ni fedha hiyohiyo ambayo wewe unatumia kufanya mambo ambayo si ya muhimu kwa sasa.Ila sasa kwa kuwa umejijengea utaratibu huu wa kusoma vitabu. Unaamua kuanza kuiwekeza hii fedha kwa ajli ya baadaye yako.
Rafiki yangu, anzisha huu utaratibu. Nina hakika mwaka mmoja baadaye utanishukuru kwa ajili ya huu utaratibu wa kipekee ambao utakuwa umeuanzisha. Je, upo tayari kwa ajili ya hiki kitu.
Kama upo tayari, anza kuwa kuchukua kitabu cha JINSI YA KUFIKI ANDOTO ZAKO Toleo la 2.
Kwenye hiki kitabu unaenda kujifunza namna ambavyo utaweza kufanikisha ndoto zako kubwa za kimaisha. Je, upo tayari?
-
Sababu Moja Kwa Nini unapaswa kuandika kitabu chako Leo
Rafiki yangu wa ukweli Karibu kwenye makala ya jumapili ya leo. Leo ninataka nikwambie kwa nini unapaswa kuandika kitabu chako kuanzia leo hii.
Naikumbuka siku za nyuma niliwahi kuandika (SABABU 18 Kwa Nini Tunaandika Vitabu na Tutaendelea Kuandika Vitabu, Na Kwa Nini Wewe Unapaswa Kuandika Cha Kwako)
Ninachofanya leo ni kukuongezea nyama kwenye kile ambacho nimewahi kuandika.
Na hapa ninasema kwamba, unapaswa kuandika kitabu chako kwa sababu kesho na kesho kutwa unaweza usiwe hapa duniani. Sasa kuandika kitabu kutakufanya uache ujumbe kwa watu wa Karibu yako ili wajue fikra zako, kile ulichokuwa unasimamia kwenye maisha, ulipotoka mpaka kufika ulipofika. Kwa hiyo, kwamwe usisite kuandika kitabu chako. Anza leo hii kuandika kitabu chako.
Nina hakika wewe babu yako angekuwa ameandika kitabu, leo hii ungekuwa unaenda kukitafuta kukisoma. Kwa hiyo, kama ambavyo wewe unatamani kujua kitu kuhusu historia ya wazazi wako, hivyohivyo, andika kitu uwaachie wanao na wajukuu wako.
Upo tayari kuandika kitabu chako? Karibu upate kitabu cha NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA. Kitakusaidia sana wewe kuanza kuandika kidogokidogo mpaka kukikamilisha hatuahatua. Kwa mfano kwenye kitabu nimeeleza kuwa unaweza kuandika kitabu chako Kama unavyoandika SMS.
Ebu fikiria kwa siku unaandika na kujibu SMS ngapi? Kwa mwaka hizi SMS zikiuunganishwa ni sawa na kitabu chenye ukubwa kiasi gani?
Ukiangalia hili, utagundua kuwa kitabu chako kinaweza kuwa kikubwa kama utatumia mbinu hii tu.
Kitabu kimeeleza vitu vingine VIDOGO unavyoweza kutumia kwenye kuandika kitabu chako na kukiuza kwa mafanikio.
Karibu upate nakala yako. Gharama yake ni 20,000/- na unatumiwa popote ulipo.
Lakini pia nina kitabu cha JINSI YA KUWA MWANDISHI MBOBEVU NDANI YA SIKU 30. Hiki nacho kinakuhusu pia. Kwa Sasa hiki kitabu kinapatikana kwa 5,000/- tu kwa mfumo wa softcopy. Karibu sana tuko pamoja.
Kupata vitabu hivi wasiliana na 0755848391.
Kila la kheri.
kwa maoni, Ushauri na maswali: godiusrweyongeza1@gmail.com
for booking: songambele.smb@gmail.com
-
Baadaye siku ya leo, nitakuwa CLOUDS FM nikiongelea Gharama za Kulipa ili kufikia ndoto zako

Helo upande wa huko. Godius Rweyongeza hapa na leo nina taarifa fupi tu kwako.
Taarifa hii ni kwamba baadaye siku ya leo nitakuwa CLOUDS FM, Kwenye kipindi Cha TEMINO.
Mada nitakayozungumzia Ni GHARAMA ZA KULIPA ILI KUFIKIA NDOTO ZAKOKipindi hiki kinaendeshwa na Harris KAPIGA pamoja na adv. Henry Mwinuka.
Muda wa kipindi ni saa 9 mchana hadi saa 11 jioni.
Hakikisha unafuatilia hiki kipindi. Kuna mengi ya kujifunza siku ya leo.
Moja ya kitu ambacho nimejitoa kuhakikisha nakifanya kwa weredi ni kuambatana na watu wenye ndoto kubwa. Sipendi kabisa watu wenye ndoto ndogo. Na ndio maana nimeandika kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO kwa ajili watu wenye ndoto kubwa tu. Upo tayari kuzifikia ndoto zako kubwa kwa viwango vikubwa? Basi hakikisha unapata nakala ya kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO.
Gharama ya nakala moja Ni 20,000/-. Tuwasiliane sasa kwa 0755848391 ili uweze kupata nakala yako leo.

-
Hii Ndio Aina Bora Uwekezaji Unayoweza Kufanya. Hakuna Uwekezaji Wenye Manufaa Kama Huu
Moja ya kitu ambacho watu wanatafuta na wangependa kupata maishani mwao ni uwekezaji mzuri. Najua na wewe unasoma hapa kwa sababu unataka uwekeze fedha zako sehemu ambayo itakupa faida kubwa. Sasa siku ya leo nataka nikwambie eneo zuri ambalo wewe mwenyewe unaweza kuwekeza na kupata faida.
Kwa siku sasa nimekuwa nikikwambia maeneo ya kuwekeza na hasa kwenye hisa, hatifungani na VIPANDE.
Huu Ni uwekezaji mzuri ambao hado nashauri uufanye, Tena kwa nguvu zako zote.
Ikiwezekana tumia nguvu ya vitu vidogo kufanya uwekezaji huu. Yaani, anza kuwekeza kidogo kidogo, Kisha endelea kuwekeza kidogo kidogo bila kuacha kwa muda mrefu. Hiki kitu kidogo unachowekeza baada ya muda mrefu kitageuka kuwa kikubwa kwa kutumia kanuni ya riba mkusanyiko.
Ila ukiachana na huu uwekezaji wa Hisa, hatifungani na vipande kuna uwekezaji mwingine mzuri ambao unaweza kuufanya na ukakupa faida kubwa pia. Na uwekezaji huu ni Kuwekeza kwenye matangazo ya BIASHARA yako.
Huu ni uwekezaji mwingine ambao unaweza kuufanya, ukakupa faida na matokeo kwa muda mrefu ujao.
Matangazo mara zote yanalenga kuleta wateja watakaonunua bidhaa fulani kwenye BIASHARA yako. Sasa matangazo yako yakifanyika vizuri, yana uwezo wa kuleta matokeo makubwa kuliko uwekezaji mwingine ambao tayari nimekwambia hapo mwanzoni.
Kwa Nini?
Kwa sababu, takwimu zinaoneshwa kuwa WAWEKEZAJI wakubwa kwenye soko la hisa, hatifungani, vipande na hata WAWEKEZAJI wa fedha za kigeni huwa wanapata faida yenye ukomo.
Mwekezaji Warren Buffet ndiye mwekezaji mwenye mafanikio ambaye huongelewa sana linapokuja suala zima la uwekezaji. Ila takwimu zinaoneshwa kuwa huwa anapata faida ya asilimia 20% ukuaji wa mwaka.Siyo Warren Buffet peke yake tu, hata WAWEKEZAJI wengine kama
Carl Icahn anapata 31% ya ukuaji kwa mwaka.
George Soros anapata 20% ukuaji wa mwaka.
Peter Lynch anapata 29% ya ukuaji wa mwaka.Kwa hiyo nataka kusema tusiwekeze?
Hapana. Ninapenda uwekezaji na Mara zote nimekuwa nikishauri uwekeze kwenye HISA, hatifungani na vipande. Kama Bado hujafungua akaunti yako ya uwekezaji, ujue wazo kuwa unajinyima fursa nzuri ya kupata faida kwa muda mrefu. Kafungue akaunti Leo hii na uanze kuweka fedha kidogo kidogo kama uwekezaji. Nimeandika mpaka kitabu cha uwekezaji kwenye hisa. Kinaitwa MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE.Ila sasa kikubwa ninachotaka ufanye pia ni Kuwekeza kwenye matangazo ya BIASHARA yako . Itangaze BIASHARA yako Mara kwa Mara na kila sehemu ambayo unajua inaweza kukuletea wateja. Huu ni uwekezaji ambao una faida kubwa sana.
Ukifanya tangazo lako vizuri, utakuta kuwa tangazo Hilo linakuletea faida kubwa hata Mara 10 ya ule uwekezaji uliofanya mwanzoni.
Unaweza kuwekeza laki moja ukapata mpaka faida ya milioni. Yaani, unatangaza kwa laki moja, unapata faida ya milioni moja. Faida ambayo ni ngumu kuipata kwenye uwekezaji wa kawaida wa hisa, hatifungani na vipande.
Hivyo kumbe, BIASHARA yako inapaswa kuwa sehemu ya kwanza kabisa ambapo utafanya uwekezaji. Kisha baada ya hapo wekeza maeneo mengine.

Je, upo tayari kuwekeza kwenye BIASHARA yako na kuikuza kwa viwango vikubwa? Upo tayari?
Kama upo tayari kuikuza BIASHARA yako kwa viwango vikubwa, nashauri usome kitabu changu cha NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA.Ili uone hii nguvu inavyoweza kufanya kazi kwa ajili yako pia.
Kila la kheri
Umekuwa nami rafiki yako wa ukweli
Godius Rweyongeza
0755848391
Dar-Tz
Kwa maoni, Ushauri na maswali: godiusrweyongeza1@gmail.comFor booking: songanbele.smb@gmail.com
-
Usifurahie kitu hiki kwenye maisha yako
usifurahie kuitwa mnyonge. Hivi umewahi kujiuliza unyonge wako uko wapi? Sasa kwa nini watu wanakuita mnyonge na muda mwingine wanasema kwamba, wanakutetea wewe. Sikiliza, pambana kwa hali yoyote ile kuhakikisha kwamba wewe hauwi mnyonge. Kwa asili ni kwamba vitu vinyonge huwa havidumu. Sisi wenyewe hatupendi tukae na vitu vinyonge. Mfugaji wa ng’ombe hawezi kukaa na ng’ombe mnyonge mwaka mzima anamlisha tu. lazima atamuuza au atamchinja.
Na kadiri ya sheria ya Darwin vitu vinyonge, havidumu. Huwa vinatoweka na kuisha kabisa, huku vitu ambavyo ni imara, vikizidi kudunda tu. sasa kazi ni kwako, kuhakikisha kwamba hauwi mnyonge kwenye kile unachofanya, badala yake unaamua kuwa ngangali.
Kama ni fedha,pambana kuhakikisha kwamba unakuwa nayo. Kama ni kazi pambana kuhakikisha
Rafiki yangu usikubali kuwa mnyonge.
Umekuwa nami,
Godius Rweyongeza
0755848391
Morogoro-Tz
Kwa maswali, maoni au ushauri: godiusrweyongeza1@gmail.com
For bookings: songambele.smb@gmail.com
-
Leo ndiyo siku ya mwisho ya kupata kitabu cha jinsi ya kufikia ndoto zako kwa bei ya ODA

Habari ya upande wa huko rafiki yangu. bila shaka unaendelea vyema kabisa. Nimekuwa nikikutaarifu kuwa leo ni siku ya uzinduzi wa kitabu cha jinsi ya kufikia ndoto zako. kitabu hiki cha kipekee kimeeleza kwa kina, jinsi gani unaweza kugundua ndoto zako na kuzifanyia kazi mpaka zikatimia.
Hivi umeshajiuliza swali ee! Kwa nini natumia neno ndoto zako? Ukweli ni kwamba hauwezi kuwa na ndoto moja tu. ni lazima utakuwa nazo nyingi, kwenye kitabu nimeeleza kwamba ni haki yako kuwa na ndoto nyingi, lakini sasa linapokuja suala zima la kuzifanyia kazi ndio unapaswa kuzifanyia kazi moja baada ya nyingine.
Kitabu hiki cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO, kinazinduliwa rasmi leo kwenye kundi maalumu la kuweka oda. Kama wewe hauko kwenye hili kundi unapaswa kufanya hivi. Weka oda yako hapa. Baada ya kuweka oda utatumiwa kiunzi maalumu cha kuingia kwenye kundi la kuweka oda.
Gharama ya kitabu hiki ni 20,000/- ila ukilipia leo nakala yako utaipata kwa 15,000’- tu. leo ni siku ya mwisho ya kupata nakalayako kwa bei ya oda.
Rafiki yangu kiukweli nisingependa wewe ukose nakala hii ya kipekee kwenye maktaba yako. Kitu kikubwa cha kufanya sasa hivi. ni kuweka oda yako kupitia kiunzi hiki hapa. Baada ya hapo utapewa utaratibu wakulipia na nakala yako, itatumwa bila kuchelewa.
Rafiki yangu karibu sana uweze kujipatia nakala ya kitabu hiki cha kipekee sana.
Umekuwa nami,
Godius Rweyongeza
0755848391
Morogoro-Tz
-
KUHUSU KITABU: NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA

Hivi umewahi kujiuliza kuwa vitu vidogo vinaweza kukusaidia kitu gani maishani mwako?
Mara nyingi sana watu huwa wana ndoto kubwa na malengo makubwa ya kufikia kifedha, kimahusiano, kibiashara au kikazi. Lakini cha kushangaza ni kwamba huwa hawafanyii kazi hizo ndoto kubwa walizonazo bali huwa wanasubiri itokee siku moja ya muujiza ambapo ndoto yao itatimia kwa asilimia zote.
Kwenye kitabu hiki unaenda kujifunza nguvu ya vitu vidogo na namna ambavyo unaweza kutumia nguvu hii kwenye maisha yako ya kila siku, kufanya makubwa.
Kupata kitabu hiki, wasiliana na 0755848391. Nakala unatumia popote ulipo. Gharama ya kitabu hiki ni 20,000/-
Umekuwa nami,
Godius Rweyongeza
0755848391
kwa maoni, ushauri au maswali: godiusrweyongeza1@gmail.com
For bookings: songambele.smb@gmail.com