Home


  • Nukuu 7 Za Kufikirisha.

    1.

    2.

    3.

    4.

    5.

    6.

    7.

  • Ni njia zipi unazitumia kusambaza bidhaa au hudhuma zako?

    rafiki yangu mpendwa salaam
    leo nataka tuongelee ni njia ambazo unazitumia kuhakikisha kwamba unasambaza bidhaa zako? Una njia moja, mbili au zaidi!

    Ninachotaka kukwambia siku ya leo ni kwamba kadri unavyokuwa na njia nyingi zaidi za kusambaza bidhaa zako ndivyo ambavyo unakuwa na uwezo wa kuwafikia wateja wengi kuliko pale unapokuwa na njia chache.

    Hivyo kama unaweza kuwa na njia nyingi za kuwafikia wateja wengi, basi zitumie.

  • Mazoea ni mabaya sana

    Mwaka fulani wakati wa mahali la saba wanafunzi waliimba wiMbo fulani unaosema
    Mazoea ni mabaya sana*2
    Wimbo huu ulikuwa ni kuwaaga darasa la saba ambao walikuwa wanamalizia masomo yao na kwenda hatua inayofuata.

    Sikumbuki nilikuwa darasa la ngapi kwa wakati hu[, na wimbo wenyewe siukumbuki vizuri sana, ila nakumbuka kiitikio kilikuwa kinaanza hivyo

    Mazoea ni mabaya sana

    na lengo kubwa la wimbo huu lilikuwa ni kuonesha kuwa la saba walishazoeleka pale shuleni, kwa hiyo kuondoka kwao kutaacha pengo. Mazoea ni mabaya sana

    Leo nimeamua kuandika hivi baada ya jana kuchelewa kulala, nikitegemea nitaamka saa 1 asubuhi, 
    Lakini wapi, saa nane tu usingizi umekata na hapa tayari nimeamka naandika.
    Mazoea ni mabaya sana.

    Juzijuzi hapa nimenunua smartwatch, nikategemea basi nitaiona ya ajabu, lakini cha kushangaza nikiikumbuka simu yangu (smartchwatch hata sina muda nayo).
    Mazoea ni mabaya sana.

    Ndiyo maana tunashauriwa tujenge mazoea kwenye vitu vizuri.
    Siyo unajenga mazoea kwenye kubeti, utashangaa unabeti hadi mke wako kama Mwijaku.
    Mazoea mabaya sana.

    Mazoea mabaya sana, ila kwa upande mwingine mazoea ni mazuri sana.
    Kama utaajizoesha vitu chanya.
    Kama kusoma vitabu, KUWEKEZA, kufanya kazoezi.
    Maana kila muda fulani wa kufanya jambo husika ukifika utajikuta unakimbia ukalifanye.
    Lakini ukijizoesha kula chipsi mayai, utashangaa unanenepa wakati ulikuwa mbaumbau, eti na wewe unakuwa bonge.
    Ila mazoea haya jamani


    Mzee mmoja hakuwa na uvumilivu.
    Msimu wa kahawa (kule uhayani kahawa ni zao lina heshima yake) ulipokuwa unafika, mibuni  ikianza kutoa maua tu, anauza maua yale kwa walanguzi ambao mara nyingi huwa wanatoa hela kidogo, ili haadaye msimu ukifika na wao waambulie kitu kwa uwekezaji wao.
    Huyu mzee kila mwaka alikuwa anauza kahawa zake kwenye hii hatua
    Na kila mwaka alikuwa anasema hajawahi kushika hata laki moja kwa wakati mmoja, ilihali kahawa zake tu, zingekomaa zingempa mamilioni kwa wakati mmoja. Mzee huyu ameaga dunia mwaka juzi akiwa hajawahi kushika laki moja kwa wakati mmoja kwenye mkono wake.

    Mazoea haya, we acha tu.

    Tena huyu mzee alizoea kujiambia kwamba sijawahi kushika laki moja. na hivyo neno lake liligeuka kuwa sheria maana imeandikwa kuwa kimtokacho mtu ndicho kimtiacho unajisi. Kasome Marko 7:20

    na wahenga wetu walishasema kitambo sana kuwa maneno huumba. ukiyatumia maneno yatakusaidia kuumbakitu kizuri au la yatakuumbia ubaya. ukiyatumia kwa mazoea (kwa kurudia rudia) akili yako inazoea kile ambacho unakuwa unajiambia.

    Badala ya wewe kujiambia maneno hasi.

    Anza kujiambia maneno chanya. maneno mazuri ambayo yatakusukuma mbele na kukufanya upambanie malengo na ndoto zako kubwa. Kamwe rafiki yangu usikubali kurudi nyuma wala kuyumbishwa na mtu au kitu chochote hasa kwenye kujisemea na kujinene ,maneno chanya. mara zote jinenee maneno chanya maana maneno yanaumba.

    Na kwa sababu yanaumba, yakiswemwa kwa mazoea kwa muda mrefu, mwisho wa siku yanakuja kwenye uhalisia.

    Ninachotaka nikusisitize wewe
    Kuanzia leo
    Anza kujenga mazoea chanya
    Kama kusoma vitabu
    Kuandika
    Kunoa kipaji chko
    KUWEKEZA
    N.k
    Mazoea ni mabaya ukiyawekeza kwenye tabia mbaya na mazuri yakiwekwa sehemu sahihi.


    Asante
    Mimi naitwa
    Godius Rweyongeza kutoka Songambele
    Tutembelee www.songambele.co.tz
    Tupo Mafiga, Tenki Bovu, Morogoro, Tanzania
    Simu zetu ni +255755848391 au +255684408755
    Hata WhatsApp ni hizohizo.
    Hatuna mbambamba wala nini



  • Kwa nini tunapaswa kuwafundisha watoto fikra za kijasiriamali tokea wakiwa shuleni

    Watoto wetu wanapaswa kufundishwa fikra za kijasiamali tokea wakiwa shuleni. Haijalishi kama watakuwa wajasiriamali na wafanyabiashara au hawatakuwa, lakini bado tunapaswa kuwafundisha wawe na fikra hizi maana zitawabeba sana kwenye maisha yao.

    Kwenye video hii nimeeleza kwa undani na kwa kina kuhusiana na hii dhana na namna ambavyo tunaweza kuanza kuitumia mara moja.

  • Nukuu 12 Za Kufikirisha:

    1.

    2.

    3.

    4.

    5.

    6.

    7.

    8.

    9.

    10.

    11.

  • Uoga wako ndiyo umasikini wako

    Watu wengi wanashindwa kuchukua hatua kwenye maisha kwa sababu tu ya kuwa na uoga. Kwenye somo la leo tunaenda kuona ni kwa namna gani unaweza kuondokana na uoga na kuweza kufanya makubwa. Haya twende kazi sasa

  • Nukuu 6 Za Kufikirisha.

    1.

    2.

    3.

    4.

    5.

    6.

  • Nukuu 13 Za Zufikirisha

    01:

    2″:

    4.

    5.

    6.

    7.

    8.

    9.

    10.

    11.

    12.

    13.

  • Upo tayari kuambiwa ukweli?

    Rafiki yangu wa ukweli. Kama unaishi kwenye hii dunia, moja ya kitu ambacho huwezi kukikwepa ni watu kukusema. watu wanaweza kukusema kwa mazuri au kwa mabaya.

    Moja ya kitu ambacho kamwe haupaswi kuogopa ni kusemwa. Kwenye hii dunia, kila mtu anasemwa, marehemu tu anasemwa, sasa wewe uliye hai unadhani itakuwaje?

    Kama hakuna mtu yeyote anayekusema, hata nashindwa niseme nini juu yako, lakini naweza kusema HAUISHI. Unapaswa kuanza KUISHI.

    SOMA ZAIDI: Kufa Leo, uishi milele

    Na kwenye kusema wapo watakaokusema kwa uzuri, na wapo watakaokusema kwa ubaya. Wapo watakaokusema wakilenga uboreshe unachofanya ili kiweze kuwa bora zaidi, na wapo watakaokusema wakikukosoa kwa kukandamiza kila juhudi unazofanya.

    Na kadiri unavyokuwa kiongozi au mtu wa ngazi za juu, ndivyo ambavyo kusemwa kwako kunakuwa kukubwa sana. Hivyo kwenye hilo eneo, usiogope kusemwa.

    njia bora ninayotaka uangalie kusemwa huku ni kuangalia ukweli. Kama wanachosema watu kina ukweli wowote ndani yake, basi huo ukweli uchukue unakufaa. Kama wanaokusema wanalenga kukusaidia uboreshe unachofanya, usiwapuuze.

    Ukweli mara zote huwa unabaki kuwa ukweli bila kujali nani anasema huo ukweli. Bila kujali ukweli huo umetoka kwenye kinywa cha nani. UKWELI NI UKWELI.

    Kama wanaokusema wanalenga kukukosoa, ila wanachosema hakina ukweli wowote ndani yake. Yaani, labda wanasema hivyo ili wakuangushe hapo wapuuze na endeelea mbele kuweka juhudi kwenye kazi unazofanya.

    rafiki yangu, mimi rafiki yako nakupenda sana na ninakutakia wakati mwema.

  • Ni Kitu Gani Kimoja Ambacho Unaenda Kukifanya Wiki Hii Nzima Mfululizo Bila Kuacha

    Leo ni jumatatu nzuri sana. Na kwa kuwa ni mwanzo wa wiki, una nafasi nzuri ya kuitumia siku ya leo kuchagua kitu kimoja ambacho utakifanya kwa msimamo wiki hii bila kuacha.

    Kama wewe ni mwandishi, wiki hii unaweza kujiwekea utaratibu wa kuandika kwa wiki nzima bila ya kuwa na sababu yoyote ambayo inakuzuia wewe usiandike. Au unaweza kuamua kwamba lazima wiki hii kila siku, niandike sura moja ya kitabu na ikamilike. Wakati mwingine hatua kama hizi zinahitaji kujisukuma kidogo au kwenye nje ya mazoea uliyonayo, lakini ukweli ni kwamba hizi ni hatua ambazo uanapaswa kuzichukua hasa pale unjapokuwa umedhamiria kusongambele na kuhakikisha unafanya makubwa bila ya kukwama au kuyumbishwa na kitu chochote.

    Ukweli ni kuwa kama unataka kufanya makubwa kuna wakati ambapo unapaswa kuchukua hatua kama hizi ili uweze kufikia mafanikio makubwa ambayo unataka.

    Kama kwa mfano unataka kutoa kitabu siku za hivi karibuni basi unatakuwa kuahakiksiha kwamba unachukua hatu kama hizi ili uweze kutoa kitabu chako.

    Ni kitu gani kimoja ambacho unaenda kukiwekea mkazo wan nguvu wiki hii?

X