Home


  • Namba Zetu Za Malipo

    Namba za malipo ya vitabu:

    Namba za lipa

    TIGO PESA: 19016638 Jina ni SONGAMBELE CONSULTANTS

    M-PESA: 5564517 jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

    Namba za kawaida

    AIRTEL MONEY: 0684408755
    TIGO PESA: 0655 848 392
    M-PESA: 0745 848 395

    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    NB: Kama namba ya malipo anatumiwa mtu ambaye yuko nje ya nchi. Iandikwe Kwa kuanza na +255

    Kwa hiyo namba zinazotumwa nje ya nchi zitakuwa
    Airtel money: +255 684 408 755
    TIGO PESA: +255 655 848 392
    M-PESA: +255 745 848 395

    KOTE Jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Kama malipo yatakuwa yanafanyika kupitia benki.

    Yafanyie kupitia

    1. CRDB BANK: 0150770710200
    2. NMB BANK: 22110047274

    Kote jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

  • Wasiliana na Godius Rweyongeza Sasa

    Habari yafuatayo ni mawasiliano Unayoweza kutumia kumpata GODIUS RWEYONGEZA

    Simu: +255 (0) 684408755

    Whatsap: +255 (0) 755848391

    Email: songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu vyake wasiliana Moja kwa Moja na +255 (0) 684408755 (more…)

  • Njia Nane Zitakazokuwezesha Wewe Kulipwa Mara Mbili Mpaka Mara Kumi Zaidi

    Moja ya tamanio la watu wengi ni kulipwa kiwango kikubwa kuliko ambavyo wanalipwa sasa hivi au  kupata kipato kikubwa zaidi ya wanavyopata sasa. Nina hakika hata wewe ungependa kulipwa zaidi ya unavyolipwa sasa, pengine ungependa kupata kipato mara mbili mpaka mara tatu zaidi ya unavyopata sasa hivi, si ndio? sasa kwenye andiko la siku ya leo tunaenda kuona mbinu ambazo zitakusaidia wewe kulipwa mara mbii mpaka mara kumi zaidi ya unavyolipwa sasa hivi. Mbinu hizi ambazo tunaenda kuona hapa, ni mbinu ambazo zimethibitishwa kufanya kazi na haziwezi kukuangusha endapo utazitumia kama zilivyoelezwa kwenye andiko la leo.

    NJIA YA KWANZA NI KUFANYA KAZI YA UNAVYOLIPWA

    Huu najua ni utamaduni ambao haujazoeleka kwa watu wengi. Kuna vijana wengi ambao siku hizi wanalia ajira mitaani ila wakishapata hizo ajira, wanarelax  na hivyo kushindwa kuchapa kazi kama inavyotakiwa. Moja ya kitu ambacho mimi mwenyewe kimekuwa kikinishangaza ni kuona kwamba vijana wengi wanaandika kwenye CV zao kwamba ni wachapakazi na wanaweza kufanya kazi kwenye hali yoyote, ila pale wanapopata kazi, wanakuwa wazembe kiasi kwamba wanashindwa kufanya kazi na kuleta matokeo ambayo wanaahidi wakati wa kuomba kazi.

    Sasa siku ya leo nataka nikwambie kwamba achana na uzembe wako, kama unataka kulipwa zaidi.  Fanya kazi kwa kujituma zaidi ya unavyolipwa, uhakika ni kwamba hiki kitu baadaye kitakufanya ulipwe zaidi ya unavyolipwa sasa.

    Usije ukachukukulia kuwa juhudi zako ambazo unaweka kwa sasa hivi, zinapotea bure. Unaweza kusema kwamba bosi wako hazioni ila ukweli ni kwamba anaziona hata kama hatakuwa hasemi. Na pengine kuna kitu cha kipekee ambacho atakuwa anakiandaa kwa ajli yako. Au hata kama bosi wako hazioni wala kujali juhudi zako ambazo unaweka. Fahamu kuwa kuna watu wengine ambao wanajali na wanapenda sana juhudi zako, hivyo, kuna siku katika mazingira na namna ambayo wewe mwenyewe hutegemei watu hao watakutafuta ili uende kufanya nao kazi.

    Hamna juhudi zako zinapotea bure. Kiufupi ni kwamba asili, ilivyo ni kwamba, hakuna kitu chochote ambacho huwa unafanya unafanya ambacho huwa kinapotea bure. Ndiyo maana wahenga wetu walituasa vizuri waliposema kwamba unavuna ulichopanda. Ukipanda mbegu nzuri, utapata mavuno mazuri, lakini wakati huohuo ukipanda mbegu mbaya utavuna mavuno mabaya.

    Ukipanda mbegu ya uchapakazi, utpata mavuno yake.

    Ukipanda mbegu ya uzembe, maavuno yake utayapata pia.

    Kwa hiyo, kwenye maisha unapaswa kuchagua, unapaswa kuchagua mbegu nzuri ya uchapakazi dhidi ya mbegu ya uzembe. Maana uchapakazi na kufanya kazi kwa bidii na kujituma zaidi ya unavyolipwa kunalipa zaidi ya kitu kinginecho chochote.

    Sikiliza, kama wewe kwenye maisha yako, unafanya kazi kwa kusukumwa. Yaani, kama ni mpaka usukumwe na kufuatiliwa ili uweze kufanya kazi. basi achana na hiyo tabia kuanzia siku ya leo. Badala yake anza kujituma na kufanya kazi hata kama hakuna mtu yeyote yule wa kukusukuma nyuma ya pazia. Kwanza sifa ya kufanya kazi bila ya kusukumwa wala kufuatliliw na mtu yeyote ndiyo sifa ya pekee ambayo watu wanaoingiza kipato kkubwa wanayo, wewe pia unapaswa kuwa nayo.

    Tena anza kuwa nayo kuanzia leo hii.

    Nakukmbuka kuna kipindi nilikuwa nafanya kazi na kijana mmoja hivi ambaye alikuwa anafanya kazi kwa bidii na kujituma sana. kiukweli nilikuwa napenda kazi zake ambazo alikuwa anafanya na siku zote hakuwahi kuniangusha. Mara nyingi sana nilipokuwa nikimpa kazi ya kufanya kwa siku husika, yeye alikuwa anaweza kuifanya ndani ya saa tatu mpaka nne, na kuimaliza kisha kuendelea na mambo mengine. Hivi union hicho kitu ee. Yaano, kwake kazi ya siku nzima anaifanya ndani ya masaa matatu na kuimalizaa.a

    Alikuwa haitaji usimamizi wangu muda wote.

    Alikuwa anajongeza snaa kwenye kazi yake na kufanya zida.

    Mara zote nilikuwa nikiona juhudi zake, nilizipenda kweli.

    Lakini kumbe kuna watu wengine ambao walikuwa wakiona juhudi zake pia. Siku moja, niliona ananifuata na kuniambia kwamba anaachan kazi kwangu. Kitu hiki kwangu kilikuw akama mwiba maana nilikuwa nikipenda kuwa na kijana kama yule anayechapa kazi na kujituma badala ya kijana anayesimamiwa na kufuatiliwa nyuma muda wote.

    Nilijaribu kumwongezea mshahara mara mbili ii tuendelee kufanya kazi kwa pamoja, lakini alikuwa ameshafikia uamuzi wa kuondoka. Mpkaka leo hii huwa anakutana naye mara kwa mara, ana furaha muda wote na anapenda kazi anayofanya huku akiendeleza juhudi zake za kuchapa kazi zaidi ya anavyolipwa.

    Hiki kitu kimenifunza sana, mbali na kwamba kufanya kazi kwa bidii kunakufanya unalipwa zaidi. lakini pia naona kwamba wanaofanya kazi kwa bidii wana furaha kuliko ambao wanzembe.

    Wanaozembea ndio wenye majungu muda mwingi, maneno mengi ambayo hayana tija, ndio wanalalamika, ndio ambao wanapenda kuonewa huruma, wanapenda kuongezwa mishahara huku wakiwa hawaweki juhudi. Naomba unisikilize kwa kitu kimoja. Weka juhudi kwenye kazi zako unafanya. Juhudi zako unawezoweka zitakufikisha mbali zaidi ya ulipo sasa hivi.

    Penda sana kufanya kazi zaidi ya unavyolipwa

    SOMA ZAIDI: JITUME KWA FAIDA YAKO

    FANYA KAZI KWA BIDII

    NJIA YA PILI NI KUSOMA VITABU

    Kusoma vitabu kuna uwezo wa kukufanya ulipwe mara mbili mpaka mara tatu au hata mara kumi zaidi ya unavyolipwa sasa hivi. kama kuna kitu ambacho unapaswa kukipa kipaumbele kwenye maisha yako nbasi ni kusoma vitabu na kupenda kujifunza mara kwa mara.

    Unaweza kuwa unajuliza, kwani kusoma vitabu kunawezaje kunifanya mimi  niongeze kipato changu mara mbili mpaka mara tatu zaidi ya ninavyoingiza sasa hivi.

    Kwanza ni kwamba kusoma vitabu na kupenda kujifunza kunakufanya unakuwa na maarifa ambayo wengine wanakuwa hawana. Hivyo, hayo maarifa yanakuwezesha wewe kufanya uamuzi ambao wengine wanakuwa hawana.

    Ebu tuchukulie mfano, umesoma na kujifunza kuhusu uwekezaji kwenye hisa. Umeuelewa vizuri na na kutumia maarifa haya mauzri uliyoyapata ukaanza kuwekeza kwenye hisa, hatifungani pamoja na vipande. Baada ya siku kadhaa, utaanza kupata gawio linatokana na uwekzaji wako kwenye hisa. Hicho ni kipato zaidi rafiki yangu ambacho ulikuwa huingizi mwanzoni rafiki yangu.  Na tena unakipata bila kuweka juhudi zaidi.

    Au tuseme unasoma kitabu kama JINSI YA KUWA MWANDISHI MBOBEBVU. Baaada ya siku chache unajifunza ujuzi wa uandishi, ujuzi ambao unalipa na ujuzi mzuri kwenye zama hizi tunazoishi. Baada ya siku si nyingi utakuwa umeweza kuwa mwandishi mzuri ambaye anaweza kuandika andiko linaloeleweka. Unaweza kukuta unapata tenda z kuandika maeneo mbalimbali ambayo hata hukutegemea kama magazetini, hicho ni kipato cha ziada rafiki yangu hapo kinakuwa kinagonga mlango.

    Lakini pia kusoma na kujifunza kunakusaidia wewe kuweza kupangilia ratiba yako na hivyo, kujua majukumu yapi uyafanye lini na majukumu yapi usiyafanye kwa wakati gani. wakati hali ni tofauti kwa mtu ambaye hasomi.

    Kusoma vitabu na kupenda kujifunza kunakufanya unakuwa mmbunifu. Kitu hikitu kinaweza kukufanya wewe ulipwe mpaka mara tano au mara kumi zaidi.

    Nakumbuka kuna mzee mmoja ambaye alikuwa anapenda sana kujifunza kupitia semina na mafunzo mbalimbali. HUYU MZEE alikuwa daktari. Kuna siku alihudhuria semina inayohusiana na upasuaji wa macho. Semina hii ilikuwa ya gharama kubwa, ila mzee huyu alilipia. Kwenye semina hii alijifunza ujuzi ambao ulikuja kumtofautisha yeye na madajtari wengine maisha yake yote.

    Kumbe, kitu kimoja ambacho unasoma kwenye kitabu kinaweza kubadili maisha yako na kukufanya kuwa mtu wa tofauti kabisa.

    NJIA YA TATU NI KUWAFIKIA WATU WENGI ZAIDI

    Kama unamhudumia mteja mmoja, unachopaswa kufahamu ni kuwa siku huyo mteja akiacha kununua kwako basi wewe utakuwa huna kipato tena. Kama umeajiriwa maana yake unamhudumia mteja mmoja ambaye ni mwajiri wako. Kwa hiyo kipato chako kitakuwa na ukomo kwa sababu mteja unayemhudumia ni mmoja.

    Sasa ebu fikiria mtu menye ujuzi kama wewe, elimu kama wewe na kila kitu kingine chochote kama wewe akiwahudumia wateja watano, unadhani atalipwa kiasi gani? maana yake atalipwa mara tano zaidi ya unavyolipwa wewe.

    Kumbe basi, mara zote angalia ni kwa namna gani ambavyo unaweza kuwahudumia wateja zaidi na kupanua masoko yako.

    Kama umeajiriwa, unaweza kuanza kuagalia namna ya kutumia ujuzi wako nje ya ajira, ili ule muda baada ya kutoka kazini uweze kuuwekeza kwenye biashara au kuwahudumia wengine zaidi. Kwa jinsi hii utakuwa untengeneza mifereji ya kulipwa zaidi hapo baadaye.

    NJIA YA NNE NI UAMINIFU

    Katika uliwngu tunaoishi sasa hivi, uaminifu ni kitu kimoja muhimu sna ambacho unahitaji. Bila uaminifu rafiki yangu takwama sana. Iwe umeajiriw au unafanya kazi kwa kujiajiri, unahitaji uaminifu  wa hali ya juu sana.

    Watu wanapenda kufanya kazi na waaminifu.

    SOMA ZAIDI: UAMINIFU NI MTAJI

    NJIA YA TANO NI KUONGEZA THMANI KWENYE BIDHAA UNAZOTOA

    Watu wanapenda kupata vitu vyenye thamani nzuri. Hakikisha kwamba kazi yoyote ile ambayo mkono wako unagusa, unaifanya kwa viwango vya juu. Kwa jinsi hii nakuhakikishia kwamba muda si mrefu, watu watamiminika ili wapate kazi zako zaidi.

    NJIA YA SITA NI KUWA NA BIDHAA ZAIDI YA MOJA.

    Ukiwa na bidhaa moja maana yake mteja akija kununua wako hiyo akiondoka ndiyo ameondoka. Yaani, hatarudi tena kununua tena. Ebu tuchukulie unauza redio tu. Mtu akinunnua kwako hawezi tena kuna kununua kwako redio maana tayari anayo.

    Ukiwa na bidhaa zaidi ya moja maana yake mteja mmoja anaweza kununua kwako zaidi ya mara moja. na hata akinunua mara moja maana yake atanunua vitu vingi kwa wakati mmoja. Mfano ni simu, earphone, chaja, memory card, n.k

    Lakini pia unamfanya mteja aweze kurudi kununua kwako mara kwa mara.

    Endapo ukiwa na bidhaa moja walau iwe ni bidhaa ambayo wateja watakuwa wanakuja kununua mar kwa mara. Mfano chumvi au sukari. Hizi ni bidhaa ambazo wateja lazima watakuja kunua mara kwa mara hata baada ya kuwa wamenunua mara ya kwanza. Kwa jinsi hii kadiri watakavyokuwa wanaunua zaidi ndivyo na kipato chako kitaongezeka. Na siyo wanunue tu wenyewe kwa kurudi. Bali warudi na wateja wengine zaidi.

    NJIA YA SABA NI KULIPWA KWA KAMISHENI

    Kama unachapa kazi kwa bidii, badala ya kukubaliana na bosi wako akulipe kwa mshahara mwisho wa mwezi, amua kwamba unaenda kulipwa kwa kamisheni. Unajiuliza hivi kulipwa kwa kamisheni ndio nini?  Kulipwa kwa kamisheni maana yake unalipwa kulingana na matokeo unayozalisha. Yaani, kwa mfano kama unafanya kazi mgahawani. Ukiuza sahani 10 na kila sahani unalipwa elfu moja maana yake siku hiyo, utalipwa elfu kumi. Lakini, ukijisukuma zaidi ukauza sahani thelathini maana yake siku hiyo utalipwa elfu thelathini. Huku ndiyo kulipwa kwa kamisheni.

    Yaani, juhudi zako zinakuwa ziaendana na bidii unavyoweka. Kadiri unavyoweka bidii zaidi kwenye kazi ndivyo ambavyo unalipwa zaidi.

    Mbinu hii unaweza kuitumia kama umeajiriwa au umejiajiri.

    Kwa mfano, kama unaona unaweza kuajiriwa kwenye biashara fulani na kumsaidia bosi wako kupata matokeo makubwa zaidi ya anavyopata sasa hivi. unaweza kuongea naye, mwambie kwamba  wewe unaweza kuwa na mbinu ya kusamsaidia kuongeza kipato kwenye biashara yako, lakini sharti akulipe kwa kamisheni. Hii ni nzuri sana maana hakuna anayepujwa. Unalipwa kwa jasho lako. Kadiri unavyoweka juhudi zaidi, ndivyo ambavyo unalipwa zaidi.

    Kama umeajirajiri unaweza kujiwekea lengo. Labda lengo la kufanya mauzo na laki tano kila siku. Na ukajiambia kwamba nikifikisha mauzo laki tano kwa siku basi mimi mmweywe nitajilipa asilimia labda kumi. Kwa hiyo, siku ambayo unakuwa hujafikisha hiyo laki tano, utajilipa kulingana na kiwango ulichoingiza

    Kama umeingiza laki moja basi utajilipa elfu kumi tu.

    Hii ni njia nzuri, japo watu wengi hawaipendi kwa sababu haijazoeleka kwenye mazingira mengi. Lakini pia siyo njia rafiki kwa watu ambao hawapendi kufanya kazi kwa bidii na kujituma zaidi.

    SOMA ZAIDI: Njia Tano Za Kuingiza Fedha Mtaani Kwako Kuanzia Leo

    Je, Kuna Namna Na Kutengeneza Fedha Kupitia Affiliate Marketing Ukiwa Nchini Tanzania?

     

    NJIA YA NANE, ACHANA NA ANASA

    Unaweza kuwa unajiuliza, kwani anasa zangu zina uhusiano  gani na kulipwa zaidi. Tena, unaweza kuhitimisha kwa kusema kwamba, mimi nitaendelea na starehe zangu ila nitafania kazi hayo mengine ambayo umeeleza hapo juu.

    Ninachotaka ni nikwambie ni kwamba, anasa zinapoteza muda wako mwingi ambao ungutumia kwa ajili ya kufanya kazi ya kukuongezea kipato. Anasa zitakufanya upoteze muda kwa wingi. Na muda ni mali.

    Kwa hiyo, achana na kupambana na mambo ya anasa kuanzia leo hii. badala yake pambana na ndoto pamoja na malengo yako. Kila siku hakikisha kwamba unafanya kitu na unakfanyia kazi kila siku. Siku siyo nyingi wa

    Lakini pia ni muhmu cha kufahamu ni kuwa kwanza anasa zinachukua fedha zako.

    pili, anasa zinakupunguzia ufanisi

    Na tatu unapokuwa unapambana na anasa, maana yake unakuwa na pambana na lengo ambalo siyo sahihi. Na hivyo, lengo la kuongeza kipato chako zaidi litakushinda.

    Rafiki yangu, hizo ndizo njia nane za kulipwa mara nane mpaka mara kumi zaidi ya unavyolipwa sasa.

  • Hii Ndiyo Sheri Ambayo Itakusaidia Wewe Kupata Chochote Kile Unchotaka

    Profesa mmoja alifanya kijiutafiti chake binafsi. Zilikuwa ni nyakati za krismasi, hivyo alichofanya ilikuwa ni kuandika kadi za krismasi kwa watu ambao walikuw hawamjui huku akiwatakia kheri ya krismasi.

    Profesa akakaa huku akisubiria majibu. Baadaye alikuja kugundua kuwa asilimia kubwa ya watu walijinu kwa kushukuru kwa kadi ile ya krismasi ambayo alitoa na , ila wengi sana hata hawakumuuliza kuwa alikuwa nani na mawasiliano yao aliyapataje.

    Hiki kitu ndiyo ninataka kianze kutupa mwanga kwa ajili ya somo letu la leo

    Leo tunaizungumzia kamnuni ya RECIPROCAL. Kulingana na kanuni hii ni kwamba, ukifanyia mtu kizuri. mtu huyo anahisi kama ana deni na anapaswa kukulipa kulingana na kile ulichomfanyia.

    Ukimpa mtu labda msaada, anajiona kwamba kuna deni ambalo anapaswa kukulipa kulingana na msaada ambao umempa.

    Hivyo, unaweza kuitumia kanuni hii kwenye biashara yako pia au kwenye kitu ambacho unafanya pia. Kadiri unavyotoa kitu chenye thamani kubwa, ndivyo watu wataona kwamba kama wana deni vile ambalo wanapaswa kukulipa na hivyo utajenga timu ya watu ambao wanakuamini kwenye kile unachofanya na hata wateja wa kudumu.

    Kila la kheri.

  • Nguvu ya uvumilivu

    Kuna ndugu mmoja alianzisha biashara huku akitegemea kwamba watu wangemiminika kwenye biashara yake siku ya kwanza. Ila watu hawakumiminika kama alivyokuwa anatarajia. Siku ya kwanza alitokea mtu mmoja wa kuuliza kuhusiana na biashara yake na kile ambacho anafanya. siku ya pili watu kadha wa kadha pia walipitia na kuangalia kuuliza uliza ila hawakununua.

    Siku ya tatu ndipo alikuja kufanya mauzo ya kwanza.

    Kadiri siku zilivyokuwa zinazidi kusoge ambele ndivyo watu walikuwa wanazidi kuongezeka kwenye kununua kwake.

    Kumbe siyo kwamba kila ukianzisha kitu watu watamiminika kwako na kujipanga ili wapate kitu chako. Hapana, itachukua muda, maana kadiri watu watakavyokuwa wakiona ukiendelea kufanya hicho kitu ndivyo ambavyo hao watu watakuwa wakivutiwa kuja kwako.

    Ukimhudumia vizuri yule mteja wako wa kwanza, atarudi kwako tena siku nyingine. nap engine hatarudi peke yake. Bali atarudi pamoja na rafiki zake na hivyo kuongeza idadi ya watu ambao wanapata huduma kwako.

    Usidharau hizi hatua ndogo ndogo unazopiga. Na usiwe na haraka. Vumilia pale unapokuwa hupati matokeo makubwa mwanzoni huku ukiendelea kuweka juhudi zaidi ili uweze kufikia mafanikio unayoyataka.

    Kila la kheri

  • Vitu Vitano Vitakvyokuwezesha Kupata  Maisha Ambayo Umekuwa Unatamani

    Siku ya leo kuna vitu vitano ambavyo naamini kwamba ukivifanyia kazi, unaenda kuwa na maisha ambayo umekuwa ukiyatamani kwa siku nyingi. Kilichokukwamisha wewe kuweza kupata maisha unayoyataka ni kwa sababu hujafanyia kazi hivi vitu vitano hapa.

     

    Kitu Cha Kwanza Ni Kujua Watu Wanataka Nini. Ukijua watu wanataka nini, wewe pia utaweza kupata kitu chochote kile ambacho unataka. Kivipi unajiuliza, iko hivi, kama kuna kitu ambacho watu wanataka na wewe ukawaletea hicho kitu, ni wazi kuwa hawa watu wantakuwa tayari kukulipia na kwa jinsi hiyo utaweza kutengeneza kipato chako kizuri tu.

     

    Lakini je, unajuaje kitu ambacho watu wanataka.

    Hapa utaangalia vitu ambavyo watu wanapenda kufuatilia

    Vitu ambavyo watu wanapenda kuongelea mara kwa mara

    Matatizo ya watu pia yanaweza kukuonesha vitu ambavyo watu wanataka

    Lakini pia kuna vitu ambavyo kwa asili tunataka. Chakula, mavazi na malazi. Na havitabadilika. Kwa hiyo, angalia ni kwa namna gani ambavyo unaweza

    Kwa hiyo kazi yako ya kwanza kabisa rafiki yangu ni kuangalia watu walio kuzunguka wanataka nini. Ukishajua kitu ambacho watu wanataka, basi wape hicho kitu, na hao watu watakuwa tayari kukulipa.

    Pili Ni Kufanya Hicho Kitu Kwa Ubora Na Ubunifu

    Kuna kanuni ambayo unaweza ukawa hujawahi kuisikia. Inaitwa copy-cut principle. Kulingana na kanuni hii ni kwamba kwa kitu chochote kile ambacho unafanya. , hata kama umeanza kufanya hicho kitu kikiwa kipya, ndani ya miezi sita, kuna watu watakuwa nao wameanza kufanya hicho kitu. Watakopi unachofanya na wataanza kukifanya wao pia.

    Hiki kitu ndiyo kinaitwa copy-cut. Unaweza kuanzisha mgahawa eneo fulani. Ndani ya miezi sita, ukakuta kuna watu watatu au wanne nao wameanzisha migahawa kama wa kwako halafu eneo hilohilo.

    Sasa ili kujitofautisha kwenye kile unachofanya unahitaji kuwa mbunifu na kuhakikisha kwamba unafanya unafanya kile unacahofanya kwa ubora

     

    Lakini ubunifuni ni nini? na utauwekaje kwenye biashara? Hii ni mada ndefu ambayo siwezi kuiongelea yote kwenye hii makala ila kwa leo itoshe kusema kwamba ubunifu ni kufanya vitu kwa namna ta tofauti na vile ulivyofanya jana. Na hapa huhitaji kufanya mapinduzi makubwa kwa wakati mmoja. Badala yake unaweza kufanya marekebisho ya kitu kimoja baada ya kingine, baada ya muda biashara yako ikawa inazidi kuboresheka zaidi.

    Mfano leo hii unaweza kujiweka kwenye viatu vya mteja wako na kuangalia kama ungekuwa mteja kwenye biashara yako, je, ungependa kupata huduma ambayo inatolewa kwenye biashara yako? Kama huduma hiyo hujaipenda basi unaangalia wapi pa kuboresha ili uweze kutoa huduma bora zaidi kwa wateja wako.

    Lakini pia kesho unaweza kuboresha kipengele cha huduma kwa wateja na kukifanya kuwa bora zaidi.

    Kwa vyovyote vile unakuwa hutulii kwenye hali ileile kila siku. Badala yake unakuwa unazidi kukua na kufanya kitu kwa ubora na ufanisi zaidi.

     

    Tatu Ni Kuwa Na Mwendelezo Wa Kile Unchofanya

    Watu wengi huwa wanapenda kuanzisha vitu ila wanaishia njiani. Sasa naomba unisikilize kwenye hili, bila kujali kwa sasa unapitia kwenye hali gani. kwa vyovyote vile jitahidi kuendeleza ulichoanzisha bila ya kukoma. Kuna watu wengi huwa wanapenda kuanzisha vitu ila huwa wanaishia njiani. Sikiliza, kitu kimoja cha uhakika ni kwamba ukiweza kuwa na mwendelezo wa kile ulichoanzisha, utaweza kufika mbali.

     

    Haijalishi umeanzia wapi, haijalishi umeanzia kwenye hali ya chini kiasi  gani. Bado utaweza kufika mbali na kuona makubwa endapo tu utakuwa na mwendelezo wa kile unachofanya bila ya kuacha.

    Nne Ni Kujifanyia Tathimini

    Ni muhimu sana uwe unajifanyia tathimini kila mara kuona vitu gani ambavyo umefanya na vimefanya vizuri na vitu gani unafanya ambavyo havijaenda vizuri. Na kwa jinsi hii utaweza kuona wapi labda kuna mwanya ili uweze kuuziba, au labda utaona kwamba kuna vitu ambavyo umekuwa unafanya kwa mazoea, na sasa unahitaji kuviboresha na kuvifanya kwa uzuri zaidi.

    Tano, Ukifanya Makosa, Usijishikize Kwenye Makosa Yako. Inuka endelea mbele. Ni kweli huwa tunafanya makosa kwenye vitu ambavyo tunafanya, ila sasa usijishike kwenye makosa yako. Badala yake ukifanya makosa, imuka, kisha songambele ili uweze kufanya makubwa zaidi.

    Kwa leo naishia hapa

    Nakutakia kila la kheri

    Godius Rweyongeza

    0755848391

  • Fanya vitu vichache kwanza

    Kuku anapoatamia mayai anasahau mpaka kula ili tu hakikishe lengo lake la kuatamia na kupata vifaranga linatimia.

    Wewe pia kuna vitu unapaswa kuachana navyo sasa hivi li uweze kufika kule unapotaka kwenda

    Siyo lazima ukimbizane na kila kitu sasa hivi.

    Fanya vitu vichache ambavyo vitekupelekea kwenye lengo na ndoto yako badala ya kukimbizana na kila kitu.

    Kila la kheri

  • Hatua Nane Za Kuwa Mwandishi Mbobevu

    Leo nataka nikupe hatua nane za kuwa mwandish mbobevu.

    1. Andika

    2.  Kila

    3. Siku

    3. Hata

    4. Kama

    5. Ni

    6. Sentensi

    7. Moja

    8. Tu.

    Rafiki yangu unakwama wapi kwenye kuandika. Naamini kwa siku huwezi kukosa hata dakika tano tu za kuanadika hata kama unaandika kitu kidogo.

    Unahitaji kuandika kila siku kwa sababu kadiri unavyoandika kila siku ndivyo unavyozidi kubobea zaidi kwenye uandishi wako.

    Je, upo  tayari kuanza marathon ya uandishi? Basi anza leo hii kwa kuandika hata utambulisho wako kwa kifupi na kitu ambacho utakuwa unaandika.

    Unaweza kunishirikisha kwenye whatsap  0755848391

    Godius Rweyongeza

  • Usiache Kufanya Mazuri Kwa Sababu Umezungukwa Na Watu Wanafanya Mabaya

    Kama umezungukwa na watu ambao wanafanya vitu ndivyo sivyo. Usikubali kuachana na tabia yako nzuri na kuanza kufanya vitu ambavyo havieleweki. Mara zote na sehemu zote hakikisha kwamba unafanya mazuri hata kama umezungukwa na watu ambao wanafanya vitu vibaya..

    Usikubali kuwa sehemu ya kuendeleza ubaya. Badala yake sambaza upendo wa kufanya mazuri.

    Unaweza usione matokeo ya kile unachofanya kwa muda mfupi. Ila uhakika ni kwamba baada ya muda matokeo hayo unaenda kuyaona.

    Kwa hiyo endelea kuonesha wema wako.

    Asili huwa huwa haisahau. Siyo kwamba utafanya mazuri na yatasahaulika. Hapana, hayo mazuri kuna watu wanaona hata kama watakuwa ni wachache. Na hata kama wengine watajidai kama hawaoni, ila watakuwa wanaona.

    Kuna siku utapata matokeo ya mbegu zako hizi za wema unazopanda.

  • Hivi Ndivyo Na Wewe Unaweza Kuandika Kitabu Historia Ya Maisha Yako Kama Sugu

    Miongoni mwa watanzania ambao wameandiaka vitabu vya historia ya maisha yao ni Sugu. Kitabu chake kinaeleza historia ya maisha yake kuanzia alipozaliwa mpaka anaingia bungeni mwaka 2010. Kina mambo mengi mzuri na ya kujifunza kwelikweli. Nashauri kama hujasoma kitabu cha Sugu, kinachoitwa Maisha na muziki ukisome. Utajifunza mengi sana ndani ya hiki kitabu. Tunaweza pia kuwasiliana kwa 0755848391 ili nikutumie nakala ya kitabu chako kwa bei chee tu.

    Sasa baada ya kusema hayo tuone ni kwa namna gani wewe pia unaweza kuandika kitabu cha kwako.

    Watu wengi wanafikiri kwamba kuandika kitabu kikubwa na kizuri kama hicho basi ni kazi kubwa. Hapana. Kuna njia mbili za kuandika kitabu kama hicho.

    SOMA: UCHAMBUZI WA KITABU CHA SUGU MAISHA NA MUZIKI. Mambo 14 niliyojifunza kwenye kitabu hiki kinachoeleza Maisha ya Sugu Kutoka Mtaani Mpaka Bungeni

    Kwanza ni kuanza kukiandika kidogo kidogo. Yaani, unakiandika hatua kwa hatua. Kwa mfano leo hii, tena sasa hivi unaweza kuamua kuanza kuandika historia ya maisha yako kwa kuandika jina lako na sehemu ulipozaliwa. Kesho ukaongeza kitu kingine kwa kuandika sehemu ulipokulia. Siku nyingine ukaandika namna ulivyosoma shule ya msingi. Siku nyingine ukaandika masomo uliyokuwa unapenda shule ya msingi. Siku nyingine ukaandika kuhusu ile siku uliyotoroka shuleni mwalimu akakuchapa.

    Muda siyo mrefu utakuta kwamba kitabu chako kinazidi kusogea na mara kitabu chako kitakuwa kimeisha. Kitachukua muda kukikamilisha. Lakini nina hakika huu mchakato utaufurahia sana. kila siku utakuwa ukiandika maneno kidogo. Hata kama ni maneno 1000 tu, lakini utakuwa umeyaandika na yatakuwepo kwenye kitabu chako bila shida yoyote ile. Nashauri sana kama una mpango wa kuandika basi usisite kuanza kuandika sasa hivi, tena leo hii. anza tu hata kama ni kidogo

    Bado huna uhakika ni kitu gani ambacho unaweza kufanya? Basi wasiliana name kwa 0755848391 ili niweze kukupa mwongozo na kukushikamkono wakati unaandika kitbu chako. Nimesaidia wengi wanaoandika vitabu vya historia ya maisha yao. Wewe unaenda kupata msaada pia. Karibu.

    Njia ya pili ya kuandika kitabu cha historia ya maisha yako. Na hii ni kama uko bize tu. kama hauko bize tumia njia ya kwanza, itakufaa sana. Kwa njia hii ya pili, maana yake unatafuta mtu ambaye anaweza kukusaidia kuandika na kupangilia matukio ya kitabu chako. Unakuwa unawasiliana naye, na yeye anakusaidia kupangilia matukio ya kitabu  chako mpaka kinakamilika.

    Unampa taarifa kwa njia ya sauti.

    Mnafanya mahojiano. Na hata anawahoji watu wako wa karibu kidogo, kisha anakusaidia kuandika kitabu kilichopangiliwa vizuri na kinachosomeka.

    Hizo ndizo njia mbili unazoweza kutumia kwenye kuandika kitabu chako.

    Kitu kimoja muhimu sana kwenye hili hapa ni kwamba unapaswa kuandika kitabu chako. Usikubali kuacha historia ya maisha yako bila kuandikwa kwenye kitabu. Kamwe usikubali kitu kama hiki kitokee kwenye maisha.

    Historia ya maisha yako, itawanufaisha sana wanao mpaka wajukuu wako.

    Kila la kheri.

  • Maswali Yanaoulizwa Mara Kwa Mara Kuhusu Semina Ya Uwekezaji Kwenye Hisa

    Unaendeleaje mwekezji siku ya leo ningependa kujibu maswali ambayo watu wamekuwa wanauliza mara kwa mara kuhusu semina ya uwekezaji kwenye hisa?
    1. Semina itaendeshwa wapi?
    Semina itaendeshwa kwa njia ya mtandao kupitia kundi maalumu la whatasap. Na inaenda kudumu kwa siku 10 mfululizo. Yaani, kuuanzia tarehe 1.8.2022 mpaka tarehe 10.8.2022
    2.Je, atakayehudhuria semina atajifunza vitu gani kwenye hii semina?
    Hii ni semina ya uwekezaji kwenye hisa. Hivyo, mtu yeyote ambaye atahudhuria hii semina atapata elimu yote ya msingi kuhusu uwekezaji kwenye hisa.
     Hiyo mwisho wa semina hii nategemea kuwa kila mshiriki
    👉🏿 atakuwa anajua maana ya hisa, hatifungani na VIPANDE.
    👉🏿Viashiria vitakavyokuonesha kwamba hapa unapaswa kununua hisa au unapaswa kuuza hisa zako.
    👉🏿 Atakuwa anajua namna ya kuchambua kampuni moja baada ya nyingine na hivyo  kufanya uamuzi bora juu ya kampuni ya kuwekeza.
    👉🏿kila mshiriki atapata maelekezo ya kufungua akaunti ya kuwekeza na matarajio yangu kuwa kabla semina Haijaisha wengine watakuwa wameshaanza kuwekeza
     👉🏿kila mshiriki atajua namna ya kutumia simu yake katika UWEKEZAJI kwenye soko la hisa na vipande.
    👉🏿Atajua kuhusu mnada wa dhamana za SERIKALI na namna ambavyo anavyoweza kununua dhamana hizi.
    Halafu tutaona kati ya hisa, hatifungani kipi unaweza kuanza nacho na namna ya kutumia vitu vyote vitatu kutengeneza utajiri.
    3. Je, kuna vitu vingine ambavyo mtu akayehudhuria semina atapata.
    Ndio vipo. Sambamba na kuhudhuria semina hii ya kipekee unaenda kupata kitabu cha bure tena hardcopy ya kitabu cha JINSI YA KUWEKA AKIBA NA KUANZA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE.
    Hiki kitabu utakipata bure bila ya kuongeza gharama ya ziada.
    4. JE, Kuna gharama ambazo zitahusika kwenye kuhudhuria semina
    NDIO GHARAMA ZIPO, na gharama hizi ni shilingi 21,000/- tu. Ukilipia hiki kiasi utaweza kuhudhuria semina ya siku 10. Na utapata bonasi ya kitabu cha JINSI YA KUWEKA AKIBA NA KUANZA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE
    5. Je, kitabu kinatumwaje kwa watu wa mikoani? Je, kuna Gharama za ziada ya kutuma
    Kitabu kitatumwa kwa basi MPAKA mkoani na hakuna Gharama ya ziada inahohitajika ili utumiwe kitabu.
    Hii nimesema Ni bonasi unaipata kwa kuhudhuria semina. Hivyo huchajiwi Gharama ya ziada. Wewe Ukilipia 21,000/ tu ya semina unakaa mkao wa kula.  bure.
    Kumbe kwa kuhudhuria semina hii Ni Kama unaua Ndege wawili kwa jiwe moja.
    Unapata mafunzo ya kina kuhusu UWEKEZAJI kwenye HISA. Na bado unapata kitabu bonasi ya kitabu cha JINSI YA KUWEKA AKIBA NA KUANZA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE.
    6. Kitabu nitakachopata kinaendana na masuala ya hisa?
    Ndiyo. Kinaitwa JINSI YA KUWEKA AKIBA NA KUANZA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE.
    Thibitisha kuwa utahudhuria semina hii ya kipekee kwa kutuma ujumbe kwenda 0684408755 Karibu sana.
    Jiunge na kundi letu la uwekezaji kwenye hisa hapa

  • Hivi Ndivyo Elfu moja inaweza kukusaidia kuhudhuria semina ya uwekezaji kwenye hisa

    Unaendeleaje rafiki yangu wa ukweli. Mimi kwa upande mwingine huku naendelea vizuri kabisa.

    Wiki ilyopita nilitangaza juu ya uwepo wa semina ya uwekezaji kwenye hisa.

    Semina hii ya kipekee itaendeshwa kwa njia ya mtandao wa whatsap kupitia kundi maalumu la semina.

    • Itadumu kwa siku 10 na kila siku itakuwa ni siku ya mafunzo kwako.
    • Baada ya semina utapata kitabu (hardcopy) cha JINSI YA KUWEKA AKIBA NA KUANZA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE. Hii ni nakala ambayo kila atakayehudhuria semina hii ataipata, mwishoni kabisa mwa semina
    • Jina lako litaandikwa kwenye kitabu utakachopokea. Ningependa kuandika jina lako kwenye hiki kitabu kinapotoka, na jina lako litaendelea kuwa kwenye hiki kitabu vizazi hadi vizazi.

    Njoo rafiki yangu uhudhurie semina hii ya kipekee, ujifunze mbinu za kuwekeza kwa faida.

    Gharama ya semina hii ni 21,000/- tu. Na kitabu cha JINSI YA KUWEKA AKIBA na kuanza kuwekeza utakipata bila gharama ya ziada. Utakipata kwa gharama hiyohiyo ya 21,000/-

    Kuna njia mbili za kulipia semina hii.

    Moja ni kulipia moja kwa moja fedha yote kwa mkupuo. Unalipa kwa namba ya 0684408755 jina ni GODIUS RWEYONGEZA.

    Au unalipa kidogokidogo.kwa kiwango utakachojiwekea wewe.

    Kiwango cha chini kabisa unaweza kuanza kulipa elfu moja kila siku kuanzia leo hii. Ambapo baada ya siku 20 utakuwa umekamilisha malipo. Karibu sana. Hakikisha kwamba kwa vyovote vile unahudhuria semina hii ya kipekee rafiki yangu. mwambie na rafiki yako.

    Ni mimi Godius Rweyongeza (Songambele)

    0755848391

    Morogoro-Tz

X