Home


  • Namba Zetu Za Malipo

    Namba za malipo ya vitabu:

    Namba za lipa

    TIGO PESA: 19016638 Jina ni SONGAMBELE CONSULTANTS

    M-PESA: 5564517 jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

    Namba za kawaida

    AIRTEL MONEY: 0684408755
    TIGO PESA: 0655 848 392
    M-PESA: 0745 848 395

    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    NB: Kama namba ya malipo anatumiwa mtu ambaye yuko nje ya nchi. Iandikwe Kwa kuanza na +255

    Kwa hiyo namba zinazotumwa nje ya nchi zitakuwa
    Airtel money: +255 684 408 755
    TIGO PESA: +255 655 848 392
    M-PESA: +255 745 848 395

    KOTE Jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Kama malipo yatakuwa yanafanyika kupitia benki.

    Yafanyie kupitia

    1. CRDB BANK: 0150770710200
    2. NMB BANK: 22110047274

    Kote jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

  • Wasiliana na Godius Rweyongeza Sasa

    Habari yafuatayo ni mawasiliano Unayoweza kutumia kumpata GODIUS RWEYONGEZA

    Simu: +255 (0) 684408755

    Whatsap: +255 (0) 755848391

    Email: songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu vyake wasiliana Moja kwa Moja na +255 (0) 684408755 (more…)

  • UNAPASWA KUACHANA NACHO

    UNAPASWA KUACHANA NACHO

    Kuna wakati unapaswa kuachana na vitu hata kama watu wanasema ni fursa nzuri.
    Au hata kama kilikuwa ni kitu unapenda kufanya kwa siku nyingi.

    (more…)

  • Njia 7 Za Kutumia Ili Kupata Wazo Bora La Biashara

    Wazo bora la biashara halishuki kutoka mbinguni~ Godius Rweyongeza

    Moja ya kitu ambacho kimekuwa kinawakwamisha watu wengi na kuwafanya washindwe kuanzisha biashara ni wazo la biashara. Watu wamekuwa wanashindwa kupata wazo la biashara, sasa kwenye kipengele hiki ninaenda kukuonesha ni kwa jinsi gani  ambavyo unaweza kupata wazo bora la biashara.

    (more…)

  • Kama Hujui Ni Kitu Gani Unapaswa Kufanya Maishani, Anzia Hapa

    Inatokea kwamba watu wengine kwenye maisha wapo kwenye hali ambayo hawaelewi wanapaswa kufanya nini wala ni wapi wanapaswa kuelekea. Sasa kwenye makala ya leo naenda kuongea na watu wa aina hii na kuona ni kwa jinsi gani ambavyo wanaweza kutumia fursa zilizopo kwenye maisha kuhakikisha kwamba wanasonga mbele.

    Hivyo, kama wewe haupo kwenye hali hii hapa basi unaweza ukaachana na makala hii ili usome nyingine ambazo zinakuhusu, ila endapo utaamua kuisoma makala hii kuna vitu viwili ambavyo nina uhakika kwamba utaondoka navyo.

    Kwanza kuna kitu ambacho unaweza kujifunza kutoka kwenye andiko hili.

    Pili unaweza kupata ushauri ambao siku nyingine unaweza kuutumia  kumsaidi amtu mwingine.

    Upo tayari niendelee?

    KAMA UPO KWENYE HALI AMBAYO HUELEWI NINI CHA KUFANYA

    Ebu chukulia kwamba ndio umemaliza chuo na ulikuwa na matarajio makubwa kwamba baada ya chuo unaenda kuajiriwa sehemu na utapata mshahara mkubwa kutokana na kazi ambayo utakuwa unafanya. Ila sasa upo mtaani na huelewi ni kitu gani ambacho unaweza kufanya. Yafuatayo ni mambo muhimu ya kuzingatia.

    Kwanza unapaswa kujua kwamba kukosa ajira siyo kwamba unakuwa umekosa kazi kabisa. Kazi zipo, badala yake unaweza kuanza kutumia kile ulichonacho

    Anza kutumia elimu yako

    Kama umesoma na una kiwango fulani cha elimu, usikae tu hovyo ukabweteka. Hiyo elimu yako kuna watu ambao inaweza kuwasaidia kwenye hali zao walizonazo. Hivyo, unaweza kuitumia elimu hiyo kuwasaidia watu wengine na watu wengine wanaweza kuwa tayari kukulipa.

    Anza kutumia kipaji chako

    Kwanza kipaji chako unakijua wewe? Kipaji chako ni sehemu nzuri ya kuanzia, unaweza kutumia kipaji chako kama sehemu ya kuanzia kutengeneza kipato, lakini pia kutengeneza mali zinazoshikika na zisizoshikika. Unaweza kutumia kipaji chako kuandaa video au igizo, mafunzo ya sauti, makala, vitabu, muziki, tovuti n.k na hivi vyote vikawa chanzo cha wewe kuanza kuingiza kipato.

    Anza kutumia ujuzi wako

    Kama umewahi kuajiriwa sehemu au umewahi kufanya kazi sehemu nyingine yoyote, jua kwamba una ujuzi tayari ambao unaweza kuanza kuutumia mtaani. Tatizo kuna watu wana ujuzi ila wanaudharau au wanajiona kwamba sio watu wa viwango hivyo vya chini, wao wanachotaka ni kazi ambazo watakuwa wanafanya huku kipupwe kikipita kwa mbaali.

    Sikia nikwambie; kila mtu anapenda kazi za aina hiyo, ila unapokuwa katika hali ambayo huelewi, usichague kazi. kwa sasa kitu kikubwa tunchoshughulika nacho ni wewe kupata kitu ambacho unaweza kuanza nacho maishani mwako na hatimaye ukaweza kusonga mbele na kufikia viwango ambavyo umekuwa unavitamani kwa siku nyingi. Ndoto zako hizo kubwa zinawezekana ila kwa sasa fanyia kazi haya.

    Anza kutumia konekisheni zako

    Kuna watu ambao umekuwa unafahamiana nao kwa siku nyingi, watu hawa wanaweza kuwa msaada kwako kwenye maisha yako, watumie hawa. Konekisheni zako zinaweza kukusaidia kwenye kupata mtaji, kukuunganisha na mteja, kupata kazi n.k. angalia kwenye hao watu wako wote unaofahamiana nao, ni mtu gani ambaye anaweza kuwa msaada kwako.

    Tumia muda wako

    Si huna kitu cha kufanya. Uwekeze muda wako vizuri maana utakuja kukusaidia sana siku zijazo. Hivyo basi, hakikisha kwamba unautuia vizuri muda wako katika kujifunza. Usichoke kujifunza. utumie pia muda wako.

    Tumia nguvu zako

    Nguvu zako kwa sasa ndiyo mtaji mkubwa ambao unapaswa kuuutumia. Anza kuutumia kwa kufanya kazi za nguvu ili upate kipato.

    Nimekwambia haya yote ili uweze kupata sehemu ya kuanzia kabisa. na pale utakapokuwa umepata sasa sehemu ya kuanzia ndipo tunaweza kuendelea mbele.

    Hakikisha kwamba baada ya kupata sehemu ya kunzia huishii tu kwenye hiyo kazi.

    Endelea mbele. Yaani, fanya hiyo kazi huku ukiwa na ndoto kubwa kwenye maisha yako.

    Weka akiba kwa ajili ya ndoto yako kubwa.

    Wekeza fedha zako kwenye maeneo kama hisa, hatifungani na vipande, nyumba za kupanga, mashamba n.k

    Kuza kipato chako kwa kuanzisha biashara n.k.

    Rafiki yangu naomba ufahamu kuwa haya yote niliyoyoasema hayatachukua muda mfupi, yatachukua muda kwelikweli. Ila ukweli ni kwamba, kama kweli utakuwa tayari kuweka kazi na kuachana na njia za mkato, kuna siku utafika.

    Najua umekuwa unatumia njia za mkato kwa siku nyingi sasa, ila hazijaweza kukufikisha popote, sasa ni muda wako wewe kuweka kazi na kuachana na njia za mkato.

    Kila la kheri

  • UBUNIFU UNABORESHA BIASHARA YAKO

    UBUNIFU UNABORESHA BIASHARA YAKO

    Kama wewe umekuwa mtumiaji wa muda mrefu kidogo wa mtandao wa WhatsApp utagundua kuwa mtandao huu umekuwa unafanyiwa marekebisho ya hapa na pale kila mara.
    Kuna kipindi haya mambo ya status au WhatsApp business hayakuwepo.

    Nakumbuka suala zima la kubold, italicize, underline na strikethrough na yenyewe hayakuwepo.

    Ila kadiri siku zilivyoendelea yamewekwa. Hayo ni machache tu kati ya marekebisho mengi ambayo wamefanya.

    Ninachotaka kukwambia ni kwamba kwenye biashara yako, ni vizuri kuwa mtu wa kufiria nje ya boksi na kufikiria zaidi ya hapo ilipo kwa sasa.

    Ubunifu utaitofautisha sana biashara yako na biashara za watu wengine. Maana hata ukisema ufanye biashara ambayo haijawahi kufanywa hapa duniani. Ndani ya miezi sita tu, kuna watu watakuona ukiifanya na wenyewe wataanza kuifanya. Kumbe basi, kitu pekee ambacho kinaenda kukutofautisha wewe na wengine ni ubunifu.

    UBUNIFU SIYO MPAKA UWE NA WAZO AMBALO HALIJAWAHI KUWEPO

    Wengi wanapofikiria ubunifu basi wanadhani, mbunifu yeyote anapaswa kuja na wazo la kipekee sana na wazo ambalo halijawahi kuonekana. Unaweza kuja na wazo la kawaida, ila kwenye biashara yako likawa linaleta mapinduzi.

    Inashauriwa walau kila siku uwe unafikiria mawazo ya kawaida kumi tu na kati ya hayo utoe moja au mawili ambayo utayafanyia kazi. Ukiwa mtu wa kufikiria hivi ni uhakika kuwa mwaka mmoja baadaye, kama ni biashara, lazima tu utakuwa umeisukuma mbali.

    UBUNIFU SIYO MPAKA UWE PROFESA

    Ubunifu ni kitu tunazaliwa nacho. Ndiyo maana utagundua kwamba kila mtoto huwa anapenda kuumba vitu mbalimbali kwa kutumia udongo, mchanga au malighafi zozote anazoona zinamfaa.

    Kwa hiyo hiki kiwe kiashiria kwako kuwa UBUNIFU ni kitu tunacho, tumezaliwa nacho na tunaenda nacho popote. Kadiri ambavyo utautumia ubunifu kwenye kazi, biashara au eneo lolote, ndivyo utakavyoimarika zaidi na zaidi.

    Ungependa kujifunza zaidi kuhusu UBUNIFU?
    Nakushauri upate nakala ya kitabu changu cha JINSI YA KUIBUA UBUNIFU ULIO NDANI YAKO.
    kwenye kitabu hiki nimeongelea tu kuhusu suala zima la UBUNIFU, mwanzo mpaka mwisho.
    Kukipata rusha elfu Saba tu (7,000/-)  kwa 0755848391 au 0684 408 755 jina ni GODIUS RWEYONGEZA.

    Unaweza pia kubonyeza hapa ili ukipate mara moja.

    NB. Kwa Sasa kitabu kinapatikana kwenye mfumo wa nakala laini(ebook).

    Umekuwa nami,

    GODIUS RWEYONGEZA

    Hakikisha Umesubscribe kwenye Channel yangu ya youtube kwa KUBONYEZA HAPA

    Jiunge na mfumo wa kupokea makala maalumu kwa njia ya barua pepe kwa KUBONYEZA HAPA

    Jipatie nakala za vitabu vyangu vya kiswahili kwa KUBONYEZA HAPA

    Kama ungependa kujifunza kuhusu uandishi kutoka kwangu wasiliana nami kwa 0755848391

    kila la kheri

  • Mambo MATATU USIYOYAFAHAMU KUHUSU KIPAJI

     

    Kwanza ni kwamba, KIPAJI hakiazimwi kama nguo. Ni kitu ambacho unazaliwa nacho.

    Pili, kwa kuwa kipaji tunazaliwa nacho hivyo hukilipii gharama yoyote kuwa nacho. Kitu hicho kinafanya kipaji kuwa na bei rahisi sana kuliko chumvi, pengine ndio maana watu wengine hata hawakithamini wala kukipa kipaumbele maishani mwao.

    Tatu, kipaji huwezi kukitumia ukakimaliza. Kadiri unavyokitumia kipaji chako ndivyo unavyozidi kukiboresha na kukifanya kuwa bora zaidi. Ukisikia wanasema mtu fulani ameshuka viwango kwenye kutumia kipaji chake, basi ujue kuna namna anajibana kwenye kukitumia.

    Kipaji ni kama misuli ya mwili, kadiri unavyokitumia, ndivyo inazidi kuimarika zaidi, usipoitumia inafhoofu.

    Umekuwa nami,

    GODIUS RWEYONGEZA

    Hakikisha Umesubscribe kwenye Channel yangu ya youtube kwa KUBONYEZA HAPA

    Jiunge na mfumo wa kupokea makala maalumu kwa njia ya barua pepe kwa KUBONYEZA HAPA

    Jipatie nakala za vitabu vyangu vya kiswahili kwa KUBONYEZA HAPA

    Kama ungependa kujifunza kuhusu uandishi kutoka kwangu wasiliana nami kwa 0755848391

    kila la kheri

  • Kitu Kimoja Cha Kufahamu Kuhusu Umaskini Na Utajiri

    Kuna kitu kimoja ambacho leo ninataka ukifahamu kuhusu utajiri na umasikini.
    Kitu hiki ni kwamba maskini wapo siku zote, ila kazana usiwe mmoja wao.

    Kwenye kila jamii unakuta kuna watu wachache wenye utajiri mkubwa   ukilinganisha na wengine wengi.

    Sasa lengo lako linapaswa kuwa ni wewe kuingia kwenye wale wachache ambao wana utajiri mkubwa.

    Utajiri ni kitu ambacho unaweza kukitengeneza kwa kufuata kanuni chache tu kama
    kuweka akiba
    Kutunza akiba hiyo na hatimaye kuiwekeza
    Kuifanya fedha ikufanyie kazi na vitu vingine vya aina hiyo

    Kwa hiyo kitu cha kwanza kabisa ambacho ninataka ufahamu ni kwamba; masikini wapo siku zote. Ila chagua kutokuwa mmoja wao.

    Pili, upende utajiri na ipende fedha, huwezi kupata wala kuishi na kitu ambacho hukipendi. Huwezi kupata fedha wala kuishi na utajiri kama huupendi utajiri. Upende utajiri nao utakupenda. Zipende fedha nazo zitakupenda.

    Wewe si unaona hata kwa watu. Mtu unapoonesha dalili za kumpenda ndio na yeye anakupenda. Ukionesha kumchukia na mwenyewe anakuchukia pia.

    Ndio maana utasikia mtu anasema, Mimi na mtu fulani huwa hatuendani. Maana yake huwa hawapatani, huwa haziivi. Hawawezi kukaa pamoja.

    Sasa kama na wewe huzipendi fedha maana yake wewe na fedha hamwendani, hampatani, haziivi na hivyo huwezi kukaa pamoja na fedha (ndio maana ukizipata unazifuja kwa kuzitumia hovyo).

    Kuanzia leo, anza kuzipenda fedha. Zipende zikupende.

    Nashauri usome vitabu vyangu vya MAISHA NI FURSA ZITUMIE ZIKUBEBE pamoja na kitabu cha MAAJABU YA KUWEKA AKIBA
    Rusha elfu 20 leo nikutumie ebooks zake leo kwa WhatsApp au barua pepe.

    Rusha fedha kwa 0684408755 jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    SOMA ZAIDI:

    Umekuwa nami,

    GODIUS RWEYONGEZA

    Hakikisha Umesubscribe kwenye Channel yangu ya youtube kwa KUBONYEZA HAPA

    Jiunge na mfumo wa kupokea makala maalumu kwa njia ya barua pepe kwa KUBONYEZA HAPA

    Jipatie nakala za vitabu vyangu vya kiswahili kwa KUBONYEZA HAPA

    Kama ungependa kujifunza kuhusu uandishi kutoka kwangu wasiliana nami kwa 0755848391

    kila la kheri

  • Sababu 03 Kwa Nini Mwezi Januari Unakuwa Mgumu Kwako

    Januari ni mwezi wa kwanza wa kila mwaka. Mwezi unaofuata mara tu baada ya sikukuu za mwisho wa mwaka. Mwezi wenyewe wa januari unaanza kwa shamrashamra za kuushangilia mwaka.

    Ni mwezi ambapo watu wanakuwa wamejichana na kula bata siku chache kabla, huku wakiwa wametumia hata fedha ambazo hawakupaswa kutumia, kitu kinachowafanya waanze mwaka wakiwa wamefuria.

    Watu wanaanza mwaka wakiwa hawana fedha huku upande mwingine fedha zikiwa zinahitajika sana.
    Kuanzia ada za watoto, kodi za nyumba, na mambo mengine

    Vyote hivyo vinahitaji hela na wakati huohuo   mahitaji mengine ya kawaida kama chakula, umeme, kulala, vikiwa vinahitaji hela pia. Hicho kitu kinawafanya watu wachanganyikiwe.

    Kuna utani mtandaoni unaosema

    Watu wafupi mwezi huu mnatupa shida, ukiwa barabarani unatembea unamwona mtu mfupi, unadhani mwanao karudishwa nyumbani kwa sababu ya ada.

    Utani mwingine unasema,
    Kuna ile minyoo ambayo ukiwa nayo unakosa hamu ya kula. Naipataje, maana hii ni januari?

    Wakati hizo kauli hizi mbili zimekaa kiutani, utani tu, ila pia zimebeba ujumbe mzito kuhusu uhalisia wa watu wengi walivyo mfukoni.

    Kwenye makala hii ninaenda kukuonesha kwa nini umefulia mwezi huu wa Januari na hatua za kuchukua ili kuondokana na hiyo hali.

    1. Umefulia kwa sababu unategemea chanzo kimoja cha kipato.
    Hakikisha unakuwa na vyanzo vya kipato zaidi ya kimoja, vitakusaidia kuondokana na ukata.

    2. Umefulia kwa sababu ulitumia fedha nyingi mwishoni mwa mwaka.ulitumia hata fedha ambazo hakupaswa kutumia.

    Suluhisho: kuanzia januari hii anza kuweka akiba maalumu utakayotumia mwishoni mwa mwaka.  Na akiba nyingine kama ambavyo nimekuwa nikikushauri. Na uwe na na nidhamu ya fedha, usitumie fedha za malengo yako mengine kwa ajili kula bata

    3. Umefulia kwa sababu huna hela za kulipa ada za watoto.

    Suluhisho: naomba ufahamu kuwa suala zima la ada za watoto, halipaswi kuwa kitu kigeni kwako. Ni kitu ambacho unakuwa unakifahamu kuanzia januari mpaka disemba. Hivyo kwa mwaka huu uanze kujiandaa kwa kuweka pembeni fedha kidogo kidogo maalumu tu kwa ajili ya ada za watoto.

    Hizo Ni baadhi ya sababu ambazo zinakufanya ufurie januari hii, ziepuke kwa manufaa yako ya sasa na miaka ijayo. Kila la kheri.

    Umekuwa nami,

    GODIUS RWEYONGEZA

    Hakikisha Umesubscribe kwenye Channel yangu ya youtube kwa KUBONYEZA HAPA

    Jiunge na mfumo wa kupokea makala maalumu kwa njia ya barua pepe kwa KUBONYEZA HAPA

    Jipatie nakala za vitabu vyangu vya kiswahili kwa KUBONYEZA HAPA

    Kama ungependa kujifunza kuhusu uandishi kutoka kwangu wasiliana nami kwa 0755848391

    kila la kheri

  • Mwaka Mpya Mambo Mapya: Kauli Inayopoteza Watu Wengi Na Kuwafanya Washindwe Kupiga Hatua Kila Mwaka

     

    Kauli ya mwak mpya na mambo mapya si kauli ngeni masikioni mwa watu. kila mwaka mpya unapoanza huwa unasikia watu wakiisema kauli hii tena kwa kujidai. Binafsi naiipenda pia kuauli hii, japo kuna watu ambao wanaitafsiri vibaya na hivyo kuitumia ndivyo sivyo.

     

    Unakuta mtu kila mwaka mpya unapoanza yeye anakazana kuhakikisha kwamba anaanza kitu kipya kwa kusema kwamba ni mwaka mpya na kuachana na vitu ambavyo alikuwa akifanya hapo mwanzo. Kama ni fursa utakuta mtu anakimbizana kudaka fursa mpya na kuachana na ile ya zamani.

     

    Ubaya wa hiki kitu ni kwamba kinakufanya ushindwe kubobea na watu wanashindw akukuelewa kuwa wewe ni mtu wa aina gani.

     

    Tafsri nzuri ya mwka mpya na mambo mapya ni kwamba unapaswa kuongeza juhudi zaidi kwenye kile ambacho wewe umekuwa unafanya kwa siku zote. Nyingine ni kwamba unapaswa kufanya mambo mapya kwa kuachana na tabia mbovu ambazo zilikuwa zinakuzuia wewe kusonga mbele na kufikia mafanikio makubwa, badala yake unapaswa kuendelea kushikiliai tabia ambzo zitakufanya uzidi kusonga mbele zaidi.

    Tafsiri nzuri ya mwaka mpya na mambo mapya ni kwamba unapaswa kutoa huduma kwa viwango vya hali ya juu sana (viwango vya nyota tano).

    Tafsiri ya mwaka mpya na mambo mapya ni kwamba kama kuna kitu kitu ulikuwa unakifanya kwa namna ya ukawaida sana, sasa unapaswa kuanza kukifanya kwa viwango vikubwa tena vya hali ya juu sana.

    Kama ulikuwa na tabia mbaya (kaa kuvuta bangi na kunywa pombe) achana nazo.

     

    Hiyo ndiyo tafsiri nzuri y mwaka mpya na mambo mapya, ila siyo kwamba kila mwaka wewe uwe unakimbizana na fursa mpya.

    Nakutakia kila la kheri rafiki yangu. umekuwa nami rafiki yako wa ukweli, Godius Rweyongeza.

     


  • Ni Vigumu Sana Kupata Mafanikio Makubwa Bila Ya Kuwa Na Sifa Hii Moja Muhimu

     

    Kwenye vitabu vitakatifu wanaeleza wazi kuwa mlango wa kuingia mbinguni ni mwembamba. Muda mwingine watakuambia kwamba wanaoitwa ni wengi ila wanaochaguliwa ni wachache.

    Sasa kitu hiki pia huwa kinajitokeza kwenye maisha ya kawaida ya mafanikio. Ni vigumu sana kupata mafanikio makubwa kirahisi, wengi wanapenda mafanikio makubwa ila wachache ambao wanaweza kufanikiwa na kufika mbali. Hii ni kutokana na ukweli kwamba mlango wa kufikia mafanikio ni mlango usiopitwa na wengi. Ila huwezi kukutana na mtu ambaye amefanikiwa huku akiwa amepitia njia laini.

    Japo njia hii ni ngumu na mbovu, ila ukiweza kuhimili vishindo na kuipita, itakufanya kuwa imara zaidi.

    Hivyo kama kuna sifa kubwa ambayo unaihitaji ili kuweza kufikia ndoto yako kubwa ni kuwa tayari kuhimili vishindo na magumu unayopitia kwenye kazi au biashara au kitu chochote unachofanya.

    Magumu ambayo unapitia japo unaweza kuyaona mabaya, ila yanakuwa yanalenga kukuimarisha na kukufanya wewe kuwa bora zaidi. na hii ndiyo sifa kubwa sana ambayo unaihitaji sana ili kuweza kufikia mafanikio makubwa.

    Umekuwa nami,

    GODIUS RWEYONGEZA

    Hakikisha Umesubscribe kwenye Channel yangu ya youtube kwa KUBONYEZA HAPA

    Jiunge na mfumo wa kupokea makala maalumu kwa njia ya barua pepe kwa KUBONYEZA HAPA

    Jipatie nakala za vitabu vyangu vya kiswahili kwa KUBONYEZA HAPA

    Kama ungependa kujifunza kuhusu uandishi kutoka kwangu wasiliana nami kwa 0755848391

    kila la kheri

  • Huu Ni Upande Ambao Ni Marufuku Kwako Kuuchagua

     

    Rafiki yangu, najua unafahamu kuwa una uhuru wa kuchagua chochote kile unachotaka kuwa. Unaweza kuchagua kuwa mwalimu, mchekeshaji, mshereheshaji, dereva, mkulima, mwanamichezo, mwanasiasa, mwanaharakati au chochote kile. Huo uhuru unao na wala hakuna mwenye uwezo wa kukuzuia wewe kwenye hilo.

    Hata hivyo, kuna kitu kimoja tu ambacho ningependa kukutahadharisha, na kitu hiki siyo kingine bali kuchagua kuwa mlaji tu. Haupaswi kuwa mlaji wa kazi za watu wengine tu, hila wewe kuzalisha kazi.

    Kwa kitu chochote kile ambacho umechagua kwenye maisha, hakikisha unachagua kuwa mzalishaji.
    Dunia tunayoishi, haipungukiwi hata kidogo na walaji, ila wazalishaji ndio wachache. Wewe kuwa huu upande wa wazalishaji

    Kama ulizoea kuingia YouTube na kuangalia video tu, kisha kuondoka, sasa ni zamu yako pia ya kuzalisha.

    Kama ulizoea kusoma vitabu vya watu wengine, na wewe zalisha hata kwa kutupa mrejesho juu ya mambo uliyojifunza kwenye vitabu husika.

    Rafiki yangu, kuanzia leo. Anza kuwa mzalishaji.

    Umekuwa nami,

    GODIUS RWEYONGEZA

    Hakikisha Umesubscribe kwenye Channel yangu ya youtube kwa KUBONYEZA HAPA

    Jiunge na mfumo wa kupokea makala maalumu kwa njia ya barua pepe kwa KUBONYEZA HAPA

    Jipatie nakala za vitabu vyangu vya kiswahili kwa KUBONYEZA HAPA

    Kama ungependa kujifunza kuhusu uandishi kutoka kwangu wasiliana nami kwa 0755848391

    kila la kheri

X