Home


  • Namba Zetu Za Malipo

    Namba za malipo ya vitabu:

    Namba za lipa

    TIGO PESA: 19016638 Jina ni SONGAMBELE CONSULTANTS

    M-PESA: 5564517 jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

    Namba za kawaida

    AIRTEL MONEY: 0684408755
    TIGO PESA: 0655 848 392
    M-PESA: 0745 848 395

    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    NB: Kama namba ya malipo anatumiwa mtu ambaye yuko nje ya nchi. Iandikwe Kwa kuanza na +255

    Kwa hiyo namba zinazotumwa nje ya nchi zitakuwa
    Airtel money: +255 684 408 755
    TIGO PESA: +255 655 848 392
    M-PESA: +255 745 848 395

    KOTE Jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Kama malipo yatakuwa yanafanyika kupitia benki.

    Yafanyie kupitia

    1. CRDB BANK: 0150770710200
    2. NMB BANK: 22110047274

    Kote jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

  • Wasiliana na Godius Rweyongeza Sasa

    Habari yafuatayo ni mawasiliano Unayoweza kutumia kumpata GODIUS RWEYONGEZA

    Simu: +255 (0) 684408755

    Whatsap: +255 (0) 755848391

    Email: songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu vyake wasiliana Moja kwa Moja na +255 (0) 684408755 (more…)

  • Kama upo chuoni na una mpango wa kujiariri; fanya hivi. Mwongozo kujiajiri baada ya kumaliza chuo

    Nakumbuka nikiwa kidato Cha tano nilitamka kauli ambayo mpaka leo hii imekuwa mwongozo mkubwa kwangu; nilisema kwamba; kwa vyovyote vile kazi yoyote ile nitakayoifanya maishani mwangu nitahakikisha naifanya kwa ubora na watu nitakaokuwa nawahudumia watafurahia.

    Kipindi hicho nilikuwa na ndoto za kuja kuwa daktari wa binadamu au mwalimu. Si unajua ukisoma PCB unakuwa na mikogo za kujiita daktari. Muda mwingine mpaka kwenye daftari unaandika jina lako kwa kutanguliza neno Dr.

    Siku mkienda maabara na labcoat ndio kabisa unapost mpaka mtandaoni ukisema, Dr. In action hahah.

    Baada ya kumaliza kidato cha sita nilianza kusoma vitabu vya mafanikio na kitu kimoja nilichokuja kugundua ni kuwa ninlikuwa nataka kuwa daktari kwa sababu tu ya kuutaka mshahara mkubwa,uliokuwa ukisemwa na watu na nilitaka kuwa mwalimu kwa sababu iliaminika kuwa ni rahisi kupata ajira kama mwalimu (mshahara siyo mkubwa ila uhakika wa ajira ni mkubwa). Sasa hapa nikagundua kuwa ukiwa mtu makini unaweza kutengeneza mshahara mkubwa hata kama siyo daktari, nikaamua sasa kwa dhati kuwa ninaenda kuwa tajiri maishani mwangu. Na hata baada ya kuingia chuo na kuhitimu niliweka mkakati ambao ndio nimeufanyia kazi naamini utaweza kukusaidia wewe. Kwa hiyo Kama upo chuoni na una mpango wa kujiariri; fanya hivi

    1. Acha cheti chako kiozee chuoni

    Kwa mfumo wa elimu ya Tanzania, watu wengi wanathamini sana vyeti kiasi kwamba mtu akishahitimu anaanza kuzunguka huku na kule na kule cheti. Elimu yenyewe hii kikawaida imekuandaa kuhakikisha kwamba mara tu baada ya kumaliza chuo unaanza kutafuta ajira mtaani, ikitokea tu hujaajiriwa basi utaanza kulalamika, utapata msongo na hata unaweza kujiua.

    Sasa, ninachotaka nikwambie wewe unayetaka kujiajiri ni kwamba soma kwa bidii, faulu ila mara tu baada ya chuo, sahau kuhusu cheti chako. Tena kiache hicho cheti chako kiozee chuoni. Wewe nenda mtaani, utafute kitu ambacho utaanza kufanya na upambane na hicho. nasema hivyo maksudi kwa sababu endapo utaanza kuhanganaika na cheti mara tu baada ya kuhitimu, utajikuta kwamba unajiingiza kwenye mtego wa kuajriwa na kuanza kukimbilia kuitafuta ajira, hivyo hatua ya kwanza kabisa ya kufanya kama unataka kujiajiri mara tu baada ya kuhitimu chuo ni kuhakikisha kwamba unaachana na cheti chako na kukiacha kiozee hukohuko chuoni.

    Cheti kitakulemaza na kukusahaulisha ndoto zako za kujiajiri.

    2. Noa kipaji chako

    Hakikisha kwamba unanoa kipaji chako na kukiendeleza kwa umakini wa hali ya juu. Tatizo la watu wengi ni kwamba wanafikiri kuwa kipaji hakifai na wala hakilipi hapa bongo, ila sasa tatizo watu wanaokwambia kuwa kipaji hakilipi hapa bongo wenyewe hawajawahi hata kunoa wala kutumia kipaji chao maishani mwao. Utakuta mtu anakwambia kwamba kipaji hakikilipi bongo ila yeye hajawahi hata siku moja kutumia kipaji cha kwake. Na hata hajui kipaji chake ni kipi.

    Wewe jifunze kwa watu ambao wanatumia vipaji vyao. Kipaji kinalipa asikudanganye vitu. Kinachofanya vipaji vya watu visiwalipe ni kwa sababu wanavifanyia kazi kikawaida, hawavipi thamani wao wenyewe, wanaibiwa na wasimamizi wao na mengineyo mengi. Kama umeamua kwa dhati kwamba unaenda kunoa kipaji chako na kukifanyia kazi bila kurudi nyuma, basi kasome kitabu cha KUTOKA SIFURI MPAKA KILELENI kina mengi ya kukusaidia wewe kuweza kunoa na kunufaika na kipaji chako. Wasiliana na 0755848391 ili kupata nakala yak oleo.

    3. Anza kuwashirikisha watu maarifa yako uliyojifunza chuoni

    Mpaka sasa hivi kuna vitu vingi ambavyo umejifunza chuoni. Unaweza kuanza kutumia vitu hivyo mara moja kwenye maisha yako kwa kuwasaidia watu wengine. Kuna vitu unavyojua, ila sasa kuna watu wengine ambao haawajui kabisa hivyo vitu na hivyo na wangependa kujua hivyo vitu. Kwa hiyo kujifunza kwako chuoni kuwe tiketi ya kuwasaidia watu. anza kuwasidia watu kwa kuwapa maarifa kulingana na kile kitu ambacho umejifunza. Kuna vitu ambavyo wewe unajua na unaviona vya kawaida, ila wengine wanavihitaji sana hivyo vitu.

    4. Fungua blogu

    Kutokana na ukweli kuwa una maarifa uliyonayo kutoka na kile ulichojifunza chuoni, na kwa kuwa tumeshakubaliana kuwa utaanza kuwashirikisha watu wengine maarifa kutokana na kile ulichojifunza chuoni, hivyo kifuatacho ni wewe kufungua blogu na kuhakikisha kwamba haya maarifa yako unayaaweka sehemu sahihi mtandaoni. Ukianza kuwashirikisha watu maarifa haya, utajikuta kwamba

    • Wewe mwenyewe unaongeza maarifa zaidi kwenye vile vitu ulivyokuwa unajua
    • Unaanza kujenga timu ya watu wanaokuamini
    • Unaanza kupata mrejesho kutoka kwa wasomaji wako
    • Unapata kipato cha kuendesha maisha yako n.k.

    Kama shida yako kwenye kufungua blogu ni kuandika, unaweza hata kupata kozi ya uandishi. Wasiliana nami kwa 0755848391 ili niweze kukusaidia

    5. chagua kitu kimoja ambacho utakufanyia kazi kwa muda mrefu bila kuacha

    Chagua kitu kimoja ambacho unaenda kukifanyia kazi kwa muda mrefu bila kuacha, kitu hicho unaweza ukawa umeanza kukifanya bila ya malipo, ila kadiri utakavyokuwa unaenda utakuwa unazidi kukiboresha ili kiweze kukuingizia fedha. Kinaweza kuwa ni kipaji chako ambacho umeshanoa, kinaweza kuwa ni ujuzi wako au elimu yako ambayo unaitumia sasa hivi kwa manufaa kuwasaidia watu wengine. Inaweza kuwa ni biashara ambayo umefungua au kitu kingine. kifanye hiki kitu na usichoke kukifanya mpaka pale kitakapokupa matokeo unayotaka.

    Kumbuka tu kuwa unaweza kupata chochote unachotaka kama utaamua na utadhamiria kweli kuhakikisha kwamba unaweka juhudi na kazi zaidi.

    PATA KITABU CHA BURE

    Umekuwa nami rafiki yako wa ukweli

    Godius Rweyongeza

    +255755848391/ Morogoro-Tanzania

  • KWA NINI UNAPASWA KUHUDHURIA DARASA RASMI YA UANDISHI 2022

    Jana nilitangaza rasmi kuwa kutakuwa na kozi ya uandishi kwa mwaka huu 2022 ambayo inaenda kuanza tarehe 16 machi, kozi hii itakafanyika kwa njia ya mtandao.

    Kutangazwa kwa kozi hiyo ni kiashiria kuwa unapaswa kuwahi nafasi yako mapema. Hii kozi hii ya uandishi. Ni kozi ya kipekee sana ambayo huwezi kupata sehemu yoyote mtandaoni.

    Nasema hivyo kwa sababu moja kuu. Wewe umekuwa unajifunza Mambo mengi kuhusu uandishi, ila cha kushangaza bado tu umekuwa unakwama na huandiki. Na Mimi ninachokukuhakikishia ni kuwa utaendelea kujifunza Mambo mengi kadiri ila kama hutajiunga na kozi hii hutakaa uandike.

    Kozi hii ni ya waandishi, siyo wale wanaojiita waandishi, ila waandishi wanaoandika, hicho ndiyo kitu Kikubwa tunachopambana nacho kwenye hii kozi.

    Mpaka kozi inafikia mwishoni utakuwa tayari umeshaandika, siyo mara moja, siyo mara mbili, ila utakuwa umeandika kiasi cha kuweza kumaliza kitabu chako.

    Hiki ni kitu siyo tu ambacho nakwambia kwa nadharia, ila ni kitu ambacho watu wengine wamekifanyia kazi kwa mafanikio makubwa.

    Sasa kama kuna watu wametumia mbinu hizi ninazofundisha kuandika na kukamilisha vitabu vyao, unadhani wewe utashindwa? Kozi imeandaliwa katika mfumo wa kukufanya uandike na ukamilishe lengo lako ndani ya muda wa kozi. Ukijiunga na kozi tutawasiliana na kuweka mpango. Utaweza kuandika hata kama hujawahi kuandika.

    Hivyo kwa mara ya kwanza baada ya kuhudhuria kozi hii utakuwa mwandishi. Yale masuala ya kujiita mwandishi mtandaoni wakati hata hujawahi kuandika kwishney.

    Kozi hii ina mwongozo uliokamilika na ina kila kitu unachohitaji kujua kuhusu uandishi.

    Mbali na hilo kwenye kozi hii:

    👉UTAANDIKA kitabu chako na kitakamilika ndani ya siku 30.
    👉Nitakusimamia na kusoma kazi zako unazoandika kila siku na kukusaidia kuziboresha.
    👉Nitakufungulia blogu ya bure.
    👉Utajifunza mengi kutokana na yale wanayoandika wenzako na maoni nitakayokuwa natoa kuhusu kazi za wenzako.
    👉Utapata kitabu Cha JINSI YA KUWA MWANDISHI MBOBEVU NDANI YA SIKU 30 bure.
    👉Utapata jarida lenye hatua 15 za kufuata ili kuandika magazetini.
    👉Utapata mafunzo ya audio zaidi ya 10. Yakiwemo mahojiano na waandishi wakubwa hapa nchini.

    👉Utaungana na waandishi wengine wanaoandika na kujifunza mengi kutoka kwao.

    Nafasi kwenye kozi hii ni 10 tu. Hivyo, kama unataka kuhudhuria kozi hii, sharti uwahi kujihakikishia nafasi yako kabla hazijaisha.

    Na gharama za kuhudhuria darasa hili la kipekee itakuwa ni laki mbili (200,000/) tu. Jihakikishie nafasi yako Sasa hivi kwa kuwasiliana na 0755848391 kabla nafasi hazijaisha.

    NAKUKUMBUSHA TU: kozi hii ni ya siku 30 tu, na huna kitu chochote cha kupoteza. Endapo utajiunga na kozi hii ila katikati mwa kozi au mwishoni ukaona kuwa haifai, utanipigia simu nami nitakurejeshea fedha yako bila kukuuliza maswali yoyote.

    Hivyo, jisajili sasa hivi kwa kuwasiliana na 0755848391.

    PATA KITABU CHA BURE

    Umekuwa nami rafiki yako wa ukweli

    Godius Rweyongeza

    +255755848391/ Morogoro-Tanzania

    G

  • Karibu Kwenye Darasa Rasmi La Uandishi Mwaka 2022

    Tangu mwaka 2019 nimekuwa naendesha darasa la uandishi ambapo huwa ninakaa na watu watano na kuwafundisha uandishi kwa kina. Darasa hili la kipekee ambalo huwa naliendesha kwa watu wachache tu, huwa linafanyika kwa njia ya mtandao, huku nikiwa na lengo la kuwafundisha na kuwanoa hao watu wachache na kuwafanya waandishi wabobevu.

    Kila mwaka darasa hili limekuwa linafanyika kwa mafanikio makubwa, huku wahusika wake wakiwa wanatoka wamenolewa na kupata ujuzi kamili wa kiuandishi. Ndio maana mwaka huu kwa mara nyingine nimeamua kuliandaa darasa hili. Hivyo, kitu cha kwanza kabisa, ningependa kutangaza kuwa darasa hili litaanza rasmi tarehe 16.3.2022 na usajili kwenye darasa hili hapa umefunguliwa tayari.

    (more…)

  •  Hiki Kitu Ndicho Chanzo Cha Mafanikio Yote

    Mwaka 1937 ni mwaka muhimu sana kwenye ulimwengu wa mafanikio.  Ni mwaka ambao kitabu cha THINK AND GROW RICH kilichapwa baada ya miaka mingi ya utafiti.

    Kwenye kitabu hiki mwandishi ameeleza mbinu za mafanikio ambazo ziliwapa utajiri mkubwa sana matajiri wa wakati huo.  Hapa wanaongelewa watu kama kama akina Rockefeller ambaye  mpaka leo hii amebaki kuwa miongoni mwa matajiri wakubwa kuwahi kutokea.

    Kutokea hapo kitabu hicho kimetengeneza matajiri wengi sana, na kimewasaidia wengi kufika mbali.

    Kitabu kimeeleza hatua 13 za kufikia mafanikio makubwa. Mwandishi anasema unapaswa kuwa na
    1. Shauku ya kufanikiwa
    2. Unapaswa kuwa na imani
    3. Unapaswa kujinenea maneno chanya
    4. Unapaswa kuwa na elimu/maarifa sahihi
    5. Unapaswa kuwa mvumilivu
    6. Unapaswa kuungana na timu ya watu sahihi na mengineyo.

    Ila sasa kuwa na hayo yote haitoshi. Hapo ndipo mwandishi anakwambia kwamba; chanzo cha mafanikio yoyote kipo kwenye WAZO. Ukishakuwa na wazo ndipo sasa utaliunganisha na shauku yako ya kufanikiwa. Ndipo utapaswa kuwa na imani kuwa utakifanikisha.

    Hapo ndipo utapaswa pia kujinenea maneno chanya na mengineyo.

    Kwa hiyo, kama unataka kufanikiwa Anza kwa kujiuliza hivi mimi nina wazo gani haswa la kunisaidia kufanikiwa? Kama huna wazo jifikirie tena.

    Wazo lako ndio chanzo kikuu cha kupata mafanikio unayotaka.

    PATA KITABU CHA BURE

    Umekuwa nami rafiki yako wa ukweli

    Godius Rweyongeza

    +255755848391/ Morogoro-Tanzania

  • Hatua muhimu ambazo wazo lako litapitia kabla ya kuonekana kwenye uhalisia

    Niseme, nisiseme! Wazo linazaliwa, linakua na muda mwingine kuzeeka mpaka kufa!

    Kwa hiyo wazo ni kama mtoto, linabebwa kama mimba. Hiki ni kipindi ambacho linakuwa kichwani mwa mtu. Linazaliwa hapa ni pale ambapo linaanza kufanyiwa kazi, linakua, hapa ni pale linapozidi kufanyiwa kazi na kuzidi kuleta matokeo kwa aliyekuwa na wazo na jamii, wazo linazeeka na hata kufa (hapa ni pale ambapo linakuwa halijafanyiwa kazi kikamilifu).

    Wanaume kama nawaona vile mnavyoguna, eti unajiuliza kwa hiyo na sisi wanaume tunabeba mimba? Naomba nieleweke tu kwamba mimba yenyewe ni ya wazo siyo mimba ya mtoto, hapo vipi.

    Mwanamke anapokuwa na mimba ya mtoto kuna vitu anapaswa kufanya ili mimba hiyo isitoke wala kuharibika. Mtoto anapozaliwa anaangaliwa kwa umakini, analelewa, analishwa na kupewa vitu vyote vya muhimu. Endapo vitu hivi vitu vyote vitatolewa bila shida yoyote, unakuwa ni uhakika kwamba LAZIMA TU mtoto atakua. Na ni kweli anakua, lakini endapo vitu fulani havitazingatiwa, basi ndio mtoto ataaza kupata utapiamlo, au magonjwa mengine.

    Sasa kitu kikubwa cha wewe kufanya ni kwamba, ukiwa na wazo la biashara, hakikisha unakimbizana kulifanyia kazi.

    Ukianza kulifanyia kazi ng’ang’ana nalo mpaka likue au ulifanikishe.

    Ukishalikuza, hakikisha unakuwa mbunifu ili liendelee kukua zaidi au kuenea maeneo mengine, la sivyo litakufa.

    PATA KITABU CHA BURE

    Umekuwa nami rafiki yako wa ukweli

    Godius Rweyongeza

    +255755848391/ Morogoro-Tanzania

  • Kitu Gani Haswa Kinahitajika Ili Kufanikisha Wazo Lako

    Mwaka 1908 ni mwaka wa kihistoria maana ndio mwaka ambao gari la kwanza lilitengenezwa na kampuni ya Ford ambayo ilianzishwa mwaka 1903,

    Gari hilo liliipa jina kampuni ya Ford na kuifanya itengeneze fedha za kutosha, kiasi kwamba watu wengi wakawa wanatamani kuanzisha biashara kampuni nyingine ambazo zingezalisha magari. Ukiangalia kwenye mtandao wa google, kampuni zilizoanzishwa kati ya mwaka 1900 mpaka 1999 ni karibia 3000.

    (more…)

  • Hizi Hapa Ni Sababu Za Kwa Nini Unapaswa Kufanyia Wazo Lako Mwaka Huu Na Sio Kusubiri

    Natumai kwamba unaendelea vyema. Ni takribani wiki nzima sasa nimekuwa nikiandika makala kuhusu wazo la biashara. Kila siku tumekuwa tunapata makala moja iliyojishosheleza na yenye ujumbe uliokamilika. Sasa leo nimerudi tena kwa lengo la kukueleza kwa nini unapaswa kufanyia wazo lako la biashara mwaka huu na sio mwaka mwingine. Najua kwamba ninachoenda kuandika hapa ni muhimu kwako endapo utakifanyia kazi. Kama unajua kwamba utasoma hapa ila ukaishia kusema kwamba huyu jamaa anaandika vizuri, basi ni bora kabisa usisome il usije ukapoteza muda wako. Mimi binafsi najali sana muda wako, maana najua kwamba muda ni mali. Sasa haina haja ya wewe kusoma hapa ukaishia kusema kwamba huyu jamaa kaandika vizuri wakati huyafanyii kazi yale unayojifunza hapa.

    Sasa baada ya kusema hayo kuna sababu NNE za kwa nini unapaswa kuanza mwaka huu kufanyia kazi wazo lako.

    (more…)

  • WAZO LA BIASHARA AINA HII LAHUWEZI KULIPATA

    Kuna mtu unaweza kumkuta anatafuta wazo la biashara ambalo halijawahi kufanyika, kitu ambacho hakijawahi kuonekana

    (more…)

  • Kwani wewe unasemaje?

    Habari ya leo,

    Mwezi wa tisa mwaka 2016, nilianza kuandika makala kwenye blog ya songambele na baada ya hapo niliendelea mbele zaidi na kuandika vitabu, nikaandika magazetini, nikatoa mada kwenye redio na runinga na hata kuandaa mafunzo kwenye YouTube.

    Kwangu hizi zote zimekuwa ni tuzo za hatua ya kwanza niliyochukua na kuanza kuandika mwaka 2016.

    Imani yangu ni kuwa lazima kwenye maandiko yangu au mafunzo yangu, utakuwa umewahi kupata kitu chochote ambacho unafanyia kazi au ambacho kimekusaidia.

    Kama hilo ni kweli, basi leo ningependa kupata mrejesho wa maandishi kutoka kwako. Imani yangu kuna wengine ambao wangependa pia kusikia kitu kama hiki.

    Ni kitu gani umependa? Kitu gani kimekuwa msaada kwako? Je, vitu ambavyo nilifundisha kwenye kitabu au makala vilikuwa na msaada?

    Ulipenda jinsi kitabu fulani kilivyokuwa?  Ni kitu gani unadhani Kama kingeongezwa kingefanya kitabu hicho kuwa bora zaidi? Tunaomba maoni yako HAPA

    Mara zote napenda mrejesho, na ninapenda kuboresha huduma na bidhaa zangu ili ziweze kuwa zenye manufaa kwako na kwa wengine zaidi.

    Maoni yoyote yanakaribishwa.

    Ni Mimi
    Godius Rweyongeza
    +255755848391
    (www.songambeletz.com)
    MOROGORO-TZ

    BONYEZA HAPA kuweka maoni yako

  • UNAPASWA KUACHANA NACHO

    UNAPASWA KUACHANA NACHO

    Kuna wakati unapaswa kuachana na vitu hata kama watu wanasema ni fursa nzuri.
    Au hata kama kilikuwa ni kitu unapenda kufanya kwa siku nyingi.

    (more…)

X