Home


  • Namba Zetu Za Malipo

    Namba za malipo ya vitabu:

    Namba za lipa

    TIGO PESA: 19016638 Jina ni SONGAMBELE CONSULTANTS

    M-PESA: 5564517 jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

    Namba za kawaida

    AIRTEL MONEY: 0684408755
    TIGO PESA: 0655 848 392
    M-PESA: 0745 848 395

    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    NB: Kama namba ya malipo anatumiwa mtu ambaye yuko nje ya nchi. Iandikwe Kwa kuanza na +255

    Kwa hiyo namba zinazotumwa nje ya nchi zitakuwa
    Airtel money: +255 684 408 755
    TIGO PESA: +255 655 848 392
    M-PESA: +255 745 848 395

    KOTE Jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Kama malipo yatakuwa yanafanyika kupitia benki.

    Yafanyie kupitia

    1. CRDB BANK: 0150770710200
    2. NMB BANK: 22110047274

    Kote jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

  • Wasiliana na Godius Rweyongeza Sasa

    Habari yafuatayo ni mawasiliano Unayoweza kutumia kumpata GODIUS RWEYONGEZA

    Simu: +255 (0) 684408755

    Whatsap: +255 (0) 755848391

    Email: songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu vyake wasiliana Moja kwa Moja na +255 (0) 684408755 (more…)

  • Bilionea Ni Mtu Wa Aina Gani?

    Bilionea ni mtu anayemiliki rasilimali zenye thamani ya bilioni moja. Bilioni ina milioni elfu moja NDANI yake. Ubilionea hupimwa kwa thamani ya fedha ya nchi husika.

    Kutokana na thamani za fedha kutofautiana, kwa sasa kipimo kinachotumika kupima ubilionea ni dola ya Marekani.

    Kwa hiyo ukisikia wanasema fulani ni bilionea, ujue ni kwa thamani ya dola za Marekani.  Hii ndio kusema kwamba unaweza unaweza kuwa na rasilimali zenye thamani ya bilioni moja kwa fedha za Tanzania ila usiwe bilionea kwa sababu kipimo kikuu kinachotumika kwa sasa kupima ubilionea ni dola za Marekani.

    Bilioni moja ya shilingi za Tanzania kwa sasa ikiwekwa kwenye dola za Marekani ni sawa na dola laki nne na elfu thelathini. Kwa hiyo, ukiwa na bilioni moja ya kitanzania wewe siyo hata milionea!

    Bilioni moja ya kitanzania ikiwekwa kwenye dola za Marekani

    Ili uwe milionea kwa thamani ya dola unapaswa kuwa na rasilimali zenye thamani ya shilingi za Tanzania bilioni 2.3 

    Jinsi ubilionea unavyopimwa

    Ubilionea (UTAJIRI)= THAMANI YA RASILIMALI-MADENI YOTE.

    Wewe mwenyewe pia unaweza kupima thamani ya utajiri wako kwa kuchukua thamani ya rasilimali zakokisha ukatoa madeni yote unayodaiwa.

    Chukua thamani ya mali zako kwa sasa kama ungekuwa unaziuza kisha toa madeni.

    Je, bilionea ana fedha zote mfukoni?

    Kwa sasa hivi ubilionea unapimwa kwa kiwango cha thamani ya rasilimali ulizonazo baada ya kutoa madeni. Mabilionea wengi wamewekeza kwenye makampuni au rasilimali zisizohamishika (kama nyumba, ardhi,) au wamewekeza kwenye soko la hisa (hisa, hatifungani na vipande), hivyo bilionea hana fedha taslimu mfukoni mwake. Utakuta ana fedha za kawaida tu za kumtosha kufanya mambo yake yote muhimu ila hana bilioni zote za fedha taslimu mfukoni.

    Ila mali zake zote zikiuzwa kwa thamani ya wakati husika zina uwezo wa kufikia bilioni husika.

    HAKIKISHA UMESOMA KITABU CHANGU CHA MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA HATIFUNGANI NA VIPANDE ili ujifunze zaidi kuhusu UWEKEZAJI. Kupata kitabu hiki rusha elfu tano kwa namba 0755848391 jina ni Godius Rweyongeza. Utatumiwa ebook yako bila kuchelewa.

    Nawezaje kuwa bilionea?

    Watu wanakuwa mabilionea kwa kurithi
    Au kwa kupambana wenyewe.

    Kama huna sehemu ambapo utarithi ubilionea basi utapaswa kupambana mwenyewe.

    Ili kuwa bilionea utahitaji kuweka kazi sana na kwa muda mrefu. Utahitaji kujipa muda, maana ubilionea hauwezi kutokea ndani ya siku moja. Unahitaji muda, kazi, KUWEKEZA, kuanguka na kusimama tena.

    SOMA ZAIDI: KUTOKA SIFURI MPAKA UBILIONEA (Mbinu Kumi Zitakazokuinua Mpaka Ubilionea)

    Je, ni kazi gani inaweza kunipa ubilionea?

    Niwe tu mkweli, hakuna kazi inayokulipa mshahara inavyoweza kukupa ubilionea.
    Ili ufikie ubilionea utapaswa kuwa na biashara na (au) kufanya Uwekezaji.

    Ukiangalia orodha ya sasa ya mabilionea, wengi wanatoka kwenye sekta mbalimbali Ila Kuna sekta 11 zinajitokeza  kwa mabilionea wengi. Nashauri upate ebook yangu ya SEKTA 11 ZA KUTENGENEZA MAMILIONI YA FEDHA TANZANIA ili ujue maeneo sahihi unapoweza kuwekeza fedha zako. Haya ni maeneo mazuri pia inavyoweza kuanzisha biashara ya kukupelekea kwenye ubilionea.
    Ebook hii inapatika kwa elfu tano (5,000/-) tu. Rusha elfu tano (5,000/-) kwa 0755848391 jina ni GODIUS RWEYONGEZA ili nikutumie ebook hii.

    Ubilionea wa MO DEWJI

    Kwa Tanzania tunaye bilionea mmoja ambaye ni MO DEWJI. Huyu ndiye ana utajiri unaofikia bilioni moja na nusu (1.5) kwa dola za kimarekani. Fedha zake zikiwekwa kwenye shilingi za Tanzania anakuwa na zaidi ya trilioni 2.

    Hii ndio kusema  kama una mpango wa kufikia ubilionea, unapaswa kujipanga walau ufikishe uwekezaji wenye thamani ya shilingi trilioni 2.

    Upo hapo?

    Kwa hiyo kuwa bilionea ndio haiwezekani kabisa?
    Hapana. Siyo kwamba haiwezekani, ngoja nikupe mbinu ya kutengeneza kufikia ubilionea.

    Ukitengeneza bidhaa inayouzwa kwa dola moja moja. Ili uwe bilionea unapaswa kuiuza kwa watu bilioni moja na unapaswa usitumie hiyo fedha. Hahaha.

    Ukiuza bidhaa hiyohiyo kwa dola mbili basi utapaswa kuiuza kwa watu milioni mia tano (500).

    Ukiiunza kwa dola kumi maana yake utapaswa kuiuza kwa watu milioni mia.

    Ukiwa na bidhaa mbili za aina hiyo maana yake utapaswa kuziuza kwa watu milioni hamsini mara mbili. Ukiwa na bidhaa tatu, utaziuza kwa watu milioni 33.3 mara tatu.

    Kwa hiyo wewe, unaweza kuangalia namba ipi unaweza kupambania. Lakini pia soma hapa kuna mbinu zaidi

    Kama nilivyoeleza hapo mwanzo. Ubilionea siyo kitu cha kulala na kuamka ukiwa umekifia. Ni kitu kinachukua muda.

    Mabilionea wengi wamefikia kiwango cha ubilionea baada ya kufanya kazi kwa miaka 20 au zaidi.

    WARREN Buffet ni miongoni mwa mabilionea maarufu kwa sasa. Ila bilionea huyu anasemekana kuwa alianza kuwekeza akiwa na umri wa miaka 11 na aliendelea kuwekeza kila mara. Ila alikuja kuufikia ubilionea akiwa na miaka zaidi ya 50.

    Ebu fikiria hili na ujipange vizuri kwa ajili ya mchezo huu wa kuufikia ubilionea, Ila hili lisikukatishe tamaa.

    Kwa hiyo nikate tamaa ya kupambania ndoto yangu ya ubilionea kwa sababu unachukua muda kuufikia?

    Unachopaswa kufahamu ni kuwa miaka 20 inaenda kupita. Sasa ikipita ni au utakuwa umeitumia kwa manufaa au umeitumia hovyo. Kama umeitumia kupambania ndoto yako ya ubilionea utakuwa umepiga hatua kubwa sana hata kama utakuwa haujaufikia ubilionea, Ila utakuwa umefika mbali.

    Ila ukikata tamaa hata kabla ya kuanza. NI wazi kuwa hata umilionea utakushinda. Utashindwa hata kuwa lakionea, hahaha.

    JE, UNA MPANGO WA KUWA BILIONEA au kufikia ndoto yako kubwa?
    karibu ujiunge na kundi letu la THINK BIG FOR AFRICA.

    BONYEZA HAPA KUJIUNGA

    AU WASILIANA NAMI KWA 0755848391

    Makala nyingine zinazohusiana na hii

  • Cha Kufanya Pale Wenzako Wanapokuzidi Elimu, Kipaji, Ujuzi, Konekisheni n.k

    KIPAJI NI DHAHABU
    Rafiki yangu, nimeandika kitabu. Kinaitwa KIPAJI NI DHAHABU. Ili kupata kitabu hiki, wasialiana na mi kwa +255 684 408 755sasa

    Kama unajua Kuna wenzako wanakuzidi, elimu, kipaji, ujuzi, konekisheni n.k. unapaswa kupiga kazi kwa bidii.

    Yaani, wewe huna maarifa, ujuzi, kipaji halafu unabweteka. Inakuwa siyo poa hata kidogo.

    Moja ya kitabu ambacho nimewahi Kusoma kikanifungua sana ni kitabu cha 50CENT na cha Kobe Bryant.

    50CENT anasema hivi, unaweza kumzidi akili, unaweza kumzidi konekisheni, unaweza kumzidi kipaji na vitu vingine vyote, ila huwezi kumzidi kuchapa kazi kwa bidii.

    Jamaa anasema anachapa kazi kwa bidii. Na kuchapa kazi kwa bidii kumemfanya kuwa alivyo. Ameeleza haya kwenye kitabu chake cha HUSTLE HARDER, HUSTLE SMARTER

    Kobe Bryant mwenyewe kwenye kitabu chake cha THE MAMBA MENTALITY anasema alikuwa anaamka asubuhi na mapema kwa ajili ya kufanya mazoezi. Hapa alikuwa anaamka asubuhi na mapema kabla ya mchezaji mwingine yeyote.
    Na alikuwa anafanya mazoezi usiku wakati wenzake wote wanaenda kulala.

    Hii nayo naweza kuihusisha na Ile ya 50CENT ya kuchapa kazi kwa bidii.

    Niliwahi kusikia eti  Mohammed Ali alikuwa hana utaratibu wa kuhesabu pushap anazopiga mpaka pale anapojisikia kuanza kuchoka.

    Kama kweli unajijua kuna wenzako wamekuzidi kipaji, akili, konekisheni, uwezo, n.k chapa kazi kwa bidii. Mambo nengine yatajipanga

    Naomba kuishia hapo.

    Uchambuzi wa kitabu cha 50 CENT huu hapa

    Tazama video hii

    Ukitaka pia kujua uchambuzi wa kitabu cha Kobe Bryant basi utabonyeza hapa.

    Tazama video hii ya Kobe Brayant

    SOMA ZAIDI: 

    Najua kuwa ungependa kupata ushauri wa karibu zaidi moja moja kwa moja kutoka kwangu. Nitafute tuone ni lini nitakuwa na muda, ili nikupangie ratiba ya kuongea na wewe. Utalipia kiasi kidogo tu.

    Saa moja ni laki moja mazungumzo kwa njia ya mtandao.

    SAA MOJA NI LAKI MBILI NA NUSU MAZUNGUMZO YA ANA KWA ANA. Malipo yanafanyika kwanza, kisha unapewa tarehe (appointment) tutakapoweza kuongea

    Tumia namba ya simu +255 755 848 391 kuwasiliana nami.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza ambaye anaishi Morogoro nchini Tanzania.

    Unaweza kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza kupitia youtube channel yake hapa

    Kwa ushauri niandikie songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu ambavyo ameandika Godius Rweyongeza, wasiliana naye kwa +255 684 408 755 na orodha ya vitabu vyenyewe unaweza kuiona HAPA. Chagua unachopenda, kisha twanga,  +255 684 408 755

    Kujiunga na programu yetu ya uandishi. Wasiliana na +255 678 848 396

    For Consultation only: +255 755 848 391  au godiusrweyongeza1@gmail.com

    Asante.

    Kila la kheri
    Umekuwa nami .
    Rafiki yako wa ukweli Godius Rweyongeza
    0755848391
    Morogoro-Tz

  • Kitu Kitakachobadili maisha yako leo hii na hata milele

    Ninataka nikwambie kitu kitakachobadili maisha yako kuanzia leo hii na kuendelea.

    Nataka ufanye zoezi hili rahisi sana.

    Anza kwa kujiuliza vitu na shughuli zako zote unazofanya.

    Sasa angalia ni shughuli ipi ambayo ukiacha kuifanya na KUWEKEZA nguvu zako kwenye shughuli zinazobaki utapata matokeo makubwa sana.

    Kama ipo achana nayo. Kisha nguvu zako na muda wako uwekeze kwenye hizi shughuli nyingine ambazo zitakupa matokeo makubwa.

    Kuna kanuni inaitwa kanuni ya 80/20
    Kadiri ya kanuni hii ni kwamba asilimia 80 ya matokeo unayopata yanatokana na shughuli kidogo unazofanya ambazo ni sawa na asilimia 20.

    Kwa hiyo kama kila siku unajishughukisha na majukumu 10, ni majukumu mawili tu ambayo yanakupa matokeo makubwa.

    Kama kama Kuna kazi nyingi zinazokuingizia kipato, unapaswa kukaa chini na kutafakari. Kuna kazi chache zinazoingiza kipato zaidi. Ukiwekeza nguvu zaidi kwenye hizo chache utapata matokeo makubwa zaidi. Na hii ndio dhana nzima ninayotaka utumie kuanzia leo hii.

    Kila la kheri
    Umekuwa nami .
    Rafiki yako wa ukweli Godius Rweyongeza
    0755848391
    Morogoro-Tz

  • Hii Ndio Siri Kubwa itakayokusaidia kutengeneza fedha Nyingi

    Unataka kijua ni kwa namna Hani unaweza kutengeneza fedha Nyingi zaidi ya unavyotengeneza sasa hivi?

    Umechoka na kipato chalo cha Sasa, ungependa kutengeneza kipato kikubwa zaidi ya unavyotengeneza Sasa?

    Ndio Kuna njia. Na njia hii Ndio ninaenda kukueleza leo kwa umakini na kwa lugha rahisi sana.

    Kwanza Anza na kufuatilia hesabu za fedha zako zinazoingia na zinazotoka. Hakikisha unaandika kila fedha inayoingia na kila fedha inayotoka.

    Pili, hakikisha hautumii fedha zaidi ya Ile unayoingiza. Mtu ambaye anaingiza elfu kumi na kutumia elfu tisa mia tano, yuko kwenye nafasi kubwa ya kuwa tajiri ukilinganisha na mtu anayeingiza elfu 10 na kuitumia elfu kumi mia tano.

    Tatu, hakikisha kwa kila fedha inayoingia unatoa kiasi cha kuweka akiba. Usidharau hili hata kama fedha uliyopokea ni kiwango kidogo sana.

    Nne, Usikope kwa ajili ya matumizi yako binafsi. Kiufupi Usikope

    Tano, kuwa na ndoto kubwa za kufikia kifedha. Iwe ni kuwa milionea au bilionea au kupata uhuru wa kifedha.

    Sita,  wekeza fedha unayopata ili ikufanyie kazi. Ukifanya kazi ili upate fedha wewe ndiye unakuwa unaifanyia kazi fedha.
    Ukiwekeza fedha yako, wewe ndiyo inakufanyia kazi. Jitahidi ujue kitu hiki kidogo kinachoitwa UWEKEZAJI,  kitakusaidia sana.

    Kuujua UWEKEZAJI anza kwa kusoma kitabu cha MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE, rusha elfu tano tu ili upate kitabu hiki

  • Jinsi Ya Kutoa Na Kupokea Mrejesho

    Mrejesho ni miongoni mwa ujuzi muhimu sana unaopaswa kuwa nao.  Aidha iwe ni kutoa au kupokea mrejesho.

    Mrejesho ni kutoa au kupokea mapendekezo ya kumsaidia mtu kuboresha kazi yake.

    Kuwa mtu wa kupokea mrejesho na kuufanyia kazi na hasa pale unapokuwa na mrejesho unaoona kabisa kwamba unaenda kuwa mrejesho wenye manufaa kwako.

    Kwetu sisi kutoa mrejesho kwa watu wengine huwa tunaona ni Jambo la kawaida sana

    Kwa mfano kusema kwamba kocha wa timu ya Simba alipaswa kumweka mchezaji fulani uwanjani, inakuwa ni rahisi sana kwetu kusema hivyo.

    Ila wewe ukipewa mrejesho unakuta kwamba inakuwa ngumu, kwako kupokea mrejesho.

    Mrejesho unakufanya unaimarika.
    Siku nyingine ukiandika kitabu, mpe rafiki yako akisome; Ila mpe ambaye unajua atakupa mrejsho baada ya kukisoma.

    Ukiwa na logo ya biashara au kampuni unaweza kumpa mtu ili akupe mrejesho baada ya kuiona logo yako.

    Unaweza kuomba mrejesho wa kukusaidia wewe kutatua tatizo

    Mrejesho pia unaweza kuwa wa maoni ya mtalaam.

    Lakini pia mrejesho unaweza kuwa ni kwa ajili ya kupata maoni ya mtu mwingine mwenye mtazamo tofauti au anayetokea eneo la tofauti na unapotokea. Na hapa simaanishi kwamba kama wewe kwenu ni Tanga basi umpe mtu wa Mtwara, Bali kuwa kama wewe ni mwanasheria basi mpe daktari akupe mrejesho. Huyu atakupa mtazamo wa kidakatari kwenye kazi yako na hivyo kuiboresha.

    Kama wewe wewe ni mwalimu mpe mhandishi akupe mrejesho. Hapo utakuwa umepata mrejesho kutoka kwa mtu mwenye mtazamo tofauti na wewe.

    Mrejesho unaweza kutolewa kwako kwa njia ya sauti, video au maandishi

    Asante sana rafiki yangu.
    Umekuwa nami rafiki yako wa ukweli
    GODIUS RWEYONGEZA
    0755848391
    MOROGORO-TZ

  • Wanawake Watano Walioshindwa Karibia Kwenye Kila Kitu Na Bado Wakashinda Kwa Kishindo


    kuna usemi wa wahenga wetu wanaosema kuwa kukatika kwa jamvi sio mwisho wa mazungumzo. Jamvi linaweza kukatika na bado mazungumzo yakaendelea, tena vizuri tu.

    Sasa leo, natakata niongee nawe kuhusu hili suala na hasa wewe mwanamke.
    Leo nimekuandalia Makala maalumu, huku nikitaka uchukue masomo makubwa kutoka kwa wanawake walioanguka na bado wakainuka na kushinda kwa kishindo kikubwa. Lakini pia nataka nikwambie kwamba, ewe mwanamke, inawezekana.

    Makala za mwanzo zinazohusiana na hii ni Kutana Na Watu Watano Walioshindwa Karibia Kwenye Kila Kitu Na Bado Wakashinda Kwa Kishindo

    Sasa acha tuanze hivi:

    1. OPRAH WINFREY (67)
      Huyu ni mwanamke mwenye ushawishi mkubwa na hasa kwenye zama hizi. Historia yake ina mengi ya kusikitisha kuhamasisha. Alibakwa akiwa na umri wa miaka 9 tena na ndugu yake. na Kisha akapata mimba akiwa na umri wa miaka 14. alijifungua na mwane akaaga dunia ndani ya wiki mbili.
      kitu hiki kilimfanya Oprah aone kama vile maisha siyo fair hata kidogo. Hivyo akawa kama amekata tamaa na kuona hakuna usalama na hasa unapokuwa umezungukwa na wanaume.
      Lakini baadqye aliamua kuachana na hayo mawazo. Akaona kuwa inawezekana kufanya makubwa.
      akaingia kwenye sekta ya utangazaji na kuwa maarufu.
      ewe mwanamke, usikubali kuonekana wa kawaida. hata kama unapitia changamoto, fahamu kuwa changamoto zipo na huwa zinatokea kwenye maisha. Ila inawezekana wewe kuwa na maisha zaidi ya hayo.

    SOMA ZAIDI: BADILI MAJI KUWA DIVAI: Jinsi Ya Kuona Fursa Katika Changamoto Unazokutana Nazo Masihani

    1. JK. ROWLING
      Huyu ni mwandishi maarufu wa vitabu hasa vya watoto.
      Mwaka 1995 ndio aliandika kitabu Cha Harry Potter. Kitabu hiki kilikataliwa na wachapaji 12 tofauti.
      Mchapaji mmoja tu ndiye aliyekikubali na hata baada ya kukikubali alimwambia Rowling kwamba utafute kazi nyingine maana, hutaweza kupata maisha mazuri kupitia uandishi wa aina hii.

    Ila hali ilikuwa tofauti baada ya kitabu kuchapwa. kiliuza nakala nyingi mpaka kufikia mwaka 2004, Rowling akawa bilionea wa Kwanza kupata ubilionea kupitia uandishi.

    Na mpaka leo hii yeye bado ni mwandishu anayelipwa sana duniani.

    1. BARBARA CORCORAN

    Huyu mwanamama anaeleza jinsi alivyoolewa na mme wake. Wakawa wamefungua kampuni na baadaye wakaachana, chanzo kikubwa kikiwa ni mme wake kumpenda karani wa kampuni yao.

    walivyoachana huyu mwanamama aliondoka ka asilimia 49 ya kampuni yake. Aliondoka wafanyakazi baadhi na hela dola elfu moja.

    wakati wakaachana mme wake alimwambia kuwa hutaweza kutoboa bila ya mimi.

    hicho kitu kilimpa hasira na akaamua kuwa kwa vyovyote vile lazima tu atoboe. na kweli alitoboa. aliweza kugeuza dola elfu moja kuwa mabilioni ya fedha.
    kitabu chake cha SHARK TALES kinaeleza alivyobadili hiyo dola elfu moja kuwa mabilioni.

    1. HELLEN KELLER
      Huyu alipata upofu akiwa na umri wa miezi 19 tu.
      Ila maisha yake alivyoyaishi alifanya makubwa kiasi kwamba dunia nzima inamkumbuka mpaka leo hii.

    Alikuwa mtu wa Kwanza mwenye ukipofu kupata shahada.
    alikuwa mkufunzi
    alikuwa mwandishi wa vitabu, kutaja ila machache.

    1. ARIANNA HUFFINGTON

    Huyu mwanamama ni mwandishi wa vitabu na mwanzilishi wa jarida la HUFFINGTON post.
    Kitabu chake cha pili kilikataliwa na wachapaji 36 kabla ya kuchapwa.

    kwa sasa ameandika vitabu 15.

    Rafiki yangu, hao ndio wanawake watano wa nguvu, chukua somo kwa mmoja wao na lifanyie kazi.

    Kila la kheri.
    Ni mimi rafiki yako wa ukweli
    Godius Rweyongeza (Songambele)
    0755848391
    Morogoro-Tz
    Wewe ni zaidi ya ulivyo

    NB. Ofa vitabu vyangu kwa bei ya ofa: kwa punguzo la nusu bei kipindi ndani ya siku hizi mbili tu. Yaani, leo na kesho. Hii ni ofa ya siku ya wanawake.

    Chagua kitabu hapa. Ofa hii inahusu vitabu vya softcopy tu.

  • Nguvu Ya Jina (jina la biashara, jina lako na Jina la brand yako)

    Bidhaa mbalimbali huwa zinatambulika kwa majina. Kila mtu huwa anatambulika kwa jina lake. Hata hivyo iko wazi kuwa baadhi ya majina yakitajwa, yanakuwa na nguvu ukilinganisha na majina mengine.

    Kuna kampuni ikizindua bidhaa fulani, watu wataikimbilia kuinunua na kampuni nyingine inaweza kuzindua bidhaa ya aina hiyohiyo ila watu wakawa hawajaikimbilia. Na ukifuatilia kiudani zaidi unaweza kugundua kuwa kilichowafanya watu waende kununua bidhaa kwenye kampuni A badala ya kampuni B, unakuta sio ubora wa bidhaa bali ni jina.

    Kitu kama hiki hapa tunaweza kukiona kwenye zama hizi hapa. Kwa mfano, kuna watu wanakimbilia kununua simu za aina fulani sio kwa sababu ya ubora wake, ila kwa sababu ya jina lake. na wengine wanahakikisha kwamba wana bidhaa zote za kampuni husika bila kubakiza hata moja. Utasikia mtu anakwambia kwamba mimi kampuni fulani ikitengeneza bidhaa yoyote ile lazima tu niinunue tu. Kinachomsukuma ni JINA.

    Asikudanganye mtu, jina lina linaweza kukufanya uuze au usiuze. Jina linaweza kukufanya upokelewe vizuri sehemu fulani au usipokelewe.

    Kitu muhimu cha kufahamu ni kuwa, watu wananunua jina. Kama huamini toa wiki moja ambayo utaenda kwa watu ukijitambulisha kama YUDA ISIKARIOTI, halafu uone jinsi watu watakavyoupokea huo utambulisho wako!

    Pale utakapotakiwa kuchagua jina la biashara yako, kampuni, bidhaa au hata tovuti yako mtandaoni, usikurupuke tu kutoa jina. Jipe muda wa kufikiri kwa kina ili upate jina ambalo ni zuri. Wahaya wana methali inyosema kuwa eibara libi, liita nyinalyo. Ikimaanisha jina baya huua mtoaji wa jina hilo.

     Kwa hiyo, kama unataka kuua bidhaa yako au biashara yako toa jina baya na kama unataka kuijenga biashara yako ipe jina zuri. Kwenye kitabu changu cha Mambo 55 Ya Kuzingatia Kabla Ya Kuanzisha Biashara, nimeeleza kiundani juu ya hatua za kuchukua kwenye kupata jina bora la biashara yako. Tuma elfu tano kwa 0755848391 kupataa kitabu hicho.

  • Kitu Cha Kufanya Ndoto Yako Inapohusisha Watu Wa Nje

    Kuna nyakati ndoto na malengo yako yanahusisha watu wa nje. Yanahusisha taasisi za serikali, makampuni fulani au hata mataifa mengine ambayo yana taratibu zake, utendaji kazi wake na kila kitu cha kwake. Watu hawa utakuta kwamba wana njia zao kutenda na kushughulika na vitu vyao katika namna ambayo inaweza isiwe rafiki kwako. Kwa mfano, unaweza kuwa na haraka ya kusajili kampuni yako au chuo chako, ila ukakuta kwamba taasisi inayo husika haioni umuhimu wa kukufanyia kile unachohitaji kwa wakati na wakati mwingine ukasumbuliwa bila ulazima wowote.

    Unaweza ukawa unahitaji leseni yako ya udereva ili ikusaidie kutimiza jambo fulani ulilonalo kwenye mpango wako na malengo yako, ila ukakuta kwamba watu wanaohusika hawana haraka na wala hawajali kukupatia leseni yako kwa wakati hata kama umekidhi viwango vyote ambavyo unastahili kuwa navyo.

    Katika hali ya kawaida watu wa aina hii wanakukwamisha na hata kukufanya ushindwe kufanikisha vitu vyako kwa wakati. wakati mwingine unaweza kuwa hata na watu ambao umewaajiri ila wakawa pia hawaelewi kile unachotaka na hivyo kuzidi kukudidimiza. Sasa zifuatazo ni njia za kukusaidia wewe kuwasiliana na watu wa aina hii ili wakufanyie mpango wako kwa wakati;

    Kwanza, waeleze watu hao mpango wako mkubwa ambao unataka kuufanyia na muda ambao ungependa mpango huo uwe umetimia.

    Ukiwaeleza watu mpango wako ambao ungependa ufanyiwe kazi ni wazi kuwa watu hao wanakuwa tayari kusaidia na kushirikiana na wewe. Muda mwingine badala ya kuonesha kwamba ndoto au lengno ni la kwako binafsi, unapaswa kulionesha kama vile lipo kwa ajili ya wakusaidia awao pia. Wape na wao lengoambalo watashirikiana na wewe kulifanyia kazi.

    Hiki kitu kimenifanya nikumbe stori moja ya namna watu walivyopunguza idadi watu waliokuwa wanakojoa juu chooni. Ni kwenye uwanja wa wakimataifa wa…

    Kulikuwa na tatizo kubwa hasa kwenye choo cha wanaume, ambapo mara nyingi walikuwawnakojjoa juu ya choo obadala ya kukojoa ndani. Sasa kilichofanyiaka ilikuw ani kuchora kitu kilichoonekana kama nziri kwenye sinki la choo.

    Kila aliyekuwa anaingia kwenye kile choo alikuwa anatamani kumwongooa yule nzirr kwenye sinki na hivyo aakawa anamlenga. Baada ya muda idadia ya wtu waliokuw wanakojoa juu ya choo walikuw wamepungua.

    Pili fahamu kuwa hauko kwenye mchezo huu kwa muda mfupi, ni mchezo ambao unaenda kuucheza kwa muda mrefu. Hivyo wewe kama wewe utapaswa kwenda vizuri, usibabishe fujo, usimdhuru mtu wa kudhulumu mtu kwa maana haufanyii hiyo ndoto kwa ajili ya kupata hela ya kula leo hii na kesho yake utaenda eneo jingine. Kwa ko hicho ni kitu ambacho unakifanya kama sehemu ya au kifanikiwe au ufe ukiwa unapambana nacho.

    Nne, fahamu kuwa watu wote wanaostahili kulipwa stahiki zao, utapaswa kuwalipa stahiki zao kwa wakati bila ya kuchelewa. na hawa watu ni wazi kuwa siyo tu kwamba utataka wakufanyie kazi kwa siku moja au mbili, hawa watu unaweza utawahitaji leo na kesho.

    Tambua mchango wa kile mtu ambaye anahusika kwenye kufanyia kazi ndoto yako na hakikisha huyo mtu anajua kwamba, yeye yana mchango kwako. hata hivyo, uwe makini watu wasije wakatumia hicho kipengele kwa ajili ya kukunyanyasa hasa wakijua kwamba mchango wao ni wa kipekee.

    Wafanyakazi wako wajue kuwa ni watu wa muhimu kwenye kazi au biashara yako, ila pia wajue kuwa wakienda kinyume na taratibu hutaweza kuwavumilia.

    Fahamu kuwa wewe unaweza kushinda kwa kufanyia kazi ndoto yako na mwingine akashinda kwa kuifanyia kazi ndoto yake. Usitake kabisaa kumuumiza mtu ili wewe uende mbali zaidi. badala yake penda kuwainua wengine maana kadiri wengine wanavyoinuka na wee unazidi kuinuka. Ndio maana mimi napenda nikuelimisha haya mabo uyafahamu maana nafahamu kuwa wewe ukiinuka, na mimi nitaweza kuinuka.

    Tafuta mtu wa kushughulika na changamoto nyingine ili wewe uwekeze nguvu zako kwenye mambo ya maana zaidi.

    Pia wenye ulimwengu wa sasa hivi ndoto yako inapasawa kuwekwa mtandaoni, sasa unapaswa kupambana na kuiweka

    umekuwa nami rafiki yako wa ukweli

    Godius Rweyongeza

    0755848391

    morogoro-Tz

  • Vitu Vya Kuepuka Ili Uweze Kuishi Maisha Mazuri

    Kwanza kabisa, hakikisha unaepuka kulalamika. Ukilalamika unakuwa unawanufaisha wale ambao wanakusikia.

    Epuka kufuatilia maisha ya watu wengine

    Epuka kutumia fedha yako yote ulyonayo bila kuweka akiba

    Epuka kukopa. Tumia dfedha yako

    Epuka kutumia fedha zaidi ya kipato chako

    Epuka kumezwa na mitandao ya kijamii

    Epuka kuianza na kuimaliza siku yako bila ya kuwa na malengo ambayo unayafnyia kazi

    Epuka kuishi bila ya ndoto kubwa

    Kila la kheri

  • Anza Na Kina Kile Ulichonacho

    Kabla hujasema kwamba haiwezekani na wala siwez i kufanya kitu fulani, jihoji kiundani na uangalie ni kitu gani unaweza kufanya. Kuna vitu vingi unaweza vizuri tu

    Kabla hujasema kwamba, sina cha kuanza nacho, angalia vizuri ikwenye mazingira yako ni kipi ulicho nacho ambacho unaweza kuanza kutumia sasa hivi. Kuna vitu ulivyo navyo ambavyo unaweza kuanza kutumia sasa.

    Kikubwa ni wewe kuabngalia vizuri rasailimali ulizonazo na kuhakikisha kwamba unazitumia vizuri.

    SOMA ZAIDI: MITAJI 8 ILIYOKUZUNGUKA NA JINSI YA KUITUMIA

    a365: ANZA KUTUMIA KILE ULICHONACHO

X