-
Karibu Kwenye Semina Ya Kufanya Makubwa Mwaka 2023: Fanikisha Ndani Ya Miezi Sita Kile Ambacho Wengine Huwa Wanafanya Kwa Mwaka Mzima

Rafiki Yangu mpendwa, bila shaka unaendelea vizuri kabisa. Moja ya jambo la msingi kabisa ambalo unahitaji kuhakikisha kwamba umelifanya kwenye maisha yako ni kujenga utaratibu wakujifunza. Kujifunza kunaweza kuwa kupitia kusoma vitabu, kusikiliza mafunzo ya sauti au mafunzo ya vitendo pamoja na semina.
Kwa kulitambua hili, mwaka huu tutakuwa na semina ya ana kwa ana ambayo itafanyika tarehe 24 juni. Itakuwa ni siku ya jumamosi na itafanyika hapa mkoani Morogoro.
Lakini kabla sijajuelez zaidi kuhusu semina, ebu kwanza tuongee kuhusu uhitaji wa wewe kufanya makubwa.
Eb u pata picha malengo uliyoyaweka ndani ya mwaka huu 2023, je, kuna hatua ambazo unaona unapiga? Je, unaona kwamba unaweza kuwa unapiga hatua zaidi lakini haujui ni kwa namna gani ambavyo unaweza kupiga hizo hatua zaidi?
Je, unajiuliza ni vitu gani ambavyo vinahitajika kwako ili kuhakikisha kwamba unapiga hatua na kuweza kufanya makubwa, naam, makubwa sana.
Nalijua hilo nap engine hilo siyo kwamba linakusumbua wewe peke yako, ni jambo ambalo linawasumbua wengi. mtu anakuwa na malengo, anaweka malengona anaanza kuyafanyia kazi, ila sasa mwisho wa siku mtu huyo anashindwa kuyafanyia kazi malengo yake mpaka kufikia mwisho. Ukifuatilia kwa undani unaweza kugunda kuwa kuna vitu viwili ambavyo vinamzuia mtu.
Msukumo wa ndani wa kufanikisha kile alichopanga au
Kukosa mbinu sahihi za kumwezesha kufanikisha malengo yake.
Kwa kulitambua hilo, nimekuandalia semina ambayo inaenda kuchoche moto wa wa wee kufanya makubwa na kuweza kufanikisha malengo yako ndani ya mwaka 2023.
Semina hii inaitwa SEMINA YA KUFANYA MAKUBWA, siyo kwa bahati mbaya, bali kwa sababu kuna maana yake.
Kwenye hii semina tunaenda kujifunza namna ambavyo unaweza kufanikisha makubwa ndani ya miezi sita, wakati wengine huwa wanafanyia kazi hayo kwa miaka mmoja mpaka miaka miwili. Unaweza kujiuliza hili linawezekanaje. Kiufupi ni kwamba linawezekana maana tumekuwa tukililifanyia kazi kwa muda sasa, kinachofuata ni kuhamishia kile ambacho tumekuwa tukikifanyia kazi kwako ili na wewe uweze kukifanyia kazi kwa muda mfupi kuliko ambavyo umekuwa ukitegemea.
Sambamba na hilo kwenye hii semina tunaenda kujifunza mambo mengine mazuri ambayo yatabadili maisha yako na mwelekeo wa maisha yako kiujumla.
Tunaenda kujifunza juu ya safari ya kuelekea uhuru wa kifedha, kwenye hii semina tutaona namna ya kuianza safari hii hatua kwa hatua, tutaona namna ya kuendedelea na hii safari na hatimaye kuhakikisha kwamba hii safari inakamilika.
Lakini siyo kwamba tutaishia hapo, tutaona namna ya kuamsha uwezo ulioala ndani yako na kuutumia kwa viwango vya juu ili uweze kufanikisha hayo yoooe ambayo tumekuambia.
Kuna watu ambao huwa wanaogopa kwamba hivi vitu, vinaweza visifanye kazi. tutaona namna ya kuondoa hofu ya kufanyia kazi malengo na ndoto zako na namna ambavyo unaweza kuwa na maisha unayotaka baada ya kuwa umeondoa hiyo hofu.
Hatutaishia hapo tu kwa wale walio kwenye mahusiano, tutaona namna ambavyo mnaweza kufanikiwa kifedha mkiwa kama wenza.
Kiufupi hii semina itakuwa imejaa mengi kwa ajili yako. Na itakuwa ni semina ya siku nzima. Semina hii itaanza saa moja asubuhi na itamalizika jioni saa 12.
Tutakuwa na siku moja nzima ambapo tutjitenge na uliwewengu na kukaa kwenye mazingira ambayo tutajifunza namna ya kupindua mambo mengi kwenye maisha yetu.
Baada ya hii semina, kitakachofuata ni kuchukua hatua na kufanyia kazi yale tutakayokuwa tumejifunza.
Hivyo, sasa naomba rasmi nichukue nafasi kukukaribisha kwenye semina hii ya kipekee.
SEMINA HII ITAFANYIKA hapa morogoro,. Itafanyika siku ya jumamosi, na itakuwa ni semina ya siku nzima kuanzia saa moja asubuhi mpaka jioni. Chakula na bites vyote utapata kwenye hii semina.
Gharama ya semina hii itakuwa ni shilingi 50,000/-
Na mwisho wa kufanya malipo kwa ajili ya semina ni tarehe 15.6.2024
Karibu sana kwenye semina ya kufanya makubwa mwaka 2023. Mwaka 2023 haturembi mwandiko!
Kwa kumalizia ningependa kukumbusha mambo machache tu.
- Semina itafanyika tarehe 24, Juni, 2023.
- Itakuwa ni siku ya jumamosi
- Itafanyika kuanzia saa moja asubuhi mpaka jioni saa 12
- Gharama ya semina ni 50,000/-
- Chakula na bites vitakuwepo.
Cha kufanya ni wewe kuthibitisha malipo yako sasa hivi. zifuatazo ni namba ambazo zitatumika kufanya malipo ya semina.
*NMB: 22110047274 JINA NI GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA*
*Mpesa: 0755848391*
*Airtel money: 0684408755
*JINA NI GODIUS RWEYONGEZA*
Kitu cha kufanya leo.
Siku ya leo fanya kitu kimoja tu rafiki yangu.
Tuma ujumbe wa kuthibitisha ushiriki wako kwenye semina. Tuma ujumbe huu kwenda whatsap
0755848391 au bonyeza hapa
Kisha niambie, utalipia kwa mpango gani.
Utalipa kiasi chote kwa pamoja au takuwa unalipa kila wiki, au kila mwezi na kiasi gani utakuwa utakuwa unalipia?
Tuma ujumbe wako hapa
Mfano:
*Mimi GODIUS RWEYONGEZA nathibitisha kushiriki semina ya mwezi wa sita*
*Nitalipia kiasi chote kwa pamoja tarehe 15 MACHI, 2023.*
*JIUNGE NA KUNDI LA WALIOTHIBITISHA KUHUDHURIA*
Karibu sana
-
Jinsi Ya Kujenga Mafanikio Makubwa Hata Kama Hauna Kitu
Hapo zamani za kale, ili kujenga utajiri ulipaswa kuwa na ardhi kubwa, ng’ombe na vitu vingine vinavyoendana na hivyo. Ulipokuwa na vitu vya aina hiyo, hapo sasa ndipo watu walikuwa wanasema kwamba mtu fulani ni tajiri. Ila leo hii mambo yamebadilika.
Baadaye ilikuwa inaaminika kwamba ili kujenga utajiri unapaswa kuwa walau na konekisheni na ndugu au mtu ambaye ni tajiri au ambaye anafanya kazi kwenye taasisi kubwa. ila leo hii mambo hayo yote yamebadilika, huhitaji kuwa na konekisheni wala ndugu yako ambaye anafanya kazi serikalini, huhitaji kuwa fisadi, huhitaji kuwa mashamba mengi wala ng’ombe elfu. Unahitaji kutumia kile ulinacho. Na kwa sababu hiyo, siku ya leo ninaenda kuandika makala ya kina inayoeleza namna ambavyo unaweza kufanikiwa kwa viwango vikubwa hata kama hauna kitu.
Hatua ya kwanza ya kujenga mafanikio makubwa hata kama hauna kitu ni
1. KUJUA KITU UNACHOPENDA NA KUANZISHA BIASHARA KWENYE KILE UNACHOPENDA
Rafiki yangu, najua kuna vitu kadha wa kadha unapenda hivi kwako vinapaswa kuwa sehemu ya kuanzia. Haitoshi tu wewe kila siku kwenye kuangalia mechi kila siku, huku ukishangilia kwamba Mayele kafunga au hajafunga. Baala yake unapaswa kuangalia fursa iliyojicicha kwenye hicho kitu mbacho unapenda na namna ambavyo unaweza kuitumia hiyo fursa kufanya makubwa.
Ukishajua kitu ambacho unapenda, basi acha kufanya mambo mengine yoyote yale, badala yake wekeza nguvu na muda wako kwenye hicho kitu unapenda.
Jenga biashara kwenye hicho kitu. Jenga hata biashara ya kuanzia chini.
2. ANGALIA RASILIMALI ZILIZO KWENYE MAZINGIRA YAKO UNAZOWEZA KUANZA KUTUMIA SIKU YA LEO
Kuna rasilimali ambazo naamini unazo ambazo unaweza kuanza kutumia.unaweza ukawa unafikiria kufanya makubwa sana ambayo pengine hayajawahi kufanyika kwenye hii dunia, lakini unachopaswa kufahamu ni kwamba, hayo makubwa unaweza kuanza nayo kidogo kidogo na kwenda nayo hatua kwa hatua mpaka ukaweza kuyafanya kuwa makubwa zaidi.
Kuna rasilimali nyingi zimekuzunguka ambazo unahitaji kuhakikisha kwamba umezitumia. Nguvu zako, muda wako, mazingira yaliyokuzunguka na mengine mengi. Tumia hizi rasilimali kuhakikisha kwamba unafanya makubwa. Naam, makubwa sana.
TATIZO SI RASILIMALI ZILIZOPOTEA
3. TOA THAMANI KUBWA TENA BURE
Najua u ataka kulipwa tena kwa viwango vya juu. IlA NJIA NZURI YA wewe kuweza kulipwa ni kuanza na kile ulichonacho, ukiweza kufanyia kazi vizuri kile ulichonacho, utaweza kufanya makubwa sana. tumia kile ulichonacho kwanza.
4. JIPE MUDA
Kila kitu hakitaweza kufanyika ndani ya siku moja. unahitaji kujipa muda ili kuweza kujenga mafanikio ambayo unataka. Mafanikio makubwa hayajengwi ndani ya siku moja au wiki moja. badala yake ni kwamba yanachukua muda.
5. JIJUE MWENYEWE
Jijue mwenyewe ni vitu gani unaweza zaidi kuliko vingine. badala ya kupambana kufanya kila kitu, wekeza nguvu na muda wako kwenye vitu vichache ambavyo unaweza kuliko kufanya kila kitu bila mpangilio.
6. PAMBANA KWA BIDII
Rafiki yangu, malengo yako na ndoto zako unapaswa kuzipambania kwelikweli bila ya kurudi nyuma. Na hili hakikisha kwamba unalifanyia kazi bila ya kurudi nyuma. Kiufupi. Hakikisha kwamba kila unapoamka mpaka unapoenda kulala, unakuwa umepambana na kupambana zaidi. ukiona imepita siku bila ya kufanya kitu chochote kwenye ndoto yako. Basi ujue hiyo siku umeipoteza.
Cha kufanya pale wenzako wanapokuzidi elimu, kipaji, ujuzi konekisheni n.k.
7. TUNZA MUDA WAKO VIZURI
Muda ndiyo rasilimali pekee ambayo inaweza unayo bure na ambayo ukiipoteza unakuwa umeipoteza. Kwa hiyo basi, mara zote pambana kuhakikisha kwamba unautumia muda wako kwa uzuri na kwa weredi mkubwa kuhakikisha kwamba muda wako unakuwa wenye manufaa.
Watu wanaofanikiwa sana na wale ambao hawafanikiwi sana wana muda uleule. Tofauti kati ya wale wanaofanikiwa sana na wale ambao wanakuwa na mafanikio ya kawaida ipo kwenye matumizi ya muda. Hivyo basi, ili uweze kufanya makubwa unapaswa kuhakikisha kwamba unautumia vizuri muda wako. Anza na dakika yako moja ya sasa, kisha pangilia saa lako moja la baadaye na kisha siku yako nzima. Muda wako ni rasilimali muhimu sana ambayo unapaswa kuitumia vizuri sana.
8. PENDA MCHAKATO
Mchakato ni muhimu zaidi kuliko lengo. Watu wengi huwa wanaweka malengo mwanzoni mwa mwaka, ila malengo ni kitu kimoja. Kufanyia kazi yale malenngo ndio jambo lenyewe haswa. Na hili ndilo ambalo ningependa ulifahamu siku ya leo
9.ACHA KUJALI SANA KILE AMBACHO WENGINE WANAFIKIRIA
Najua kuna mengi sana ambayo watu wengine wanafikiria. Acha kujali sana mambo ambayo watu wengine wanafikiria. Badala yake wekeza muda wako na nguvu zako kwenye kile unachofanya tu.
soma zaidi: Vitu 21 Ambavyo Ni Lazima Kufanya Hata Kama Una Kipaji Kikubwa
Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.
Godius Rweyongeza ni mwandishi wa vitabu zaidi zaidi ya 20. Na ni mwendeshaji wa mtandao wa Songambele. Amekuwa akiandika kwenye huu mtandao huu tangu mwaka 2016. Kitabu chake cha Kutoka Sifuri Mpaka Kileleni kimekuwa #1Best Seller kwa muda sasa kwenye mtandao wa GETVALUE
Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.
Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.
Mtandaoni, vitabu vyake unaweza kuvipata kupitia mtandao wa GETVALUE kwa KUBONYEZA HAPA
-
Kitu muhimu ambacho kila mtu anapswa kukifhamu
Rafiki yangu, najua kuna vitu vingi ambavyo unahitaji kufahamu. Ila siyo kila kitu unachokifahamu kina manufaa chanya kwako. kwa mfano unaweza kufahamu kuwa kuna ajali fulani sehemu fulani, ila siyo kwamba hiyo ajali ina manufaa yoyote kwako. au kwa wewe kufahamu kuwa kuna vita sehemu fulani, hilo kwa kupande wako siyo kwamba linakuwa na matokeo chanya ambayo unaweza kuyatumia.
Ila kwa upande mwingine kuna vitu ambavyo ni muhimu kwako kuvifahamu na baada ya kuvifahamu unapaswa kuhakikisha kwamba umetumia maarifa na kila kitu ulichokipata kwa manufaa zaidi. moja ya kitu ambacho wewe unahitaji kuhakikisha kwamba umekifahamu kwa undani zaidi ni THAMANI YAKO.

Karibu upate kitabu hiki cha kipekee sana. Gharama yake ni 30,000 tu Thamani ni kitu cha muhimu sana ambacho unahitaji kuhaikisha kwamba umekifanyia kazi, tena unahitaji kuhakikish kwamba unakifanyia kazi sasa hivi rafiki yangu
Ukijua thamani yako, utaokoa mengi sana rafiki yangu.
Thamani yako inakusaidia wewe kupangilia muda na kazi zako ambazo unafanya. hii ndiyo kusema kwamba badala ya kufanya vitu hovyohovyo, unakuwa unafanya vitu kwa ustaarabu na kwa utaratibu mzuri ambao umeupangilia. Kitu ambacho hujakipangilia hukifanyi.
Pili kujua thamani yako kunakusaidia kujua vitu vya kukubali kwenye maisha yako na vitu ambavyo unapaswa kukataa. Siyo kila kitu unaweza kukifanya, kuna baadhi ya vitu unaweza kuvikubali na kuamua kuvifanya kwenye maisha yako, ila kuna baadhi ya vitu unapaswa kuacha kuvifanya ili uwekeze nguvu zako na muda wako kwenye kukuza thamani yako zaidi.
Hii inakusaidia kuwekeza muda wako kwenye sehemu zenye nguvu na kuachana na sehemu ambazo hazina nguvu kwa upande wako.
Rafiki yangu kama kuna sehemu ambapo wewe unapaswa kuwekeza muda wako na nguvu zako basi ni kwenye thamani yako. Hakikisha kwamba unaijua thamani yako kw aundani.
Nimeandaa kitabu kizuri kwa ajili yako kitakachokusaidia wewe kwenye hili. Kitabu kinaitwa JINSI YA KUONGEZA THAMANI YAKO.
Karibu sana uweze kujipatia nakala yako siku ya leo.
Kupata nakala tuwasiliane kwa 0684408755 jina ni GODIUS RWEYONGEZA
-
Wewe unapenda kitu gani?

Kati ya vitu vyote, nilipenda vitabu zaidi– Nikola Tesla
Wewe unapenda kitu gani? Nadhani hili ni swali ambalo ukiuliza kwa vijana kama sisi wa siku hizi utapata majibu ya ajabu Sana.
Kama unaweza kuvumilia *pressure,* Basi uliza hilo swali. Ila Kama una *pressure* ya haraka basi usiliuze labda Kama umechoka kula ugali. Hahaha
Nakwambia hivyo, kwa sababu majibu utakayopata kutokana na swali Hilo yatakusikitisha sana.
Mimi sitataja majibu utakayopata, hivyo kaulize mwenyewe…..
Utagundua mwanzoni nimeanza na nukuu ya Nikola Tesla ananasema Kati ya vitu vyote, vitabu ndivyo nilipenda zaidi.
Sijajua wewe upande wako vipi.
Leo nimeona nikusisitize zaidi huu ya umuhimu wa vitabu. Vitabu ni vya muhimu Sana kwenye maisha. Nakumbuka siku za nyuma niliwahi KUANDIKA kitabu kizima kinachoeleza NGUVU KUBWA iliyo kwenye Kusoma vitabu na jinsi ya kuitumia hiyo NGUVU kufanya makubwa.
Nashauri na wewe usome hiki kitabu maana kina Mambo mengi mazuri sana ndani yake ambayo yatakunufaisha na wewe. Na ubora ni kwamba unaweza kukipata bure hapa
Kwa kuwa vitabu vina Mambo mengi mazuri. Leo nataka nikwambie kwamba vitabu vina uwezo wa kukutoa kwenye ukilaza kuwa gwiji. Nikola Tesla ambaye nimeanza kwa kutoa nukuu yake hapo mwanzoni, alikuwa gwiji wa Aina yake.
Alifanya Mambo mengi mazuri kwenye ulimwengu wa ugunduzi. Ni mmoja wa watu wanaoaminika kwamba waligundua redio.
Lakini ukifuatilia nyuma yake unakuta kwamba alikuwa anapenda kusoma vitabu. Sijajua Hilo linakuwaje, Ila kila Mara ukifuatilia historia za watu waliofanya MAKUBWA, Kati ya Mambo mengi ambayo najifunza Kutoka kwa hao watu ni kusoma vitabu.
Ninapoandika hapa nipo nasoma historia ya Mkurugenzi maarufu wa kampuni GE. Jack Welch, nadhani ukitafua Google wakurugenzi Bora wa nyakati zote, Ni lazima Jina la huyu jamaa ulikute.
Lakini kinachonishangaza ni kwamba pamoja na mengine mazuri ambayo alifanya ila bado alikuwa anapenda kusoma vitabu.
Hivyo, nadhani usomaji wa vitabu, unabaki kuwa ni moja ya jambo muhimu sana kwenye ulimwengu wa leo. Yaani, unabaki kuwa ni jambo la muhimu mno.
Kati ya vitu vyote ambavyo utafanya, basi hakikisha kwamba unasoma na vitabu pia. Vitabu Ni muhimu Sana.
Tenga muda hata kama Ni kidogo kuhakikisha unasoma vitabu.
Pakua kitabu Cha bure hapa ili uweze kukisoma zaidi
Kila la kheri
-
Hiki kitu kimoja tu kinaweza kukufanya ulipwe zaidi ya unavyolipwa Sasa
Rafiki yangu, najua Mara kwa mara huwa nakwambia njia mbalimbali za kukusaidia KUONGEZA kipato chako.
Nafanya hivyo kwa sababu nakupenda. Najua wazi kuwa haupaswi kutegemea chanzo kimoja cha kipato. Lakini pia najua wazi kuwa kama chanzo chako kimoja ni ajira Basi maana yake unapaswa kuhakikisha kwamba umepanbana na kuongeza vingie zaidi zaidi ili vitakavyokuingizia kipato bila Kokomo.
Nadhani, kama Kuna mchezo ambao kila mmoja anapaswa kuufurahia hapa duniani Basi ni mchezo wa kuhakikisha kwamba anaongeza kipato chake Mara kwa mara. Na hili linawezekana vizuri sana. Na ndio maana nimekuwa nasukumwa kukwambia njia mbalimbali za kuongeza kipato chako, na hata nimeandika vitabu kadha wa kadha vya kukusaidia kwenye hili Kama kitabu cha
MAAJABU YA KUWEKA AKIBA
JINSI YA KUONGEZA THAMANI YAKO na
MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE.Sasa siku ya leo nataka nikwambie kitu kimoja ambacho kitakufanya wewe uweze kulipwa zaidi ya unavyolipwa sasa. Kitu hiki siyo kingine bali ni uhakika wa kutegemewa kufanya jambo na ukalifanya.
Yaani, kwamba mtu anaweza kujiamini kwamba utafanya Jambo fulani, na kweli Hilo jambo ukalifanya bila shida yoyote.
Hili ni jambo ambalo unapaswa kujijengea.
Moja ya kitu ambacho kimekuwa kinanishangaza ni kuwa vijana wengi huwa wanaandika kwenye CV zao kuwa ni wachapakazi na wanaweza kufanya kazi hata kwenye msukumo mkubwa. Utakuta MTU ameandika kwenye CV yake kuwa “I can work under pressure”. Lakini Sasa njoo kwenye uhalisia. Huyo mtu hawezi kufanya hata za kawaida tu.Ulimwachia kazi na ukaondoka huyo mtu anakuwa siyo wa kutegemewa. Ni mpaka uwepo ndipo anaweza kufanya kazi. Kama haupo hawezi kufanya kazi.
Ukiwa na tabia ya Aina hii huwezi kutegemea kulipwa zaidi kama ambaye anategemea kufanya kitu na anahakikisha kwamba amekifanya.
Hivyo, Kuanzia siku ya leo nataka uwe mtu wa kutegemewa.
Kutegemewa kufanya kazi na ukalifanya.
Kutegemewa utawahi na ukawahi
Kutegemewa kufanikisha kitu au vitu fulani na ukaweza kuvifanikisha.Rafiki yangu, inawezekana na ninakitakia kila la kheri.
-
Hiki kitu kimoja hakiwezi kukupa mafanikio unayotaka
Watu wengi wanapenda kupata mafanikio kiasi kwamba ukiingia kwenye chumba Chenye watu kumi na Kuuliza wangapi wanapenda kufanikiwa? Utashangaaa kuona mikono zaidi ya kumi ikiwa imenyooshwa juu. Kwa Nini? Kwa sababu baadhi ya watu wanapenda Sana mafanikio kiasi kwamba wanakuwa tayari kunyoosha mikono miwili juu.
Japo watu wengi wanapenda mafanikio, Ni wachache Sana ambao wanakuwa tayari kuchukua hatua na kuweka juhudi kupata mafanikio wanayotaka. Unakuta MTU anaendelea kufanya vitu kwa namna ileile waliyokuwa wanafanya babu zake Huku akitegemea kupata matokeo ya TOFAUTI.
Hiki kitu Albert Einstein alikiita ujinga aliposema; ujinga ni kufanya vitu vilevile huku ukitegemea kupata matokeo ya TOFAUTI.
Kumbe kwa mantiki hiyo ili upate matokeo ya TOFAUTI. Ni sharti. Na ninasema sharti uwe tayari kuchukua hatua za TOFAUTI.
Hatua za kuanzisha biashara Kama ulikuwa hauna biashara.
Hatua za kuongeza mauzo Kama tayari uneanzisha biashara
Hatua za kujenga timu na kuwa na wasaidizi kwenye biashara. Huwezi kuendelea kufanya majukumu yooote kwenye biashara huku ukitegemea kupata matokeo ya makubwa.
Hatua za KUTANGAZA biashara yako na nyingine nyingi.Ni kweli hatua hizi muda mwingine zinaogopesha.
Ni kweli hatua hizi muda mwingine zinatufanya tusijisikie sawa. Ila zinapaswa kuchukuliwa Mara zote. -
Vitu Saba vya KUZINGATIA unapokuwa na miadi na watu
Rafiki yangu wa ukweli, siku ya leo Ningependa nikwambie vitu saba unavyopaswa KUZINGATIA pale unapokuwa na miadi na watu.
Kwenye ulimwengu wa Biashara, miadi Ni jambo ambalo haliepukiki. Utahitaji kukutana na Wateja. Utahitaji kukutana na wasambazaji, utahitaji kukutana na washirika, utahitaji kukutana na wafanyakazi na wengineo wengi…
Sasa yafuatayo ni mambo saba ya kuzingatia
Kwanza. Unapokuwa na miadi na watu hakikisha kwamba unawahi kwenye miadi hiyo. Ikitokea kwamba una changamoto inayokuzuia wewe kufika eneo husika kwa wakati, basi wajulishe wahusika.
Pili, unapokutana na watu usigawe umakini wako. NGUVU zako na Akili Yako yote iwe kwenye hiyo miadi.
Tatu, usitumie simu Wala kifaa kingine wakati unaongea na watu.
Nne, hakikisha unakuwa na kalamu na karatasi na andika yale ambayo wengine wanaongea. Chukua notsi. Hii itaonesha namna ulivyo makini kwenye kufanyia Kazi majukumu yako.
Tano, usiingilie Kati mazungumzo ya mtu. Mwachie MTU nafasi ya kuongea mpaka mwisho Kisha ndiyo wewe uingilie kati.
Sita, sikiliza umakini anavyosema mwingine. Haipendezi kuona kwamba mtu fulani anasema jambo fulani Tena kwa namna ya kueleweka halafu wewe unakazana Kuuliza. Hivi umesemaje hapo?
Saba, vaa vizuri ili kuendana na mkutano husika.
Rafiki yangu, hayo ndiyo mabo saba ya kuzingatia pale unapokuwa na miadi. Nikutakie wakati mwema rafiki yangu wa ukweli
Jinsi Ya Kufanya Na Kukamilisha Majukumu Yako Kwa Wakati
Ni Mimi rafiki yako
Godius Rweyongeza
0755848391 -
Kwa nini vijana wengi hawawekezi kwenye soko la Hisa, hatifungani na vipande
Mwishoni mwa mwaka Jana nilipata kuhudhuria mkutano mkuu wa mwaka wa mfuko wa umoja kwa njia ya mtandao. Mkutano huu ulikuwa unafanyika kwenye ukumbi wa Mwalimu Nyerere UBUNGO lakini pia ulikuwa ulifanyika kwa njia ya mtandao.
Kitu kikubwa kilichokuwa kinaongelewa kwenye huu mkutano ilikuwa ni ripoti ya mwaka 2021/2022 ya mfuko wa umoja.Baada ya ripoti kuwasilishwa Kuna watu walionekana wanaguswa kwa namna mkutano mzima ulivyokuwa umejaa wazee na watu wenye umri wa kustaafu kwa asilimia kubwa.
Hii ilitoa picha kuwa hawa watu ndio wawekezaji wakubwa kwenye mfuko, na hivyo vijana wameachwa nyuma.
Swali kulikuwa kwa Nini vijana hawawawekezi?
Sikumbuki Kama Kuna MTU alijibu hili swali, Ila leo Ningependa kukupa sababu chache tu kuonesha kwa nini vijana hawawekezi?
Kwanza hawana elimu. Ujue elimu ndiyo inaondoa kiza na toongotongo machoni pa mtu na hivyo kumfanya awekeze.
Kama hauna elimu sahihi, Basi jua waziwazi kabisa kuwa huwezi kuwekeza.
Na ndio maana nimeamua kwa dhati kuhakikisha kwamba elimu hii ya uwekezaji naiweka kwenye maandishi kwenye kitabu hiki Cha kipekee cha MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE.

Hakikisha unapata nakala yako siku ya leo kwa 20,000/- tu. Wasiliana nami kwa 0755848391
-
KUWA IMARA

Tunaishi katika dunia ambayo haipendi vitu ambavyo siyo imara. Na hili jambo la KUWA imara halijaanza leo. Limekuwepo kwa siku nyingi sana.
Vitu ambavyo vimekuwa imara kwa miaka mingi ya nyuma, ndivyo ambavyo viliendelea kuishi, huku vile ambavyo siyo imara vikidhoofu na kufa.
Watu wanyonge, mimea minyonge, wanyama wanyonge havina nafasi kubwa ya kuishi Kama vile vitu ambavyo ni imara. Hivyo, na wewe unapaswa KUWA imara.
Najua hiki kitu kinaweza kuonekana cha ajabu sana hasa kwa upande wako ukizingatia kwamba umezoea kuambiwa KUWA wewe Ni MNYONGE. Na hivyo kuna watu wanakutetea wewe na unyonge wako.
Ninachotaka kukwambia ni kuwa, usikubali kuwa MNYONGE. Unyonge ni hali ya chini ambayo MTU yeyote hapaswi kuibeba.
Unapaswa KUBEBA ujasiri, uthubutu, na sifa nyingine za aina hii.Unyonge haukai meza moja na ujasiri. Unyonge hauwezi kukaa meza moja na uthubutu. Unyonge hauwezi kukaa meza moja na utawala.
Ukiwa MNYONGE unanyongwa na haki yako hupewi. Huo ndio ukweli.Kitabu: How to Win Friends and Influence People
Hivyo, nataka ujiondoe kwenye hali ya unyonge kuanzia Leo hii na uanze kuwa jasiri, uwe imara.
Kanuni ya Darwin
Darwin na wanasayansi wengine waliotangulia kabla yake kama akina Lamark na wengine ambao wamefuata baada Yao wamethibitisha kuwa viumbe ambavyo huwa ni vinyonge huwa vinapotea na kutoweka kwenye uso wa dunia, huku vile ambavyo ni imara viking’aa na kufanya makubwa zaidi.Mfano wa kawaida ni kwenye wanyama. Ukiwa na mbuzi au kuku umewafuga. Halafu hao wanyama ukawawawekea chakula. Wanyama ambao ni imara watakuwa mstari wa mbele kula na hata watafukuza wale ambao siyo imara. Wale ambao siyo imara watafukuzwa na kukaa pembeni. Ni mpaka pale wanyama walio imara watakapokuwa wamemaliza kula ndio na wale wanyonge watakula. Kama chakula ni kidogo, Basi wanyama wanyonge wataishia kujiramba tu.
Hiki kitu hata sisi kwetu wanadamu ,hujawahi kuona kwenye sherehe kinaletwa chakula watu wanakigombania? Unajua ni watu wa aina gani ambao huwa wanaishia kula chakula cha aina hiyo? Ni wale ambao huwa wanakuwa imara. Wanyonge wanakaa pembeni.
Na hiki halitokei kwenye chakula tu, Bali hata kwenye tendo. Wanyama ambao siyo imara hawapati nafasi ya kufanya tendo na wanyama wengine. Kitu kinachofanya mbegu zao zisisambae Kutoka kizazi kimoja KWENDA kingine.
Katika ulimwengu wa leo unahitaji kuwa imara.
Achana na dhana ya kujiita MNYONGE kuanzia leo.
Kuna watu wamekuwa wanakuita MNYONGE . Na hata wewe mwenyewe umekuwa unajiita MNYONGE. Rafiki yangu sikiliza, kuanzia leo hii kataa kuitwa MNYONGE. Na wala wewe mwenyewe usijiite MNYONGE.Anza kuishi kama MTU imara. Ongea Kama MTU ambaye yuko imara. Tembea kwa kujiamini kama MTU ambaye yuko imara. Kwa jinsi hiyo, utakuwa umetengeneza ulimwengu wako wa TOFAUTI na watu watakupenda.
Utakuwa kama Moto. Moto ni hatari sana. Ukiugusa tu, unaungua. Lakini watu duniani kote wanaupenda kinachofanya watu wapende Moto ni kwa sababu ya uimara wake. Moto hautetereki kwenye uimara wake. Ukiingia kwenye kumi na nane zake unaungua. Ukitumia vizuri unakusaidia kutengeneza vitu vingine ambavyo ni imara. Mfano, ukiutumia kuunguza tofali unazifanya imara zaidi.
Lakini ukiutumia vibaya unaunguza nyumba. Mbali na madhara yote ambayo Moto unaweza kufanya ila tunaupenda kwa sababu ya uimara wake. Tukiwa na baridi tunawasha Moto na kuusogelea karibu kwa sababu tunajua kwamba moto ni imara na hauyumbishwi na baridi. Hivyo tunausogelea ili tupate joto.
Tukihitaji nyama choma, tunaenda kutafuta moto kwa mara nyingine. Tunajua moto ni imara na utatusaidia kugeuza nyama ya kawaida kuwa choma.
Tukihitaji chakula, tunaufuata Tena Moto. Tunamenya ndizi zetu na kuziweka kwenye moto, noto unaturudishia ndizi zikiwa zimeiva.
Huo ndio uimara wa Moto.
Na wewe unahitaji kuwa imara pia
-
Maisha Yako Ni wajibu wako
Maisha Yako Ni wajibu wako, usisubiri MTU aje akusaidie wewe kufanya vitu ambavyo wewe mwenyewe unapaswa kufanya.
Ebu chukulia vitu vya kawaida tu Kama KUTUNZA muda
Kuweka akiba
Kuamka mapema
Kufanya Kazi kwa bidii
Kusoma vitabu na kufanyia kazi Yale unayojifunza.Je, hivi unahitaji mtu akusaidie kuvifanya? Na hivi unalalamika kwamba serikali haijavifanya kwa niaba yako? Hivi kweli uko siriazi na maisha yako?
Chukua hatamu ya maisha yako kuanzia leo hii, maana maisha ni wajibu wako. Ukishinda ni juu yako. Ukishindwa ni juu yako pia.
Kazi ya kufanya siku ya leo.
Angalia vitu ambayo umekuwa unalalamikia Sana.
Jiulize je, vipo ndani ya uwezo wangu?Kama. Vipo ndani ya uwezo wako, vifanye. Kama vipo nje ya uwezo wako, achana navyo.
Kila la kheri.