-
VITU viwili usivyovijua kuhusu kitabu Cha jinsi ya kufikia ndoto ZAKO
Unaendeleaje rafiki yangu, bila shaka kila kitu kinaenda vyema kabisa. Leo hii nina habari njema kwako..
Habari njema kuhusu kitabu cha jinsi ya kufikia ndoto ZAKO.
Kitabu hiki ambacho kinaenda kuzinduliwa tarehe 20 Mei.1. Usichokijua kuhusu hiki kitabu ni kwamba watu wanaendelea kuweka oda ya kitabu hiki.
Ukiweka oda unapata kitabu hiki Cha kipekee kwa bei ya punguzo. Yaani, badala ya wewe kununua hiki kitabu kwa 20,000/- unakipata kwa 15,000/- tu. Kitabu hiki utatumiwa popote pale ulipo Duniani.2. Usichokijua kuhusu kitabu Cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO ni kwamba kitabu hiki kinapatikana kwa ;
Mfumo wa nakala ngumu (hardcocopy) ambayo gharama yake ni 20,000/- ila ukiweka oda unakipata kwa 15,000/-
Kuna na audiobook yake pia. Ambaye utaipata kwa 15,000/- Ila ukiweka oda utaipata kwa 10,000/-
Unaweza kusikiliza sample ya audiobook hapa
Hivi eti kwa mfano unashindwaje kupata nakala yako.
Ebu weka Oda yako sasa hivi. Andika jina lako hapa chini
Mfano: Godius Rweyongeza 0755848391 (Morogoro mjini-Morogoro)
Weka oda yako leo, upate nakala ya kitabu kwa bei ya punguzo
-
Zawadi hii utaipata endapo utaweka Oda ya kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO tu.

Habari ya upande wa huko. Bila shaka unaendelea vizuri kabisa. Leo hii nina zawadi ila sasa hii zawadi siyo ya kila mtu. Hii zawadi ni kwa ajili watu wachache ambao wanataka kupiga hatua na kufika mbali.
watu wenye ndoto kubwa
watu ambao wanazifanyia kazi ndoto zao kwa KUTUMIA mwongozo sahihiKiufupi hii zawadi itawaendea wale wote watakaoweka oda ya kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO. Kitabu hiki Cha kipekee kitazinduliwa tarehe 20 Mei. Na kila mtu aliyeweka oda siku hiyo atatumiwa kitabu popote pale alipo.
Kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO kinagharimu 20,000/-
Ila kwa wale ambao wataweka oda watakipata kwa gharama ya 15,000/- tu.Oda inawekwa kwa kutuma ujumbe wenye
Jina lako.
Namba yako ya simu na
Mahali ulipoMfano, GODIUS RWEYONGEZA 0755848391 (Morogoro mjini-Morogoro).
Nitumie huu ujumbe kwa SMS/WhatsApp 0755848391
Sasa acha tuongelee zawadi yangu kwako basi.
Zawadi hii ni ya ebook inayoitwa MAAJABU YA MTANDAO WA INTANETI.
Ndani ya hii ebook utajifunzaUmuhimu wa smartphone kwa mfanya biashara na mtu mwenye ndoto kubwa.
Namna ya kuutumia mtandao wa intaneti kwa manufaa ili kuifanikisha ndoto yako
Jinsi ya kujiweka mtandaoni mapema kabla ya wateja wako
Mtandao wa intaneti kama sehemu ya kukuingizia kipato
Na mambo mengine mengi…
Nataka niitoe hii ebook kwa watu wenye ndoto kubwa kwa sababu,
Siku hizi mambo yamebadilika. Mtandao umekuwa na nguvu kubwa. Sasa sitaki wewe na ndoto yako kubwa uachwe na haya mabadiliko.
Ukipata hii ebook maana yake utaweza kufanyia kazi ndoto yako vizuri, tena ukiunganisha na NGUVU YA MTANDAO WA INTANETI! Mambo yatakuwa ni 🔥🔥! Tutakutana kwenye hii ebook.
Haya yote utayapata tarehe 20 Mei 2022.Cha kufanya. Weka oda yako leo.
Kitabu kama kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO kinagharimu shilingi 20,000/- Ila ukiweka oda utakipata kwa 15,000/- za Kitanzania tu. Uko tayari!Unaweza kujiunga na kundi letu la watu walioweka oda tu.
Kujiunga bonyeza hapa -
Nitakuwa Live Kupitia FADECO FM Leo Saa Tano Asubuhi
Habari ya upande wa huko
Godius Rweyongeza hapa kwa mara nyingine. Leo kuanzia saa tano asubuhi mpaka saa sita mchana nitakuwa live kupitia FADECO FM.
Nitazungumzia kuhusu mchango wa smartphone kwa mfanyabiashara na jinsi unavyoweza kutengeneza fedha mtandaoni.
Unaweza kufuatilia kipindi kupitia 100.8 FM au mtandaoni kwa KUBONYEZA HAPA
Godius Rweyongeza kutoka SONGAMBELE
0755848391
Morogoro-Tz -
Kundi Maalumu Kwa Ajili Ya Uzinduzi Wa Kitabu Cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO
Hello, nimetengeneza kundi maalumu kwa ajili ya uzinduzi wa kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO toleo la pili.Kama umeweka oda ya kitabu ingia kwenye hili kundi ili uendelee kupata updates kuhusiana na kitabu Pia kama hujaweka oda ingia kisha weka Oda.Twambie jina lako. Namba yako ya simu naUko wapi Mfano:Godius Rweyongeza 0755848391 (Morogoro mjini; Morogoro)Kitabu kitazinduliwa tarehe 20 Mei, 2022. Na nakala zitaanzia kusambazwa siku hiyohiyo kwenda maeneo mbalimbali hapa nchini.Kwa wakazi wa Dar,Morogoro na Pwani utafikishiwa nakala yako ofisini au nyumbani kwako.Bei ya kitabu ni 20,000/- Ila ukiweka oda utakipata kwa 15,000/- tu.Kuna bonus zaidi kwa watakaoweka oda tu.Kujua kuhusu hizi bonasi, jiunge kwenye kundi letu hili hapa ili uendelee kupata updates.
-
Nini mchango wa smartphone kwa mfanyabiashara?
Binafsi napenda sana maswali. Napenda maswali kwa sababu maswali ndiyo yanatufanya tukue, maswali ndiyo yameifanya dunia iwe kama ilivyo leo hii. Hii ni kutokana na dhana ya wanasayansi kutaka kujua zaidi. Watu wanajiuliza hivi kitu fulani kikifanyika kwa namna fuani itakuwaje? Hivi kweli ugonjwa fulani hauwezi kupatiwa tiba? Hivi hatuwezi kufanya utaratibu wa kwenda kwenye anga na kuishi? Hayo ndiyo maswali ndio huwa yanaanzisha tafiti na mwisho wa siku watu wanakuja na majibu.Napenda sana maswali kwa sababu maswali yanakufanya unakua. Maswali yanakufanya unajua yale uliyokuwa hujui, maswali yanakufanya mjinga kwa dakika moja ila mwisho wa siku yanakuacha ukiwa mwelevu maisha yako yote.
Na hii dhana ya kuuliza maswali kwa sisi binadamu tunazaliwa nayo. Tukiwa watoto tulikuwa tunauliza maswali sana aisee…
Leo ungeweza kuuliza maswali kuhusu Mungu? Kesho yake ukauliza maswali kuhusu kitu au mtu fulani uliyemwona na keshokutwa ungeweza kuuliza hata jinsi watoto wanavyopatikana! 😂😂, ila utoto jamani…
Sasa leo hii kuna swali nimeulizwa. Swali linasema kwamba nini mchango wa smartphone kwa mjasiriamali? Eti, nini mchango wa smartphone au simu janja kwa mjasiriamali? Kuna mchango wowote kweli kama upo?

Ili tujue umuhimu wa smartphone kwa mfanyabiashara, tunapaswa kuangalia takwimu kwanza.
Gazeti la Jamhuri la Jumanne Disemba 17-23, 2019 liliandika hivi
Ripoti ya mawasiliano ya juni 2019 ya TCRA inaonesha kuwa idadi ya watumiaji wa intaneti hapa nchini imefikia 23,142,960 na kati ya hao 22,281,727 wanatumia mtandao huo kupitia simu za mkononi.
Nayo kampuni ya GlobalData Technology ya Uingereza imesema ifikapo 2024, idadi ya simujanja itafikia milioni 30 hali inayotarajiwa kuongeza matumizi ya data mara dufu kutokana sababu zifuatazo:
- Uwepo wa teknlojia husika ya (3G,4G&4G+).
- Uwepo wa simu za mkononi zinazowezesha matumizi ya intaneti.
- Uelewa wa kidigitali. Watu wanazidi kuelimika katika matumizi ya inteneti.
- Uwepo wa majukwaa rafiki kama mitandao ya kijamii (facebook, twitter n,k).
- Kampuni za simu kutoa vifurushi vinavyowezesha wateja kutumia intaneti kwa urahisi zaidi.
- Maudhui sahihi.
Hizo ndizo takwimu rafiki yangu. Kiufupi ni kuwa watu zaidi milioni 23 sasa hivi unaposoma hapa wanatumia mtandao wa intaneti na idadi inazidi kuongezeka kila siku. Hizi takwimu hizi hazimhusishi rafiki yangu ambaye amenunua simujanja jana kwa mara ya kwanza! Halafu ujue nipo siriazi, kuna rafiki yangu kanunua simu janja jana na jana hiyohiyo tukaongea kwa whatsap video, chezea simu janja wewe!
Siku hizi mtu anaweka akiba maalumu kwa ajili ya kununua simujanja. Kama ambavyo mimi na wewe tunaweka akiba ya kununua kiwanja! Pengine wewe mwenyewe leo hii upo unaweka akiba kwa ajili ya kununua simu janja nyingine….
Kitu kikubwa kuhusu simujanja au smartphone ni kwamba, siku hizi huwezi kutengenisha maisha yetu ya kila siku na hizi simu. Sisi ni simu na simu ni sisi. Kila tunapoenda tunazo. Ni kama vile simu zimekuwa sehemu ya pili ya maisha. Simu zimekuwa kama nguo!
Kuna watu wanapenda simu zao kuliko hata wenza wao! Mungu anawaona

Ukiingia kwenye daladala unakuta mtu anatumia simu, unaweza kupanda kituo kimoja na kushuka kituo kingine, mtu asijue kama ulikuwa umekaa pembeni yake. Watu wanasahau mpaka kushuka kwenye vituo vyao kisa wanatumia smartphone zao. Kuna mpaka mtu anakwambia kwamba maisha bila ya smartphone ni magumu sana. kwani unadhani uongo? Watu wa aina hiyo unao hapo mtaani, mtu ambaye akipotelewa simu yake anaomboleza mpaka kila mtu anajua…mtu ambaye akikosa kifurushi cha kuingia mtandaoni siku hiyo anakonda ghafla.
Hayo ndiyo maisha ya sasa.
Imenibidi nieleze hayo yote kwanza, ili mwisho wa siku tuweze kujua umuhimu wa simujanja au smatphone kwenye maisha ya sasa hivi, na kwa mfanyabiashara.
Kama mtu anashinda na simu yake kwa kutwa nzima, si fursa hiyo? Na siyo tu kwamba anashinda nayo, bali tafiti zinaonesha kwamba mtu wa kawaida anaiangalia simu yake mara 2617 kwa siku. Wakati wale watumiaji konki wanagusa simu zao mara 5427.
Ona,
- Mtu akiamka asubuhi kitu cha kwanza anagusa simu yake kabla hata ya sala.
- Chakula siku hizi tunaagiza kwa simu
- Pesa tunatuma kwa simu
- Wapendwa wetu tunawasiliana nao kwa simu
- Usafiri siku hizi tunauita kwa simu. Hatuna tena muda wa kujipanga eti unasubiri boda au teksi.
- Mpaka biashara zenyewe zinasimwamiwa kwa simu. Kama wewe hujaanza umechelewa.
SOMA ZAIDI: JINSI YA KUTENGENEZA FEDHA MTANDAONI-2
Kwenye biashara lengo la biashara yoyote ile ni kupata wateja. Au kwa lugha nyingine, watu wa kununua bidhaa kutoka kwenye biashara husika na hivyo kuleta faida. Sasa kama watu unaowahitaji wewe kwenye biashara yako, wanatumia simu muda wote unafanyaje? Hapo sasa ndipo unapaswa kufunguka..
Zama za sasa hivi zimebadilika sana…
Kwa hiyo, mfanyabiashara kwenye ulimwengu wa leo, huna budi kuhakikisha kwamba biashara yako, unaiweka kwenye mazingira ya kuonekana kwa watu hawa wanaoshinda wanatumia simujanja zao.
Hii ndio kusema kwamba kama watu wanashinda facebook, basi wewe biashara yako inapaswa kuwepo facebook.
Kama watu wanashinda instagram wewe pia biashara yako inapaswa kuwepo huko.
Tengeneza kurasa za biashara yako kwenye mitandao yyote ya kijamii. MIMI PIA NINAZO KURASA kwenye mtandao wa Facebook, instagram na google my business. Unaweza kuzitembelea na kuzipenda pia. Itakuwa fureshi sana….
Mfanyabishara yeyote makini, anapaswa kuona fursa kubwa kwenye matumizi ya simu janja na hivyo atumie hii fursa.
Kwa hiyo kama wewe ni mfanyabiashara hakikisha kwamba
BIASHARA YAKO UMEIWEKA MTANDAONI.
Si unajua ee, siku hizi mtu akiwa na tatizo, sehemu ya kwanza kabisa anapokimbilia ni mtandaoni. Anaperuzi ili aweze kupata suluhisho lake. Hii ndiyo kusema kwamba, kama leo hii unamiliki biashara na hujaiweka mtandaoni, kuna watu wanakosa huduma yako kwa sababu tu hujaweka biashara yako mtandaoni. Maana yake ni kwamba, kama wewe biashara yako inahusiana na sabuni na mtu akiwa na shida akaingia mtandaoni na kutafuta kitu kinachoendana na sabuni. Atakikosa kwa sababu, wewe hujaingia mtandaoni kumwekea kitu cha aina hiyo, na kwa jinsi hii utakuwa umepishana na gari la mshahara…
Siku hizi biashara zinafanyika mtandaoni aisee….
Wateja wako wanapaswa kukuta wewe mtandaoni.
Yaani, mteja akiwa ana tatizo, akitafuta kitu, moja kwa moja google imlete kwako. kama wewe unafuga mbuzi au kuku, ikitokea tu mtu akatafuta kitu kinachohusiana na mbuzi au kuku, basi moja kwa moja aletwe kwako…
SOMA ZAIDI: Je, Viwanja Vya Zama Hizi Vimehamia Mtandaoni
SASA WANAKUKUTAJE MTANDAONI
Ndio kama ambavyo nimeshaeleza hapo mwanzoni. Tengeneza kurasa za mitandao ya kijamii. Lakini kikubwa zaidi, na hapa nasema kikubwa zaidi ni wewe kuhakikisha kwamba unakuwa na tovuti. Kwa mfanyabiashara yeyote yule ambaye yuko makini na angependa kunufaika na biashara yake mtandaoni, basi hakikisha una tovuti au blogu ya biasahra yako…
Mitandao ya kijamii kuna wakati huwa inapoteza baadhi ya vitu ambavyo umeweka. Ila tovuti, haipotezi kitu labda wewe uamue kukiondoa…
Na ubora ni kwamba tovuti unakuwa unaimiliki wewe mwenyewe kama ambavyo Zuckeberg anamiliki facebook. Na wewe tovuti yako, ni ya kwako tu na wala hakuna mtu wa kukuingilia kwenye hili eneo..
Kwa hiyo basi, nashauri sana sana, utengeneze tovuti au blogu. Ukihitaji msaada kwenye hili, nicheki kwa 0755848391 ila kaa ukijua kwamba kuna gharama kidogo utapaswa kutoa, japo hizo gharama zisikuogopeshe kama kweli upo siriazi na biashara yako, maana zinaenda kujilipa ndani ya muda mfupi tu. Utapoteza kidogo sasa hivi, kwa ajili ya faida kubwa hapo baadaye.
Kuna mengi sana ya kusema kuhusu simu na mtandao wa intaneti ila kwa leo, nataka niishie hapa tu. Mjadala uendelee kwenye eneo la kutoa maoni hapa chini…
By the way, kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO toleo la pili kitazinduliwa tarehe 20 mei, 2022. Hakikisha kwamba unapata nakala yako kwa bei ya punguzo leo hii. Nakala moja ya kitabu inagharimu 20,000/- ila wewe ukiweka oda utaipata kwa 15,000/- tu.
Na sasa leo hii napenda nikwambie kwamba, kama utaweka oda. Utapata pia ebook ya bure ya Maajabu ya mtandao wa intaneti. Ambapo ndani yake nimeeleza kwa kina
- Umuhimu wa smartphone kwa mfanya biasahra
- Namna ya kuutumia mtandao wa intaneti kwa manufaa
- Jinsi ya kujiweka mtandaoni mapema kabla ya wateja wako
- Mtandao wa intaneti kama sehemu ya kukuingizia kipato
- Na mambo mengine mengi…
Weka oda yako leo hii kwa kuwasiliana nami kwa 0755848391. Au nitumie ujumbe tu wenye jina lako, namba yako ya simu na mahali unapoishi
Mfano
1.Godius Rweyongeza 0755848391 (Morogoro mjini, Morogoro).
2.
3.
4.
5.
Na wewe nitumie jina lako sasa.
-
Jinsi Ya Kuweka Oda ya Kitabu Cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO
Hello! Bila shaka unaendelea vyema. Kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO (hardccopy) kitatoka rasmi tarehe 20.5.2022
Hili ni toleo la pili la kitabu hiki cha kipekee.
Karibu uwe miongoni mwa watu ambao watapata nakala ya kitabu hiki.
Kwa wakazi wa mikoa ya Dar, Pwani na Morogoro mtafikishiwa nakala popote pale mlipo.
Kama upo nje ya hiyo mikoa, utatumiwa nakala mpaka ikufikie.
Nakala moja inauzwa kwa gharama ya 20,000/- Ila ukiweka oda leo hii utakipata kwa 15,000/- tu.
Na hii ni kwa wale tu watakaoweka oda! Baada ya hapo hutaweza kupata kitabu hiki kwa Bei ya 15,000/-.
Save 5,000/- kwa kuweka Oda ya kitabu.
Sisi tutakufikishia kitabu tarehe 20 au siku moja baada ya kitabu kuzinduliwa.
Cha kufanya nitumie ujumbe wenye jina lako na mahali ulipo…
Tarehe 20. Tutakufikishia hiki kitabu.- Godius Rweyongeza 0755848391 (Morogoro Mjini-Morogoro)
2.
- 4.
5. Soma hiki kitabu, utaona kwa nini 2022 haitakuwa sawa na 2022!
-
Usiweke bajeti kwenye AKILI yako.
Kama umeanza kufanya hivyo, basi kuanzia leo iondoe bajeti hiyo maana ni kikwazo kikubwa sana. Akili yako itumie kubuni vitu vipya, itumie kufikiria mbinu mpya za kutatua matatizo, itumie kuongeza MAUZO kwenye biashara.
Tafiti nyingi zimefanyika na tafiti hizi mara zote zimekuja na jibu moja kuwa watu wengi wanatumia chini asilimia kumi ya uwezo wao. Kwa hiyo, ukikutana na mtu ambaye ameweza kufanya vitu ambavyo unaviona kwamba ni vikubwa, jua kwamba hajatumia hata asilimia 15 ya uwezo wake, bado anachezea chini ya asilimia kumi. Sasa ebu fikiria na wewe ukiweza kutumia hata asilimia 10 tu ya uwezo au akili yako. Unadhani utafika wapi?
Kama hawa wanasayansi wote ambao wamefanya makubwa au hawa wana wagunduzi, wote wametumia chini ya asilimia kumi, na wewe ukiongeza uwezo wako kidogo si unaweza hata kuwafikia?
James William aliwahi kunukuliwa akisema kwamba, kulinganisha na vile tunavyopaswa kuwa, watu bado wamelala.
Yaani, bado uko usingizini, hujaweza kutumia uwezo wako kadiri inavyotakiwa.
Ubora wa vitu hivi ni kwamba hakuna hata kimoja ambacho unaweza kusema kwamba nimekitumia mpaka kimeisha. Kipaji hakitumiki mpaka kikaisha, ujuzi wako hautumiki mpaka ukaisha, kadiri unavyotumia kipaji chako, ndivyo ambavyo kinazidi kuwa bora zaidi, kadiri unavyotumia akili yako, ndivyo ambavyo akili yako inazidi kuimarika zaidi. Anza leo hii kuvitumia.
Sasa unawezaje kutumia uwezo wako, akili au kipaji chako kwa viwango vikubwa?
Baada ya kusoma hapa nina hakika utaanza kusema kwamba ninataka nifike mbali, na ninataka nifanye makubwa. na ni kweli kabisa.
HATA HIVYO, unaweza kujikuta kwamba unatumia maarifa haya vibaya na mwisho wa siku unaishia kuangukia pua. Hapa nataka nikupe mwongozo sahihi ili usije ukaangukia pua.
Mara nyingi mwanzoni mwa mwaka watu huwa wanaweka malengo makubwa ya kufanya vitu vikubwa. Unakuta mtu kaweka malengo ya kukimbia, pengine baada ya kusikia habari kuwa kukimbia ni kitu muhimu kwa afya. Lakini siku ya kwanza tu mtu anakimbia kilomita tano, kesho yake anaamka akiwa hana hamu tena ya kukimbia, amechoka.
Sasa unachotakiwa kwenye kufanyia kazi kipaji na uwezo wako wa kiakili ni wewe kuhakikisha kwamba, unajiwekea lengo la kukua walau kwa asilimia moja kila kukicha. Yaani, kwamba leo hii uweze kuutumia uwezo wako kwa viwango vikubwa kidogo kulinganisha na vile ulivyoutumia jana. Kesho uutumie uwezo wako kwa asilimia moja zaidi ya vile ulivyoutumia leo. Kila siku walau utumie uwezo wako kwa asilimia moja juu zaidi ya vile ilivyokuwa jana.
Wajapani hiki kitu wanakiita kaizen au constant improvement. Yaani, kwamba kila mara na kila siku unahakikisha kwamba unajiongeza na kukua zaidi ya ilivyokuwa hapo jana.
Mfano, tuseme kwamba una lengo la kunoa kipaji chako cha uandishi. Unaanza kidogo kidgo na hakuna kurudi nyuma kila siku.
Leo unaamua kuanza kuandika maneno 10 tu ya ujumbe mfupi. Kesho unaongeza, maneno unaandika maneno kumi na tano.
Kesho kutwa maneno kumi na saba. Ila unakuwa haurudi nyuma. Unaendelea kukifanyia kazi kipaji chako bila ya kuchoka na bila ya kurudi nyuma.
Mimi nakuamini sana, nategemea kwamba baada ya hapa unaenda kutumia uwezo wako bila ya kurudi nyuma.
-
Kuna Nini Kwenye Toleo La Pili La Kitabu Cha Jinsi Ya Kufikia Ndoto Zako

Jana nilitangaza kuwa tarehe 20 Mei toleo la pili la kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO litakuwa tayari. Nakala zitafikishwa mpaka nyumbani kwako au ofisini kwako kwa wakazi mikoa ya Dar, Pwani na Morogoro. Hata hivyo, kama upo nje ya hii, mikoa, nakala zitatumwa na utazipokea vizuri tu. Nakala moja ni 20,000/- . hata hivyo, ukiweka oda ya kitabu sasa hivi utaweza kukipata kitabu kwa elfu kumi na tano. Hivyo, utaokoa elfu tano nzima.
Sasa unaweza kuwa unajiuliza kuwa kuna nini kwenye toleo hili la pili na kwa nini napaswa kusoma toleo la pili? Kwa nini eti?
Hapa sasa naenda kukupitisha kwenye toleo la pili kwa ufupi.
Nakumbuka mara tu baada ya kutoa toleo la kwanza, kitabu kilianza kusomwa na watu mbalimbali. Na muda huohuo nilianza kupokea mrejesho kuhusiana na kitabu kilivyokuwa kikisaidia watu. Asilimia kubwa ya watu waliosoma kitabu hiki walinipa mrejesho (sio wote).
Hivyo, nilichofanya kwenye toleo hili la pili, baada ya kuwasiliana na wale waliotoa shuhuda zao kuhusu kitabu, nimehusisha baadhi ya hizo shuhuda. Sijaweka nyingi sana, ila kuna shuhuda za kweli chache kutoka kwa wasomaji wangu wa toleo la kwanza.
Pili, kuna ongezeko la sura mbili mpya ambazo hazikuwepo mwanzoni. Ikumbukwe kuwa mwanzoni kitabu kilikuwa na sehemu tatu. Huku kikiwa na sura kumi na sita. Kwenye toleo hili jipya, kuna ongezeko la sura mbili mpya. kitu ambacho kinafanya kitabu sasa kiwe na sura 18. Kitabu kimeendelea kuwa na sehemu tatu, ila zenye sura 18.
Tatu, kuna marekebisho na vitu vichache Ila vyenye nguvu vimeongezwa karibia kwenye kila sura ya zamani. Na hivyo kufanya sura zote ziwe updated zaidi kuendana matakwa ya sasa.
Hili ndilo toleo la pili la kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO. Na sasa unaweza kuweka oda yako. Badala ya elfu ishirini (20,000/-) unaenda kupata kitabu hiki kwa shilingi 15,000
Weka oda yako sasa hivi kwa kuandika jina lako hapa. chini au kutuma ujumbe wenye jina lako sehemu ulipo kupitia namba hii 0755848391
Andika jina lako hapa chini (au nitumie ujumbe kwa 0755848391)
Sitaki ukose nakala hii ya kipekee sana. hivyo, jiweke kwenye orodha ya wale watakaopokea nakala hii ya kipekee kwa elfu 15,000/- tu badala ya 20,000/-
Andika jina lako hapa chini
1. Godius Rweyongeza 0755848391 (Morogoro Mjini-Morogoro)
2.
3.
4.
5.
6.
7.
8.
9.
10.
11.
-
Kama Unataka Mali: Maeneo Matano Unapoweza Kupata Mali Halali…
Unalikumbuka lile shairi la kama mnataka mali mtaipata shambani? Ila shairi hili…walilisoma baba zetu, sisi tumelisoma na sasa watoto wetu wanaenda kulisoma pia. Hahah
Kitu kikubwa kwenye hili shairi ni kwamba kama unataka mali utaipata shambani. Leo hii nilikuwa nafiria hivi kwamba huyu mwandishi wa hili shairi angekuwa analiandika sasa hivi, hivi kweli bado angeendelea kusema kwamba kama mnataka mali mtaipata shambani au angesema kitu kingine?
Hapo ndipo nimegundua kwamba dunia ya sasa imebadilika sana sana kuliko zamani hizo. Nadhani mwandishi wa shairi hili leo hii angekuwa anatunga tena hili shairi, kuna kitu fulani ambacho angeongezea na hicho ndicho nimeamua kukiandika kwa mfumo wa makala siku ya leo kwa hiyo kama unataka mali. Haya hapa ndiyo maeneo muhimu unapoweza kuipata.
KWANZA KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI
Nadhani tuanze na ushauri wa mwandishi wa shairi mwenyewe. bado shamba ni eneo zuri tu kutengeneza mali hata kwenye ulimwengu wa leo. hata hivyo kuna mabadiliko makubwa wakati shairi linaandikwa na wakati wa leo. Mashamba ya leo hii ni ya kidigitali. Ni kweli bado utapata mali shambani, ila sasa haupaswi kulima hovyohovyo,
- unapaswa kulima kitalaalam na kufuata taratibu zote za kilimo.
- unapaswa kulima huku ukitunza mazingira
- unapaswa kutumia mbegu bora, kilimo kinaanzia kwenye mbegu, ukipanda mbegu mbaya utapata mavuno mabovu, unavuna ulichopanda.
- Lima hata kwa kutumia vifaa vya kisasa kama greenhouse na mwangilia kwa kutumia mfumo wa kisasa kama drip irrigation. Hapa sasa ndio utafurahia kilimo.
siyo unaendelea kusema kwamba kama mnataka mali mtaipata shambani wakati unaendelea kulima kwa mbinu zilizopitwa na wakati. Utapata mavuno kidogo na mwisho wa siku kilimo utaona hakifai. tafuta watalaam wakuelekeze. Kwa hiyo napenda nimalizie hii pointi kwa kusema kwamba kama unataka mali utaipata shambani, ila sasa lima kisasa.
PILI KAMA UNATAKA MALI ANZISHA, KUKUZA BIASHARA YAKO
Moja ya njia ambayo watu wngi wanatumia kwenye kuingiza kipato ni njia ya AJIRA. ahata hivyo, hii njia ina kikomo. kila mwezi kuna kiwango fulani cha fedha ambacho unapewa na mwajiri wako. hakiongezeki sana sana na hata pale kinapoongezeka, ongezeko linakuwa ni dogo.
Ila sasa kuna huyu jamaa anaitwa biashara. malipo kwenye biashara hayana ukomo. Ukomo pekee kwenye biashara yako ni ule ambao wewe mwenyewe unajiwekea. kadiri unavyoikuza biashara yako, ndivyo ambavyo unaweza kupata mshahara mkubwa zaidi. hapo bado kuna faida ya biashara.
Kumbe kwenye ulimwengu wa leo, kama unataka mali, biashara ni sehemu nyingine unapoweza kupat mali..
TATU KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA KWENYE UWEKEZAJI
Uwekezaji ni kitu kingine ambacho unaweza kufanya na kikakusaidia wewe kuingiza kipato bila hata ya wewe kufanya kazi. lakini kikubwa zaidi ni kwamba uwekezaji wenyewe ni mali. Kama utawezekeza vizuri, uwekezaji unaweza ukakufikisha mpaka kwenye uhuru wa kifedha.
Kuna uwekezaji wa aina mbalimbali,
- uwekezaji kwenye majengo
- uwekezaji kwenye soko la hisa
- uwekezaji kwenye soko la mitaji
- uwekezaji kwenye hatifungani, vipande n.k
Nashauri baada ya hapa uchague eneo moja ambapo unaenda kuwekeza, kisha uanze kulisoma na kulitafiti kiundani ili uweze kulielewa. Unataka kuwekeza kwenye hisa? Anza kwa kusoma kitabu changu cha MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE, gharama yake ni 5,000/- tu. Tuwasiliane kwa 0755848391.
NNE, KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA KWENYE SEKTA YA AFYA
Hii ni sehemu nyingine ambapo unaweza kupata mali
Labda niseme tu kwamba kila mtu anapenda awe na afya bora. Mtu akiumwa yuko tayari hata ajikopeshe kwa ndugu jamaa na marafiki ili apate huduma za matibabu.
Kama alikuwa ameweka akiba yake anakuwa tayari kwenda kuitoa kwa ajili ya kutibiwa.
Kama wewe unaweza kuwasogezea watu huduma za matibabu karibu yao ni njia ya kutengeza kutengeneza mali pia
TANO KAMA UNATAKA MALI UTAIPATA KWENYE SEKTA YA ELIMU
Kuongezeka kwa watu kunafanya sekta ya elimu izidi kupamba moto pia. Hii ndio kusema kwamba shule zilizopo sasa hivi haziwezi kutosheleza ongezeko la watu.
Tena kuna sera na misemo mbalimbali kuhusu elimu ambazo watu wamezishikilia, wapo wanaosema elimu ni ufunguo wa maisha, wengine wanasema; elimu ni nuru/mwanga, elimu ni daraja n.k.
Sambamba na hiyo misemo kuna imani maarufu ambayo tayari ipo kwamba maisha bila shule hayawezekani. Kwa hiyo, lazima mtu aende shule asome kwa bidii ndiyo aweze kufanikiwa maishani mwake.
Kwa hiyo, lazima shule zijengwe nyingine mpya ili kukidhi matarajio ya watu kuhusu elimu. Na wewe unaweza kuchamgamkia fursa hii moja kwa moja na kuianza safari yako ya kutengeza mamilioni ya fedha.
SOMA ZAIDI: TATIZO SI RASILIMALI ZILIZOPOTEA tatizo unamwibia Petro Kumlipa Paulo
HITIMISHO
Najua kuwa kuna maeneo zaidi ya haya, ila kwa leo nimekuletea hayo tu. Kama utapenda kujifunza zaidi, nashauri uhakikishe umepata ebook yangu inayoitwa SEKTA 11 ZA KUTENGENEZA MAMILIONI YA FEDHA TANZANIA. inapatikana kwa elfu tano (5,000/-)tu
-
YAH: UJIO WA TOLEO LA PILI LA KITABU CHA JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO

Kitabu cha Jinsi Ya Kufikia Ndoto Zako Hello upande wa huko, siku ya leo nina furaha kubwa sana. na ninapenda kukujulisha kuwa nakala za kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO toleo la pili, zinaenda kuanza kupatikana kuanzia tarehe 20 Mei 2022.
Kwa mara ya kwanza kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO nilikizundua mwaka 2020 mwishoni, na sasa mwaka huu 2022 toleo la pili linakuja.
Karibu sana rafiki yangu uweze kujipatia nakala ya kitabu cha jinsi ya kufikia ndoto zako toleo la pili.
Gharama ya kitabu itakuwa ni shilingi elfu 20. Ila kwa yeyote atakaweka oda ya kupata kitabu hiki, atakipata kwa elfu 15,000 tu.
Kwa wakazi wa Dar, Morogoro na Pwani mtafikishiwa nakala mpaka mlangoni kwako au ofisini kwako siku ya kuzinduliwa au siku moja baada ya kitabu kuwa sokoni.
Kwa ambao mko nje ya mikoa niliyotaja hapo juu, mtatumiwa nakala na zitawafikia bila shida yoyote.
Hapa kikubwa tuwasiliane rafiki yangu. Nimeanza kupokea oda na hapa unachoweza kufanya ni kujiandikisha kwa ajili ya kuja kupokea kitabu hiki cha kipekee
Jiandikishe kwa kutuma ujumbe kwenda namba 0755848391.
Au andika hapa chini. andika jina lako, mahali ulipo na namba yako ya simu. Kwa ambao wataweka oda ya kitabu watakipata kwa shilingi elfu kumi na tano (15,000) badala ya elfu ishirini (20,000/-)
Andika jina lako hapa chini (au nitumie ujumbe kwa 0755848391)
Sitaki ukose nakala hii ya kipekee sana. hivyo, jiweke kwenye orodha ya wale watakaopokea nakala hii ya kipekee kwa elfu 15,000/- tu badala ya 20,000/-
Andika jina lako hapa chini
1. Godius Rweyongeza 0755848391 (Morogoro Mjini-Morogoro)
2.
3.
4.
5.
6.
7.
8.
9.
10.
11.