Notice: Function WP_Interactivity_API::_process_directives was called incorrectly. Interactivity directives failed to process in "" due to a missing "DIV" end tag. Please see Debugging in WordPress for more information. (This message was added in version 6.6.0.) in /home/songambele/public_html/wp-includes/functions.php on line 6085
Home - SONGA MBELE

Home


  • Namba Zetu Za Malipo

    Namba za malipo ya vitabu:

    Namba za lipa

    TIGO PESA: 19016638 Jina ni SONGAMBELE CONSULTANTS

    M-PESA: 5564517 jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

    Namba za kawaida

    AIRTEL MONEY: 0684408755
    TIGO PESA: 0655 848 392
    M-PESA: 0745 848 395

    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    NB: Kama namba ya malipo anatumiwa mtu ambaye yuko nje ya nchi. Iandikwe Kwa kuanza na +255

    Kwa hiyo namba zinazotumwa nje ya nchi zitakuwa
    Airtel money: +255 684 408 755
    TIGO PESA: +255 655 848 392
    M-PESA: +255 745 848 395

    KOTE Jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Kama malipo yatakuwa yanafanyika kupitia benki.

    Yafanyie kupitia

    1. CRDB BANK: 0150770710200
    2. NMB BANK: 22110047274

    Kote jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

  • Wasiliana na Godius Rweyongeza Sasa

    Habari yafuatayo ni mawasiliano Unayoweza kutumia kumpata GODIUS RWEYONGEZA

    Simu: +255 (0) 684408755

    Whatsap: +255 (0) 755848391

    Email: songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu vyake wasiliana Moja kwa Moja na +255 (0) 684408755 (more…)

  • KITABU: JINSI YA KUONGEZA THAMANI YAKO: Njia Za Uhakika Zitakazokufanya Ulipwe Mara Kumi Zaidi ya Unavyolipwa Sasa

    Sisi binadamu ni viumbe ambao tunapenda kuthaminiwa, kuheshimiwa na tunataka watu watambue uwepo wetu. Ukienda kwenye mkutano au kwenye sherehe fulani, wakiwatambulisha watu wote halafu wakakuacha wewe bila kukutambulisha, ni wazi utajisikia vibaya na pengine utasema kwamba wamekudharau.

    Au ukienda sehemu watu na wote wakapewa vinywaji na chakula, halafu ukasahaulika wewe, ni wazi kuwa wewe mwenyewe utang’aka. Ila upande mwingine wa shilingi, ni kuwa ukienda sehemu watu wakatambua uwepo wako, wakakupa heshima zote. kama ni vinywaji wewe ukapewa kwa kipaumbele, utafahamu kuwa hawa watu wamenithamini, na pengine utataka na wengine wajue hilo.

    Thamani ni kitu muhimu sana ambacho unahitaji kuwa nacho.

    Kwenye kurasa za kitabu hiki unaenda kujifunza namna ambavyo unaweza kuongeza thamani yako zaidi.

    Mbinu unazoenda kujifunza kwenye kitabu hiki zitakusaidia kuongeza thamani yako mara mbili mpaka mara kumi zaidi.

    Naomba nieleweke kwamba ninaposema kuongeza thamani yako simaanishi kwamba, utaongeza thamani kwa kuwa mrembo zaidi. Wala simaanishi kwamba utaongeza thamani kwa kupata followers zaidi mtandaoni, na wala simaanishi kwamba unaongeza thamani yako kwa kuwa mrefu, mfupi, mtu wa miraba minne, mweusi, mweupe au maji ya kunde! Endapo hayo yatatokea, basi tutashukuru pia kuwa yametokea.

    Bali haswa namaanisha kuongeza thamani yako kwa kulipwa zaidi. Ukitumia mbinu zilizoainishwa kwenye hiki kitabu, utakuwa na uwezo wa kulipwa mara mbili mpaka mara kumi zaidi. Hivi kwa mfano, unaanzaje kuacha kutumia mbinu hizi ili uweze kulipwa zaidi ya unavyolipwa sasa hivi?

    Gharama ya kitabu hiki ni 20,000/- kupata nakala yako. Tafadhali wasiliana nami kwa 0755848391 ili niweze kukutumia nakala yako

  • KITABU KIPYA: JINSI YA KUONGEZA THAMANI YAKO

    Rafiki yangu mpendwa

    Salaam,

    Moja ya kitu muhimu sana unachopaswa kukifanyia kazi kwenye maisha yako ni thamani yako. Ila kwanza labda tujiulize thamani ni nini? Ili tujue maana halisi ya thamani nimelazimika kuangalia kwenye kamusi ya Kiswahili sanifu, ambayo inasema Kuwa thamani ni gharama au ubora wa kitu kutokana na hali na kuhitajika kwake na jamii.

    Sawa hiyo ni maana ya thamani, na je, ipi itakuwa maana ya thamani binafsi. Thamani yako tunaweza kuiona kwa kuangalia vitu viwili muda na kiasi cha pesa unacholipwa ndani ya huo muda. Kwa mfano, kuna mtu kwa siku anaingiza kipato cha milioni kumi. Wakati kuna ambaye anaingiza kipato cha laki moja. Na wakati huohuo kuna ambaye hata elfu kumi hapati.

    Kumbe hawa watu watatu thamani yao binafsi haiwezi kuwa moja. Pengine unajiuliza, imekuwaje mimi nimeamua thamani ya mtu ipimwe kwa kiwango cha fedha anachoingiza. Ukweli ni kuwa siyo mimi niliyegundua hili. Hiki ni kitu ambacho watu wengi wamekuwa wanakitumia kutoa thamani kwa watu, na hata kwenye familia nyingi mtu mwenye pesa anathaminiwa sana kuliko ambaye hana fedha.

    Vikiitishwa vikao vya familia, kama kuna kuna watu wawili, mmoja mlevi mlevi na mwingine ni mtu ambaye anafanya biashara na ana kipato kizuri. Ikitokea mlevi akachangia kitu, watu watasema huo ni ulevi hata kama kaongea pointi ya maana, ila mwenye hela hata akiongea pumba, anaonekana ameongea pointi na hata kupigiwa makofi. Chezea hela wewe! Mtu mwenye hela yake anaitwa bosi mkubwa hata kama ni mdogo. Hahaha.

    Sasa kwa kwa vile tunaishi kwenye dunia ambayo inathamanisha watu hivyo, hatuna budi kujua hili ili tuongeze thamani zetu au wewe unasemaje? Wewe pia unapaswa kujua thamani yako kwa sasa hivi, lakini pia unapaswa kufanya juhudi ili kufanya thamani yako iongezeke zaidi.

    Mbinu unazoenda kujifunza kwenye kitabu hiki zitakusaidia kuongeza thamani yako mara mbili mpaka mara kumi zaidi. Yaani, utaweza kulipwa mara mbili mpaka mara kumi zaidi ya unavyolipwa sasa hivi. Kumbe basi naomba nieleweke kwenye suala moja tu, ninaposema kwamba unaenda kujifunza mbinu za kukusaidia wewe kuongeza thamani yako. Simaanishi kwamba, utaongeza thamani kwa kuwa mrembo zaidi. Wala simaanishi kwamba utaongeza thamani kwa kupata followers zaidi mtandaoni, na wala simaanishi kwamba unaongeza thamani yako kwa kuwa mrefu, mfupi, mtu wa miraba minne, mweusi, mweupe au maji ya kunde!

    Bali namaanisha kuongeza thamani kwa kulipwa zaidi. Ukitumia mbinu zilizoainishwa kwenye hiki kitabu, utakuwa na uwezo wa kulipwa mara mbili mpaka mara kumi zaidi. Hivi kwa mfano unaanzaje kuacha kutumia mbinu hizi ili uweze kulipwa zaidi ya unavyolipwa sasa hivi.

    Kabla hatujazama zaidi kwenye kitabu, ngoja kwanza tuone namna unavyoweza kujua thamani ya muda wako kwa sasa

    Jinsi Ya Kujua Thamani Ya Muda Wako

    Mimi na wewe tuna bahati ya kuwa na rasilimali nyingi ambazo tunaweza kutumia kwenye maisha yetu ya kila siku.

    Rasilimali hizo ni kama

    • Ardhi
    • Madini
    • Maji
    • Fedha
    • Muda ……

    Kati ya hizo rasilimali zote, muda ndio rasilimali ambayo ukiipoteza huwezi kuipata. Hivyo, unahitaji kuweza kuitumia vizuri rasilimali hii ya kipekee.

    Na leo nataka nikwambie namna ambavyo unaweza kujua thamani ya muda wako. Kujua thamani kutakusaidia zaidi kuwekeza nguvu zako kwenye kufanya kazi na majukumu ambayo ni ya muhimu, huku ukiachana na majukumu ambayo siyo ya muhimu

    Ili tujue thamani ya muda wako, kwanza unapaswa kujua kiasi gani unataka kuingiza kwa mwaka mmoja ujao. Ebu kwa mfano tuseme kwamba una mpango wa kuingiza milionoi 100. (Hiki kitu tukiite A)

    Kitu cha pili cha kujiuliza ni muda kiasi gani ambao uko tayari kufanya kazi kwa wiki? Kama kwa siku unafanya kazi kwa saa 15 na kwa wiki unafanya kazi kwa siku sita. Maana yake kwa wiki unafanya kazi kwa saa 90 (Hiki kitu tukiite B).

    Na kitu cha tatu ambacho tunataka tujue ni je, kwa mwaka utakuwa tayari kufanya kazi kwa wiki ngapi? Kwa kawaida mwaka una wiki 52. Sasa ni wiki ngapi utakuwa tayari kufanya kazi ukiondoa wiki za mapumziko. Kama unapumzika kwa mwezi mzima kwa mwaka, maana yake unafanya kazi kwa wiki 48 tu kwa mwaka (hiki kitu tukiite C).

    Sasa kifuatacho, ngoja tuone thamani ya muda wako kwa kutumia vipengele hivyo hapo juu. Kujua thamani ya muda wako utachukua.

    Thamani ya saa lako moja= (A÷B÷C)

    Kwa hiyo kama una mpango wa kuingiza milioni 100 (100,000,000) kwa mwaka na upo tayari kufanya kazi kwa saa 90 kwa wiki kwa wiki 48. Hivyo,

    Thamani ya saa lako moja=(100,000,000÷90÷48)=23,146

    Kwa hiyo wewe thamani ya saa moja kwako ni sawa na 23,148. Ukifanya kazi yoyote ambayo ni ya chini ya hivyo viwango, basi unakuwa umejishusha.

    Kama ulikuwa hujawahi kupima thamani ya muda wako, Ebu fanya hivyo siku ya leo. Utajifunza vitu vingi na kikubwa zaidi ni kwenye utunzaji mzuri wa muda wako ili kazi unazofanyaa ziendane na viwango vya thamani yako.

    Lakini ubora ni kwamba unaweza kuongeza thamani ya saa lako moja kutoka kiwango cha chini na kukipandisha juu kabisa.

    Hakuna kiwango cha ukomo wa thamani ya muda wako unachoweza kutengeneza

    Sasa wacha tuzame ndani zaidi kwenye hiki kitabu ili uweze kuona ni kwa namna gani unaweza kuongeza thamani yako hatua kwa hatua. Mbinu unazoenda kujifunza kwenye hiki kitabu ni mbinu ambazo wanatumia watu wanaolipwa kiwango kikubwa cha fedha kwa siku, wiki na mwezi. Ubora ni kuwa mbinu hizi ukizitumia wewe mwenyewe unaenda kupata matokeo makubwa ambayo hata hapo awali ulikuwa hujafikiria kuwa unaweza kuyapata.

    Miaka kadhaa iliyopita nilikuwa namsikiliza Les Brown, kwenye yale maongezi akawa anasema kwamba alipokuwa anaitwa kwenye semina alikuwa analipwa dola elfu moja kwa kila maongezi. Ila sasa siku moja katika kuongea na baadhi ya watu waliokuwa wanatengeneza kiasi kikubwa zaidi ya hapo, walimwambia kuwa unaweza kulipwa zaidi ya hapo. Wakamwambia kuwa badala ya kulipwa dola elfu moja unaweza kulipwa mpaka dola elfu tano kwa saa moja. Les Brwon anasema kwamba hiki kitu kilimpa hofu kwanza, lakini baadaye alipoanza kukifanyia kazi, kitu hiki kikaleta matokeo makubwa akawa ameanza kulipwa hicho kiasi na baadaye akaweza kulipwa zaidi ya hapo.

    Ninachotaka kukwambia ni kuwa, unaweza kulipwa zaidi ya unavyolipwa sasa hivi. na mbinu zilizoainishwa kwenye hiki kitabu zinajieleza waziwazi tu.

    Wasalaam,

    Godius Rweyongeza

    0755848391

    Morogoro-Tz

    24 Agosti, 2022.

    Gharama ya kitabu hiki ni 20,000/- hardcopy.

    Kitabu hiki ni 20,000/-. li kupata kitabu hiki, wasiliana nami kwa 0755848391 sasa ili nikutumie popote pale ulipo.

  • Umuhimu wa kuwa na pesa ya dharula

    Chukulia kwamba unaenda Bukoba, umepanda Basi la umma. Ila unapofika Nyakanazi au Biharamulo gari linakata Moto. Katika hali ya kawaida kitakachofuata Ni wewe kutafuta Usafiri mwingine, hapa kama hauna fedha ya dharula, Ni wazi kuwa utaingia choo ambacho siyo sahihi.

    Tena bora safari yako iwe inaishia Biharamuro, Ila kama unaenda Bukoba mjini, Karagwe-Kaisho, hapo safari yako itakuwa bado sana. Ni kweli utakuwa umeshaingia ndani ya manispaa ya Bukoba ila kwa upande mwingine utakuwa bado hujaweza kufika mbali

    Fedha ya dharula Ni Nini?
    Fedha ya dharula Ni Ile fedha ambayo unakuwa nayo kama akiba kwa ajili Jambo lolote ambalo hukutuzamia kutokea. Endapo litatokea hili Jambo ambalo hukutuzamia litatokea, Basi hiyo fedha ya dharula itatumika.

    Mfano unaweza kuwa unatazamia safari itachukua saa nne. Lakini safari ikachukua saa mara mbili zaidi ya kile ulichotazamia. Kunaweza kusiwe na gharama za ziada kwa upande wa  usafiri, lakini ukakuta zipo gharama zaidi upande wa chakula, vinywaji n. K.

    Na hii gharama ya ziada ndiyo itafanya kazi.

    Je, kuwa na fedha ya dharula si kufikiri hasi?
    Unaweza kuwa unajiuliza, hivi nikiwa na fedha ya dharula si nitakuwa nafikiria hasi wakati Mimi napaswa kuwa nafikiri chanya mara zote?

    Kuwa na fedha siyo kufikiri hasi. Bali Ni kufikiri katika uwekezekano (possibility thinking).
    Hizi dharula huwa zinatokea katika biashara, hizi dharula zipo hivyo, ni jukumu lako wewe  kuhakikisha unajiandaa nazo.

    Kutojiandaa na dharula ni sawa na kukwepa ngumi ya uso kwa kufumba macho.

    Dharula hutokea maishani
    Dharula huwa zinatokea maishani. Inaweza kuwa ni mfanyakazi unayemtegemea vizuri sana kuacha kazi au kuumwa na hivyo wewe kwa upande mwingine ukakwama.

    Inaweza kuwa ni kifaa unachokitegemea kuzima ghafla. Mfano mimi Ni Mwandishi, na huwa natumia kompyuta kwenye uandishi. Lakini changamoto ambayo huwa nakutana nayo kwenye uandishi Ni kuwa Kuna wakati kompyuta inaweza kukuchezea na kukataa kuwaka. Au siku hiyo simu ikawa kama imeingiwa na pepo wachafu.

    Sasa katika mazingira kama haya kama hauna kifaa kingine cha dharula. Ni wazi kuwa utakwama Sana.

    Umuhimu wa fedha za dharula
    1. Inakusaidia kukamilisha Jambo lako Kama ulivyopanga bila kukwama.
    Kama ulikuwa unajenga na umepiga bajeti ya nyumba Ni milioni 50, Ni muhimu uwe na milioni walau tano za ziada ambazo zinaweza kukupiga tafu pale Ambapo Mambo yanaenda ndivyo sivyo.

    2. Inakusaidia kuacha kuwasumbua watu hovyohovyo
    Ngoja nikurudishe kwenye mfano wetu wa awali wa wewe kwenda Bukoba na gari likashindwa kuendelea na safari baada ya wewe kufika Biharamuro.

    Ni wazi kuwa Kama hutakuwa na fedha ya dharula, utakwama. Hapa utaanza kuwapigia simu watu wengine ili wakusaidie.

    Ila ukiwa na fedha ya dharula wewe mwenyewe, utajikinga mwenyewe na Mambo yako yataendelea bila kuwasumbua watu.

    3. Fedha ya dharula itakupunguzia msongo
    Hutakaa na kuanza kuwaza, sijui mjomba atatuma fedha au hatatuma. Atatuma kwa wakati au atachelewa. Utakachofanya, utachukua hela yako na Kuendelea na safari yako.

    4. Hutamwambia kila mtu shida zako. Kama hauna fedha ya dharula, utapaswa kujieleza kwa kila MTU ukiomba msaada, hata yule ambaye ulikuwa hutazamii kumweleza changamoto zako, utalazimika kufanya hivyo.

    5. Utakuwa na uhakika wa maisha. Utakuwa hauishi kwa kubahatisha.

    Rafiki yangu, ni muhimu Sana uwe na fedha ya dharula. Hii fedha itakusaidia katika maeneo mengi ya maisha.
    Inashauriwa walau uwe na fedha ya miezi sita mpaka mpaka mwaka mzima, hii ni fedha ya dharula ambayo Unaweza kufikia muda wowote. Hivyo basi rafiki yangu changamka, usiache kuweka akiba. Fedha ya dharula ni muhimu sana.

  • Njia Saba (07) Bora Za Kutangaza Ujuzi Wako Kwa Watu

    Rafiki yangu siku ya leo ningependa kikufundishe njia Saba Bora za KUTANGAZA UJUZI WAKO KWA watu, kiasi Cha kuweza kuwashawishi watu waweze kutoa hela zao mfukoni na kukulipa.

    Naomba ifahamike hapa kuwa ninapoongelea Aina za ujuzi namaanisha, kile kitu ambacho tayari unacho na unaweza kukipangilia vizuri kikaanza kuleta mafanikio.
    Kuna watu wanaposikia ujuzi Basi wanadhani kinapaswa kuwa ni kitu cha kipekee sana kitu ambacho hakijawahi kufanyika au kuonekana ssehemu yoyote.


    Ujuzi unaweza kuwa elimu au taaluma yako.


    Ujuzi unaweza kuwa kitu ambacho umefanya kwa muda mrefu na Sasa umebobea.

    Kwenye hicho kitu kiasi kwamba unaweza kuwafundisha wengine wakanufaika nacho.


    Ujuzi unaweza kuwa wa kujifunza pia mtandaoni

    SOMA ZAIDI: AINA TATU ZA UJUZI UNAOHITAJI ILI KUONGEZA THAMANI YAKO NA KULA MEMA YA NCHI

    Kwenye makala ya leo ningependa nikuoneshe njia Saba za kutangaza ujuzi wako

    Kwanza unaweza kutangaza ujuzi wako mtandaoni


    Pili unaweza kuwatumia watu wanaokujua kutangaza ujuzi wako


    Tatu ni kuandaa na kuonesha kazi zako


    Nne Ni kuomba rufaa


    Tano nii kuwa na data za wateja walionunua na wale wanaonesha nia ya kufanya.


    Sita ni kuwatembelea watu walipo na saba

    na saba ni kupitia kufanya kazi ambayo ni bora kabisa kiasi kwamba hakuna mtu yeyote anayeweza kukupuuza.

    Rafiki yangu hizo ndiyo njia saba za kutangaza ujuzi wako kwa watu, na habari njema ni kwamba, unaweza kuchagua njia moja ambayo unaweza kuanza kutumia sasa hivi.

    kisha ukaanza kuitumia.

    Kama kuna njia kati ya hizo utaitumia halafu ikaleta matokeo, usiache kuitumia hiyo njia. Endelea kuitumia zaidi na zaidi hku ukiboresha ili uweze kuwafikia watu kwa wingi zaidi.

    SOMA ZAIDI: 

    Kwa leo naomba niishie hapo rafiki yangu.

    Najua kuwa ungependa kupata ushauri wa karibu zaidi moja moja kwa moja kutoka kwangu. Nitafute tuone ni lini nitakuwa na muda, ili nikupangie ratiba ya kuongea na wewe. Utalipia kiasi kidogo tu.

    Saa moja ni laki moja mazungumzo kwa njia ya mtandao.

    Kwa mazungumzo ya ana kwa ana utalipia LAKI MBILI NA NUSU kwa saa

    Malipo yanafanyika kwanza, kisha unapewa tarehe (appointment) tutakapoweza kuongea

    Tumia namba ya simu +255 755 848 391 kuwasiliana nami.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza ambaye anaishi Morogoro nchini Tanzania.

    Unaweza kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza kupitia youtube channel yake hapa

    Kwa ushauri niandikie songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu ambavyo ameandika Godius Rweyongeza, wasiliana naye kwa +255 684 408 755 na orodha ya vitabu vyenyewe unaweza kuiona HAPA. Chagua unachopenda, kisha twanga,  +255 684 408 755

    Kujiunga na programu yetu ya uandishi. Wasiliana na +255 678 848 396

    For Consultation only: +255 755 848 391  au godiusrweyongeza1@gmail.com

  • Nguvu ya fedha; Itumie Ikubebe

    Hivi umewahi kujiuliza fedha kama fedha ina nguvu gani maishani mwangu, kwenye maisha ya familia yangu au hata maisha ya watu wengine wa karibu sana kwenye andiko la leo ambapo unaenda kujifunza nguvu hizi muhimu za fedha na jinsi ambavyo unaweza kutumia nguvu hizi hapa kwa manufaa yako.

    1. Nguvu ya kufanya maamuzi. Kwenye hili andiko ninaenda kuandika mengi kuhusiana na nguvu ya pesa. ila kitu kimoja ambacho pesa itakupa kama utakuwa nacho ni nguvu ya kufanya maamuzi, yaani, ukiwa na pesa yako, utakuwa na uwezo wa kuamua chochote kile unachotaka. Unaweza kuamua utembelee eneo gani na eneo gani usitembelee. Hata kwenye vikao vya familia, ukiwa na pesa, nguvu ya wewe kufanya maamuzi inakuwa kubwa ukilinganisha na yule ambaye anakuwa hana pesa. SIyo tu kwenye familia, hata kwenye ngazi za maamuzi ya kitaifa, mpaka kimataifa. Leo hii Marekani linafahamika kama taifa lenye nguvu, kwa sababu wanatumia nguvu ya pesa kufanya maamuzi ambayo kama huna pesa hawezi kuyafanya.

    Chukulia mfano, wa kawaida tu. kuna nchi za Afrika zinawekewa vikwazo kwa sababu ya kuwa na uhusiano na nchi ya urusi au washirika wake, ila wakati huohuo, nchi ya Marekani ambayo inaziwekea nchi za afrika hivyo vikwazo, yenyewe ina uhusiano wa karibu sana na washirika wa Urusi, na haiwekewi vikwazo.

    Aah, halafu umewahi kusikia wapi maishani kwako kwamba nchi maskini imeiwekea nchi tajiri vikwazo. Hiyo ndiyo nguvu ya pesa aiseee. Yaani, ukiwa na pesa, ni kama vikwazo vinakuwa hamna. Ndio maana unapaswa kuwa nayo, pesa ni sabuni. Hahaha, sabuni ya roho. Kuwa nayo aisee!

    2. nguvu ya kununua. Ukiwa na fedha unakuwa na nguvu ya manunuzi. Kwa pesa yako unaweza kuamua kununua jambo fulani au la unaweza kuacha. Unaweza kuamua kununua sasa hivi, au la unaweza kuamua kununua baadaye.

    Unaweza kuamua kuringa kidogo kabla ya kutoa hela. Hata hivyo, hela si ya kwako tu. Hii ni nguvu ya fedha. Ndio maana wewe unahitaji kuhakikisha kwamba unakuwa na pesa.

    Hata ukiomba mtu akupunguzie bei, siyo kwamba unakuwa upungiziwe bei kwa sababu ya mtu akuonee huruma, bali kwa sababu una pesa.

    3. nguvu ya kuwekeza. Fedha unaweza kuitumia kuwekeza kwenye eneo lolote. Kuwekeza ni kuifanya fedha ikutumikie, yaani, unaifanya pesa ikuingizie pesa zaidi hata pale unapokuwa umelala. Hicho ni kitu ambacho unahitaji ukifanyie kazi rafiki yangu.

    Kama hujaanza kuwekeza, mwaka huu kuwekeza kunapaswa kuwa kwenye vipaumbele vyako.

    Na kwa kuanzia hakikisha kwamba unasoma kitabu changu cha MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE

    Hakikisha una pesa, na hakikisha kwamba unaitumia pesa yako kuwekeza.

    4. nguvu ya kutoa na kusaidia jamii. Rafiki yangu, huwezi kusaidia watu kama hauna pesa. Huwezi kusaidia watu kama wewe mwenyewe unahitaji msaada. hahah, unahitaji uwe na pesa ili uweze kusaidia watu. Ni rahisi tu hivyo. Fedha ndiyo inakupa nguvu ya kusaidia watu. Kama unayo unaweza kuwasaidia watu, kama hauna, daah, ni ngumu kuasaidi watu.

    5. nguvu ya nguvu ya kununua muda kwa ajili yako. Pesa inaweza kukusaidia wewe kununua muda. Unajiuliza pesa inanunuaje muda, ningependa kukwambia kwamba pesa inanunua muda pale ambapo unakuwa umeajiri watu wengine wakusaidie kufanya baadhi ya majukumu, na hivyo kukupa mwanya wewe wa kuendelea na majukumu mengine. Upo hapo rafiki yangu.

    6. Nguvu ya kutibiwa. Kuna watu wengi huwa wanakufa kwa sababu tu ya kukosa huduma bora za kimatibabu, na wanakosa huduma bora kwa sababu hawana nguvu ya pesa. Ukiwa na nguvu ya pesa, kwanza ukijisikia vibaya tu utawahi hospitali, unakuwa hauna cha kuanza kusikilizia sijui kuona kama muujiza utatendeka ukapona. Ila kama hauna nguvu ya pesa, utaanza ooh, eti unasikilizia kuona kama utapona. Oooh, sijui imeenda endaje. Tafuta fedha ikuzoee aisee.

    7. nguvu ya kujenga mahusiano. Tafiti nyingi zimefanyika, na imegundulika kwamba moja ya kitu ambacho huwa kinafanya watu waachane kwenye mahusiano, ni kwa sababu ya pesa. hivyo, unahitaji uwe na pesa ili uweze kufanya makubwa zaidi. na siyo tu uwe na pesa, bali uwe na elimu sahihi kuhusiana na pesa.

    8. Nguvu ya kuchagua aina ya maisha unayotaka. Pesa inakupa nafasi yaw ewe kuchagua aina ya maisha ambayo wewe mwenyewe unataka, usupokuwa na fedha unaweza kuwa mtumwa kwa kulazimika muda mwingine kufanya kazi ambazo hata wewe mwenyewe hupendi.

    11. nguvu ya kubadili mwonekano wako

    Kuna siku moja kwenye mtandao watu waliweka picha ya msanii Zuhura, maarufu kama Zuchu, akiwa bado na maisha ya kawaida. Aliyeweka ile picha akawa amesema kwamba huyu ndiye Zuchu kabla hajatoka kimaisha.

    Lakini sasa hivi nguvu ya pesa imembadilisha.

    Pesa rafiki yangu ina uwezo wa kubadili mwonekano wako. Ukiwa nayo, mwonekano wako tu, unaongea.

    12. nguvu ya kukufanya ujiamini. Pesa ina uwezo wa kukufanya ujiamini.Yaani, inakufanya ujiamini kuliko yule ambaye hana. Yaani, ukitoka nyumbani ukiwa unajua kwamba hakuna chakula, unadaiwa kodi, na makorokoro mengine kibao, hata kujiamini kwako kunapungua tu. Ila kama unajua una mzigo wa kutosha nyuma ya pazia, hapo unakuwa kwenye nafasi nzuri ya kujiamini kuliko mtu mwingine yeyote. Hiyo ndiyo nguvu ya pesa.

    Rafiki yangum, fedha unapaswa kuwa nayo. Unapaswa kuwa nayo, maana kuwa nayo tu, kutavutia vitu vingi kwenye maisha yako. Hivyo itafute. Lakini usiishie tu kutafuta fedha, bali pia kuwa na maarifa sahihi ya kifedha. Haya yatakusaidia wewe kufanya makubwa zaidi wkenye maisha yako. Kila la kheri

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.

    Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.

    Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.

  • Kitu kimoja ambacho hupaswi kuacha kufanya hata kama una nguvu ya pesa

    umeshapata nakakla zako? Wasiliana na 0755848391 sasa kupata nakala zako. kila nakala bei yake ni 20,000/-
    umeshapata nakakla zako? Wasiliana na 0755848391 sasa kupata nakala zako. kila nakala bei yake ni 20,000/-

    Rafiki yangu mpendwa, ila shaka unaendela vizuri. Kwa upande mwingine mimi nipo vizuri kabisa. leo nataka tujadiliane kwa pamoja kuhusiana na kitu kimoja ambacho hupaswi kuacha kufanya hata kama una nguvu ya pesa. na kitu hiki ni kujadiliana muuzaji kuhusiana na bei anayokuuzia bidhaa.

    Yaani, kiufupi ni kwamba mtu akitaka kukuuzia kitu kwa bei fulani, mara zote jadiliana naye ili uone namna ambavyo anawez akukupunguzia kiasi fulani kwenye hicho kiasi ambacho amekwambia.

    Hiki kitu unapaswa kukifanya bila kujali una fedha nyingi kiasi gani.

    Mara nyingi mfano mtu akikwambia kwamba anauza bidhaa au kitu fulani kwa 20,000/-. Wewe anza kujadiliana naye kwa kumwambia kwamba una kiasi pungufu, pengine nusu yake tu. komaa hapohapo, na ikiwezekana ongeza kiasi kidogo tu.

    Mwisho wa siku utajikuta kwamba unaweza kupata hiyo bidhaa kwa bei nzuri sana.

    SIyo kwamba ukifanya hivi ni kiashiria cha umasikini, bali  hiki kitu kinafahamika kama negoatiaon. Na negotiation ni mojawapo ya ujuzi muhimu sana ambao unauhitaji, na unakufaa sana, na utakusogeza mbali sana kimaisha.

    Rafiki yangu, huu ujuzi hakikisha kwamba unakuwa nao kwa vyovyote vile. Na utumie popote pale unapokuwa bila ya kurudi nyuma.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.

    Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.

    Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.

  • Fanya kazi kwanza, tutaongea

    /

    Mr. Beast ni moja ya watu maarufu sana kwenye mtandao wa youtube. Yeye alianzia chini kabisa kwenye ulimwengu wa youtube, hakuwa na umaarufu wowote kama huu alionao sasa hivi. alianza kurekodi video moja baada ya nyingine,. Nyingi hazikufanya vizuri, lakini jamaa hakukata tamaa aliendelea, baada ya miaka mingi ya kuweka kazi bila ya kukata tamaa, ndipo video zake zilikuja kutambulika na baada ya hapo umaarufu wake umekuwa unaongezeka kila siku na kila kukicha.

    Sasa kuna siku aliulizwa, hivi una ushauri gani kuhusu watu ambao ndio kwanza wanaanza kuingia kwenye ulimwengu wa youtube. Alisema kwamba hawa wanapaswa kuendelea kuweka kazi. Yaani, wasitegemee kwamba wanaenda kupata matokeo makubwa kwa haraka na ndani ya siku moja. Hakuna kitu kama hicho. matokeo makubwa yatakuja kweli, ila yanahitaji kwanza muda. Lakini pia yanahitaji mtu uweke kazi.

    Siyo mtu unarekodoi video moja na kuweka youtube huku ukitegemea kupata m atokeo na mafanikio makubwa ndani ya hiyo siku. Hakana kitu kama hicho, badala yake unapaswa kuwa na mwendelezo kwenye kile ambacho wewe mwenyewe unafanya, yaani, unapaswa kufanya kitu ulichochagua kila siku bila kuacha na kwa mwendelezo.

    Kadiri ya Mr. Beast anasema kwa mtu ambaye anataka kutoboa kwenye ulimwengu wa youtube anapaswa kuwa walau amerekodi video za kuanzia mia moja. hapo sasa ndipo tunaweza kuanza kuongea kuhusu kupata wafuasi. Hapo siyo kwamba huyo mtu katoboa, ila ndio mnaweza kuanza kuongea.

    Hee, Na anasema kwamba kwenye kila video ambayo utarekodi unapaswa kuendelea kuiboresha na kuifanya kuwa bora zaidi ya ile ya kwanza. Yaani, siyo unarekodi video nyingi lakini zinakuwa hazina ubora wowote. Hapana, badala yake ni kwamba hizi video unapaswa kuwa unaziongezea ubora kila unaporekodi.

    Najua asilimia kubwa ya wasomaji wangu siyo watu wanaotengeneza maudhui ya youtube. Na wala siyo kwamba kwa makala hii basi nawataka waanze kurekodi maudhui kwa ajili ya kuweka youtube.

    Bali nataka kila anayesoma ujumbe huu aondoke na kitu kimoja kikubwa. Na kitu hiki ni kwamba, kama  unaanzia chini, unapaswa kuweka kazi kwenye kitu ambacho unafanya. siyo unafanya kitu hicho mara moja au mara mbili halafu huoni matokeo unaacha. ACHA utani aisee, endelea kuweka kazi mpaka kieleweke.

    Na siyo unafanya kazi kwa maozea,bali kila mara unaboresha na kufanya kazi ambayo ni bora zaidi kuliko mwanzo.

    Toa mazoea, fanya kazi tena kwa bidii sana. Tutaongea baadaye

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.

    Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.

    Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.

  • Kuwa bora

    umeshapata nakakla zako? Wasiliana na 0755848391 sasa kupata nakala zako. kila nakala bei yake ni 20,000/-
    umeshapata nakakla zako? Wasiliana na 0755848391 sasa kupata nakala zako. kila nakala bei yake ni 20,000/-

    Moja ya dhana ambayo watu wengi tumekuwa hatujifunzi ni kuwa vitu ambavyo ni bora ndivyo ambavyo huwa vinapendwa. Hakuna mtu huwa anapenda kukaa karibu na vitu dhaifu, vitu ambavyo siyo vizuri na vitu ambavyo  havivutii.

    Ili uweze kunielewa vizuri kwenye hili, nitatolea mfano ambao unaweza kukuudhi kidogo. Hivi eti kwa mfano, unaweza kuchukua chakula chako kizuuuri ambacho umekipika na kikapikika na kwenda kula kwenye dampo? Ji bu lipo wazi kabisa, huwezi kufanya hivyo, kwa nini kwa sababu dampo siyo sehemu bora ambapo unaweza kula chakula chako hicho kitamu ambacho umedhamiria kula.

    Hivyo hivyo, kwenye maisha ya kawaida, hakuna mtu ambaye anapenda kujihusisha na vitu vibaya. Na hata mzazi anapokuwa analea watoto wake atawaepusha na watoto wengine ambao wana tabia mbaya.

    Lengo la mimi kukuandikia haya yote ni kukujulisha kuwa unapaswa kuwa bora kwenye kile unachofanya. Yaani, kwamba unapaswa kujiwekea viwango vya daraja la kwanza. Viwango vikubwa ambavyo utakuwa unavifanyia kazi na kuvifikia

    Ubora wa wewe kujiwekea hivi viwango ni kwamba utavutia kwako watu wengine wa viwango vikubwa pia. Chuma kinanoa chuma. Na vitu vya aina moja mara nyingi huwa vina tabia ya kukaa pamoja.

    Hivyo kama viwango vyako ni dhaifu, utajikuta kwamba unapata marafiki na watu ambao pia wana viwango dhaifu. Hiki kitu kitapelekea wewe kuishi maisha ambayo ni dhaifu pia . Sasa mwaka 2023 azimio lako linapaswa kuwa ni moja tu. unapaswa kuazimia kwamba mwaka 2023, ni mwaka wangu wa kufanya kazi zangu kwa viwango vya juu.

    Hiki kitu kitakufanya uvutie kwako watu wngine wenye viwango vya juu pia.

    Kama unaajiri, hakikisha kwamba unaajiri watu wa viwango vya juu.

    Marafiki wako wawe marafii ambao wana viwango vya juu pia.

    Rafiki yangu, huu ni mwaka wako ila tu siyo kwamba uishie kusema kwamba huu ni mwaka wangu kwa maneno, bali matendo yako yanapaswa kudhihirisha hilo.

    Ukiwa bora watu hawawezi kukupuuza.

    Asante sana

    Kupata makala zaidi kutoka kwangu, hakikisha kwamba umejaza taarifa zako hapa

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.

    Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.

    Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.

  • Iambie dunia kile unachotaka kufanya, ila  kwanza kioneshe hicho kitu

    Rafiki yangu, habari ya siku ya leo. Hongera sana kwa siku hii ya leo nay a kipekee sana. mimi kwa upande wangu rafiki yangu siku ya leo, nina kitu kimoja tu ambacho ningependa kukwambia. Na kitu hiki siyo kingine bali ni kwamba kama kuna kitu ambacho ungependa kuiambia dunia, basi hicho kitu unapaswa kukisema kwa dunia, ila kwanza unapaswa kuonesha kwa vitendo kwamba unaweza kukifanya hicho kitu.

    Ujue hii dunia haipungukiwi na wasemaji hata kidogo, bali inapungukiwa na watendaji. Unachotakiwa kufanya ni kwamba wewe unapaswa kuwa mtendaji sana na wala siyo muongeaji sana.

    Mara zote kuwa mtendaji, na onesha kile ambacho unataka kusema kwa dunia kwa vitendo na wala siyo kwa maneno.

    Mara nyingi nimekuwa nikiwaambia watu waseme malengo na ndoto zao waziwazi, kisha wazifanyie kazi. Ila sasa nimegundua haya masula ya kusema malengo na ndoto zako kwa watu hivihivho tu ni upotezaji wa muda. Na mwaka huu nataka ufanye kitu kimoja tu. Malengo na ndoto zako, usiziseme kwa mtu yeyote, kabisa. wewe fanyia kazi tu malengo na ndoto zako bila kusema chochote na kwa yeyote. nina hakika rafiki yangu, kwamba mpaka kufikia mwishoni mwa mwaka. matendo yako yataongea zaidi kuliko ambavyo ungeongea kwa maneno.

    Ni hayo tu ambayo nilitaka kukwambia siku ya leo. Kabla sijaachana na wewe kabisa kuna kitu kimoja ambacho ningependa ufahamu. Na kitu hiki kwamba mwaka huu 2022, mwezi Juni tutakuwa na semina mkoani MOROGORO.

    Semina hii itafanyika juni tarehe 24, hapahapa mkoani Morogoro.

    Kwenye semina hii, unaenda kupata mafunzo ya kipekee yatayokusaidia wewe kupiga hatua na kusonga mbele kwa juhudi kubwa sana.

    Semina hii ya ana kwa ana, itafanyika kwenye mojawapo ya hoteli hapa Morogoro mjini, na itakuwa semina ya siku moja tu.

    Gharama ya semina hii itakuwa 50,000 tu. Malipo yote yatafanyika kwa namba 0687848391 jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Karibu sana.

  • Jinsi ya kuitumia nguvu ya mara kumi zaidi kufanikisha makubwa

    Rafiki yangu, sina shaka unaendelea vizuri kabisa. hongera sana kwa siku hii ya kipekee sana. siku ya leo ningependa kuongea na wewe juu ya suala moja tu. Na suala hili ni namna ambavyo unaweza kuitumia nguvu ya mara kumi zaidi kufanikisha malengo yako, na kitu chochote kile ambacho umepanga. Kiufupi kwenye hii makala nataka nikuoneshe ni kwa namna gani ambavyo unaweza kuitumia nguvu ya mara kumi zaidi kuhakikisha kwamba unafanikisha makubwa sana.

    Utakuwa unajiuliza hii nguvu ya mara kumi ndiyo nguvu gani na inafanyaje kazi?

    Na mimi ningependa kuanzia hapo. Nguvu ya mara kumi kumi zaidi iko hivi, kwa chochote kile ambacho unapanga kupanga, unapaswa kukizidisha mara kumi zaidi. Kwa kuanzia tuanze na malengo yako. Kama una lengo lako lolote ambalo umeweka sasa hivi, zidisha mara kumi zaidi ya lengo ambalo umeweka sasa hivi.

    Kwa mfano kama umeweka lengo la kuingiza kipato cha milioni moja kwa mwezi. Unapaswa kulizidisha hilo lengo lako mara kumi zaidi. yaani, badala ya kuwa na lengo la kuingiza milioni moja kwa mwezi, kuwa na lengo la kuingiza milioni kumi kwa mwezi.

    Kama una lengo la kuingiza milioni kumi, zidisha mara kumi zaidi. Liwe ni milioni 100. Yaani, kitu chochote kile utakachofanya kwenye maisha yako, hakikisha kwamba unakifanya kwa viwango vya mara kumi zaidi ya kawaida.

    Mahusiano yako, yawekee lengo la kuyaboresha mara kumi zaidi.

    Biashara yako, iwekee lengo la kuikuza mara kumi zaidi.

    Wteja wako, weka lengo la kuwaongeza mara kumi zaidi.

    Mtaji wako, weka lengo la kuukuza mara kumi zaidi

    Oooh, kama nakuona vile unavyostuka na kuanza kuona kama vile lengo linakuwa ni kubwa sana. na ndio maana, kuna hii nguvu ya mara kumi zaidi.

    Maana, uwezo wa hii nguvu siyo tu kwamba upange peke yake. Bali upange na kutekeleza kile ulichopanga. Kwa hiyo, maana yake mipango yako inapaswa kuwa ni mipango ya mara kumi zaidi, lakini sambamba na kuwa na mipango ya mara kumi zaidi, unapaswa kuwa na vitendo ambavyo ni mara kumi zaidi.

    Yaani, baada ya kuwa umezidisha lengo lako na kulifanya kuwa lengo kubwa sana. sasa kinachofuata ni wewe kuzidisha kila kitu ambacho utafanya. Unapaswa kuzidisha hatua ambazo unachukua mara kumi zaidi.

    Kwa lengo lako la kuingiza milioni moja, pengine ulikuwa umejiwekea kwamba ukiuza bidhaa kwa wateja 10 tu, utakuwa umeweza kulifikia. Ila kwa lengo lako jipya ambalo umeweka. Yaani, hili lengo la mara kumi zaidi. maana yake utahitaji  kuhudumia wateja mara kumi zaidi ya wale ambao ulikuwa umepanga kuwahudumia.

    Na ili uweze kuhudumia wateja mara kumi zaidi ya wale ambao unawahudumia, maana yake unapaswa kuchukua hatua za kutafuta wateja mara kumi zaidi. Kwa sababu ili uweze kuwa na wateja 100 wanaonunua kwa wiki au kwa mwezi. Lazima uwe na wateja zaidi ya hao. Maana yake kutakuwepo na wengine ambao hawatanunua, sasa baada ya kutoa 100 wanaonunua, ndipo na wewe unakuja kubaki na wale wachache ambao wananunua.

    Kwa hiyo basi rafiki yangu, naomba kitu kimoja tu. kuanzia sasa hivi, anza kufikiri mara kumi zaidi ya sasa.

    Kama ni pesa, fikiri mara kumi zaidi ya unavyofikiri sasa hivi. chukua hatua mara kumi zaidi ya unavyochukua sasa hivi.

    Kutana na watu mara kumi zaidi ya unaokutana nao sasa hivi. piga simu kwa wateja mara kumi zaidi ya unavyopiga sasa hivi.

    Fanya mazoezi mara kumi zaidi ya unavyofanya sasa hivi. Hii ndiyo tiketi ambayo inawatofautisha watu ambao wanafanya makubwa na wale ambao wanafanya vitu kwa namna ya ukawaida sana. Kama wewe hutaki kuwa mtu wa kawaida, basi unahitaji kuhakikisha kwamba unachukua hatua za tofauti ili uweze kufika kule unapotaka.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.

    Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.

    Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.

X