Home


  • Namba Zetu Za Malipo

    Namba za malipo ya vitabu:

    Namba za lipa

    TIGO PESA: 19016638 Jina ni SONGAMBELE CONSULTANTS

    M-PESA: 5564517 jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

    Namba za kawaida

    AIRTEL MONEY: 0684408755
    TIGO PESA: 0655 848 392
    M-PESA: 0745 848 395

    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    NB: Kama namba ya malipo anatumiwa mtu ambaye yuko nje ya nchi. Iandikwe Kwa kuanza na +255

    Kwa hiyo namba zinazotumwa nje ya nchi zitakuwa
    Airtel money: +255 684 408 755
    TIGO PESA: +255 655 848 392
    M-PESA: +255 745 848 395

    KOTE Jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Kama malipo yatakuwa yanafanyika kupitia benki.

    Yafanyie kupitia

    1. CRDB BANK: 0150770710200
    2. NMB BANK: 22110047274

    Kote jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

  • Wasiliana na Godius Rweyongeza Sasa

    Habari yafuatayo ni mawasiliano Unayoweza kutumia kumpata GODIUS RWEYONGEZA

    Simu: +255 (0) 684408755

    Whatsap: +255 (0) 755848391

    Email: songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu vyake wasiliana Moja kwa Moja na +255 (0) 684408755 (more…)

  • Kitu Cha Kufanya Ndoto Yako Inapohusisha Watu Wa Nje

    Kuna nyakati ndoto na malengo yako yanahusisha watu wa nje. Yanahusisha taasisi za serikali, makampuni fulani au hata mataifa mengine ambayo yana taratibu zake, utendaji kazi wake na kila kitu cha kwake. Watu hawa utakuta kwamba wana njia zao kutenda na kushughulika na vitu vyao katika namna ambayo inaweza isiwe rafiki kwako. Kwa mfano, unaweza kuwa na haraka ya kusajili kampuni yako au chuo chako, ila ukakuta kwamba taasisi inayo husika haioni umuhimu wa kukufanyia kile unachohitaji kwa wakati na wakati mwingine ukasumbuliwa bila ulazima wowote.

    Unaweza ukawa unahitaji leseni yako ya udereva ili ikusaidie kutimiza jambo fulani ulilonalo kwenye mpango wako na malengo yako, ila ukakuta kwamba watu wanaohusika hawana haraka na wala hawajali kukupatia leseni yako kwa wakati hata kama umekidhi viwango vyote ambavyo unastahili kuwa navyo.

    Katika hali ya kawaida watu wa aina hii wanakukwamisha na hata kukufanya ushindwe kufanikisha vitu vyako kwa wakati. wakati mwingine unaweza kuwa hata na watu ambao umewaajiri ila wakawa pia hawaelewi kile unachotaka na hivyo kuzidi kukudidimiza. Sasa zifuatazo ni njia za kukusaidia wewe kuwasiliana na watu wa aina hii ili wakufanyie mpango wako kwa wakati;

    Kwanza, waeleze watu hao mpango wako mkubwa ambao unataka kuufanyia na muda ambao ungependa mpango huo uwe umetimia.

    Ukiwaeleza watu mpango wako ambao ungependa ufanyiwe kazi ni wazi kuwa watu hao wanakuwa tayari kusaidia na kushirikiana na wewe. Muda mwingine badala ya kuonesha kwamba ndoto au lengno ni la kwako binafsi, unapaswa kulionesha kama vile lipo kwa ajili ya wakusaidia awao pia. Wape na wao lengoambalo watashirikiana na wewe kulifanyia kazi.

    Hiki kitu kimenifanya nikumbe stori moja ya namna watu walivyopunguza idadi watu waliokuwa wanakojoa juu chooni. Ni kwenye uwanja wa wakimataifa wa…

    Kulikuwa na tatizo kubwa hasa kwenye choo cha wanaume, ambapo mara nyingi walikuwawnakojjoa juu ya choo obadala ya kukojoa ndani. Sasa kilichofanyiaka ilikuw ani kuchora kitu kilichoonekana kama nziri kwenye sinki la choo.

    Kila aliyekuwa anaingia kwenye kile choo alikuwa anatamani kumwongooa yule nzirr kwenye sinki na hivyo aakawa anamlenga. Baada ya muda idadia ya wtu waliokuw wanakojoa juu ya choo walikuw wamepungua.

    Pili fahamu kuwa hauko kwenye mchezo huu kwa muda mfupi, ni mchezo ambao unaenda kuucheza kwa muda mrefu. Hivyo wewe kama wewe utapaswa kwenda vizuri, usibabishe fujo, usimdhuru mtu wa kudhulumu mtu kwa maana haufanyii hiyo ndoto kwa ajili ya kupata hela ya kula leo hii na kesho yake utaenda eneo jingine. Kwa ko hicho ni kitu ambacho unakifanya kama sehemu ya au kifanikiwe au ufe ukiwa unapambana nacho.

    Nne, fahamu kuwa watu wote wanaostahili kulipwa stahiki zao, utapaswa kuwalipa stahiki zao kwa wakati bila ya kuchelewa. na hawa watu ni wazi kuwa siyo tu kwamba utataka wakufanyie kazi kwa siku moja au mbili, hawa watu unaweza utawahitaji leo na kesho.

    Tambua mchango wa kile mtu ambaye anahusika kwenye kufanyia kazi ndoto yako na hakikisha huyo mtu anajua kwamba, yeye yana mchango kwako. hata hivyo, uwe makini watu wasije wakatumia hicho kipengele kwa ajili ya kukunyanyasa hasa wakijua kwamba mchango wao ni wa kipekee.

    Wafanyakazi wako wajue kuwa ni watu wa muhimu kwenye kazi au biashara yako, ila pia wajue kuwa wakienda kinyume na taratibu hutaweza kuwavumilia.

    Fahamu kuwa wewe unaweza kushinda kwa kufanyia kazi ndoto yako na mwingine akashinda kwa kuifanyia kazi ndoto yake. Usitake kabisaa kumuumiza mtu ili wewe uende mbali zaidi. badala yake penda kuwainua wengine maana kadiri wengine wanavyoinuka na wee unazidi kuinuka. Ndio maana mimi napenda nikuelimisha haya mabo uyafahamu maana nafahamu kuwa wewe ukiinuka, na mimi nitaweza kuinuka.

    Tafuta mtu wa kushughulika na changamoto nyingine ili wewe uwekeze nguvu zako kwenye mambo ya maana zaidi.

    Pia wenye ulimwengu wa sasa hivi ndoto yako inapasawa kuwekwa mtandaoni, sasa unapaswa kupambana na kuiweka

    umekuwa nami rafiki yako wa ukweli

    Godius Rweyongeza

    0755848391

    morogoro-Tz

  • Vitu Vya Kuepuka Ili Uweze Kuishi Maisha Mazuri

    Kwanza kabisa, hakikisha unaepuka kulalamika. Ukilalamika unakuwa unawanufaisha wale ambao wanakusikia.

    Epuka kufuatilia maisha ya watu wengine

    Epuka kutumia fedha yako yote ulyonayo bila kuweka akiba

    Epuka kukopa. Tumia dfedha yako

    Epuka kutumia fedha zaidi ya kipato chako

    Epuka kumezwa na mitandao ya kijamii

    Epuka kuianza na kuimaliza siku yako bila ya kuwa na malengo ambayo unayafnyia kazi

    Epuka kuishi bila ya ndoto kubwa

    Kila la kheri

  • Anza Na Kina Kile Ulichonacho

    Kabla hujasema kwamba haiwezekani na wala siwez i kufanya kitu fulani, jihoji kiundani na uangalie ni kitu gani unaweza kufanya. Kuna vitu vingi unaweza vizuri tu

    Kabla hujasema kwamba, sina cha kuanza nacho, angalia vizuri ikwenye mazingira yako ni kipi ulicho nacho ambacho unaweza kuanza kutumia sasa hivi. Kuna vitu ulivyo navyo ambavyo unaweza kuanza kutumia sasa.

    Kikubwa ni wewe kuabngalia vizuri rasailimali ulizonazo na kuhakikisha kwamba unazitumia vizuri.

    SOMA ZAIDI: MITAJI 8 ILIYOKUZUNGUKA NA JINSI YA KUITUMIA

    a365: ANZA KUTUMIA KILE ULICHONACHO

  • Njia Tano Rahisi Za Kukuza Biashara Kwenye Zama Hizi Za Mtandao

    Rafiki yangu hongera sana kwa siku hii nyingine na ya kipekee sana. Siku ya leo ningependa nikuelekeze njia tano tu ambazo zitakusaidia wewe kukuza biashara yako kwenye zama hizi za intaneti. Njia hizi ni rahisi kufanyika na unaweza kuzifanyia kazi popote pale ulipo

    Kwanza hakikisha kwamba biashara yako ipo kwenye mtandao. Kwenye zama hizi hapa mtu akitaka kitu, sehemu ya kwanza kabisa ambapo anakimbilia ni mtandaoni, hivyo ni jukumu lako kuhakikisha kwamba na wewe unaiweka biashara yako mtandaoni ili watu wakiingia mtandaoni wanatafuta kitu waweze kuikuta. Watu wanapaswa kuikuta biashara yako mtandaoni,  na njia rahisi ya watu kuikuta biashara yako mtandaoni ni kwa wewe kuhakikisha kwamba

    • Umefungua blogu au tovuti ambapo watu wakitafuta kitu watakukuta tayari ukiwa una kitu ambacho unaweka
    • Kuwa na akaunti ya google my business.
    • Kuwa na akaunti za mitandao ya kijamii na kuhakikisha kwamba unazitumia vilivyo
    • Kuwa na namba ya simu ya biashara na kuhakikisha kwamba unaitumia vilivyo kwa kutunza mawasiliano ya wateja wako na kuhakikisha kwamba wateja wako wanawasiliana na wewe kupitia namba hiyo.
    • Ikumbukwe kuwa namba ya biashara siyo namba ya simu binafsi.

    Rafiki yangu, hizo hapo ndio njia ambazo unaweza kutumia kuhgakikisha unakuza biashara yako hasa kwenye zama hizi hapa.

    Kila la kheri.

    Ni mimi rafiki yako wa ukweli Godius Rweyongeza

  • Jinsi Ya Kutatua Changamoto Unazokutana Nazo

    Habari ya siku hii njema sana rafiki yangu wa ukweli. Leo ni siku nyingine ya kipekee sana na leo nataka nikwambie kwamba usikubali kamwe kwenye maisha yako changamoto zikuzuidi wewe kukufanya ushindwe kufanikisha malengo yako.

    Siku zote changamoto huwa zinatokea. Changamoto ni kama zinatokea kukuonesha kwamba je, uko siriazi kweli na kile kitu ambacho unataka. Sasa kama hauko seriazi ndio utakuta kwamba unataka tamaa na kuishia njiani. Ila kama kweli uko siriazi utapambana kuhakikisha kwamba unaitatua hiyo changamoto na kuendelea mbele.

    Kitu muhimu unachopaswa kufahamu ni kwamba hauko peke yako mwenye changamoto. Wakiitwa watu wote hapa na wakaambiwa kwamba waweke changamoto zao hapo mezani halafu mgawane hizo changamoto, utakuta kwamba changamoto za kwako ni ndogo sana kuliko za hao watu wengine. Kuna watu wana changamoto kubwa kuliko wewe. Hivyo basi kitu kimoja ambacho ninaweza kukushauri hapo rafiki yangu ni kwamba jitahidi upambane na hali yako mpaka kieleweke. Kamwe, usikate tamaa kwenye kutatua changamoto au kufanyia kazi changamoto ambazo zinatokea maishani mwako.

    Upo level gani kwenye kutatua changamoto

    Hivi umewahi kujua kuwa kuna level za kutatua changamoto? Kama ulikuwa hujui basi kaa chini ili nikujuze rafiki yangu. Changamoto zina viwango bana. Ukiona kwamba umekutana na changamoto na imekushinda wewe kuitatua, basi ujue kwamba changamoto hiyo ina nguvu kubwa kuliko wewe.

    Binafsi huwa napenda kuziweka changamnoto kwenye mstari wenye namba moja mpaka kumi. Wewe ukikutana na changamoto ambayo ni kubwa kuliko wewe, maana yake lazima utaka tamaa na kuishia njiani na kuona kama vile hakuna maisha baada ya hapo.

    Ila kama wewe ni mkubwa kuliko changamoto, ukikutana na changamoto ambayo umeizidi kwako, itakuwa ni rahisi kuitatua. Hivyo, basi unapaswa kuwa makini kwenye kufanyia kazi changamoto kwenye maisha yako.

    Ukikutana na changamoto kubwa, tuseme changamoto namba 7 na wewe uko kwenye viwango vya namba 5 ni wazi kuwa hiyo changamoto utaikimbia tu. Ila kama wewe uko kwenye viwango vya namba 9 kwenye kutatua changamoto na ukakutana na changamoto namba 7 ni wazi kuwa hiyo changamoto kwako itakuwa ni rahisi sana.

    Jijengeea uwezo wak utatua changamoto. Hiki ni kitu muhimu sana. Unapaswa kujijenea uwezo wa kutatua changamoto. Ukikutana na changamoto, usizikimbie, kuwa tayari kuzifanyia kazi mpaka utoboe.l changamoto ni sehemu ya maisha tu. Hivyo, kuwa tayari kuzifanyia kazi.

    Changamoto huwa haziishi. Njia pekee ya wewe kumaliza changamoto ni wewe kuwa mkubwa kuliko changamoto zenyewe. na kamwe usije ukakimbia changamoto uliyokutana nayo.

    Kila la kheri

    Umekuwa nami rafiki yako wa ukweli

    Godius Rweyongeza

  • NGUVU YA NENO: MANENO HUUMBA NA KAULI 101 UNAZOPASWA KUZIEPUKA ILI KUFANIKIWA

    UTANGULIZI

    Maneno huumba. Ni usemi mfupi wa wahenga ila wenye maana kubwa sana. ni ukweli kuwa maneno yana uwezo wa kuumba kitu chochote. Ukitaka maneno yakuumbie kitu kizuri, basi unaongea maneno chanya. Ukitaka maneno yakuumbie kitu kibaya basi unaongea unaongea maneno hasi. Ni hivyo tu. Sasa kwenye kitabu hiki nimeona nikuletee kauli 101 ambazo unapaswa kuziondoa kwenye kamusi ya maongezi yako. La sivyo kauli hizi hapa zinaenda kukuangusha chini na kukufanya uendelee kupata matokeo mabaya. Kauli zenyewe ni;

    1. Kumekucha na makucha yake

    Hii ni kauli ambayo Watu wengi huwa wanaitumia katika kuonesha kuwa dunia siyo fair, dunia siyo nzuri na wala haifai. Ukisema kumekucha na makucha yake maana unategemea mabaya yatokee ndani ya hiyo siku, ndio maana unasema kumekucha na makucha yake.

    Sasa badala ya wewe kuamka asubuhi na kusena kuwa kumekucha na makucha yake, amka asubuhi na anza kujisemea kuwa leo ni siku nzuri sana. Siku ya Leo ninaenda kufanya makubwa.
    Kwa jinsi hiyo utaianza siku yako kwa namna chanya na hata kila utakachokutana nacho utakitafsiri katika namna chanya, tofauti na pale ambapo utaianza siku yako kwa mtazamo hasi, kila kitu kitakachotokea kwako, kitaonekana kibaya.

    2. Sina fedha/sina hela

    Hii ni kauli ambayo moja kwa moja inakufunga na kukufanya usione upenyo wa kutoka. Ukisema sina hela maana yake unakuwa unainyima akili uwezo wa kufikiri nje ya boksi na kuona fursa gani zaidi unazoweza kupata.

    Badala ya kusema sina fedha, unaweza kujiuliza hivi hapa nawezaje kupata fedha? Au ni mbinu gani naweza kuitumia kupata fedha? Ukisema hivi unakuwa umeifungua dunia nyingine ya fursa na kuona vitu ambavyo watu hawaoni.

    Kuna misemo ambayo imezoeleka kutolewa na watu siku hizi kiasi kwamba imekuwa ni sehemu ya pili ya maisha ya hawa watu. Unakuta mtu anasema “usawa huu wa Magufuri pesa imekuwa ngumu sana”. Utasikia mwingine anasema “vyuma vimekaza” wakati mwingine akitaka kukwambia kuwa hana pesa basi utasikia akisema, “sina hata mia mbovu”. Yaani kumaanisha kuwa hana kitu kabisa mfukoni mwake.

    Ukifuatilia kwa umakini. Yaani kwa jicho la tai anayeuangalia mchezo kutokea juu angani na kutoa tathimini, unaona wazi kabisa kuwa suala la vyuma kukaza sio jambo la leo au jana.  Historia inaonesha kuwa katika kila nyakati kumekuwa na mambo kadha wa kadha ambayo yamekuwa yakitokea na kusababisha vyuma kukaza. Hata hivyo kitu kimoja kimebaki uhakika siku zote. Wale wanaotengeneza pesa siku zote huwa hawaoni kukaza kwa vyuma kama tatizo. Badala yake huwa wanaona fursa kwenye hilo.

    Ngoja nikueleze kiundani suala hili ili uweze kunielewa. Kukaza kwa vyuma kama wanavyosema wengine maana yake ni kutokuwepo kwa pesa. Sasa tujiulize ni kitu gani kinakufanya wewe ukose pesa?  Unaweza kuwalalamikia watu wote duniani ila mwisho wa siku mtu anayesababisha kukaza kwa vyuma ni mmoja tu. Na mtu huyu ni wewe.  Hii unatokana na ukweli kwamba pesa inafuata mkondo kwa wale wanaoiita. Kama wewe hauiiti ije kwako haiwezi kuja, utapishana nayo njiani tu.

    Leo hii nataka nikuoneshe namna utakavyoiita pesa ije kwako na iendelee kuwa ya kwako milele na milele. Siku nyingine kabla hujasema pesa ni ngumu hakikisha unarudi hapa kusoma andiko hili ili uone Kama umelitendea haki. Ila kama utasoma hapa na kuishia tu kusema kuwa huyu jamaa anaandika vizuri basi mimi nakuhakikishia utaendelea kusema kuwa pesa ni ngumu. Kama utasoma hapa na kufanyia kazi ulichojifunza hapa, basi tutakutana sehemu siku moja ukifurahi kwa sababu ya kile ukichojifunza hapa siku ya leo.

    MOJA, KAMA PESA NI NGUMU MAANA YAKE HUJATOA HUDUMA KWA JAMII
    Zig Ziglar amewahi kusema kuwa utapata kitu chochote unachotaka kama utawasaidia watu kiasi cha kutosha kupata kile wanachokitaka. Kitu ambacho unapaswa kuelewa hapa ni kuwa kuna watu wana pesa zako mkononi mwao. Ila hizo pesa hazitakuja kwako kirahisi. Labda uwakabe (na ukifanya hivyo jela itakuwa rafiki yako). Ila njia pekee ya kuzitoa hizo pesa kwa watu na kuzileta kwako ni kuhakikisha kuwa una bidhaa ambayo unaweza kuwauzia hao watu. Hiki kitu ndicho Zig Ziglar anakiita kuwasaidia watu kupata WANACHOTAKA.
    Kuna watu wanahangaika kwa sababu huduma fulani hawaipati vizuri. Lakini wewe ukiweza kuwafikishia hiyo huduma kwa ustadi watakuwa tayari kukulipa na hiki ndicho Zig Ziglar anakiita kuwasaidia watu kupata WANACHOTAKA.

    Kuna watu hawajui kwamba wewe ni mtaalamu na umesomea ujuzi fulani chuoni. Sasa huo ujuzi uliojifunza chuoni ukiweza kuutafsiri na kuuleta kwenye maisha ya kawaida hapa mtaani. Ukautumia ujuzi huo kuwasaidia watu kupata kitu fulani ambacho unaona kitaalamu hakifanyiki vizuri. Hapo utakuwa umewasaidia watu kupata kitu wanachokitaka.

    Nikukumbushe kuwa pesa hazitakuja kwako kama wewe utakuwa tu umelala halafu unaishia kusema pesa ni ngumu au vyuma vimekaza. Pesa itakuja kwako pale ambapo utaamua kutatua matatizo ambayo jamii inakumbana nayo.
    Muuza maji hapati pesa kwa kuuza maji bali kwa kutatua tatizo lako la kiu.

    Mtu daladala hapati pesa kusafirisha abiria, bali kwa kutatua tatizo lako la kusafiri na kufika eneo husika mapema.
    Mitandao ya simu haipati pesa kwa kuuza vocha bali kwa kuunganisha na watu walio mbali na wewe.
    Wewe unatatua tatizo gani?

    Shida yako wewe imelala kwenye  haya maeneo mawili.
    Kwanza unaamini kuwa hakuna kitu kingine kipya unaweza kufanya kuondokana na hali hiyo uliyonayo.

    Yaani, umejikatia tamaa mwenyewe. Na kama umekata tamaa mwenyewe hata akitokea mtu akakupa mamilioni ya pesa hayatakusaidia. Cha kufanya inuka tena na anza kupambana.

    Tatizo lako la pili, unaona kuwa haya ninavyoongea hapa yanawafaa wengine na sio wewe. Huchukui hata hatua ya kuanza, unabaki kusema tu haya yanawafaa watu wenye hela zao bana. Hivi unadhami hao unaosema wana hela zao walizaliwa nazo? Kuna wengine walikuwa na maisha mabaya pengine zaidi ya wewe. Kuna wengine walikuwa na madeni makubwa kuliko hata wewe hapo. Ila walisimama wakabeba majukumu yao na sasa unawaonea gere. Usipochukua hatua UTAJIJU.

    2. KAMA PESA NI NGUMU MAANA YAKE UNAWAHUDUMIA WATU KIDOGO

    Kiasi cha pesa unachoingiza kinaweza kuniambia ni idadi gani ya watu unaowahudumia. Kama unaingiza pesa kidogo maana yake UNAWAHUDUMIA WATU KIDOGO. Kama kuna kiasi kikubwa unaingiza maana yake unawahudumia watu wengi. Hii wala hata sio hesabu ngumu kama unavyofikiria.

    Ebu tuseme wewe na Paulo mnauza maji. Paulo anawauzia watu 1000 na wewe unawauzia watu 100 kila siku na kipimo mnachotumia kuuza ni kile kile, bei pia sawa, unadhani nani atapata pesa zaidi?

    Ukiona pesa ni ngumu unapaswa kujua kuwa unawahudumia watu kidogo. Kama umeajiriwa ujue unafanya biashara na mteja mmoja tu ambaye ni bosi wako. Sasa usitegemee ulipwe kwa viwango sawa na mtu ambaye anatoa huduma kwa wateja mia, elfu au laki moja.

    3. KAMA PESA NI NGUMU UJUE KUWA HUJAJUA MISINGI NA MIIKO YA PESA.

    Ni kawaida kuwa mwanasheria akienda chuoni lazima atafundishwa misingi ya sheria na miiko kwenye sheria. Daktari pia anafundishwa misingi na miiko.

    Mwajiriwa kazini ataambiwa mambo anayopaswa kufanya kazini na yale anayopaswa kuepuka. Pesa pia ina misingi yake na miiko yake. Ukiona ni ngumu kwako basi ujue hii misingi hujaijua.
    Hujajua kuwa unapaswa kuweka akiba kwa kila kiasi unachopata.
    Hujajua pia kuwa unapaswa kupunguza matumizi yako na kubaki na mtumizi ya lazima tu.
    Hujajua kuwa unapaswa kuanza kuwekeza ili pesa yako ikuzalie pesa zaidi.
    Hujajua kuwa haupaswi kutumia zaidi ya kipato chako.
    Hujajua pia kuwa haupaswi kukopa pesa ili utumie ili uje ulipe.
    Hujajua pia kuwa mtu akikuahidi pesa, haupaswi kuiweka kwenye hesabu zako mpaka utakapokuwa umeipokea mikononi mwako.

    Hiyo ndio misingi ya pesa miiko ya pesa.

    HITIMISHO.
    Naamini baada ya kuwa umesoma hapa, hutakuja kukosa mia mbovu kuanzia leo. Maana tayari unajua jinsi pesa inavyopatikana mpaka inavyotumika. Nikutakie kila la kheri.


    3. Ni Bora kuzaliwa mbwa ulaya

    Kuna wanaosema ni bora kuzaliwa mbwa ulaya kuliko kuzaliwa mtu Tanzania/Afrika.

    Hiki Ni kiwango cha juu kabisa cha kutojikubali. Usipojikubali wewe unadhani nani atakuja kukubali wewe. Unapaswa kujikubali wewe kwa namna ulivyo.

    Nakumbuka miaka kadhaa ya nyuma  kuna mtu wa karibu alinifuata na kuniambia kuwa alikuwa hapendi ufupi aliokuwa nao. Bora angekuwa mrefu kidogo. Niliwahi kuona pia mdada mmoja ambaye alikuwa hapendi mwonekano wa masikio yake. Kitu hiki Ni kibaya Sana. Na kinakufanya ushindwe kufanyia kazi mambo unayoweza kwenye maisha yako.

    Upo hapo ulipo kwa sababu maalumu,na kusudi maalumu. Ndio maana umezaliwa sehemu ulipozaliwa, ukaenda kusoma shule uliyosoma, ukakutana na watu ambao umekutana nao. Yote hiyo ni maandalizi ya siku ambapo utapaswa kutumia nguvu na uwezo wako.

    Konekisheni unazokutana nazo leo hii ni maalumu kwa ajili ya kuja kukufikisha sehemu fulani, watu unaokutana nao  watakuja kukusaidia ukianza kutumia fursa zilizokuzunguka.

  • Kama Huna Fedha Basi Kuna Maeneo Haya Matano Unayakosea

    2. Sina fedha/sina hela

    Hii ni kauli ambayo moja kwa moja inakufunga na kukufanya usione upenyo wa kutoka. Ukisema sina hela maana yake unakuwa unainyima akili uwezo wa kufikiri nje ya boksi na kuona fursa gani zaidi unazoweza kupata.

    Badala ya kusema sina fedha, unaweza kujiuliza hivi hapa nawezaje kupata fedha? Au ni mbinu gani naweza kuitumia kupata fedha? Ukisema hivi unakuwa umeifungua dunia nyingine ya fursa na kuona vitu ambavyo watu hawaoni.

    Kuna misemo ambayo imezoeleka kutolewa na watu siku hizi kiasi kwamba imekuwa ni sehemu ya pili ya maisha ya hawa watu. Unakuta mtu anasema “usawa huu wa Magufuri pesa imekuwa ngumu sana”. Utasikia mwingine anasema “vyuma vimekaza” wakati mwingine akitaka kukwambia kuwa hana pesa basi utasikia akisema, “sina hata mia mbovu”. Yaani kumaanisha kuwa hana kitu kabisa mfukoni mwake.

    Ukifuatilia kwa umakini. Yaani kwa jicho la tai anayeuangalia mchezo kutokea juu angani na kutoa tathimini, unaona wazi kabisa kuwa suala la vyuma kukaza sio jambo la leo au jana.  Historia inaonesha kuwa katika kila nyakati kumekuwa na mambo kadha wa kadha ambayo yamekuwa yakitokea na kusababisha vyuma kukaza. Hata hivyo kitu kimoja kimebaki uhakika siku zote. Wale wanaotengeneza pesa siku zote huwa hawaoni kukaza kwa vyuma kama tatizo. Badala yake huwa wanaona fursa kwenye hilo.

    Ngoja nikueleze kiundani suala hili ili uweze kunielewa. Kukaza kwa vyuma kama wanavyosema wengine maana yake ni kutokuwepo kwa pesa. Sasa tujiulize ni kitu gani kinakufanya wewe ukose pesa?  Unaweza kuwalalamikia watu wote duniani ila mwisho wa siku mtu anayesababisha kukaza kwa vyuma ni mmoja tu. Na mtu huyu ni wewe.  Hii unatokana na ukweli kwamba pesa inafuata mkondo kwa wale wanaoiita. Kama wewe hauiiti ije kwako haiwezi kuja, utapishana nayo njiani tu.

    Leo hii nataka nikuoneshe namna utakavyoiita pesa ije kwako na iendelee kuwa ya kwako milele na milele. Siku nyingine kabla hujasema pesa ni ngumu hakikisha unarudi hapa kusoma andiko hili ili uone Kama umelitendea haki. Ila kama utasoma hapa na kuishia tu kusema kuwa huyu jamaa anaandika vizuri basi mimi nakuhakikishia utaendelea kusema kuwa pesa ni ngumu. Kama utasoma hapa na kufanyia kazi ulichojifunza hapa, basi tutakutana sehemu siku moja ukifurahi kwa sababu ya kile ukichojifunza hapa siku ya leo.

    MOJA, KAMA PESA NI NGUMU MAANA YAKE HUJATOA HUDUMA KWA JAMII
    Zig Ziglar amewahi kusema kuwa utapata kitu chochote unachotaka kama utawasaidia watu kiasi cha kutosha kupata kile wanachokitaka. Kitu ambacho unapaswa kuelewa hapa ni kuwa kuna watu wana pesa zako mkononi mwao. Ila hizo pesa hazitakuja kwako kirahisi. Labda uwakabe (na ukifanya hivyo jela itakuwa rafiki yako). Ila njia pekee ya kuzitoa hizo pesa kwa watu na kuzileta kwako ni kuhakikisha kuwa una bidhaa ambayo unaweza kuwauzia hao watu. Hiki kitu ndicho Zig Ziglar anakiita kuwasaidia watu kupata WANACHOTAKA.
    Kuna watu wanahangaika kwa sababu huduma fulani hawaipati vizuri. Lakini wewe ukiweza kuwafikishia hiyo huduma kwa ustadi watakuwa tayari kukulipa na hiki ndicho Zig Ziglar anakiita kuwasaidia watu kupata WANACHOTAKA.

    Kuna watu hawajui kwamba wewe ni mtaalamu na umesomea ujuzi fulani chuoni. Sasa huo ujuzi uliojifunza chuoni ukiweza kuutafsiri na kuuleta kwenye maisha ya kawaida hapa mtaani. Ukautumia ujuzi huo kuwasaidia watu kupata kitu fulani ambacho unaona kitaalamu hakifanyiki vizuri. Hapo utakuwa umewasaidia watu kupata kitu wanachokitaka.

    Nikukumbushe kuwa pesa hazitakuja kwako kama wewe utakuwa tu umelala halafu unaishia kusema pesa ni ngumu au vyuma vimekaza. Pesa itakuja kwako pale ambapo utaamua kutatua matatizo ambayo jamii inakumbana nayo.
    Muuza maji hapati pesa kwa kuuza maji bali kwa kutatua tatizo lako la kiu.

    Mtu daladala hapati pesa kusafirisha abiria, bali kwa kutatua tatizo lako la kusafiri na kufika eneo husika mapema.
    Mitandao ya simu haipati pesa kwa kuuza vocha bali kwa kuunganisha na watu walio mbali na wewe.
    Wewe unatatua tatizo gani?

    Shida yako wewe imelala kwenye  haya maeneo mawili.
    Kwanza unaamini kuwa hakuna kitu kingine kipya unaweza kufanya kuondokana na hali hiyo uliyonayo.

    Yaani, umejikatia tamaa mwenyewe. Na kama umekata tamaa mwenyewe hata akitokea mtu akakupa mamilioni ya pesa hayatakusaidia. Cha kufanya inuka tena na anza kupambana.

    Tatizo lako la pili, unaona kuwa haya ninavyoongea hapa yanawafaa wengine na sio wewe. Huchukui hata hatua ya kuanza, unabaki kusema tu haya yanawafaa watu wenye hela zao bana. Hivi unadhami hao unaosema wana hela zao walizaliwa nazo? Kuna wengine walikuwa na maisha mabaya pengine zaidi ya wewe. Kuna wengine walikuwa na madeni makubwa kuliko hata wewe hapo. Ila walisimama wakabeba majukumu yao na sasa unawaonea gere. Usipochukua hatua UTAJIJU.

    2. KAMA PESA NI NGUMU MAANA YAKE UNAWAHUDUMIA WATU KIDOGO

    Kiasi cha pesa unachoingiza kinaweza kuniambia ni idadi gani ya watu unaowahudumia. Kama unaingiza pesa kidogo maana yake UNAWAHUDUMIA WATU KIDOGO. Kama kuna kiasi kikubwa unaingiza maana yake unawahudumia watu wengi. Hii wala hata sio hesabu ngumu kama unavyofikiria.

    Ebu tuseme wewe na Paulo mnauza maji. Paulo anawauzia watu 1000 na wewe unawauzia watu 100 kila siku na kipimo mnachotumia kuuza ni kile kile, bei pia sawa, unadhani nani atapata pesa zaidi?

    Ukiona pesa ni ngumu unapaswa kujua kuwa unawahudumia watu kidogo. Kama umeajiriwa ujue unafanya biashara na mteja mmoja tu ambaye ni bosi wako. Sasa usitegemee ulipwe kwa viwango sawa na mtu ambaye anatoa huduma kwa wateja mia, elfu au laki moja.

    3. KAMA PESA NI NGUMU UJUE KUWA HUJAJUA MISINGI NA MIIKO YA PESA.

    Ni kawaida kuwa mwanasheria akienda chuoni lazima atafundishwa misingi ya sheria na miiko kwenye sheria. Daktari pia anafundishwa misingi na miiko.

    Mwajiriwa kazini ataambiwa mambo anayopaswa kufanya kazini na yale anayopaswa kuepuka. Pesa pia ina misingi yake na miiko yake. Ukiona ni ngumu kwako basi ujue hii misingi hujaijua.
    Hujajua kuwa unapaswa kuweka akiba kwa kila kiasi unachopata.
    Hujajua pia kuwa unapaswa kupunguza matumizi yako na kubaki na mtumizi ya lazima tu.
    Hujajua kuwa unapaswa kuanza kuwekeza ili pesa yako ikuzalie pesa zaidi.
    Hujajua kuwa haupaswi kutumia zaidi ya kipato chako.
    Hujajua pia kuwa haupaswi kukopa pesa ili utumie ili uje ulipe.
    Hujajua pia kuwa mtu akikuahidi pesa, haupaswi kuiweka kwenye hesabu zako mpaka utakapokuwa umeipokea mikononi mwako.

    Hiyo ndio misingi ya pesa miiko ya pesa.

    HITIMISHO.
    Naamini baada ya kuwa umesoma hapa, hutakuja kukosa mia mbovu kuanzia leo. Maana tayari unajua jinsi pesa inavyopatikana mpaka inavyotumika. Nikutakie kila la kheri.

  • Ifahamu Kanuni Ya Asilimia Moja Na Jinsi Ya Kuitumia

    Hii ni kanuni ambayo ukiifahamu utaishi maisha mazuri na utafanya makubwa kwa nguvu kidogo sana.

    Yaani, itakuwa kama unagusa tu na mambo yanajipanga.

    Kulingana na kanuni hii ni kwamba, Kila siku kwako inapaswa kuwa ni siku ya kukua kwa asilimia moja tu.

    Kama umeweka malengo basi siku ya leo yafanyie kazi kwa asilimia moja, na kesho yafanyie kazi kwa asilimia moja nyingine, hivyohivyo na kesho kutwa na siku zifuatazo. Baada ya muda hizo siku moja moja zitaunganisha nguvu na hizo asilimia moja moja zitaungana na kuleta matokeo mkusanyiko ambayo ni makubwa.

    Kama una biashara, Kila siku ikuze kwa asilimia moja tuu. Leo ongeza bidhaa fulani ambayo watu wanahitaji ila hawapati kwako. Kesho boresha huduma kwa wateja
    Kesho kutwa hakikisha hesabu za biashara zipo sawa n.k.

    Baada ya muda nguvu ya riba mkusanyiko itafungamana na kutengeneza kitu Kikubwa.

    Kama upo kwenye mahusiano unaweza kuitumia pia hii kuboresha mahusiano yako na kufanya nyumba yako kuwa mbingu hapa duniani . Kila siku, ifanye kuwa siku ya kuboresha mahusiano yako. Siku ya leo boresha mahusiano yako kwa asilimia moja tu. Leo unaweza kuandika barua ya kumpongeza mwenza wako kwa kupika wali mzuri.
    Kesho ukamletea zawadi ya heleni.
    Keshokurwa ukampa muda wa kuongea na wewe ili atoe ya moyoni. Kwa vyovyote vile hakikisha kila siku unakuza mahusiano yako kwa asilimia moja tu basi.

    SOMA ZAIDI: Sheria Tano Za Nguvu Zitazokusaidia Kushinda Mengi Kwenye Maisha Ya Mtaani. Zifuate Kwa Faida Yako, Zivunje Kwa Hasara Yako

    Unataka kusoma vitabu? Tumia kanuni hii hii katika usomaji. Kila siku soma kurasa kadhaa. Kurasa hizi zitakuongezea maarifa na kukufanya uwe bora kila kunapokucha.

    PATA ZAWADI YA KITABU CHA BURE HAPA

    Unataka kuamka mapema. Anza kesho kuamka saa 12 kasoro dakika moja. Kisha kila siku amka dakika moja kabla ya ile ya jana. Kama kesho kesho ukiamka saa 11 dakika 59, kesho kutwa amka saa 11 dakika 58 Utajikuta una uwezo wa kuamka muda unaotaka wew.

    SOMA ZAIDI: Kuamka Asubuhi Na Mapema Ni Tabia (Njia Sita Za Uhakika, Zilizothibitishwa Na Zisizoshindwa Zitakazokuwezesha Kujenga Tabia Ya Kuamka Asubuhi Na Mapema)

    Unataka kuandika kitabu? Andika maneno 500 kila kwa mwezi utakuwa umeandika maneno 15,000+. Maneno 500 siyo mengi Sana. Ila ukiyaandika kwa siku 30 mkusanyiko wake ni mkubwa Sana.

    Unataka kufanya mazoezi? Tumia kanuni hiihii, leo Anza na push-up moja tu. Kesho piga push-up mbili. Keshokutwa tatu. Unaona eeh, yaani huhitaji kutunia nguvu kubwa kufanya mabadiliko. Unatumia nguvu kidogo ila unafanya mabadiliko makubwa. Hivi kweli hata muda muda wa kupiga push-up moja utakosa leo. Kweli?

    SOMA ZAIDI: HUWEZI KUMKODISHA MTU WA KUKUPIGIA PUSH UP

    Unataka kujifunza lugha mpya? Anza tu kwa kwenda dukani na kununua daftari ya kutumia kujifunza lugha. Kisha kila siku jifunze neno moja la ziada.
    Kwenye kitabu cha KUTOKA UMASKINI MPAKA MAFANIKIO CHA ERICK SHIGONGO ameeleza alivyokuwa akijifunza misamiati kidogo tu ya kiingereza kila siku na hatimaye akawa MBOBEVU kwenye kiingereza.

    Yaani, kwa kutumia hii nguvu unaweza kufanya chochote unachotaka hapa duniani. Hakuna kitakachokushinda.

    Kitu kimoja labda ni kwamba Kuna uamuzi usipoufanya leo, muda utapita na utaishia tu kujuta kwa nini hukufanya uamuzi. Usipoanza kuweka akiba leo, miaka 10 ijayo utakuwa bado unalia kuwa huuna mtaji. Sasa si Bora tu uanze kutumia hii kanuni ya asilimia moja kuanzia leo.

    Usipoandika kitabu chako leo hii, miaka 10 ijayo utakuwa unalalamikiwa kuwa ulikuwa na ndoto ya kuwa mwandishi ila hujaandika.

    Mimi sitakuvumilia, ndio maana leo nimekwambia mapema ili uanze kuchukua hatua.

    Kuna mzee mmoja alikuwa na ndoto ya kuwekeza kwenye kilimo cha miti tangu miaka 1990. Hakufanya hivyo kwa kuhairisha kila mara.
    Vijana walikuja kupanda miti miaka ya 2005 na Sasa hivi wanakula matunda yeye anaishia tu kusema Bora ningepanda miti miaka hiyo.

    Sitaki uje kujuta. Chukua hatua kuanzia leo hii. Inawezekana.

    NB. Kama unataka kuachana na tabia mbaya, amua tu kuwa unaachana nazo mara moja. Usiache pombe kwa kanuni ya asilimia moja.
    Usiache sigara kwa kanuni ya asilimia moja.
    Usiache uzinzi kwa kanuni ya asilimia moja.

    Hivi vitu amua tu kwamba unaachana navyo na muda uoiokuwa unautumia kufanya hivi vitu vibaya utumie kufanya vitu vya maana na vitu vya kukujenga.

    Sambaza upendo, sambazabujumbe huu kwa rafiki zako pia.

    Ni Mimi rafiki yako wa ukweli
    Godius Rweyongeza

    0755848391

    Morogoro

  • Mitandao Ya Kijamii Kama Dozi

    Siku hizi mitandao ya kijamii imekuwa ni aina mpya ya dozi. Na dozi hii haitumiki mara mbili kwa siku au mara tatu.mtu anatumia dozi hii kadri anavyojisikia.

    Na kuna mwingine aina hii ya dozi anaitumia ikiwa ya kwanza anapoamuka na bado anaendelea kuitumia siku nzima mpaka kulala.Je, hayo ni matumizi sahihi ya mitandao?

    1. Jiwekee utaratibu wa kuwekeza muda wako kwenye mambo ya muhimu

    2. Usiingie mtandaoni hovyohovyo kiasi cha kuharibu ufanisi wa kazi zako. Kuwa na utaratibu maalumu na ingia kufanya vitu vya maana.

    3. Fanyia kazi vitu chanya unavyojifunza mtandaoni. kila la kheriKuna mafunzo nimekuandalia leo kwenye channel yangu ya Youtube. ingia hapa kujifunza.

    👇Hivi Huu Mshangao Nilionao Na Wewe Unao? Au Kwako Ni Kawaida Tu?

    TUWASILIANE 0755848391Usisahau KUSUBSCRIBE

  • Jinsi Ya Kulipwa Kwa Kufanya Kile Unachopenda

    Unaendeleaje rafiki yangu.

    Leo ni siku ya kipekee sana. binafsi nimeona nije kwako kwa lengo la kukueleza kitu kidogo tu, namna ambavyo wewe unawezakulipwa kwa kufaya kitu unachopenda.

    Zamani mambo yalikuwa shaghalabaghala. Ulikuwa unatakiwa kusoma kozi fulani na baadaye kwenda kufanya kufanya kazi hata kama kozi au sekta husika ulikuwa huipendi. Ila leo hii mambo yamebadilika, kuna njia mpya za kukusaidia wewe kufanya kile unachopenda na hata ukaweza kulipwa kwa hicho kitu.

    Labda kwanza nikuulize wewe, ni kitu gani ambacho unapenda kufanya maishani mwako? Ni kitu gani ambacho haipiti siku bila ya wewe kukifanya? Ni kitu gani hicho?

    Nimeshuhudia watu wakilipwa kwa vile vitu wanavyofanya kuanzia kwa waangalia tamthiliya, wasoma vitabu, wapenzi wa mpira, waandishi, public spkeakers, walimu, watafiti n.k.

    Ngoja nikuulize tena, wewe ni kitu gani ambacho unapenda kufanya kutoka moyoni? Je, ungependa kulipwa kwa kufanya hicho kitu. Basi kaa mkao wa kula

    Kama wewe ni mpennzi wa kusoma vitabu, siku za nyuma nilishaelez namna ambavyo unaweza kulipwa kwa kusoma vitabu hapa.

    Hakikisha umeangalia video hii youtube: imeeleza mbinu za kulipwa kwa kusoma vitabu

    Kwa ambao wanapendelea kufanya vitu vingine tuendelee mbele.

    Kwanza ukishajua ni kitu gani ambacho unapenda, unapaswa kwenda hatua ya ziada na kuanza kufanya kile kitu hata kama ni kwa udogo. Anza kufanya kile kile na washirikishe watu wajue kwamba wewe ni mtaalamu kwenye hicho kitu.Aanza kujenga hadhira ya watu ambao wanafuatilia kazi zako.

    Kama unapenda kuimba, anza kuimba.

    Kama unapenda kuchora,  chora.

    Kama unapenda kuandika andika.

    Kiufupi kwa chochote kile unachopenda kukifanya basi hakikisha kwamba unatafuta namna ya kuwafanya watu wajue kwamba unachopenda kufanya kutoka moyoni ni hicho.

    Na njia nzuri ya kuwaambia watu ni kwa wewe kufanya na kuweka kwenye vitendo kile unachopenda.

    Unaweza kufanya hivyo kwa kurekodi video na kuwashirikisha au kwa kuandika makala au kwa kuchora na kuweka michorao yako mtandaoni.

    Hii ni hatua ya kwanza ambapo utajitambulisha kwa watu na watu wataanza kujua kwamba upo.

    Hatua ya pili ni kuhakikisha kwamba unaanza kujenga timu ya wafuasi kindakindaki. Kwenye wale wafuasi wako, kuna wale ambao watakuwa wanapenda kufuatilia kazi zako kwa ukaribu zaidi. Yaani, wale watakaokuwa wanapenda kufuatilia kazi zako kiasi kwamba ikitokea ukakaa kimya kwa siku mbili au tatu kabla hujatoa kazi zako kulingana na utaratibu wako watakupigia mpaka simu kujua kuna kitu gani ambacho kinaendelea.

    Kama unatoa mafunzo kwa  njia ya video au sauti, kuna watu watakuwa wanafuatilia kazi zako kiasi kwamba ikipita siku moja au mbili ukiwa hujatoa kazi yako watahoji kwa kutuma jumbe fupi au hata kupiga simu.

    Hawa ni watu wachache ambao unawahitaji kwenye safari yako.

    TATU, jiwekee utaratibu wa kuwa unatoa kazi zako. unapaswa kuwa na utaratibu maalumu wa kutoa kazi zako, kama unatoa kazi zako mara moja kwa wiki au kila siku, hakikisha kwamba unafanya. mfano mimi ukija hapa kwenye hii blogu, ni lazima tu  kila siku zitawekwa makala mbili mpya. kila siku. Sasa na wewe tengeneza kijiutaratibu chako na kifuate.

    Nne angalia ni namna gani unaweza kutengeneza bidhaa inayoendana na wafuasi wako.

    Kama utafuata hatua ya kwanza na pili vizuri, hatua ya nne ni rahisi sana, hasa kwenye ulimwengu wa leo. Kadiri utakavyokuwa ukifanya kile kitu unachofanya, kuna watu watajitokeza kwa kuuliza maswali. Haya maswali unayoulizwa, kuwa makini nayo, maana hizi ndizo dukuduku ambazo zinawasumbua watu. sasa na bidhaa zako hazipaswi kwenda mbali sana na hizi dukuduku. Hivyo unaweza kutengeneza bidhaa au huduma katika namna ya kujibu hayo maswali.

    Tano, uza bidhaa uliyotengeneza kutokana na dukuduku au tatizo linalowakumba watu. Kwa kuwa ulishawasoma watu tangu mwanzo, sasa kifuatacho ni wewe kuanza kuwapa huduma au kitu ambacho walikuwa wanauhitaji wao. Kile ambacho wao walikuwa wanakuuliza mara kwa mara.

    Na hapa kwenye kuuza kuna watu ambao wataanza kukwambia kwamba haupaswi kuuza kitu chochote, badala yake huduma zako zote zinapaswa kuwa bure. Ila siyo kweli, kuna huduma ambazo watu wanapaswa kulipia na kuna huduma za bure. Kama ni huduma za kulipia, basi ziwe za kulipia kweli ili zikuwezeshe wewe kujikimu na kuweza kuendelea kutoa huduma nyingine zaidi.

    Mimi ukija hapa kwenye blogu, utakutana na makala mbili za kukuelimisha wewe kila siku. Huzilipii chochote, lakini pale ninapoandika kitabu, basi utatoa kiasi kidogo kupata kitabu au kozi husika.

    Nashauri pia usome ebook ya KIPAJI NI DHAHABU. Ina mengi ya kukusaidia wewe kwenye kujenga kipaji chako, kukikuza na kukiendeleza. Baada ya kusema hayo, naomba nikutakie kila la kheri.

    KIPAJI NI DHAHABU: Jinsi Ya Kukigundua, Kukinoa Na Kutumia Kipaji Chako Kwa Manufaa

    NB. Nashauri sana uhakikishe kwamba kazi zako ni za viwango mara zote.

    Ni mimi

    Godius Rweyongeza

    0755848391

    Morogoro-Tz

X