-
Namba Zetu Za Malipo
Namba za malipo ya vitabu:
Namba za lipa
TIGO PESA: 19016638 Jina ni SONGAMBELE CONSULTANTS
M-PESA: 5564517 jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA
Namba za kawaida
AIRTEL MONEY: 0684408755
TIGO PESA: 0655 848 392
M-PESA: 0745 848 395Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA
NB: Kama namba ya malipo anatumiwa mtu ambaye yuko nje ya nchi. Iandikwe Kwa kuanza na +255
Kwa hiyo namba zinazotumwa nje ya nchi zitakuwa
Airtel money: +255 684 408 755
TIGO PESA: +255 655 848 392
M-PESA: +255 745 848 395KOTE Jina ni GODIUS RWEYONGEZA
Kama malipo yatakuwa yanafanyika kupitia benki.
Yafanyie kupitia
- CRDB BANK: 0150770710200
- NMB BANK: 22110047274
Kote jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA
-
Wasiliana na Godius Rweyongeza Sasa
Habari yafuatayo ni mawasiliano Unayoweza kutumia kumpata GODIUS RWEYONGEZA
Simu: +255 (0) 684408755
Whatsap: +255 (0) 755848391
Email: songambele.smb@gmail.com
Kupata vitabu vyake wasiliana Moja kwa Moja na +255 (0) 684408755 (more…)
-
Ukifanya kitu unachopenda Ubunifu unakuwa mwingi.
…….muda si mrefu nimetoka kuongea na mteja wetu mmoja ambaye yuko mkoani Mara (Msoma mjini).
Ambaye amepokea kitabu Cha jinsi ya kufikia NDOTO ZAKO na kuanza kukisoma.Kitu cha pekee nilichopenda kutoka kwake ni usemi wake anaosema kuwa ukifanya kitu unachopenda, Ubunifu unakuwa mwingi.
Na hiki kitu nimeona nikushirikishe na wewe pia.
Kuna utafiti unaonesha kuwa watu wengi wanakufa siku ya jumatatu baada ya kula Bata wikendi halafu jumatatu wanaamka na kwenda kufanya kazi wasiyopenda. Hicho kitu tu, kinawakatisha tamaa.
Ndiyo maana nimeupenda huu usemi, kiasi cha kuwa tayari kukushirikisha huu usemi na wewe.
Ujumbe mkubwa nilio nao kwako siku ya leo ni kwamba ufanye kazi au kitu unachopenda.
Ukifanya kitu unachopenda hutachoka
Ukifanya kitu unachopenda ubunifu unakuwa mwingi.Thomas Edison alikuwa analala saa tatu kwenye maisha yake na kuamka mapema kwenda kazini. Siku moja aliulizwa kwa nini unafanya sana kazi.
Aliwajibu watu kwa kuwaambia kuwa sijawahi kufanya kazi.
Umeona ee! Alikuwa anafanya kitu anachopenda. Hivyo, kwake hakuona kama hiyo ilikuwa kazi.
Hivi wewe unafanya unachopenda kweli? Unafanya unachopenda?
Ngoja nikukumbushe, “ukifanya kitu unachopenda, ubunifu unakuwa mwingi”.
Kwa jioni ya leo naishia hapa.
Halafu ujue kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO kipo tayari. Na watu wanapokea nakala zao popote pale walipo. Wewe pia unaweza kupata nakala yako kwa Bei ya oda. Ujue gharama ya kitabu hiki ni 20,000/- Ila habari njema ni kuwa ukilipia kitabu hiki kabla ya tarehe 20 Mei. Utakipata kwa 15,000/- unaanzaje Sasa kwa mfano kukosa nakala yako.
Ebu nitumie ujumbe wako sasa hivi
Tuma ujumbe kwa
0755848391
Au WhatsApp
https://wa.me/message/3PMZSAFONLHAP1Ili utumiwe kitabu chako.
Umewkuwa nami
Godius Rweyongeza
0755848391
Morogoro-TzUkifanya kitu unachopenda ubunifu unakuwa mwingi.
-
Tumebaki Na Siku 3 Tu Za Kupata Kitabu Cha Jinsi Ya Kufikia Ndoto Zako Kwa Bei Ya Oda
[wpcdt-countdown id=”5798″]
Hello, habari ya leo. Bila sahaka unaendelea vyema.
Kwa siku sasa nimekuwa nikikwambia kuhusiana na kitabu cha jinsi ya kufikia ndoto na jinsi ambavyo unaweza kupata nakala yako. Kitabu hiki kinazinduliwa tarehe 20 Mei, hata hivyo, oda zimeshaanza kuwekwa.
Na ubora ni kuwa nakala za kitabu zimetoka mapema. Hivyo, nimeona badala ya kusubiri mpaka tarehe 20 Mei ndio nitume vitabu. NI bora nianze kutuma nakala sasa hivi, maadam zipo. Kwa hiyo, kila aliyeweka oda ya kitabu na kulipia. Tayari ametumiwa kitabu chake au la anatumiwa leo na wengine vitabu vyao vipo njiani.
Sasa leo wakati naagalia kwenye tarehe hapa, nikaona kwamba, zimebaki siku chache tu kabla ya tarehe ya mwisho ya wewe kupata kitabu hiki kwa bei ya oda.
IPO HIVI, kitabu hiki gharama yake ni 20,000/- ila ukiweka oda siku ya leo unaenda kupata kitabu hiki kwa gharama ya 15,000/- tu.
Sasa kilichobaki rafiki yangu ni wewe kuchangamka ili uweze kupata kitabu hiki.
Cha kufanya sasa hivi, weka oda yako kwa kutuma ujumbe kwenda namba 0755848391
Tuma ujumbe wenye jina lako
Namba yako na mahali ulipo.
Mfano: Godius Rweyongeza 0755848391 (Morogoro mjini-Morogoro)
Ukishatuma huo ujumbe utapewa maelekezo ya kulipia, ili uweze kupata nakala yako mapema.
Karibu sana rafiki yangu, tuko pamoja.
-
Kitu Kimoja Cha Kufanya Kama Hauna Fedha Sasa Hivi
Usikubali kubaki kuwa huna fedha halafu ukaendelea kusema tatizo langu sina fedha. Usipochukua hatua leo, kesho na kesho kutwa bado utakuwa unasema tatizo langu ni fedha.
SOMA ZAIDI: Kama Hauna Hata Mia Mbovu Jua Unakosea Hapa
Chukua hatua.
Tafuta bidhaa yoyote unayoweza kuuza. Nenda kwa watu uuze. Unachopaswa kujua ni kuwa fedha zako wanazo watu. Ila huwezi kwenda kwa watu na kuwalazimisha wakupe hiyo fedha. Huo utakuwa wizi au unyang’anyi. Njia bora ya wewe kupata fedha kwa watu ni kuwapa hao watu huduma au bidhaa wanayotaka.SOMA ZAIDI: Ijue maana nzuri ya MASIKINI
Zig Ziglar aliwahi kunukuliwa akisema; unaweza kupata chochote unachotaka kama utawasaidia watu kupata kile wanachotaka.
Huwa napenda kuwaambia watu kuwa matajiri nao wanaomba fedha. Ila hawaombi kama ombaomba wa mtaani, wenyewe wanaomba fedha kwa kukuletea kitu unachotaka.
Na wewe anza kuomba fedha kitajiri.
Kumbuka: unaweza kupata chochote unachotaka kama utawasaidia watu kupata kile wanachotaka.
Kila la kheri.Umekuwa nami rafiki yako, Godius Rweyongeza. Tuwasiliane kwa 0755848391
For booking: songambele.smb@gmail.com au songambele@songambele.com
UMESHAPATA NAKALA YA KITABU CHA JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO. Kama bado, tuwasiliane kwa 0755848391 ili uweze kupata nakala yako.
-
Nidhamu ni nini?
Nidhamu ni kuamua kufanya kitu, bila kujali unajisikia kufanya kile kitu au hujisikii. Matendo yako ya kila siku ndiyo yanaweza kutuambia kuwa una nidhamu kwenye eneo gani na hauna nidhamu kwenye eneo gani. Kwa mfano, kama umejiwekea utaratibu wa kuweka akiba kila siku, na ukaweka akiba kila siku, hapo unakuwa umejijengea nidhamu binafsi.
Nidhamu ni kitu ambacho kinawatofautisha wanaofanikiwa na wale ambao hawafanikiwi kwenye maisha. Ni kitu kidogo ambacho unahitaji ili uweze kufika mbali kimaisha. Bila nidhamu rafiki yangu, unaweza kuanza na mamilioni ya fedha kwenye maisha na ukayapoteza. Na ukiwa na nidhamu, unaweza kuanza na shilingi kidogo tu, ukazibadili kuwa mamilioni ya fedha.
Sasa jiulize, je, wewe una nidhamu kwenye kile unachofanya? Una nidhamu kweli?
-
Vitu vinazaliwa, vitu vinakua na hatimaye kuzeeka
Ni kanuni ya maisha kuwa vitu lazima vinazaliwa, vitu vinakua na hatimaye kuzeeka. Hakuna kitu ambacho kinapaswa kubaki hivyo hivyo, kila kitu kinapaswa kuwa kwenye mwendo muda wote na sehemu zote. kumbe, kuna wakati unaweza kutakiwa kuwa sehemu fulani, ambayo ni sehemu ya chini kwenye mchakato wako wa kupanda, sehemu mbayo pengine wewe kwa upande wako huipendi, ila haipaswi kuwa hivyo, ikiwezekana unapaswa kuipenda kwa sababu, kila kitu kina wakati wake.
Kama huu ni muda ambao unapaswa kuwa kwenye ngazi fulani, basi kazi kama mtu ambaye yuko kwenyehiyo ngazi, ifanye kazi ukiwa kwenye hiyo ngazi kwa weredi na uaminifu wa hali ya juu. Baadaye kadiri muda unavyoenda utakua na kupanda juu zaidi. hii ni kanuni ya asili.
-
Nguvu Ya Vitu Vidogo Kuelekea Mafanikio Makubwa
Helo leo ninayo furaha kutambulisha kwako kitabu cha Nguvu ya vitu vidogo kuelekea mafanikio makubwa. Ni kitabu cha kipekee sana. kabla sijasema mengi kuhusu kitabu hiki, nataka nikupe kwanza utangulizi wa kitabu ili uweze kuuusoma. Karibu
Hivi umewahi kujiuliza kuwa vitu vidogo vinaweza kukusaidia kitu gani maishani mwako?
Hivi kwa mfano, kitu kidogo kama kuamka asubuhi na mapema kinaweza kukusaidia nini maishani mwako kikifanywa kila siku na kwa mwendelezo? Au je, kitu kidogo kama kuwekeza au kuweka akiba kikifanywa kila mara kwa muda mrefu kinaweza kukusaidia nini? Kwenye kitabu hiki hapa tunaenda kuona nguvu ya vitu vidogo na jinsi nguvu hii inavyoweza kukusaidia wewe kufikia mafanikio makubwa maishani mwako.
Mara nyingi sana watu huwa wana ndoto kubwa na malengo makubwa ya kufikia kifedha, kimahusiano, kibiashara au kikazi. Lakini cha kushangaza ni kwamba huwa hawafanyii kazi hizo ndoto kubwa walizonazo bali huwa wanasubiri itokee siku moja ya muujiza ambapo ndoto yao itatimia kwa asilimia zote.
Kitu kama hiki hapa hakiwezekani. Ni wazi kuwa lengo lako la mwaka haliwezi kutimia siku ya mwisho ya mwaka baada ya wewe kuwa umekaa mwaka mzima bila ya kufanya kitu chochote, badala yake kama kweli utaweka kazi na kufuata hatua zote unazopaswa kufuata ili kulifikia hilo lengo lako la mwaka basi utalifikia kwa kufanya vitu kidogo kidogo kila siku.
Kitu chochote kikubwa kinaweza kufanikishwa kwa kuchukua hatua ndogondogo na kwa mwendelezo na hatimaye kuzifanya ziwe hatua kubwa. Mafanikio makubwa siyo kufanya vitu elfu moja mara moja, ila kufanya vitu vidogo mara elfu moja, yaani, kwa mwendelezo na bila kuchoka. Hivi vitu vidogo hatimaye vinapelekea kitu kikubwa na mafanikio makubwa.
Confucius, mwanafalsafa wa Kichina aliwahi kunukuliwa akisema kwamba, “safari ya maili elfu moja huanza na hatua moja”. Hii ndiyo kusema kwamba mambo makubwa siku zote huwa yanaanza kwa hatua ndogondogo kisha kuendelea kukuzwa. Hakuna kitu kikubwa ambacho unakiona leo hii ambacho kilianza kikiwa kikubwa hivyohivyo. Ndiyo maana wahenga walisema kwamba; “hata mbuyu ulianza kama mchicha.” Jogoo anayewika kuna siku alikuwa kifaranga.
Ukitaka kugundua kwamba vitu vikubwa huanza kwa udogo basi unaweza kuangalia ujenzi wa ghorofa. Huwa unaanza kwa hatua ndogo ndogo za kuchimba msingi, baadaye huwa wanaanza kuweka jiwe au tofali moja baada ya jingine hatimaye kitu kilichokuwa chini huwa kinaendelea kusimama na kufikia hatua ya kuwa kitu kikubwa sana.
Siku moja nilikuwa nasoma historia ya jengo ambalo limo kwenye maajabu saba ya dunia. Jengo hili siyo jingine bali ni jengo la Taj Mahal. Hili ni miongoni mwa majengo yaliyojengwa kwenye karne ya 15, na jengo lenye historia ndefu na kubwa sana. Unajua jengo hili lilijengwa kwa miaka mingapi? Unaweza kuwa sahihi. Lilijengwa kwa miaka ishirini na mbili (22). Kila siku watu walikuwa wanaweka tofali moja, siku nyingine tofali jingine, siku nyingine nondo, hatimaye lile jengo lilikamilika baada ya miaka 22!
Wajenzi hawakusubiri mwaka wa 22 ili wajenge hilo jengo. Ila walikuwa wakilifanyia kazi hilo jengo hatua kwa hatua kila siku bila kuchoka. Hili nalo litupe picha ya kuwa vitu vikubwa vinawezekana kufanyika na kuja katika uhalisia endapo vitafanyiwa kazi kwa kuanza kidogo kidogo, na kwa mwendelezo na kupewa muda ili viweze kuanzia chini na kukua.
Usidharau vitu vidogo. Kuna mfano, wa nyuki aliyeingia kwenye sikio la tembo na kuanza kupiga kelele. Tembo yule alianza kuruka huku na kule ili nyuki yule atoke kwenye sikio lake ila nyuki hakutoka. Tembo alianza kuangusha miti na kujibamiza kwenye miti pengine akidhani kwamba huyo nyuki atatoka ila huyo nyuki hakutoka. Baada ya muda mrefu wa kuhangaika, tembo alianguka na hivyo akawa amepoteza maisha. Kinaweza kuonekana kama kitu cha kushangaza, ila vitu vidogo muda mwingine huwa vina madhara makubwa sana.
Mbu ni wadogo, ila madhara yake ni makubwa. Sindano ni ndogo sana ila ikikuchoma, wewe mwenyewe ni wazi kuwa utakipata cha mtema kuni. Kwa hiyo basi, nikuombe kuwa ujenge utaratibu wa kuheshimu vitu vidogo maana vinaweza kukupelekea kwenye mafanikio makubwa au la vikakupelekea kwenye anguko kuu maana kuna nguvu katika vitu hivi vidogo. Nguvu hii inaweza kukuinua ukiitumia vizuri ila ukiitumia vibaya itakuangusha. Na nguvu hii ndiyo tunaenda kuiona kwenye kitabu hiki hapa.
Endapo utakisoma kitabu hiki na kuanza kufanyia kazi yale utakayojifunza, sipati picha jinsi ambavyo utaanza kujenga six packs ambazo umekuwa unatamani kwa siku nyingi, akiba utakayoweka, vitabu utakavyoweza kuandika, utakavyoweza kukamilisha majukumu yako kwa wakati, jinsi utakavyoboresha mahusiano yako na mengine mengi.
Kila la kheri
Godius Rweyongeza
Februari 15,2020
Morogoro-Tz
-
Kama haupo tayari kupoteza, hautaokota
KUNa wakati unahitaji upoteze kitu ili uweze kupata kitu. Kama haupo tayari kupoteza usitegemee kuokota.
Kama hauko tayari kupoteza mbegu za mahindi, usitegemee kwamba unaenda kuvuna mahindi.
Nadhani hii inaenda vizuri na ule usemi wa kihenga unaosema kwamba mtaka cha uvunguni sharti ainame. Au ule usemi wa kuwa mficha uchi hazai
Sasa swali ni kwako ni kitu gani upo tayari kupoteza kwa sasa ili uweze kunufaika kwa hapo baadaye.
-
Audiobook ya kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO hii hapa
Habari ya upande wa huko rafiki yangu. bila shaka kila kitu kinaenda vyema kabisa. Leo hii nina furaha kukutaarifu kuwa kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO, kina audiobook yake pia.
Audio hii itaanza kupatikana kuanzia mei 20, 2022.
hata hivyo, leo hii nina sample kidogo tu kukuonjesha.
unaweza kuisikiliza hapa.
ukimaliza kuisikiliza, usiache kuweka oda ya audiobook au kitabu chenyewe.
kitabu kinauzwa 20,000. ila ukiweka oda unakipata kwa shilingi 15,000 tu.
audio inauzwa kwa 15,000 ila ukiweka oda unaipiata kwa 10,000 tu.
chaguo ni lako, chagua kimoja kati ya hivyo, kisha nitumie ujumbe. tuma ujumbe wa kuweka oda kwenda namba 0755848391. Karibu sana.
-
VITU viwili usivyovijua kuhusu kitabu Cha jinsi ya kufikia ndoto ZAKO
Unaendeleaje rafiki yangu, bila shaka kila kitu kinaenda vyema kabisa. Leo hii nina habari njema kwako..
Habari njema kuhusu kitabu cha jinsi ya kufikia ndoto ZAKO.
Kitabu hiki ambacho kinaenda kuzinduliwa tarehe 20 Mei.1. Usichokijua kuhusu hiki kitabu ni kwamba watu wanaendelea kuweka oda ya kitabu hiki.
Ukiweka oda unapata kitabu hiki Cha kipekee kwa bei ya punguzo. Yaani, badala ya wewe kununua hiki kitabu kwa 20,000/- unakipata kwa 15,000/- tu. Kitabu hiki utatumiwa popote pale ulipo Duniani.2. Usichokijua kuhusu kitabu Cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO ni kwamba kitabu hiki kinapatikana kwa ;
Mfumo wa nakala ngumu (hardcocopy) ambayo gharama yake ni 20,000/- ila ukiweka oda unakipata kwa 15,000/-
Kuna na audiobook yake pia. Ambaye utaipata kwa 15,000/- Ila ukiweka oda utaipata kwa 10,000/-
Unaweza kusikiliza sample ya audiobook hapa
Hivi eti kwa mfano unashindwaje kupata nakala yako.
Ebu weka Oda yako sasa hivi. Andika jina lako hapa chini
Mfano: Godius Rweyongeza 0755848391 (Morogoro mjini-Morogoro)
Weka oda yako leo, upate nakala ya kitabu kwa bei ya punguzo
-
Zawadi hii utaipata endapo utaweka Oda ya kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO tu.
Habari ya upande wa huko. Bila shaka unaendelea vizuri kabisa. Leo hii nina zawadi ila sasa hii zawadi siyo ya kila mtu. Hii zawadi ni kwa ajili watu wachache ambao wanataka kupiga hatua na kufika mbali.
watu wenye ndoto kubwa
watu ambao wanazifanyia kazi ndoto zao kwa KUTUMIA mwongozo sahihiKiufupi hii zawadi itawaendea wale wote watakaoweka oda ya kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO. Kitabu hiki Cha kipekee kitazinduliwa tarehe 20 Mei. Na kila mtu aliyeweka oda siku hiyo atatumiwa kitabu popote pale alipo.
Kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO kinagharimu 20,000/-
Ila kwa wale ambao wataweka oda watakipata kwa gharama ya 15,000/- tu.Oda inawekwa kwa kutuma ujumbe wenye
Jina lako.
Namba yako ya simu na
Mahali ulipoMfano, GODIUS RWEYONGEZA 0755848391 (Morogoro mjini-Morogoro).
Nitumie huu ujumbe kwa SMS/WhatsApp 0755848391
Sasa acha tuongelee zawadi yangu kwako basi.
Zawadi hii ni ya ebook inayoitwa MAAJABU YA MTANDAO WA INTANETI.
Ndani ya hii ebook utajifunzaUmuhimu wa smartphone kwa mfanya biashara na mtu mwenye ndoto kubwa.
Namna ya kuutumia mtandao wa intaneti kwa manufaa ili kuifanikisha ndoto yako
Jinsi ya kujiweka mtandaoni mapema kabla ya wateja wako
Mtandao wa intaneti kama sehemu ya kukuingizia kipato
Na mambo mengine mengi…
Nataka niitoe hii ebook kwa watu wenye ndoto kubwa kwa sababu,
Siku hizi mambo yamebadilika. Mtandao umekuwa na nguvu kubwa. Sasa sitaki wewe na ndoto yako kubwa uachwe na haya mabadiliko.
Ukipata hii ebook maana yake utaweza kufanyia kazi ndoto yako vizuri, tena ukiunganisha na NGUVU YA MTANDAO WA INTANETI! Mambo yatakuwa ni 🔥🔥! Tutakutana kwenye hii ebook.
Haya yote utayapata tarehe 20 Mei 2022.Cha kufanya. Weka oda yako leo.
Kitabu kama kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO kinagharimu shilingi 20,000/- Ila ukiweka oda utakipata kwa 15,000/- za Kitanzania tu. Uko tayari!Unaweza kujiunga na kundi letu la watu walioweka oda tu.
Kujiunga bonyeza hapa