Home


  • Namba Zetu Za Malipo

    Namba za malipo ya vitabu:

    Namba za lipa

    TIGO PESA: 19016638 Jina ni SONGAMBELE CONSULTANTS

    M-PESA: 5564517 jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

    Namba za kawaida

    AIRTEL MONEY: 0684408755
    TIGO PESA: 0655 848 392
    M-PESA: 0745 848 395

    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    NB: Kama namba ya malipo anatumiwa mtu ambaye yuko nje ya nchi. Iandikwe Kwa kuanza na +255

    Kwa hiyo namba zinazotumwa nje ya nchi zitakuwa
    Airtel money: +255 684 408 755
    TIGO PESA: +255 655 848 392
    M-PESA: +255 745 848 395

    KOTE Jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Kama malipo yatakuwa yanafanyika kupitia benki.

    Yafanyie kupitia

    1. CRDB BANK: 0150770710200
    2. NMB BANK: 22110047274

    Kote jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

  • Wasiliana na Godius Rweyongeza Sasa

    Habari yafuatayo ni mawasiliano Unayoweza kutumia kumpata GODIUS RWEYONGEZA

    Simu: +255 (0) 684408755

    Whatsap: +255 (0) 755848391

    Email: songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu vyake wasiliana Moja kwa Moja na +255 (0) 684408755 (more…)

  • Amsha Uungu Ulio Ndani Yako: Siri Kuu Ya Mafanikio Kutoka Kwa Socrates

     

    Socrates anaaminika kuwa miongoni mwa watu waliokuwa na busara katika ugiriki yote katika nyakati zake.

    Kipindi hicho kijana mmoja alimfuata kumwomba ushauri wa namna ya kufanikiwa.

    Kwa busara Socrates akamwambia njoo siku fulani. Yule kijana akawa kweli ametokea siku hiyo ili aambiwe siri ya mafanikio. Nadhani yule kijana alikuwa anataka njia ya mkato ya kufanikiwa (kulala maskini-kuamka tajiri)

    Alichofanya Baana Socrates ilikuwa ni kumwambia yule kijana amfuate. Waliambatana na yule kijana mpaka kwenye mto, huku Socrates akiendelea kumwambia yule kijana amfuate.

    Yule kijana aliendelea kumfuata kwa uoga. Walipofika katikati ya maji, Socrates alimshika yule kijana kwa nguvu na kumzamisha KWENYE maji.

    Yule kijna akaanza kuhangaika kuona Kama angetoka, ila akashindwa. Akahangaika akashindwa.

    Baada ya kuona hakuna tumaini la kuachiwa, kijana akatumia nguvu zote kujitetea akawa ameweza Kutoka chini ya maji.

    Kwa hasira kijana akamwambia mzee Socrates, Mimi nimekuomba uniamboe siri ya kufanikiwa wewe unataka kuniua.

    Hivi ungekuwa wewe ninavyokujua ungefanyaje? Nadhani sasa wewe ndio ungemzamisha mzee Socrates mazima…. hahaha, tuendelee….

    Socrates akamjibu kwa kusema, ulipokuwa chini ya maji ni kitu gani ulikuwa unakitaka sana. Yule kijana akajibu kwa kusema KUPUMUA

    Socrates akiendelea kumwambia kwamba  ulifanya chini juu ili upate hilo.

    Sasa kama unataka kufanikiwa unapaswa pia kuyapa kipaumbele mafa kama ambavyo kipaumbele chako kilikuwa kupumua ulipokuwa majini.

    Ndani yetu tuna nguvu ya ziada ya kutuwezesha kufanya makubwa. Ila nguvu hii isipotumika inabaki ikiwa imelala tu.

    Ni mpaka pale tunapokuwa katika mazingira ya hatari ndipo tunajikuta tunafnya makubwa ambayo hatukutegemea. Inapotokea hatari ndio unakuta mtu anakimbia wakati asku zote huwa anawaambia watu kuwa yeye na kukimbia ni kama maji na mafuta.

    Rafiki yangu, usisusubiri hatari itokee.

    Anza leo kuutumia uwezo mkubwa. Jisukume wewe mwenyewe

    Uaisubiri ufukuzwe na mbwa ndio ujue kwamba unaweza kukimbia mbio za marathon!

    Usisubiri nyumba iungue ndio ugundue kwamba unaweza kuokoa watu.

    Usisubiri profesa wako akamwambie andika kitu fulani ukilete ndani ya saa 48 ndio ugundue kwamba unaweza kuandika kila siku, tena kitu kinachoeleweka.

    Kuna ukuu ndani yako. Utumie… Utumie rafiki yangu

    Ni Mimi
    Godius Rweyongeza
    0755848391
    Morogoro-Tz

    Kupata mafunzo Zaidi BONYEZA HAPA

    Kupata eBooks BONYEZA HAPA

  • Kinachokukwamisha Wewe Kuandika Kitabu Chako Ni Hiki..

    Kama Kuna kitu watu wamekuwa wanasema kwamba halijakaa sawa ni mfumo wa elimu. Umekuwa unalalamikiwa kwa
    Kukaririsha watu vitu
    Kutokujjenga watu wenye ujuzi
    Kutokuwaandaa wahitimu kwa ajili ya maisha baada ya chuo n.k.

    Kwenye hili naweza kusema kuwa Kuna kitu kimoja watu huwa wanakisahau. Kitu hiki ni namna mfumo wa elimu unavyozuia watu kutumia uwezo wao mkubwa wa kuandika.

    Unaweza kukuta mtu alikuwa na ndoto kubwa kwenye maisha ya kuandika vitabu ila baada ya chuo hatamani kuandika tena

    Kwa Nini?
    Moja ya kitu ambacho mwanachuo anapaswa kufanya anapokuwa chuoni ni utafiti. Na utafiti huu huwa unapaswa kuwasilishwa kwa njia ya maandishi.

    Sasa elimu yetu unakuta kwamba kabla ya kukamilisha andiko lako lako la utafiti, unabinywa kwelikweli. Unazungushwa huku na kule na mpaka mtu anamaliza kuandaa andiko lake, anakuwa amehenyeka sana.

    Kitu hicho kinawafanya wengi wakose hamu ya kuandika baada ya chuo. Nadhani na wewe utakuwa mmoja wao.

    Ila kikwazo kama hiki kinaondoleka.
    Ili kukusaidia kuondoa kikwazo hicho nimeandaa darasa rasmi la uandishi ambapo Mimi ninaenda kukusimamia na mwanzo mpaka mwisho kuwa mwandishi MBOBEVU.

    Darasa hili litakalofanyika kwa njia ya mtandao, linaenda kuwa la kipekee sana. Utavunja hiyo hali inayokuzuia wewe kuandika kuandika. Kwa mara ya kwanza kwenye maisha yako utaaandika na kukamilisha kitabu chako.

    Kama umependa hicho kitu ebu rusha mikono juu kidogo kushangilia ushindi huo….

    Shangilia ushindi huo maana ni uhakika kuwa ukijiunga na kozi hii, ushindi huo unaupata tu.

    Sambamba na hilo kwenye kozi hii:

    👉Nitakusimamia na kusoma kazi zako unazoandika kila siku na kukuelekeza namna bora ya kuziboresha

    👉Nitakufungulia blogu ya bure.
    👉Utajifunza mengi kutokana na yale wanayoandika wenzako na maoni nitakayokuwa natoa kuhusu kazi za wenzako.
    👉Utapata kitabu Cha JINSI YA KUWA MWANDISHI MBOBEVU NDANI YA SIKU 30 bure.
    👉Utapata jarida lenye hatua 15 za kufuata ili kuandika magazetini.
    👉Utapata mafunzo ya audio zaidi ya 10. Yakiwemo mahojiano na waandishi wakubwa hapa nchini.

    👉Utaungana na waandishi wengine wanaoandika na kujifunza mengi kutoka kwao.

    Nafasi kwenye darasa hili ni 10 tu. Hivyo, kama unataka kuhudhuria darasa hili, sharti uwahi kujihakikishia nafasi yako kabla hazijaisha. Na gharama ya kozi hii ni laki mbili (200,000)

    jihakikishie nafasi yako sasa hivi kwa kuwasiliana nami kwa 0755848391


  • AMSHA UUNGU ULIO NDANI YAKO: Sifa 3 Za Kimungu Unazopaswa Kuzitumia Kuanzia Leo

     

    Mwaka 2017 nilipata kusoma kitabu cha FROM VICTIM TO VICTOR. Nilipata kujifunza mengi sana Kutoka kwenye kitabu hiki kuliko unavyoweza kufikiria.

    Kitabu hiki kilichoandikwa na Mzimbabwe Joseph C. Musharika kina mafunzo mengi ambayo na wewe yanaweza kubadilisha maisha yako. Mwandishi amezaliwa katika familia ya kikristo kama ilivyo asilimia kubwa ya Waafrika. Kalelewa na kupewa makuzi na maadili ya kikristo na baadaye kwenye maisha yake akawa mwijilisti.

    Kitu kimoja kilichoanza kumshangaza mwandishi ni kuona jinsi wakristo walivyokuwa hawatumii uwezo wao ipasavyo, walivyokuwa wanalaani utajiri na kuishi maisha ya kawaida.

    Hivyo mwinjilisti Joseph C. Musharika akaamua kuwa ataishi maisha ya tofauti, atajenga utajiri na kutumia uwezo wake kadiri awezavyo.

    Baada ya miaka mingi ya kufanya hivyo mwandishi akaona siyo vibaya nikiandika kitabu ili Waafrika wenzangu waweze kunufaika, maana imeandikwa kwamba watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa.

    Kitabu chake cha From Victim To Victor amekigawa kwenye sehemu kuu mbili.

    Sehemu ya kwanza ya kwanza ameiita KWA SURA NA MFANO WAKE na sehemu ya pili ndiyo KUTOKA UHANGA MPAKA USHINDI (From victim to Victor).

    SEHEMU YA KWANZA YA KITABU: KWA SURA NA MFANO WAKE

    Mwandishi kaanza sehemu hii  kwa kueleza jinsi ambavyo tumeumbwa kwa sura na mfano wa mwenyezi Mungu na tuna uwezo mkubwa kuliko vile tunavyoweza kufikiri.

    Kitu kimoja kilichonishangaza kutoka kwa mwandishi ni namna anavyotafsiri ile stori mnara wa babeli. Kabla yake na baada yake sijaona mtu ambaye anaitafsiri kwa kina na kwa namna ya upekee hivyo. Na kwa kuwa somo la leo nataka tuuone jinsi ya kuamsha uungu ulio ndani yako basi nitaenda na hiki kipengele cha mnara wa Babeli.

    Kama wewe siyo mkristo utanisamehe, ila andiko la leo lina mazuri ya wewe kujifunza pia. Mpaka hapo naomba uniruhusu kwanza niweke stori ya mnara wa babeli, kama ilivyoelezwa kwenye kitabu cha MWANZO 11:1-9, kisha niendelee;

    Kwanza, watu wote duniani walikuwa na lugha moja na walitumia maneno yaleyale. Basi, ikawa watu waliposafirisafiri kutoka mashariki, walifika katika nchi tambarare huko Shinari, wakakaa. Kisha wakaambiana, “Haya! Na tufyatue matofali, tuyachome moto vizuri.” Walikuwa na matofali badala ya mawe, na lami badala ya chokaa. Wakasema, “Na tujijengee mji na mnara ambao kilele chake kitafika mbinguni ili tujipatie jina, tusije tukatawanyika duniani kote.” Ndipo Mwenyezi-Mungu akashuka chini kuuona mji huo na mnara walioujenga binadamu.

    Mwenyezi-Mungu akasema, “Tazama, watu hawa ni taifa moja na wote wana lugha moja; huu ni mwanzo tu wa yale watakayoyafanya. Lolote wanalokusudia kulifanya watafanikiwa.

    Haya, na tushuke chini na kuivuruga lugha yao ili wasielewane wao kwa wao.” Hivyo, Mwenyezi-Mungu akawatawanya mahali pote duniani, nao wakaacha kuujenga ule mji. Mji huo ukaitwa Babeli, kwa sababu huko ndiko Mwenyezi-Mungu alikoivuruga lugha ya dunia yote, na kutoka huko akawatawanya watu kila mahali duniani.

    Swali la kwanza mwandishi analouliza Ni je, wangeweza kujenga mnara unaofika mbinguni? Mimi nakumbuka nilisema wasingeweza, hii ni kutokana na uelewa niliokuwa nao tangu mwanzo. Lakini mwandishi katika hali ya kushangaza alisema wangeweza na hiki Kitu ndicho kinatuleta kwenye point yetu ya kwanza kwa siku ya leo itakayokusaidia wewe kuamsha uungu ulio ndani yako.

     

    #1. UMOJA

     

    Mwandishi anasabhawa jamaa wangeweza kwa sababu walikuwa na umoja.

    Rejea: Kwanza, watu wote duniani walikuwa na lugha moja na walitumia maneno yaleyale

    Watu wote walikuwa na umoja na lugha waliyoitumia ni moja. Yaani, walikuwa wanaongea wanaelewana. Walikuwa wanapanga na kufikia muafaka. Hivyo, ndivyo walivyokuwa wanaishi.

    Umoja haujawahi kufelisha watu hata siku moja, labda kama hao watu walikuwa na umoja feki. Ndio maana hata siku hizi tunasikia Kuna misemo kama umoja ni nguvu utengano ni udhaifu, kwa pamoja tunaweza. Akina mama tushikamane n.k.

    Hii yote ni kuonesha kwa namna ambavyo umoja unaweza kufanya makubwa. Ukitaka kuwagawa watu ondoa ule umoja uliokuwepo. Ukitaka kuijenga nchi, waunganishe watu, na ukitaka kuisambaratishe acha watu wapigane wenyewe.

    Mwandishi amasema Mungu ni mmoja, ndio maana kwenye Biblia unakutana na maneno kama na tumuumbe mtu kwafano wetu. (Mwanzo 1:26)

    Kwa hiyo basi kama unataka kuamsha uungu ulio ndani yako jenga umoja kwanza. Jenga umoja kati yako na familia yako, umoja Kati yako na wafanyakazi wako, au wenzako, na kikubwa zaidi umoja Kati yako mwenyewe.

    Umoja haujawahi kufelisha mtu hata siku moja.

    Labda unaweza kusema kwa nini sasa hawakuweza kufika huko mbinguni? Kwa Leo naomba niseme Kama mwandishi alivyosema: hakukuwa mpango wa Mungu wake pale, ila uwezo wa hao watu kufika mbinguni ulikuwepo ndio maana Mungu mwenyewe aliona afadhali achanganye lugha yao. 

    Rejea: Tazama, watu hawa ni taifa moja na wote wana lugha moja; huu ni mwanzo tu wa yale watakayoyafanya. Lolote wanalokusudia kulifanya watafanikiwa

    Hayo hapo juu ni maneno ya Mungu. Mungu anasema watu hawa ni taifa moja,  na wana lugha moja. Huu ni mwanzo tu wa Yale watakayoyafanya. Maana hapo badaye wangeweza kufanya makubwa zaidi ya hapo. Lakini Mungu anasema sentensi nyingine yenye uzito zaidi anaposema. Lolote wanalokusudia kukifanya wafafanikiwa.  Lolote wanalokusudia watafanyaje….?

    Naomba nisisitize tena juu ya umoja. Kama unataka kufanya makubwa zaidi. Jenga umoja maana lolote utakaloamua kufanya, utafanikiwa?

     

    #2. UBUNIFU

    Hivi ni nani aliyewafundisha hawa jamaa kufyatua tofali, ni chuo gani hasa kiliwafundisha kujenga ghorofa? Hawa jamaa walikuwa wabunifu. Vitu ambavyo watu siku hizi wanakaa darasani kujifunza, hawa jamaa walikuwa wanavijua kwa kubuni.

    kile mtu kapewa vinasaba vya ubunifu ndani yake. tatizo la watu wengi ni kwamba hawataki kuutumia huo ubunifu waliopewa. wewe pia umepewa huo ubunifu. ni jukumu lako wewe kuhakikisha kwamba unaeda mbali zaidi na kuutumia. u

     

    #3. Kuwa na NDOTO kubwa

    Hawa jamaa walikuwa na ndoto kubwa haswa. Ndoto ya kufika wapi? Mbinguni. Kwa sasa usiniulize mbingu iko wapi. Ila walau ninachotaka ufahamu ni kuwa walikuwa na ndoto kubwa. Na walikuwa hawapo tayari kurudi nyuma.

    Wewe pia unapaswa kuwa na ndoto kubwa, kubwa sana unazozifanyia kazi.hapo ndio utaweza kuamsha uungu ulio ndani yako. Ndoto kubwa zitakusukuma wewe kufanya kazi zaidi na kutumia uwezo wako kwa viwango vikubwa.

    Kwa ndoto kubwa tu walivyokuwa nayo hawa jamaa, Mungu alilazimika kushuka kutoka mbinguni ili aone kile walichokuwa wanataka kufanya. 

    Rejea: Ndipo Mwenyezi-Mungu akashuka chini kuuona mji huo na mnara walioujenga binadamu

    wewe umewahi kusikia au kuona wapi Mungu anashuka kutoka mbinguni ili kushuhudia ndoto kubwa waliyokuwa nayo watu? 

    Sasa na wewe kuanzia sasa anza kuwa na ndoto kubwa ambazo utazifanyia kazi.  Sidhani kama Mungu atashuka kutoka mbinguni ili kushudia ndoto yako, ila nina uhakika kwamba uking’ang’ania kuifanyia kazi ndoto yako. Mungu atakuwa pamoja na wewe na utaweza kuifanikisha.

    Kma na wewe una ndoto kubwa ya kufika mbali kwenye maisha yako, nashauri usome kitabu JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO. Utajifunza mengi ya kukusaidia wewe kuweza kuzifikia ndoto zako. kukipata wasiliana na: 0755848391 sasa hivi

    Kwa leo niache niishie hapo. Kupata uchambuzi kamili wa kitabu hiki jiunge na mafunzo yetu yanayotolewa kwa njia ya barua pepe.  Uchambuzi wote wa kitabu hiki utatolewa huko. BONYEZA HAPA kujiunga.

    Umekuwa nami

    Godius Rweyongeza

    0755848391

    Morogoro-Tz

     

  • Karibu kwenye Duka La Mtandaoni La Songa Mbele

    Kuna msemo mmoja wa kilatini unasema kwamba furahi na wanaofurahi, huzunika na wanaohuzunika.

    Sasa leo hii siyo kwamba nahuzunika bali nina furaha na mimi nimeona nikukaribishe wewe ili nikumegee hii furaha. Si unajua hivi vitu vinaambukizwa?

    Furaha yangu ni kutangaza duka la mtandaoni ambapo wewe au mtu yeyote anaweza kuingia na kununua bidhaa itakayokuwa inapatikana humo.

    Kwenye duka hili la mtandaoni kutakuwa na bidhaa za aina tatu tu.

    Mafunzo kwa njia ya makala au ebooks
    Mafunzo kwa njia ya sauti (audio) na
    Mafunzo kwa njia ya video.

    Kama ni makala basi itakuwa inajadili mada moja kwa undani kabisa ili wewe uweze kuielewa.
    Kama ni audio basi itakuwa pia imezama ndani kujadili kitu fulani na itakuwa siyo chini ya dakika 30.
    Kama ni video bsi na yenyewe haitakuwa chini ya dakika 20.

    Na itakuwa ni kila wiki unapata kitu kimojawapo kati ya hivyo kwenye hili duka.

    Vigezo na masharti

    Huwa ukiingia kunua vidhaa kwenye tovuti yoyote ile ni lazima huwa unakuta kuna vigezo na masharti vingi kweli.
    Aidha kwa upande wangu kwa sasa nimeamua kuwa kigezo na masharti kitakuwa kimoja tu. Kama vitahitajika vingine basi vitaongezwa baadaye ila kwa sasa, kigezo na masharti Ni kwamba ukinunua bidhaa yotote kwenye duka letu na ukapata bidhaa inayoenda kinyume na matarajio yako au bidhaa iliyo chini ya viwango  Basi nitakulipa mimi.
    Yaani, utakurudishiwa fedha zako na nitakuongezea fedha nyingine kama hizo ulizolipia bidhaa hiyo. Hivyo, utapokea fedha yako na ya ziada. Kama ulitoa elfu tano basi utarudiahiwa elfu kumi, tena bila kuulizwa maswali.

    Na simaanishi hili kwa udogo, nalimaanisha haswa. Hicho ndiyo kigezo ambacho naenda kujitoa kuhakikisha kinakamilika bila kujali napitia katika hali gani kwa wakati husika na sisemi hilo ili nikushawishi ukanunue bidhaa leo hii.

    Ila nasema hivi, “hicho ndiyo kigezo na kiwango nilichojiwekea”, hivyo wewe ununue au usinunue, mimi nitaendelea kusimamia hicho kigezo kila siku ya maisha yangu.

    Nimeamua nijitoe hivyo.

    Kwa sasa hivi kuna bidhaa gani kwenye duka? Kwa sasa kuna ebook ya MITAJI 8 ILIYOKUZUNGUKA NA JINSI YA KUITUMIA tu. Nyingine zitaendelea kuwekwa kadiri muda unavyoenda.

    Je, naweza kununua bidhaa moja kwa moja kwenye duka hili?
    K
    wa sasa bado halijakaa kwa mfumo unaokuwezesha wewe kununua bidhaa moja kwa moja. Hivyo, kwa Sasa ukihitaji bidhaa yoyote ile, tuwasiliane kwa simu 0755848391 ili nikutumie. Tutaendelea kuliboresha duka letu mpaka uweze kununua moja kwa moja bila kuhitaji msaada zaidi Kutoka kwangu.

    Je, unapenda kupata ebook ya MITAJI 8 ILIYOKUZUNGUKA NA JINSI YA KUITUMIA? BONYEZA HAPA

    Kupaya mafunzo Zaidi: BONYEZA HAPA

  • Ninahitaji Watu 10 Nami Nitawafanya Kuwa Waandishi Wabobevu Ndani Ya Siku 30

    Mwishoni mwa mwaka 2019 nilianzisha darasa maalumu la kufundisha uandishi. Ambapo katika darasa hili nilikuwa nafundisha mbinu za kiuandishi kwa mtu ambaye hajawahi kuandika kabisa au ambaye tayari ameanza kuandika ila hajaweza kubobea na kujenga nidhamu inayostahili katika uandishi. Katika darasa hili tulijifunza mbinu mbalimbali za kiuandishi na kila kitu unachohitaji kujua kuhusu uandishi.

    Kwa mara ya kwanza kabisa darasa hili tuliliendesha kwa siku 66, mara ya pili darasa hili tulikuja kuliendesha kwa siku 30 tu. Waliojifunza mbinu za kiuandishi kwenye darasa hili sasa hivi ni waandishi wazuri sana.

    Tokea hapo darasa hili limekuwa endelevu, kila mwaka likiendeshwa mara mbili au mara tatu na sasa kwa mwaka huu 2022, darasa hili litaanza tarehe 16,Machi 2022. Hii ni private writing class ukiwa na mimi hapa Godius Rweyongeza na kwenye darasa hili nitakupa mbinu za kiuandishi ambazo hakuna kitabu, mwalimu au sehemu yoyote ile unaweza kuzipata.

     

    Kwenye darasa hili hapa unaenda

    • Kujifunza kila kitu kuhusu uandishi
    • Utaanza kuandika (kumbuka sio tu utajifunza kuandika, ila utaanza kuandika, mfumo wa darasa hili umelenga kukufanya uandike badala ya kujifunza tu, na kuna mbinu ya kukusukuma wewe kuandika badala ya kuishia kujifunza maarifa peke yake)
    • Utapata msaada wa karibu kutoka kwangu wa kiuandishi kwa siku 30 mfululizo. Ndio maana nasema, nahitaji watu watu kumi tu, ambao nitawafanya kuwa waandishi wabobevu ndani ya siku 30 zijazo.

    Sambamba na hayo kwenye kozi hii

    👉Nitakusaidia UANDIKE kitabu chako na kitakamilika ndani ya siku 30.
    👉Nitakusimamia na kusoma kazi zako unazoandika kila siku na kukuelekeza namna bora ya kuziboresha

    👉Nitakufungulia blogu ya bure.
    👉Utajifunza mengi kutokana na yale wanayoandika wenzako na maoni nitakayokuwa natoa kuhusu kazi za wenzako.
    👉Utapata kitabu Cha JINSI YA KUWA MWANDISHI MBOBEVU NDANI YA SIKU 30 bure.
    👉Utapata jarida lenye hatua 15 za kufuata ili kuandika magazetini.
    👉Utapata mafunzo ya audio zaidi ya 10. Yakiwemo mahojiano na waandishi wakubwa hapa nchini.

    👉Utaungana na waandishi wengine wanaoandika na kujifunza mengi kutoka kwao.

    Nafasi kwenye darasa hili ni 10 tu. Hivyo, kama unataka kuhudhuria darasa hili, sharti uwahi kujihakikishia nafasi yako kabla hazijaisha.

     

    Unaweza kujiuliza kwa nini watu kumi na kwa nini siku 30 tu?

    Naomba sasa usogeze kiti chako karibu ili nikwambie nini kinaendelea. 

    Kwanza nahitaji watu kumi ambao kwangu itakuwa rahisi kuwasimamia na kufuatilia mwenendo wa kila mmoja ndani ya hizo siku 30. Ningeweza kusema watu 100, ila sasa kuwafuatilia watu 100 wote kila siku kwa siku 30 ni ngumu. Ndiyo maana nasema hii ni private masterclass na kila anayejiunga na darasa hili hapa ni V.V.I.P

     

    Sasa ngoja nikujibu kwa nini nimechagua siku 30 na sio siku tano au kumi au 60 au 100.

    Moja ya lengo muhimu kabisa tutalifanyia kazi kwenye darasa hili hapa ni kuhakikisha kwamba unajenga tabia ya kuandika. Yaani, unaufanya uandishi unakuwa sehemu ya pili ya maisha yako.

    Sasa kulingana na utafiti uliofanyika kwenye moja ya chuo kikuu Marekani, tabia mpya huwa inajengwa ndani ya siku 66. Hizi ni siku ambazo unajenga tabia mpya kiasi inafikia hatua ya wewe kufanya kile kitu kama sehemu ya pili ya maisha yako. Hata hivyo utafiti huu unasema kwamba sio kwamba tabia inajengeka siku ya mwisho, yaani siku ya 66. Kipindi hiki cha siku 66 kimegawanyika katika vipengele vitatu.

    Kuna siku 22 za kwanza, zipo siku 22 za pili na siku 22 za tatu. Siku za 22 kwanza huwa ni za kuachana na tabia ya zamani.

    Siku 22 zinazofuata huwa ni za kujenga misingi ya tabia mpya na siku 22 za mwisho huwa ni za kuimarisha tabia mpya.

     

    Sasa kitu kimoja cha kushangaza ni kwamba kuna watu ambao huwa wanawahi kushika tabia mpya mapema na kuna wale ambao huwa wanachelewa. Wanaoshika tabia  mapema huwa inawachukua siku 21 au 22 tu. Ndio maana vitabu vingi vya hamasa utakuta vimeandika kuwa inachukua siku 21 kujenga tabia mpya. Ila kwa utafiti binafsi nilioufanya kwenye suala la uandishi tu. siku 30 zinatosha kabisa kumfanya mtu ambaye hajawahi hata kuandika sentensi kuwa mbobevu. Ndio maana leo hii ninasema kwamba, ninahitaji watu KUMI, nami nitawafanya kuwa waandishi wabobevu ndani ya siku 30. 

     

    Sisi kwenye darasa letu tutakuwa na kitu cha tofauti. Badala ya kutumia siku 66 zilizogwanyika kwenye siku 22-22-22 tutatumia 30 zilizogawanyika kwenye siku 10-10-10..

    Yaani, tutakuwa na siku 10 za mwanzo. Hizi zitakuwa za kujenga tabia ya kuandika. Baadae tutakuwa na siku 11 za pili. Hapa sasa tutaingia ndani kabisa kwenye misingi na saikolojia ya uandishi yenyewe.

     Na hatimaye tutakuwa na siku 11 za mwisho, hizi zitakuwa za kuandika andiko linalojiuza lenyewe. Ndio namaanisha andiko linalojiiuza.

     

    Sasa kwa yeyote atayehudhuria darasa hili atapata kwanza kitabu changu kinachohusu uandishi., sambamba na yote niliyosema hapo juu 

    Atapata mwongozo wa uandishi (huu ni muhimu sana hasa kwa mtu anayeanza na hajawahi kuandika)

     

    Darasa hili litaendeeshwa kwa njia ya whatasap na ili uhudhurie darasa hili hapa utapaswa kulipia laki mbili (200,000) tu. Nikuhakikishie kuwa hiki ni kiasi kidogo sana, sana kulinganisha na kile unachoenda kujifunza kwenye darasa hili hapa. na fedha hii hapa bado una uwezo kuipata wakati wowote wakati darasa linaendelea au baada ya darasa kuisha endapo utaona kwamba hujanufaika na darasa hili. Ndio namaanisha kwamba fedha yako yote utaipata, endapo hutaridhika na darasa au kupata thamani inayoendana na laki mbili baada ya kuwa umehudhuria darasa hili hapa.

    Na utaratibu wa kulipa ni kama ifuatavyo; utatuma fedha kwa 0755848391 jina ni GODIUS RWEYONGEZA, kisha baada ya hapo utanitaarifu ili niweze kukuunga kwenye kundi.

    Ukilipia leo

    • Utapata kitabu cha JINSI YA KUWA MWANDISHI MBOBEVU PAPO HAPO
    • UTAFUNGULIWA BLOGU YAKO LEO
    • UTAPATA JARIDA LENYE HATUA 15 ZA KUFUATA ILI KUANDIKA MAGAZETINI leoleo
    • Tutapanga ratiba kwa pamoja ya mimi na wewe kuongea kwa dakika 15 kwa njia ya simu. Hii ni muhimu kwani itanisaidia kujua nini hasa lengo lako kwenye hizi siku 30 na tutakuwa tukifanya kazi kuhakikisha kwamba linakamilika.
    • Lakini pia utapata Audio 3 Za mwanzo.(HAYA YOTE UNAYAPATA KABLA DARASA HALIJAANZA NA HAPO NDIO KWANZA UNAKUWA BADO HATA HUJAPATA ASILIMIA 10 KILE KITAKACHOKUWA KWENYE KOZI
    • Nitakutumia na mwongozo wa uandishi

     

     Kwa mwaka huu darasa linaanza tarehe 16, machi. Na litadumu kwa siku 30.

     

    Chukua hatua sasa uthibitishe ushiriki wako kwa kulipia laki mbili (200,000/-) kwenda namba 0755848391 JINA ni Godius Rweyongeza. 

     

    Baada ya hapo nitumie ujumbe kunitaarifu kwa namba hiyohiyo.

     Ikumbukwe nafasi ni kumi tu! Zikiisha hakutakuwa na nafasi ya ziada.

     

    Njoo ujifunze uandishi kutoka kwangu, nakuhakishia unaenda kujifunza ujuzi wa kipekee sana kwa namna ya kipekee.

     

    Chukua hatua sasa lipia kwa 0755848391

     

    Kila la kheri

    Godius Rweyongeza

    Morogoro-Tz

     

     Ninahitaji watu kumi nami nitawafanya kuwa waandishi wabobevu ndani ya siku 30 tu!

     

     

     

  • Njia 7 Rahisi Za Kujenga Tabia Zitakazodumu

    Katika familia au maeneo yaliyo mengi muda wa kupata kifungua kinywa, chakula cha mchana au cha jioni unajulikana, muda huo ukifika unakuta majukumu yaliyokuwa yanafanyika yanahairishwa kwa ajili tu ya kukamilisha jukumu la kupata chakula kwa wakati husika.

    Ukifika muda wa chakula hakuna mtu  anayejiuliza mara mbili tatu kwamba aende kula muda huo au la aache. Ila badala yake muda ukifika mtu anaenda kula tu. Sasa kitu kama hiki ndicho kinakosekana kwa watu wanaotaka kujenga tabia mpya.

    1.
    Kama unataka kujenga tabia, tenga muda maalumu utakapokuwa unafanyaia kazi tabia hiyo. Ukishaweka muda pembeni kinachokuwa kimebaki Ni wewe kuonekana eneo la tukio ndani ya huo muda.

    Kwa mfano kama unataka kujenga tabia ya kuandika. Tenga muda wa kuandika, labda saa 11 asubuhi mpaka saa 12 asubuhi.

    Ukifika muda huo, onekana kwenye eneo la tukio. Fungua kompyuta kama unatumia kompyuta na Anza kuandika.
    Inakuwa rahisi kwako kujenga tabia yako kihivyo. Na ndani ya huo muda haupaswi kamwe kufanya kitu kingine tofauti na kile ulichodhamiria. Kama ni kuandika basi utapaswa kuandika hata kama hujisikii.

    USISEME kwamba ngoja niutumie muda huu kufanya kitu kingine halafu baadaye nitaandika. Amua muda huo kwamba nitaandika au la sitafanya kitu kingine.
    Ni bora ndani ya muda huo ukae ukiwa unaingalia kompyuta yako bila kuandika kukiko kwenda kufanya kitu kingine, kitu ambacho najua huwezi.

    Hivyo, utajikuta unalazimika kuandika kitu tu. Wewe andika kitu tu, hata Kama kitu hicho siyo bora ila andika. Muda wako ukiisha, achana na hicho kitu nenda kafanya mambo mengine

    2.
    Kitu cha pili kitakachokusaidia wewe kujenga tabia yako ni mazingira. Yaweke mazingira yako ili yaendane na tabia yako mpya unayotaka.
    Kama unataka kusoma vitabu, Basi tenga eneo maalumu la kusomea vitabu.  Kisha lizungushe eneo hili na vitabu.

    Uliwahi kufanyika utafiti kwenye chuo kimoja Marekani. Kwenye utafiti huo, waliongeza maeneo maji yalipokuwa yanapatikana kwenye mgahawa. Mwanzoni kulikuwa na maeneo mawili  yenye maji. Hata hivyo, baada ya huu utaratibu mpya maeneo yaliongezeka kutoka mawili.

    Yaani, karibia kwenye kila kona ya mgahawa ilikuwa na maji. Kila ulipokaa uliona maji

    Kilichotokea ni kwamba kulikuwa na ongezeko kubwa la watu kunywa maji kuliko ilivyokuwa mwanzo.

    Mwanzoni watu walikuwa wanakunywa soda kwa wingi ila sasa zamu hii unywaji wa maji ukawa umeongezeka.

    Kwa hiyo ikawa imegundulika kwamba ukibadili mazingira unaweza kubadili mengi. Kama unataka kujenga tabia ya kusoma vitabu, zungusha mazingira yako na vitabu vya kutosha. Hii njia unaweza pia kuitumia kuwajengea wanao au familia yako tabia ya kusoma vitabu.

    Badala ya kuwa unanunua movie nyingi, jitoe kununua vitabu vya kutosha, Kisha hakikisha vitabu hivi vipo kwenye maeneo yanayoonekana kwenye familia yako. Hili litawafanya wanze kusoma kidogo kidogo.

    3.
    Njia ya tatu ya kujenga tabia kirahisi Ni kutofautisha vifaa vyako. Hapa unapaswa kuamua kuwa kifaa fulani Ni kwa ajili ya kazi fulani. Kwa mfano, Kama una simu mbili unaweza kuzitenganisha. Moja ikawa maalumu kwa ajili ya kusoma vitabu na kuandika na nyingine ikawa maalumu kwa ajili ya mawasiliano.
    Kwa hiyo inakuwa inajulikana kwamba ukishika simu fulani, hapo moja kwa moja kifuatacho ni kusoma au kuandika tu.
    Ukishika simu nyingine kazi yake ni kuchati na mawasiliano mengine

    4.
    Njia ya nne Ni kuwajulisha watu wako wa karibu juu ya tabia yako mpya. Wambie wajue kabisa kuwa ukikaa kwenye meza fulani hutaki usumbufu. Ndani ya muda huo mambo mengine yaendelee kama ambavyo ungekuwa ofisini au safarini. Usisumbukiwe na mtu yeyote unapokuwa meza au chumba fulani.

    5.
    Njia ya tano ya kujenga tabia mpya kirahisi ni kuwaambia watu ambao watakushirikiria. Unawaambia watu kuwa nitafanya kitu fulani na hivyo kwako inakuwa ni rahisi kutekeleza kile ulichopanga  maana unakuwa unajua kwamva endapo sitafanyia kazi hiki Kitu, Kuna watu watanishikiria.

    6

    Njia ya sita ni ya kutumia zawadi na adhabu. Hapa unaamua kuwa nikifanya na kukamilisha kitu fulani nitajipongeza na nisipofanya nitajiadhibu. Kwa mfano, unaweza kujiwekea utaratibu kuwa kila siku baada ya kukimbia kilomita moja nitakuwa nakunywa glass moja ya juisi fresh. Siku ambayo hujakimbia hakuna kunywa. Hiki Kitu kinaweza kukupa hamasa maana utakuwa unajua kwamba mara tu baada ya kukimbia kilomita moja kuna juisi fresh. Kama nakuona unavyojilamba!!!

    7
    Njia saba ni kutafuta mtu ambaye kazi yake ni kukushikilia wewe. Kwa mfano, unaweza kusema kwamba kila siku nitawapigia wateja 10 kuongea nao kuhusu biashara au bidhaa zilizo kwenye biashara yangu. Ukamshirikisha mtu kitu hiki, na kumwambia endapo sitafanya hivyo nitakulipa kiasi fulani. Hapa kinapaswa kuwa kiasi ambacho kitakuuma wewe kiasi kwamba utajisukuma kufanya hivyo la sivyo usipofanya hivyo utapaswa kulipa faini.

    Niendelee au nisiendelee……

    Mengine utayakuta kwenye kitabu cha NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA. Unaweza kusapoti ukamilishwaji kwa kitabu hiki kilicho jikoni kwa kununua ebook hiyo hapo chini kwa elfu 2 tu
    BONYEZA hapo chini kununua au wasiliana nami sasa kwa 0755848391 ili nikutumie.

    Upendo utawale

    Imeandikwa na GODIUS RWEYONGEZA

  • MITAJI 8 ILIYOKUZUNGUKA NA JINSI YA KUITUMIA

    Kama kuna shida ambayo inawakabili vijana walio wengi kwenye ulimwengu wa leo basi ni kitu kinachoitwa mtaji. Mtaji limekuwa ni tatizo kubwa sana kwa vijana wengi na hata watu wazima, hata hivyo nipende kusema kwamba hakuna sifa yoyote kwenye kutokuwa na mtaji.

    Kuna watu ambao kila mwaka wanalalamika kwamba hawana mtaji, unaweza kukuta kwamba mtu alikuwa analalamika mwaka 2010 kuwa hana mtaji, mwaka 2015 pia alikuwa analalamika na mwaka 2020 bado alikuwa analalamika kuwa hana mtaji na bado ataendelea kulalamika mwaka 2025. Kwa nini, kwa sababu kulalamika kwamba hauna mtaji ni rahisi sana kuliko kujitoa kwa vitendo kuutafuta huo mtaji.

    Kwenye andiko hili ninaenda kukuonesha ni kwa namna gani ambavyo unaweza kuupata mtaji, na ubora mitaji ninayoizungumzia kwenye andiko hili tayari unayo ila tu unaipuuzia, au unaitumia ila sasa hujajua namna ya kuitumia vizuri zaidi kwa manufaa, na hiki ndiyo kitu ambacho ninaenda kueleza.

    Hadithi Ya Mtu Aliyeuza Shamba La Alamsi Kwenda Kutafuta Almasi

    Ujue nikikwambia kwamba tayari mtaji unao unaweza kuona kama vile ni kitu cha ajabu sana, na pengine unaweza kuamua kupuuzia kusoma andiko lililobaki. Binafsi sikulazimishi, ila walau ningependa kukuhakikishia kuwa asilimia kubwa ya mtaji unaouhitaji tayari unao.

    Kabla sijakwambia mitaji hiyo ningependa nikudokeze kidogo hadithi ya mtu ambaye aliishi miaka mingi iliyopita. Mtu huyu alikuwa anaishi maisha mzuri na hakuwa na shida wala kitu chochote kinachomsumbua. Labda alikuwa na changamoto kama ambavyo mimi na wewe tunakutana nazo kila siku.

    Siku moja mtu huyu alitembelewa na mchungaji ambaye alimwambia kwamba ukiwa na almasi inayolingana na kidole chako tu, unaweza kuimiliki dunia nzima. Baada ya mazungumzo hayo mchungaji aliondoka na kwenda nyumbani kwake. Huku yule bwana ambaye alijulikana kama Ali Hafed akiwaza namna ambavyo angeweza kupata almasi iliyolingana na kidole chake tu. Kesho yake bwana Ali Hafed aliuza mali zake na shamba lake, kisha aliikabidhi familia yake kwa jirani yake na kuondoka kwenda kusikojulikana ili kuitafuta almasi. Alianza kuzunguka huku na kule ili kuipata almasi lakini baada ya muda mwingi wa mahangaiko bila kupata chochote fedha yake iliisha, alipata mfadhaiko na hata kuchoka. Baadaye, mtu huyu alikutwa amekufa kandokando ya mto Barcelona nchini Hispania.

    Huku nyumbani kwake alipotoka, shamba lake lilichukuliwa na bwana mpya ambaye siku moja wakati ananywesha mifugo wake aliona jiwe lililompendeza sana kutokana na mg’ao wake. Hivyo aliamua kuondoka na hilo jiwe mpaka kwake. Nyumbani kwake aliliweka hilo jiwe eneo la wazi tu.

    Ingekuwa siku hizi basi tungesema kwamba aliliweka mezani (sebuleni). Sasa ikawa imetokea tena yule mchungaji akawa anapita kwenye lile eneo, alipofika kwa yule jamaa aliyechukua shamba la Ali Hafed alishangaa kuona jiwe ambalo moja kwa moja alilitambua kama almasi, pale pale kwa sauti ya mshangao aliuliza, Ali Hafed karudi?!

    Aliambiwa hapana. Kwa nini unauliza hivyo. Alisema “hii ni alamasi na mimi nikiiona naitambua tu” alisema hivyo huku akionesha kidole chake kwenye jiwe alilokuwa amebeba yule bwana kutoka kule shambani. Kumbe loo, bwana Ali Hafed alikuwa ameuza shamba la almasi kwenda kutafuta almasi kusikojulikana.

    Inawezekana bwana Al Hafed alikuwa analalamika mara nyingi sana kwamba hana mtaji, maisha magumu, vyuma vimekaza na maneno mengine ya aina hiyo wakati akiwa amelalia mtaji mkubwa. Unadhani huyu bwana alikuwa anahitaji mtaji wa fedha?

    Walau kwa hilo tutakubaliana kuwa huyu jamaa alikuwa haitaji mtaji fedha maana alikuwa tayari amezungukwa na almasi za kutosha. Sasa alikuwa anahitaji nini? Ukiniuliza mimi nitakwambia kwamba kilichohitajika kwake ilikuwa ni kufunguliwa tu kiakili. Alihitaji kupata maarifa sahihi ambayo yangemwezesha kujua almasi inafananje tu. Kwa sababu kutokana na hadithi hii tunaona kwamba huyu bwana japo alizunguka kutafuta almasi, ila alikuwa haijui. Laiti angekuwa anajua almasi inavyofanana, asingeuza shamba lake.

    Na hiki kitu tunakiona kwenye jamii yetu. Unaweza kukuta mtu analalamika kwamba anataka mtaji, lakini  muulize kwamba wewe unataka mtaji wa shilingi ngapi na ukiupata utaufanyia nini? Hapo ndipo mtu ataanza kujiuma uma. Sasa mtu wa aina hiyo si sawa na Al Hafed tu!

    Inawezekana bwana Al Hafed aliipita almasi nyingi tu njiani kwenye kuzunguka kwake, lakini kwa sababu tu alikuwa haijui bado aliendelea kuitafuta. Yaani, kama kukimbiza upepo basi huyu bwana alikuwa anakimbiza upepo kweli!

    Na hapa ebu mfikirie mtu ambaye hajui kiwango gani cha mtaji anataka wala hajui anataka fanye nini. ataendelea kulalamika tu kwamba hana mtaji, wakati labda mtaji wake aliokuwa anahitaji ni simu yake tu.

    Dhana Potofu Kuhusu Mtaji

    Moja ya dhana iliyopo kuhusu mtaji ni kwamba, mtaji ni inapaswa kuwa fedha nyingi sana. kwa hiyo kuna watu ambao wanakuwa wanafikiria kwamba ukizungumzia mtaji unakuwa unaongelea mamilioni ya fedha. Labda milioni 50. Kwa wengi ukiongea kwamba nina milioni 200, hapo sasa ndipo watafahamu kuwa kweli una mtaji ila ukiwaambia kwamba una elfu 50, wataona kama masihala vile.

    Labda kitu kimoja kikubwa nilichojifunza kwenye maisha ni kuanza na ulichonacho ili kufanya kinachowezekana kwa wakati huo. Kabla hujafanya yasiyowezekana unapaswa kuwa tayari kuanza kutumia kile ulichonacho kwanza.

    Ukiwa Mwaminifu Kwenye Mambo Madogo Utaaminika Kwenye Makubwa Pia

    Kwenye Biblia kuna mfano ambao unajieleza vizuri tu. mfano huu ni wa bwana mmoja ambaye alikuwa anataka kusafiri na kwenda safari ya mbali. Kabla ya kusafiri huyu bwana aligawa mali zake kwa watu watatu. Mmoja alimpa talanta tano, mwingine alimpa talanta mbili na mwingine akampa moja. Yule aliyekuwa na talanta tano na yule wa mbili walizizalisha vizuri tu na kuziongeza mara dufu yake, ila huyu wa talanta moja akawa ameichukua na kuizika. Mpaka bwana wake aliporudi ndipo jamaa akaanza kulalamika kwa kumwabia bwana wake kwamba, nilijua kuwa wewe unavuna usipopanda na maneno mengine…wenzake waliokuwa wametumia vizuri zile talanta, bwana wao alipokuja aliwasifia kwa kuwambia, vyema mtumishi mwenye haki, umekuwa mwaminifu kwenye mambo madogo utakuwa mwaminifu kwenye mambo makubwa pia.

    Huwezi kuaminiwa fedha nyingi wakati kile kidogo ulichonacho kinakushinda kukitunza.

    Najua kwamba watu wengi wanapenda kupata fedha nyingi za mtaji, ila wanashindwa kutumia zile kidogo walizonazo. Huwezi kuaminiwa na kupewa fedha nyingi wakati zile kidogo zinakushinda tu. anza kutumia vizuri kwanza zile fedha kidogo ulizonazo ili uweze kuaminiwa na kupewa fedha nyingi zaidi ya hizo hapo. kuwa mwaninifu kwenye mambo madogo kwanza kabla hujakabidhiwa mambo makubwa

    Hata mtu au bashara ikienda kukopa benki huwa haipewi fedha zaidi ya vile inavyoweza kulipa. Kwa nini? kwa sababu,inapaswa kuonesha kwanza kile kile kiasi kidogo inaweza kutumia vizuri na kukikuza zaidi ya hapo. Maana kuna watu wakipata fedha zaidi ya vile wanavyostahili ni kama wanarukwa na akili zao. Kuwa mwaminifu kwanza kwenye mambo madogo, utakabidhiwa makubwa. anza kuwa mwaminifu kwa kile ulichonacho leo hii

    Inawezekana jamaa aliyepewa talanta moja kwenye biblia alikuwa analalamika pia kuwa hana mtaji. Pengine kwa kuona wenzake waliopewa talanta tano kwa mbili, aliamua kususa kuitumia haya hiyo moja.

    La leo hii ukiambiwa talanta moja ni sawa na shilingi ngapi, unaweza kuona kwamba huyu jamaa alikuwa amepewa mtaji mkubwa tu ambao hakuutumia. Nikwambie talanta moja ni sawa na shilingi ngapi?

    Kadiri ya mtandao wa Wikipedia, kwa viwango vya sasa hivi, talanta moja ni sawa na dola milioni moja na laki nne. Ambazo ukiziweka kwenye fedha za Tanzania zinafika bilioni 2 na zaidi. kumbe huyu jamaa alipewa utajiri mkubwa sana, ila hakuutumia.

    Ninachotaka kukwambia leo hii ni kwamba na wewe unao utajiri mkubwa sana, kuliko ambavyo unafirikia, kuna mitaji uliyonayo ila huitumii na sasa wacha tuanze kuiona…

    N.B. Ili kuendelea kusoma mpaka mwisho, utapaswa kupata ebook hiyo hapo chini kwa shilingi elfu 2 tu badala ya shilingi elfu 3. Lipia kwa 0684408755 jina ni GODIUS RWEYONGEZA. Ukishalipia, utatumiwa ebook hiyo kwa whatsap.

    Kupata eBook hii bonyeza hapo chini au wasiliana nami kwa 0755848391

    Kama unataka kupata ebook kama hiyo bure kila mwishoni mwa wiki. Basi Bonyeza Hapa

  • Hiki Kitu Nilichoambiwa Kuhusu Wewe Ni Cha Kweli?

    Hivi ni kitu gani huwa kinakupa furaha na kupata hali ya ukamilifu kwenye maisha yako?
    Mwaka 2013 chuo kikuu cha North Carolina kwa ushirikiano na watafiti wa UCLA. Walifanya utafiti na kugundua kuwa moja ya kitu kinachowafanya watu furaha ni ile hali ta kukamilisha jukumu au kitu ambacho mtu amekuwa anatamani kufanya kwa siku nyingi.


    Looh, ebu fikiria ni kitu gani umekuwa unatamani kufanya na kukamilisha? Ni kitu gani kipo ndani yako ambacho unatamani ungekifanya na kukikamilisha?
    Je, ni kuandika kitabu?
    Waandishi wengi wa vitabu wameripoti kujisikia huru na kuwa na ile hali ya kuwa kuna jambo wamelitiza baada ya kuandika kitabu.

    Kwa wengine kuandika kitabu kunawapa utambulisho mpya na kuwafanya sasa waonekane ni viwango fulani.
    Hii ni kutokana na ukweli kuwa ukimwambia mtu nimeandika kitabu. Anachukulia hilo suala kwa umakini mkubwa. Anakuweka kwenye viwango vingine. Unakuwa mwandishi kweli kweli maana kuna watu wanajiita waandishi huku wakiwa hawajahi hata kuandika makala fupi tu.


    Hivi wewe kitabu chako ndio utakiandika lini? Utakikamilisha lini na kukitoa?
    Natamani mwaka huu nione kitabu chako kikiwa kimekamilika. Na ninaweza kukusaidia katika hili la kuandika kukamilisha kitabu chako mwaka huu. Ninaweza kukushika mkono kwa kukupa mbinu na taratibu za kufuata mpaka ukamilishe kitabu chako. 


    Siyo Hilo tu, changamoto nyingine ya waandishi ni kuandika vitabu visivyouzika. Mwandishi unakaa navyo kabatini… Kwa lugha yetu vijana tunasema, UNAPIGA NAVYO PICHA….Hilo nalo lina suluhisho lake.
    Kama ungependa nikushike mkono kwenye kuandika kitabu chako. Basi karibu kwenye darasa rasmi la uandishi mwaka 2022. Darasa hili ni la kimtandao na litafanyika kwa njia whatsap. Ndani yake utapata mafunzo ya kina ya kuandika.

    👉UTAANDIKA kitabu chako na kitakamilika ndani ya siku 30.
    👉Nitakusimamia na kusoma kazi zako unazoandika kila siku na kukusaidia kuziboresha.
    👉Nitakufungulia blogu ya bure.
    👉Utajifunza mengi kutokana na yale wanayoandika wenzako na maoni nitakayokuwa natoa kuhusu kazi za wenzako.
    👉Utapata kitabu Cha JINSI YA KUWA MWANDISHI MBOBEVU NDANI YA SIKU 30 bure.
    👉Utapata jarida lenye hatua 15 za kufuata ili kuandika magazetini.
    👉Utapata mafunzo ya audio zaidi ya 10. Yakiwemo mahojiano na waandishi wakubwa hapa nchini.

    👉Utaungana na waandishi wengine wanaoandika na kujifunza mengi kutoka kwao.Nafasi kwenye kozi hii ni 10 tu. Hivyo, kama unataka kuhudhuria kozi hii, sharti uwahi kujihakikishia nafasi yako kabla hazijaisha.

    Na gharama za kuhudhuria darasa hili la kipekee itakuwa ni laki mbili (200,000/) tu. Jihakikishie nafasi yako Sasa hivi kwa kuwasiliana na 0755848391 kabla nafasi hazijaisha.

    NAKUKUMBUSHA TU: kozi hii ni ya siku 30 tu, na huna kitu chochote cha kupoteza. Endapo utajiunga na kozi hii ila katikati mwa kozi au mwishoni ukaona kuwa haifai, utanipigia simu nami nitakurejeshea fedha yako bila kukuuliza maswali yoyote.Hivyo, jisajili sasa hivi kwa kuwasiliana na 0755848391.

    Au BONYEZA HAPA  kuwasiliana nami sasa hivi

  • Jinsi ya kufanyia wazo majaribio kwenye soko

    Nakumbuka nikiwa mwaka wa kwanza wa masomo yangu ya shahada ya kilimo cha bustani, nilikuwa napenda sana kupiga hesabu za mazao mbalimbali ya kilimo na baadhi ya rafiki zangu kwa wakati huo. Kila tulipokuwa tukikaa na kupiga hesabu za zao fulani, ilikuwa inaonekana faida tu, tena faida kubwa sana. Nakumbuka kwa mfano siku moja tulipiga hesabu za kilimo cha nyanya,

    • gharama za kuweka zikawa kama milioni nne na nusu,
    • hlafu fedha yote iliyokuwa inapatikana baada ya mauzo ilikuwa ni milioni saba na nusu hivi,
    • ulipokuwa ukitoa gharama zote ulikuwa unabaki na kama milioni tatu au milioni na mbilinusu hivi.

    Hizo zilikuwa ni hesabu za kwenye karatasi, “tena unapata hela yako ndani ya miezi mitatu tu”, tulikuwa tunajiambia. Ukipiga hesabu hizo na kuona fedha inavyopatikana unaweza kesho yake kuamkia benki kuwaambia wakupe mkopo wa milioni tano, kwa uhakika kuwa utarudisha hela yao na ya ziada ndani ya miezi mitatu tu.

    Usicheke kuna jamaa baada ya kupiga hesabu kama hizi alienda baa kujipongeza kwanza, akawa amekunywa fedha yote ikaishia huko…Tutacheka baadaye ngoja tuendelee kwanza.

    Kama umewahi kuwa na wazo lolote lile maishani, utakuwa unakubaliana nami kuwa wazo ni kitu kimoja na kulifanyia na kuliweka kwenye uhalisia ni kitu kingine. Mara nyingi ukiwa na wazo la biasahra utakuta kwamba kinachokuja kwenye akili yako kwanza ni upande wa faida, unafikiri na kuona ni kwa namna gani utapata faida, unaona kwamba ukifanyia kazi wazo lako na kufanya kitu fulani na kitu fulani muda siyo mrefu utakuwa uemeweza kutengeneza fedha nyingi sana.

    Lakini sasa ajabu ni pale unapoamua kuingia kwenye ulingo wa kufanyia kazi kile ambacho umeamua kufanyia kazi, hapo ndipo utakutana na uhalisia. Mambo mengi ambayo hapo mwanzo hukuyatarajia yatatokea. Ndiyo maana wahenga wanasema kwamba utamu wa ngoma sharti uingie ucheze.

    Ukifuatilia takwimu za kibishara zinaonesha kwamba asilimia 5 tu ya biashara huwa zinaendelea kuwepo baada ya mwaka mmoja. Yaani, kama zikianzishwa biashara 100 biashara 95 huwa zinakufa ndani ya mwaka mmoja na ni biashara tano tu ndizo huwa zinaweza kuendelea baada ya kipindi hicho.

    Unajua kwa nini?

    Kuna sababu nyingi sana ambazo zimetolewa kuelezea jambo hili hapa ila mojawapo ya sababu ambazo unapaswa kuifahamu ni kuwa ni rahisi kuwa na wazo ila unapoanza kulifanyia kazi ndio unaona uhalisia wa kitu hicho na hapo ndipo watu wengi huwa wanakimbia. Unaweza kuona kwamba ukitengeneza bidhaa fulani itakuwa yenye manufaa na kuwasaidia watu, ukipiga hesabu za kwenye karatasi unaona unaenda kupata hela nyingi sana ila sasa ingia mchezoni uone…

    Asa ufanyeje unapokuwa na wazo/

    KITU CHA KWANZA KABISA NI KULIFANYIA KAZI.

    Ukiwa na wazo, hakikisha kwamba unalifanyia kazi na kuliweka kwenye uhalisia. Kwa vyovyote vile hata kama bado hujawa anza kulifanyia kazi. utajifunza mengi zaidi kadiri utakavyokuwa unalifanyia kazi kuliko pale ambapo utakuwa hujalifanyia kazi.

    Kwa mantiki hii nitachukulia kuwa una wazo la kuandika kitabu au kuwa mwandishi mbobevu. Unafanyaje? Kitu cha kwanza ni wewe kuanza kulifanyia kazi wazo lako la kuandika. Anza kuandika hata kama ni makala fupi na kuziweka mtandaoni. Fungua blogu na weka makala zako huko. Usisubiri mpaka uwe tayari, wewe anza tu.

    Mpaka hapo umeshafaulu

    PILI Pata mrejesho na ufanyie kazi

    Kadiri utakavyokuwa unafanyia kazi wazo lako watu wataanza kukupa mrejesho, kuna wale ambao watakuuliza maswali. Kuna ambao watataka kujua zaidi kuhusu kitu fulani, na mengineyo. Pokea hiyo mirejesho na kisha ona ni kwa namna gani unaweza kuifanyia kazi.

    Kwa mfano wetu wa wewe unayetaka kuwa mwandishi, pale ambapo utakuwa umeanza kuandika kwenye blogu, watu wataanza kuuliza maswali, haya maswali utakuwa ukiyajibu na utaona kwamba kuna aina fulani ya maswali yanaulizwa zaidi. Utayafanyia kazi hayo maswali na hata kutengeneza kitabu chako.

    Hapo sasa utakuwa umejibu maoni ya wasomaji wako kitalaam.

    TATU; Kusanya mawasiliano ya watu ambao wanaweza kuwa wateja wako wa wa kwanza. Kama unaandika ni rahisi sana, unaweza kutengeneza mfumo wa barua pepe wa kupokea makala ambapo watu wanajiandikisha ndipo wanapata makala hizo .

    NNE, tengeneza bidhaa kisha ijaribishe kwa watu wachache wa kwanza

    Baada ya kuwa umeanza kufanyia kazi wazo lako na kupata mrejesho, sasa kifuatacho ni wewe kutengeneza bidhaa kulingana kile ambacho umekuwa unafanya sasa kwa muda. Na bidhaa hiii unaweza kuitengeneza kulingana na maswali ambayo watu wamekuwa wanakuuliza kwa wingi sana. kwa hiyo kama sehemu ya kujibu maswali haya hapa tengenez bidhaa yenye suluhisho.

    Na vile ulishakuwa na orodha ya watu ambao unaweza kuanza kuwaauzia sasa unaweza kuwattumia hawa watu

    TANO, uza bidhaa kwa watu wengi zaidi

    Sasa baada ya kuwa umefuata hizo hatua zote hapo juu kifuatacho ni wewe kuhakikisha unaenda mbali na kuuza bidhaa yako kwa watu wengi zaidi. na hapa unaweza kwenda mpaka kuanza kuitangaza bidhaa yako kwa watu wengine zaidi

    Kama unavyoona, hizo ni hatua muhimu unazopaswa kufuata kulitoa wazo katika wazo na kulileta uhalisia. Hatua hizi zinatekelezeka, ni jukumu lako sasa kuhakikisha kwamba umeziweka kwenye uhalisia.

  • Kama kweli umejitoa na unataka kujifunza kwa kina kuhusu uandishi, BASI SOMA HAPA

    Mwaka 2016 nilipoanza kuandika ulikuwa ni mwaka ambao niliamua na kujitoa kuwa ninaenda kujifunza kwa kina kabisa kuhusu uandishi. Tokea mwaka huo nimejifunza na kusoma vitabu vingi kuhusu uandishi. Nimesoma makala za kutosha kuhusu uandishi. Siyo hilo tu, nimefanyia kazi vitu vingi nilivyosoma na kuviweka katika matendo kwa kuandika vitabu 17 makala zaidi ya elfu mbili. nimeandika kwenye magazeti makubwa hapa nchini na mambo mengine mengi.

    Nimeitumia kila nafasi niliyoipata kuhudhuria semina na kozi zote fupi na ndefu ili kujifunza mambo kadha wa kadha kuhusu uandishi.

    Katika kufanya haya yote nimekusanya maarifa ambayo huwezi kuyapata sehemu nyingine yoyote kwa pamoja, ni maarifa ya kipekee ambayo siyo tu kwamba nimeyakusanya na kuyaweka sehemu, bali mimi mwenyewe nimeyafanyia kazi katika mchakato mzima wa kuandika na kuchapa vitabu vyangu.

    Kila nilipochapa kitabu kimoja, nikawa najifunza na kusoma zaidi ili kujua namna ya kuboresha kitabu kitakachofuata. Kila niliochapa toleo la kwanza nikawa nazama tena ndani ili kujifunza namna nitakavyoboresha toleo la pili.

    Kwa jinsi hiyo basi nimeweza kujifunza mambo mengi kwa kipindi hicho kuliko kawaida.

    Na sasa nipo tayari kukushirikisha wewe maarifa haya kuhusu uandishi wa vitabu kwenye DARASA maalumu litakalofanyika mtandaoni kuanzia tarehe 16. Machi mwaka huu.

    SOMA ZAIDI: Karibu Kwenye Darasa Rasmi La Uandishi Mwaka 2022

    SOMA PIA: KWA NINI UNAPASWA KUHUDHURIA DARASA RASMI LA UANDISHI MWAKA 2022

    Gharama ya kuhudhuria darasa hili hapa ni laki mbili (200,000) na hapa ninataka niseme kitu, maana kuna watu ambao wanafikiri kwamba nimeweka gharama kubwa sana, pengine na wewe unafikiri hivyo.

    Binafsi nimekuwa nikiwekeza kwenye kujifunza uandishi kwa nguvu zote kama vile maisha yangu yote yanategemea uandishi. Sisemi hivyo ili ujue kwamba nimewekeza hela nyingi. Potelea mbali…

    Kitu kikubwa ninachotaka ujue ni kwamba kuna madini ya pekee unayoenda kupata kwenye hii kozi kuliko ambavyo unaweza kupata kwenye kozi nyingine au kitabu kingine. Darasa hili ninalokwambia lina mkusanyiko na muunganiko wa maarifa ambayo nimeyakusanya kwa kipindi cha miaka mitano sasa.

    Kwa hiyo unaenda kupata uzoefu wa miaka yote mitano ukiwa tayari umechakatwa na kuwekwa pamoja ndani ya siku 30 tu. Hiki ni kitu cha kipekee sana.

    Naomba unisikilize mimi kwa kitu hiki, kama utaamua kuanzia leo hii kuanza kukusanya na kujifunza kitu kimoja baada ya kingine peke yako, maana yake itakuchukua wewe miaka mitano kujua haya yote ambayo ninaenda kukufundisha ndani ya siku 30 zijazo. Na hapa ni kama tu utaupa uandishi kipaumbele kama ambavyo huwa naupa kipaumbele.

    Kuna watu huwa wanasema kwamba makala zako zinavutia na unajua kuzipangilia… nawakaribisha tukutane kwenye darasa hili hapa maana unaenda kujifunza siri zote za uandishi kwenye hili darasa

    Kama sasa umeamua kwamba hili darasa sitaki linipite, njoo tufanye kazi uone jinsi utakavyojifunza mambo mengi na ya kipekee sana…

    Ubora ni kwamba hauna kitu cha kupoteza. Ukilipia laki mbili (200,000) halafu katikati ya kujifunza au baada ya darasa kuisha ukaona fedha uliyotoa na kile ulichojifunza haviendani, utakuwa huru kuomba kurudishiwa fedha yako NA UTARUDISHIWA. Nasisitiza tena kwamba fedha yako yote utarudishiwa, tena bila kuulizwa maswali yoyote.

    Kama kweli umejitoa na unataka kujifunza kwa kina kuhusu uandishi, basi tuwasiliane sasa kwa 0755848391.

    Au bonyeza tu HAPA kuwasiliana nami kwa haraka zaidi.

    Unaweza kuanza kulipia kidogokidogo kuanzia sasa hivi ila mwisho wa kulipia ni tarehe 10.3.2020.

    Kama unahisi kabisa huwezi kulipia gharama za darasa hili au zimekuwa kubwa kupitiliza, basi utaniambia nitajua kitu gani cha kukusaidia.

    Karibu

    BONYEZA HAPA kuwasiliana na mimi kwa haraka. BONYEZA HAPA

    SOMA ZAIDI: Karibu Kwenye Semina Rasmi Ya Uandishi Mwaka 2022

    PATA KITABU CHA BURE

    Umekuwa nami rafiki yako wa ukweli

    Godius Rweyongeza

    +255755848391/ Morogoro-Tanzania

X