Home


  • Namba Zetu Za Malipo

    Namba za malipo ya vitabu:

    Namba za lipa

    TIGO PESA: 19016638 Jina ni SONGAMBELE CONSULTANTS

    M-PESA: 5564517 jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

    Namba za kawaida

    AIRTEL MONEY: 0684408755
    TIGO PESA: 0655 848 392
    M-PESA: 0745 848 395

    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    NB: Kama namba ya malipo anatumiwa mtu ambaye yuko nje ya nchi. Iandikwe Kwa kuanza na +255

    Kwa hiyo namba zinazotumwa nje ya nchi zitakuwa
    Airtel money: +255 684 408 755
    TIGO PESA: +255 655 848 392
    M-PESA: +255 745 848 395

    KOTE Jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Kama malipo yatakuwa yanafanyika kupitia benki.

    Yafanyie kupitia

    1. CRDB BANK: 0150770710200
    2. NMB BANK: 22110047274

    Kote jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

  • Wasiliana na Godius Rweyongeza Sasa

    Habari yafuatayo ni mawasiliano Unayoweza kutumia kumpata GODIUS RWEYONGEZA

    Simu: +255 (0) 684408755

    Whatsap: +255 (0) 755848391

    Email: songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu vyake wasiliana Moja kwa Moja na +255 (0) 684408755 (more…)

  • Njia nzuri na ya pekee ya kupata matokeo yadumuyo

    Kama kuna mtu ambaye amekufikisha wewe juu, mtu huyohuyo anaweza kukuangusha chini.

    Kama umetumia njia ya mkato, njia hiyohiyo inaweza kukurudisha chini

    Njia nzuri na ya pekee ya kupata matokeo yadumuyo ni kufuata mchakato.
    Mchakato unakujenga.
    Hata ukianguka unaweza kusimama tena maana unakuwa unaujua mchakato. Rafiki yangu, kazana kuujua mchakato, kisha ufuate.

  • Mwongozo Sahihi Wa Kufikia Malengo Na Ndoto Zako

    Ebu kwa mfano fikiria hili

    Umezaliwa na kukua katika mazingira ambayo wewe mwenyewe kabisa unaona huyapendi.

    Baadaye unasikia kuwa ukitaka kufanikiwa unapaswa kuweka malengo. Unaweka malengo lakini bado huoni matokeo makubwa, badala yake ni kama umeamua kujifukia kwenye shimo.

    Habari za kuwa unapaswa kuwa mvumilivu zinakufikia. Unasema ngoja niwe mvumilivu kwanza.
    Lakini bado hola!

    Unafanyaje sasa? Kwani sasa hakuna suluhisho tena.

    Ninachotaka ufahamu ni kuwa suluhisho lipo. Malengo yako na ndoto kubwa vinaweza kufikika ukiwa na mwongozo sahihi wa kufanya hivyo.

    Mwongozo sahihi utakaokuonesha namna sahihi haswa ya kuweka malengo. Nimegundua japo wengi wanapambana sana kila siku Ila hawana malengo sahihi. Maelekezo ya kuweka malengo mengi siyo sahihi, ndio maana wengi wanakosea na ukishakosea hapo ujue utakosea na sehemu nyingine.

    Lakini pia unahitaji kuanza kufanyia kazi malengo yako kwa kutumia hata rasilimali ulizonazo. Wengi wanadhani hawana rasilimali yoyote iliyowazunguka. Zipo. Tena unayo mitaji 8 unavyoweza kuanza nayo leo hii

    Lakini pia unahitaji kuwa na timu ya watu sahihi. Kwani wewe hujawahi kusikia kuwa chuma kinanoa chuma? Au hujawahi kuambiwa kuwa kaa karibu na waridi unukie.
    Kizungumkuti ni kuwapata hawa watu sahihi.

    Unahitaji vitendo, vitendo, vitendo ili kufanikisha malengo na ndoto zako.

    Lakini pia kuna gharama unapaswa kulipa ili ufanikishe malengo na ndoto zako.

    Rafiki yaangu, kama nilivyosema. Bila mwongozo sahihi utagonga mwamba.

    Njoo unipatie nakala yako leo kwa bei ya punguzo kwa shilingi elfu 10 tu. Utaongeza gharama kidogo za kutumiwa kitabu mpaka ulipo. Mimi rafiki yako nipo Morogoro.

    Ukitaka softcopy ya kitabu hiki kwa bei ya punguzo leo. Utakipata kwa elfu 7 tu. Hili punguzo kwa ajili yako tu rafiki yangu na halidumu kwa muda mrefu.

    Wahi Leo hii ujipatie nakala ya kitabu cha KUTOKA SIFURI MPAKA KILELENI Kwa bei ya punguzo.

    Hardcopy ni 10,000/-
    Softcopy ni 7,000/-

    Pia vitabu vyangu vingine nimeviwekea punguzo la asilimia 30 kwa leo.

    Wahi sasa tuma fedha kwa 0755848391 jina ni GODIUS RWEYONGEZA.
    Fanya hivyo Sasa hivi.

    nimimi rafiki yako

    Godius Rweyongeza

  • Wateja wako wasikusahau

    Hakikisha kila mara unawasiliana na wateja wako. Usipowasiliana na wateja wako mara kwa mara watakusahau na hata kushindwa kuja kununua kwako. Kitu hiki kinaweza kupekelekea wateja wako kwenda kununua kwa washindani wako.

    Weka utaratibu wa kuwasiliana na wateja wako kila mara.

    Tafuta sababu (excuse) nzuri ya kuwasiliana na wateja wako.
    Mfano siku ya kuzaliwa kwao wapigie simu au watumie ujumbe.
    Siku ya kuzaliwa kwa ndugu yake mpigie simu.
    Watakie kheri ya mwezi mwezi mpya.
    Watakie kheri ya sikukuu yoyote.

    Katika kuongea nao kihivyo, utakuta kwamba unaweza kufanya mauzo na hao wateja wako.

    Tumia kifurushi chako cha kila mara. Kuongea na wateja wako.

    Kila la kheri
    Umekuwa nami
    Godius Rweyongeza
    0755848391
    Morogoro-Tz



  • Ushauri: Mbinu Za Kuuza Kitabu Kwa Mafanikio Makubwa

    Unaendeleaje rafiki yangu. leo hii ninaenda kuwa najibu swali nililoulizwa na mmoja wetu ambaye anapitia kwenye changamoto baada ya kuwa amezindua kitabu chake na hakijafanya vizuri. Ebu kwanza tuone anachosema;

    Habari yako kaka kwa mara nyingine!!!

    Pole na hongera kwa kuendelea na wajibu ulokuleta duniani.

    Ni takribani wiki 1 toka nitoe kitabu changu kiitwacho “THAMANI YA UHAI “. Nimejaribu kutangaza via WhatsApp na Facebook, ila sijapata hata mtu mmoja akihitaji kazi yangu.

    Hiyo imepelekea kujihoji maswali kadhaa ambayo nimeamua kukushirikisha wewe. Maswali hayo ni kama haya :

    1. Hivi, mtu anatakiwa atafute soko la bidhaa au huduma yake ndipo aitoe au kuifanya au afanye ndipo atafute soko? Kipi kianze na kipi kifuatiwe?
    2. Hivi, watu huwa wanataka confirmation toka kwa watu wengine ili wanunue bidhaa au huduma ya mtu?
    3. Ni njia zipi zinatumika kutangaza bidhaa au huduma ili mtu apate wateja wengi na kupata faida anayoitarajia?
    4. Kuna watu ambao wanataka uwape chochote kitu ndipo wakusaidie kutangaza biashara yako. Je, ni sahihi kufanya hivyo? Ni kweli inaweza kumhakikishia mtu kupata atakacho?

    Binadamu wengi ni vigeugeu, wanataka watumie vipaji vya wengine kujinufaisha wao. Hiyo ndio hofu yangu.

    Mmh!!! Hayo ndio maswali yanayotawala kichwani mwangu bila ya kuwa na majawabu ya uhakika. Natumaini mrejesho mzuri toka kwako.

    Ahsante sana na Mungu akubariki daima.

    Habari yangu ni njema kabisa. Kwanza ningependa kukupongeza kwa hatua kubwa uliyochukua ya kuandika kitabu, kukihariri mpaka kukichapa. Hii ni hatua ambayo hiwezi kufanywa na watu wengi. wengi wameweza kuwa na ndoto kubwa za uandishi ila kwa miaka mingi sana hawajawahi kuandika hata sentensi moja. hivyo, kwa upande wangu nipende kukupongeza sana kwa hatua hiyo ambayo wewe mwenyewe umeweza kuifikia. Kitabu ni kitu ambacho kinadumu vizazi hata vizazi. Watoto wako na wajukuu wako watanufaika nacho na kwa hakika wataona kwamba wewe ulikuwa mtu unayejituma.

    Shida ambayo unakumbana nayo wewe sasa hivi siyo kwamba upo peke yako. Wiki hii tu nimeongea na waandishi kama watatu na wote wanapitia kwenye changamoto kama hiyo hiyo ambayo wewe mwenyewe unapitia. Na hao ni wale tu ambao nimeongea nao. Na hiyo inaweza kukupa picha ni kwa namna gani ambavyo changamoto hizi zinawasumbua wengi.

    Na. pengine kuna wengine ambao wapo kwenye hali mbaya zaidi.

    Mitandao Ya Kijamii Inakuhadaa

    Najua kwamba wengi wanapenda kuitumia mitandao ya kijamii  na kwa wengi mitandao hii ya kijamii ni sehemu ya kuonesha umaarufu wao au namna ambavyo wanavyokubalika. Iila kukubalika huku ambako kunaonekana kwenye mitandao ya kijamii siyo kukubalika halisi kwenye maisha ya kawaida. Wengi wanaokubali kazi zako mtandao wanazikubali tu bila hata kujua kama wamezikubali.

    Ndio maana kuwa na wafuasi wengi kwenye hii mitandao siyo kigezo cha kuuza na wala kuwa na likes nyingi siyo kigezo cha kuuza zaidi. unaweza kuwa na wafuasi wengi ila bado ukawa huwezi kuuza bidhaa yako kwa watu wengi.

    Sasa Je, Usiitumie Mitandao Ya Kijamii?

    Hapana, endelea kuitumia mitandao ya kijamii. Ila sasa anza kuitumia kiusahihi kama ambavyo ninaenda kukuonesha muda siyo mrefu.

    MAJIBU YA SWALI LA KWANZA:Hivi mtu anapaswa atafute soko la bidhaa au huduma yake

    Zipo njia mbili za kuleta bidhaa au huduma sokoni ila njia nzuri ni kuleta bidhaa kulingana na kitu ambacho watu wanataka au wanapenda kulingana na changamoto walizonazo.

    Hii inakuwa ni rahisi kwako kutangaza bidhaa yako maana moja kwa moja bidhaa yako au huduma yako inakuwa inagusa tatizo ambalo watu wanalo. Wewe ukienda kwa watu hutatumia nguvu kubwa kutangaza bidhaa yako. Badala yake utakachofanya ni kuongelea tatizo ambalo watu wanalo na namna ambavyo litatatatuliwa.  Hakuna mtu ambaye ana tatizo ambaye angependa tatizo lake liendelee kuwepo mara zote.

    Watu wanapenda kupata huduma nzuri na za uhakika zinazotatua changamoto zao. Hii ni njia nzuri kuleta bidhaa sokoni na kuanza kuiuza siyo kwa kuuza bidhaa yenyewe bali suluhisho lililobebwa na bidhaa yako.

    Kwa hiyo, kifupi wakati unatengeneza bidhaa au huduma zako anzia kwenye akili ya mteja. Jiulize mteja anataka nini? na hapa kama mwandishi haupaswi kukaa chini na kujiuliza swali la aina hiyo. la sivyo utapoteza muda mwingi nab ado hutapata kitu cha maana.

    Ushauri wangu kwa waandishi wote ni huu:

    • Fungua blogu au tovuti. Na anza kuandika kwenye blog. Blg ni nzuri na haiwezi kulinganishwa na mtandao wowote ule wa kijamii. Haina ufanano wake.

    Mfano mzuri tu wa blogu ni kwenyekutunza kumbukumbu. Mimi kwenye blogu yangu nikitafuta makala niliyoandika mwaka 2016, hainichukui hata dakika mbili. ila nikiingia facebook leo hii nitafuta makala niliyoandika mwaka 2016, nitakesha.

    Lakini pia mitandao ya kijamii inapoteza vitu vingine baada ya muda. Leo hii mi

    Sasa blogu inakusaidia kupangilia kazi zako kwa uhakika. Mitandao ya kijamii imewekwa kwenye mfumo wa kuonesha vitu vya vinavyojiri sasa hivi (breaking news) ili kuwafanya watu waendelee kuitumia. Hivyo, vitu vya nyuma hawana muda navyo.

    Ila wewe kama mwandishi ukiandika kitu leo hii, kikasomwa na watu. kitu hicho hicho kinaweza kuwa na manufaa miaka mitano ijayo kwa watu wengine. Makala kama hii ninayoandika hapa, ikija kusomwa na mtu mwaka 2025 mwenye changamoto kama yako, bado itamfaa sana na bado atapata kitu cha kufanyia kazi. hivyo basi kama mwandishi kitu cha kwanza kabisa cha kukushauri. Toa uso wako facebook kwanza kwanza na utengeneze blogu. Blogu ni kitu kinachodumu. Siyo kitu cha siku moja tu.

    • Kitu cha pili, tengeneza email list. Hii ni orodha ya watu ambao wanakubali kazi zako kwa viwango vya juu kiasi kwamba wanwakuwa tayari kutoa baruapepe zao kwa ajili ya wewe kuwatumia mafunzo zaidi. hawa sasa ndio marafiki zako wa kweli ambao ukienda nao vizuri baadaye watakuwa tayari kukulipa kutokana na kazi zako unazofanya.

    Hivyo, badala ya kukazana kukuza wafuasi kwenye mitandao ya kijamii, kazana kukuza email list yako. Kitu hiki watu wengi hawakipendi kwa sababu email list siyo kitu kinachoonekana kwa watu. ukiwa na watu 1000 wamesubscribe kwenye email yako. Hawawezi kuonekana kwa mtu moja kwa moja labda tu wewe uamue kuwaonesha watu, na watu wengi wanapenda kufanya vitu ambavyo vinaonekana kama kuwa na followers kwenye hii mitandao ya kijamii.

    • Kitu cha tatu, usitafute watu au wateja unapokuwa na njaa ya kuuza kitabu chako. Badala yake onesha kwamba unawajali na kuwathamini siyo tu kwa fedha zao bali kwa asili unawajali. Kila mara toa mafunzo na andika kiasi kwamba ujenge uaminifu kwa watu ili ikifika hatua ambapo utakuwa na bidhaa ambayo unayotaka kuiuza. Uweze kuiuza kwako kirahisi maana tayari wameshajenga uminifu kwako. hakuna mtu anapenda kuiachia fedha yake ambayo ameitafuta kwa hali ngumu kwa namna rahisi sana. hakuna.
    •  
    • Kila mtu anaipenda fedha yake. Kwa hiyo lazima wewe uwe ttayari umewadhihirishia kuwa wanaweza kutoa fedha zao kwako bila kupoteza kitu ndipo wafanye hivyo. Hapo sasa ndio unaweza kujiwekea utaratibu wa kuandika kwenye blogu yako kila mara ili watu waweze kuwa wanafuatilia mafuzno yako bila ukomo.

    Sasa kadiri utakavyokuwa unaandika, kuna watu watakaojitokeza kuuliza maswali na kutokana na vitu ambavyo viwasummbua.  Haya ndiyo matatizo ambayo yanawakumba watu na hivyo vitabu au huduma unazoweza kutoa. Yaani, huhitaji kuumiza kichwa sana. Ukishaanza kuandika, maswali yanakuwa mengi. Na unaweza kuyajibu maswali haya kwa kuwaandikia watu vitbu maana maswali au changamoto nyingine zinajirudia mara kwa mara.

    MAJIBU YA SWALI LA PILI: Hivi watu wanapenda konfirmationa kutoka kwa watu wengine ili wanunue  bidhaa au huduma.

    Jibu ni ndio. TENA NDIO KUBWA. unavyoona Pepsi wanatangaza soda ya mkubwa wao akiwepo Diamond anakunywa mkubwa wao, siyo tu kwamba wanabahatisha. Hapo wanatumia umaarufu wake na kuwafanya watu wengine wakubali zaidi hiyo bidhaa.

    Kiukweli ni kwamba, hata wewe, mtu unayemkubali akikwambia kwamba kanunue kitu fulani badala ya kitu fulani, ni wazi kuwa utawahi kwenda kukichukua. Sasa saikolojia ya watu ndivyo inafanya kazi hivyo.

    Ukiweza kupata mtu wa kuwashawishi wengine wanunue bidhaa zako itakuwa vizuri. Ila kwa kuanzia fanya kama ambavyo nimekueleza. Tengeneza blogu, andika huko kwenye blogu yako, tengeneza email list ya watu ambao wanakubali kazi zako.

    Kisha baada ya hapo toa thamani kwenye kazi ambazo unafanya. ili hawa watu wachache ambao wameanza kufuatilia kazi zako waweze kuzisambaza kwa watu wengine zaidi na zaidi. na hivyo ndivyo confirmation yako inavyoanza.

    Hapa hauna excuse, ukitafuta njia ya mkato ya kuonekana maarufu mtandaoni, fanya hivyo. Ila ukiwa na ndoto kubwa na uandishi wako, basi utapaswa kufanya hivyo, miaka kadhaa ijayo hizi mbinu zitakuwa zimekusaidia wewe kusogea na kufika mbali sana.

    Tumia njia ya shuhuda. Waombe watu wachache ambao wamesoma kitabu chako wakupe shuhuda. Zitumie hizi shuhuda kwenye kutangaza chako zaidi. onesha kwamba mtu alikuwa na hali fulani kabla ya kusoma kitabu chako na sasa baada ya kusoma kitabu chako amepata matokeo fulani.

    Pia penda kuomba picha za watu wanaosoma vitabu. hii itawasaidia kuona watu wengine kuwa kitabu chako kimesambaa ila wao tu ndio hawajapata nakala ya kitabu chako. Hivyo, itakusaidia kuendelea kusogeza mauzo.

    MAJIBU SWALI LA TATU: Ni njia zipi zinatumika kutangaza bidhaa au huduma ili mtu apate wateja wengi na faida anayotarajia.

    Vitu vyote ambavyo nimekuwa nakueleza tangu mwanzo vilenga kukusaidia wewe kutangaza na kupata mafuriko ya wateja. Hivyo anza kwa kufanyia kazi hivyo kwanza.

    Pia nimeandaa audio yenye inayoeleza MBINU 23 ZA KUUZA. Na hii ni maalumu kwa ajili ya waandishi tu. naomba upate muda wako usikikilize hapa.

    Tatu. Usitangaze mara moja

    Kwa mbinu ambazo utazisikiliza hapo juu, usitangaze bidhaa yako mara moja au mara mbili. endelea kuitangaza mara kwa mara.

    Tafiti nyingi zinaoesha kwambna mtu anaposikia tangazo au kitu mara ya kwanza anakuwa hajali. Ila anapokisia kuanzia mara saba ndio anakuwa tayari kuchukua hatua.

    Pia andika kitabu kingine. kama mwandishi usiwe na kitabu kimoja. Ukiuza kitabu kimoja na mteja akanunua kwako, baada ya hapo unampoteza maana unakuwa hauna kitu kingine cha kumuuzia. Ila sasa ukiwa na vitabu hata viwili au vitatu maana yake mtu akinunua cha kwanza utaweza kumshawishi anunue na cha pili au ajiunge na huduma fulani au apate kozi fulani n.k.

    Kwa njia hiyo sasa ndio unakuwa unaanza kupata faida yako.

    Mambomengine nimeyaeleza kwenye audio hii hapa. ifuatilie vizuri ina mazuri kwa ajili yako.

    MAJIBU SWALI LA NNE: Kuna wAtu wanataka uwape chochote kitu   ndipo wakusaidie kuytangaza biashara yako. Je, ni sahihi kufanya hivyo, ni kweli inaweza kumhakikishia mtu kupata anachokitaka.

    Hapa nashauri kwanza uangalie na watu alionao mtu husika. Kama ana watu wanaoendana na wale uliowalenga ni sahihi kumlipa ili akutangazie bidhaa yako. Khayo ni matangazo ambayo unapaswa kufanya pia.

    Na hii ni njia n yingine ya confirmation pia. Mtu akisikia kutoka kwa yule anayefuatilia kuwa amesoma kitabu chako na kimemfaa basi atakuwa tayari nay eye kutoa fedha ili akipate. Ila kuwa makini, hakikisha kweli huyu mtu anao wafuasi na watu ambao wanaendana na bidhaa zangu. kisha mpe hela akutangazie. Ni vizuri ukianza kidogo ili uone mrejesho.

    Kuna vitu hapa ninataka uvijue pia

    Kwanza, watu wanaokwambia toa kitabu tutanunua mara nyingi huwa hawanunui

    Kuna watu wanaweza kukwambia kuwa tupo nyuma yako. Toa kitabu tutakisoma. Ila ukishatoa kitabu wanaingia mitini. Hiki kitu kisikukatishe tamaa, wewe weka nguvu na weka kazi. hakuna kazi ambayo huwa inapotea bure hata kidogo. unaweza usione matokeo kwa muda mfupi ila kwa muda mfupi matokeo yataonekana tu. endelea kupambana.

    Pili kuna vitabu vingi ambavyo havikufanya vizuri hapo mwanzoni ila sasa baadaye vikafanya kazi vizuri. Historia za waandishi wa aina hiyo ni nyingi tu. hivyo, na wewe endelea kukizania kitabu chako.

    Tatu, Tangaza kitabu kama chako kama vile hakuna maisha nje ya kitabu chako. Yaani, iwe kama vile kitabu ni tiketi ya kwenda mbinguni.

    Nne, jifunze copywriting. Huu ni ujuzi muhimu ambao utakusaidia sana kama mwandishi. Kama kuna kitabu kimoja cha copywriting utakachopaswa kusoma basi kiwe ni Cha How To Write A Copy That Sells Cha Ray Edwards

    MUHIMU SANA: Hakikisha umepata kitabu (ebook) cha JINSI YA KUWA MWANDISHI MBOBEVU NDANI YA SIKU 30 kwa elfu tano tu leo hii. Kitabu hiki kina mengi ya kukusaidia wewe. Rusha elfu tano sasa 0755848391 jina Ni GODIUS RWEYONGEZA. Baada ya hapo utatunitumia baruapepe yako au namba yako ya WhatsApp ili nikutumie kitabu.

    Karibu

  • Gharama Sita Unazopaswa kulipa ili kufikia ndoto zako.

    Ukiwa na ndoto kubwa unapaswa kuwa tayari kulipa gharama. Ni vigumu kufikia ndoto kubwa bila ya kulipia gharama ndoto zako.

    Na linapoongelewa suala zima la gharama basi watu wengi wanadhani gharama ni pesa peke yake.

    Hapana. Hizi hapa ni gharama sita unazopaswa kulipa ili kufikia ndoto zako

  • Uhuru wa kifedha ni nini?

    Uhuru wa kifedha ni pale ambapo unakuwa na fedha za kukutosha kwa kutumia kipindi fulani.

    Kama wewe matumizi yako kwa siku ni shilingi elfu tano. Ukiwa na milioni moja maana yake utakuwa na uhuru wa kifedha wa  siku 200.

    Ila ukiwa na shilingi milioni moja na matumizi yako kwa siku ni laki moja maana yake wewe una uhuru wa siku 10 tu.

    Uhuru kamili wa kifedha ni pale unapokuwa na fedha ya kukutosha wewe kutumia maisha yako yote hata kama hutafanya kazi.

    Unapokuwa na uhuru kamili wa kifedha, unakuwa hulazimiki kufanya kazi tena.

    Hii ndio kusema kwamba kama kwa siku unatumia shilingi elfu tano kwenye matumizi yako, wewe unakuwa na elfu tano na zaidi za kutumia maisha yako yote. Fedha inapaswa kuwa zaidi ya ile unayotumia kwa sababu kila mwaka kuna mfumuko wa bei unaotokea.

    Jinsi ya kutengeneza uhuru wako wa kifedha

    Ili kutengeneza uhuru wako wa kifedha, utapaswa kwanza kujua kiwango kamili cha fedha unachohitaji kupata. Kiwango kinapaswa kuwa kikubwa pengine kufikia  umilionea  au ubilionea.

    Mahitaji yanatofautiana kati ya MTU mmoja na mwingine.

    Baada ya hapo anza kuweka kazi ili ufikie uhuru kamili wa kifedha ambao kiuhalisia unahitaji muda kufikia.
    Unahitaji pia kuweka kazi ya kutosha
    Unahitaji kuzalisha thamani na kuwapa watu kile ambacho wao wanataka.

    umeshajiunga na THINK BIG FOR AFRIKA wewe?

  • KWA NINI UNAPASWA KUANZISHA BIASHARA

    1 zama zimebadilika

    Mambo yanabadilika aisee! Zamani ulikuwa hivi, ulitakiwa kwenda shule, kusoma kwa bidii ma baadaye ulikuwa na uhakika wa kupata ajira. Siku hizi mambo yamekuwa tofauti. Kuna watu wengi ambao wamehitimu na wapo mtaani ila kazi hawana. Kwa hiyo je, tuendelee kuwambia wanetu na washikaji zetu kuwa waende shule wasome kwa bidii ili waje wapate ajira. Inabidi tuseme ukweli kuwa ajira hakuna. Ila kuna njia mpya ya kuishi hapa mjini na njia hiyo ni kuanzisha biashara

    Iko hivi, biashara ndio njia pekee ya kufika mbali iliyobaki kwenye zama hizi.

    Kama unataka kufika mbali. Anzisha biashara.

    2. Hakuna ukomo wa kipato.

    Unapoajiriwa kuna na kiasi cha mshahara ambacho unapaswa kukipokea kila mwezi. Na kiasi hiki kinakuwa fixed. Kama ikitokea mshahara ukapandishwa basi ni baada ya muda mrefu wa wewe kuwa umefanya kazi.

    Siku hizi hata ule ushauri wa kwamba ukiongeza elimu utaongezewa mshahara haufanyi kazi tena.

    Ila kwenye biashara hakuna ukomo wa kipato hata kidogo, unaweza kuanzisha biashara na kuikuza biashara hiyo.

    Kadiri itakavyokua ndivyo utapata kipato zaidi. Hapo Sasa ndipo unapaswa kuhakikisha una biashara.

    3. Utajifunza mengi

    Biashara inakufundisha mengi. Ukiwa kweye biashara unalazimika kujua mambo mengi Kama mauzo, masoko, namna ya kuajiri, na mengineyo. Kiukweli kwenye biashara unapata kujifunza mengi, Mambo ambayo usingeweza kujifunza kama ungekuwa umeajiriwa.

    Maana ukiwa umeajiriwa  Mwajiriwa wako atakutaka ufanye kitu kimoja tu ambacho akiwa amelenga umletee matokeo fulani..

    4. Utafanya unachopenda

    Kazini utafanya kazi yoyote unayopangiwa. Ila biashara utafanya unayoipenda na hivyo muda wote na mara zote utakuwa unafanya unachopenda Unapokuwa kwenye biashara.

    Kuna tafiti zimeripoti watu wengi kuaga dunia siku ya jumatatu kwa sababu tu wanafanya kitu ambacho wao hawapendi.

    Tafitikama hizi hazipo kwa wafanya biasahra maana wengi wanafanya vitu ambavyo wao wenyewe wanapenda kufanya.

    5. Utakuwa mchango mkubwa kwa jamii

    Biashara yako itatatua matatizo ambayo yanawakumba watu, hivyo wewe utakuwa umewasaidia watu kupata suluhisho la tatizo lililokuwa linawasumbua.

    Ebu fikiria mtu kama Steve Jobs aliyegundua simujanja. Alitatua matatizo ya watu wengi wengi Sana.

    Leo hii tunaweza kuwasiliana na watu wa nje ya nchi bila tatizo au shida yoyote.

    Na ukiangalia biashara zote kubwa zinatatua tatizo fulani ambalo linawakumba watu.

    Google wanachofanya ni kutatua tatizo la watu kupata taarifa kwa wakati.

    Facebook wanachofanya ni kuunganisha watu

    6. Kujipangia muda wa kazi.

    Kuna watu ambao wanakuwa na uzalishaji wa hali ya juu asubuhi na wengine usiku. Ukianziaha biashara utafanya kazi kulingana na muda mbapo wewe unakuwa na uzaliahaji wa hali ya juu NB. Ni ukweli kwamba unapoanzisha biashara wewe ndiwe unakuwa bosi wako mwenyewe. Ila kiuhalisia utapaswa kuweka kazi hasa kwa siku za mwanzo za biasahra yako. Inachukua muda

  • Ndoto siyo ile unayoota ukiwa umelala, ndoto ni ile unayoona ukiwa macho

    Kama kuna kitu ambacho utapaswa kufanya maishani mwako na kikawa ni kitu chenye manufaa makubwa kwako ni kukaa chini na kuandika ndoto yako chini. Unaweza kuona kukaa chini kupanga vitu ambavyo ungependa kufikia maishani mwako kama ujinga, ila ukweli ni kwamba ukishindwa kupanga unakuwa unapanga kushindwa. Kiuhalisia muda ambao unatumia kupangani mdogo ukilinganisha na manufaa unayopata baadaye. Unaweza kutumia saa moja asubuhi kupangilia siku yako, ila sasa hilo likakufanya ufanikishe makubwa na wakati huohuo ukaepusha mambo mengine ambayo yangeweza kutokea kinyume na matarajio.

    Unaweza kutumia wiki moja kupangilia juu ya mwaka wako, ila hiyo wiki utakayoitumia ikakufanya uokoe mwaka wako. Kwa hiyo, usiogope kukaa chini na kupanga. Unapaswa kuwa na ramani kamili ya wapi ungependa kufika baada ya mwaka, baada ya miaka mitano, kumi, ishirini na hata zaidi. kiufupi linapokuja kwenye suala zima la kupanga weka mipango yako kama vile utaishi milele ila ifanyie kazi mipango yako leo kama vile hii ndio siku yako ya mwisho.

    Kazi ya kufanya wiki hii:

    Kaa chini na upangilie mambo ambayo ungependa kufanikisha baada ya miaka 20, kumi, mitano na mwaka mmoja.

    Kisha panga malengo ambayo utayafanyia kazi mwezi huu, wiki hii na leo hii n.k.

    Kumbuka kupanga muda wa wewe kwenda kupangilia ndoto zako za miaka 5, 10, 30 n.k. ni sehemu ya mpango unaopaswa kuuweka. Hivyo, chukua hatua sasa.

  • UPO TAYARI KUJIANDAA KWA MIAKA MINNE IJAYO?

    Mashindano ya olympiki ni miongoni mwa mashindano yenye nguvu sana. Yanapendwa na watu lakini pia washiriki wake huwa wanajiandaa kwa kipindi kirefu kabla ya mashindano yenyewe. Washiriki wa mashindano hayo wanajiandaa kila siku kwa kipindi cha miaka minne kwa ajili ya shindano ambalo linadumu kwa dakika kadhaa kisha kupotea. Na ndani ya dakika hizo ndipo mshindi huwa anapatikana na kupewa zawadi nono.

    Sasa swali langu kwako siku ya leo ni kwamba je, na wewe upo tayari kuweka kazi na juhudi kwa kipindi cha miaka minne, mitano sita mpaka kumi mfululizo kabla ya kupata matokeo na kula vinono ambavyo ungependa kupata? Unapaswa kuwa tayari kufanya hivi kwa sababu mafanikio makubwa huwezi kuyapata kwa usiku mmoja tu. Mafanikio makubwa ni matokeo ya vitu vidogo vidogo ambavyo unafanya kila siku vikiunganishwa kwa pamoja. Usiidharau siku moja na kukaa ukisubiri ufike mwisho wa mwaka ambapo utapata mafanikio makubwa, badala yake fanya kitu leo. Ukiunganisha hivi vitu vidogo vidogo, mwishoni mwa mwaka utakuwa umeweza kufanya makubwa.

    Kazi ya kufanya siku ya leo.

    Andika chini vitu vidogo ambavyo unaenda kufanya siku ya leo kulingana na lengo lako la mwaka huu. Kisha vifanyie kazi. endelea kufanya hivyo kila siku kwa siku 365 zijazo.

  • Kwa nini unapaswa kuanzisha biashara

    1 zama zimebadilika

    Mambo yanabadilika aisee! Zamani ulikuwa hivi, ulitakiwa kwenda shule, kusoma kwa bidii ma baadaye ulikuwa na uhakika wa kupata ajira. Siku hizi mambo yamekuwa tofauti. Kuna watu wengi ambao wamehitimu na wapo mtaani ila kazi hawana. Kwa hiyo je, tuendelee kuwambia wanetu na washikaji zetu kuwa waende shule wasome kwa bidii ili waje wapate ajira. Inabidi tuseme ukweli kuwa ajira hakuna. Ila kuna njia mpya ya kuishi hapa mjini na njia hiyo ni kuanzisha biashara

    Iko hivi, biashara ndio njia pekee ya kufika mbali iliyobaki kwenye zama hizi.

    Kama unataka kufika mbali. Anzisha biashara.

    2. Hakuna ukomo wa kipato.

    Unapoajiriwa kuna na kiasi cha mshahara ambacho unapaswa kukipokea kila mwezi. Na kiasi hiki kinakuwa fixed. Kama ikitokea mshahara ukapandishwa basi ni baada ya muda mrefu wa wewe kuwa umefanya kazi.

    Siku hizi hata ule ushauri wa kwamba ukiongeza elimu utaongezewa mshahara haufanyi kazi tena.

    Ila kwenye biashara hakuna ukomo wa kipato hata kidogo, unaweza kuanzisha biashara na kuikuza biashara hiyo.

    Kadiri itakavyokua ndivyo utapata kipato zaidi. Hapo Sasa ndipo unapaswa kuhakikisha una biashara.

    3. Utajifunza mengi

    Biashara inakufundisha mengi. Ukiwa kweye biashara unalazimika kujua mambo mengi Kama mauzo, masoko, namna ya kuajiri, na mengineyo. Kiukweli kwenye biashara unapata kujifunza mengi, Mambo ambayo usingeweza kujifunza kama ungekuwa umeajiriwa.

    Maana ukiwa umeajiriwa  Mwajiriwa wako atakutaka ufanye kitu kimoja tu ambacho akiwa amelenga umletee matokeo fulani..

    4. Utafanya unachopenda

    Kazini utafanya kazi yoyote unayopangiwa. Ila biashara utafanya unayoipenda na hivyo muda wote na mara zote utakuwa unafanya unachopenda Unapokuwa kwenye biashara.

    Kuna tafiti zimeripoti watu wengi kuaga dunia siku ya jumatatu kwa sababu tu wanafanya kitu ambacho wao hawapendi.

    Tafitikama hizi hazipo kwa wafanya biasahra maana wengi wanafanya vitu ambavyo wao wenyewe wanapenda kufanya.

    5. Utakuwa mchango mkubwa kwa jamii

    Biashara yako itatatua matatizo ambayo yanawakumba watu, hivyo wewe utakuwa umewasaidia watu kupata suluhisho la tatizo lililokuwa linawasumbua.

    Ebu fikiria mtu kama Steve Jobs aliyegundua simujanja. Alitatua matatizo ya watu wengi wengi Sana.

    Leo hii tunaweza kuwasiliana na watu wa nje ya nchi bila tatizo au shida yoyote.

    Na ukiangalia biashara zote kubwa zinatatua tatizo fulani ambalo linawakumba watu.

    Google wanachofanya ni kutatua tatizo la watu kupata taarifa kwa wakati.

    Facebook wanachofanya ni kuunganisha watu

X