Home


  • Namba Zetu Za Malipo

    Namba za malipo ya vitabu:

    Namba za lipa

    TIGO PESA: 19016638 Jina ni SONGAMBELE CONSULTANTS

    M-PESA: 5564517 jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

    Namba za kawaida

    AIRTEL MONEY: 0684408755
    TIGO PESA: 0655 848 392
    M-PESA: 0745 848 395

    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    NB: Kama namba ya malipo anatumiwa mtu ambaye yuko nje ya nchi. Iandikwe Kwa kuanza na +255

    Kwa hiyo namba zinazotumwa nje ya nchi zitakuwa
    Airtel money: +255 684 408 755
    TIGO PESA: +255 655 848 392
    M-PESA: +255 745 848 395

    KOTE Jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Kama malipo yatakuwa yanafanyika kupitia benki.

    Yafanyie kupitia

    1. CRDB BANK: 0150770710200
    2. NMB BANK: 22110047274

    Kote jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

  • Wasiliana na Godius Rweyongeza Sasa

    Habari yafuatayo ni mawasiliano Unayoweza kutumia kumpata GODIUS RWEYONGEZA

    Simu: +255 (0) 684408755

    Whatsap: +255 (0) 755848391

    Email: songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu vyake wasiliana Moja kwa Moja na +255 (0) 684408755 (more…)

  • Hiki Kitu Tu,Kitakufanya Uwe Na Maisha Ya Kawaida

    Imewahi kukutokea ukaangalia labda igizo au ukasoma kitabu na kuona ni cha kawaida sana na wewe ungeweza kabisa kuigiza hilo igizo au ungeweza pia kuandika kitabu husika?

    Unajua kitu gani kinakutofautisha wewe na huyo aliyeigiza hilo igizo au aliyeandika kitabu husika?

    Kinachokutofautisha ni kuchukua hatua. Mwenzako anachukua hatua na kuigiza igizo alilo nalo ndani yake, wewe unaogopa na kusubiri kila kitu kikae sawa kwa upande wako, unasubiri mpaka ubobee kwenye kuigiza ili uanze kuigiza. Kitu Kikubwa ni kwamba huwezi kubobea bila ya wewe kuchukua hatua ya kwanza na kukamilisha kazi yako ya kwanza, hata Kama ni kidogo.

    Kazi ya kufanya leo: fikiria kitu ambacho umekuwa unafikiria kufanya kwa siku nyingi, kisha anza kukifanya mara moja. Kuanza kufanya kitu ndiyo kutakupelekea kwenye kubobea ba hatimaye kuwa bingwa.

    Umekuwa nami,

    GODIUS RWEYONGEZA

    Hakikisha Umesubscribe kwenye Channel yangu ya youtube kwa KUBONYEZA HAPA

    Jiunge na mfumo wa kupokea makala maalumu kwa njia ya barua pepe kwa KUBONYEZA HAPA

    Jipatie nakala za vitabu vyangu vya kiswahili kwa KUBONYEZA HAPA

    Kama ungependa kujifunza kuhusu uandishi kutoka kwangu wasiliana nami kwa 0755848391

    kila la kheri

  • Kwa Nini watu wengi husahau malengo ya mwaka mpya Mapema Sana

     

    Juzi tarehe 19 ilikuwa ni siku rasmi ambapo watu wengi huwa wanaacha kufanyia kazi malengo yao na kuanza kuishi maisha ya kawaida. Hii siyo siku ambayo nimeibuni bali ni kutokana na tafiti kuntu zilizofanywa na watafiti wanaoaminika duniani. Na siyo kwamba zimefanywa kwa watu kumi au ishirini, bali zimefanyika kwa watu zaidi ya milioni 800. Ndio milioni mia nane!

    Katika kuwafuatilia watu hawa, iligundukilika kuwa WATU HAWA WANAKUWA NA MOTISHA KUBWA sana wanapoanza mwaka mpya, ila motisha hiyo inapungua zaidi na kwa wengi siku ya 19 ndipo wanaagana kabisa na malengo yao.

    Sasa kwa nini watu huwa wanaachana na malengo yao mapema? Hiki ndicho naenda kueleza kwenye makala ya leo.

    Kwanza ni kuwa na matamanio makubwa huku wakipenda kupata matokeo ya haraka. Mtu anaanza mwaka mpya akiwa na unene wa kupitiliza, anapoanza mwaka anaweka malengo ya kuagana na unene wake huku akiwa anataka kuagana na unene huo ndani ya siku chache tu. Baada ya hapo anaanza mazoezi, ila ndani ya siku 14 za kwanza kunakuwa hakuna mabadiliko yotote ya maana anayoyaona, anaanza kuvunjika moyo. Mpaka siku ya 18 bado pia kunakuwa hakuna kitu kikubwa akbacho kimeonekana. Mtu anaamua kuagana na malengo yake na hiyo inakuwa imeishia hapo.

    Ambacho huyu mtu anasahau ni kwamba kufanyia kazi na kufikia malengo kunahitaji mchakato. Mwanzoni kabisa unaweza usione matokeo yotote, Ni mpaka pale utakapong’ang’ania tena na tena, ndipo matokeo yataanza kujitokeza.

    Siku 18 za kwanza zinakuwa bado sana kwa wewe kuachana na malengo yako.

    Pili, ni msukumo wa vyombo vya habari.
    Mwishoni mwa mwaka vyombo vya habari vinasisitiza sana kuhusu malengo na neno MWAKA MPYA linaibwa sana. Watu mpaka wanafundishwa namna ya kuweka malengo, ila sasa ule mchakato wa kufanyia kazi malengo huwa unasahaulika.  Na vyombo vyenyewe huwa haviendelei kuweka msisitizo  baada ya mwaka mpya kufika. Na hicho ndicho huwa kinawafanya watu kuachana na malengo yao mapema.

    Ninachotaka ufahamu ni kuwa malengo unayoweka yanapaswa kutoka ndani yako, wala kusiwepo na msukumo wa nje au mtu mwingine. Ukiwa na msukumo kutoka nje utaishia njiani mapema sana.

    Hivyo ni vitu viwili ambavyo huwafanya watu washindwe kufanyia kazi malengo yao na kuachana nayo mapema. Viepuke ili uweze kufanyia kazi malengo yako mwaka huu na kuyakamilisha kwa kishindo.

    SOMA ZAIDI: KONA YAA SONGA MBELE; IKO WAPI MOTISHA YA JANUARI MOSI?.🤷🏽‍♂🤷🏽‍♂

    Lengo Lako Kuu La Mwaka 2022 Ni Lipi? Au Ndio Unamwachia Mungu🤔?

    Umekuwa nami,

    GODIUS RWEYONGEZA

    Hakikisha Umesubscribe kwenye Channel yangu ya youtube kwa KUBONYEZA HAPA

    Jiunge na mfumo wa kupokea makala maalumu kwa njia ya barua pepe kwa KUBONYEZA HAPA

    Jipatie nakala za vitabu vyangu vya kiswahili kwa KUBONYEZA HAPA

    Kama ungependa kujifunza kuhusu uandishi kutoka kwangu wasiliana nami kwa 0755848391

    kila la kheri

  • Usidharau vitu vidogo vina uwezo wa kukufikisha mbali Sana

    Mwaka 1969 binadamu kwa mara ya kwanza aliingia mwezini. Unaambiwa kompyuta iliyotumika kipindi hicho kumwingiza mtu mwezini ilikuwa na uwezo mdogo sana, uwezo wake ulikuwa mdogo mno kiasi cha kuzidiwa na simu janja tunazotumia sasa.

    Ila iliweza kutumika kutufikisha mwezini. Ndiyo maana nimekuwa nakushauri kuwa makini na vitu vidogo, kutokana na madhara au matokeo yatokanayo na vitu hivyo.

    Mbu ni wadogo, ila madhara yake kwa watu ni makubwa. Wana uwezo wa kusababisha malaria ambayo najua unajua madhara yake.

    Wewe pia usidharau hatua ndogo ndogo. Akiba kidogo kidogo unayoweka kila siku, ina uwezo wa kukufikisha mbali. Usidharau.

    Maneno 500 ya kitabu chako unayoandika kila siku, Kuna siku yatakufanya wewe utambulike Kama mwandishi MBOBEVU.

    Mazoezi hayo unayofanya kila siku, yanazidi kuimarisha mwili wako zaidi.

    Ni kitu gani kidogo unekuwa unafikiria kufanya kwa siku nyingi, ila hujakifanya. Ebu nenda kakifanye leo.

    Soma zaidi: NGUVU YA RIBA MKUSANYIKO

    Umekuwa nami,

    GODIUS RWEYONGEZA

    Hakikisha Umesubscribe kwenye Channel yangu ya youtube kwa KUBONYEZA HAPA

    Jiunge na mfumo wa kupokea makala maalumu kwa njia ya barua pepe kwa KUBONYEZA HAPA

    Jipatie nakala za vitabu vyangu vya kiswahili kwa KUBONYEZA HAPA

    Kama ungependa kujifunza kuhusu uandishi kutoka kwangu wasiliana nami kwa 0755848391

    kila la kheri

  • Leo ndiyo Siku Ambayo Watu Wengi Husahau Malengo Yao Ya Mwaka Na Kuanza Kuishi Kwa Mazoea

     

    Leo ni tarehe 19 jnuari 2022.  Ukiangalia tangu tuuanze mwaka huu, hata hatuna siku nyingi. Ila cha kushangaza ni kwamba kuna watu ambao tayari wameshasau malengo yao.

    Zimefanyika tafiti na imethibitishwa  kuwa tarehe 19 ya kila mwaka mpya, ni tarehe ambayo watu wengi huwa wanasahau malengo yao na hivyo kuendelea kuishi kimazoea.

    Swali langu la kwanza kwako leo bado unayakumbuka malengo yako uliyoweka mwanzoni mwa mwaka huu? Kama huyakumbuki, basi jua wazi kuwa Kuna sehemu kuna tatizo na hizi hapa ni mbinu za kukusaidia siyo tu kuyambuka malengo yako bali kuyafikia.

    SOMA ZAIDI: Lengo Lako Kuu La Mwaka 2022 Ni Lipi? Au Ndio Unamwachia Mungu🤔?

    Moja, jikumbushe malengo yako kila siku. Tena ujikumbushe kwa kuyaandika chini. Fanya hivyo, asubuhi na jioni kila siku kwa siku zilizobaki mpaka ufikie lengo lako. Haufanyi hivyo tu ilimradi umefanya, badala yake unafanya hivyo kwa sababu unaukumbusha ubongo na akili yako kwamba inapaswa kuwekeza nguvu kwenye kutimiza malengo na siyo kingine.

    Pili, kila siku andika chini mbinu au njia za kukusaidia wewe kufikia lengo lako. Jiulize kila siku, Ni kitu gani kimoja ambacho naweza kufanya Leo kikanisaidia kufikia lengo langu. Ukikipata, kifanyie kazi.

    Tatu, ungana na timu ya watu sahihi ambayo inaweza kukusaidia wewe kufikia lengo lako.

    Nne, usikimbizane na malengo mengi kwa wakati mmoja. Fanyia kazi lengo moja kwa wakati

    Tano, ipangilie kila siku inayokuja kwako na itumie vizuri kuhakikisha umefikia lengo lako.

    Sita, kila siku, fanya kitu kuelekea malengo yako.

    Kwa leo ni hayo tu. Nakutakia kila la kheri.

  • Hakuna shida katika kupenda fedha…

    Mara nyingi sana huwa nasikia watu wananiambia kuwa unaipenda sana fedha wewe? Au wengine huwa wanasema “unaijua hela”! Na Mimi huwa nawajibu kuwa “ ndiyo naipenda fedha ndiyo maana na yenyewe inanipenda”. Au huwa nawaambia nilizaliwa nayo.

    Ninachotaka ufahamu ni kwamba kitu ambacho hukipendi hakiwezi kukupenda wewe. Kama huipendi fedha, ndiyo maana wewe ni masikini kwa sababu fedha nayo inawapenda watu wanaoioenda.

    Kuanzia leo, Anza kuipenda fedha.

    Soma zaidi: Ijue maana nzuri ya MASIKINI

    Umekuwa nami rafiki yako wa ukweli Godius Rweyongeza

    Hakikisha Umesuscribe kwenye Channel yangu ya youtube kwa KUBONYEZA HAPA

    Jiunge na mfumo wa kupokea makala maalumu kwa njia ya barua pepe kwa KUBONYEZA HAPA

    Jipatie nakala za vitabu vyangu vya kiswahili kwa KUBONYEZA HAPA

    Kama ungependa kujifunza kuhusu uandishi kutoka kwangu wasiliana nami kwa 0755848391

    kila la kheri

  • Kutana na Mwajiriwa Ambaye Haitaji Mshahara Ila Anafanya Kazi Kwa Bidii. Nakushauri Baada Ya Kusoma Makala Hii Umwajiri Huyu Jamaa

    Leo napenda kumtambulisha kwako mwajiriwa mtiifu kuliko wote duniani,  anafanya kazi kwa saa 24 siku saba za wiki. Hadai mshahara wala marupurupu yoyote. Yeye anachojua ni kufanya kazi kwa bidii kila wakati na kutoa matokeo kadiri unavyomwelekeza. Nimekuwa namtumia mwajiriwa huyu kwa siku nyingi sasa na hizi ndizo sifa nilizobaini kwake.

    Anaweza kusalimia wateja,
    Anaweza kueleza jinsi bidhaa zangu zinavyofanya kazi
    Anajibu maswali yanayoulizwa mara kwa mara.
    Anatoa mawasiliano yangu ya wateja wanaohitaji kufahamu zaidi kuhusu huduma zangu.
    Anatoa shuhuda za watu walionufaika na kazi zangu.
    Anatoa maelekezo ya jinsi ya kulipia huduma zangu au vitabu vyangu.

    Kama kuna kitu kingine cha ziada, bado anaweza kukifanya. Mwajiriwa huyu siyo mwingine bali ni tovuti na blogu.
    Kimojawapo kati ya hivi kinaweza kukupa matokeo ila kwa upande wangu natumia blogu.

    Soma zaidi tofauti Kati ya tovuti na blogu.

    Nikiandika kitu kwenye blogu yangu leo hii, hakibadiliki wala kutoweka labda pale nitakapoamua kufanya hivyo. Kama ni ujumbe wa kuelimisha kama huu utaendelea kuwa hewani. Utasomwa leo hii na utasomwa miaka mitano ijayo bila kubadilika.

    Hii ndio maana na wewe unahitaji kuwa blogu. Ebu kwa mfano jiulize status yako ya whatsap uliyoandika januari mosi, 2022 iko wapi? Kwa mfano kama kuna mtu aliisoma na akaipenda na leo hii angependa kurejea tena kuiona atafanyaje kuiona? Kiufupi, jibu ni haiwezekani.

    Sasa mambo ni tofauti kwa blogu. Yenyewe ukiweka kitu hakitoweki baada ya saa 24 au baada ya muda fulani. Kinaendelea kuwepo. Kama mtu atakisoma au kukisikiliza leo, anaweza pia kurejea kwake miaka kadhaa mbeleni na kusoma tena.

    Blogu inafanya kazi saa 24 kwa siku Saba 7 za wiki.

    Mtu akiingia mtandaoni usiku na kufungua blogu yako, atanufaika sawasawa na yule atayeingia wakati wa jua kali saa saba mchana.

    Blogu yenyewe inafanya kazi bila kujali kuna baridi au mvua.

    Kwenye blogu unaweza kuweka makala au mafunzo kuhusu bidhaa au huduma zako.
    Unaweza kuwapa watu maelekezo ya namna ya kununua bidhaa yako yoyote.
    Unaweza kuwaelekeza watu jinsi ya kuwasiliana na wewe au watu wengine.
    Unaweza kujibu maswali yanayoulizwa mara kwa mara n.k.

    Kwa hakika blogu ni mwajiriwa mzuri ambaye unaweza kumtumia kwenye biashara yako na akafanya kazi bila kuchoka.
    Je, wewe upo tayari kumtumia mwajiriwa huyu?

    Karibu nikutengenezee blogu yako leo hii. Tuwasiliane kwa 0755848391 

    Umekuwa nami rafiki yako wa ukweli Godius Rweyongeza

    Hakikisha Umesuscribe kwenye Channel yangu ya youtube kwa KUBONYEZA HAPA

    Jiunge na mfumo wa kupokea makala maalumu kwa njia ya barua pepe kwa KUBONYEZA HAPA

    Jipatie nakala za vitabu vyangu vya kiswahili kwa KUBONYEZA HAPA

    Kama ungependa kujifunza kuhusu uandishi kutoka kwangu wasiliana nami kwa 0755848391

    kila la kheri

  • Kitu Kimoja Ambacho Hujawahi Kuambiwa kuhusu Kufanya Makubwa

     

    Kama unataka kufanya makubwa, unapaswa kuwa tayari kuishinda hofu na uoga unaokukabili unapoanza kufanya kitu hicho mwanzoni.

    Nakumbuka Kuna wakati nilikuwa naogopa na  kujiuliza kwamba nitaongea nini nikukutana na mtu fulani. Ila cha kushangaza muda kidogo baada ya kukutana na mtu huyo mazungumzo yalikuwa yanajiendesha yenyewe kiasi kwamba nilikuwa sijiulizi nitaongea nini.

    Hapo ndipo nilipogundua kuwa mazungumzo yanakuwa rahisi unapoanza kuzungumza.

    Wakati mwingine nilikuwa najiuliza hivi nitaanzaje kuandika? Ila nilipokuwa naanza, ndipo mambo yalikuwa yanakuwa rahisi. Kumbe, kuandika ni rahisi unapoanza kuandika.

    Nilikuwa rafiki yangu aliyekuwa anapenda kufanya mazoezi. Kila nilipokuwa nikijipanga kuanza, nilikuwa najihoji, hivi itakuwaje. Mbona Kama mwili hautaki kufanya mazoezi? Baadaye nilikuja kugundua kuwa mwili wenyewe unapenda kufanya mazoezi pale unapoanza kufanya mazoezi.

    Kitu hiki kinafanya kazi hata kwa vitu vingine kwenye maisha. Urahisi wa jambo haupatikani pale unapoanza bali kadiri unavyoendelea kukifanya hicho kitu. Kuna vitu ni vigumu mwanzoni, vigumu zaidi katikati ila rahisi mwishoni.

    SOMA ZAIDI: KONA YA SONGA MBELE; IKO WAPI MOTISHA YA JANUARI MOSI?.🤷🏽‍♂🤷🏽‍♂

    Zijue Aina Mbili Za Mbadiliko

    Umekuwa nami rafiki yako wa ukweli Godius Rweyongeza

    Hakikisha Umesuscribe kwenye Channel yangu ya youtube kwa KUBONYEZA HAPA

    Jiunge na mfumo wa kupokea makala maalumu kwa njia ya barua pepe kwa KUBONYEZA HAPA

    Jipatie nakala za vitabu vyangu vya kiswahili kwa KUBONYEZA HAPA

    Kama ungependa kujifunza kuhusu uandishi kutoka kwangu wasiliana nami kwa 0755848391

    kila la kheri

  • USHAURI MUHIMU: Kama una ndoto ya kuwa mwandishi na unawaza nani ATAHARIRI, ATACHAPA na jinsi utakavyouza kazi zako Basi Soma hapa.

    Siku ya leo najibu swali nililoulizwa na mmoja wa wasomaji wangu. Anasema;

    Hi Godius.
    Naitwa Juma Mazengo Malale, kwa sasa nipo Shinyanga, ndoto yangu nikuwa mwandishi wa vitabu. Mpaka sasa nipo kwenye mchakato, changamoto ipo kwenye mambo kama haya.
    1. Nani atahariri kazi yangu.
    2. Nani atachapa.
    3. Wapi nitauza.
    4. Nitamudu gharama
    5. Kitabu kibebe page ngapi?

     

    Habari yangu ni njema ndugu yangu. Karibu kwenye ulimwengu wa waandishi na hongera sana kwa hatua hiyo uliyoamua ya kuwa mwandishi.

    Hata hivyo pongezi zangu hupaswi kuzichukua zote kwa sababu kwa maelezo yako, inaonekana umeamua kuanza kuandika ila bado hujaanza kuandika; kitu ambacho ni muhimu sana,  linapokuja suala zima la uandishi.

    Kiufupi hakuna mtu anaitwa mwandishi kwa sababu eti anatamani kuwa mwandishi au kwa sababu ana mpango wa kuja kuwa mwandishi siku moja. Kama ilivyo kweli kwamba hakuna mtu anaitwa mwanasheria kwa kutamani kuwa mwanasheria bali kwa sababu ameingia darasani, amesomea, amefuzu na anafanyia kazi fani yake.

    Mwandishi ni mwandishi kwa sababu anaandika. Kwa hiyo, nataka na wewe uanze kuitwa mwandishi tena kuanzia leo, na utaweza hilo kwa kuanza kuandika.

    Hatua hiyo moja tu itaweza kukufungulia fursa za kujua vitu vingine vingi. Kwenye swali lako umeuliza

    1. Nani atahariri kazi yangu.
    2. Nani atachapa.
    3. Wapi nitauza.
    4. Nitamudu gharama
    5. Kitabu kibebe page ngapi?

    Naweza kuanza kujibu maswali hayo baada ya kujihakikishia kuwa umeanza kuandika.

    Kwa kuwa najua baada ya kusoma hapa utaendelea mbele na kuanza kuandika , basi acha niendelee kukujuza zaidi, ila sharti langu kwako ni moja tu. Uweke mpango wa kuandika mara tu baada ya kusoma makala haya.

    UTAANDIKA KUHUSU NINI
    Kuna maeneo mengi ambayo wewe unaweza kuandikia. Unaweza kuandika mengi kuhusu
    👉maisha yako (maisha yako ni ya tofauti sana, unaweza kuwa unayachukulia poa, ila kuna mengi kutokana na maisha yako ambayo yanaweza kuwa msaada kwa watu wengine).

    👉 Unaweza kuandika kuhusu ujuzi ulio nao ambao uliwahi kuupata kwa kufanya kazi fulani.

    👉 Unaweza kuandikia eneo la taaluma yako. Kama kuna vitu umejifunza basi kuna watu wengine ambao wangependa kuvifahamu kwa kina hivyo vitu, unaweza kuwaelimisha watu kuhusu hivyo vitu kupitia maandishi yako.

    👉 Unaweza kuandika kuhusu kitu unachopenda kufuatilia. Kama kuna kitu unapenda kufuatilia, basi unaweza kuamua kuzama ndani zaidi ili kukifuatilia hicho kitu huku ukiwa unawajuza wengine kwa kuwaandikia.

    👉 Yapo mambo mengine ya kuandikia, ila kwa leo hayo yatoshe. Mengine utayasoma kwenye kitabu changu cha JINSI YA KUWA MWANDISHI MBOBEVU NDANI YA SIKU 30.

    NANI ATAHARIRI KAZI YANGU
    Wewe ndiye unapaswa kuwa mhariri wa kazi yako ukiwa mtu wa kwanza. Pia kuna wahariri watalaam ambao utawasiliana nao baada ya kukamilisha kazi yako, nao watakuwa tayari kukusaidia. Hivyo, Anza kuandika kwanza, ukifikia hatua ya uhariri wa kazi yako, itakuwa rahisi tu kukuunganisha na wahariri

    NANI ATACHAPA KAZI YAKO
    Wachapaji pia wapo wa kutosha. Anza kuandika kwanza na soma kitabu cha JINSI YA KUWA MWANDISHI MBOBEVU NDANI YA SIKU 30 ili uweze  kupata zaidi mambo mengine kwa undani.

    NITAMUDU GHARAMA
    Ndio utaweza kumudu gharama.

    KITABU KIBEBE PAGE NGAPI.
    Itategemea unandikia nini na unataka kueleza mada kiundani kiasi gani. Binafsi nikiwa naandika kitabu huwa sifikirii sana kuhusu kurasa za kitabu. Ila huwa nafikiria zaidi kuhusu kile nilichonacho kuhusu mada husika. Huwa najitahidi kuandika kila kitu ninachojua na mwisho wa siku upande wa kurasa huwa unajipanga wenyewe. Ila kwa kuwa umeuliza kuhusu kurasa, basi acha nikwambie kwamba viwango vya kimataifa vya kuita kitu kitabu ni kurasa 50. Ila hili lisikuwazishe sana, Anza kuandika kwanza mambo mengine yanajipanga kadiri utakavyoendelea.

    Kwa leo inatosha na ninakomea hapo. Hata hivyo, nakushauri sana, usome kitabu changu cha JINSI YA KUWA MWANDISHI MBOBEVU NDANI YA SIKU 30. Kitabu hiki kina kila kitu unachohitaji kujua kuhusu uandishi wa vitabu na makala.

    Kipate kitabu hiki kwa 6,500/- tu. Kupata kitabu hiki utatuma hicho kiasi kupitia 0684 408 755 jina ni GODIUS RWEYONGEZA.

    Umekuwa nami,

    GODIUS RWEYONGEZA

    Morogoro-Tz

    0755848391

  • USIPOJITAMBUA, KUNA WATU WACHACHE WANAOJITAMBUA WATAKUTUMIA WANAVYOTAKA

    Kuna stori moja ya mchungaji huko Nigeria, ambayo nimelazimika nikushikirishe kwa lengo la kukwambia kitu. Na stori hii ni ya mchungaji Dr. JS Yusuf wa Nigeria ambaye yeye ameanzisha utaratibu wa kuuza chupi kwa wanawake. Chupi hizi zina picha yake na anasema kwamba, mwanamke yeyote atakayevaa chupi hizi, atakuwa na mvuto kwa wanaume na ataweza kumpata mwanaume bora, asiyedanganya, na Wala hawezi kuachika. 

    Kiufupi, mchungaji anawahidi wanawake kuwa wakivaa chupi zake, basi hawatakuwa na maumivu yoyote ya moyo na pia itawakinga dhidi ya magonjwa. Na chupi hizi zinauziwa madhabahuni.

    Kutokana na kijistori hiki, nimeona niseme haya ili yaweze kukusaidia.

    Kwenye dunia hii kujitambua ni muhimu sana, unapaswa kufanya chini juu, kuhakikisha kwamba unakuwa na ndoto kubwa na kusudi la kuwa hapa duniani na kujiweka bize na mambo yako. 

    USIPOJITAMBUA kuna watu wachache wanaojitambua watakutumia wewe, kadiri watakavyo. Watakuendesha na wewe utaendesheka. Mfano mzuri unaweza kuuona kwa wanasiasa. Huwa wanawaendesha wafuasi wao kwa sera na maoni ya hapa na pale. Leo anaweza kusema hili, wafuasi wake wakashangilia, na kesho yake akasema lile wafuasi wakashangilia. 

    Pia, ujifunze kuwa na msimamo na kusimamia ndoto zetu, malengo na kusudi la maisha yetu. Usiwe mtu wa kuyumbishwa, usiwe bendera hufuata upepo.

    Tatu, fahamu kuwa nguvu ya kweli ya kukusaidia wewe kusonga mbele, tayari unayo. Ndio maana James Allen aliwahi kusema; ugunduzi mkubwa niliougundua kwenye zama zangu ni kuwa binadamu ana uwezo mkubwa kuliko unavyoweza kufikiri. Na watalaamu wengi wamethibitisha hili. Utafiti mwingine umeonesha kuwa watu wengi wanatumia chini ya asilimia kumi ya uwezo wao. Hata wale unaowaona  kama wamefanya makubwa, jua kabisa wametumia chini ya asilimia kumi.

    Kwa hiyo, wewe tayari unao uwezo mkubwa ndani yako. Ila sasa ukikaa na kuanza kusubiri sijui chupi ziamshe uwezo huo, utasubiri sana. Nashauri uwe mtu wa kutumia nguvu na uwezo ulionao. Anza leo.

    Nashauri uanze kusoma kitabu changu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO. Pata hardcopy kwa elfu 20 tu. Na soft copy kwa elfu kumi.

    SOMA ZAIDI:  Jinsi ya kuwa na fedha kama serikali

    Jitambue uoke maisha yako. Wasiliana nami leo kupata nakala yako kupitia 0755848391.

  • Lengo Lako Kuu La Mwaka 2022 Ni Lipi? Au Ndio Unamwachia Mungu🤔?

    Jana nilienda kumtembelea mwalimu wangu wa shule ya msingi ambaye kwa sasa ni mstaafu. Kama ilivyo kawaida ya watanzania wengi, nilipofika alifungulia runinga ili tuburudike kwa kuangalia manjonjo ya kimambele.

    Alifungulia channel ya Clouds na nilipoangalia tu kwenye kioo cha runinga nilikutana na swali lililosema,  *Lengo lako kuu la mwaka 2022 Ni lipi? Au ndio unamwachia Mungu🤔?*

    Sikutanii, swali hili lilivuta sana umakini wangu. Kwa miaka kadhaa ambayo nimekuwa nikiongea na vijana na watu mbalimbali kuhusu maisha, wengi wamekuwa wakiishia kuniambia hawana malengo badala yake wanamwachia Mungu maana yeye ndiye kila kitu/ mweza yote/ alpha na omega.

    Hawajui wanataka nini badala yake wanamwachia Mungu.
    Hawana mipango ya kesho kwa kusema kwamba huwezi kupanga, mambo yajayo kwa kuwa Mungu tu ndiye anajua. Hawajifunzi hata kwa serikali inayoweka bajeti kila mwaka na  yenye mipango ya kufanyia kazi kwa mwaka mzima unaofuata. Yaani unakuta kamtu hakana malengo, kanisani hakaendi, dhambi kanafanya kila siku halafu ukikauliza lengo lake kanakwambia namwachia Mungu.???

    Sasa kabla sijaendelea mbele naomba kukuuliza wewe [WEKA JINA LAKO HAPA], Lengo lako kuu la mwaka 2022 Ni lipi? Au ndio unamwachia Mungu🤔?

    USIMBEBESHE MUNGU MSALABA USIO WAKE.

    Ndio Mungu ndio kila kitu, lakini amekuumba wewe na mauwezo makubwa sana na bado amekupa UHURU WA KUCHAGUA mazuri na mabaya. Hivyo, jukumu la kuchagua aina ya maisha unayotaka ni la kwako.

    Mungu hawezi kukuchagulia wewe kuwa masikini wala tajiri, huo ni uchaguzi unaouchagua mwenyewe kupitia maamuzi unayofanya na vitendo vyako vya kila siku. Na hata mamuzi ya mwaka 2022 iweje yapo mikononi mwako. USIMBEBESHE MUNGU MSALABA USIO WAKE.

    Kwenye Biblia Mungu aliwapa uhuru wa kuchagua watoto mapacha (Esau na Yakobo). Mmoja alichagua kuwa mwindaji (mtu aliyekuwa anafanya kazi za nguvu) na mwingine alichagua kukaa nyumbani (alikuwa anafanya kazi kwa akili).

    Sasa na wewe usipochagua wapi unataka kwenda, wapi unataka kufika na aina ya mtu unayetaka kuwa, utakuwa unamwangusha Mungu aliyekupa uwezo wa kipekee na shetani atakuzomea wewe!

    Na hata Mungu akitaka kushusha baraka zake juu yako, atashindwa azishushie wapi kwa sababu hujaegenea popote. Wewe kwako maisha ni bora liende. Ukisukumwa unasukumika, wakienda unaenda, wakirudi unarudi, upepo wa kaskazini ukivuma unakupeperusha, wa kusini nao unakupeperusha….wewe ni bendera gazeti, mlingoti tope!

    MAISHA YAKO NI WAJIBU WAKO
    Maisha yako ni wajibu wako, ukishinda ni juu yako, na ukishindwa ni juu yako.

    Ndiyo maana wewe unapaswa KUWEKA mipango ya wapi unataka kwenda na wapi unataka kufika. Na hapo ndipo sasa Mungu atatokea KUBARIKI KAZI ZA MIKONO YAKO.

    Watu wengi wanatumia kigezo cha Mungu kama kigezo cha wao kutofanya kazi. Ndio maana wengine wanasema aliyekupa wewe ndio kaninyima mimi. Wakati wanasema hivyo Mungu anawaambia kasome Mithali 6:6-11.
    Lakini pia Mungu anawasisitizia kuwa hana upendeleo bali anaibariki mikono ya mtu yeyote anayejishughulisha.

    LENGO LAKO KUU LA MWAKA

    Ili mwaka wako uweze kwenda vizuri, unapaswa kuwa na malengo ambayo utayafanyia kazi ndani ya mwaka huu.

    Kuwa na lengo kuu moja ambalo utalifanyia kazi, kiasi kwamba mpaka mwaka huu unafika mwishoni uweze kusema kwamba kweli mwaka huu nimeweza kufanya kitu.
    Kitu cha kufanya leo.
    Weka lengo lako kuu la mwaka huu.
    Kisha baada ya hapo andika malengo yako mengine. Hivyo, unaweza kuwa na  zaidi ya lengo moja ila lengo lako kuu la mwaka 2022 liwe moja.

    Ukiwa na lengo moja kuu inakuwa rahisi kwako kuwekeza nguvu zako kwenye hilo lengo. Ukiwa na lengo kuu utakuwa tena siyo bendera hufuata upepo.

    Kazi yako ya kufanya leo, andika lengo lako kuu la mwaka 2022?

    Unaweza kunishirikisha lengo lako kupitia simu/WhatsApp +255755848391

    Naomba nimalizie kwa kukuuliza, “Lengo lako kuu la mwaka 2022 Ni lipi? Au ndio Unamwachia Mungu🤔?”

    NAKUKUMBUSHA TU!

    Unaweza kupata nakala yoyote ya kitabu changu kwa elfu 3 tu. Chagua nakala unayopenda hapa (BONYEZA HAPA KUONA VITABU VYANGU)
    https://www.getvalue.co/home/seller_collection/393

    Kisha tuma elfu 3 ili niweze kukutumia kitabu ulicholipia.

    Ukihitaji kupata vitabu vyangu vyooote kwa pamoja. Utalipia elfu 50 tu. Vipo vitabu 17.
    Lipia kwa 0755848391 jina ni GODIUS RWEYONGEZA.

    MWISHO WA OFA HII NI TAREHE 10  JANUARI 2022
    Karibu.

    GODIUS RWEYONGEZA
    +255755848391
    Bukoba-Tanzania
    www.songambeleblog.blogspot.com

X