Home


  • Sababu 15 kwa nini haupaswi kuwa na plan B

    Kwenye uchaguzi wa mwaka 2015 kuikuwa na utani ambao ulikuwa unasambaa mtandaoni. Mmoja wa watu alitengeneza meme fulani hivi ambayo ilikuwa ikimwongelea waziri mkuu mstaafu Edward Lowassa. Ilikuwa inasema kuwa kila mara unapaswa kuwa na Plan B kama Lowassa. Amekatwa CCM asigombee urais, amehamia CHADEMA, na sasa akishindwa kuingia ikulu kwa tiketi ya CHADEMA anahama nchi anaenda kugombea Senegal.

    Sina hakika sana kama nchi iliyokuwa inatajwa ilikuwa ni Senegal kweli, ila nina uhakika na kitu kimoja tu. kitu hiki ni kuwa baada ya uchaguzi wa mwaka 2015 hapa nchini Tanzania, kulikuwa na nchi nyingine hapa barani affrika iliyokuwa inategemea kufanya uchaguzi. Kwa hiyo, aliyetengeneza hiki kichekesho alikuwa akionesha kuwa endapo Lowassa atashindwa kuingia ikulu kwa tiketi ya CHADEMA basi angehama nchi, kwenda kugombea huko maana mara zote alikuwa na plan B.

    Ok ok, siku ya leo siko hapa kumwongelea Lowassa wala kuongelea siasa, ila nipo hapa kuongelea kitu kimoja tu. PLAN B. kumekuwe[o na maoni mengi sana ya watu wakisema kwamba unapaswa kuwa na plan B kwenye maisha yako.

    Tena watu wamekuwa wakisema hili kwa msisitizo mkubwa sana, kwamba endapo utashindwa kwenye plan A, yaani, ile plan ambayo unaifanyia kazi sasa hivi, basi utapaswa kuhamia kwenye plan B. Siku ya leo nipo hapa kukwambia kuwa haupaswi kuwa na PLAN B kwenye maisha yako na zifuatazo ni sababu 15 kwa nini haupaswi kuwa na PLAN B

    KWANZA, SIYO SALAMA KWA AFYA YAKO

    Wengi wanafikiri kuwa ukiwa na plan B, basi mpango fulani ukishindwa  utaachana nao na kuingia kwenye mpango mwingine. Hiki kitu ndicho kimewafanya watu wengi washindwe kuendelea kwenye maisha. Unakuta mtu ana mpango mzuri, ila sasa haufanyii kazi mpango wake kwa kujitoa kwa sababu ana mpango mwingine unaoelekeana na huo ambao anauita PLAN B.

    Tuchukulie mfano tu wa mtu ambaye amehitimu chuo na anatamani kuanzisha biashara. Unakuta mtu wa aina hii anashindwa kuanzisha biashara au hata akiianzisha hiyo biashara inashindwa kukua kwa sababu moja tu, mtu huyu muda wote anakuwa anafikiria kuwa nikizuga tu kwenye biashara na ikafeli naenda kutafuta kazi. Kwa hiyo, yeye muda wote anajua kuwa hata biashara isipofanya vizuri, yeye atakuwa na sehemu ya kuangikia ambayo ni ajira. Kitu hiki sasa hakiwezi kumfanya mtu ajisukume na kufanya makubwa zaidi. pale ambapo mtu anakuwa anajua kwamba kuna sehemu ya kuangukia basi, ujue wazi kuwa huyo mtu hatajisukuma kufanya makubwa.

    Kijana ambaye anajua wazi kuwa nyumbani kwao kuna kila kitu (wa kishua), hatajisukuma kufanya vitu na kupambana, badala yake atakuwa anjua kwamba hata asipofanya kitu chochote, pele nyumbani vitu si vipo tu.

    Wakati hali ni tofauti kwa kijana ambaye anakuwa anajua kwamba asipopambana basi siku hiyo hana ugali.

    Au yule anayekuwa anajua kuwa anapaswa kupambana kwa ajili ya wazazi wanaomtegemea yeye.

    Siku moja nilikuwa namsikiliza Les Brown kwenye mojawapo ya mazungumzo yake. Les Brown akawa amesema kwamba alikuwa anauza bidhaa nyumba kwa nyumba. Hivi unajua kweli mauzo ya nyumba kwa nyumba au unayasikia redioni tu.

    Mauzo ya nyumba kwa nyumba ni yale ambayo unakuwa unaenda unagonga nyumba moja baada ya nyingine na kuwaambia bidhaa uliyonayo, huku ukiwashawishi wanunue. Mfano, unachukua kitabu changu cha  NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA. Unaenda nacho nyumba kwa nyumba ukikiuza. Unagonga kila nyumba na kuwaambia kuwa hapa nina kitabu kizuri kinachoweza kukusaidia wewe kufanikisha lengo lolote kubwa kwa kuchukua hatua ndogondogo kila siku. Unatoa maelekezo kedekede, kisha unawaambia watu wakupe hela uwaachie kitabu.

    Sasa haya mauzo, yanahitaji moyo sana. Maana unapokuwa unagonga mlangoni mwa mtu, unakuwa huna uhakika kama huyo mtu anataka hiyo bidhaa au hataki. Unakuwa hujui kama huyo mtu atapenda kupata kitabu cha NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA au la hatataka,

    Hujui kama huyo mtu ana shida ya sabuni yako, au tayari anazo sabuni.

    Mauzo ya aina hii, kibongobongo wanafanya wachache sana, hata wale wanaozunguka mitaani na laini za simu hawajafikia hicho kiwango cha kugonga mlango mmoja baada ya mwingine. mara nyingi wanapita tu mtaani wanatembea.

    Sasa kwenye mauzo ya aina hii, kuna matatu ambayo unaweza kukutana nayo.

    • Mteja anaweza kukwambia, ndio nataka bidhaa. Tukitumia mfano wetu hapo juu, anaweza kusema anataka kupata kitabu cha NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA
    • Au anaweza kukwambia kwa sasa hapana, labda siku nyingine
    • Au anaweza kukwambia, hapana
    • Au anaweza kukwambia hapana pamoja na matusi juu yake.

    Sijui unanielewa. Sasa hakuna kitu kinakatisha tamaa kama majibu mawili ya mwisho, hasa unapokuwa unajijua una bidhaa nzuri ambayo ingeweza kumsaidia mteja kama ambavyo mimi nina kitabu cha NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA na ninajua sana kuwa kinaweza kukusaidia wewe. Rusha basi, elfu ishirini ili upate nakala yako (Hardcopy). Namba ya kurusha hela ni 0755848391 jina ni GODIUS RWEYONGEZA.

    Kitu hiki, huwa kinawafanya watu wachache sana wajihusihe na na mauzo haya. Ila sasa, ubora wa mauzo haya ni kwamba, kadiri unavyokutana na watu wengi zaidi, ndivyo unavyouza zaidi. Ukikutana na watu kumi. Saba au nane watakataa, ila watatu au wawili watanunua. Kwa hiyo, unakataliwa sana ila pia unauza zaidi. Sasa Les Brown alisema kwamba, yeye alikuwa analazimika kuendelea na mauzo haya kwa sababu tu hakuwa na njia nyingine ya ziada kwenye maisha yake ya kupata kipato isipokuwa hiyo.

    Anasema kuna rafiki yake walianza pamoja hii kazi ila aliishia njiani,kwa sababu alikuwa na plan B. ila yeye hakuwa na plan nyingine yoyote ile isipokuwa kuhakikisha kwamba ameuza, maana la sivyo, mama yake asingeweza kupata chakula siku hiyo.

    PILI WATU WALIOFANIKIWA SIYO WALE WENYE PLAN B

    Watu wengi walioweza kufanikiwa kwenye maisha siyo wale waliofanya jambo fulani wakiwa na plan B kwenye kichwa chao, bali wale waliofanya lile jambo kwa moyo wote wakiwa wanajua kuwa ni au walifanye hilo jambo na kulifanikisha au la wafe wakiwa wanapambia hilo jambo.

    Siku moja nilikuwa nasikiliza hotuba ya Arnold Schwaznegger. Kwenye hiyo hotuba Arnold alisema kuwa yeye kwenye maisha hapendi kuwa nap la B.

    Mimi mwenyewe sipendi kabisa kuwa na plan B. kwa vyovyote vile, kwenye maisha watu wenye plan B huwa hawafanikiwi.,waliofanikiwa kwenye maisha ni wale ambao walikuwa na plan moja tu, wale walioweka nguvu na muda wao wote kwenye kitu kimoja na wakakifanya bila kurudi nyuma.

    TATU, UKIKWAMA UNARUDI NYUMA

    Unapokuwa na plan B. ukikutana na kikwazo kidogo tu, hapohapo unarudi nyuma. Maana unajua kuwa utaenda kuegemea sehemu fulani. Ila pale unapokuwa unajua kuwa ni lazima nifanye hiki kitu, au la nitakufa nikiwa napambia hiki kitu, basi utapambana kwa nguvu zako zote kuhakikisha kuwa kile kitu unakifanyia kazi bila ya kurudi nyuma.

    Moja ya kitu ambacho watu wengi wamekuwa hawafahamu ni kuwa vikwazo kwenye maisha lazima tu vitokee. Yaani, hakuna namna yoyote ile kwenye maisha unaweza kuishi bila ya kuwa vikwazo. Vikwazo vinatokea kwenye maisha, sasa utakuwa na plan B ngapi?

    Ndio maaana kwenye ndoa unaambiwa ukishakuwa na mwenza wako unakuwa naye milele. Kwa sababu wanajua kuwa kwenye ndoa kuna vikwazo vingi, sasa ebu fikiria kila mtu akiingia kwenye ndoa na plan B. Huyo mtu ataoa au ataolewa na wanagapi? Maana kila atakapokutana na kikwazo tu, maana yake ataachana na mwenza wake na kwenda kuolewa na mtu mwingine ambaye anadhani hana changamoto. Na mwenyewe akiwa na changamoto anaachana naye tena. Ndio maana unaambiwa uishi na mwenza wako kwenye shida na raha (NO PLAN B)

    Kwa hiyo, kama ilivyo kwenye ndoa, vivyo hivyo kwenye maisha. Uanapaswa kuchagua kitu kimoja na kuamua kukomaa na hicho kitu bila ya kurudi nyuma hata kama unakutana na changamoto kiasi gani.

    Ubora changamoto na vikwazo ambavyo unakutana navyo kwenye maisha, siyo kwambna ni vikwazo, badala yake kila unapokutana na changamoto au vikwazo kwenye maisha, maana yake unapata somo kutoka kwenye hivyo vikwazo na hizo changamoto, kitu ambacho kinakufanya uweze kuwa imara kwa siku ambazo zinazofuata.

    Ebu chukulia mfano wa kawaida tu,

    Ebu tuchukulie kwa mfano umeanzisha biashara, halafu kadiri unavyoenda unakutana na changamoto ya kutoona hela kwenye biashara yako. Mwanzoni unaanza kufikiri kuwa labda hawa watakuwa ni chuma ulete. Lakini kadiri unavyoendelea kufuatilia zaidi, unagundua kuwa siyo chuma ulete, ila tatizo liko kwako. unagundua kuwa tatizo umekuwa unachukua hela ya biashara na kuifanya kuwa hela yako.

    Yaani, umekuwa hutenganishi kati ya hela yako na hela ya biashara. Hivyo, unaamua kuwa kuanzis sasa utaanza kutengenisha kati ya hela yako na hela ya biashara. Unaamua wazi kuwa kamwe kwenye maisha yako, hutachukua hela ya biashara uitumie kma ya kwako. Badala yake utakuwa unajilipa wewe mshahara kama mfanyakazi kwenye biasahara yako na kiasi kingine utakuwa unakiacha kwenye biashara. Lakini unaenda mbali zaidi kwa kuhakikisha kwamba unatunza kumbukumbu za hela zote zinazoingia na kutoka kwenye biashara. Rafiki yangu, hiki kitu kidogo tu, kina nguvu kubwa sana. kubwa mno, nakwambia.

    Baada ya muda ni wazi kuwa utaanza kuona matokeo ya tofauti, na matokeo ya tofauti maana yake wewe umeshatatua changamoto au kikwazo kilichokuwa kinakurudisha nyuma na sasa unaendelea mbele. Siku nyingine ukikutana na changamoto au kikwazo kingine ni wazi kuwa hutarudi nyuma, badala yake utaendelea mbele zaidi.

    Mfano siku nyingine ukikutana na kikwazo cha mauzo kidogo, suluhisho la kikwazo hiki siyo kuacha kufanya ile biashara unayofanya na kukimbilia kufanyia kazi plan B. Badala yake suluhisho lake ni wewe kutafuta wateja zaidi. na ili kupata wateja zaidi maana yake unapaswa kujifunza mbinu mpya za mauzo na masoko. Kumbe ukiwa na plan B, maana yake unakosa akili ya kujiongeza na kufanya makubwa zaidi, ila ukiwa na plan hiyohiyo na ukakomaa nayo, unakuwa na akili ya ziada.

    Kabla sijamalizia hii pointi ningependa nitoa kwa ufupi sana hadithi ya Heran Cortes. Huyu jamaa alienda na jeshi dogo kupigana vita na jeshi kubwa. Walienda na boti na baada ya kuwa wameshuka salama kwenye boti, aliamuru boti zote zichomwe moto.

    Kitu hiki kilituma ujumbe kwa wanajeshi wake kuwa hakuna plan B. Maana yake, walipaswa kushinda hiyo vita, au la walipaswa kufia hapohapo.

    Sasa hiki kitu kina maana gani kwako, maana tumeshatoka kwenye hizo zama za kivita, ila kitu kimoja cha uhakika tunachojifunza kutoka hii stori fupi ni kutokuwa na plan B kwenye maisha. Plan B,  inakwamisha. Plan B inakufanya uwe na sehemu ya kuegemea na hivyo, unashindwa kutimiza wajibu wako kwa viwango vikubwa.  Niendelee au niishie hapa!

    Ebu basi subscribe kwenye channel yangu ya youtube kwanza halafu tuendelee. BONYEZA HAPA kufanya hivyo.

    NNE; HAUFIKIRII INJE YA BOKSI

    Siku za karibuni nimekuwa naongea na rafiki yangu mmoja ambaye huwa anafuatilia mafunzo yangu kwa njia ya mtandao. Anafanya kazi ya ubodaboda,ila anaonekana kama ameikatia tamaa. Maana ni kama haoni matokeo kwenye kile anachofanya na hata malipo yake anaona siyo makubwa sana. wiki iliyopita, nilimpa mbinu kadha wa kadha za kumsaidia kuongeza wateja zaidi na hivyo kulipwa zaidi.

    Sasa jana wakati naongea naye akaniambia ameanza kuona matokeo. Nikawa nimemwambia kuwa asifanye hicho kitu mara moja tu, badala yake awe na mwendelezo. Kwa siku ya jana nikamwambia kitu kimoja tu, nikawambia nenda ukannunue mfuko wa pipi. Halafu kwa kila abiria unayesafiri naye hakikisha kwamba unampa pipi ili aende anakula. Hiki kitu kilimshangaza kidogo ila alikifurahia sana.

    Akaanza kuniambia habari za basi ambazo huwa zinatoa pipi, biskuti na soda. Akaniambia kuna mwalimu wake alisafiri na basi wakampa pipi, soda na biskuti na tangu siku hiyo mwalimu huyo akawa ameapa kuwa atasafiri na basi hiyo hiyo siku zote ili apate soda, biskuti na pipi.

    Nikawa nimemwambia kuwa unapokuwa umesafiri na basi, unalipia nauli karibia elfu hamsini, sitini au sabini. Kwenye hiyo nauli yako, wenyewe wanatoa elfu mbili tu, wanakununulia wewe pipi mbili, soda moja na biskuti. Unapewa na huwasahau, sasa hiki kitu unaweza kukitumia. Ukimpa mtu pipi ya shilingi mia moja kutoka kwenye elfu mbli ya usafiri wako wa bodaboda unakuwa hujapunguza kitu kikubwa. ila unakuwa umejenga mteja wako wa nguvu maana siku nyingine yule mtu akitaka usafiri, hataanza kumtafuta bodaboda mwingne, badala yake atakutafuta wewe ili apate pipi ya kulamba njiani, wakati unamsafirisha. Daah, halafu darasa la kulipia kabia mimi nakupa bure hapa, hahaha.

    Kama nakuona na wewe unavyoenda kuitumia hii mbinu niliyompa jamaa jana. Hahaha

    Ila kitu kikubwa ninachotaka kumwambia ni kuwa mawazo ya kuboresha biashara au kitu chohote kile hayatoki kwa watu ambao wana plan B. mtu mwenye plan B akifeli anawaza kwenda kwenye kilimo, kwenye kilimo akilima tikiti zikamwangusha anawaza kwenda kwenye madini, kwenye madini akikutana na changamoto anawaza kwenda bandarini maana anasikia habari za watu wanaopata mabilioni. Akiwa hajatulia bandarini anasikia habari za watu wanaouza mbao Iringa anaenda Iringa. Akiika tu iringa, habari za kilimo cha mpunga Ifakara zinamfikia anahamia ifakara, sikiliza rafiki yangu, huwezi kutoboa kwenye maisha ukiwa na plan nyinginyingi hivyo. Kuwa na plan moja kisha komaa na hiyo.

    Ubora ni kuwa kadiri siku zinavyokuwa zinaendelea kusogea mbelea wewe mwenyewe unakuwa unazidi kuimarika na kuwa bora zaidi.

    Kabla sijaendelea mbele zaidi, naomba ufanye kitu kimoja. Weka barua pepe yako hapa chini,ili uwe unapokea mafunzo zaidi kutoka kwangu kwa njia ya baruapepe.  Fanya hivyo sasa hivi ili tuendelee

    TANO; PLAN B  INAKUKWAMISHA KUFANIKISHA PLAN YAKO KUU

    Ule muda unaouweka kwenye kufikiria plan B. Ule muda unaoutumia kufanyia kazi plan B, ni muda ambao unaupoteza, badala yake muda huu wote ungeweza kuuweka kwenye jambo lako kuu na kulifanyia kazi mpaka likafikia viwango vikubwa.

    Ujue unapokuwa na mambo mengi ambayo unafikiria kufanya, unakuwa hauweki akili yako na nguvu zako sehemu moja, ila unapokuwa na jambo moja na unapokoma na huilo jambo maana yake hata ukikutana na kikwazo au kitu chochote kile cha kukukwamisha, maana yake utapambana  kuhakikisha kwamba unalifanyia kazi jambo husika mpaka uweze kulifanikisha.

    SI TA; TAFITI ZINAONESHA KUWA PLAN B ni chanzo cha KUTOKUFANYA VIZURI

    Wanasayansi katika chuo kikuu cha Wharton na chuo Wisconsin walifanya utafiti kwa watu ambao waliwagawa kwenye makundi mawili. Kundi la kwanza lilikuwa la watu ambao walikuwa waliambiwa wafanye jambo fulani. Na kundi la pili liliambiwa lifanye jambo fulani, ila kwanza lilipaswa kufikiria endapo mambo hayataenda kulingana na matarajio yao itakuwaje. Kwa lugha nyingine ni sawa na kusema kwamba kundi la pili lilitakuwa kuwa na plan B.

    Mwisho wa siku majibu ya utafiti huo yalioonesha kuwa waliokuwa na plan B hawakufaya vizuri ukilinganisha na wale waliokuwa na plan moja tu.

    Mimi sina cha kuongeza, maana utafiti umeongea na umemaliza.

    Hivi nilisema kuna sababu 15 ee kwa nini haupaswi kuwa na plan B. Na bado unataka niendelee au niishie hapa! kama umependa makala hii, utapenda pia kitabu changu kipya cha JINSI YA KUONGEZA THAMANI YAKO. Weka oda leo upate punguzo la kitabu hiki, soft copy itaanza kupatikana tarehe 10.10.2022. Na gharama ya softcopy ni 10,000/- ila ukilipia kabla ya tarehe 10, utaipata kwa elfu saba tu. Kwenye hiki kitabu nimejadili kwa kina mada hii ya plan B. Nina uhakika utaipenda tu. na sababu zilizobaki nimezimalizia kwenye kitabu.

    Umekuwa nami GODIUS RWEYONGEZA

    Asante sana kwa kusoma makala hii. hakikisha unajaza taarifa zako hapo chini ili uwe miongoni mwa watu ambao wataku wanapokea makala zangu kwa njia ya baruapepe. Huwa naandika makala nyingine zaidi na kuzituma kwa njia ya baruapepe. Ningependa na wewe uzipokee hizi makala, jaza taarifa zako hapa chini ili uzipate.

  • Viashiria 15 kuwa kipaji chako kitakufikisha mbali

    KIPAJI NI DHAHABU
    Rafiki yangu, nimeandika kitabu. Kinaitwa KIPAJI NI DHAHABU. Ili kupata kitabu hiki, wasialiana na mi kwa 0755848391 sasa

    Rafiki yangu mpendwa karibu sana kwenye makala ya siku ya leo. Na leo tunaenda kuona viashiria 15 vinayoonesha kuwa kweli hiki kipaji chako ulichonacho kinaenda kukufikisha mbali.

    1. upo tayari kuanza kidogo

    Kama upo tayari kuanza kidogo kisha kuendelea kukifanyia kazi kipaji chako ili kuhakikisha kwamba unakikuza na kukifikisha juu zaidi, basi hiki ni kiashiria tosha kuwa kipaji chako siku moja kitakufikisha mbali sana.

    2. Unafanya mazoezi mara kwa mara

    Bila kujali kuwa una kipaji kikubwa kiasi gani, mazoezi ni lazima ili uweze kukisukuma kipaji chako juu zaidi. kwa hiyo, kama una kipaji na unafanya mazoezi ya kipaji chako. Siyo mara moja na wala siyo mara mbili, bali kila siku. Basi ujue kuwa hiki kipaji chako kinaenda kukufikisha mbali kwelikweli.

    3. Unapenda kujifunza

    Kuna maarifa mengi yamejicficha kwenye vitabu. mtu ambaye hajifunzi na kupata maarifa mapya, ni mzee hata kama ana miaka 21 na mtu ambaye anajifunza na kupata maarifa, ni kijana hata kama ana miaka 75. Sasa wewe ni mzee au kijana? Kama wewe ni kijana, basi hiki ni kiashiria tosha kuwa unaenda kufanikiwa kwa viwango vikubwa

    4. Kufanya mambo ya msingi na kuachana nay ale ambayo siyo ya msingi’

    Ujue ndani ya siku kuna mambo  mengi ambayo unaweza kufanya, unaweza kuutumia muda kwenye kuchati, unaweza kuutumia muda wako kupiga soga na marafiki, unaweza kuutumia muda wako kwenye kuperuzi na mengineyo mengi. Ila kama kwa vyovyote vile unatoa muda wako na kuuwekeza kwenye kipaji chako na kufanya majukumu ambayo ni ya msingi kwako, hiki ni kiashiria tosha kwamba kwa vyovyote vile rafiki yangu, unaenda kufanikiwa kwenye kipaji chako na kipaji chako kitakufikisha mbali.

    Hivyo rafiki yangu, endelea kupambana na kufanya mambo ya msingi huku ukiachana na yale ambayo siyo ya muhimu.

    5. Kujihusisha na marafiki na watu chanya

    CHUMA KINANOA CHUMA. Huu ni usemi ambao huwa napenda kuusema na kuusisitiza, ningependa na wewe uufahamu pia, kuwa chuma, kinanoa choma. Hivyo, wale watu ambao unakuwa unatumia muda mwingi ukiwa nao, ni wazi kuwa wewe unaenda kuchukua tabia zao. Kama muda wako mwingi unautumia ukiwa na watu ambao wananoa vipaji vyao na kuvifanyia kazi, hicho ni kiashiria kingine kuwa wewe unaenda kufanya makubwa na kipaji chako.

    Nikiwa kwenye maonesho ya nanane na vitabu vyangu (2022)

    6. Una malengo na unayafanyia kazi

    Kama una malengo na hayo malengo unayafanyia kazi. labda ni malengo ya kufanya mazoezi, au malengo ya kujifunza, basi hiki ni kiashiria tosha kwamba unaenda kufanikiwa kwa viwango vikubwa sana. sasa swali langu kwako siku ya leo ni je, un malengo. Na je, hayo malengo unayafanyia kazi?

    7. Ukianguka unainuka

    Watu wengi huwa wanaanza vitu, pale wanapokutana na changamoto basi wanaachana na kile wanachofanya na hivyo kuendelea na maisha yao kama kawaida. Sikiliza rafiki yangu, changamoto ni moja ya kitu ambacho unahitaji kukifanyia kazi kwenye maisha yako. Changamoto hazijawahi kukosa kwenye maisha. Unapaswa kuzifanyia kazi, na kila unapoanguka, basi usisite kuinuka maana kuanguka ni sehemu ya maisha.

    8. Unapenda kujichangamotisha

    Ujue sisi binadamu hatupendi kufanya vitu vya tofauti. Mara zote huwa tunapenda kufanya vitu vilevile kwa namna ileile bila ya usumbufu wowote ule. Sasa kama unapeda kujichangamotisha na muda mwingine kuchukua hatua ambazo siku za nyuma ulikuwa hujawahi kuchukua, basi ukae ukijua kuwa hiki ni kiashiria tosha kuwa utafanikiwa sana na hicho kipaji chako.

    9. Upo tayari kwenda hatua ya ziada

    Wengi kwenye maisha wanapenda mabadiliko, ila hakuna ambaye yuko tayari kwenda hata hatua moja ya ziada ili kutengeneza hayo mabadiliko. Ila kama wewe unaenda hatua ya ziada na kufanya zaidi vile unavyopaswa kufanya, basi hiki ni kiashiria tosha kuwa unaenda kufanikiwa sana kwenye kile unachofanya.

    10.Unajiongoza

    Kuna watu wengi sana kama hawajielewi vile, ni mpaka awepo mtu wa kuwaongoza na kuwaonesha kitu gani cha kufanya, ndipo na wao wanaweza kufanya kitu. Kama hakuna mtu wa kuonesha au kuwaongoza kufanya hicho kitu, basi utakuta kwamba wale wanabweteka.

    Sasa kama unaweza kujiongoza kwenye majukumu yako na kuyafanya bila hata kuhitaji usimamizi, basi ujue wazi kuwa unaenda kufika mbali  sana na hicho kipaji chako.

    11. Unajikubali

    Kama hujikubal, basi hakuna mtu ambaye atakukubali. Rahisi tu kama hivyo.

    12. Unajali sana muda

    Muda ni mali. Hili wala hata halina ubishi, kama unatumia muda wako vizuri kwenye kunoa na kuendeleza kipaji chako badala ya kufanya mambo mengine ambayo hayana manufaa, basi hiki ni kiashiria iosha kuwa unaenda kufanikiwa sana na kipaji chako na utafika mbali.

    Rafiki yangu naomba utambue kwamba kwa siku tuna saa 24 tu. Sasa hizi saa unapaswa kuhakikisha kwamba umezitumia vizuri na kwa manufaa yako, kama wewe unautumia muda wako vizuri, basi hongera sana. Ila kama hautumii muda wako vizuri, basi jihoji mara mbilimbili ili kuanzia leo hii uanze kuutumia muda wako kwa manufaa na kwenye malengo na ndoto zako ambazo unafanyia kazi

    13. Una kocha

    Kama una kocha wa kukusimamia na kukufuatilia kwenye kile unachofanya, basi hiki ni kishiria kingine kuwa unaenda kutoboa. Asilimia kubwa ya watu wenye vipaji huwa wanakwama kwa sababu hawana msimamizi wa kuwafutilia kwa ukaribu, kitu ambacho huwa kinawafawanya wafanye vitu kwa motisha kwa siku chache na  baadaye kupoteza hiyo motisha. Ila unapokuwa na motisha na mtu wa kukusimamia nyuma yako, maana yake hata ukukikutana nchangamoto au kitu chochote, bado utajisukuma na kusongambele ili uweze kufikia malengo na ndoto zako.

    14. Unapata muda wa kupumzika

    Ni kweli kuwa unapaswa kupambana kwa ajili lya kuhakikisha unafanyia kazi kipaji, malengo na ndoto zako ili uweze kufikia malengo makubwa sana kwenye maisha. Ila pia unapawa kuwa na muda wa kupumzika ili usije ukafanya kazi kupitiliza mpaka ukapata burnout.

    Hiki ni kitu cha msingi ambacho huwa wanakifanyia kazi watu wanaofanikiwa na vipaji vyao, na wewe ukikifanyia kazi, basi hii itakuwa ishara tosha kuwa wewe unaenda kufanikiwa na kipaji chako.

    Unaweza kufanya kazi saa 18 kila siku jumatatu mpaka jumamosi, na jumapili ukapumzika na kupata muda wa kutosha wa kupumzika.

    15. unajali sana mahusiano yako

    Kama unajali sana mahusiano yako, mahusiano ya mwenza wako na familia yako. Basi ujue kwamba unaenda kufika mbali. Mwenza wako ni kiungo muhimu sana, kama mko sawa kwenye safari yenu ya mafanikio mtafika haraka, ila kama mnakinzana ni vigumu sana kufika.

    Sasa kuanzia leo hii, hakikisha kwamba mahusiano yako na mwenza wako unayatunza vizuri ili yaweze kukaa kwa usawa.

    Tofauti na hapo mimi nakutakia kila la kheri.

    Umekuwa name,

    Godius Rweyongeza

    0755848391

    Morogoro-Tz

  • Vitu 21 Ambavyo Ni Lazima Kufanya Hata Kama Una Kipaji Kikubwa

    KIPAJI NI DHAHABU
    Rafiki yangu, nimeandika kitabu. Kinaitwa KIPAJI NI DHAHABU. Ili kupata kitabu hiki, wasialiana na mi kwa 0755848391 sasa

    Rafiki, una kipaji si ndio! Hongera sana, mbali na kuwa una kipaji na unakifanyia kazi na una maono makubwa ya kukipeleka mbali kipaji chako mpaka kwenye ngazi za kimataifa. Ila kuna vitu vya msingi sana ambavyo hupaswi kuacha kufanya hata kama una kipaji kikubwa. kwenye hii sura ninaenenda kukushirikisha vitu 21 ambavyo hupaswi kuacha kufanya hata kama una kipaji kikubwa

    1. Unapaswa kuweka akiba.

    Rafiki yangu, bila kujali una kipaji kikubwa kiasi gani, haupaswi kuacha kuweka akiba. Mara zote hakikisha kwamba unaweka akiba kutokana na kiasi cha fedha ambacho unapokea. Hata kama ni kidogo kiasi gani. hakikisha kwamba mara zote unatoa kiasi kidogo na unakiweka kama akiba. Moja ya shida ambayo huwa inawakumba watu wenye vipaji wanapofikia umri wa kustaafu ni kuwa wanakuwa hawana akiba wala hela ambayo wanaweza kutumia. Yaani, mtu amekuwa anapambana kwa miaka mingi, ila sasa unapofika wakati kula matunda ya jasho lake, anakuwa hana matunda ya kula. Rafiki yangu, nataka wewe ujiondoe kwenye huu mtego kwa kuhakikisha kwamba unaweka akiba na kuwekeza. Na kiwango cha kuweka akiba siyo kikubwa sana, ni aslimia kumi tu ya kila kiasi ambacho kinaingia kwenye mfuko wako. Rafiki yangu, hiki ni kitu ambacho unapaswa kukipambania kila mara.

    Ila kwa hapa ningependa kukueleza mambo yafuatayo kuhusu uwekaji wa akiba

    Kwanza, leo hii nenda kafungue akaunti benki ambayo utakuwa unaweka akiba yako. Utafiti unaonesha kuwa watu wenye akaunti za benki, wanakuwa na utaratibu wa kujiwekea akiba, ukilinganisha na wale ambao hawana akaunti za benki.

    Anza kuweka akiba yako, hata kama ni kidogo. Ubora benki wanaruhusu kuweka kiasi cha chini ambacho ni elfu moja. hivyo, kila ukipata kiasi fulani cha fedha rafiki yangu, hakikisha kwamba unaweka akiba bila kukosa. Hiki kiasi hiki, kitakuja kukusaidia siku za mbeleni kwenye uwekezaji au hata malengo yako ya kukuza kipaji chako zaidi.

    NB: usiweke fedha yako chini ya godoro. Hizi zama za kuweka fedha chini ya godoro zimeshapitwa na wakati. sana tafuta kuweka akiba yako, sehemu ambayo huwezi kuifikia kwa haraka sana. Inaweza kuwa ni kwenye laini ya simu ambayo hujui namba yake siri yake ya mpesa.

    Inaweza kuwa ni benki au kwenye mifuko ya uwekezaji ya pamoja ya UTT. Kwa kuwa kitabu hiki siyo cha uwekaji wa akiba wala uwekezaji, basi naomba ukasome kitabu changu kinaitwa MAAJABU YA KUWEKA AKIBA na kingine kinaitwa MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE. Hivi vitabu viwili vitakufundisha kwa kina suala zima la fedha. Wasiliana nami kwa namba 0755848391 sasa.

    2. Unapaswa kuwekeza

    Rafiki yangu, kitu kingine muhimu sana ambacho unapaswa kujua na kukipa nguvu kubwa sana ni uwekezaji. Unapokuwa na kipaji, maana yake wewe unakuwa unafanya kazi kwa ajili ya kuingiza fedha. Usipokuwepo moja kwa moja maana yake siku hiyo hakuna kitu chochote kile ambacho kinaweza kufanyika kwa manufaa. Sasa kipaji chako kinakuwezesha wewe kupata fedha, na unapopata fedha unapaswa kuwekeza pia. Uwekezaji ni moja ya eneo ambalo linakufanya wewe uwe unapata fedha bila hata ya kuwepo kufanya kazi.

    Kwa hiyo basi rafiki yangu, napenda kukuhakikishia kuwa uwekezaji ni moja ya jambo muhimu sana kwenye maisha yako, ambalo unapaswa kufanya. Kwa hiyo, wekeza. Kwa kuwa wewe ni mgeni kwenye uliwengu wa uwekwezaji, basi hakikisha kuwa unaanza kuwekeza na kwa kuanzia, basi anza kuwekeza kwenye mifuko ya uwekezaji wa wa pamoja.

    Na ujue kiwango unachohitaji kuanza nacho ili uweze kuwekeza siyo kikubwa sana kama ambavyo unaweza kufikiria. Ni kiwango kidogo tu, ukiwa na elfu kumi unaweza kufungua akaunti kwenye mfuko wa umoja na baada ya hapo unaweza kuendelea kuwekeza zaidi na zaidi kwa kuweka kiwango cha chini cha elfu tano.

    Baada ya kuwa umefanya kazi kwa miaka yako yote, haupaswi kuwa mstaafu aliyefulia.

    Siku siyo nyingii nilikuwa nikisoma nikifuatilia historia ya Michael Jordan, nilichokuja kugundua kutoka kwa huyu jama ni kwamba, amewekeza kiasi cha kumwezesha kununua timu ya kikapu. Alipokuwa mchezaji, kile kiasi cha fedha alichokuwa analipwa alikuwa hatumii chote.

    Moja ya kitu kinachowafanya watu wenye vipaji bongo (wachezaji, wanariadha, wanamziki n.k) kufuria baada ya kustaafu ni kuwa pale wanapokuw wanaingiza fedha, basi wanaendekeza starehe kuliko wanavyowekeza. Hiki kitu unapaswa kuepukana nacho. Kuna madhara mawili ya kuendekeza starehe. Kwanza utajiona kama vile umefika kule unapotakiwa kwenda wakati bado ndio kwanza safari yako imeanza.

    Pili, ukiendekeza starehe utasahau kuchapa kazi na hivyo kushuka kwenye kiwango unachofanyia kazi kipaji chako. Unaukumba wimbo wa Tundaman na Chege wanaosema Starehe gharama?

    3. Unapaswa kujifunza na kufikiri kibiashara

    Kinachowakwamisha vijana wengi wa kitanzania kwenye vipaji vyao ni wao kufikiri kuwa; kwa kuwa wana vipaji basi wanapaswa kupambana wao kama wao tu. Sikiliza, kama unataka kipaji chako kifike mbali, basi kiweke kibiashara.

    Hii ndio kusema kwamba, angalia namna ya kuwahusisha watu wengine wakusaidie kwenye kipaji chako. Hawa wanaweza kuwa ni watu watakaokusaidia wewe kusambaza kile unachofanya, au wale watakaokusadia kuwafikia wateja wako. Kwa vyovyote vile, hakikisha kwamba kipaji chako hakikugandi, kifanye kuwa biashara ndio utafika mbali zaidi. Ndio maana huwa unaona wengine wanakuwa na meneja na vitu kama hivyo. Naombe nieleweke,kwenye hili kwamba, hakuna mtu ambaye huwa anafanya makubwa kwa kutumia dhana ya jeshi la mtu mmoja. Jeshi la mtu mmoja siyo practical kwenye ulimwengu wa leo. Ni kweli utaanza peke yako, lakini huwezi kutoboa kiwango cha kimataifa ukiwa ni jeshi la mtu mmoja! Unahitaji timu!

    4.Unapaswa kujifunza ujuzi wa kuongea na kuwasilisha kile ulichonacho mbele ya watu

    Hata kama una kipaji ni kama cha Khaby Lame, bado utapaswa kujifunza kuongea mbele watu. kwa sababu kuna siku utapaswa kuongea mbele ya watu. Watu watakuhoji na wewe utalazimika kuwasilisha mada mbele yao katika namna ambayo inaeleweka, kumbe kuongea mbele ya watu ni moja ya jambo ambalo haliepukiki rafiki yangu.

    5. Unapaswa kujenga tabia ya kusoma vitabu

    Vitabu ni nyenzo. Unajua nyezo lakini? Shule ya msingi tulijifunza kuwa kuna mzigo na jitihada. Hiki kitu kilikuwa kinarahisisha ufanyaji wa kazi. ambapo mtu ulikuwa na uwezo wa kusukuma mzigo mkubwa kwa nguvu kidogo. sasa vitabu pia ni wenzo daraja la kwanza! Vinakusaidia wewe kusukuma maisha na kusonga mbele kwa nguvu kidogo unayoweka kwenye vitabu.

    6. Kuondokana na uoga

    Uoga umewafanya watu wengi washindwe kufanyia kazi vipaji na uwezo wao. Uoga umewafanya watu washindwe kuthubutu, uoga umewafanya watu wapunguze kasi ya kufanyia kazi malengo yao. Rafiki yangu, ondokana na uoga, simama kisha songambele.

    7. Kuweka malengo na kuhakikisha kwamba unayafanyia kazi bila ya kuishia njiani

    Mwanzoni mwa mwaka watu wengi huwa wanaweka malengo ila waengi huwa wanaishia njiani. Kila mwaka unapasawa kuweka lengo ambalo utalifanyia kazi ili kuona wapi unafikisha kipaji chako.

    Linaweza kuwa ni lengo la kuongeza idadi ya watu wanaofuatilia kazi zako mitandaoni. Linaweza kuwa ni lengo la kuuza kazi zako kwa watu milioni moja. linaweza kuwa ni lengo la kuajiri mtu au watu kadhaa. linaweza kuwa ni lengo la kushirikiana na baadhi ya watu kwenye kazi zako n.k.

    Kwa vyovyote vile hakikisha kwamba unakuwa na malengo. Na malengo yako yanapaswa kuwa yamegawanywa kwenye malengo ya wiki, mwezi, mwaka na hata miaka mitano au kumi ijayo.

    Tonny Robinns aliwahi kusema kwamba, kuweka malengo ni hatua ya kwanza ya kubadili yasiyowezekana kuwa yanayowezekana.

    8. Kukubali kuwa maisha ni wajibu wako

    Kama kuna kitu ambacho kimekuwa kinawakwamisha vijana na watu wengi, ni pale ambapo wao wanafikiri kuwa maisha siyo wajibu wao, badala yake wanafikiri kuwa kuna mtu, ambaye anaweza kuwa ni serikali au mjomba ambaye anahusika na maisha yao. Naomba nikwambie hili na ulipokee rafiki yangu, ukweli ni kuwa maisha ni wajibu wako. Ukifeli ni juu yako na ukifanikiwa ni juu yako. Ukilifahamu hili, utaishi maisha kwa raha mustarehe sana rafiki yangu. Unajua kwa nini? Kwa sababu, hutakaa na kuanza kumsubiri mtu ili akusaidia kwenye kufanyia kazi maisha yako, badala yake utapambana kuhakikisha kamba maisha yanakuwa ni wajibu wako kwelikweli.

    Utaachana na malalamiko ambayo unatoa sasa hivi. badala ya kusema kwamba serikali haitoi ajira, wewe utapambana kuona ni kwa namna gani unaweza kutengeneza ajira. Ujue unaweza kuwa unalalamika kuwa hakuna ajira, kumbe wewe ndiye unapaswa kuwa mtoaji wa ajira.

    9. kuwa kiongozi

    Wengi huwa wanachanganya uongozi na cheo. Kitu hiki huwafanya wengi wafikiri kuwa kiongozi ni lazima uwe na cheo. Hapana.

     Haikuhitaji uwe na watu na watu wanakuja kwako kwako kuleta kesi ili uwe kiongozi. Maana yake unaweza kuwa mkulima ila wewe ni kiongozi, mwalimu bodaboda au yeyote ila ni kiongozi. Siku zote nimekuwa nawaambia watu kwamba kila mtu ni kiongizi tangu kuzaliwa kwake.

    Kama wewe unaweza kuamka asubuhi na kupangilia mipango yako jinsi itavyoonda na kujiwwkea ratiba nzuri na kuifuata basi wewe ni kiongozi. Kama wewe hauna mtazamo wa kushawishi watu kufanya vizuri zaidi katika shughuli zao basi wewe ni mfuasi.
    Hata kama utakuwa na cheo cha uongozi watu hawataweza kukufuata kwa sababu wanaona matendo yako hayaendani na kile unachosema.

    Kiongozi wa ngazi ya juu ambaye muda wote amejifungia hataki kuongea na watu wala hataki kuwa karibu na watu basi huyo sio kiongozi ni mfuasi.

    10. kuamka mapema

    Siwezi kukumbuk ni marangapi nimekuwa nikisisitiza juu ya umuhimu wa kuamka mapema, lakini bado nalazimika kuendelea kufanya hivi. kuamka asubuhi na mapeka kuna manufaa mengi sana.

    Kwanza unaamka muda ambao watu wengi wamelala. Hakuna kelele (labda kama unakaa ghetto na washikaji, wanaowasha muziki usiku kucha,hahah). Muda huo hakuna mtu wa kukupigia simu, labda kama utaamka kuongea na mchumba wako aliye Moshi wakati wewe uko Mwanza. Hakuna watu wanakuja kukugongea chumbani kwako. yaani, ni wewe tu na Mungu wako.

    Kitu hiki kinakupa nafasi nzuri tu yaw ewe kupata muda wa kufikiri, kupanga ratiba yako ya siku hiyo, kupanga watu ambao utaenda kuwapigia, kupanga watu ambao utaenda kukutana nao na mengine mengi. Kwa hiyo basi rafiki yangu, itumie nafasi ya kuamka asubuhi na mapema vizuri sana.

    Nakubaliana na Benjamin Franklin aliyewahi kusema kwamba, kuamka asubuhi na mapema na kulala mapema kunamfanya mtu awe na afya njema, tajiri na mwenye busara.

    11. kuinuka baada ya kuanguka

    Maisha ni safari rafiki yangu, na kama ilivyo safari yoyo tile. Lazima kwenye kusafiri kwako kuna sehemu ambapo utakutana na mlima, hivyo utapanda huo mlima, na kuna sehemu utakutana na bonde, utashuka. Rafiki yangu, hizi zote ni sehemu za maisha na zinatokea kwenye maisha yetu ya kila siku. Sasa inapotokea umejikwaa kwenye safari yako, basi usije ukarudi nyuma na kuacha kufanyia kazi kile unachopaswa kuwa unafanyia kazi. Endelea kupambana rafiki yangu, mpaka kieleweke. Ukianguka inuka. Inawezekana.

    12. Kuanza na kile ulichonacho

    Wengi huwa wanasubiri wawe na kila kitu ndio waanze, wewe usisubiri kuwa na kila kitu ili uweze kuanza. Anza na kile ulichonacho.

    • Usisubiri uwe maarufu ili unoe kipaji chako, anzia hapo hapo ulipo na hicho ulichonacho.
    • Usisubiri uwe kama rais Mwinyi ili uandike kitabu. Andika kitabu, halafu hiyo ngazi yake utaifikia mbele ya safari.
    • Usisubiri mpaka uwe na fedha ili uanze kuweka akiba, anza kuweka akiba kwa kiwango hicho hicho ulichonacho. Ngoja nikwabie kitu, asilimia kubwa ya vitu unavyohitaji kufanya, unaweza kuanza kuvifanya sasa hivi bilaya kuchelewa.

    13. epuka kujilinganisha na watu wengine

    Daah, kama kuna kitu kinawatafuta vijana wengi basi ni hiki; kujilinganisha.

    • Eti kwa sababu fulani kaajiriwa basi ngoja na mimi nipambane ili niajiriwe.
    • Eti kwa sababu fulani kajenga nyumba kijijini kwetu basin a mimi mpaka nikajenge.
    • Eti kwa sababu, fulani yuko kwenye mahusiano na mimi lazima nimpate wa kwangu. Haya bwana kampate,hahaha

    Ukijilinganisha, ni wazi kuwa hutaweza kuishi maisha yako kwa namna ambavyo unataka wewe. Maisha yako yatakuwa ni magumu sana,sana. Ishi maisha yako na furahia hilo. Furahia hatua wanazopiga wengine, maana siyo kila hatua lazima na wewe uipige kwa wakati huohuo.

    Wakati wengine wanajenga kijijini, wewe uko hapa unawekeza kwenye UTT. Mtu anaweka milioni 50 kwenye kujenga nyumba ya kuishi na familia yake, wewe unaweka milioni hamsini UTT, kwenye mfuko wa hatifungani, unaotoa gawio kila mwezi. Nani kawin hapa? Kama huelewi uwekezaji huu wa kwenye mifuko ya Utt, unaweza usinielewe ninachojaribu kukueleza hapa, ndio maana nakushauri upate kitabu changu cha maajabu ya kuwekeza kwenye hisa, hatifungani na vipande ili uweze kunielewa vizuri hapa. Ebu rusha elfu tano tu, kwenye simu yangu nikurushie hiki kitabu. Namba ya simu 0755848391 jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Kitabu hiki kinapatikana kwa elfu tano tu (sotfcopy0
    Kitabu hiki kinapatikana kwa elfu tano tu (sotfcopy)

    14. Epuka kufuatilia maisha ya watu wengine

    Moja ya kitu ambacho unahitaji kuhajkikisha kwamba unaachana nacho kama unataka kufika mbali na kuachana na suala zima la kufuatilia maisha ya watu wengine. Kuna watu wengine wanajua mwenendo wa maisha ya watu wengine, kuliko wanavyo jua kuhusu maisha yao. Hli ni kosa kubwa ambalo unaweza kufanya kwenye maisha yako. Hakikisha kwamba unayajua maisha yako kuliko mtu mwingine au kwa lugha nyingine jifuatilie wewe mwenyewe kuliko unavyomfuatilia mtu mwingine. hivi kwa mfano, kama wewe ungekuwa ni kampuni, je, watu waengewekeza kwenye hiyo kampuni kununua hisa zake, wewe mwenyewe ungewekeza kwenye kampuni wewe kununua hisa zako mwenyewe! Kama jibu ni hapana, maana yake unahitaji kujiboresha.

    Na njia nzuri ya kujiboresha, ni wewe kuacha kufuatilia maisha ya watu wengine, na kufuatilia zaidi maisha yako wewe mwenyewe.

    15.kutokuhofu kuhusu kile ambacho watu wengine wanafikiri juu yako

    Watu wengine wanasemaje kuhusu wewe? Kwa chochote kile unachokuwa unafanya, fahamu kuwa kuna watu ambao watakusema.

    Hata ukicheka, kuna watu watasema, hebu mwone na huyu anavyocheka. Sasa unataka nichekeje? Binadamu bwana…

    Kwa hiyo hilo lifahamu na wala lisikuchanganye.

    Kama kuna kitu cha kuondoka nacho hapa ni kuwa kila mtu ana kazi yake. Wewe kazi yako ni kuhakikisha kuwa kipaji chako king’aa. Wengine kazi yao ni kuhakikisha kuwa wanakusema.

    Nadhani umenielewa hapo.

    14. kuwa na mipango ambayo unaifanyia kazi

    Hakuna mtu ambaye huwa anaandika mipango ya kuwa mnene, mzembe,mjinga, asiyejali au baba/mama aliyetelekeza watoto.

    Lakini ukweli ni kuwa kama hutaweka mipango ya kuwa afya njema, mchapakazi, anayejali, ni sawa na kuweka mipango ya kuzembea.

    Kwa hiyo usije ukajishangaa umekuwa mnene, mzembe, asiyejali. Hukuweka mipango ya kuwa na hivi vitu, ila kwa kutokuweka mipango, unakuwa unastahili kuvipata.

    Nimeandika sana, sasa mpaka naandika kuandika faslsafa. Ebu niishie hapa mengine nayaacha kwa ajili ya siku zijazo.

    Kama una swali, maoni, au kitu chochote ungependa kusema, basi au hata ungependa kuchangia kidogo kwa ajili ya kuwezesha makala bora ziendelee kuwa hewani, basisi usisite kutucheki kupitia 0755848391.

    ©Haki zote zimehifadhiwa

    Nimesikiliza na nitasikiliza tena

  • Vitu vitano (05) Vitakavyokufanya uheshimike

    Rafiki yangu bila shaka unaendelea vyema kabisa. siku ya leo ningependa kukushirikisha vitu vitano ambavyo vitakufanya wewe uweze kuheshimika kwenye kazi, kwenye mahusiano na kwenye maisha kiujumla. Kwa hiyo, kama unataka kuheshimika rafiki yangu, hivi hapa ni vitu vitano ambavyo unapaswa kuanza kufanyia kazi mara moja.

    1. KITU CHA KWANZA NI KUCHAPA KAZI

    Kazi ni kitu ambacho kinampa mtu heshima. Na hata maandiko mbalimbali yamethibitisha na kusisitiza hili la kufanya kazi kwa namna tofauti tofauti, huku maandiko maarufu yakiwa yale yanayosema kwamba asiyefanya kazi basi asile. Rafiki yangu, kazi ni moja ya kipimo cha utu.

    Kwa hiyo, kama unataka kuheshimika kwenye jamii, basi fanya kazi.

    Kwa watu wengi unapoongelea kazi, basi kinachokuja kwenye kichwa chao au kwenye akili zao ni kuwa ajira.  Yaani, kazi fulani hivi ya kukaa ofisini huku kukiwa na kiyoyozi, huku wenyewe wakiwa wananesa kwenye kiti fulani hivi amazing! Rafiki yangu, kuna tofauti kubwa sana kati ya kazi na ajira.

    Kamusi ya Kiswahili sanifu inasema kazi ni shughuli anayofanya mtu kama vilekulima, kuandika au kufundisha.

    Huku ikisema kuwa ajira ni kazi izitolewazo au zifanywazo kwa malipo katika kampuni serikalini au kwa mtu binafsi.

    Kumbe kwa mantiki hiyo ndiyo kusema kwamba, kazi zipo nyingi. Kufanya kazi siyo lazima uwe umeajiriwa chini ya mtu, unaweza kufanya kazi hata kama hujaajiriwa. Unaweza kujishughulisha wewe mwenyewe. Kwa mfano unaweza kuanza kutengeneza vitumbua na kusambaza kwa kuanzia mtaani kwako. hivi kweli kitu kama hiki nacho kinaweza kukushinda?

    Kitumbua kimoja kinauzwa shilingi 100. Kila siku ukijiwekea lengo la kutengeneza vitumbua na kuuza vitumbua 500, maana yake kila siku utakuwa unaingiza kiasi cha shilingi  elfu hamsini.  ili uweze kufanikisha lengo lako hili la kuuza vitumbua 500 kila siku unahitaji walau uwe na kijana mmoja ambaye anajituma na anafanya kazi kwelikweli. Mmoja wenu, anaweza kuwa yeye au wewe anakaa chini na kutengeneza vitumbua, huku mwingine akizunguka mtaani na kusambaza vitumbua kwa watu wenye uhitaji, ikiwa ni pamoja na kwenda kwenye maeneo yenye mkusanyko mkubwa watu kama stendi na sokoni.

    Rafiki yangu, kwa jinsi hii unakuwa umejitengenezea kazi lakini wakati huohuo unakuwa tayari umetengenza ajira. Kwenye hiyo shilingi elfu hamsiini uliyouza ndani ya siku husika, ukitoa gharama au mtaji wa biashara yako. Huwezi kukosa kubaki na hela ya kwako, tena hela ya maana tu. ebu tuchukulie baada ya kutoa gharama zote ukabaki na elfu ishirini tu. Hii siyo hela kidogo, ukiwa unaingiza kiasi hiki cha hela kwa mwezi ni sawa na laki sita!

    Wewe unakuwa siyo mtu wa viwango vya kawaida. Mpaka hapo unakuwa umeua ndege wawili kwa jiwe moja, ukiendelea kukaza unashangaa baada ya miaka mwiili una kiwanda chako cha kutengeneza vitumbua. Usicheke, ujue hapa naongea vitu siriazi!

    Kwa hiyo, rafiki yangu, achana na dhana ya kulia kuwa hauna kazi kuanzia leo hii. tafuta kazi na anza kufanya kazi.

    • Inaweza kuwa ni kutengeneza vitumbua kama nilivyokwambia
    • Inaweza kuwa ni vitu vingine kama kuuza karanga, kulima mboga, na vitu vingine vingi
    • Nadhani kuna mawazo mengi ambayo unaweza kuanza kufanyia kazi leo hii, tena ambayo yanahitaji mtaji mdogo tu!

    Tatizo kubwa linalowakumba vijana wengi ni kudharau kazi wakati hawana kazi. Na hii zaidi ni kwa wasomi ambao wamehitimu vyuo na ngazi nyingine, wanaona kwamba baadhi yakazi siyo kazi za viwango vya, hivyo, kitu pekee ambacho wao wanaamua kufanya ni kukaa bila kufanya kazi.

    Rafiki yangu, kama hauna kazi na haujui kitu gani unaswa kufanya, basi usidharau. Chagua kazi yoyote ile kisha anza kuweka juhudi kwenye hiyo kazi. Ifanye ili iweze kukuingizia kipato.

    Siyo eti kwa sababu umesoma basi muda wote unabaki kusuka nywele huku ukihofia kwenda shambani kufuga na kulima, huku ukiendelea kulalamika kuw ahuna kazi.

    Kuuza vitu vya mia mia

    Hapo juu nimetolea mfano wa mtu ambaye ameamua kujiajiri kwa kufanya kuuza vitumbua. Tena nikatolea mfano kuwa kitumbua kimoja kinauzwa shilingi mia moja! (japo vipo vitumbua ambavyo vinauzwa zaidi ya hapo). sasa hapa ninachotaka kukwambia ni kuwa vitu vya mia mia vinawapa hela kuliko unavyoweza kufikiria.

    Ndio maana unaona mpaka mabilionea wanazidi kutegeneza vitu vya mia mia! Hivi kiberiti, kinauzwa shilingi ngapi vile… Huku mtaani kwetu kinauzwa shilingi mia moja sijajua huko kwenu. Mo Dewji ni bilionea mkubwa hapa Tanzania, ila huku mtaani kuna viberiti ambavyo ametengeneza yeye.

    Hivi, pipi zinauzwa shilingi ngapi vile…najua utaniambia bei tofauti zikiwemo za mia moja na mia mbili au hata zaidi..

    Kuna watu wenye hela zao, wamewekeza mabilioni ya hela wanatengeneza pipi eti. Tena pipi zingine zinauzwa shilingi hamsini tu za Kitanzania.

    Ninachotaka kukwambia ni nini? ninataka kukwambia kwamba usidharau vitu vidogo, maana hivi vitu vidogo mwisho wa siku huwa vinakuwa na matokeo makubwa kuliko unavyoweza kufikiri.

    2. KUTHIBITI HISIA ZAKO

    Najua kuna watu wengi ambao tunaishi nao kwenye jamii na huwa wanatukosea au hata muda mwingine kutulazimisha tuingie kwenye migogoro nao.

    Unaweza kushangaa unatembea mtu anakukanyaga halafu anakutukana. Au unaendesha gari, mtu akaku overtake katika eneo ambalo kisheria halafu anakuoneshea ile ishara fulani hivi ya kidole….

    Sasa haya yote watu wanaweza kuyafanya ili kukukasirisha wewe, ila moja ya kitu ambacho unahitaji kukifanya ni wewe kuthibiti hisia zako. muda mwingine watu wanapokuwa wanafanya vitu kama hivi, wewe unahitaji kuwa mpole na hata kuwachukulia kama watoto wadogo.

    Mtoto mdogo akikutukana, basi wewe utasema kwamba huu ni utoto. Sasa na kwa hawa inapaswa kuwa hivyohivvyo, badala ya wewe kukimbizana nao na kugombana nao, badala yake weka nguvu kubwa  kwenye malengo yako na ndoto zako. Wachkulie tu kama watoto wadogo, mtoto mdogo akikutukana ni wazi kuwa wewe huwezi kumtukana na kukasirika. Badala yake utasema huu ni utoto tu

    3. KUSIKILIZA ZADI YA UNAVYOONGEA

    Hiki ni kitu kingine ambacho kitakufanya uweze kuheshimika zaidi ujue dunia imejaa na waongeaji zaidi ya wasikilizaji, na kusikiliza ni ujuzi ambao unapaswa kuwa nao kwenye hizi zama.

    Mimi kuna watu huwa wananipigia simu na kuongea watakavyo, kwa sababu huw wanajua kuwa tu nitawasikiliza. Unkuta mtu shida yake siyo kubwa sana, ila sasa anahitaji mtu ambaye atamsikiliza kwa umakini na kumpa muda way eye kuongea. Kile kitendo cha mtu kusikilizwa kinampa pumziko la roho nay eye anakuwa kama ametua mzigo mkubwa.

    Rafiki yangu, anza kujenga utaratibu wa kusikiliza badala ya kuongea sana. nakuhakikishia kuwa utajifunz amengi kutoka kwa watu kuliko pale unapokuwa muongeaji sana.

    NNE, KUWAACHA WATU KWENYE NAFASI NZURI KULIKO ULIVYOACHA.

    Rafiki yangu, nataka nikupe zoezi moja kuanzia siku ya leo. Na zoezi hili ni kuwa, kila unapokutana na mtu, angalia ni kwa namna gani utamwacha katika hali nzuri kuliko ulivyomkuta. Unaweza kufikiri kwamba ili ufanye hili basi utahitaji kuwa na fedha, hapana.

    Moja unaweza kuongeza juhudi ambazo watu wanaweka kwenye kazi wanazofanya. Kuna watu wanafanya kazi au vitu ila hawajawahi kupata mtu wa kuwapongeza na kukubali kile wanachofanya. Sasa kwa nini wewe usiwape moyo na kuwaambia kwamba kile wanachofanya ni kitu kizuri na chenye manufaa kwa jamii. Nakwambia rafiki yangu, hiki ni kitu kidogo, ila chenye nguvu kubwa sana ambacho unapaswa kuzingatia.

    Je, na hilo rafiki yangu, linaweza kukushinda?

    5.  KUWA NA FEDHA ZAKO MWENYEWE

    Nadhani hili halina ubishi, kwenye hii blogu nimekuw anikiandika mara kwa mara kuhusu fedha. Lakini kwa lleo ningependa kusema kitu kimoja tu kuhusu fedha.

    Na kitu hiki ni kuwa, fedha inakufanya uheshimike hata kama ni mdogo, na kama hauna fedha unadharaulika hata kama ni mtu mzima.

    Mfano rahisi tu ni kwenye vikao vya familia. Mwenye fedha kwenye kikao anasikilizwa kuliko ambaye hana fedha.

  • Tofauti Kati Ya Kazi na Ajira

    Kazi ni kitu ambacho kinampa mtu heshima. Na hata maandiko mbalimbali yamethibitisha na kusisitiza hili la kufanya kazi kwa namna tofauti tofauti, huku maandiko maarufu yakiwa yale yanayosema kwamba asiyefanya kazi basi asile. Rafiki yangu, kazi ni moja ya kipimo cha utu.

    Kwa hiyo, kama unataka kuheshimika kwenye jamii, basi fanya kazi.

    Kwa watu wengi unapoongelea kazi, basi kinachokuja kwenye kichwa chao au kwenye akili zao ni kuwa ajira.  Yaani, kazi fulani hivi ya kukaa ofisini huku kukiwa na kiyoyozi, huku wenyewe wakiwa wananesa kwenye kiti fulani hivi amazing! Rafiki yangu, kuna tofauti kubwa sana kati ya kazi na ajira.

    Kamusi ya Kiswahili sanifu inasema kazi ni shughuli anayofanya mtu kama vilekulima, kuandika au kufundisha.

    Huku ikisema kuwa ajira ni kazi izitolewazo au zifanywazo kwa malipo katika kampuni serikalini au kwa mtu binafsi.

    Kumbe kwa mantiki hiyo ndiyo kusema kwamba, kazi zipo nyingi. Kufanya kazi siyo lazima uwe umeajiriwa chini ya mtu, unaweza kufanya kazi hata kama hujaajiriwa. Unaweza kujishughulisha wewe mwenyewe. Kwa mfano unaweza kuanza kutengeneza vitumbua na kusambaza kwa kuanzia mtaani kwako. hivi kweli kitu kama hiki nacho kinaweza kukushinda?

    Kitumbua kimoja kinauzwa shilingi 100. Kila siku ukijiwekea lengo la kutengeneza vitumbua na kuuza vitumbua 500, maana yake kila siku utakuwa unaingiza kiasi cha shilingi  elfu hamsini.  ili uweze kufanikisha lengo lako hili la kuuza vitumbua 500 kila siku unahitaji walau uwe na kijana mmoja ambaye anajituma na anafanya kazi kwelikweli. Mmoja wenu, anaweza kuwa yeye au wewe anakaa chini na kutengeneza vitumbua, huku mwingine akizunguka mtaani na kusambaza vitumbua kwa watu wenye uhitaji, ikiwa ni pamoja na kwenda kwenye maeneo yenye mkusanyko mkubwa watu kama stendi na sokoni.

    Rafiki yangu, kwa jinsi hii unakuwa umejitengenezea kazi lakini wakati huohuo unakuwa tayari umetengenza ajira. Kwenye hiyo shilingi elfu hamsiini uliyouza ndani ya siku husika, ukitoa gharama au mtaji wa biashara yako. Huwezi kukosa kubaki na hela ya kwako, tena hela ya maana tu. ebu tuchukulie baada ya kutoa gharama zote ukabaki na elfu ishirini tu. Hii siyo hela kidogo, ukiwa unaingiza kiasi hiki cha hela kwa mwezi ni sawa na laki sita!

    Wewe unakuwa siyo mtu wa viwango vya kawaida. Mpaka hapo unakuwa umeua ndege wawili kwa jiwe moja, ukiendelea kukaza unashangaa baada ya miaka mwiili una kiwanda chako cha kutengeneza vitumbua. Usicheke, ujue hapa naongea vitu siriazi!

    Kwa hiyo, rafiki yangu, achana na dhana ya kulia kuwa hauna kazi kuanzia leo hii. tafuta kazi na anza kufanya kazi.

    • Inaweza kuwa ni kutengeneza vitumbua kama nilivyokwambia
    • Inaweza kuwa ni vitu vingine kama kuuza karanga, kulima mboga, na vitu vingine vingi
    • Nadhani kuna mawazo mengi ambayo unaweza kuanza kufanyia kazi leo hii, tena ambayo yanahitaji mtaji mdogo tu!

    Tatizo kubwa linalowakumba vijana wengi ni kudharau kazi wakati hawana kazi. Na hii zaidi ni kwa wasomi ambao wamehitimu vyuo na ngazi nyingine, wanaona kwamba baadhi yakazi siyo kazi za viwango vya, hivyo, kitu pekee ambacho wao wanaamua kufanya ni kukaa bila kufanya kazi.

    Rafiki yangu, kama hauna kazi na haujui kitu gani unaswa kufanya, basi usidharau. Chagua kazi yoyote ile kisha anza kuweka juhudi kwenye hiyo kazi. Ifanye ili iweze kukuingizia kipato.

    Siyo eti kwa sababu umesoma basi muda wote unabaki kusuka nywele huku ukihofia kwenda shambani kufuga na kulima, huku ukiendelea kulalamika kuw ahuna kazi.

    Kuuza vitu vya mia mia

    Hapo juu nimetolea mfano wa mtu ambaye ameamua kujiajiri kwa kufanya kuuza vitumbua. Tena nikatolea mfano kuwa kitumbua kimoja kinauzwa shilingi mia moja! (japo vipo vitumbua ambavyo vinauzwa zaidi ya hapo). sasa hapa ninachotaka kukwambia ni kuwa vitu vya mia mia vinawapa hela kuliko unavyoweza kufikiria.

    Ndio maana unaona mpaka mabilionea wanazidi kutegeneza vitu vya mia mia! Hivi kiberiti, kinauzwa shilingi ngapi vile… Huku mtaani kwetu kinauzwa shilingi mia moja sijajua huko kwenu. Mo Dewji ni bilionea mkubwa hapa Tanzania, ila huku mtaani kuna viberiti ambavyo ametengeneza yeye.

    Hivi, pipi zinauzwa shilingi ngapi vile…najua utaniambia bei tofauti zikiwemo za mia moja na mia mbili au hata zaidi..

    Kuna watu wenye hela zao, wamewekeza mabilioni ya hela wanatengeneza pipi eti. Tena pipi zingine zinauzwa shilingi hamsini tu za Kitanzania.

    Ninachotaka kukwambia ni nini? ninataka kukwambia kwamba usidharau vitu vidogo, maana hivi vitu vidogo mwisho wa siku huwa vinakuwa na matokeo makubwa kuliko unavyoweza kufikiri.

  • Vitu Viwili Kuhusu Kipaji Ambavyo Hakuna Mtu Amewahi Kukwambia

    Jana nilikuwa naangalia mahojiano kati ya mtengenezaji wa maudhui kutoka Ghana maarufu sana kama Wode Maya na msanii wa Zimbabwe Jah Prayzah.

    Kuna mengi waliyongea ila mimi binafsi niliondoka na mawili ambayo yamenigusa na ambayo nimeona nikushirikishe na wewe.

    Kitu  cha kwanza kabisa Jah Prayzah alisema hivi, mimi sikuchagua kuwa msanii ila nilichaguliwa kuwa msanii. Hii maana yake nini, maana yake ni kwamba kuimba kupo ndani yake. Hiki ni kipaji chake cha kuzaliwa nacho kabisa.

    Nimekuwa nakushauri mara kwa mara rafiki yangu kuwa na wewe uhakikishe unajifanyia tathimini ili uweze kugundua na kutumia kipaji chako.  Ukigundua kipaji chako rafiki yangu na ukakitumia, mara zote utakuwa ukifanya kazi yako na majukumu yako kwa furaha. Kwa sababu unafurahia kazi au kile unachofanya.

    Kuna siku Arnorld Schwarzenegeer aliwahi kuulizwa, kwa nini, unakuwa na furaha sana muda wote mbali na kuwa unakuwa unanyanyua vyuma kwa muda wa saa tano kila siku. Watu walimuuuliza hivi kwa sababu waliona wengine waliokuwa wananyanyua vyuma hawakuwa na furaha hata kidogo kwenye maisha yao. Kwa kujibu hili Arnorld Swacherzenegger alisema kwamba, ninapenda ninachofanya. Rafiki yangu, kipaji chako ni kitu ambacho kinapaswa kitu kinachotoka moyoni. Kitu ambacho huoni kama umelzimishwa au umesukumwa kukifanya, badala yake unahisi kama kuna msukumo wa ndani kabisa ambao unakusukuma wewe kukifanyia kazi kipaji chako na kukifanikisha kwa viwango vikubwa

    Kitu cha pili Jah Prayzah alisema kwamba, mimi mpaka leo bado nafanya kazi kwa bidii kama msanii mchanga. Yaani, bado najituma kwa nguvu zangu zote kama msanii ambaye hajatoboa, na sasa ndio anatafuta namna ya kuweza kutoboa na kwenda hatua ya ziada kwenye maisha.

    Hiki kitu rafiki yangu na wewe kitumie kwenye kazi zako na kwenye kitu chochote kile ambacho unafanya. mara zote fanya kazi kama vile wewe bado ni mchanga kwenye sekta ambayo unafanyia kazi, hata pale unapokuwa umekua na umeweza kufika viwango vya juu. Kwa nini?

    Ili niweze kujibu kwa nini yako kwa undani zaidi, naomba nikutolee mfano mzuri kwenye biashara, mwanzoni mtu anapoanzisha biashara anakuwa anajituma na kuweka nguvu kubwa sana kuhakikisha kwamba biashara yake inakua. Anatafuta wateja, anawapigia simu na mambo mengine mengi. Yote haya anayafanya kwa lengo moja tu, la kuhakikisha kwamba anafanya mauzo zaidi kwenye biasahra yake. Lakini kadiri biashara hiyo inavyokuwa inazidi kukua, inafikia hatua ambapo yule mtu anasahua ile misingi iliyomwinua na hivyo, kujikuta kwamba anaanza kufanya kazi kwa mazoea.

    Na hapo ndipo anguko la biashara nyingi huwa linatokea.

    Hiki kitu huwa hakitokei tu kwenye biashara peke yake, bali pia kwenye kwa watu wenye vipaji vyao. Unakuta mtu ana kipaji kizuri, anakifanyia kazi, anakua na kufikia viwango vya juu, ila sasa baada ya muda anasajisahau, anarelax na kuanza kuishi maisha ya kawaida sana. kitu ambacho huwa kinamepekea kwenye anguko. Hapa ndipo huwa unasikia habari za kwamba

    Msanii fulani ameshuka kiwango

    Au mchezaji ameshuka kiwango

    Kinachomfanya ashuke kiwango siyo kitu kingine bali ni kwamba zile juhudi alizokuwa anaweka mwanzoni kwenye kazi, sasa haweki juhudi hizohizo, kitu hiki kinamfanya aanze kushuka kidogo kidogo na baadaye anashuka kabisa.

    Kwa hiyo rafiki, mara zote fanya kazi kama vile ndio kwanza unatafuta maisha.

    KIPAJI NI DHAHABU
    Rafiki yangu, nimeandika kitabu. Kinaitwa KIPAJI NI DHAHABU. Ili kupata kitabu hiki, wasialiana na mi kwa 0755848391 sasa

    Rafiki yangu, ili kukurahisishia safari yako ya kukifanyia kazi kipaji chako. Nimekuandalia kitabu maalumu kabisa, kinaitwa Kipaji ni Dhahabu. Nashauri sana uweze kusoma kitabu hiki cha kipekee kwa shilingi elfu kumi tu.

    Kupata nakala yako, wasiliana nami kwa 0755848391

  • Kitu hiki kimoja kitakutofautisha wewe na watu wengine wenye kipaji kama cha kwako

    KIPAJI NI DHAHABU
    Rafiki yangu, nimeandika kitabu. Kinaitwa KIPAJI NI DHAHABU. Ili kupata kitabu hiki, wasialiana na mi kwa 0755848391 sasa

    Kama kuna kitu ambacho kinaweza kukutofautisha wewe na watu wengine wenye kipaji kama cha kwako basi kitu hiki siyo kingine bali ni kujifunza na kulielewa eneo ambalo unafanyia kazi kwa undani zaidi kuliko mtu mweingine yeyote. Yaani, unahakikisha kuwa taarifa zote za  muhimu kuhusana na kipaji chako unakuwa nazo na unazitumia kwa manufaa kuhakikisha kwamba unaweza kufika kule uhnaptaka kufika kwenye maisha yako.

    Ukiwa na taarifa sahihi ni rahisi pia kufanya maamuzi bora (sound choice). Kwa hiyo, jitahidi kuhakikisha kwaba unalifanyia kazi. na njia ya wewe kulifanyia hili kazi ni kuhakikisha kwamba unajifunza kila mara kwa kusoma vitabu na kupitia majarida mbalimbali.

    Kamwe usikifikie hatua ambapo utajiona kama vile umefika au umekamilika. Badala yake infanye kila dakika ambayo upo hapa duniani kuwa ni dakika yako ya kujifunza na kukielewa vizuri kipaji chako nje ndani, hili jambo hili rafiki yangu. ukilifanyia kazi baada ya siku nyingi sana ni wazi kuwa hili jambo moja tu litakufikisha mbali.

    Kama huamini lijaribu kwa kuliweka kwenye vitendo ili uweze kuona maajabu yake na namna ambavyo litafanya kazi kwako. kumbuka kwamb alinafanya kazi kwa wengine, na litafanya kazi kwako pia.

  • Hiki kitu Kimoja Tu, Kitakufanya Utumie Kipaji Chako Kwa Viwango Vikubwa

    KIPAJI NI DHAHABU
    Rafiki yangu, nimeandika kitabu. Kinaitwa KIPAJI NI DHAHABU. Ili kupata kitabu hiki, wasialiana na mi kwa 0755848391 sasa

    Leo asubuhi nimeamka na kuangalia video moja ambayo Kobe Braynat alikuwa akihojiwa na Patrick Bet-David. Moja ya swali ambalo Kobe Brayant aliulizwa ni kuwa ni msukumo gani ambao umekuwa ukimsukuma kujituma na kuhakikisha anakuwa jinsi anakuwa mchezaji bora. Kati ya mengi ambayo ameongea, kitu kikubwa amesema sitaki siku moja nije nianze kujuta kuwa ningeweza kuwa zaidi ya hapo. nataka nihakikishe kamba natumia uwezo wangu kwa viwango vya juu  kiasi kwamba hakuna siku hata moja ambayo nitakaa na kuanza kujuta kwa nini sikuweza kukamilisha jambo fulani ambao nilipaswa kuwa niweza kufanikisha.

    Kobe Brayant

    Rafiki yangu, sijui wewe upo kwenye hali gani kwenye maisha, na wala hata siui kipaji wala uwezo wako ni upi. Ila kitu kimoja cha kuhakika ni kuwa kama na wewe utayatumia haya maneno ya kobe Brayant kwenye maisha yako ni wazi kuwa unaenda kufika mbali na kufanya makubwa. Hii ndio kusema kwamba utajituma zaidi ya unavyofanya sasa hivi, siyo ilimradi tu umejituma, bali ukiwa unajua kuwa sitaki hata siku moja kuja kujutia.

    Rafiki yangu, kama una nafasi ya kufanya makubwa leo hii, usiwe mzembe. Yafanye haoyo  makubwa.

    Kama unaweza kufanya mazoezi leo, fanya hivyo.

    Kama kuna wateja ambao unaweza kuwapigia simu leo hii ili waje kununua kwako, wapigie simu.

    Kama kuna kitu unaweza kufanya, kifanye. Kwa vyovyote vile rafiki yangu, hakikisha kwamba, mara zote unajisukuma kuwa bora zaidi ya vile ulivyo sasa hivi.

    Rafiki yangu kama kila mtu kwenye hii dunia akifanya kile anachopaswa kufanya kwa namna anavyopaswa kukifanya, ni wazi kuwa hii dunia itakuwa sehemu nzuri sana.

    Nzuri kwelikweli!

    Lakini ukweli ni kuwa hatuwezi kusubiri kila mtu afanye ndio na sisi tuanze…

    Mimi na wewe tuanze. Tufanye kile tunachopaswa kufanya, wengine wataona na wataiga kutoka kwetu…

    Timiza wajibu wako kama unavyopaswa kuutimiza.

    Kama wajibu wako ni kupika chakula…kipike vizuri sana.

    Kama wajibu wako ni kucheza..cheza

    Kama wajibu wako ni kufundisha fanya hivyo

    Fanya hivyo kiasi kwamba hakuna mtu mwingine ambaye anaweza kufanya kazi unayofanya kwa viwanvgo unavyofanya. Kwa jinsi hiyo utakuwa umejitofautisha…

  • Sababu Sita Zisizopingwa Kwa Nini Unapaswa Kuendeleza Kiapaji Chako

    KIPAJI NI DHAHABU
    Ili kupata kitabu hiki, wasialiana na mi kwa 0755848391 sasa

    Kwenye kitabu cha Acres of Diamond, mwandishi ameeleza historia ya jamaa ambaye aliambiwa kuwa ukiwa na almasi yenye ukubwa kidole unaweza kuimiliki dunia. Huyu jamaa kusikia hivyo, aliamua kusafiri kwenda kuitafuta dhahabu ambayo mwisho wa siku hakuipata!

    Siku hizi bado watu wanatafuta dhahabu! Utasikia watu wanapeana stori kuwa ukienda kwenye machimbo ya Geita au Mererani basi wewe kutoka kimaisha ni njenje tu! lakini ukiachana na hayo ni ukweli kuwa  mbali na hayo madini na hizo dhahabu ambazo unaweza kupata kutoka kwenye hayo maeneo, kuna dhahabu  ambazo watu wanazo ila wanaonekana kutozitumia vizuri na dhahabu hizi siyo nyingine bali ni uwezo na vipaji tulivyonavyo. Ukifahamu thamani ya kipaji, utajihidi kuhakikisha kwamba unatumia kipaji chako kwa nguvu zako zote bila kuacha. KIPAJI NI DHAHABU. Na unapaswa kukinoa vizuri rafiki yangu.

    Kwa leo nataka niingie kwa undani na kukueleza sababu sita kwa nini hasa unapaswa kunoa kipaji chako, ili kiweze kuwa chenye manufaa kwako wewe mwenyewe.

    Sababu ya kwanza ni Umezaliwa Nacho Wewe Ila Siyo Chako

    Huwa napenda kuwaambia watu kuwa unapewa kipaji sio kwa manufaa yako, bali kwa manufaa ya jamii nzima. Na kuthibitisha hili hapa huwa napenda kutolea mfano wa mwanamziki.

    Mwanamziki akiimba wimbo wake sio tu kuwa unamnufaisha yeye peke yake, bali wimbo huo unakufaisha hata wewe ambaye unausikiliza. Tena unakuta kwamba wewe msikilizaji ndiye unasikiliza ule wimbo kuliko hata mwanamziki mwenyewe. Kwa hiyo, wewe unapokuwa na kipaji unapaswa kukifanyia kazi sio tu kwa ajili ya manufaa yako bali kwa manufaa ya watu wengine pia.

    Kuna watu wengine ili waweze kufanikisha vipaji vyao wanahitaji wewe ufanyie kazi kipaji chako kwanza. Ebu chukulia mfano wa mtu kama Albert Einstein. Huyu ni mtu ambaye alikuwa na kipaji cha hesabu mpaka akaweza kuja mlinganyo maarufa sana kwenye fikizia wa E=Mc2. Lakini Einstein sio baba wa fikizia!

    Inawezekana kama akina Newton na Galileo wasingeweka njia, basi kipaji cha Einstein kisingeonekana. Kwa hiyo hakikisha unatumia kipaji chako, kwa ajili ya manufaa yako, kwa ajili ya manufaa ya jamii, na kwa ajili pia ya kuhamasisha watu wengine.

    Mwaka 2007 ulikuwa ni wa kipekee kwenye ulimwengu wa kidigitali. Ni mwaka ambao kwa mara ya kwanza simu janja (smartphones) zilivumbuliwa na kuletwa kwenye umma wa watu. hata hivyo, cha kushangaza ni kwamba, aliyegundua simu hizi, alishalala zamani ila simu hizi zimeendelea kuwa zenye faida na manufaa kwa watu wengine zaidi yake. Hiki kitu kikuoneshe na wewe kuwa kipaji au huo uwezo ulio nao ndani yako siyo tu kwamba ni wa kwako peke yako, bali upo pia kwa ajili ya manufaa ya watu wengine.

    Leo hii watu wengi wananufaika kwa kutumia simu janje pengine kuliko hata aliyetengeneza simu hizo. Simu zinawaingizia watu fedha, simu zimetumika kuwaunganisha watu walio mbali, simu zimewezesha kuwatumia fedha ndugu zetu walio mbali…

    Kuna watu wameweza kugundua vitu vingine kwa sababu tu walikuwa na simu au walikuwa wanajua kuna simujanja. Kwa mfano, hizi app za simu zimetengenezwa mara tu baada ya kuwepo kwa simu. Kuna watu maisha yao yanategemea app za simu tu.

    Sasa ebu jiulize kama aliyetengeneza simujanja angeamua kufa na uwezo wake, leo hii hawa watu ambao maisha yao yanategemea app za simu peke yake wangekuwa wapi?

    Kumbe muda mwingine kipaji chako kinaweza kuwa kimebeba ajira za watu wengine ila wewe hujui tu. Ebu kifanyie kazi siyo tu kwa ajili ya manufaa yako, bali kwa ajili ya manufaa ya watu wengine pia.

    Sababu ya pili ni kuwa kuna watu wanaweza kubadlil maisha kwa sababu ya kipaji chako. Endapo utafanyia kazi kipaji chako na kukifanikisha kuna watu ambao watajifunza kwako na watataka kunoa vipaji vyao ili wawe kama wewe.

    Hujawahi kusikia mtu anasema nikikua nataka niwe kama mtu fulani. Sasa kuendeleza kipaji chako kunawafanya  watu watamani sana  kuwa na maisha kama ya kwako.

    Kuna watu wengine watanoa na kufanyia kazi vipaji vyao kwa sababu wanajifunza kwako.

    Ngoja ni kwambie kitu rafiki yangu. ujue kitu kimoja kwenye maisha ni kuwa kwa vyovyote vile, popote pale ulipo kuna watu ambao wanajifunza kitu kutoka kwako. Inawezekana nyuma yako kuna watu wawili au mmoja ambao ni mashabiki wako, sasa hawa watu wakikuona wewe unafanyia kazi kipaji chako, ni wazi kuwa wenyewe watatamani sana kuweza kunoa kipaji chao na kukifanikisha,

    Kuna watu wamekuwa wanamziki baada ya kuwa wamemwona mtu wa mtaani kwao kwenye runinga au kumsikia kwenye redio. Hiki kitu kimewapa hamasa kubwa na hivyo wao wakapambana ili na wao waweze siku moja kuonekana kwenye redio na runinga.

    Na mimi nina uhakika leo hii ukifanyia kazi kipaji chako, kuna watu nyuma yako watapenda na watakuwa tayari kutaka kufuata nyayo zako. usiwaangushe, noa kipaji chako. Kiendeleze mpaka kiimarike.

    Sababu ya tatu ni kuwa utaishi maisha ambayo unayapenda. Utafiti maarufu ni kuwa watu wengi huwa wanakufa jumatatu asubuhi. Kwenye utafiti huu wanaonesha kuwa wengi wa wale ambao huwa wanakufa siku ya jumatatu ni wale ambao huwa hawapendi kazi zao. Yaani, mtu anaenda kazini lakini kazi yenyewe anayoifanya siyo ile ambayo anapenda.

    Hivyo akishakula bata siku za wikendi, halafu akaamka jumatatu akiwa anafahamu kuwa anaenda kufanya kazi ambayo hapendi, anakata tamaa na kupoteza maisha.

    Rafiki yangu, kipaji chako ni kitu ambacho unakipenda. Unapofanyia kazi kipaji chako, maana yake unakuwa unafanyia kazi kile ambacho wewe mwenyewe unapenda. Sijui umenielewa mpaka hapo.

    Hiki kitakufanya uishi miaka mingi na kheri duniani! Watu wanaofanya kile wanachopenda wana furaha, wana amani ya mwili na roho, wanajiamini kwenye kazi zao na hawana msongo

    Ila kama unafanya kazi ambayo huipendi matokeo yake yanakuwa ni tofauti. Na utafiti mwingine unaonesha kwamba watu wanaotumia uwezo na vipaji vyao wanafanya vizuri zaidi kwenye kazi kuliko wale ambao hawatumii vipaji na uwezo wao.

    Sababu ya nne ni kuwa utatengeneza fedha kutoka kwenye kipaji chako

    Kadiri utakavyokuwa unakitumia kipaji kuna watu wataona kwamba wanaweza kunufaika na kipaji chako, na hivyo kuwa tayari kulipia ili wapate vitu vingi zaidi kutoka kwako

    Sababu ya tano ni kuwa utaacha alama inayodumu milele. Kwa kazi ambazo utazifanya kutokana na kipaji chako, mwisho wa siku unaenda kuacha alama ambayo itadumu kwa siku nyingi hata baada ya wewe kuwa umeaga dunia.

    Sababu ya sita kujiondolea majuto. Usipofanyia kazi kipaji chako, kuna siku utaanza kujuta kwa nini hukufanyia kazi kipaji chako. Kwanza, utasikia kwenye vyombo vya habari kwamba vijana machachari sehemu fulani, wameweza kufanya mambo makubwa. Wakati nawe, ulipaswa kuwa kijana machahari kama hao wanaotajwa. Hiki kitu  kitakuumiza na kukukatisha tamaa.

    Pili, utaanzisha usemi utakaokuwa unautoa kama hadithi kwa watoto mpaka kwa wajukuu wako. Utaanza kuwaambia, bwana mnamwona fulani, nilisoma naye ila sasa hivi hashikiki. Kama si hivyo huenda ukasema kwamba, nilikuwa ninakaa naye darasa moja ila sasa hivi amefanikiwa sana. Utasema, kuna kipindi huyu mtu alikuwa na maisha mabaya ila sasa hivi maisha yake yamebadilika sana. Au pengine utasema, mimi ndiye nilikuwa kinara darasani na huyu jamaa hakuwahi hata kuonekana kwenye zile kumi bora. Binafsi, nimekuwa ninawavumilia sana wazee ambao wanasema hivi. Ila wewe, sitakuvumilia hata kidogo.

    Nitakuuliza, wakati hawa wanapambana wewe ulikuwa wapi? Ni kitu gani kilikuzuia wewe kufanya makubwa? Je, hawa watu walikufunga kwenye mti wakaanza kuchapa kazi, sasa ndiyo wamekuja kukufungua? Kiukweli sitakuvumilia.

    Rafiki yangu, hizo ni sababu zangu sita kwa nini wewe unapaswa kufanyia kazi kipaji chako tena, kuanzia leo hii. rafiki kama kuna zawadi unapaswa kujipa wewe mwenyewe kwenye maisha, basi ni zawadi ya kufanyia kazi kiapji chako. Halafu ujue kwamba nina zawadi ya kitabu ya kitabu. Kipokee kitabu chenyewe kwa kujaza taarifa zako hapa chini

    kitabu cha maajabu ya kuweka akiba

  • Jinsi Ya Kutangaza Kipaji Chako

    Moja kati ya kitu ambacho nimekuwa nikiwaambia watu wengi ni kuwa tuna bahati ya kuishi kwenye ulimwengu wa leo tunaoishi. Mababu zetu wangekuwa wanarudi leo hii na kuona fursa kibao zilizotuzunguka, ni wazi kuwa wenyewe wangetuonea gere.

    Mambo ambayo miaka hiyo yalikuwa hayawezekani, leo hii yanawezekana, tena siyo kwamba yanawezekana kidogo, yanawezekana sana tu.

    Ebu chukulia kwa mfano jinsi ilivyokuwa kazi ngumu kunoa kipaji chako miaka ya nyuma. Tusiende mbali sana, tuongelee miaka michache hii baada ya uhuru. Kiukweli, kunoa na kuendeleza kipaji chako ilikuwa ni moja ya kazi ngumu kitu hiki kilifanya watu wengi washindwe kunoa na kuendeleza vipaji vyao. Na hata wengine kwa kukosa maarifa sahihi kama ambayo nimeandika kwenye kitabu cha KIPAJI NI DHAHABU, walishindwa kabisa kujua vipaji vyao.

    KIPAJI NI DHAHABU
    Ili kupata kitabu hiki, wasialiana na mi kwa 0755848391 sasa

    Ebu tuchukulie mfano kuwa ulikuwa na kipaji cha kuimba, miaka hiyo na labda ulikuwa mkoa wa Mtwara. Kwanza ili kurekodi wimbo ulipaswa kwenda studio na kuwasilisha wazo lako, ambapo studio wazo lako lingeweza kukubaliwa au kukataliwa, lakini pia ulipaswa kuwa na hela kubwa ya kukusaidia kurekodi wimbo wako.

    Baada ya kuwa umerekodi huo wimbo ulipaswa kuwa na mtu wa kusambaza hizo nyimbo zako na hata wafadhili wa kukupiga tafu kwenye kazi zako.

    Siyo hilo tu, kama miaka hiyo ulitaka kutangaza wimbo wako, njia za kipekee na za uhakika za kutangaza wimbo huo, zilikuwa ni kupitia vyombo vya habari. Kwa kuwa vyombo vingi vya habari vilikuwa Dar, wewe uliyekuwa Mtwara, ulilazimika kusafiri mpaka Dar ili ukutane na watu hawa wa vyombo vya habari au la kutangaza kipaji chako kwenye hivi vyombo vya habari ilikuwa ni ngumu sana.

    Na hata baada ya kukutana nao kutokana na mfumo uliokuwepo wangeweza kukukubali au kukukatalia au hata kutaka uwape rushwa kubwa ili wakufanyie tangazo.

    Sasa chukulia hiyo hali na jinsi mambo yalivyo sasa hivi, kwa sasa hivi mambo yamebadilika kwa asilimia 100. Huo mchakato wote umevunjwa kiasi kwamba unaweza kufanya hayo yote bila kizuizi kikubwa.

    Kama una wimbo au kipaji cha kuimba na ukatunga wimbo wako. Unaweza kwenda studio na kurekodi wimbo wako

    • kwa gharama nafuu sana na
    • bila vikwazo

    Pengine unaweza ukawa hauna hela ya kurekodi, ukaamua tu kuanza kutumia simu yako kurekodi wimbo wako na hata baadaye ukautoa.

    Kama nakuona vile unavyoguna kuwa haiwezekani kurekodi wimbo kwa kutumia simu!

    Ila kabla hujakataa kabisa hilo wazo kuna vitu viwili ambavyo ningependa kukwambia.

    Kama unatumia simu janja (smartphone), simu yako ina uwezo mkubwa kuliko kompyuta iliyopeleka mtu mwezini. Huo ni ukweli nambari moja. Sasa ebu fikiria kompyuta iliyopeleka mtu mwezini ilikuwa na uwezo mdogo kuliko simu yako janja, je,unadhani kompyuta zilizokuwa zinatumika kurekodi nyimbo miaka hiyo zilikuwa zinafananaje? Ni wazi kuwa uwezo wake ulikuwa ni mdogo zaidi. Kumbe simu yako hiyo ni mgodi mkubwa sana ambao umeulalia, jitahidi sana ili uweze kuutumia mgodi huu.

    Niendelee au nisiendelee!

    Ukweli nambari mbili ambao utakufungua macho zaidi ni juu ya vijana wa Nigeria waliorekodi movie kwa kutumia simu. Vijana hawa kutoka Nigeria Kaskazini, walikuwa na simu moja hivi ambayo imekwaruzwakwaruzwa kwenye kioo. Ila waliitumia hiyo hiyo kama kamera kuhakikisha kwamba wanarekodi tamthiliya.

    Kumbe kama una simu kubwa, maarufu kama simu janja au smartphone basi jua wazi kuwa umelalia hazina kubwa sana ambayo haupaswi kuichezea rafiki yangu. Ni hazina ambayo mababu zetu hawakuwa nayo, ila wewe una bahati ya kuwa nayo. Usiitumie ktu kuchati, bali itumie kwa manufaa.

    Kuna watu wamerekodi video na kuziweka kwenye mitandao kama youtube na tiktoka na hatimaye kunufaika na kupata fedha. Kuna watu wametengeneza kazi mbalimbali za sanaa kwa kutumia simu zao. Mimi nimeitumia simu yangu kuandika vitabu na kuendesha mitandao ya blogu yangu ya songambele (www.songambele.co.tz). Rafiki yangu badala ya kusubiri siku ambayo utakuwa na rasilimali kubwa na za kipekee hakikisha  kwamba unaanza kuzitumia hizi rasilimali za kawaida ulizonazo. Ukiweza kuzitumia vizuri hizi rasilimali kidogo ulizonazo, ukipata rasilimali kubwa ni uhakika kuwa utaweza kufanya makubwa zaidi ya hapo.

    vijana wa Nigeria wakirekodi Movie kwa kutumia simu yao

    Bado unafikiri haiwezekani kurekodi muziki wako kwa kutumia simu? Kama unafikiri kitu hiki  hakiwezekani basi fikiri tena!

    Kwenye mtadao wa Tiktok kuna kijana mmoja maarufu sana ambaye ana wafuasi wengi kuliko watu wote kwenye mtandao huo. Kijana huyu si mwingine bali ni kijana Kaby Lame. Huyu kijana ni raia wa Senegali anayeishi Italia. Mpaka mwaka 2020 alikuwa ni mmoja wa wafanyakazi kwenye kiwanda kimojawapo pale nchini ITALIA, wakati wa kipindi cha Corona kampuni aliyokuwa nafanyia kazi ilipunguza wafanyakazi. Akiwa haelewi ni kitu gani ambacho angeweza kufanya katika kipindi kama hiki, aliamua kuchukua simu yake na kuanza kurekodi video fupifupi alizokuwa akifanya kama uchambuzi fulani hivi wa tamthiliya.

    Alianza kidogo kidogo, na mara punde hizi video zake zilianza kushika kasi. Leo hii ni mmoja wa vijana wenye ushawishi mkubwa sana kwenye mtandao wa TIKTOK, lakini kitu kikubwa ambacho  alianza nacho ni simu yake aliyokuwa nayo.

    Khaby Lame

    Leo hii najua vijana ambao wana ndoto na vipaji vikubwa, ila wanasubiri kupata mfadhili kutoka maeneo ambayo wenyewe hawajui kama atatokea.

    Miaka kadhaa nyuma kabla hata sijajua kama kuna watu waliweza kurekodi movie kwa kutumia simu na kabla sijajua kuwa kuna akina Khaby Lame ambao wanarekodi video fupifupi kwa kutumia simu, nilikuwa nikiongea na mmoja wa ndugu zangu wa karibu ambaye moyoni mwake alikuwa akipenda kuigiza.

    Nilimweleza namna ambavyo angeweza kuanza kufanyia kazi kipaji chake cha kuigiza huku akijirekodi kwa kutumia simu yake. Nilipomwambia wazo huyu ndugu alilikataa kabisa, huku akisema kwamba haiwezekani kufanya kitu kama hico. Leo hii kile alichokuwa anasema kwamba hakiwezekani kuna watu wameweza kukifanya kwa manufaa na kujulikana duniani.

    Pengine yeye leo hii asingekuwa maarufu kama hawa, lakini angekuwa anafanya kitu anachopenda. Lakini mpaka ninavyoandika hapa, bado amesubiri muujiza fulani wa kumnyanyua na kumfanya aigize. Anasubiri awe na kamera za kisasa na timu ya kumrekodi.

    Hiki kitu kinanikumbusha usemi wa kuwa, pale unaposema kwamba haiwezekani, anatokea mtu mbele yako ambaye anakifanya. Wewe ukiendelea kusema kwamba haiwezekani, basi jua kwamba muda si mrefu kuna watu mbele yako ambao watatokea na kufanya kile kitu ambacho wewe mwenyewe ulikuwa unasema kwamba hakiwezekani.

    Baada ya kuwa umeanza kufanyia kazi kipaji chako, hakikisha kwamba hauishii tu kwenye kuanza kukifanyia kazi. lakini kuwa na mwendelezo wa kile unachofanya. Hiki ni kitu ambacho huwa kinawaangusha watu wengi. kuna watu kadha wa kadha ambao huwa wanaanza kufanyia kazi vitu ila huwa wanaishia njiani. Rafiki yangu, usifanyie kazi kipaji chako mara moja kisha ukatulia. Kuwa na mwendelezo kwenye kufanyia kazi kipaji chako. Usifanyie kazi kipaji chako mara moja, kifanyie kazi mara kwa mara.

    Hii ni njia bora ya kujitangaza bila kutumia gharama kubwa. kuna watu wanaweza kupuuza kazi zako kadhaa za kwanza, ila wakiona unaendelea kuweka juhudi kubwa kwenye kile unachofanya inafikia hatua wanaanza kufuatilia kazi zako, na hivyo unakuwa umewateka na kuwaleta kwako.

    Kuna watu watafuatilia kazi zako na kuwaambia watu wengine juu yako. Kwa jinsi hii,kazi zako zinakuwa zinakutangaza zaidi kwenye maeneo mbalimbali

    Wekeza kwenye kipaji chako. Pale unapokuwa unapata hela, usitumie zote kwa pamoja. Badala yake toa kiasi fulani ambacho utakirudisha kwenye kipaji chako. Utakirudisha kwenye kipaji kwa kununua vifaa vya kisasa zaidi ambavyo zitakusaidia kutoa kazi ambazo ni bora kadiri siku zinavyoenda. Utawekeza tena kwenye kipaji chako kwa kukitangza ili kiweze kwenda mbali kuliko ilivyokuwa mwanzoni. Na kujifunza vitu mbalimbali ili uzidi kubobea zaidi.

    Na kwenye ulimwengu wa leo kuna njia lukuki za kutangza kipaji chako.

    Unawezakutengaza kipaji chako kwenye mtandao wa intaneti . Google wana mfumo wao wa kutengeneza matangazo ambapo hayo matangazo unayaonesha mbele ya watu wanaoendana na tangazo lako. Lakini pia kuna mitandao kama youtube ambapo unaweza kutangaza kipaji chako huku.

    Mtandao kama instagram pia ni mtandao mzuri kwa ajili ya kutangaza kipaji chako, ambapo kwa gharama kidogo tu unaweza kuwafikia melfu kwa maelfu ya watu. Hiki kitu kilikuwa hakiwezekani miaka ya nyuma. Ebu chukukulia miaka ya nyuma kama ungependa kujitangaza kwenye gazeti. Gharama tu kuchukua nusu ukurasa kwenye gazeti, ni kubwa sana. na hii siyo kwa miaka ya nyuma tu, bali mpaka leo hii. Bado ukitaka kutangaza kipaji chako kwa njia magazeti au redio na runinga, gharama yao ya kutangaza kazi yako au kipaji chako ni kubwa ukilinganisha na mitandao kama facebook, twitter na instagram. Ambapo kwa gharama kidogo tu unaweza kufanya matangazo ambayo yatawafikia watu wengi

    Kwa leo naishia hapa.

    Kesho nitaendeea

    Mimi ni rafiki yako Godius Rweyongeza

    0755848391

    Morogoro-Tz

    Kupata ebook ya MAAJABU YA KUWEKA AKIBA utalipia elfu tano tu. Namba ya simu ni 0755848391

X