Home


  • Njia Saba (07) Bora Za Kutangaza Ujuzi Wako Kwa Watu

    Rafiki yangu siku ya leo ningependa kikufundishe njia Saba Bora za KUTANGAZA UJUZI WAKO KWA watu, kiasi Cha kuweza kuwashawishi watu waweze kutoa hela zao mfukoni na kukulipa.

    Naomba ifahamike hapa kuwa ninapoongelea Aina za ujuzi namaanisha, kile kitu ambacho tayari unacho na unaweza kukipangilia vizuri kikaanza kuleta mafanikio.
    Kuna watu wanaposikia ujuzi Basi wanadhani kinapaswa kuwa ni kitu cha kipekee sana kitu ambacho hakijawahi kufanyika au kuonekana ssehemu yoyote.


    Ujuzi unaweza kuwa elimu au taaluma yako.


    Ujuzi unaweza kuwa kitu ambacho umefanya kwa muda mrefu na Sasa umebobea.

    Kwenye hicho kitu kiasi kwamba unaweza kuwafundisha wengine wakanufaika nacho.


    Ujuzi unaweza kuwa wa kujifunza pia mtandaoni

    SOMA ZAIDI: AINA TATU ZA UJUZI UNAOHITAJI ILI KUONGEZA THAMANI YAKO NA KULA MEMA YA NCHI

    Kwenye makala ya leo ningependa nikuoneshe njia Saba za kutangaza ujuzi wako

    Kwanza unaweza kutangaza ujuzi wako mtandaoni


    Pili unaweza kuwatumia watu wanaokujua kutangaza ujuzi wako


    Tatu ni kuandaa na kuonesha kazi zako


    Nne Ni kuomba rufaa


    Tano nii kuwa na data za wateja walionunua na wale wanaonesha nia ya kufanya.


    Sita ni kuwatembelea watu walipo na saba

    na saba ni kupitia kufanya kazi ambayo ni bora kabisa kiasi kwamba hakuna mtu yeyote anayeweza kukupuuza.

    Rafiki yangu hizo ndiyo njia saba za kutangaza ujuzi wako kwa watu, na habari njema ni kwamba, unaweza kuchagua njia moja ambayo unaweza kuanza kutumia sasa hivi.

    kisha ukaanza kuitumia.

    Kama kuna njia kati ya hizo utaitumia halafu ikaleta matokeo, usiache kuitumia hiyo njia. Endelea kuitumia zaidi na zaidi hku ukiboresha ili uweze kuwafikia watu kwa wingi zaidi.

    SOMA ZAIDI: 

    Kwa leo naomba niishie hapo rafiki yangu.

    Najua kuwa ungependa kupata ushauri wa karibu zaidi moja moja kwa moja kutoka kwangu. Nitafute tuone ni lini nitakuwa na muda, ili nikupangie ratiba ya kuongea na wewe. Utalipia kiasi kidogo tu.

    Saa moja ni laki moja mazungumzo kwa njia ya mtandao.

    Kwa mazungumzo ya ana kwa ana utalipia LAKI MBILI NA NUSU kwa saa

    Malipo yanafanyika kwanza, kisha unapewa tarehe (appointment) tutakapoweza kuongea

    Tumia namba ya simu +255 755 848 391 kuwasiliana nami.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza ambaye anaishi Morogoro nchini Tanzania.

    Unaweza kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza kupitia youtube channel yake hapa

    Kwa ushauri niandikie songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu ambavyo ameandika Godius Rweyongeza, wasiliana naye kwa +255 684 408 755 na orodha ya vitabu vyenyewe unaweza kuiona HAPA. Chagua unachopenda, kisha twanga,  +255 684 408 755

    Kujiunga na programu yetu ya uandishi. Wasiliana na +255 678 848 396

    For Consultation only: +255 755 848 391  au godiusrweyongeza1@gmail.com

  • Nguvu ya fedha; Itumie Ikubebe

    Hivi umewahi kujiuliza fedha kama fedha ina nguvu gani maishani mwangu, kwenye maisha ya familia yangu au hata maisha ya watu wengine wa karibu sana kwenye andiko la leo ambapo unaenda kujifunza nguvu hizi muhimu za fedha na jinsi ambavyo unaweza kutumia nguvu hizi hapa kwa manufaa yako.

    1. Nguvu ya kufanya maamuzi. Kwenye hili andiko ninaenda kuandika mengi kuhusiana na nguvu ya pesa. ila kitu kimoja ambacho pesa itakupa kama utakuwa nacho ni nguvu ya kufanya maamuzi, yaani, ukiwa na pesa yako, utakuwa na uwezo wa kuamua chochote kile unachotaka. Unaweza kuamua utembelee eneo gani na eneo gani usitembelee. Hata kwenye vikao vya familia, ukiwa na pesa, nguvu ya wewe kufanya maamuzi inakuwa kubwa ukilinganisha na yule ambaye anakuwa hana pesa. SIyo tu kwenye familia, hata kwenye ngazi za maamuzi ya kitaifa, mpaka kimataifa. Leo hii Marekani linafahamika kama taifa lenye nguvu, kwa sababu wanatumia nguvu ya pesa kufanya maamuzi ambayo kama huna pesa hawezi kuyafanya.

    Chukulia mfano, wa kawaida tu. kuna nchi za Afrika zinawekewa vikwazo kwa sababu ya kuwa na uhusiano na nchi ya urusi au washirika wake, ila wakati huohuo, nchi ya Marekani ambayo inaziwekea nchi za afrika hivyo vikwazo, yenyewe ina uhusiano wa karibu sana na washirika wa Urusi, na haiwekewi vikwazo.

    Aah, halafu umewahi kusikia wapi maishani kwako kwamba nchi maskini imeiwekea nchi tajiri vikwazo. Hiyo ndiyo nguvu ya pesa aiseee. Yaani, ukiwa na pesa, ni kama vikwazo vinakuwa hamna. Ndio maana unapaswa kuwa nayo, pesa ni sabuni. Hahaha, sabuni ya roho. Kuwa nayo aisee!

    2. nguvu ya kununua. Ukiwa na fedha unakuwa na nguvu ya manunuzi. Kwa pesa yako unaweza kuamua kununua jambo fulani au la unaweza kuacha. Unaweza kuamua kununua sasa hivi, au la unaweza kuamua kununua baadaye.

    Unaweza kuamua kuringa kidogo kabla ya kutoa hela. Hata hivyo, hela si ya kwako tu. Hii ni nguvu ya fedha. Ndio maana wewe unahitaji kuhakikisha kwamba unakuwa na pesa.

    Hata ukiomba mtu akupunguzie bei, siyo kwamba unakuwa upungiziwe bei kwa sababu ya mtu akuonee huruma, bali kwa sababu una pesa.

    3. nguvu ya kuwekeza. Fedha unaweza kuitumia kuwekeza kwenye eneo lolote. Kuwekeza ni kuifanya fedha ikutumikie, yaani, unaifanya pesa ikuingizie pesa zaidi hata pale unapokuwa umelala. Hicho ni kitu ambacho unahitaji ukifanyie kazi rafiki yangu.

    Kama hujaanza kuwekeza, mwaka huu kuwekeza kunapaswa kuwa kwenye vipaumbele vyako.

    Na kwa kuanzia hakikisha kwamba unasoma kitabu changu cha MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE

    Hakikisha una pesa, na hakikisha kwamba unaitumia pesa yako kuwekeza.

    4. nguvu ya kutoa na kusaidia jamii. Rafiki yangu, huwezi kusaidia watu kama hauna pesa. Huwezi kusaidia watu kama wewe mwenyewe unahitaji msaada. hahah, unahitaji uwe na pesa ili uweze kusaidia watu. Ni rahisi tu hivyo. Fedha ndiyo inakupa nguvu ya kusaidia watu. Kama unayo unaweza kuwasaidia watu, kama hauna, daah, ni ngumu kuasaidi watu.

    5. nguvu ya nguvu ya kununua muda kwa ajili yako. Pesa inaweza kukusaidia wewe kununua muda. Unajiuliza pesa inanunuaje muda, ningependa kukwambia kwamba pesa inanunua muda pale ambapo unakuwa umeajiri watu wengine wakusaidie kufanya baadhi ya majukumu, na hivyo kukupa mwanya wewe wa kuendelea na majukumu mengine. Upo hapo rafiki yangu.

    6. Nguvu ya kutibiwa. Kuna watu wengi huwa wanakufa kwa sababu tu ya kukosa huduma bora za kimatibabu, na wanakosa huduma bora kwa sababu hawana nguvu ya pesa. Ukiwa na nguvu ya pesa, kwanza ukijisikia vibaya tu utawahi hospitali, unakuwa hauna cha kuanza kusikilizia sijui kuona kama muujiza utatendeka ukapona. Ila kama hauna nguvu ya pesa, utaanza ooh, eti unasikilizia kuona kama utapona. Oooh, sijui imeenda endaje. Tafuta fedha ikuzoee aisee.

    7. nguvu ya kujenga mahusiano. Tafiti nyingi zimefanyika, na imegundulika kwamba moja ya kitu ambacho huwa kinafanya watu waachane kwenye mahusiano, ni kwa sababu ya pesa. hivyo, unahitaji uwe na pesa ili uweze kufanya makubwa zaidi. na siyo tu uwe na pesa, bali uwe na elimu sahihi kuhusiana na pesa.

    8. Nguvu ya kuchagua aina ya maisha unayotaka. Pesa inakupa nafasi yaw ewe kuchagua aina ya maisha ambayo wewe mwenyewe unataka, usupokuwa na fedha unaweza kuwa mtumwa kwa kulazimika muda mwingine kufanya kazi ambazo hata wewe mwenyewe hupendi.

    11. nguvu ya kubadili mwonekano wako

    Kuna siku moja kwenye mtandao watu waliweka picha ya msanii Zuhura, maarufu kama Zuchu, akiwa bado na maisha ya kawaida. Aliyeweka ile picha akawa amesema kwamba huyu ndiye Zuchu kabla hajatoka kimaisha.

    Lakini sasa hivi nguvu ya pesa imembadilisha.

    Pesa rafiki yangu ina uwezo wa kubadili mwonekano wako. Ukiwa nayo, mwonekano wako tu, unaongea.

    12. nguvu ya kukufanya ujiamini. Pesa ina uwezo wa kukufanya ujiamini.Yaani, inakufanya ujiamini kuliko yule ambaye hana. Yaani, ukitoka nyumbani ukiwa unajua kwamba hakuna chakula, unadaiwa kodi, na makorokoro mengine kibao, hata kujiamini kwako kunapungua tu. Ila kama unajua una mzigo wa kutosha nyuma ya pazia, hapo unakuwa kwenye nafasi nzuri ya kujiamini kuliko mtu mwingine yeyote. Hiyo ndiyo nguvu ya pesa.

    Rafiki yangum, fedha unapaswa kuwa nayo. Unapaswa kuwa nayo, maana kuwa nayo tu, kutavutia vitu vingi kwenye maisha yako. Hivyo itafute. Lakini usiishie tu kutafuta fedha, bali pia kuwa na maarifa sahihi ya kifedha. Haya yatakusaidia wewe kufanya makubwa zaidi wkenye maisha yako. Kila la kheri

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.

    Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.

    Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.

  • Kitu kimoja ambacho hupaswi kuacha kufanya hata kama una nguvu ya pesa

    umeshapata nakakla zako? Wasiliana na 0755848391 sasa kupata nakala zako. kila nakala bei yake ni 20,000/-
    umeshapata nakakla zako? Wasiliana na 0755848391 sasa kupata nakala zako. kila nakala bei yake ni 20,000/-

    Rafiki yangu mpendwa, ila shaka unaendela vizuri. Kwa upande mwingine mimi nipo vizuri kabisa. leo nataka tujadiliane kwa pamoja kuhusiana na kitu kimoja ambacho hupaswi kuacha kufanya hata kama una nguvu ya pesa. na kitu hiki ni kujadiliana muuzaji kuhusiana na bei anayokuuzia bidhaa.

    Yaani, kiufupi ni kwamba mtu akitaka kukuuzia kitu kwa bei fulani, mara zote jadiliana naye ili uone namna ambavyo anawez akukupunguzia kiasi fulani kwenye hicho kiasi ambacho amekwambia.

    Hiki kitu unapaswa kukifanya bila kujali una fedha nyingi kiasi gani.

    Mara nyingi mfano mtu akikwambia kwamba anauza bidhaa au kitu fulani kwa 20,000/-. Wewe anza kujadiliana naye kwa kumwambia kwamba una kiasi pungufu, pengine nusu yake tu. komaa hapohapo, na ikiwezekana ongeza kiasi kidogo tu.

    Mwisho wa siku utajikuta kwamba unaweza kupata hiyo bidhaa kwa bei nzuri sana.

    SIyo kwamba ukifanya hivi ni kiashiria cha umasikini, bali  hiki kitu kinafahamika kama negoatiaon. Na negotiation ni mojawapo ya ujuzi muhimu sana ambao unauhitaji, na unakufaa sana, na utakusogeza mbali sana kimaisha.

    Rafiki yangu, huu ujuzi hakikisha kwamba unakuwa nao kwa vyovyote vile. Na utumie popote pale unapokuwa bila ya kurudi nyuma.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.

    Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.

    Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.

  • Fanya kazi kwanza, tutaongea

    /

    Mr. Beast ni moja ya watu maarufu sana kwenye mtandao wa youtube. Yeye alianzia chini kabisa kwenye ulimwengu wa youtube, hakuwa na umaarufu wowote kama huu alionao sasa hivi. alianza kurekodi video moja baada ya nyingine,. Nyingi hazikufanya vizuri, lakini jamaa hakukata tamaa aliendelea, baada ya miaka mingi ya kuweka kazi bila ya kukata tamaa, ndipo video zake zilikuja kutambulika na baada ya hapo umaarufu wake umekuwa unaongezeka kila siku na kila kukicha.

    Sasa kuna siku aliulizwa, hivi una ushauri gani kuhusu watu ambao ndio kwanza wanaanza kuingia kwenye ulimwengu wa youtube. Alisema kwamba hawa wanapaswa kuendelea kuweka kazi. Yaani, wasitegemee kwamba wanaenda kupata matokeo makubwa kwa haraka na ndani ya siku moja. Hakuna kitu kama hicho. matokeo makubwa yatakuja kweli, ila yanahitaji kwanza muda. Lakini pia yanahitaji mtu uweke kazi.

    Siyo mtu unarekodoi video moja na kuweka youtube huku ukitegemea kupata m atokeo na mafanikio makubwa ndani ya hiyo siku. Hakana kitu kama hicho, badala yake unapaswa kuwa na mwendelezo kwenye kile ambacho wewe mwenyewe unafanya, yaani, unapaswa kufanya kitu ulichochagua kila siku bila kuacha na kwa mwendelezo.

    Kadiri ya Mr. Beast anasema kwa mtu ambaye anataka kutoboa kwenye ulimwengu wa youtube anapaswa kuwa walau amerekodi video za kuanzia mia moja. hapo sasa ndipo tunaweza kuanza kuongea kuhusu kupata wafuasi. Hapo siyo kwamba huyo mtu katoboa, ila ndio mnaweza kuanza kuongea.

    Hee, Na anasema kwamba kwenye kila video ambayo utarekodi unapaswa kuendelea kuiboresha na kuifanya kuwa bora zaidi ya ile ya kwanza. Yaani, siyo unarekodi video nyingi lakini zinakuwa hazina ubora wowote. Hapana, badala yake ni kwamba hizi video unapaswa kuwa unaziongezea ubora kila unaporekodi.

    Najua asilimia kubwa ya wasomaji wangu siyo watu wanaotengeneza maudhui ya youtube. Na wala siyo kwamba kwa makala hii basi nawataka waanze kurekodi maudhui kwa ajili ya kuweka youtube.

    Bali nataka kila anayesoma ujumbe huu aondoke na kitu kimoja kikubwa. Na kitu hiki ni kwamba, kama  unaanzia chini, unapaswa kuweka kazi kwenye kitu ambacho unafanya. siyo unafanya kitu hicho mara moja au mara mbili halafu huoni matokeo unaacha. ACHA utani aisee, endelea kuweka kazi mpaka kieleweke.

    Na siyo unafanya kazi kwa maozea,bali kila mara unaboresha na kufanya kazi ambayo ni bora zaidi kuliko mwanzo.

    Toa mazoea, fanya kazi tena kwa bidii sana. Tutaongea baadaye

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.

    Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.

    Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.

  • Kuwa bora

    umeshapata nakakla zako? Wasiliana na 0755848391 sasa kupata nakala zako. kila nakala bei yake ni 20,000/-
    umeshapata nakakla zako? Wasiliana na 0755848391 sasa kupata nakala zako. kila nakala bei yake ni 20,000/-

    Moja ya dhana ambayo watu wengi tumekuwa hatujifunzi ni kuwa vitu ambavyo ni bora ndivyo ambavyo huwa vinapendwa. Hakuna mtu huwa anapenda kukaa karibu na vitu dhaifu, vitu ambavyo siyo vizuri na vitu ambavyo  havivutii.

    Ili uweze kunielewa vizuri kwenye hili, nitatolea mfano ambao unaweza kukuudhi kidogo. Hivi eti kwa mfano, unaweza kuchukua chakula chako kizuuuri ambacho umekipika na kikapikika na kwenda kula kwenye dampo? Ji bu lipo wazi kabisa, huwezi kufanya hivyo, kwa nini kwa sababu dampo siyo sehemu bora ambapo unaweza kula chakula chako hicho kitamu ambacho umedhamiria kula.

    Hivyo hivyo, kwenye maisha ya kawaida, hakuna mtu ambaye anapenda kujihusisha na vitu vibaya. Na hata mzazi anapokuwa analea watoto wake atawaepusha na watoto wengine ambao wana tabia mbaya.

    Lengo la mimi kukuandikia haya yote ni kukujulisha kuwa unapaswa kuwa bora kwenye kile unachofanya. Yaani, kwamba unapaswa kujiwekea viwango vya daraja la kwanza. Viwango vikubwa ambavyo utakuwa unavifanyia kazi na kuvifikia

    Ubora wa wewe kujiwekea hivi viwango ni kwamba utavutia kwako watu wengine wa viwango vikubwa pia. Chuma kinanoa chuma. Na vitu vya aina moja mara nyingi huwa vina tabia ya kukaa pamoja.

    Hivyo kama viwango vyako ni dhaifu, utajikuta kwamba unapata marafiki na watu ambao pia wana viwango dhaifu. Hiki kitu kitapelekea wewe kuishi maisha ambayo ni dhaifu pia . Sasa mwaka 2023 azimio lako linapaswa kuwa ni moja tu. unapaswa kuazimia kwamba mwaka 2023, ni mwaka wangu wa kufanya kazi zangu kwa viwango vya juu.

    Hiki kitu kitakufanya uvutie kwako watu wngine wenye viwango vya juu pia.

    Kama unaajiri, hakikisha kwamba unaajiri watu wa viwango vya juu.

    Marafiki wako wawe marafii ambao wana viwango vya juu pia.

    Rafiki yangu, huu ni mwaka wako ila tu siyo kwamba uishie kusema kwamba huu ni mwaka wangu kwa maneno, bali matendo yako yanapaswa kudhihirisha hilo.

    Ukiwa bora watu hawawezi kukupuuza.

    Asante sana

    Kupata makala zaidi kutoka kwangu, hakikisha kwamba umejaza taarifa zako hapa

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.

    Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.

    Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.

  • Iambie dunia kile unachotaka kufanya, ila  kwanza kioneshe hicho kitu

    Rafiki yangu, habari ya siku ya leo. Hongera sana kwa siku hii ya leo nay a kipekee sana. mimi kwa upande wangu rafiki yangu siku ya leo, nina kitu kimoja tu ambacho ningependa kukwambia. Na kitu hiki siyo kingine bali ni kwamba kama kuna kitu ambacho ungependa kuiambia dunia, basi hicho kitu unapaswa kukisema kwa dunia, ila kwanza unapaswa kuonesha kwa vitendo kwamba unaweza kukifanya hicho kitu.

    Ujue hii dunia haipungukiwi na wasemaji hata kidogo, bali inapungukiwa na watendaji. Unachotakiwa kufanya ni kwamba wewe unapaswa kuwa mtendaji sana na wala siyo muongeaji sana.

    Mara zote kuwa mtendaji, na onesha kile ambacho unataka kusema kwa dunia kwa vitendo na wala siyo kwa maneno.

    Mara nyingi nimekuwa nikiwaambia watu waseme malengo na ndoto zao waziwazi, kisha wazifanyie kazi. Ila sasa nimegundua haya masula ya kusema malengo na ndoto zako kwa watu hivihivho tu ni upotezaji wa muda. Na mwaka huu nataka ufanye kitu kimoja tu. Malengo na ndoto zako, usiziseme kwa mtu yeyote, kabisa. wewe fanyia kazi tu malengo na ndoto zako bila kusema chochote na kwa yeyote. nina hakika rafiki yangu, kwamba mpaka kufikia mwishoni mwa mwaka. matendo yako yataongea zaidi kuliko ambavyo ungeongea kwa maneno.

    Ni hayo tu ambayo nilitaka kukwambia siku ya leo. Kabla sijaachana na wewe kabisa kuna kitu kimoja ambacho ningependa ufahamu. Na kitu hiki kwamba mwaka huu 2022, mwezi Juni tutakuwa na semina mkoani MOROGORO.

    Semina hii itafanyika juni tarehe 24, hapahapa mkoani Morogoro.

    Kwenye semina hii, unaenda kupata mafunzo ya kipekee yatayokusaidia wewe kupiga hatua na kusonga mbele kwa juhudi kubwa sana.

    Semina hii ya ana kwa ana, itafanyika kwenye mojawapo ya hoteli hapa Morogoro mjini, na itakuwa semina ya siku moja tu.

    Gharama ya semina hii itakuwa 50,000 tu. Malipo yote yatafanyika kwa namba 0687848391 jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Karibu sana.

  • Jinsi ya kuitumia nguvu ya mara kumi zaidi kufanikisha makubwa

    Rafiki yangu, sina shaka unaendelea vizuri kabisa. hongera sana kwa siku hii ya kipekee sana. siku ya leo ningependa kuongea na wewe juu ya suala moja tu. Na suala hili ni namna ambavyo unaweza kuitumia nguvu ya mara kumi zaidi kufanikisha malengo yako, na kitu chochote kile ambacho umepanga. Kiufupi kwenye hii makala nataka nikuoneshe ni kwa namna gani ambavyo unaweza kuitumia nguvu ya mara kumi zaidi kuhakikisha kwamba unafanikisha makubwa sana.

    Utakuwa unajiuliza hii nguvu ya mara kumi ndiyo nguvu gani na inafanyaje kazi?

    Na mimi ningependa kuanzia hapo. Nguvu ya mara kumi kumi zaidi iko hivi, kwa chochote kile ambacho unapanga kupanga, unapaswa kukizidisha mara kumi zaidi. Kwa kuanzia tuanze na malengo yako. Kama una lengo lako lolote ambalo umeweka sasa hivi, zidisha mara kumi zaidi ya lengo ambalo umeweka sasa hivi.

    Kwa mfano kama umeweka lengo la kuingiza kipato cha milioni moja kwa mwezi. Unapaswa kulizidisha hilo lengo lako mara kumi zaidi. yaani, badala ya kuwa na lengo la kuingiza milioni moja kwa mwezi, kuwa na lengo la kuingiza milioni kumi kwa mwezi.

    Kama una lengo la kuingiza milioni kumi, zidisha mara kumi zaidi. Liwe ni milioni 100. Yaani, kitu chochote kile utakachofanya kwenye maisha yako, hakikisha kwamba unakifanya kwa viwango vya mara kumi zaidi ya kawaida.

    Mahusiano yako, yawekee lengo la kuyaboresha mara kumi zaidi.

    Biashara yako, iwekee lengo la kuikuza mara kumi zaidi.

    Wteja wako, weka lengo la kuwaongeza mara kumi zaidi.

    Mtaji wako, weka lengo la kuukuza mara kumi zaidi

    Oooh, kama nakuona vile unavyostuka na kuanza kuona kama vile lengo linakuwa ni kubwa sana. na ndio maana, kuna hii nguvu ya mara kumi zaidi.

    Maana, uwezo wa hii nguvu siyo tu kwamba upange peke yake. Bali upange na kutekeleza kile ulichopanga. Kwa hiyo, maana yake mipango yako inapaswa kuwa ni mipango ya mara kumi zaidi, lakini sambamba na kuwa na mipango ya mara kumi zaidi, unapaswa kuwa na vitendo ambavyo ni mara kumi zaidi.

    Yaani, baada ya kuwa umezidisha lengo lako na kulifanya kuwa lengo kubwa sana. sasa kinachofuata ni wewe kuzidisha kila kitu ambacho utafanya. Unapaswa kuzidisha hatua ambazo unachukua mara kumi zaidi.

    Kwa lengo lako la kuingiza milioni moja, pengine ulikuwa umejiwekea kwamba ukiuza bidhaa kwa wateja 10 tu, utakuwa umeweza kulifikia. Ila kwa lengo lako jipya ambalo umeweka. Yaani, hili lengo la mara kumi zaidi. maana yake utahitaji  kuhudumia wateja mara kumi zaidi ya wale ambao ulikuwa umepanga kuwahudumia.

    Na ili uweze kuhudumia wateja mara kumi zaidi ya wale ambao unawahudumia, maana yake unapaswa kuchukua hatua za kutafuta wateja mara kumi zaidi. Kwa sababu ili uweze kuwa na wateja 100 wanaonunua kwa wiki au kwa mwezi. Lazima uwe na wateja zaidi ya hao. Maana yake kutakuwepo na wengine ambao hawatanunua, sasa baada ya kutoa 100 wanaonunua, ndipo na wewe unakuja kubaki na wale wachache ambao wananunua.

    Kwa hiyo basi rafiki yangu, naomba kitu kimoja tu. kuanzia sasa hivi, anza kufikiri mara kumi zaidi ya sasa.

    Kama ni pesa, fikiri mara kumi zaidi ya unavyofikiri sasa hivi. chukua hatua mara kumi zaidi ya unavyochukua sasa hivi.

    Kutana na watu mara kumi zaidi ya unaokutana nao sasa hivi. piga simu kwa wateja mara kumi zaidi ya unavyopiga sasa hivi.

    Fanya mazoezi mara kumi zaidi ya unavyofanya sasa hivi. Hii ndiyo tiketi ambayo inawatofautisha watu ambao wanafanya makubwa na wale ambao wanafanya vitu kwa namna ya ukawaida sana. Kama wewe hutaki kuwa mtu wa kawaida, basi unahitaji kuhakikisha kwamba unachukua hatua za tofauti ili uweze kufika kule unapotaka.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.

    Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.

    Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.

  • Hivi unajua Nini kuhusu uwekezaji wa hisa, hatifungani na VIPANDE?

    Katika kuongea kwangu na rafiki zangu. Nimekuja kugundua kitu Kimoja kutoka kwa Watu kadha wa kadha ambao nimeongea nao.

    Hawana ufahamu kamili kuhusu uwekezaji wa hisa au hawajui kabisa.

    Hiki kitu Godius, Kimenikusuma niandae kitabu kinachohusu uwekezaji wa hisa, hatifungani na vipande kwa ajili yako.

    Ni kitabu ambacho hupaswi kukikosa rafiki yangu. Ndani yake unaenda kujifunza vitu vigumu kwa lugha rahisi.
    1. Utapata kujua hisa ni Nini?
    2. Kwa nini unahitaji KUWEKEZA KWENYE HISA
    3. Vigezo vya KUZINGATIA KABLA YA HUJAWEKEZA FEDHA YAKO
    4. SOKO LA HISA TANZANIA NA JINSI LINAVYOFANYA KAZI.
    5. NAMNA YA KUSOMA RIPOTI ZA DSE
    6. MFUKO WA PAMOJA WA UWEKEZAJI
    7. MIFUKO YOTE YA UTT IKIWA IMEELEZWA KWA KINA NA KWA LUGHA RAHISI
    8. NJIA RAHISI YA KUTUMIA KIKOKOTOZI CHA UTT AMIS
    9. HATIFUNGANI NI NINI?

    Na Mambo mengine mengi….

    Kitabu kitajibu maswali yako na dukuduku zako zote kuhusu uwekezaji kwenye HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE.

    Sasa umefika wakati wa wewe kuchukua hatua ili kuhakikisha kwamba unapata kitabu hiki cha kipekee. Huu ni uamuzi bora ambao utafanya ndani ya huu mwaka na utakuwa na manufaa makubwa kwako. Sasa chukua hatua upate kitabu hiki kwa 20,000/- tu.

    Utatumiwa kitabu hiki popote pale utakapokuwa. Kama utakuwa mbali kidogo, utaongeza gharama za kusafirisha kitabu ambazo ni 5,000/-

    Kwa hiyo jumla utalipia 25,000/-

    Chukua uamuzi Sasa hivi. Lipia kwa 0755848391 jina ni GODIUS RWEYONGEZA.

    Kumbuka kuwa endapo hutalipia Leo hii. Mwaka mmoja au miaka mitano ijayo, bado utakuwa unaendelea kushangaa shangaa tu, ukiwa hujui chochote kuhusu hisa. Sasa kwa nini usichukue uamuzi ili upate hiki kitabu?

    Haya lipia Sasa Sasa kwa 0755848381 jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Karibu sana.

  • Zifuatazo ni mada 15 utakazojifunza kwenye semina ya Kufungua mwaka 2023!

    Wahenga wanasema hayawi hayawi, Sasa yamekuwa. Rafiki yangu wa ukweli, kwa siku sasa nimekuwa nikikwambia juu ya habari Semina ya Kufungua mwaka 2023. Najua umekuwa unajiuliza hivi hii semina itafanyika kweli? Jibu langu Ni kwamba lazima semina ifanyike bila kukwama. Maana mwaka 2023 haturembi mwandiko

    Semina hii itaanza tarehe 15.1.2023 na itadumu mpaka mwezi wa Pili mwanzoni. Gharama ya hii semina Ni 15,000/-. Gharama ya Semina inalipwa kwa namba 0755848391 jina ni GODIUS RWEYONGEZA.

    Lengo la hii semina Ni kwamba ujifunze njia za uhakika zitakazokuwezesha wewe ulipwe walau mara mbili zaidi mwaka 2023! Na zifuatazo ni mada utakazojifunza

    Tarehe 14 Utangulizi wa Semina Mambo Muhimu ya Kuzingatia.
    Mada: Nini maana ya THAMANI BINAFSI NA JINSI YA KUJUA THAMANI YAKO!

    Tarehe 15: JINSI YA KUWEKA MALENGO, KUYAFANYIA KAZI NA KUYATIMIZA 2023: JINSI MALENGO YANAVYOWEZA KUONGEZA THAMANI YAKO

    Tarehe 16: JINSI UNAVYOWEZA KUWA NA KITU AMBACHO HAKUNA MTU ANAWEZA KUKIFANYA. NA KWA NINI NI MUHIMU KWENYE ULIMWENGU WA LEO WA KOMPYUTA, INTANETI NA ROBOTI

    Tarehe 17: AINA TATU ZA UJUZI UNAOUHITAJI ILI KUONGEZA THAMANI YAKO 2023 ILI KULA MEMA YA NCHI!

    Tarehe 18: KWA NINI UNAHITAJI KUACHA MAZOEA NA KUFANYA KAZI ZAIDI YA UNAVYOLIPWA. NA MATOKEO GANI UNAPASWA KUTEGEMEA

    Tarehe 19: NGUVU YA KUFANYA MAZOEZI + NGUVU YA SAA ELFU KUMI

    Tarehe 20: JINSI UBUNIFU UNAVYOWEZA KUKUONGEZEA THAMANI YAKO BINAFSI NA KUKUINUA KWENYE BIASHARA.

    Tarehe 21: JINSI YA KUTENGENEZA MSHAHARA WAKO MWENYEWE (Njia 10 zilizothubitishwa)

    Tarehe 22: MWAKA 2023 USISHINDANE KWA BEI LABDA KAMA WEWE NI ROCKEFELLER! MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA ILI KUJITOFAUTISHA

    Tarehe 23: UNAHITAJI KUWAHUDUMIA WATU WENGI ZAIDI: JINSI YA KUFANYA HIVYO 2023……

    Tarehe 24: JINSI YA KUSIMAMIA UKICHOPANGA NA UNACHOSEMA 2023

    Tarehe 25: VITU VITAKAVYOKUFANYA UHESHIMIKE 2023

    Tarehe 26: HUHITAJI KUWA NA PLAN B 2023 (SABABU 15 ZILIZOTHUBITISHWA)

    Tarehe 27: KUWA ORIGINAL 2023

    Tarehe 28: MUDA, MALI YENYE THAMANI: JINSI KUTUNZA MUDA WAKO 2023

    Tarehe 29: UNAHITAJI KUWA NA VYANZO VINGI VYA KIPATO

    Tarehe 30: JINSI YA KUONGEZA KUJIAMINI KWAKO na MATOKEO YAKE KWENYE KUONGEZA THAMANI YAKO BINAFSI

    Huo ndio mkeka wetu wa mwaka 2023! Haturembi mwandiko! Njoo ujifunze JINSI YA KUONGEZA THAMANI YAKO mwaka 2023! Nakuhakikishia utakayojifunza ukiyafanyia kazi, yataongeza kipato chako mwaka 2023 walau mara mbili. Na hiki Ni kiwango Cha chini. Watu watakaohudhuria hii semina Nina hakika wataupiga mwingi Sana.

    Lakini siishii hapo. Baada ya semina, nitakupa audio, yenye mafunzo yoote ili uweze kuisikiliza kwa mwaka mzima utakaofuata.

    Mwaka 2023! Haturembi mwandiko!
    Kama na wewe hutaki kuremba mwandiko, basi njoo ujiunge na hii semina. Lipia 15,000/- yako Sasa kwa namba ya simu 0755748391 jina ni GODIUS RWEYONGEZA.

    Karibu sana

    Mwaka 2023! Haturembi mwandiko!

  • Sababu yako ni ipi

    Kila kitu huwa kinafanyika kwa sababu…

    Kuna mtu unayeweza kuwa unawona anafanya jambo fulani, ukafikri labda yeye ana kipaji na uwezo mkubwa kukliko wewe, ila baadaye ukija kufuatilia ukagundua kwamba suala kubwa siyo kwamba ana uwezo  mkubwa kulliko wewe. Siyo kwamba ana konekisheni nyingi kuliko wewe, siyo kwamba amebarikiwa kuliko wewe, labda tu ni kwamba ana SABABU KUBWA KULIKO WEWE. Yaani, ile kwa nini yake ni kuwa

    Sababu ndizo huwa zinatusukuma sisi kufanya jambo fulani au kutofahanya jambo fulani. Sababu ndizo huwa zinatusukuma sisi kujituma kwenye kufanyia kazi jambo fulani au kutofanya na kuacha jambo fulani.

    Ukiwa na sababu kubwa ndiyo inakusukuma wewe kuamka asubuhi na mapema kwa ajili ya kwenda kufanyia kazi malengo na ndoto zako, huku wengine wakiwa wamelala. Sababu haihitaji visingizio. Sababu haihitaji urudi nyuma, sababu haihitaji urembe mwandiko.

    Sababu inahitaji kitu kimoja tu uzalishe matokeo.

    Wewe sababu kubwa inayokusuma wewe kufanyia kazi malengo yako ni ipi. Au visingizio ndivyo vimekutawala?

X