Home


  • Namba Zetu Za Malipo

    Namba za malipo ya vitabu:

    Namba za lipa

    TIGO PESA: 19016638 Jina ni SONGAMBELE CONSULTANTS

    M-PESA: 5564517 jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

    Namba za kawaida

    AIRTEL MONEY: 0684408755
    TIGO PESA: 0655 848 392
    M-PESA: 0745 848 395

    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    NB: Kama namba ya malipo anatumiwa mtu ambaye yuko nje ya nchi. Iandikwe Kwa kuanza na +255

    Kwa hiyo namba zinazotumwa nje ya nchi zitakuwa
    Airtel money: +255 684 408 755
    TIGO PESA: +255 655 848 392
    M-PESA: +255 745 848 395

    KOTE Jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Kama malipo yatakuwa yanafanyika kupitia benki.

    Yafanyie kupitia

    1. CRDB BANK: 0150770710200
    2. NMB BANK: 22110047274

    Kote jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

  • Wasiliana na Godius Rweyongeza Sasa

    Habari yafuatayo ni mawasiliano Unayoweza kutumia kumpata GODIUS RWEYONGEZA

    Simu: +255 (0) 684408755

    Whatsap: +255 (0) 755848391

    Email: songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu vyake wasiliana Moja kwa Moja na +255 (0) 684408755 (more…)

  • Kinachokwamisha wewe kufika mbali.

    Umekuwa unakwama kufika mbali kwenye maisha na kushindwa kufikia ndoto zako kwa sababu tu hujawa na ndoto  kubwa kiasi cha kutosha. Maneno ya busara yanasema hivi,

    unapaswa kulenga kuifikia nyota kiasi kwamba hata ukishindwa uufikie mwezi.

    Sasa ebu fikiria hili, wewe ndoto yako siyo kubwa kiasi cha kulenga kuifikia nyota badala yake umelenga kufika kileleni mwa mti, unadhani ukishindwa utaangukia wapi? Si utaangukia baharini?

    Kuanzia Leo hii weka ndoto  zako kubwa Kisha anza kuzipambania.

    Lakini pia labda niseme ndoto kubwa ndio njia pekee iliyobaki ya kuweza kuishi vizuri hapa duniani. Ndio hakuna njia nyingine .

    Kama kikiwekwa chakula mezani na chakula kikawa ni kidogo, viumbe wenye nguvu ndio watakula na wale ambao hawana nguvu wataishia kujilamba midomo tu. Hali hiyo ikiendelea kwa muda mrefu ndio sasa unakuta viumbe ambao hawana nguvu wanakufa, wanabaki wale wenye nguvu tu.

    Kwenye zama za sasa kuwa na ndoto kubwa limebaki kuwa ni hitaji la lazima (basic need).

    Kwa nini? Kwa sababu ndoto kubwa ndiyo njia pekee ya wewe kuendelea kuishi kwenye ULIMWENGU wa leo.

    Ebu wewe chukulia watu wote ambao unawafahamu wamefanya makubwa kwenye zama za sasa. Orodhesha hata watu 10 unaowafahamu. Hakuna hata mmoja mwenye ndoto ndogo au ndoto za kawaida. Wote wana ndoto kubwa.

    Chukulia mtu kama,
    Elon Musk na ndoto yake kubwa ya kwenda sayari za mbali.

    Kwenye ulimwengu wa sasa kama unataka kufanya makubwa na basi kuwa na ndoto kubwa, Kisha zipambanie kila kukicha.

    Kuwa na ndoto za  kuufikia uhuru wa kifedha
    Kuwa na ndoto za kukuza kipaji chako kimataifa
    Kuwa na ndoto kubwa haswa; Kisha Anza kuzifanyia kazi.

    Rafiki yangu, kiufupi kuwa na ndoto kubwa.

    Nakumbuka kuna mtu aliwahi kusema kuwa rafiki zangu ni watu wenye ndoto kubwa. Siwapendi wenye ndoto ndogo. Binafsi na mimi siwapendi wenye ndoto ndogo. Kama wewe una ndoto ndogo, bora tu usiwe rafiki yangu maana hata utanikwamisha mimi.

    Utatoa nguvu hasi kwangu. Mimi nataka marafiki wenye ndoto kubwa na ambao wameamua kuwa watazifanyia kazi ndoto zao kubwa au la watakufa wakiwa wanazipambania.

    Kina kila kitu, unachohitaji kujua kuhusu ndoto zako. Leo hii lipia 19800 upate nakala ngumu au elfu 10 upate softcopy.

    Changamka sasa.

  • Usidharau fedha hata kama ni kidogo

    Leo nataka ni kwambie kwamba fedha siyo kitu ambacho unapaswa kudharau.

    Unaweza kukuta mtu ana fedha kiasi fulani ila akawa anakidharau.

    Na hata akakitumia hovyo, ila unachopaswa kufahamu ni kuwa usidharau fedha.

    Hivi hujawahi kujiuliza kwa nini Mo Dewji na utajiri wake wote kwa nini bado anaendelea kutengeneza hadi viberiti?

    Kiberiti kimoja huku mtaani tunakinunua shilingi mia moja, ambayo kiuhalisia ndiyo fedha ndogo. ila jamaa na ubilionea wake wote bado anatengeneza viberiti. Kiufupi Mo anauza viberiti.

    Na yeye hadharau fedha ndogo kwa sababu anajua kwamba fedha haina udogo, ubilionea haukamiliki bila ya kiasi hicho kidogo.

    Sasa kazi ni kwako kuanzia leo hii kuhakikisha kwamba unaanza kujenga nidhamu kwa fedha yako hata kama ni kidogo.

  • KIPAJI NI DHAHABU-2: wekeza kwenye uwezo wako na siyo kwenye udhaifu wako

    Kila mtu kuna eneo ambalo yuko vizuri.  Ukishaligundua hilo eneo ndilo sasa unapaswa kulipa nguvu na kuachana na udhaifu wako. Ukikazana kuboreaha udhaifu wako huwezi kufika mbali hata kidogo kwenye maisha.

    Ukiwekeza kwenye uwezo wako zaidi na kuufanyia kazi, utakuwa bora zaidi.

  • Kutoka Kwenye Ajira Mpaka Kujiajiri: HATUA 09 Za Kufuata Kutoka Kwenye Ajira Mpaka Kujiajiri

    Leo nataka nikupe mwongozo muhimu ambao unaweza kuutumia katika kuanzisha biashara hasa ukiwa umeajiriwa. Ebu fikiria kwamba umeajiriwa leo hii na unataka uanzishe biashara yako ili ujiajiri.

    Huu mwongozo ninaoenda kukupa hauna mfanano wake, kiufupi hakuna mtu mwingine ambaye amewahi kukwambia kitu Kama hiki, na wala hata hamna kitabu wala ebook ya kununua ambayo imefunguka kiundani kuhakikisha inakupa mwongozo sahihi kama huu.

    Ukiufuata huu mwongozo utafika mbali. Ninachotaka ufahamu ni kwamba, kujiajiri siyo rahisi hata kidogo. Ndio maana watu wengi ambao wanafundisha kujiajiri wenyewe wameajiriwa.

    Wengi wanaogopa sana kutoka kwenye ajira ambayo wameizoea na ambayo inawapa kipato cha uhakika kila mwishoni mwa mwezi mpaka kujiajiri na kumiliki biashara inavyoweza kujiendesha yenyewe na kuwapa kipato cha uhakika . Lakini inawezekana.

    Sasa zifuatazo ni hatua za kufuata

    HATUA YA KWANZA: Anza kwa kutengeneza ndoto kubwa ambayo ungependa kuifikia hapo baadaye

    Hapa unapaswa kujua kwa uhakika kuwa ungependa kuwa nani hapo baadaye. Ni kweli Sasa hivi upo ajirani, ila picha yako ya hapo baadaye ni ipi. Ukiwa na maono au ndoto kubwa ni rahisi kupitia hatua nyingine zinazofuata kwa sababu tayari una ndoto kubwa ambayo inakusuma. Hii ndio picha yako na huo ndio mwongozo wako wa uhakika ambao unataka ufuate.

    Sasa ebu jiulize nataka kufika wapi miaka mitano au kumi ijayo? Kaa chini ujipe muda wa kufikiri na kuandika chini ndoto yako.

    Pasipo na maono watu huangamia. Kitu cha kwanza kitakachokuangamiza wewe ni kukosa ndoto kubwa. Siriazi, unahitaji ndoto kubwa.

    Halafu kwa sababu nataka nikusaidie kwa ukamilifu ngoja nikwambie kitu hiki, hakikisha unajipa muda wa kuwa peke yako wa kukaa chini na kutafakari MAISHA YAKO. KAMA HUWEZI KUPATA UTULIVU KATIKA ENEO UNAPOKAA BASI TAFUTA ENEO UTAKAPOPATA UTULIVU NA KUFIKIRI KUHUSU MAISHA YAKO BILA YA  BUGHUDHIWA.

    Unaweza hata kuamua kwenda kwenye hoteli na kununua maji au juisi ili tu upate mazingira tulivu yatakayokusaidia kufikiri na kujenga ndoto yako kubwa.

    Hii ndio hatua ya kwanza. Ifanyie kazi hii kwanza.

    HATUA YA PILI: ANZA KUWEKA AKIBA

    Hiki ni kitu ambacho unapaswa kukifanyia kazi pia. Sasa tayari una ndoto kubwa ya kujiajiri hapo baadaye, Anza kujenga Tabia ya kuweka akiba. Kwa haraka wewe utahitaji kuweka akiba za aina mbili. Aina ya kwanza ni akiba  yako ya dharula. Hii ni Ile akiba ambayo inaweza kuendesha maisha yako kwa miezi isiyipungua sita endapo maisha yako yatapatwa na changamoto yoyote.

    Unapaswa kuwa na aina hii ya akiba. Akiba ambayo endapo chochote kitatokea kwenye ajira yako basi utaweza kuendesha maisha yako bila hofu.

    Aina ya pili ya akiba ni akiba sasa kuanzisha biashara. Nakuahauri Leo ukatengeneze akaunti yako ya benki ili uanze kuweka akiba. Kama ulikuwa hujaanza hakikisha hili suala unalipa kipaumbele kwenye maisha yako kuanzia sasa.

    Kuna vitu au Tabia ambazo ulikuwa nazo kabla ya kufikiria kuanzisha biashara. Ila sasa hizi tabia unapaswa kuachana nazo. Ebu kaa chini na ufikirie juu ya tabia gani ambazo ulikuwa nazo ila siyo nzuri. Vitu kama kunywa pombe, kupoteza muda mtandaoni, kununua vitu ambavyo wewe mwenyewe huhitaji. Hivi ni vitu ambavyo utapaswa kuachana navyo.

    Ngoja nikwambie kitu, hivi vitu ulikuwa unavifanya wakati umeajiriwa a kwenye ULIMWENGU wa kujiajiri vitakukwamisha sana. Yaani, huwezi kuendelea kupenda vitu vinavyokupa raha ya muda mfupi na bado ukapenda kujiajiri. KUJIAJIRI MAANA YAKE UMEAMUA KUWEKEZA MUDA WAKO, ELIMU YAKO, KATIKA BIASHARA AMBAYO UTAIKUZA KWA AJILI YA MANUFAA YA SASA NA  baadaye.

    Wachezqji wa mpira wa miguu kuna vyakula hawali, kwa sababu tu ni wachezaji wa mpira wa miguu. Wengine wakila hivyo vyakula haviwadhuru ila wachezaji hawatakiwi kwa sababu wenyewe wamechagua aina fulani ya maisha. Wewe pia Kuna aina fulani ya maisha ambayo unapaswa kuishi. Kuna vitu fulani ambavyo wengine wanafanya ila kwa wewe mwenye ndoto ya kujiajiri hupaswi kuvifanya. Kwa wengine hivyo vitu ni sawa tu Ila kwako siyo sawa.

    Na Kuna vitu ulikuwa hufanyi unapaswa kuanza kuvifanya, vitu kama kupenda kysoma vitabu, kutunza afya yako n.k.

    Kama unataka kujiajiri haswa unapaswa kupenda kujifunza.  Kujifunza kunahusisha vitu vingi kama kusoma vitabu, kuangalia wengine wanavyofanya biashara yao na kupata funzo ambalo na wewe unaweza kulifanyia kazi kwenye biashara yako, kuwauliza wafanyabiashara wengine wanavyofanyia kazi, kuongea na wateja ili ujue wanachotaka wao.

    Kiufupi unapojiajiri kujifunza kwako hakupaswi kuwa na ukomo. Mjasiriamali wa kweli huwa hana siku ya likizo. Kwake kila siku ni siku ya kujifunza kitu kipya ambacho atakifanyia kazi kwenye biashara yake.

    Kupitia kujifunza utaweza kujua washindani wako wana nini na wewe kitu gani hauna. Kupitia kujifunza utapata kuona mpenyo ulipo na jinsi ambavyo unaweza kuutumia  KATIKA kuanzisha biashara mpya.

    Wafanyabiashara wakubwa wote ni  wasomaji wazuri. Bill Gates anasemekana anasoma vitabu 52 kwa mwaka.
    WARREN BUFFET HUWA ANATUMIA ASILIMIA 80 YA MUDA WAKE KWENYE KUSOMA. Kiukweli kwa wafanyabiashara wengi kusoma kwao ni  nguzo muhimu ya kukuza biashara zao.

    Elon Musk ni bilionea mkubwa kwa sasa akiwa ni tajiri nambari moja duniani. Ila historia ya huyu jamaa ni historia yenye mafunzo makubwa ndani yake. Ameanzisha na mpaka sasa anaendesha BIASHARA ambazo hapo mwanzoni alikuwa hajui chochote kuhusu hizo biashara, ila sasa hivi anaziendesha vizuri na kwa manufaa makubwa Sana. Unajua kwa nini? Kwa sababu ya tabia yake ya kupenda kujifunza. Yaani, kujifunza hakujawahi kumwangusha mtu. Ebu na wewe kujaribu.

    Hapa Sasa tunakuja kwenye kipengele kingine muhimu sana kwako. Sasa ni muda wa kujua Aina ya biashara ambayo unaenda kuanzisha. Unahitaji wazo la biashara.
    Je, unapataje wazo la biashara?

    Wazo lako la biashara linaweza kutokana na  ujuzi wako au taaluma yako. Tuseme kwa mfano wewe ni mwanasheria, unaweza kutumia ujuzi wako wa sheria kwa ajili na kuanzisha biashara inayoendana na ujuzi wako.

    Au labda wewe ni dakatarj. Unaweza kuanzisha biashara inayoendana na ujuzi wako.

    Kama una uzoefu KATIKA eneo au kitu fulani unaweza kuanzisha biashara kwenye hicho kitu pia.

    Unaweza pia kutumia wazo lililopo kwa Sasa kuanzisha biashara yako. Kuna biashara ambazo watu wengine wanafanya na wewe unaweza kufanya biashara kama hiyo, Ila sasa zamu hii kwa ubora au kwa kuongeza vionjo fulani ambavyo vitakutofautisha.

    Angalia vitu unavyopenda. Unapenda mpira, Kuna biashara inayoenda na hilo unavyoweza kufanya.
    Unalenda muziki? Kuna biashara inayoendana na hiyo unavyoweza kufanya.

    Matatizo yanayowakumba watu pia Ni biashara.
    Nimeandika sana kuhusu namna unavyoweza kupata wazo la biashara, kwa kuanzia unaweza kusoma Makala hizi hapa kwenye blogu hiihii.

    Lakini pia Kuna biashara au mahitani ambayo ni ya asili. Ni mahitani AMBAYO watu kwa asili wanayahitaji. Chakula, mavazi na malazi.
    Nashauri pia usome ebook yangu inayoeleza SEKTA 11 ZA KUTENGENEZA MAMILIONI YA FEDHA TANZANIA. Rusha elfu tano kwa 0755848391 nikutumie ebook hii.

    Sasa tayari umeshapata wazo la biashara, lakini pia kama ni mtaji tayari unao. Sasa kifuatacho ni wewe kuanzisha biashara.

    Kitu muhimu ninachotaka kukwambia hapa ni kwamba umetangaza vita kubwa. Kama ni maji basi umeyavulia nguo. Sasa kifuatacho ni kuyaoga.

    Ikumbukwe kwamba bado una AJIRA lakini pia una BIASHARA. Ni vitu viwili vinavyokuhitaji.

    Biashara yoyote changa inakuhitaji Sana. Hivyo, utapaswa kwanza kuhakikisha kwanza unafanya kazi (AJIRA) yako vizuri. Fika ajirani kwako kwa wakati, fanya kazi kwa bidii na kwa ubora wa hali ya juu.

    Halafu tumia muda wako wa ziada kufanya biashara yako. Huu unaweza kuwa ni asubuhi sana kabla hujaenda ajirani au jioni mara tu baada ya kutoka ajirani.

    Ni kweli utachoka lakini sasa hiyo ndiyo gharama AMBAYO utapaswa kuilipa ili kuweza kuvifanikisha biashara yako.

    Muda ule uliokuwa unatumia kuzurura mtandaoni, Sasa ni muda wa biashara yako. Muda ule uliokuwa unautumia kunywa pombe au kupiga soga na washikaji, sasa ni muda wako wa biashara.

    Hiki kitu kinawezekana na ubora ni kwamba wewe siyo wa kwanza kufanya hivyo. Lakini pia ubora zaidi mimi nipo kukusaidia kwenye hili, nitahakikisha nakushika mkono mwanzo mwisho. Nashauri ujiunge na kundi langu la THINK BIG FOR AFRIKA ili tuendelee kuwa karibu sana muda wote.

    HATUA YA SABA: TUNZA HESABU ZOTE ZA BIASHARA VILIVYO
    Endesha biashara yako kitalaamu kuanzia siku ya kwanza. Kinachokwamisha biashara nyingi na wafanyabiashara wadogo ni kukosa mfumo mzuri wa kuwasaidia kutunza hesabu za biashara. Rafiki yangu, anza biashara yako vizuri.

    Ebu chukulia kama ndio ungekuwa unaenda kuiuza biashara yako ndani ya mwaka mmoja. Na wanunuzi wa biashara yako wanahitaki kuona fedha zote zilizoingia kwenye biashara na jinsi zilivyotumika.

    Na hesabu nzuri za kuanza kutunza ni hesabu za mapato na matumizi.
    Ukiweza kutunza hizo kwa kuanzia, utafika mbali.

    Ikumbukwe kuwa maisha ya ya kujiajiri ni tofauti kidogo na maisha ya ajira. Unapoajiriwa unakuwa chini ya bosi wako. Ila ukijiajiri wewe mwenyewe ndiye unakuwa bosi wako.

    Ajirani unapaswa kuwahi kwa sababu usipowahi kuna adhabu au madhara yatatokea. Ila sasa wewe mwenyewe ndiye bosi wako mwenyewe. Ni au unafanya au hufanyi.  

    Wewe mwenyewe ndiye unapaswa kujifuatilia, wewe mwenyewe ndiwe unapaswa kuhakikisha majukumu ya biashara yako yamefanyika bila kuachwa.

    Jisimamie na jisukume kwa siku za kwanza kuhakikisha unafika mbali. Ukitoboa hapa, ni wazi kuwa utajiwekea historia yako ya kipekee sana

    Kazi kubwa unayopaswa kupambana nayo baada ya kuanzisha biashara ni kuhakikisha inakua na inaweza kukuingizia kipato kikubwa kila mwezi ambacho ni kikubwa ni sawa au kinakaribia kile cha mshahara uliokuwa unaupokea.

    Ukishafikia hii ngazi Sasa ndipo unaweza kufikiria kuacha ajira yako na kuweka nguvu kwenye biashara yako.

    Hili linaweza lisiwe suala au kitu ambacho unaweza kukamilisha ndani ya muda mfupi. Ila kinawezekana. Na ndio maana tangu mwanzo nimekwambia uwe na  ndoto kubwa,  kazi yako utakuwa ni kupambana ili ufikie ndoto yako kubwa.

    Rafiki yangu ngoja, nikwambie kitu. Hizi hatua zinaweza kuonekana nyingi, Ila ukweli ni kwaamba inawezekana na hiki ndio kitu ambacho nimesisitiza tangu mwanzo mpaka hapa ninapohitimisha makala hii. Rafiki yangu, inawezekana kujenga biashara na ukaisimamisha ukiwa umeajiriwa.

    Karibu sana tufanye kazi kwa pamoja. Nashauri ujiunge na kundi langu la THINK BIG FOR AFRIKA. Ambapo utakuwa karibu nami na utajifunza zaidi kuhusu biashara. Jiunge na THINK BIG FOR AFRIKA kwa kuwasiliana nami kupitia 0755848391

    Rasilimali nyingine unazohitaji ni:

    Kitabu cha KUTOKA SIFURI MPAKA KILELENI (15,000) (Hardcopy &soft copy)

    JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO (20,000/-) Hardcopy &soft copy)

    MAAJABUYA KUWEKA AKIBA (5,000/-) soft copy

    MAMBO 55 YA KUZINGATIA KABLA YA KUANZISHA BIASHARA (5,000/-) soft copy.


  • KIPAJI NI DHAHABU-1 binadamu wote ni sawa ila uwezo ni tofauti

    KIPAJI NI DHAHABU-1 binadamu wote ni sawa ila uwezo ni tofauti

    Walau siyo mara yako kusikia kuwa binadamu wote ni sawa. Au kusikia haki sawa kwa wote. Japo kuna huo usawa kwa watu wote,  linapokuja suala zima la kipaji na  uwezo mkubwa tulionao tunatofautiana.

    Ndio maana kuna watu wanajulikana kama multi-talented. Wana uwezo katika maeneo tofauti tofauti na wanaweza kuyafanyia kazi hayo maeneo kwa ustadi.

    Diamond uwezo wake upo kwenye kuimba au basi tuseme Diamond kipaji chake ni kuimba. Samatta kipaji chake ni kucheza mpira.
    Shigongo kipaji chake ni kutunga hadithi tamu, wewe pia unapaswa kugundua kipaji chako.

    Una uwezo mkubwa ndani yako ambao hujaanza kuutumia. Thomas Edison aliwahi kunukuliwa akisema kwamba, laiti kama tungeutumia uwezo mkubwa tulionao Kama inavyostahili, sisi wenyewe tungejishangaza kwa matokeo ambayo tungepata”

    Uwezo wako ni mkubwa kiasi kwamba kama ungeishi miaka elfu moja bado usingeweza kuutumia ukaisha.

    Kipaji huwa hakitumiwi kikaisha. Badala yake kadiri unavyokuwa unakitumia ndivyo kinakuwa kinazidi kuimarika zaidi.

    Wewe unafahamu kipaji chako?
    Pata ebook ya kipaji ni dhahabu kwa gharama ya elfu tano tu (5,000/-).

  • Hiki kitu ndicho kitakusaidia wewe kukaa kwenye gemu la mafanikio kwa muda mrefu mpaka ukashinda

    Kila mtu anapenda  kufanikiwa. Yaani, hapa ufahamu kabisa kuwa ni kila mtu  anapenda. Hakuna mtu anapenda kushindwa. Ukiingia kwenye chumba chochote ambacho kina watu, ukiuliza wangapi wanapenda kufanikiwa. Wote watanyosha mikono juu na tena wengine watanyosha mikono miwili juu.

    Sasa swali letu ni kwa nini watu wengi huishia kufeli wakati wanapenda kufanikiwa.

    Najua hapa unaweza kutoa sababu nyingi kama watu kutokuwa na malengo makubwa, kutojisukuma zaidi na mengineyo kama hayo; ila kitu kimoja kikubwa ambacho kinafelisha wengi ni watu waliowazunguka.

    Ebu fikiria mtu wa kawaida amezungukwa na wangapi waliofanikiwa au wenye kiu kubwa ya mafanikio? Wangapi?
    Ukifuatilia utakuta ni sifuri.
    Mtu anatoka kwenye familia masikini
    Anasoma na watu masikini
    Anaoa au kuolewa na mtu masikini
    Ila yeye ana ndoto ya kufika mbali.

    Watu waliomzunguka wengine wote ni masikini na hakuna mwenye mtazamo wa kusema kwamba anataka kufika mbali kiuchumi. Na hawa ndio wanampa ushauri huyu mtu. Unadhanai atatoboa? Thubutu.

    Yaani, ushauri upewe na masikini unadhani atakupa ushauri gani?

    Siyo kwamba nadharau au kumshusha mtu, Ila ninachotaka ufahamu ni kwamba, chuma kinanoa chuma.

    chuma kinanoa chuma

    Ukizingukwa na chuma uwezekano wa wewe kunolewa kuwa chuma ni mkubwa. Ndio maana ni muhimu kwako kuzungukwa na timu ya watu sahihi.

    Timu ya watu waliokuzunguka wana uwezo wa kukusaidia wewe kufanya makubwa au kushindwa kufanya makubwa.

    Unataka kujiajiri? HAKIKISHA una timu sahihi iliyokuzunguka ya kukusaidia kufanya hivyo.

    Unataka kufikia umilionea au ubilionea, hakikisha una timu sahihi ya kukusaidia kufanya hivyo.

    Na timu sahihi ni watu ambao wamewahi kufanya hivyo au wanafanya hivyo kwa vitendo sasa hivi.

    Kitu ambacho ni kigumu sana kukipata kwenye jamii. Wengi kwenye jamii Wana mipango mizuri ya mdomoni tu ya kufika mbali, Ila hawana mipango madhubuti ya vitendo.

    Hiki kitu kinachokosekana kwenye jamii, ndicho tulichonacho kwenye THINK BIG FOR AFRIKA

    Think big for Afrika ni jamii ya tofauti kabisa ambayo huwezi kuikuta sehemu nyingine. Iko hivi, hii ni jamii ya watu wenye ndoto kubwa za kufika mbali na sote kwa pamoja tunashikiriana kuhakikisha tunafika mbali.

    Kila mmoja ni sehemu ya timu na kila mtu anamshika mkono mwenzake kuhakikisha kwamba  haachwi mtu nyuma.

    Kila mtu ana ndoto kubwa ya kufanyia kazi na amezungukwa na wengine wanaozifanyia kazi. Ni sehemu maalumu yenye vyuma vinavyonoa vyuma.

    Karibu ujiunge na jamii hii ya kipekee sana.
    Ili kujiunga unapaswa kuwa na shauku ya kufanikiwa na kufika mbali na uwe tayari kufanya kazi kwa vitendo ili ufikie mbali.

    Utaungana na watu sahihi walio kwenye gemu
    Utapata mafunzo sahihi kila siku.
    Utashirikiana na wenzako na mengineyo mengi.

    Karibu sana ndani ya jumuiya hii ya kipekee. Eneo la kwanza kabisa la kujiunga jamii hii ni kupitia mafunzo yanayotolewa kwenye kundi la WhatsApp na baruapepe.

    Mafunzo haya ya kipekee ambayo huwezi kuyapata kwingine yanatolewa kila siku kwenye maeneo hayo mawili.

    Gharama za kujiunga na mafunzo haya ni 10,000 kwa mwezi.

    Ila ukilipia kuanzia miezi mitatu kuna punguzo la asilimia 10. Hivyo, utalipia elfu 27000 badala ya elfu 30.

    Ukilipia kwa miezi sita kutakuwa na punguzo la asilimia 20. Hivyo, utalipia elfu 48,000 badala ya elfu 60.

    Na ukilipia kwa mwaka mzima kutakuwa na punguzo la asilimia 30. Hivyo utalipia 84,000 badala ya 120,000

    Mafunzo haya maalumu yanatumwa kwa njia ya barua pepe na WhatsApp kwenye kundi la THINK BIG FOR AFRIKA

    kila siku utapokea makala moja yenye mafunzo ya kina

    kila jumapili utapokea ebook moja yenye uchambuzi wa kitabu, au andiko liliojadili mada fulani kwa kina kuhusu biashara, malengo au vipaji

    inaweza kutokea kwamba jumapili ukatumiwa audio au video itakayokuwa inahusu jambo fulani hasa kuhusu biashara badala ya ebook.

    Sambamba na hilo utakuwa na nafasi ya kunipigia na kuongea nami kwa ajili ya ushauri zaidi muda wowote utakapohitaji

    Jiunge leo hii kwa kulipia ada ya mwezi mmoja, mitatu, sita au mwaka mzima.

    Lipia kwa namba 0755848391 jina ni GODIUS RWEYONGEZA.
    Baada ya kulipa niambie nikuunge.

    Karibu sana Think Big For Afrika.

    Umekuwa nami

    Godius Rweyongeza

  • Jinsi Ya Kupima Thamani Ya Utajiri Ulionao

    Kama una ndoto kubwa na za kufika mbali basi ni muhimu kwako kujua utajiri ulionao kwa sasa. Hii itakupa nguvu ya wewe kuendelea kupambana zaidi ili uweze kufika mbali.

    Muda wa wewe kupima Utajiri wako.

    Kutokana na shughuli kuwa nyingi, huwezi kuwa unapima Utajiri wako kila siku. Ila unaweza kuwa unapima Utajiri wako walau mara moja kila baada ya miezi mitatu. Au hata mara moja kila mwezi. Hapa utaangalia namna ulivyoweza kukuza utajiri wako kulinganisha na siku za nyuma na lakini pia kuweka mpango wa kukuza Utajiri wako kwa siku zijazo.

    Sasa napimaje thamani ya Utajiri wangu?

    Kupima thamani ya Utajiri wako, fanya hivi; chukua thamani ya mali zote unazomiliki toa madeni yote.

    UTAJIRI= THAMANI YA RASILIMALI-MADENI YOTE.

    Utakachopata ndio utajiri wako kwa wakati husika. Sasa je, wewe una kiwango gani kwa sasa.
    Ni mamilioni
    Ni malaki
    Ni maelfu?

    Kwa kiwango chochote ulichonacho sasa hivi, kazana kukikuza zaidi. Inawezekana

    SOMA ZAIDI: Bilionea Ni Mtu Wa Aina Gani?


  • Milionea Ni Nani?

    Milionea ni mtu anayemiliki rasilimali zenye thamani ya milioni moja.

    Kutokana na thamani za fedha kutofautiana, kwa sasa kipimo kinachotumika kupima umilionea ni dola ya Marekani.

    Kwa hiyo ukisikia wanasema fulani ni milionea, ujue ni kwa thamani ya dola za Marekani.  Hii ndio kusema kwamba unaweza unaweza kuwa na rasilimali zenye thamani ya milioni moja kwa fedha za Tanzania ila usiwe milionea kwa sababu kipimo kikuu kinachotumika kwa sasa kupima umilionea ni dola za Marekani.

    Milioni moja ya shilingi za Tanzania kwa sasa ikiwekwa kwenye dola za Marekani ni sawa na dola mia nne thelathini na mbili. Kwa hiyo, ukiwa na milioni moja ya kitanzania unakuwa hata hujafikisha utajiri wenye viwango hata maelfu!

    Ili uwe milionea kwa kipimo cha dola unapaswa kuwa na rasilimali zenye thamani ya shilingi za Tanzania bilioni 2.3

    Napenda kusisitiza tu kuwa kipimo kinachotumika Utajiri kwa watu wote ni kimoja ili kusiwepo mchanganyiko. Kwacha ya Zambia ina thamani kidogo ukilinganisha na shilingi ya Tanzania. Na shilingi ya Tanzania ina thamani kidogo ukilinganisha na shilingi ya Kenya.
    Shilingi ya Kenya ina thamani kidogo ukilinganisha na Rand ya Afrika kusini.

    Sasa ebu fikiria milionea kwa thamani ya fedha za Zambia, Kenya, Tanzania, Afrika Kusini na Marekani watakuwa sawa endapo kila nchi itatumia sarafu yake kupima umilionea?

    Ndio maana kinatumika kipimo cha aina moja kupima Utajiri wa watu wote duniani. Kwa sasa dola ndiyo inatumika kama siku zijazo kutakuwa na mabadiliko tutajuzana.

    Jinsi umilionea unavyopimwa

    Umilionea (UTAJIRI)= THAMANI YA RASILIMALI-MADENI YOTE.

    Wewe mwenyewe pia unaweza kupima thamani ya utajiri wako kwa kuchukua thamani ya rasilimali zako kisha ukatoa madeni yote unayodaiwa.

    Chukua thamani ya mali zako kwa sasa kama ungekuwa unaziuza kisha toa madeni.

    Je,milionea ana fedha zote mfukoni.

    Kwa sasa hivi umilionea unapimwa kwa kiwango cha thamani ya rasilimali ulizonazo baada ya kutoa madeni. Mamilionea wengi wamewekeza kwenye makampuni au rasilimali zisizohamishika (kama nyumba, ardhi,) au wamewekeza kwenye soko la hisa (hisa, hatifungani na vipande), hivyo milionea hana fedha taslimu mfukoni mwake. Utakuta ana fedha za kawaida tu za kumtosha kufanya mambo yake yote muhimu ila hana milioni zote za fedha taslimu mfukoni.

    Ila mali zake zote zikiuzwa kwa thamani ya wakati husika zina uwezo wa kufikia milioni husika.

    HAKIKISHA UMESOMA KITABU CHANGU CHA MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE ili ujifunze zaidi kuhusu UWEKEZAJI. Kinapatikana kwa elfu tano tu, irushe kupitia 0755848391 Jina ni GODIUS RWEYONGEZA ili nikutumie ebook.

    Nawezaje kuwa milionea?

    Watu wanakuwa mamilionea kwa kurithi
    Au kwa kupambana wenyewe.

    Kama huna sehemu ambapo utarithi umilionea basi utapaswa kupambana mwenyewe.

    Ili kuwa milionea utahitaji kuweka kazi sana na kwa muda mrefu. Utahitaji kujipa muda, maana umilionea hauwezi kutokea ndani ya siku moja. Unahitaji muda, kazi, KUWEKEZA, kuanguka na kusimama tena.

    SOMA ZAIDI: Hii Ndio Siri Kubwa itakayokusaidia kutengeneza fedha Nyingi

    Je, ni kazi gani inaweza kunipa umilionea?

    Niwe tu mkweli, hakuna kazi inayokulipa mshahara inavyoweza kukupa umilionea.
    Ili ufikie umilionea utapaswa kuwa na biashara na (au) kufanya uwekezaji.

    Kwa sasa ya mamilionea, wengi wanatoka kwenye sekta mbalimbali ila Kuna sekta 11 zimejitokeza  kuwa mamilionea wengi.

    Nashauri upate ebook yangu ya SEKTA 11 ZA KUTENGENEZA MAMILIONI YA FEDHA TANZANIA ili ujue maeneo sahihi unapoweza kuwekeza fedha zako. Haya ni maeneo mazuri pia unavyoweza kuanzisha biashara ya kukupelekea kwenye umilionea.
    Ebook hii inapatika kwa elfu tano (5,000/-) tu. Rusha elfu tano (5,000/-) kwa 0755848391 jina ni GODIUS RWEYONGEZA ili nikutumie ebook hii.

    Mamilionea Wa Tanzania

    Wengi wa wale wanaojiita mamilionea kwa Tanzania siyo mamilionea!  Hauwi milionea kwa kupokea mshahara wa milioni moja kwa mwezi. Rafiki yangu Kama wewe mshahara wako ni milioni, usijidai kuwa sasa wewe ni milionea. Umilionea ni viwango vingine kabisa kama ambavyo tumeona.

    Kama kwa mwezi unapokea mshahara wa milioni moja utahitaji mishahara ya aina hiyo mara elfu tatu (3,000) ili ufikie umilionea. Mishahara ambayo huwezi kuipokea kipindi cha maisha yako yote!

    Kwa hiyo  umilionea ndio haiwezekani kabisa?
    Hapana. Siyo kwamba haiwezekani, ngoja nikupe mbinu ya kutengeneza kufikia umilionea.

    Ukitengeneza bidhaa inayouzwa kwa dola moja moja. Ili uwe milionea unapaswa kuiuza kwa watu milioni moja na unapaswa usitumie hiyo fedha. Hahaha.

    Ukiuza bidhaa hiyohiyo kwa dola mbili basi utapaswa kuiuza kwa watu laki tano.

    Ukiiunza kwa dola kumi maana yake utapaswa kuiuza kwa watu laki moja.

    Ukiwa na bidhaa mbili za aina hiyo maana yake utapaswa kuziuza kwa watu elfu hamsini mara mbili. Ukiwa na bidhaa tatu, utaziuza kwa watu elfu 33.3 mara tatu.

    Kwa hiyo wewe, unaweza kuangalia namba ipi unaweza kupambania.

    Kama nilivyoeleza hapo mwanzo. Umilionea siyo kitu cha kulala na kuamka ukiwa umekifia. Ni kitu kinachukua muda.

    Mamilionea wengi wamefikia kiwango cha umilionea baada ya kufanya kazi kwa miaka 10 au zaidi.

    Kwa hiyo nikate tamaa ya kupambania ndoto yangu ya umilionea kwa sababu unachukua muda kuufikia?

    Unachopaswa kufahamu ni kuwa miaka 10 inaenda kupita. Sasa ikipita ni au utakuwa umeitumia kwa manufaa au umeitumia hovyo. Kama umeitumia kupambania ndoto yako ya umilionea utakuwa umepiga hatua kubwa sana hata kama utakuwa haujaufikia umilionea, Ila utakuwa umefika mbali.

    Ila ukikata tamaa hata kabla ya kuanza. Ni wazi kuwa hata ulakionea utakushinda. Utashindwa hata kuwa elfunea, hahaha.

    Kwa Tanzania miaka 10 ni mhura wa utawala wa rais. Kwa hiyo, rais ukiamua kupambana rais anapoingia madarakani mpaka anapotoka, unaweza kuufikia umilionea kwenye mhura wake.

    JE, UNA MPANGO WA KUWA MILIONEA?
    karibu ujiunge na kundi letu la THINK BIG FOR AFRICA.

    BONYEZA HAPA KUJIUNGA.

  • UWEKEZAJI NI NINI?

    Moja ya eneo ambalo limekuwa halieleweki miongoni kwa watu wengi basi ni UWEKEZAJI.

    Kumekuwepo na dhana mbalimbali kuhusu UWEKEZAJI na WAWEKEZAJI. Hizi dhana zimewafanya watu wengi washindwe KUWEKEZA huku wachache wanaoilewa dhana hii wakiwa wanawekeza kwenye maeneo ya muhimu kwa manufaa makubwa.

    Dhana potofu kuhusu UWEKEZAJI.

    Kumekuwepo na dhana mbalimbali kuhusu UWEKEZAJI. Na moja ya dhana kubwa  ambayo imekaa kwenye vichwa vya watu wengi ni dhana kuwa mwekezaji ni mtu wa nje. Fungulia redio au runinga, kila utakaposikia wakizungumzia kuhusu UWEKEZAJI au MWEKEZAJI basi wanakuwa wanamwongelea mtu wa kigeni.

    Hiki kitu kimemfanya watu wengi waamini kwamba mtanzania hawezi kuwa mwekezaji. Au kiufupi tu kuwa kama wewe siyo mtu kutoka nchi za nje basi basi wewe siyo MWEKEZAJI. Au labda nikuulize wewe, ni mara ngapi umeona au kusikia watanzania wakijiita wawekezaji?

    Hata hivyo, ifahamike kuwa siyo kwamba mtanzania hawezi kuwa mwekezaji. Wewe mwenyewe unaweza kuwa mwekezaji mzuri tu.

    MWEKEZAJI anapaswa kuwa na fedha nyingi

    Dhana nyingine kuhusu uwekezaji ni kwamba mwekezaji anapaswa kuwa na fedha nyingi. Nenda kaongee na mtu yeyote unayemfahamu na ongelea kuhusu UWEKEZAJI, ataanza kukuuliza kwani wewe una fedha za kutosha. Wengi wamekuwa wanaamini kwamba ili uwe MWEKEZAJI unapaswa kuwa na mamilioni na mamilioni, ila ukiwa kiasi kidogo tu basi hufai kuwa MWEKEZAJI.

    Siku siyo nyingi mtandaoni kulikuwa na kichekesho kilichowagawa watu kwenye vipengele kulingana na ukubwa wa kipato chao.

    Kilikuwa kinasema hivi

    Kama wewe

    una maelfu ya fedha basi wewe ni elfunea

    Una malaki ya fedha basi wewe ni lakionea

    Una mamilioni ya fedha basi wewe ni milionea

    Una mabilioni ya fedha basi wewe ni bilionea.

    Una matrilioni ya fedha basi wewe ni trilionea

    Una mazilioni ya fedha basi wewe ni zilionea.

    Tujuane wewe uko wapi?

    Japo kililenga kuchekesha watu Ila kwetu kina funzo kubwa sana. Na funzo hili ni kwamba kulingana na imani ya watu wengi kuhusu UWEKEZAJI kama wewe ni elfunea au lakionea basi huwezi kuwa MWEKEZAJI.

    Hata hivyo tunaenda kuona muda sio mrefu kuwa huhitaji kuwa milionea au bilionea ili uwekeze, unaweza kuanza KUWEKEZA kutokea popote  ulipo.

  • Mafanikio ni nini?

    Kwa mwanafunzi mafanikio yake ni kufaulu mtihani.
    Kwa mwanachuo mafanikio yake yanaweza kuwa kupata kazi baada ya kuhitimu.
    Kwa aliyepata ajira mafanikio kwake yanaweza kuwa ni  kupandishwa cheo au kuoa/ kuolewa au kuanzisha biashara au kujiajiri.

    Hivyo, hakuna maana moja ya mafanikio ambayo inaweza kuwekwa kama maana ya kimataifa ya mafanikio

    Maana ya mafanikio unajipa mwenyewe. Wewe mwenyewe unapaswaa kujipa maana ya mafanikio.

    Jua ni kitu kipi ukikifanya au ukikikamilisha kinakuwa kinaashiria kuwa umefanikiwa?

    Lakini pia kitu kingine unapaswa kujipa orodha ya vitu ambavyo utavifanya maishani.
    Orodhesha vitu ambavyo unataka ufanikishe au ufikie.
    Kwa mfano orodha yako inaweza kuwa na vitu kama
    Gari utakalomiliki
    Nyumba
    Mwenza wako
    Sehemu utazotembelea kabla ya kufa
    Vitu utakavyofanyia kazi kabla ya kufa n.k.

    Kwenye kitabu chake cha Who Will Cry When you Die, Robin Sharma anashauri uandike vitu 101 utakavyofanyia kazi kabla ya kifo chako. Na hivi ndivyo vitabeba maana yako ya mafanikio.

    Hata hivyo hivi vitu visibebe furaha yako kwa kutaka kuvifanikisha. Bali wewe ufurahie ule mchakato wa kufanikiwa zaidi na kwa kuvifanyia kazi.

    MAKALA NYINGINE ZINAZOENDANA NA HII:

X