Home


  • Namba Zetu Za Malipo

    Namba za malipo ya vitabu:

    Namba za lipa

    TIGO PESA: 19016638 Jina ni SONGAMBELE CONSULTANTS

    M-PESA: 5564517 jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

    Namba za kawaida

    AIRTEL MONEY: 0684408755
    TIGO PESA: 0655 848 392
    M-PESA: 0745 848 395

    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    NB: Kama namba ya malipo anatumiwa mtu ambaye yuko nje ya nchi. Iandikwe Kwa kuanza na +255

    Kwa hiyo namba zinazotumwa nje ya nchi zitakuwa
    Airtel money: +255 684 408 755
    TIGO PESA: +255 655 848 392
    M-PESA: +255 745 848 395

    KOTE Jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Kama malipo yatakuwa yanafanyika kupitia benki.

    Yafanyie kupitia

    1. CRDB BANK: 0150770710200
    2. NMB BANK: 22110047274

    Kote jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

  • Wasiliana na Godius Rweyongeza Sasa

    Habari yafuatayo ni mawasiliano Unayoweza kutumia kumpata GODIUS RWEYONGEZA

    Simu: +255 (0) 684408755

    Whatsap: +255 (0) 755848391

    Email: songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu vyake wasiliana Moja kwa Moja na +255 (0) 684408755 (more…)

  • Vitu Viwili Ambavyo Havitapitwa na wakati kwenye zama hizi

    Tuna facebook, twitter na mitandao mingine ya kijamii. Kila mtu anakazana sana kuhakikisha kwamba kwenye hii mitandao anakuwa na wafuasi wengi

    Hata hivyo, ukweli ni kwamba hii mitandao huimiliki wewe. Muda wowote ule wanaomiliki hii  mitandao wanaweza kufanya chochote na watu wazuri wanaofuatilia kazi zako wakashindwa kuziona tena. Hii ni mbaya sana.

    Instagram wanaweza kukufungia leo na watu wote ambao wanafuatilia kazi zako huku wakashindwa kuona vitu vizuri wanavyopata kutoka kwako.

    Facebook na majukwaa mengine yote yanaweza kukufungia na watu wakakosa vitu vizuri kutoka kwako. Unakumbuka kilichomtokea Trump?

    Ila kuna vitu viwili ambavyo kwenye zama za leo ni uhakika hakuna mtu anaweza kukuzuia ukiwa navyo.

    Kwanza ni email list

    Hawa ni watu wanaokuwa wamejiunga na mfumo wako wa kupokea mafunzo kwa njia ya baruapepe. Unaweza kupoteza wafuasi wako wa facebook, instagram au sehemu nyingine lakini hawa huwezi kuwapoteza. Hawa watu ni wako na umiliki wa haya mawasiliano unakuwa nayo wewe wala siyo Zuckerberg au mtu mwingiine.

    Halafu isitoshe barua pepe ni kitu binafsi. Unapokuwa unawasiliana mtu kwa njia ya barua pepe unakuwa unawasiliana naye yeye kama yeye. Hivyo, inakuwa rahisi kujenga uhusiano wa karibu na watu wako. Kwa sababu wanaweza kufunguka kwako chochote na wewe unaweza kufunguka kwao chochote. Kwa hiyo mnajenga uhusiano wa kudumu.

    Baruapepe za watu unakuwa nazo wewe, siyo kwamba wanakuwa nazo facebook au instagaram ambao wanaweza kusepa na followers wako muda wowote.

    Kwa hiyo rafiki yangu, japo unajenga wafuasi kwenye hii mitandao. Ebu fikiria pia kuhusu namna unavyoweza kujenga email list yako. Mfumo wa kupokea makala kwa njia ya barua  pepe ambapo watu wako watakuwa wanapokea mafunzo kwa njia ya baruapepe.

    Unaweza kuanza kujenga huu mfumo kupitia jukwaa kama mailchimp, mailmunch, mailerlite na nyinginezo nyingi zilizopo. Chagua moja na komaa hiyo kwa kuanzia.

    Pili Ni Tovuti Au Blogu

    Hki ni kitu kingine ambacho wewe mwenyewe una umiliki nacho na wala siyo facebook wala twitter. Hawana mamlaka yeyote huku.

    Ebu chukulia mfano wa kawaida tu. ukiandika status ya whatsap inapotea baada ya saa 24.

    Leo hii kuna vitu ambavyo uliandika kwenye instagrama yako mwaka 2020 ila unavitafuta na huwezi kuvipata. Na isitoshe hakuna namna ambavyo unaweza kumwambia mtu arejee masomo yako ya nyuma ii kujifunza na kunufaika zaidi. Ila mimi kwenye blogu hapa naweza.

    Mfano, soma hili somo nililoandika siku za nyuma kwa KUBONYEZA HAPA

    Unaona ee! Hiki kitu kwenye blogu nakifanya ndani ya sekunde tu na kinaisha, ila ukitaka kufanya hivi facebook, inabidi utenge masaa ya kutafuta kile ulichoandika siku za nyuma.

    Ukibahatika kukiona ndio unaweza kumwonesha mtu akiangalie. Rafiki yangu naomba unisikilize kwenye hili

    Kuwepo facebook, kuwepo instagram, ila kitu kimoja tu ni kwamba usiache kuwa na blogu yako pamoja na email list maana hivi ni vitu viwili ambavyo unaweza kumiliki mtandaoni.

    Hii ni maalumu kwa ajili yako wewe unayefanya biashara kwa njia ya mtandao na unataka kujenga mtandao wa watu utakaodumu nao bila kuwapoteza. Na ngoja nikwmabie kitu. Hivi

    Kila la kheri

    Umekuwa name Godius Rweyongeza (Songambele)

    0755848391

    Morogoro-Tz

  • KITABU CHA MY STORY kipo, hivi ndivyo unaweza kukipata

    KUPATA KITABU HIKI, tuma baruapepe kwenda songambele.smb@gmail.com

    Rafiki yangu mpendwa unaendeleaje. Kwenye mojawapo ya makala ambazo nimewahi kuandika hapa siku za nyuma nilieleza kuwa nina kitabu cha MY STORY cha Mohmmed Ibn

     Sasa watu wengi wamekuw wananiomba niwatumie hiki kitabu, leo nimeona nikwambie kwamba unaweza kupata hiki kitabu. Kama utakaitaka basi nitumie ujumbe kwa njiaa ya baruapepe ili nikutumie.

    Baruapepe yangu ni godiusrweyongeza1@gmail.com au songambele.smb@gmail.com

    Kichwa cha habari andika KITABU CHA MY STORY

  • Njoo rafiki yangu ujifunze mbinu za kuwekeza kwa faida.

    Unaendelea rafiki yangu. Bila shaka kila kitu kipo Safi kwa upande wako.

    Mimi huku naendelea vyema.

    Nilikuwa najiuliza, Hivi umeshajiunga na semina ya uwekezaji kwenye HISA ambayo itaendeshwa kwa njia ya mtandao kuanzia tarehe 1.8.2022?

    Kama ulikuwa hujui Ni kwamba kwenye semina hii ya kipekee, unaenda kujifunza mengi kuhusu uwekezaji kwenye HISA

    Baada semina hii utaanza moja kwa moja kuwekeza.

    Semina hii ya kimtandao, itadumu kwa siku 10. Na baada ya semina unaenda kupata kitabu (hardcocopy) bila gharama ya ziada.

    Gharama ya semina hii Ni 21,000/- tu.
    Ambapo
    Utapata mafunzo ya semina kwa siku 10. Mafunzo yatatolewa kwa mfumo wa Makala, sauti na video
    Utapata kitabu (Hardcopy) Cha JINSI YA KUWEKA AKIBA NA KUANZA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE.
    Jina lako litaandikwa kwenye kitabu pia. Kila mshiriki wa semina jina lake litaandikwa kwenye hiki kitabu hiki.

    ….nisingependa usikose semina hii ya kipekee. Ebu thibitisha ushiriki wako kwa kulipia leo hii.

    Malipo yote yanafanyika kupitia Namba ya simu (Airtel money) 0684408755 jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Ukishalipia wewe unabaki kusubiri mafunzo haya ya kipekee sana.

    Njoo rafiki yangu ujifunze mbinu za kuwekeza kwa faida.

  • Hii dhana ambayo kila kijana anapaswa kuachana nayo

    Vijana tupambane, ifike hatua haya mabango yaondolewe mitaani kwetu.

    Vijana wanapokuwa wanafikiria kuanzisha kitu, kitu Cha kwanza wanafikiria kupata mtaji au msaada. Nakumbuka wakati naanza chuo mwaka 2016 nilimwambia rafiki yang hivi, mpaka nahitimu chuo nataka niwe na uwezo wa kuajiri vijana kumi”. Yeye aliniambia “mpaka  nahitinu chuo nitakuwa nimetafuta na kupata wadhamini kumi” 

    Sasa nadhani vijana tunapaswa kubadili fikra zetu.

    Tubadili namna tunavyofikiri maana mitaji mingine tayari tunayo.
    Una nguvu zako. ZITUMIE hizi kuchapa kazi
    Una akili itumie kubuni vitu
    Una kipaji, kitumie.
    Una muda, utumie
    Una ujuzi/elimu itumie pia.

    Kwa vyovyote vile, usikubali kuendelea kubaki ulivyo. Nakubaliana na Martin Luther King Jr aliyesema kwamba, Kama huwezi kupaa, kimbia. Kama huwezi kukimbia tembea, Kama huwezi kutembea Basi tambaa Ila kwa vyovyote vile usikubali kubaki ulivyo. Pambana uwezo unao.

    Tuachane na dhana ya kwamba Kuna mtu atasimamia na kufanya vitu kwa niaba yetu.
    Maisha yako ni wajibu wako kijana. Ukiendeleza kusubiri misaada kutoka sijui wapi ili ufanikishe malengo yako. Utasubiri Sana.

    Anza hata kidogo
    Fanya Kitu
    Wanaopata bahati Ni wale walio kwenye mwendo siyo wale wanaokaa vijiweni tu wakisubiri bahati.

  • Namna ya kukabiliana na ukosefu wa ajira kwa vijana. Njia Saba Zilizothibitishwa (Njia Namba 2, 4 na 7 ni muhimu sana)

    Mwishoni mwa mwezi uliopita nilisafiri kwenda Dar kutembea. Nikiwa Dar nilipata nafasi ya kuongea na mmoja wa rafiki zangu. sijui ilikuwaje lakini kwenye maongezi yetu kuna sehemu tulifika tukaanza kuongelea suala zima la ajira, na hapo ndipo akawa ananiambia kwamba yeye alihitimu mwaka 2006 na kupata ajira miezi mitatu baada ya kuhitimu.

    Kwa maneno yake akawa ameianiambia, “siyo kama ninyi vijana wa siku hizi mnahitimu na kukaa mtaani miaka na miaka bila kupata ajira”. Aliendelea kuniambia na hiyo miezi mitatu aliyokaa bila kupata ajira ni sawa na alichelewa kupata ajira.

    Siku hizi hali ni tofauti. Vijana wanaozidi kuhitimu kila mwaka ni wengi ila wanaoajiriwa ni wachache sana. Kilio kikubwa cha vijana sasa hivi ni ajira. Sasa nini kifanyike ili kuondokana na hali kama hii?

    Sasa viafuatavyo ni vitu ambavyo kwa leo ningependa kushirikisha kuonesha ni kwa namna gani tunaweza kuondokana na tatizo la ajira

    Moja. Kufanya kazi kwa bidii kunaweza kukukutanisha meza moja na wafalme

    Ukisoma CV za vijana wengi wanajinadi kamawachapakazi na wanaofanya kazi kwa bidii. Na ambao wapo tayari kufanya kazi kwenye mazingira na hali yoyote. (nasema ukisoma CV za vijana wengi kwa sababu mimi mwenyewe hata CV ya kuombea kazi sina na sina mpango wa kutengeneza moja. nataka matendo yangu na kazi zangu tu ziongee mbele ya watu.

    Lakini kitu cha kushangaza ni kwamba, vijana hawa hawa ambao wanajinadi kwamba wanaweza kufanya kazi kwa bidii wakiajiriwa hawafanyi kazi kwa bidii. Mwajiri asipokuwepo hawawezi kujisimamia na kuchapa kazi badala yake wanachapa soga.

    Ongea na mwajiri yeyote, atakwambia asilimia kubwa ya tatizo analokumbana nalo kwa vijana wa siku hizi anaowaajiri ni uzembe. Mtu hataki kujituma na kufaya kazi kwa bidii.

    Inaweza kushanganza ila ni kweli, kijana ameajiriwa anatumia muda mwingi facebook na instagram kwa siku kuliko anavyoutumia kweye kazi yake, asa unashangaa hivi huyu ameajiriwa  na kampuni ya facebook au nini kinaendelea.

    USHAURI WANGU: vijana wenzangu tupende kufanya kazi kwa bidii. Tukipewa kazi tuifanye kwelikweli kwa viwango vya juu. Kazi ni moja ya kitu ambacho kinaweza kukuinua juu, juu sana. nimekuwa nikiandika mara kwa mara humu kuwa kazi inaweza kukufanya ukutane meza moja na wafalme. Kazi inaweza kukuinua juu.

    Ninachojua ni kwamba, unaweza ukawa hauna elimu kubwa, unaweza ukawa hauna ujuzi mkubwa, unaweza ukawa hauna konekisheni kubwa, ila kazi tu ikakuinua.

    Sidhani kama kuna mwajiri anachukuia mtu anayefanya kazi kwa bidii. Mtu anayejituma na kufanya kazi kwa viwango vya juu. Hakuna mwajiri wa aina hii. kwa hiyo vijana tupende kazi.

    SOMA ZAIDI: WANAOSHEREKEHEA KUHITIMU CHUO TUWAAMBIE UKWELI? AU TUWAACHE KWANZA WAFUMUE NYWELE ZAO ZA GRADUATION?

    Mbili, tuwaambie vijana watembee na ujuzi mtaani na siyo Vyeti

    Dunia ya sasa hivi imebadilika sana. Kuna kazi au ajira zilizokuwepo siku za nyuma, ila siku hizi hazipo au la zinaelekea kuisha. Siku hizi kuna hizi mashine ambazo zinaweza kufanya kazi ya watu wawili mpaka kumi au hata zaidi kwa wakati mmoja. Kwa hiyo, mashine moja inakula ajira za watu kumi

    Na sasa hivi kuna mshine zinatibu,

    Mashine ambazo zinafanya kazi za kihasibu

    Mashine ambazo zinafanya kazi za kilimo mpaka mapishi.

    na mashine hizi haziitishi mgomo, mashine hizi haziombi kufanya kazi kwa saa chache zinafanya kazi saa 24 siku saba za wiki. Ebu chukulia mfano wa ATM benki. Hii mashine kila siku inafanya kazi, haina likizo na wala haitakuja kulilia likizo hata siku moja, haiwezi kugoma na wala haiwezi kudai ongezeko la mshahara. Gharama pekee inayotumika kwenye hii mashine ni gharama ya kuinunua na gharama za maintainace.

    Sasa ili kijana uweze kuishi kwenye ulimwengu huu wa mashine unapaswa kujitofautisha.

    Nakumbuka siku moja wenye mtandao wa Quora Kuna mtu aliuliza, nawezaje kuwa Kama Elon Musk, Jeff Bezos au Bill Gates?  Justin Musk ambaye ni mke wa zamani wa Elon Musk, alijibu kwa kusema HUWEZI. Ila kama unataka kufikia kwenye viwango walivyofikia basi chagua kitu kimoja kisha bobea kwenye hicho kitu kiasi kwamba hakuna mtu ambaye anaweza kubobea kwenye hicho kitu kama wewe. Kisha baada ya hapo bobea kwenye kitu kingine. Mfano, bobea kwanza kwenye uhasibu kisha bobea kwenye kompyuta. Baada ya hapo unganisha hivyo vitu viwili kutengeneza kitu kimoja.

    Alimalizia kwa kusema, uliweza kufanya hivyo, nakuhakikishia hakuna mtu hata mmoja ambaye anaweza kukufikia kwenye kitu utakachofanya. Na wala hakuna mashine itaweza kuchukua kazi yako.

    NDIYO MAANA vijana tunapaswa kutembea na ujuzi mtaani. Mwenye ujuzi halali njaa, mwenye cheti mhhh!

    Sasa na wewe Unapaswa kubobea. Dunia ya leo bado inawapenda sana wabobevu na inawalipa vizuri ukilinganisha na watu wa kawaida.  Sasa swali langu kwako, unaemda kubobea katika nini?

    Kama ungependa kubobea kwenye uandishi hakikisha unajipatia nakala ya kitabu hiki Cha JINSI YA KUWA MWANDISHI MBOBEVU NDANI YA SIKU 30. Bonyeza hapa.

    Tatu, vijana tuwe waaminifu

    Kuna akili ambazo vijana wengine wanakuwa nazo, zinakuwa siyo nzuri. Mtu anawaza aajiriwe halafu aanze kupiga cha juu. Yaani, aanze kuiba. Uaminifu ni mtaji mkubwa. Watu wanapenda kufanya kazi na waaminifu. Uaminifu ni kitu  muhimu bila kujali umeajiriwa au umeajiajiri

    Siku za nyuma hapahapa kwenye hii blogu niliwa hia kuandika namna ambavyo kijana mmoja alikusanya vijana wengine na wakaunda kampuni huku wakimshirikisha mmwekezaji. Wazo lao lilikuwa ni kulima mboga mboga, kwa kuanzia na nyanya na mboga nyinginezo.

    Walikubaliana na mwekezaji kuwa wao wangekuwa na asilimia sitini ya umiliki wa kampuni (walikuwa vijana watano) na mwekezaji angepata asilimia 40.

    Wakati taratibu za kusajili kampuni zikiendelea, mwekezaji alimpa kiongozi wao milioni saba. Mradi ulikadiriwa kuwa wa milioni 30. Kijana alipopokea hela akatokomea kusikojulikana.

    Kama vijana tunahitaji kuwa waaminifu kwenye kazi zetu.

    waaminifu kwa wale tunaofanya nao kazi

    Waaminifu kwa kwenye bidhaa zetu. Ukimuuzia mtu bidhaa, umuuzie bidhaa inayoendana na hela aliyotoa. Kiuhalisia bidhaa yako inapaswa kuwa na thamani zaidi hata fedha inayotoka. Hiki kitu ndicho tupambane nacho. Bila uaminifu, sahau kuhusu mafanikio yoyote yale maishani mwako.

    SOMA ZAIDI: Jinsi Ya Kuanzisha Biashara Bila Mtaji Tanzania

    Nne;KIJANA FANYA KITU

    Huwa napenda kuwaambia vijana wenzangu kuwa haifai wewe kuendelea kulalamika tatizo la ajira huku ukiwa umekaa kwenye kochi. Ebu fanya kitu chochote kile ambacho ni halali na kinaweza kukuingizia kipato.

    Usikae tu na kujiita msomi, huku ukiwa huna hata kitu chochote cha kukuingizia kipato.

    Fanya chochote

    Uza karanga

    Uza madazi, vitumbua n.k.

    Najua vitu kama hivi kwa wasomi wengi ni kichekesho, kwa sababu wengi wanapenda wakae kwenye ofisi yenye kiyoyozi. Yaani, mtu amehitimu halafu aanze kuuza mandazi. Inaonekana ajabu kweli.

    Ila ushauri wangu kwako kijana mwenzangu ni huu: Fedha zako wanazo watu wengine.Hapo hapo ulipo kuna watu wana fedha zako, ila huwezi kuzichukua hizo fedha kwa nguvu, huo utakuwa ni wizi.

    Njia nzuri ya wewe kupata fedha ni kuwapa kitu wanachotaka. Na moja ya kitu ambacho wanataka ni chakula. Kwa hiyo unaweza kuwapa hicho ili wakupe fedha. Ndiyo maana hapo juu nikasema kwamba unaweza hata kuuza mandazi au vitumbua.

    Najua wazi kuwa una malengo ya kuwa kwenye ofisi kubwa yenye kiyoyozi, ila hilo kwa saas awacha tuliweke pembeni. Pambana kwanza upate hela.

    Najua siyo kitu cha viwango vyako ila kwa kuwa ni halali kinaweza kukufikisha mbali.

    Ngoja sasa nikwambie siri ambayo hakuna mtu alikuwa amefikiria kukwambia. SIri yenyewe ni hii. vitu vidogo vina hela aisee! Shhhh! Usimwambie mtu.

    Mtu akiwa akiwa ananunua kitu cha shilingi mia moja kama kitumbua. Hajiulizi mara mbilimbili. Anatoa mia au mia mbili na wewe unampa kitumbua chako, na kuendelea mbele.

    Lakini ukiwa unauza kitu cha elfu kumi. Aisee, mtu atajihoji sana sana kabla ya kutoa hela yake. Ndiyo maana unaona hata matajiri wakubwa bado wanatengeneza vitu vya hela ndogo kama pipi na kiberiti.

    SOMA ZAIDI: Kama Unataka Mali: Maeneo Matano Unapoweza Kupata Mali Halali…

    Tuseme kwa mfano umeamua kuuza vitumbua vyako, unaweza kuungana na mwezako. Mkatengeneza ofisi yenu ya uongo na ukweli.

    Au kama huoni mwenzako wa kuungana naye, basi unaweza kuajiri kijana mmoja.

    Akawa anatengeneza vitumbua halafu wewe unasambaza. Tafuta basikeli hata ya kuazima. Zunguka mitaani, na kwa siku mnajiwekea lengo la kuuza vitumbua 300 mpaka 500. Hiyo ni sawa na elfu 30 mpaka 50 kila siku. Ukitoa gharama uliyoweka kwenye hivyo vitumbua hukosi cha kwako kila siku. Rafiki yangu, miaka mitano mpaka kumi ijayo, tutakuwa hatuongelei kijana wewe ambaye hukuwa na ajira, bali kijana wewe uliyetengeneza ajira za watu. hivi ndivyo watu waliofanya makubwa walivyoanza.

    Hivi kweli hata mtaji wa kuanzisha biashara ya karanga kweli utakosa?

    Hivi hata mtaji wa vitumbua utakosa kweli rafiki yangu? kweli..

    Kama hauna huo mtaji ila una simu kubwa ambayo unaitumia kusoma hii makala. Uza hata hiyo simu kwanza upate mtaji, kisha chapa kazi. siku za mbeleni utanunua simu nyingine.

    Nimeeleza zaidi kuhusiana na suala zima la mtaji kwenye kitabu changu cha NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA. Kiufupi hiki kitabu unapaswa ukipate na ukifanye kuwa mwongozo kwako, kwa sababu kimeeleza ni kwa namna gani unaweza kutumia nguvu ya vitu vidogo kwenye kila eneo la maisha yako. Na vile unaanzia chini kabisa, basi unahitaji hiki kitabu kama mwongozo wako wa kukusaidia kufanyia mpango kazi wako mpaka ukufikishe kileleni.

    Tano: Geuza kitu ulichosomea kuwa ajira

    Hivi kwa nini tunasoma? Hizi shahada za awali hizi ni za nini? Haoa naweza kuwa mtazamo tofauti na walio wengi. ila huu ndiyo mtazamo wangu na hiki kitu ndiyo mimi nasimamia. Mimi naamini kwamba, tunasoma ili tuje kutatua matatizo yaliyo kwenye jamii zetu. Tunasoma ili kuja kutengeneza ajira.

    Kwa hiyo kwa kitu ambacho umesoma, angalia ni kwa namna gani unaweza kukitumia hicho kitu kwenye jamii yako kusaidia watu.

    Umesomea sheria, je, hiyo inawasaidiaje watu waliokuzunguka.

    Wewe ni mtalaamu wa kilimo, watu waliokuzunguka wananufaika na utalaamu wako?

    Ni mtaalamu sijui wa IT, huo utalaamu wako unauletaje kwenye mazingira yetu ya huku mtaani. Kuna vitu unajua na unaweza kuwa unavichukulia poa, ila watu huku mtaani wanavihitaji sana.

    Umesomea masuala ya biashara, wasaidie watu kukuza biashara zao. Zile mbinu ulizojifunza chuoni onogea na watu wenye biashara ndogo huku mtaani ili wazitumie. Hawajui hata namna hata namna ya kutunza hesabu zao za kibiashara, kila siku wanasema kuna chuma ulete anachukua fedha zao. Wasaidie kwenye hilo.

    Wasaidie kuwafikia wateja. Wakiona mbinu zako hizo zinawasaidia baadaye ukisema kwamba wakulipe ili mfanye kazi zaidi, watakuwa tayari. Maana watajua unaenda kuwasaidia zaidi.

    Kijana msomi, ebu badilisha elimu yako kuwa ajira yako basi. Ebu wasidie watu waliokuzunguka kwanza, watu hao hao watakuwa tayari kukulipa, maana wewe ukiwapa mbinu za kuwainua hawawezi kukuacha.

    SOMA ZAIDI: Cha kufanya pale wenzako wanapokuzidi elimu, kipaji, ujuzi konekisheni n.k.

    Sita, Vijana tujitangaze

    Kama una ujuzi au una kitu chochote ambacho unajua kinaweza kusaidia watu , kitangaze watu wakijue. Kuwa na bidhaa nzuri bila kuitangaza kwa watu ni sawa na kujinongongeza mwenyewe kwa kumwambia binti kuwa nakupenda kwenye giza.

    Ukiwa na bidhaa,

    Saba; Vijana tushikane mkono

    Njia pekee ambayo tunaweza kusaidia vijana kuondokana na hili tatizo la ajir ni kuwashika mkono au kwa lugha ya mtaani kuwaungisha pale wanapokuwa na bidhaa au wnapoonesha juhudi za kufanya kitu fulani. Tusapoti juhudi za vijana wenzetu.

    Ni kweli mtu anaweza kuwa ameanza kwa kufanya kitu kwa udogo, ila tukizidi kumsapoti kitakua.

    Hapa naongea na ninyi nyote wenye tabia za kupenda vitu vya nje ya kudharau vitu vya ndani. Utasikia mtu anasema, aah, kitu chenyewe kimetengenezwa na mtanzania. Wabongo hakuna kitu chochote.

    Tukisapotiana sisi vijana tutafika mbali.

    Moja ya ndoto yangu kubwa ni kuona watu wakiacha kwenda China kutafuta bidhaa. Badala yake vitu hivyo wavipate hapa nchini. Mfano, badala ya mtu kwenda china kununua nguo, kwa nini vijana wa kitanzania tusitengeneze nguo na kuziuza hapa kwa bei sawa na ile ya china.

    Kuna vijana wengi wanashona nguo. Ila je, tunawasapoti.

    Tunataka wainuke.

    Jamani, tuwasapoti watu wanaofanya vitu.

    Mtu akianzisha mgahawa kanunue chakula kwake

    Mtu akilima mboga, nunua kwake.

    Mtu akiinua kipaji chake, kisapoti

    Tatizo la watu ni kwamba unaweza kuwa unapambana na bado wanataka wakija kwenye  biashara yako uwape vitu bure. Mtu umepambana na kupata mtaji wako na sasa umefungua duka,, wanataka wakija kwako uwape vitu bure tu. Wengine wanakopa na kulipa hawalipi. Hivi kweli, tutafika kwa namna hii?

    Vijana tusapotiane.

    Tena inabidi tuanze kusapotiana kwa vitendo kuanzia sasa hivi. Ebu shirikisha hii makala kwenye makundi mengine ya whatsap ili vijana wengi wasome ujumbe huu. hakikisha kwamba hakuna kijana unayemjua ambaye hajasoma huu ujumbe.

    Subscribe kwenye channel yangu ya youtube pia.  Enhee, hapo naona sasa umeanza kunielewa kwenye dhana nzima ya kusapotiana.

    Nakaukaribisha pia upate vitabu vyangu vya NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA na JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO kila kitabu ni elfu ishirini (20,000). Ukituma 40,000/- tu unapata vitabu vyote viwili na nikakusafirishia bure.

    Karibu sana

    umekuwa nami Godius Rweyongeza

    Kupata makala zaidi kutoka kwangu weka mawasiliano yako hapa chini ili uendelee kujifunza zaidi kutoka kwangu kila siku. Jaza taarifa zako hapa

    Kwa mawasiliano na mimi tafadhali usisite kutuma ujumbe kwa Email: songambele.smb@gmail.com

    Whatsap +255755848391

    For Booking: songambele.smb@gmail.com

  • Karibu kwenye semina ya uwekezaji kwenye Hisa

    Habari ya leo rafiki yangu. bila shaka unaendelea vyema kabisa. karibu kwenye semina ya uwekezaji kwenye hisa. Hii ni semina ya kipekee sana ambayo itaendeshwa kwa njia ya mtandao kuanzia tarehe 1 Agosti 2022. Katika semina hii ya kipekee unaenda kujifunza kila kitu unachohitaji kujua kuhusu uwekezaji wa hisa.

    Semina hii ya kipekee itadumu kwa siku 10 mfululizo na itaendeshwa kwa njia ya mtandao. Kwa siku hizi 10 utapata mafunzo ambayo yatatolewa kwa njia ya maandishi, sauti na video.

    Kwenye semina hii unaenda kujifunza kila kitu unachohitaji kujua kuhusu uwekezaji wa hisa na kikubwa zaidi ni kwamba utapata nakala moja (hardcopy) ya kitabu cha MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE

    Gharama za semina hii ni 21,000 tu. Namba ya malipo ya semina ni 0684408755

    Jiwekee nafasi yako kwa kulipia leo.

    Ni Mimi
    Godius Rweyongeza
    0755848391
    Morogoro-Tz

  • Aina Tano (05) Za Ujuzi Unazohitaji Ili Kuwa Milionea Kwenye Ulimwengu Wa Leo

    Kwenye makala niliyotuma kwa watu wa nguvu ambao huwa wanapokea makala zangu kwa njia ya email jana. Niliandika kwamba zama zimebadilika na wewe unapaswa kubadilika. Kama hujajiunga na mfumo wetu wa kupokea makala kwa njia ya barua pepe nina hakika huo ujumbe hukuuona,  hivyo, leo nimelazimika kuuweka huo ujumbe kwenye blogu yetu hapa ili na wewe uweze kuuona na kikubwa zaidi ni kwamba uweze kunufaika nao. Hivyo unaweza kuusoma kwa kubonyeza hapa rafiki yangu.

    Sasa baada ya jana kukwambia kwamba zama zimebadilika, basi leo nataka nikwambie aina saba za ujuzi unaopaswa kuwa ili uweze kutoboa kwenye ulimwengu wa leo ambao umebadilika sana.

    SOMA ZAIDI: Vitu Viwili Ambavyo Havitapitwa na wakati kwenye zama hizi

    Unashangaa ee!

    Usishangae! Unapaswa kuzoea kitu hiki, kwa sababu ulimwengu wa leo umebadilika sana. Kwenye uliwengu wa leo umilionea ni neno ambalo unapaswa kulitumia sana, na hata wewe unapaswa kupambana sana kuhakikisha kwamba unaufikia walau umilionea kama siyo ubilionea.

    Sasa ujuzi huu ndiyo utakufanya wewe utobe.

    1. Ujuzi wa kuongea mbele ya watu wa  kuwasilisha mada au kitu unachofikiria

    kuna watu wengi wana vitu vizuri sana ndani yao. ila vitu wanashindwa kuvifikisha kwa watu kutokana na kukosa ujuzi sahihi wa kuwasilisha kile walichonacho. Naomba unisikilize mimi kwenye hili. Kwenye uliwengu wa leo unahitaji sana ujuzi wa kuongea mbele ya watu.

    Hata kama umeajiriwa. huu ujuzi ni muhimu kwako, maana ujuzi huu pekee tu unaweza kukufikisha kwenye umilionea. Dunia ya leo bado inawapenda sana watu ambao wanaweza kusimama mbele ya watu na kuwasilisha mada kwa namna ambayo inaeleweka.

    Naamini, wewe ni kama mimi huwa hupendi mtu anayesimama mbele ya watu kuongea na kuanza kumung’unya maneno. Au mtu anayesimama na kuwasilisha mada kama vile anaogopa dunia itammeza.

    Huwa siwapendi watu wa aina hii. Ila ukifuatilia wengi ambao huwa wanaoongea mbele ya watu, huwa wanaongea kwa namna ya kipumbavu kama hii.

    Rafiki yangu, unahitaji kujitofautisha. Kuanzia leo hii anza kujenga ujuzi wa kusimama mbele ya watu na kuongea. Uongee na watu wawe na shauku ya kukusikiliza wewe ukiongea. Siyo unaongea mpaka unaboa watu wanaanza kutafuta simu zao ziko wapi ili wachati.

    huu ni ujuzi ambao haufundishwi shuleni, ila ni ujuzi ambao unahitaji kujifunza ili uweze kula mema yanchi. Nakwambia rafiki yangu, kamwe, usije ukafanya kosa la kuishi bila ya huu ujuzi.

    anza leo kujifunza ujuzi huu baada ya kusoma hapa. Kuna kozi kibao mtandao ambazo unaweza kusoma na zikakusaidia kupata ujuzi huu. Ukweli ni kwambaa kama kuna ukomo ambao utakuzia, basi utakuwa ni ukomo ambao umejiwekea mwenyewe.

    2. ujuzi wa kuanzisha na kusimamia na kukuza biashara

    Huu ni ujuzi ambao unauhitaji rafiki yangu. kwenye ulimwengu wa leo kuwa na biashara ni moja ya hitaji la muhimu sana.

    Najua unaweza kuwa unasema kwamba ajira peke yake inanitosheleza.

    Ninachotaka kukwambia ni kwamba kama unataka kufikia kiwango cha  kuwa na fedha ambacho kitakupa uhuru. Basi kuwa na biashara ni lazima.

    Ni kweli ajira inakupa kipato. Ila nina  uhakika kipato chako hakiwezi kuwa kikubwa sana kiasi cha kukufanya uweze kufurahia mambo mengine matamu yaliyo kwenye hii dunia.

    Lakini pia kipato cha ajira pekee, nina hakika hakitoshi kukufanya wewe uweze kuwekeza na kufanya mambo mengine ya kipekee.

    Kwa Tanzania, asilimia kubwa ya wafanyakazi wanalipwa chini ya milioni moja kwa mwezi. Hiki kiasi kinaweza kukutosha tu kula, kunywa na kufanya mambo mengine ya kawaida. Ila hakiwezi kukutosha wewe kufanyia kazi ndoto zako mpaka kuweza kuzifikia. Na hapa ndiyo maana, unahitaji kuwa na biashara

    Ubora wa biashara ni kwamba inaweza kukupa kipato kisicho kuwa na kikomo.

    Kadiri utakavyoweka juhudi kubwa kwenye biashara yako ndivyo ambavyo utaweza kuongeza kipato chako zaidi.

    Kwa hiyo nakushauri rafiki yangu uweze kuanzisha biashara. Hata kama ni kijibiashara kidogo, anza na hicho.

    Kama umeajiriwa, tumia muda wako wa ziada baada ya kutoka kazini au kabla ya kwenda kazini kwa ajili ya kufanyia kazi biashara yako.

    Rafiki, usiridhike na hayo maisha. Maisha yanabadilika kila kukicha. Hivyo, kwa vyovyote vile, pambana kuhakikisha kwamba unaanzisha hata kijibiasahra kidogo ambacho kitakupa kipato bila ukomo.

    SOMA ZAIDI:

    Tatu jifunze ujuzi ambao unaweza kukuingizia kipato cha milioni moja na zaidi

    Kama nilivyoandika kwenye makala ya jana. Kuna aina fulani za ujuzi kwenye ulimwengu wa leo ambao ukiwa nao, unaweza kukuingizia kipato cha milioni  moja na zaidi. na hii syo kwa mwezi, siyo kila baada ya siku mbili au tatu. Bali ni kwa siku moja. aina hizi za ujuzi zipo rafiki yangu, chagua aina walau moja ya ujuzi wa aina hii kisha anza kuujenga.

    Kabla sijakupa mifano ya aina  hii ya ujuzi nataka wewe mwenyewe uweze kutafakari kuhusu watu ambao unawafuatilia sana kwenye mitandao ya kijamii.

    Hivi watu wa aina hii ni wapi? Wana kitu gani ambacho kinakufanya uwafuatilie. Ukifuatilia kwa umakini utagundua kuwa baadhi ya hawa watu wana huo ujuzi ndio maana hata wewe unawafuatilia. Inawezekana ni ujuzi wa kuongea mbele ya watu na kuwasilisha mada zao kwa ustadi wa hali ya juu sana, inawezekana ni ujuzi wa kuandika, inawezekana ni ujuzi wa kuuza, unaweza pia kuwa ni ujuzi kuunda timu sahihi ya watu, unaweza kuwa ni ujuzi wa kung’ang’ania kitu kimoja mpaka kieleweke au ujuzi wa kuburudisha.

    Kwa vyovyote vile ebu na wewe chagua ujuzi wako ambao unataka kuwa nao maishani. Kisha anza kuujenga.

    Tena unaweza kuwa aina mbli za ujuzi na kuziunganisha na kuwa kitu kimoja. Hiki kitu kitalaamu kinaitwa skill sexing au idea sexing. Unaweza kukisoma zaidi kwa kubonyeza hapa

    SOMA ZAIDI: Kitu kimoja ambacho watu hawajui kuhusu uwekezaji

    Nne, jifunze kusema hapana kadiri uwezavyo

    Huu ni ujuzi ambao unapaswa kuwa nao pia. Maana kama utafuata mbinu ambazo nimekueleza hapa, muda siyo mrefu wewe utakuwa ni mtu wa viwango vingine. muda siyo mrefu kila mtu atakuwa anahitaji muda wa kuwa na wewe.

    Sasa hapa, unahitaji kuwa bahili wa muda wako. Unakuwa bahiri siyo kwa ubaya bali kwa uzuri. Ili uweze kuwekeza muda wako kwenye kufanya kazi za maana kwako na kuachana na kazi ambazo hazikujengi wala kukuongezea kitu chochote.

    Kwa hiyo, kama unataka kuujenga umilionea, jifunze kusema hapana nyingi kwa vitu ambavyo siyo vya muhimu kwako na vitu mbavyo havikusogezi wewe kwenye kufanikisha lengo lako. Badala yake wekeza muda wako huo kwenye kufanyia kazi malengo na ndoto zako mpaka uweze kuzikifia.

    SOMA ZAIDI: Huyu Ni Mtu Ambaye Lazima Utamwambia Hapana

    Tano ujuzi wa kuwekeza

    Huu ni ujuzi mwingine ambao unauhitaji. Rafiki yangu unahitaji uwe na ujuzi wa kuwekeza ili uweze kutunza fedha zako unazopata kwa uzuri na kwa namna ambayo itakusaidia wewe kuendelea kukuza utajiri wako.

    Nimeandika zaidi kuhusu uwekezaji na hasa uwekezaji kwenye hisa kwenye kitabu cha maajabu ya kuwekeza kwenye hisa, hatifungani na vipande. Unaweza kukipata hicho kitabu kwa kufuata maelekezo haya hapa

    maelekezo ya kupata kitabu cha MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE haya hapa

    Au unaweza kuwasiliana moja kwa moja na +255 684 408 755 sasa.

    SOMA ZAIDI: 

    Najua kuwa ungependa kupata ushauri wa karibu zaidi moja moja kwa moja kutoka kwangu. Nitafute tuone ni lini nitakuwa na muda, ili nikupangie ratiba ya kuongea na wewe. Utalipia kiasi kidogo tu.

    Saa moja ni laki moja mazungumzo kwa njia ya mtandao.

    SAA MOJA NI LAKI MBILI NA NUSU MAZUNGUMZO YA ANA KWA ANA. Malipo yanafanyika kwanza, kisha unapewa tarehe (appointment) tutakapoweza kuongea

    Tumia namba ya simu +255 755 848 391 kuwasiliana nami.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza ambaye anaishi Morogoro nchini Tanzania.

    Unaweza kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza kupitia youtube channel yake hapa

    Kwa ushauri niandikie songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu ambavyo ameandika Godius Rweyongeza, wasiliana naye kwa +255 684 408 755 na orodha ya vitabu vyenyewe unaweza kuiona HAPA. Chagua unachopenda, kisha twanga,  +255 684 408 755

    Kujiunga na programu yetu ya uandishi. Wasiliana na +255 678 848 396

    For Consultation only: +255 755 848 391  au godiusrweyongeza1@gmail.com

  • ZAMA ZIMEBADILIKA: MAISHA YAMEBADILIKA PIA

    Leo kwenye status ya moja za rafiki yangu aliweka picha ikionesha jinsi bei za vyakula zilivyokuwa chini siku za nyuma. Unaweza kuona mwenyewe picha yenyewe hapa👇🏿👇🏿

    Ukiangalia hapo utagundua bei zilikuwa chini kweli!
    Maziwa yalikuwa shilingi 100. Bei ya maji ya kandoro kwa sasa 🙈! Sijui maji ya kandoro kipindi hicho yalikuwa yanauzwa shilingi ngapi🤔.

    Au basi..

    Kitu kikubwa ninachotaka kukwambia leo ni kwamba Zama Zimebadilika! Na bado zitazidi kubadilika.

    Wewe pia unapaswa kubadilika.

    Najua wengi wanapenda mabadiliko ila ambao wako tayari kuchukua hatua kupata hayo mabadiliko ni wachache sana, yaani, wachache mno.

    Kitu cha kufahamu ni kuwa mabadiliko kwenye maisha lazima yatatokea.
    Wewe unapaswa kuwa sehemu ya mabadiliko hayo.

    Na njia nzuri ya kufanya mabadiliko Ni kutumia nguvu ya vitu vidogo.

    Hii Ni falsafa kubwa ambayo nimeeleza kwenye kitabu changu cha NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA.

    …..njoo ujipatie nakala ya kitabu hiki. Nina hakika hutajutia maishani mwako.

    Uwekezaji wa kitabu hiki ni moja ya uwekezaji wa kipekee ambao unaweza kuufanya.

    Ukiitumia NGUVU hii ya VITU VIDOGO hakuna ambacho kitakushinda hapa duniani.

    Ebu chukua hatua leo. Upate nakala yako leo rafiki yangu.
    Nakala moja gharama take Ni 20,000/-

    Tuma fedha Sasa kwa 0755848391 jina ni GODIUS RWEYONGEZA

  • Hivi Ndivyo Tunaweza Kufanya Biashara Za Kitanzania Zikue Zaidi

    Kwa Dakika moja Tu Leo Nataka Nikwambie Ni Kwa Namna Gani Unaweza Kufanya Biashara ya Rafiki Yako Ikue Zaidi Na Zaidi Ya Ilivyokuwa Mwanzo.

    Njia hii ni kununua kwake. Hii ndio njia bora nay a kipekee sana. Maana kwa jinsi hiyo utamfanya mwenye biashara apate kipato cha kumwezesha kuikuza biashara yake

    Kwa hiyo badala ya kukaa kwenye kikjiwe na kupiga majungu. Badala ya kumakatisha tamaa mpambanaji, ebu sikiliza, nenda kanunue kwake. Hicho ni kitendo cha kiungwana ambacho unaweza kufanya na kufanya biashara ya rafiki yako ikue.

    Ifikie hatua watu tuache kuagiza bidhaa kutoka nje ya nchi. Tununue bidhaa kutokea hapahapa kwetu. Na njia ya kufanya hivi ni kumsapoti mwezako anayefanya kitu kizuri

    Ni hivyo tu.

    Kama umeilewa hii makala basi nenda kamsapoti mwenzako badala ya kupiga majungu.

  • Kitu Kimoja Cha Kufanya Unapokutana Na Watu

    Unaendeleaje rafiki yangu mpendwa. Siku ya leo ningependa tujadili kitu kimoja cha kufanya unapokutana na watu. Kitu hiki ni kubadili maisha yao na Kuyafanya kuwa bora zaidi kuliko ulivyowakuta.

    Yaani, kuwainua na kuwafanya wajisikie vizuri ZAIDI Kuliko pale walipokuwa hawajakutana na wewe.

    Hii Ni moja sifa ya viongozi na watu wote WALIOFANIKIWA.

    Kwa hiyo kila ukikutana na mtu, angalia ni kitu gani unaweza  kufanya kumwacha bora zaidi ya vile ulivyokuta mwanzoni?

    Kuwa sehemu ya kusambaza upendo,  na furaha. Kuwa mtu wa kuhamasisha watu. Kuwa mtu wa kuwaacha watu Bora ZAIDI ya vile ulivyokuta. Hivi ndivyo viongozi wote wakubwa wanavyofanya.

    Ukikutana nao unapata hamasa ya kwenda kufanya kazi kwa ubora ZAIDI.

    Siyo kwamba wanakukatisha tamaa.
    Siyo kwamba wanakufanya ujisikie wa chini Kuliko wao. Bali wanakuwa nyuma yako kuhakikisha kwamba wanakusuma uende mbele zaidi.

    Kila la kheri.

X