Home


  • Namba Zetu Za Malipo

    Namba za malipo ya vitabu:

    Namba za lipa

    TIGO PESA: 19016638 Jina ni SONGAMBELE CONSULTANTS

    M-PESA: 5564517 jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

    Namba za kawaida

    AIRTEL MONEY: 0684408755
    TIGO PESA: 0655 848 392
    M-PESA: 0745 848 395

    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    NB: Kama namba ya malipo anatumiwa mtu ambaye yuko nje ya nchi. Iandikwe Kwa kuanza na +255

    Kwa hiyo namba zinazotumwa nje ya nchi zitakuwa
    Airtel money: +255 684 408 755
    TIGO PESA: +255 655 848 392
    M-PESA: +255 745 848 395

    KOTE Jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Kama malipo yatakuwa yanafanyika kupitia benki.

    Yafanyie kupitia

    1. CRDB BANK: 0150770710200
    2. NMB BANK: 22110047274

    Kote jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

  • Wasiliana na Godius Rweyongeza Sasa

    Habari yafuatayo ni mawasiliano Unayoweza kutumia kumpata GODIUS RWEYONGEZA

    Simu: +255 (0) 684408755

    Whatsap: +255 (0) 755848391

    Email: songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu vyake wasiliana Moja kwa Moja na +255 (0) 684408755 (more…)

  • Jinsi Mafanikio Makubwa Yanavyojengwa

    Picha hapo chini ni picha ya jengo la Taj Mahal. Jengo hili lipo kwenye Maajabu Saba ya dunia.
    Hili jengo lilichukua miaka 22 kujengwa Mpaka kukamilika.

    Jengo la Taj Mahal

    Hiki kitu kikupe picha ya kuwa vitu vizuri kwenye maisha huwa haviji kirahisj. Najua unapenda sana kupata vitu vizuri, lakini vitu vizuri huwa haviji kirahisi. Ni mchakato.

    Ndio maana wahenga wetu wanasema kwamba hata mbuyu ulianza kama mchicha. Hii ni kuonesha kuwa vitu vizuri, vipo, lakini vinajengeka kidogokidogo.

    Tena wakati mwingine vinaweza kuonekama vinaanza kimasihala vile.

    Ebu fikiria kama wajenzi wa ghorofa. Ukikuta wanaanza kujenga ghorofa, wewe mwenyewe unaweza kufikiri wamechanganyikiwa. Eti wanajenga ghorofa Ila wanaanza kwa kushuka chini. Hahaha
    Wanachimba shimo reeefu kwenda chini…

    Hivi ndivyo mazuri yanavyoanza, siyo kwamba mara zote mazuri yataanza kwa uzuri wake. Muda mwingine msingi unajengwa kwanza, halafu ndio Mambo mengine yanafuata.

    Rafiki yangu, labda nisisitize tu. Ni kitu gani unapenda kufikia au kupata maishani mwako?

    Basi kipe muda. Anza kukifanyia kazi taratibu bila kuchoka. Kumbuka kwamba inawezekana kama hautarudi nyuma.

    Hatua moja moja itakufikisha mbali tu.

    Inawezekana. Kila la KHERI
    Godius Rweyongeza
    0755848391
    Morogoro-Tz

    NB: Kama umependa makala hii utapenda pia mafunzo ninayotuma kwa baruapepe. Jaza taarifa zako hapa chini ili uwe miongoni mwa watu wanaopokea mafunzo haya

  • Ufanyeje unapokuwa unasoma vitabu huku unasahau?

    Unaendeleaje rafiki yangu, juzi kuna mtu aliniambia kwamba anapenda kusoma vitabu, ila sasa tatizo lake ni kwamba akisoma anasahau alichosoma kwenye kitabu na hata kabla ya kumaliza kusoma kitabu husika.

    Kitu hiki ndicho kimeniweka hewani siku ya leo nili niweze kukiandikia maana najua kuna watu wengi pia ambao wanapata shida hii.

    Kwanza ninachopenda kusema ni kwamba kama unasoma na unasahau, usiache kusoma vitabu. Endelea hivyo hivyo bila kuacha.

    Usitake kuona matokeo kwa siku moja. kuna kitu kinaitwa riba mkusanyiko. Yaani, vitu vidogovidogo vinakusanyika kutengeneza kitu kimoja kikubwa. Unaweza leo hii usione matokeo ya kile unachosoma, ila kumbe yanakusanyika na siku moja katika hali ambayo hutegemei, ukapata matokeo ya tofauti.

    Kwa hiyo, kama unasoma vitabu na unasahau, usiache kusoma endelea kusoma.

    Kitu cha pili, baada ya kuwa umesoma kitabu, jiulize ni kitu gani kimoja ambacho nimetoka nacho kwenye hiki kitabu? Ni kitu gani kimoja? Usitaka kuondoka na kila kitu kwenye kitabu. Wewe ukipata kitu kimoja tu kutoka kwenye kitabu na hicho kitu ukakifanyia kazi. inatosha.

    Kwa mfano, ukisoma kitabu kuhusu fedha na uwekezaji. Toka na kitu kimoja kama kuweka akiba kila unapopokea mshahara wako. Hicho kitu kifanyie kazi. raha ya vitabu ipo kwenye kufanyia kazi kile ulichojifunza na siyo kwenye kusoma tu.

    Kwa sasa hivi sina la ziada

    Mimi naitwa Godius Rweyongeza kutoka SONGAMBELE

    Tuwasiliane kwa 0755848391

    Baruapepe yangu ni GodiusRweyongeza1@gmail.com

    NB. Kama umependa makala hii, utapenda makala zangu za kipekee ninazotuma kwa njia ya barua pepe. WEKA JINA LAKO Na BARUA PEPE YAKO hapa chini ili niweze kukutumia taarifa zako.

  • JINSI YA KUTENGENEZA FEDHA MTANDAONI-2

    Umewahi kujiuliza ni kwa namna gani unaweza kutengeneza kipato kwa njia mtandao wa intaneti? Umewahi kujiuliza kitu kama hiki?

    Kuna kipindi nilikuwa nikisikia stori za watu kama Millard Ayo, kwamba hawa watu wanatengeneza fedha kwa njia ya mtandao. Sasa wali langu lilikuwa hivi hawa watu wanawezaje kutengeneza fedha kwa njia ya mtandao? Wanawezaje, hilo swali tu mpaka sasa hivi limenifungulia  dunia na kunifanya niweze kuona vitu vingi sana ambavyo kiuhalisia nisingeweza kuviona bila ya kujiuliza swali la alina hiyo.

    Najua kuna watu wengine wengi wanajiuliza swali la aina hii? Pengine na wewe utakuwa unajuliza swali la aina hii. Sasa swali langu kwako ni je, unawezaje kutengeneza fedha kwa njia ya mtandao? Unawezaje?

    Kabla sijajibu hili swali, nataka kwanza tujue kwenye maisha watu wanatengenezaje fedha? Kwa mfano, wewe unatengezaje fedha? Kama umeajiriwa, maana yake unaenda kazini unafanya kazi na mwisho wa mwezi unalipwa, unatoa thamani kwanza ndipo unakuja kulipwa.

    Kama unafanya biashara, maana yake unapaswa kuwa na bidhaa ambazo watu wanazihitaji, na unapaswa kuzileta bidhaa hizo kwa watu sahihi ili wakupe fedha. Bado tunarudi palepale kwamba unapaswa kutanguliza thamani kwanza.

    Kwa chochote kile unachofanya na kinakuingizia fedha halali, ni wazi kuwa utakuwa unafanya kitu kwanza, kisha kitu hicho ndipo unakuja kulipwa.

    Nimeona niliweke hili wazi, maana vijana wengi wanapofikiri kutengeneza fedha mtandaoni, basi kitu cha kwanza kabisa wanachofikiri ni kukaa bure bila kufanya kazi yoyote na kulipwa fedha ndefu. Hakuna kitu kama hicho.

    Mtandao wa intaneti haumaanishi kwamba ulale na utengeneze fedha ya bure bila kufanya kitu chochote. Badala yake mtandao wa intaneti, upo kurahisisha huduma unauyoitoa au kuifanya bishara yako iweze kuwafikia watu wengi zaidi kwa haraka na kwa gharama kidogo.

    Kiufupi kwenye ulimwengu wa leo kila mtu anapaswa kujitahidi kudandia teknolojia.

    Kwa biashara au kitu chochote kile ambacho unafanya unapaswa kukiweka mtandaoni, ili kiweze kuonekana ka watu wengi zaidi. kitu ambacho kitakusaidia wewe kukutana na wateja sahihi wa biashara yako.

    Kwa hiyo nifanyeje ili niweze kutengeneza fedha mtandaoni.

    ANZA KWA KUTOA THAMANI

    Ngoja nikwambie kitu, watu wanapenda fedha zao. Hakuna mtu ambaye ametafuta fedha kwa shida, atapenda kuona kwamba fedha alizozitafuta kwa shida zinapotea bila manufaa yoyote yale, badala yake kila mtu anapenda kuona kwamba fedha zake alizozitafuta kwa shida anazitumia vyema. Kwa hiyo, kitu cha kwanza kabisa unachopaswa kufahamu kama unataka kutengeneza fedha mtandaoni ni kwamba unapaswa kutoa thamani kwa watu.

    Wasaidie watu kupata wanachotaka

    USIINGIE MTANDAONI KWA KUFIKIRI KUTAPELI WATU

    Kama nilivyokwambia ni kwamba watu wanapenda fedha zao, hivyo usije ukaingia mtandaoni kwa kufikiri kwamba unaweza kuwatapeli watu fedha zao na kutokomea. Hizo ni fikra za kimasikini sana na hicho kitu ndicho kimefanya vijana wengi washindwe kuendelea  wala kufanya kitu chochote kikubwa maishani.

    Mara zote kuwa na fikra za namna gani ambavyo unaweza kuwasaidia watu kwanza. Watangulize watu mbele, maana watu wakinufaika na wewe ndio unakuwa unanufaika. Sijui unanielewa…

    BADILI KITU UNACHOFANYA NA KUWA CHA KITEKNOLOJIA

    Ukiangalia biashara kubwa za sasa hivi, hakuna kitu kikubwa ambacho wanafanya tofauti na kwamba biashara hizo nyingi zilikuwepo kwa miaka mingi sana iliyopita.

    Biahsara ya kuuza vitabu ni biashara ambayo imekuwepo kwa miaka mingi sana, ila sasa kijana mmoja alifikiria kwamba badala ya kuwa tunazunguka na kutoka huku kwenda kule tukitafuta vitabu kwenye maduka ya vitabu, kwa nini vitabu visiwe vinauzwa mtandaoni na watu wanaweza kuvinunua mtandaoni, hapo ndipo ulipokuja mtandao wa Amazon.

    Magari na usafiri wa taxi umekuwepo kwa siku nyingi sana. ila kilichofanyika kwenye ulimwengu wa leo ni kuweka vitu hivi kwenye mtandao wa intaneti. Kwa hiyo, unaweza kununua gari mtandaoni, unaweza kukodisha gari mtandaoni, unaweza kuwasiliana na boda akusafirishe kwa njia mtandao

    Nakwambia hivi vitu ili ujue kwamba, unapozungumziwa mtandao, usianze kufikiria kitu cha ajabu cha kufanya kwa njia ya mtandao wa intaneti. Badala yake uanze kutumia vitu hivyo vhiyo ulivyonavyo sasa hivi na kuviweka mtandaoni.

    Biashara hiyo hiyo uliyonayo sasa hivi, unapaswa kuiweka mtandaoni na kunufaika na uwepo wa mtandao

    Kipaji chako hichicho ulichonacho, unapaswa kukiweka mtandaoni na kunufaika na uwepo wa intaneti.

    Mgahawa wako huohuo, utengenezee ukurasa mtandaoni au hata tovuti, kisha sasa ndio uje kunufaika na uwepo wa mtandao.

    Rafiki yangu, kwa kitu chochote na kwa vyovyote vile, hakikisha kwamba,

    WEKA BIASHARA YAKO MTANDAONI

    Kwa biashara yako yoyote ile ambayo unafanya, hakikisha kwamba biashara hii unaiweka mtandaoni. Hata kama ni kipaji chako.

    Kuna njia nyingi za kuweka biashara yako mtandaoni kama kufungua tovuti au blog, kutengeneza ukurasa kwenye mitandao ya kijamii, kutengeneza

    Anza kuwaonesha watu bidhaa zako, kama utahitaji kuwafundisha watu kuhusu bidhaa zako wafundishe ili waweze kuzielewa kiundani

    Jibu maswali na maoni ya watu

    Kusanya mawasilino ya watu wanaohitaji bidhaa zao na wasiliane nao

    Wauzie bidhaa zako

    Hakikisha pia umeangalia video hii hapa chini ambayo ina mafunzo ziaidi kuhusu namna unavyoweza kutengeneza fedha mtandani.

    Umekuwa nami

    Godius Rweyongeza kutoka SONGAMBELE

    kama umependa makala hii, nakuhakikishia kuwa utapenda na mafunzo yetu mengine tunayotoa kwa njia ya barua pepe. Jiunge na mafunzo hayo kwa kujaza taarifa zako hapa chini,

  • MAAJABU YA KUAMKA ASUBUHI NA MAPEMA

    Benjamin Franklin ambaye anafahamika kama mwananchi wa kwanza Marekani alikwahi kuandika kwamba kulala mapema na kuamka asubuhi na mapema kunamfanya mtu awe na afya njema, tajiri na mwenye busara. Haya maneno aliyaandika zaidi ya miaka 200 iliyopita kwenye moja ya barua aliyokuwa anaandika kwa mwanae. Pengine Franklin angekuwa anarudi leo hii angeshangaa kwa jinsi maneno hayo machache yalivyopata umaarufu hasa kwenye ulimwengu maendeleo binafsi na hamasa. Maneno yake sasa yanatumika kama sehemu ya kuwahamasisha ili wajenge tabia ya kuamka mapema.

    Leo hii ukiingia kwenye mtandao wa Google, na kuandika neno early to bed, early to rise utapata matoke zaidi ya laki mbili na elfu sabini. Hii ndio kusema kwamba huu usemi ni miongoni mwa semi zinazotumika sana.

    Kipindi Benjamin Fraklin anasema hivyo hakukuwa na maendeleo makubwa kwenye teknolojia na sayansi kama ilivyo sasa hivi. Tafiti za kisayansi zimethibitisha kwa asilimia 100 kuwa maneno ya Benjamin Franklin ni ya ukweli na uhakika. Hivyo, kulala mapema na kuamka mapema kuna uwezo wa kukufanya uwe na afya njema, uwe tajiri na mwenye busara.

    Pengine unaweza kujiuliza nawezaje kuwa na afya njema kwa kulala na kuamka mapema tu? Unaweza kuendelea kujiuliza pia kuwa nawezaje kuwa na utajiri kwa sababu ya kulala na kuamka mapema? Na mwisho unaweza kujiuliza nawezaje kuwa na busara kwa kulala na kuamka mapema?

    Sasa hapo naomba uvute kiti chako ili nikuoneshe jinsi kulala mapema kulivyo na nguvu hizo zote na zaidi ya hapo.

    JINSI KULALA MAPEMA NA KUAMKA ASUBUHI NA MAPENDA KUNAVYOWEZA KUKUFANYA UWE NA AFYA NJEMA

    Imethibitishwa kuwa muda wa kulala kwa mwanadamu yeyote unapaswa kuwa kati ya saa sita mpaka nane. Suala la nani analala masaa sita au saba au nane linategemea na mtu mmoja mmoja. Kuna wale ambao mwili wao unawahitaji kulala saa saba, kuna wale ambao mwili wao unawaruhusu kulala saa nane. Mwili ukiunyima usingizi wa kutosha utakuwa unajichosha na itafikia hatua ambapo wewe mwenyewe utapoteza nguvu na uwezo wako wa kufanya kazi kwa weredi.

    Nimewahi kusikia hadithi ya mzee mmoja aliyekuwa bahiri na hakutaka kupanga chumba cha kulala. Hivyo, akawa anajibana na kulala kwenye jiko la kazini kwake. Kadiri siku zilizyokuwa zinasogea mzee huyo akawa kama anaumwa. Ila hospitali walipokuwa wanapima ugonjwa wakawa hawaoni chochote. Ndipo watu walimshauri apange chumba na apate muda wa kutosha wa kulala. Alipopanga chumba ndani ya wiki moja ya kupata usingizi unaoeleweka, afya yake ikawa imerudi kwenye hali ya kawaida.

    Kumbe usingizi ni muhimu sana kwa afya yako. Kitu kingine kuhusu kulala mapema ni kwamba, saa moja  unalola kabla ya saa sita usiku ni bora zaidi kuliko masaa matatu unayolala baada ya saa sita za usiku. Yaani,  mwili huwa una mpangilio wake wa kibaiolojia (biological rythm) ambapo katika masaa fulani kuna shughuli zainafanyika. Muda wa kuanzia saa nane mpaka saa 10 ni mida ambayo mwili unakuwa unajitengeneza, hivyo ni muda ambao mtu ananufaika kama ameshalala kwa muda na kuwa kwenye usingizi mzito. Hivyo, kulala mapema kunaufanya mwili kukamilisha zoezi hilo vizuri. Pia mtu anapowahi kulala anapata muda mzuri wa kuwa kwenye usingizi mzito (REM SLEEP) kuliko anayechelewa kulala. Usingizi mzito ndiyo wenye manufaa zaidi kwenye mwili

    Kama huamini, toa siku moja ulale saa nne usiku na uamka saa kumi na moja ambayo hayo yatakuwa ni masaa nane kamili. Kisha toa siku nyingine ulale saa saba usiku na uamke saa moja asubuhi. Utagundua kwamba siku uliyolala saa saba usiku na kuamka saa moja asubuhi ni siku ambayo unaamka umechoka huku ukiwa hauna nguvu ila siku uliyoamka saa kumi na moja ni siku ambayo unaamka mwili ukiwa umetulia kwa asilimia zote. Hii ndio maana napenda kukwambia kwamba kulala mapema na kuamka mapena kunamfanya mtu awe mwenye afya njema.

    JINSI KULALA MAPEMA NA KUAMKA MAPEMA KUNAVYOWEZA KUKUFANYA UWE TAJIRI

  • Kama unafikiri elimu Ni ghali, jaribu ujinga

    Siku Kama mbili zilizopita hivi, nilikuwa naongea na mama mmoja ambaye anamiliki salooon kubwa mkoani Mwanza. Katika kuongea aliniambia kitu ambacho nilikidaka vizuri. Alisema, Mimi nimetumia gharama kubwa kujifunza mambo ya saloon. Gharama ambayo nimewekeza Ni kubwa sana.

    Hiki kitu kilikumbusha Ile stori ya kwamba Kama unafikiri elimu Ni ghali jaribu ujinga.

    Na kitu ambacho kinaonekana kwa mtu yeyote ambaye amebobea. Hakuna MBOBEVU yeyote ambaye amebobea ndani ya siku moja. Wote wamewekeza gharama tena kwa muda mrefu, kabla ya kufikia hapo unapowaona sasa hivi.

    Katika ulimwengu wa leo wengi wanapenda matokeo ya haraka bila kulipa gharama. Unaweza kuyapata ila fahamu kuwa hayatakuwa ya kudumu.

    Kuna watu wengi ambao wanapenda wapate elimu nzuri bila kulipia, rafiki yangu mpendwa, elimu ni gharama. Tena siyo gharama kidogo, gharama kubwa.

    Wakati mwingine unakuta gharama unayilipia haiendani na thamani kubwa utakayoipata kwenye kitu husika. Huwa napenda kutokea mfano wa vitabu vyangu. Labda kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO au KUTOKA SIFURI MPAKA KILELENI. Hivi vitabu thamani yake ni kubwa kuliko unacholipia.

    Kama na wewe upo tayari kulipia kidogo, rusha elfu ishirini nikutumie vyote viwili. Kila kimoja ni elfu elfu kumi. Hizo Ni soft copy.

    Kila hardcocopy ni elfu 20.

  • Kiwango Cha Elimu Unachopaswa Kuwa nacho ili uandike kitabu

    Leo nimepokea ujumbe wa MTU anateniuliza, kiwango gani Cha Elimu unapaswa kuwa nacho ili uandike kitabu?

    Swali hili limenivutia sana kiasi kwamba nimeona niandike Makala na kuileta kwako.

    Kwenye ulimwengu wa uandishi kuna waandishi wa kila aina.

    Kuna waandishi wenye PHD,
    Kuna waandishi wenye shahada moja
    Kuna waandishi ambao wameishia darasa la saba n.k.

    Kwa hiyo, hakuna kiwango maalumu cha elimu ambacho MTU anatakiwa kuwa nacho.

    Kitu kikubwa kwenye uandishi ni mwandishi kuhakikisha ameijua mada anayoiandikia kiundani. Ameitafiti na kuifuatilia nje ndani.

    Hicho ndiyo kitu muhimu sana.

    Kiufupi ni kwamba kama unajua kusoma na kuandika Basi unapaswa kuandika.

  • Tuna saa 24 tu kwa siku

    Kila siku tuna saa 24 tu. Hakuna siku ambayo utakuwa na saa zaidi ya hizo, hivyo, unatakiwa kuutumia vizuri muda wako.

    Watu waliofanya makubwa, na watu wanaofanya vitu vya kawaida wote Wana saa 24.

    Sasa kwa Nini wewe usitumie muda wako vizuri?

  • Baadaye Siku Ya Leo Nitasikika Kwenye Temino Ya Clouds Fm

    Hello upande wa huko

    Nimeshaamka mapema siku ya leo kama ilivyo kawaida yangu. Na kama kawaida hapa nipo nyuma ya PC yangu nikiwa naandika kitu.

    Leo sina kitu kikubwa sana cha kukwambia labda taarifa fupi tu kuwa

    Baadaye siku ya leo Nitakuwa kwenye Temino ya Clouds Fm, kipindi kinachoendeshwa na Harris Kapiga, tukipiga stori kuanzia saa tisa mpaka saa 11.

    Nakala ngumu ya kitabu cha Kutoka Sifuri Mpaka Kileleni ni 20,000/- tu. na ninaweza kukutumia popote pale ulipo Afrika Mashariki.

    Nakala laini ya kitabu cha kutoka Kutoka Sifuri Mpaka Kileleni ni 10,000/- tu.

    Lipia leo hii nakala yako kwa

    Ni mimi rafiki yako,

    Godius Rweyongeza

    075584831

    Morogoro-Tz

  • Ajionavyo Mtu Ndivyo Alivyo

    Miongoni mwa usemi maarufu sana Ni ule usemi wa Napoleon Hill ambapo anasema chochote ambacho akili yako inaweza kushikilia na kuamini, kinaweza kufikika.

    Ndio maana unashauriwa kujenga picha ya kile unachotaka kufikia. Ikikaa kichwani mwako kwa muda mrefu, huku ukiwa unaifanyia kazi. Ujue kwamba itafikia hatua utaifikia

    Sasa wewe picha yako kubwa unayoiona ni ipi?

  • Vitu Vitano Vya Kukusaidia Kuendelea Kuwasha Moto Wa Kufanikisha Malengo Yako.

    Lengo lilikuwa ni kukufungua na kukuonesha kuwa mwaka huu mpya umeuanzaje au ndio kwanza unazubaa zubaa.

    Nadhani ambao huwa hawasahau ni wenye lengo la kuoa/kuolewa tu!!
    Maana wakikupa kadi hata kama ni Januari na wanafunga ndoa mwezi wa tisa.  Halafu ukajichanganya ukatoa ahadi, watakudai ahadi yako mpaka utoe senti ya mwisho…

    Naona unacheka! Umekumbuka ule ujumbe unaokukumbusha kutimiza ahadi yako nini?

    Sasa leo nataka nikuulize kwa mara nyingine, hivi bado kweli unakumbuka lengo lako la mwaka huu? Bado kweli una motisha ya kulifanyia kazi?
    Bado unajisukuma kulifanyia kazi?

    Kwa hiyo, hakikisha kila siku asubuhi unajikukumbusha malengo yako, mchana unajikumbusha malengo yako, jioni unajikumbusha malengo pia.

    Jikumbushe malengo yako pia unapokwama au unapokuwa katika hali  ya sintofahamu.

    Kila siku jipe jukumu la kufikiria mawazo 10 ambayo unaweza kuanza kufanyia kazi mara moja ili yakusaidie kufanikisha lengo lako.
    Ushawahi kufanya hili zoezi.
    Lianze leo hii.
    Anza sasa hivi ni mawazobyapi 10 ambayo unaweza kufanyia kazi leo hii yakakusaidia kusogea karibu na lengo lako?
    Je, ni kuanza kusoma kitabu fulani…
    Je, ni kupiga simu..
    Je, ni kuonana na MTU fulani..
    Je, ni kuachana na tabia fulani…

    Ni nini sasa…ebu andika chini.

    Bado huamini tu, najua kuamini kwa mwafrika ni mpaka aguse 😂😂. Haya, pata nakala yako sasa hivi ili ujionee mwenyewe.
    Nakala ngumu ni elfu 20. Na nakala laini ni elfu 10. Tuwasiliane Sasa hivi kwa 0755848391.

    Niache kwanza niendelee mbele maana safari bado…

    Toa ripoti kila Mara kwake ili aweze kuona maendeleo yako. Ukikwama mshirikishe ili akuoneahe namna unavyoweza kuendelea mbele zaidi…

    Iko hivi, lengo huwa halitimii kwa siku moja mwishoni mwa mwaka. Kila siku Ni siku yako kufanyia kazi lengo lako.

    Huwezi kuweka lengo na kusubiri lengo Hilo lije kutimia mwishoni mwa mwaka. Lengo lako linapaswa kufanyiwa kazi kila siku. Jumatatu mpaka jumapili, siku saba za wiki.

    Pambana kila Mara kuhakikisha unalifanyia kazi.

    Bado unataka niendelee au umechoka?
    Umechoka eti!
    Kama bado una motisha na nguvu zaidi kama Mimi, weka jina lako na email yako ili niendelee kukupa mafunzo yalioenda shule kama hili kupitia email. Fanya hivyo Sasa hivi hapa chini 👇🏿👇🏿

X