Home


  • Namba Zetu Za Malipo

    Namba za malipo ya vitabu:

    Namba za lipa

    TIGO PESA: 19016638 Jina ni SONGAMBELE CONSULTANTS

    M-PESA: 5564517 jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

    Namba za kawaida

    AIRTEL MONEY: 0684408755
    TIGO PESA: 0655 848 392
    M-PESA: 0745 848 395

    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    NB: Kama namba ya malipo anatumiwa mtu ambaye yuko nje ya nchi. Iandikwe Kwa kuanza na +255

    Kwa hiyo namba zinazotumwa nje ya nchi zitakuwa
    Airtel money: +255 684 408 755
    TIGO PESA: +255 655 848 392
    M-PESA: +255 745 848 395

    KOTE Jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Kama malipo yatakuwa yanafanyika kupitia benki.

    Yafanyie kupitia

    1. CRDB BANK: 0150770710200
    2. NMB BANK: 22110047274

    Kote jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

  • Wasiliana na Godius Rweyongeza Sasa

    Habari yafuatayo ni mawasiliano Unayoweza kutumia kumpata GODIUS RWEYONGEZA

    Simu: +255 (0) 684408755

    Whatsap: +255 (0) 755848391

    Email: songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu vyake wasiliana Moja kwa Moja na +255 (0) 684408755 (more…)

  • Kitu kinachowakwamisha wengi ukiwemo wewe

    Wengi wanakwama kwenye maisha, siyo kwa sababu nyingine bali kwa sababu tu ya UJUAJI. Yaani, wanajua, na hata hii makala wataipitia juu juu kwa sababu tu wanajua.

    Umewahi kuona watu wa aina hiyo ee. Ukianza kuongea naye jambo anakwambia na hilo nalijua.

    Mkianza kuongelea mada fulani, anajijua. Yaani, anajua kila kitu, 

    Kwenye mahusiano, yeye ndiye nyota.

    Mkiongelea michezo anajua kila kitu.

    Mkiongelea kuhusu siasa, anajua kila kitu.

    Mkiongelea usomaji wa vitabu, anajua kila kitabu,

    Mkiongelea wasanii, anajua kila kitu mpaka chakula waichokula leo…..

    UJUAJI, UJUAJI, UJUAJI.

    Muda mwingine wewe unapaswa kuwa msikivu. Wasikilieze wengine wanasemaje, utapata kujifunza mengi, na utapata mengi ya kufanyia kazi kwenye maisha kuliko ukiwa mjuaji zaidi.

    Wengi wanakwama maishani kwa sababu ya ujuaji mwingi. Mtu anasoma makalaunayoandika kwa juu kwa kusema kwamba ANAJUA.

    Au mwingine anasoma ila hafanyi kazi, kwa kusema kwamba anajua.

    Mwisho wa siku hapati matokeo. Anaendelea kuwa na maisha yaleyale.

    Labda nikuulize, ni kwa kiwango gani ujuaji umekukwamisha wewe kufika mbali maishani. TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

  • Mbinu za kutimiza malengo yako

    Habari ya leo rafiki yangu. Moja ya mada ambayo nimeiandikia sana kuliko mada nyingine, Ni mada ya malengo.
    Kuanzia namna ya kuweka malengo
    Namna ya kuyafanyia kazi malengo yako
    Namna ya kuyafanikisha na Mambo mengine yanayouhusiana na malengo

    Nimeandika makala nyingi zinazohusiana na hii mada.

    Leo hii kuna mtu kaniuliza mbinuza kutimiza malengo yake. Nimeona nimrudishe nyuma kwenye hizi makala za kitambo ili aweze kufaidika na uhondo uliopo humu; maana ya kale ni dhahabu.

    ujumbe kutoka kwa mmoja wa wasomaji wangu.

    Makala nyingine hizi hapa

    Ninaweza kuendelea zaidi ya hapa. Kwenye tovuti hii Kuna makala nyingi kuhusu malengo Kuliko unavyoweza kusoma kwa wiki moja au mwezi. Anza na hizi nilizokutumia.

    Hizi makala kwa umoja wake ni zaidi ya kitabu. Siriazi! Ebu zisome, Kisha utaniambia.

    mpaka wakati mwingine. Kama umependa Makala hizi, tafadhali usisite kujiunga na mfumo wetu wa kupata mafunzo zaidi hapa chini. Ebu weka jina lako na barua pepe yako, na sisi tutakusuprise kwa mafunzo zaidi.

  • Njia Rasmi Ya Mkato Itakayokupa Mafanikio Makubwa

    Chagua kitu kimoja, Kisha hakikisha kwamba unakijua kitu hicho nje ndani

    Kama ni biashara basi amua kuijua nje ndani.
    Kama ni kipaji chako basi zama na ubobee kwelikweli.

    Kama ni njia ya mkato, basi hii ndio njia pekee ya mkato unavyoweza kutumia kufikia kule unapotaka.

    Ukiwa mtu wa kugusa vitu kwa juu juu. Hutakaa ubobee na mara zote utakuwa unaona kama unachelewa kufanikiwa.

    Kumbe tatizo ni lako.

    Jipe miaka mitano mpaka kumi ya kuzama kwenye kufanya kitu ulichochagua bila kuacha.

    Kama umenielewa, jiunge na mfumo wetu wa kupokea mafunzo kwa barua pepe. Jiunge hapa chini

  • Uwezo mkubwa ulio ndani yako

    Leo nimeikumbuka sana siku nilipoenda kumtembelea rafiki  yangu. Kama ulivyo utaratibu wetu waafrika. Alinikaribisha kwa kuleta vinywaji pale mezani.

    Lilikuwa Jambo la furaha sana kukutana na hiyo rafiki yangu na stori zilianza bila kuchelewa, huku tukikumbushana baadhi ya mambo yaliyowahi kutokea siku za nyuma na hata kutaniana.

    Wakati stori zinazidi kukolea, glasi mojawapo pale mezani ilidondoka chini na kupasuka.

    Hili hambo lilinifanya nitafakari sana, ukizingatia zile glasi zilikuwa bado mpya kabisa.

    Nilibaki najisemea kimoyomoyo kwamba hii glasi imeharibika ikiwa bado na uwezo makubwa ndani yake ambao ulikuwa haujatumika.

    Hiki kitu kunatokea kwa watu wengi pia..
    Kuna watu wengi wenye uwezo mkubwa ila huwa hawautumii hata kidogo. Uwezo huu wa kipekee ungeweza kuinufaisha dunia…

    Pengine hata wewe uko kwenye hili kundi.

    Labda swali la kujiuliza hapa ni kwamba unautumia KWELI uwezo wako? Unautumia?

    Kama hautumii uwezo wako ipasavyo, unadhani kitu gani kinakuzuia wewe kuweza kufanya hivyo?

    Amua kuanzia leo hii kuwa nitakutumia uwezo wangu.
    Nitakutumia kipaji changu, nitatumia ubunifu wangu au chochote kile nilichonacho.

    Kitumie tafadhali, manufaa siyo kwa ajili yako tu. Bali yanakuwa kwa watu wote

    Mpaka hapo umenielewa?

    Kama umenielewa, weka email yako hapa chini, ili niendelee kukuelewesha zaidi kupitia jumbe zangu za kipekee nikazotuma kwa njia ya email kila siku.

    Jaza taarifa zako hapa👇🏿👇🏿

  • UAMINIFU NI MTAJI

    Mwaka 2018, nilisafiri kwenda Arusha na baadaye nikaenda Bukoba kwa wazee kusalimia. Ilikuwa ni safari ya zaidi ya mwezi…

    Nikiwa Arusha kuna jamaa alinitafuta. Alikuwa mshikaji ninayemfahamu. Au basi niseme tulikuwa tunasoma wote pale SUA.

    Aliniambia anataka nimkope fedha kama laki tano hivi, na angenirudishia hiyo fedha ndani ya wiki…
    Kuna fedha alikuwa anaisikilizia….

    Nilimwambia wiki moja siyo kubwa sana, subiri wiki ipite, utapata hiyo fedha unayoisikilizia na utaendelea na kazi zako.

    Alivyo niganda sana, nikamwambia nipo safarini (of course na mwenyewe alikuwa anajua hili) na nimewacha mtu kwenye biashara yangu. Fedha isingeweza kutolewa bila ya mimi kuwepo kuweka sahihi (kitu ambacho kilikuwa kweli pia).

    Akatulia…

    Sasa ngoja nifupishe stori. Mwaka mmoja baadaye nilikuja kupata taarifa kuwa kumbe kipindi kile anakopa kwangu, alikuwa akikopa kwa wengine pia.

    Kuna ambao tulikuwa wagumu na hatukutoa fedha zetu na wengine walimpa. Kitu ambacho siyo kibaya…

    Ila sasa huyu jamaa hakuwarudishia fedha zao….kitu ambacho ni kibaya.

    Sasa ninachotaka niseme leo ni nini?

    Kwanza, nataka niseme kwamba uaminifu ni mtaji. Ukiaminiwa aminika.

    Pili, nataka niseme kwamba, upende hela zako. Hakuna mtu mwingine anayeweza kupenda fedha zako kama wewe. Hakuna.

    Tatu, usipende kukopa kama hauedeshi microfinance ya kukopesha. Si unajua kukopa harusi….au umesahau..

    Nne, jiongezee kipato chako katika namna ambayo hutahitaji kukopa tena maishani mwako.

    Ni hayo tu.

    Mpaka wakati mwingine
    Mimi ni Godius Rweyongeza

    Hakikisha umejiunga na mfumo wetu wa kupata mafunzo zaidi kwa kujaza taarifa zako hapa chini.👇🏿👇🏿

  • Anza wewe kubadilika.

    Unazikumbuka kampeni za mwaka 2015!!! Unazikumbuka? Ni miongoni mwa kampeni zilizokuwa motomoto. Kila mgombea alikuwa na hoja zake kubwa ambazo alikuwa akitoa kwa wapiga kura ili waweze kumchagua.

    Kitu kikubwa kwenye kampeni hizi yakikuwa mabadiliko.

    Kila mgombea alikuwa akiongelea namna ambavyo ataleta mabadiliko endapo atapewa madaraka.
    Magufuri alikuwa anasema Tanzania ya viwanda.
    Lowassa alikuwa anasema Movement For Change.

    Wote walikuwa wanazungumzia mabadiliko Ila kwa namna tofauti.

    Na maelfu kwa maelefu walikuwa wanakuaanyika kuwasikiliza.

    Kila mtu alikuwa anapenda mabadiliko…..

    Kiufupi hakuna mtu asiyependa mabadiliko…

    Wote wanapenda mabadiliko. Au wewe hutaki?

    Lakini changamoto kubwa ni kwamba unataka mabadiliko pasipo kutaka kubadilika wewe.

    Wewe mwenyewe ndiwe unapaswa kuwa chachu ya mabadiliko kabla ya mtu mwingine yeyote yule.

    Kama kuna mabadiliko unataka, Anza wewe kubadilika.

    Ukisubiri mabadiliko yatokee juu, halafu wewe uyapokee, utasubiri sana.

    Kama unataka mabadiliko ya kiuchumi, Anza kubadili uchumi wako kwanza.

    Napenda Sana usemi wa Martin Luther King Jr. Anasema kila mtu akifangia mbele ya nyumba yake, dunia yote itakuwa Safi.

    Au kwa lugha rahisi sana kwamba kila mtu akifanikisha majukumu yake, mambo mengine yote yataenda sawa.

    Kuna hii nukuu ambayo niliwahi kuambiwa kuwa ni ya mwalimu Nyerere. Inasema kwamba play your part.

    Yaani, timiza wajibu wako. Ukitimiza wajibu wako na mwenzako akatimiza wajibu wake, Basi hakuna kitakachokwama.

    Sijui naeleweka….

    Kama umenielewa jiunge na mfumo wetu wa kupokea mafunzo zaidi, ili niendelee kukuelewesha zaidi kila siku kwa baruapepe. Jaza taarifa zako hapa chini👇🏿👇🏿

  • Kitabu Ambacho Utatamani Kuwa Ungekuwa Umekisoma Miaka Mitano Iliyopita

    Kuna mwaka nilikutanana mzee mmoja ambaye alikuwa anatamaani sana kuwekeza kwenye kilimo cha miti ila hakuweza.

    Kilichomkwamisha ilikuwa ni kukosa mwongozo sahihi.

    Labda niseme kwamba watu wengi wamekwama maishani mwao kwa kukosa mwongozo.

    Leo hii nataka nikupe kitabu kimoja tu ambacho wewe mwenyewe utashangaa kwa nini hukukipata miaka mitano iyopita

    Kipate hapa Ni bure, halafu kinapatikana kwa lugha adhimu ya Kiswahili

    Hiki hapa

    [birdsend form=16776]

  • Ilikuwaje Mpaka Nikaandika Vitabu 10 Na zaidi

    Ilikuwaje?

    Kwa wasionijua, basi wanafikiri kwamba Godius Rweyongeza ni jitu fulani hivi la miraba minne. Lenye miaka zaidi 60+ na mabusara kama yote…

    Hahaha!

    Miaka sina mingi kiviiile, labda mabusara nadhani nitakuwa nayo. Ila mama yangu alinifundisha nisiwe najisifia…

    Binafsi nilikuwa na ndoto ya kuandika kwa siku nyingi sana, tangu nasoma. Nakumbuka nikiwa kidato cha tatu au cha nne, niliongea na mama yangu nikamwambia kwamba nikihitimu kidato cha nne nitaandika riwaya (novel).

    Baada ya kuhitimu kidato cha nne nilirudi nyumbani na kukaa miezi kama nane hivi, ila sikuwahi kuandika ile novel ya ndoto zangu…

    Mama yangu alikuwa ananiuliza mara kwa mara, wewe si ulisema kwamba utaandika novel baada ya kuhitimu kidato cha nne… Nikawa namwambia ndio ila nitaandika..

    Siku zikazidi kusogea… mara likizo yangu ikaisha na nikatakiwa kuanza kidato cha tano..

    Hiyo nazungumzia ilikuwa ni mwaka 2013 /2014….

    Kama umezaliwa miaka ya 1960… 2014 siyo mbali hata kidogo.. maana una mastori ya kuanzia uhuru mpaka leo..

    Ila kama umezaliwa 2000, basi 2014 utaona ni mbali kiviile. Na hata ukipiga stori za kitambo unapiga za 2014 au 2015 wakati wazee wanajua mpaka ya vita vya Kagera… Wewe vita vya Kagera unavisoma tu vitabuni….

    [birdsend form=16776]

    Basi wacha niendelee…

    Baada ya kuingia kidato cha tano, nilisahau kidogo kuhusu ndoto yangu mpaka baada ya kuhitimu kidato cha sita.

    Sitaki nikuchose,

    Baada ya kuingia chuo, niliweka lengo kuwa mpaka nahitimu chuo napaswa kuwa nimeandika vitabu 11.

    Nakumbuka nilimshirikisha rafiki yangu mmoja hilo akakuna kichwa, akaniambia ungeweza kuandika hivyo vitabu,ila siyo kwa maisha ya chuo na hasa Chuo cha SUA.

    Nikamwambia hicho wacha nikifanyie kazi, nikifeli, nifeli nikiwa kazini..

    Nikifupisha stori zaidi ni kwamba, mpaka nahitimu chuo nilikuwa nimeandika vitabu 8. Sikuweza kuandika vitabu 11, ila walau nilikuwa nimeweza kuandika vitabu 8…

    Kitu gani kilinisaidia kuweza kuandika hivyo vitabu, na kuandika vitabu zaidi baada ya maisha ya chuo..

    Kitu kimoja kikubwa ni kwamba nilikuwa na lengo ambalo nilikuwa nalifanyia kazi.

    Usipokuwa na lengo au malengo ambayo unayafanyia kazi maishani mwako, ujue kabisa kwamba unaenda kukwama. Kikwazo kidogo tu, kitakukwamisha wewe na kukurudisha nyuma.

    Malengo yatakuonesha wapi uwekeze nguvu zako na vitu gani unapaswa kuachana navyo ili uweze kufika mbali.. ni uhakika kuwa mpaka sasa hivi utakuwa umeshaweka malengo ya kufanyia kazi maishani mwako.

    Kama mpaka leo hii hauna malengo, maana yake unaishi tu. Yaani, kunakucha na kuchwa huku wewe ukiwa unazunguka bila mwelekeo.

    Acha kila kitu unahofanya sasa hivi uweke malengo.

    Lakini pia hakikisha kwamba umesoma kitabu cha Kutoka Sifuri Mpaka Kileleni. Hiki kitabu kina mwongozo mzuri wa kukusaidia wewe kufikia malengo yako. Sura ya pili nzima ya kitabu hiki imeingia kiudani kueleza malengo na jinsi ambavyo yanafanya kazi. Kisome kitabu hiki, kitakusaidia sana.

    Kinapatikana kwa 20,000/- nakala ngumu. softcopt utaipata kwa 10,000.

    Wasiliana nami sasa kwa 0755848391 ili nikutumie kitabu.

    Umekuwa nami rafiki  yako wa ukweli

    Tuwasiliane kwa 0755848391

    Ji

  • NGUVU YA KUWEKA MALENGO

    Umewahi kujiuliza malengo yanaweza kuwa na nguvu gani kwenye maisha yako. Kama ulikuwa hujui ni kwamba malengo ni kama petroli kwenye moto.

    unajua ukiweka moto kwenye petroli ni kitu gani ambacho kinaenda kutokea…Moto utawaka zaidi, si ndio…

    malengo na yenyewe yako hivyohivyo. Ukiweka malengo, yatakusukuma kufanya makubwa zaidi

    karibu sana ujipatie ebook ya kipekee ya nguvu ya malengo. Itakusaidia wewe kujua namna nzuri na ya kipekee ya kuweka malengo, namna ya kuyafanyia kazi malengo yako mpaka yakatimia, lakini pia utapata mwongozo wa kukusaidia wewe kuendelea kuyafanyia kazi malengo yako. Je, upo tayari?

    Karibu

  • Mipango yangu ya miaka 100 ijayo

    Nilipokuwa mdogo, nilikuwa napenda sana kusikiliza redio. Kila siku SAA kumi na mbili asubuhi ilikuwa lazima  nisikilize DW habari za ulimwengu. Mchana na jioni ilikuwa hivyo hivyo, yaani, ilikuwa kama dozi .

    Siku moja wakati nasikiliza habari, walitangaza kwamba kufikia mwaka 2050 kuna viumbe watakuwa wamepotea na kutoweka kwenye uso wa dunia.

    Watu niliokuwa nao walianza kulalamika. Kila mtu alishangaa kuona ni kwa nini wanazungumzia mambo ya mwaka 2050 sasa. Wakati bado kuna muda mwingi sana. Rafiki yangu mmoja alithubutu kusema ni uongo. Huku mwingine akisema wazungu wanapoteza sana muda.

    Hali hii inaweza kukupa picha ni kwa jinsi gani watu hawataki kuangalia mbeleni. Ni kwa jinsi gani watu hawana mipango ya mbeleni.

    Labda nikuulize wewe unataka uwe umefikia Nini mpaka mwaka 2050?

    Najua..

    Najua..

    Najua utaniambia umri wangu umeenda kwa hiyo 2050 ni mbali. Sawa, na mimi nakubaliana na wewe.

    Ila vipi una mpango wa  hata wa miaka 10 au mitano? Au na penyewe ni mbali?

    Andika Malengo yako ya miaka 1/2/3/5/10/25.

    Watu wengi wanaamini katika msemo unaosema leo ni leo asemaye kesho ni mwongo. Hali hii imewafanya watu wengi kusitasita kuweka mipango yao ya muda mrefu. Hivyo kuamini kwamba kila wanachopata sasa ni kwa ajili ya sasa na kesho itajipa yenyewe. Hali hii itakunyima motisha ya kusonga mbele na kufanya mambo makubwa.

    Mara zote na siku zote unapaswa kuwa na mpango na ndoto za muda mrefu.

    Unapaswa kupanga kama vile utaishi milele na kufanyia mipango yako leo kama vile utakufa kesho.

    Siku siyo nyingi nilikuwa nasoma wasifu wa Jack Ma. Unaitwa Alibaba: The House That Jack Ma Built. 

    Ndani yake mwandishi anasema kwamba wakati Jack Ma anaanzisha kampuni ya ALIBABA alikuwa na mpango wa kufanya kampuni hiyo idumu kwa miaka 102. 

    Miaka 102 ni mingi, wachache sana wanaishi hiyo miaka.

    Ila jamaa alianzisha kampuni yake na huo mpango.

    Kampuni ya Alibaba ilianzishwa mwaka 1999 na Jack Ma alikuwa tayari na miaka 36. Maana yake tunapozungumzia miaka 102 baada ya hiyo kampuni kuanzishwa, tunaiongelea miaka ya 2101!!!!!!

    Sidhani kama Jack Ma atakuwa bado anaishi, Ila huyu jamaa ana maono makubwa ya kufikiri mpaka huko atakapokuwa ameshaaga dunia ..

    Hii ndio nguvu ya maono, MTU mwenye maono ya mpaka mwaka 2101. Siyo sawa na mtu mwenye lengo la kulala leo na kuamka kesho akaonane na mchepuko wake! 

    Na wewe kuanzia Leo weka maono ya muda mrefu. Unaweza usiwe hai hiyo miaka. Lakini maono yako hayatakufa. Ndio maana tunapaswa kufanya vitu kwa kuwafirikia hata wanetu…ili waweze kuwa waendelezaji wa vitu tulivyoanzisha. Tunaoneahe runavyofanya ili na waweze kuwa waendelezaji wa kile tunachofanya…

    NB. Kama bado hujapata nakala ya kitabu cha KUTOKA SIFURI MPAKA KILELENI, fanya hivyo leo. Nakala ngumu ni 20,000

    Nakala laini ni 10,000 tu.

X