Home


  • Namba Zetu Za Malipo

    Namba za malipo ya vitabu:

    Namba za lipa

    TIGO PESA: 19016638 Jina ni SONGAMBELE CONSULTANTS

    M-PESA: 5564517 jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

    Namba za kawaida

    AIRTEL MONEY: 0684408755
    TIGO PESA: 0655 848 392
    M-PESA: 0745 848 395

    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    NB: Kama namba ya malipo anatumiwa mtu ambaye yuko nje ya nchi. Iandikwe Kwa kuanza na +255

    Kwa hiyo namba zinazotumwa nje ya nchi zitakuwa
    Airtel money: +255 684 408 755
    TIGO PESA: +255 655 848 392
    M-PESA: +255 745 848 395

    KOTE Jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Kama malipo yatakuwa yanafanyika kupitia benki.

    Yafanyie kupitia

    1. CRDB BANK: 0150770710200
    2. NMB BANK: 22110047274

    Kote jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

  • Wasiliana na Godius Rweyongeza Sasa

    Habari yafuatayo ni mawasiliano Unayoweza kutumia kumpata GODIUS RWEYONGEZA

    Simu: +255 (0) 684408755

    Whatsap: +255 (0) 755848391

    Email: songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu vyake wasiliana Moja kwa Moja na +255 (0) 684408755 (more…)

  • Baadhi Ya Vyanzo Vya Kipato Ambavyo Unaweza Kuwa Navyo

    1. Ajira
    Hiki ni chanzo maarufu ambacho wengi huwa wanakuwa nacho. Chanzo hiki huwa kinaingiza kipato (ujira) kila baada ya muda fulani (siku,wiki au mwezi). Kwa MTU yeyote ambaye hana sehemu ya kuanzia hakikisha walau unaanzia kwenye ajira.

    Ukipata ajira hakikisha unaifanya kwa uaminifu na kwa kujituma. Maana ajira inaweza kukupelekea wewe kupata vyanzo vingine zaidi.

    2. Kitabu
    Naamini wewe utakuwa na uzoefu  mkubwa ambao wengine wanatamani kuupata kutoka kwako. Uzoefu huu unaweza kuuweka kwenye kitabu na watu wakasoma hiki kitabu.

    Kama wewe umekuwa unafuga ng’ombe kwa miaka kumi sasa, tayari una uzoefu wa kutosha wa kuandika kitabu kuhusu ufugaji wa ng’ombe. Utumie uzoefu huu, kuandika kitabu. Kuna watu watapenda kusoma kitabu chako.

    Leo hii unaposoma hapa, Kuna MTU sehemu anajiuliza naweza kuanza kufuga ng’ombe wa kisasa. Nini kinahitajika? Napaswa kuepuka Nini? Napata wapi ndama wa kuanza nao? MTU huyuhuyu anaendelea kujiuliza, hivi ng’ombe huwa wanachanjwa? Kila baada ya muda gani? Kwa Nini?

    Na wewe una uzoefu huu, Tena wa miaka mitatu, mitano au kumi na zaidi. Kwa Nini usiandike kitabu?

    Naomba unisikilize, kaa chini andika kitabu ili watu waweze kunufaika na uzoefu wako huu.

    Japo watu watapaswa kununua kitabu chako ili wanufaike, ila ubora ni kwamba baada ya hawa watu kusoma kitabu chako, watakushukuru sana kwa namna ulivyowasaidia.

    Unajiuliza unawezaje kuanza kuandika kitabu? Pata nakala ya kitabu cha JINSI YA KUWA MWANDISHI MBOBEVU. Nakala laini ni 5,000/- tu. Tuma fedha kwa namba ya simu 0755848391 jina ni GODIUS RWEYONGEZA.

    Kitabu ni chanzo cha kipato ambacho unakitengeneza mara moja na kinaendelea kuwepo kwa miaka yote. Watu wanaendelea kununua  kile ulichoandika miaka kadhaa iliyopita.

    Mfano ukiandika kitabu mwaka ujao wa 2023 na ukakimaliza na kuanza kukiuza. Kitabu hicho kitaendelea kuwafaa watu hata mwaka miaka kumi, ishirini, hamsini na zaidi.

    Kuna mtu atanunua kitabu hichohicho ulichoandika mwaka 2023, atakinunua mwaka 2035. Kazi yako ya Mara moja tu, itakulipa maisha yako yote. Hiki ni chanzo kizuri cha kipato ambacho unapaswa kukitengeneza.

    Cha kushangaza utasoma hapa na kutikisa kichwa bila kuchukua hatua ya kuanza kuandika kitabu.

    Enewei,
    Ngoja mimi nikuache

    Ila matokeo yako ya kesho yanaathiriwa na uamuzi unaofanya sasa hivi. Na uamuzi unaofanya Sasa hivi Ni au upate kitabu cha JINSI YA KUWA MWANDISHI MBOBEVU kwa shilingi 5,000/- au la uache!

    Kwa uamuzi wowote ule utakaochukua, fahamu kuwa una madhara kwenye kesho yako. Sasa je, upo tayari kuiharibu kesho yako kwa sababu hutaki kuchukua hatua ya kupata KITABU hiki?

    Changamka sasa. Lipia 5,000/-  upate kitabu Cha JINSI YA KUWA MWANDISHI MBOBEVU, ili ujifunze namna ya kutengeneza mfereji wako mwingine wa kipato.

    Katika ulimwengu wa leo unaweza kuandika kitabu na kukiuza kwa njia ya mtandao. Kwa hiyo, ukatoa kitabu kwa gharama ndogo. Kumbe tofauti na wengine wanavyofikiri kuchapa lazima uwe na fedha nyingi, bado kuna uwezekano wa wewe wa kuchapa na kuuza kitabu kwa njia ya mtandao.

    3. Kozi
    Kama kilivyo kitabu, kozi pia ukiiandaa inadumu kwa muda mrefu. Unaiandaa Mara moja ila inadumu kwa muda mrefu huku ikikuingizia kipato.

    Labda unajiuliza Kati ya kitabu na kozi, niandae kipi? Nashauri uandae kitabu kwanza, Kisha uandae kozi.

    Nazungumzia uwekezaji kwenye hisa, hatifungani na vipande. Huu ni uwekezaji muhimu sana ambao wewe rafiki yangu unapaswa kuhakikisha kwamba umeufanya.

    4. Uwekezaji
    Yees, na Mimi ninapozungumzia uwekezaji siongelei Mambo ya Bitcoin, sijui crypto currency au sijui nini?

    Ni uwekezaji ambao ni uhakika kuwa unaweza kukuingizia kipato hata Kama umelala? Kama hujawahi kuingiza kipato ukiwa umelala, hakikisha unachukua uamuzi Tena leo, wa kuanza kuwekeza kwenye HISA, hatifungani na vipande.


    5.  Biashara
    Biashara chanzo kingine Cha kipato ambacho kwenye ulimwengu wa Sasa Ni CHANZO ambacho lazima uwe nacho. Hata kama umeajiriwa, bado unahitaji kuwa na biashara yako ambayo itakuwa unaiendesha kwa pembeni hata kama ni ndogo.

    Sote tunajua kuwa mshahara huwa haubadiliki mara kwa mara. Lakini kipato kwenye biashara hakina ukomo. Unaweza kukuza kipato chako kadiri uwezavyo. Hivyo, nakushauri na wewe uhakikishe unakuwa na biashara yako. 

    6. Kamisheni
    Kamisheni ni kipato unachopata kutokana na mauzo ya vidhaa fulani ambayo siyo yako au kwa kuwaelekeza watu wanunue vidhaa fulani. Hii ni Aina ya kipato ambayo Unaweza kuifanyia kazi pia.

    Mfano, mimi Sasa hivi nalipa kamisheni ya asilimia 40 pale unapomleta mteja akanunua Audiobooks au softcopy zangu. Kumbe mteja mfano akinunua Audiobook ya kitabu cha NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA, ambayo kwa Sasa naiuza 10,000/-

    Wewe unapata 4000/-. Just kwa kumweleza mteja tu aje kununua kwangu na akanunua.

    Kwa ambaye angependa tufanye kazi pamoja kwenye hili, hakikisha tunawasikia kwenye WhatsApp yangu leo.

    BONYEZA HAPA 👇🏿 kuchati nami
    https://wa.me/message/3PMZSAFONLHAP1

    Karibu sana

    7. Mrabaha
    Mrabaha ni malipo unayopata kutokana na kazi ya sana au kazi ya kubunifu.

    Wasanii wa muziki huwa wanalipwa mrabaha kwa kazi zao kutumiwa kwenye vyombo vya habari na maeneo mengine. Mchoraji pia anaweza kupata mrabaha kutokana na kazi yake ya kuchora.

    Mwandishi anaweza kupata mrabaha pale kitabu/ kazi yake inapochapwa na kuuzwa. Na kampuni za uchapishaji.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.

    Godius Rweyongeza ni mwandishi wa vitabu zaidi zaidi ya 20. Na ni mwendeshji wa mtandao wa Songambele. Amekuwa akiandika kwenye huu mtandao huu tangu mwaka 2016. Kitabu chake cha Kutoka Sifuri Mpaka Kileleni kimekuwa #1Best Seller kwa muda sasa kwenye mtandao wa GETVALUE

    Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.

    Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.

    Mtandaoni, vitabu vyake unaweza kuvipata kupitia mtandao wa GETVALUE kwa KUBONYEZA HAPA

  • Viashiria Vinne Vya Uhuru wa kweli. Kama hauna hivi vitu jua huna Uhuru..

    Leo Ni tarehe 9 Disemba, ni siku uhuru hapa nchini Tanzania. Sikupanga kuandika chochote kuhusiana na uhuru, ila ngoja niandike haya machache kuhusiana na uhuru wako binafsi.

    Watu wengi huwa wanachanganya kuwa kwa kuwa nchi iko huru Basi na wao wako huru. Siyo kweli, Kuna viashiria ambavyo vinaweza kuonesha kuwa wewe uko huru au hauko huru. Vifuatavyo Ni viashiria muhimu vinavyoonesha kuwa wewe uko huru.

    Ukiona viashiria hivi vinakupiga chenga, basi pambana ili uweze kupata Uhuru wako

    Kiashiria namba moja ni Uhuru wa kazi.
    Uhuru wa kazi ni pale Ambapo unakuwa hulazimiki kufanya kazi ili uingize kipato. Lakini pia unakuwa unafanya kazi unayoipenda na siyo kufanya kazi unayolazimishwa kufanya. Labda nikuulize unaipenda kazi unayoifanya?

    Uhuru wa kazi haumaanishi kwamba uwe mzembe. Mimi Ni mwumini mzuri Sana wa kufanya kazi kwa bidii. Mara zote na siku zote hakikisha unajituma kwenye Kazi, ila fanya kazi unayoipenda.

    Kiashiria namba 2 ni Uhuru wa fedha

    Wazungu huwa msemo unaosema fuck you money. F*ck you money ni kiwango Cha fedha ambacho ukiwa nacho hakuna mtu yeyote anaweza kukuzuzua. Hiki ni kiasi Cha pesa ambacho ukiwa nacho hata bosi wako akizingua unaweza kumwambia f*ck you!

    Kwa kusema hivi simaanishi uanze kutoa matusi kwa watu, Ila hiki ni kiasi Cha fedha ambacho ukiwa nacho, kinakupa uhuru.

    Watu wengi huko makazini hawana Uhuru wa kuongea. Wana hoja nzuri ila wanashindwa kuzitoa kwa sababu wanahofia zinaweza kukataliwa na hivyo wakafukuzwa kazi.

    Muda mwingine bosi anazingua au anawalazimisha kufanya vitu kinyime na vile wanavyoamini, lakini bado wanafanya kwa sababu hawana fedha, maana wakimpinga hawama kazi, hivyo hawana hela.

    Kama bado hujawa na kiasi cha pesa cha kukufikisha kwenye kiwango cha f*ck you money, jua bado unapaswa kuendelea kupambana ili upate uhuru wako, maana sasa hivi huna uhuru.

    Kiashiria namba tatu ni uhuru wa muda. Yaani, kwamba unakuwa na Uhuru wa kupangilia ratiba zako. Una Uhuru wa kwenda popote bila kuathiriwa na kitu chochote.
    Je, unao uhuru wa muda?

    Kiashirikia namba nne Ni uwezo wa kuingiza fedha hata kama umelala.
    Kama huwezi kuingiza fedha hata kama umelala jua bado hujawa na uhuru. Unapaswa kupambana kuhakikisha kwamba unaweza kuingiza fedha hata kama umelala. Inawezekanaje? Ndio inawezekana kupitia uwekezaji na kuwa biashara

    Hakikisha umesoma kitabu changu cha MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE ili ujifunze mbinu za uwekezaji ambazo zitakusaidia wewe kuingiza fedha ukiwa umelala?

    Je, ni Uhuru upi ambao hauna?
    Hauna Uhuru wa kazi. Basi soma kitabu cha JINSI YA KUONGEZA THAMANI YAKO (softcopy 10,000/-)

    Hauna Uhuru wa muda? Soma kitabu cha KUTOKA SIFURI MPAKA KILELENI (Hardcopy 12,000/-) na softcopy 7,000/-

    Hauna Uhuru wa kazi? Soma kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO na NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA. Kila kitabu Ni 20,000/-

    Hauna Uhuru wa fedha. Soma kitabu cha MAAJABU YA KUWEKA AKIBA na kitabu Cha MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE 20,000/-

    Hivyo, ni vitabu muhimu ambavyo unapaswa kusoma kama unataka kupata Uhuru wa kweli.

    Unapenda nikupe ofa siku ya leo ya Uhuru? Ndio inawezekana. Bonyeza hapa
    Kisha andika OFA YA UHURU!

    Nitakupa ofa ya kitabu unachotaka siku ya leo.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.

    Godius Rweyongeza ni mwandishi wa vitabu zaidi zaidi ya 20. Na ni mwendeshji wa mtandao wa Songambele. Amekuwa akiandika kwenye huu mtandao huu tangu mwaka 2016. Kitabu chake cha Kutoka Sifuri Mpaka Kileleni kimekuwa #1Best Seller kwa muda sasa kwenye mtandao wa GETVALUE

    Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.

    Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.

    Mtandaoni, vitabu vyake unaweza kuvipata kupitia mtandao wa GETVALUE kwa KUBONYEZA HAPA


  • Kwa Nini Unahitaji Kuwa Na Vyanzo Vingi Vya Kipato

    Unahitaji Kuwa na vyanzo vingi vya kipato

    Moja ya Kitu Cha muhimu ambacho unahitaji  kuhakikisha umekizingatia ni kuwa na vyanzo vingi vya kipato. Labda swali la kwanza la kujiuliza ni je, vyanzo vingi vya kipato maana yake nini?

    Vyanzo vingi vya kipato, Ni pale unapokuwa unaingiza kipato kwa njia zaidi ya moja. Yaani, siyo tu unakuwa unategemea njia moja ili kupata fedha, bali unakuwa na uhakika wa kuingiza kipato kupitia vyanzo mbalimbali. Vyanzo hivyo vinaweza kuwa ni
    1. Ajira yako
    2. Ujuzi wako
    3. Uwekezaji
    4. Biashara
    4.  Kamisheni
    5. Mrabaha n.k

    Kwa nini unahitaji kuwa na chanzo zaidi ya kimoja cha kipato.

    Rafiki yangu, hiki Kitu cha kuwa na chanzo zaidi ya kimoja cha kipato, hakifundishwi shuleni na hata majumbani. Hii ni elimu ambayo MTU unajiongeza kwa kuhakikisha unakuwa nayo huku mtaani. Ila ni elimu ya lazima na wala siyo hiyari.

    Kuna sababu nyingi za kwa nini unapaswa kuwa na vyanzo vingi vya kipato.

    Kwanza ni kwa sababu ya mabadiliko ambayo huwa yanatokea. Hiki kitu kinaweza kufanya baadhi ya vyanzo vya kipato  visikuingizie kipato. Mfano mfumuko wa bei ambao umetokea mwaka huu, kwa namna moja au nyingine unakuta kwamba unaathiri kipato chako, pia. Unakuta kwamba fedha uliyokuwa nayo haitoshi kukuwezesha wewe kununua bidhaa husika. Ndio maana unahitaji kuhakikisha kwamba unakuwa na chanzo kingine Cha kipato

    Pili, ni Kujijengea kinga. Kama unakitegemea  na chanzo kimoja tu cha kipato ili uingize fedha, unakuwa unapotea rafiki yangu. Kwa sababu inaweza kutokea siku moja ambapo chanzo hicho kikawa hakijaingiza kipato kama inavyostahili. Hiki Kitu kitakufanya wewe ukwame kufanikisha malengo yako. Lakini unapokuwa una chanzo zaidi ya kimoja, huo ndio unakuwa ni mwanzo wa wewe kupiga hatua Kubwa kimaisha. Kwa sababu chanzo kimoja Cha kipato kinapokwama, kingine kinakuwa tayari kufanya kazi kwa ajili yako na kuhakikisha kwamba kimekuinua zaidi.

    Tatu, Huwa Kuna mabadiliko ya hapa na pale ambayo huwa yanatokea karibia kwenye kila sekta, ambayo huwa yanapelekea aidha kipato kushuka au hata muda mwingine kukoma kabisa. Ninachoshauri rafiki yangu Ni wewe kujiwekea Kinga kwa kuhakikisha unakuwa na chanzo zaidi ya kimoja Cha kipato.

    Nne, ili kuingiza fedha kwa nyakati tofauti. Chanzo maarufu ambacho watu wanacho ni ajira. Ajira huwa inaingiza fedha kwa MTU mara moja kwa mwezi, mwishoni mwa mwezi, lakini unaweza kuwa na vyanzo vingine ambavyo vinaweza kukuingizia kipato tofauti na ajira na hivyo kukupa uhakika zaidi.

    Tano, kufanya mishahara yako ikutane. Imezoeleka miongoni mwa wafanyakazi kuwa mishahara huwa haikutani, vyanzo vingi vya kipato vina uwezo wa kuifanya mishara yako iweze KUKUTANA.

    Sita, vyanzo vingi vya kipato, vina uwezo wa kukufanya ufanye uwekezaji. Kama mshahara pekee ulikuwa haukutoshi, sasa vyanzo vingi vya kipato, vinakuwezesha wewe kufanya uwekezaji pia. Chanzo kimoja kinaweza kutumika kwa ajili ya uwekezaji na chanzo kingine kikasaidia kwenye matumizi ya hapa na pale ya kila siku 

    Sifa ya vyanzo vingi vya kipato

    Kuna watu baada ya kusikia kuwa wanapaswa kuwa wanapaswa kuwa na vyanzo vingi vya kipato wameenda kichwakichwa na kujikuta waanzisha vyanzo vingi vya kipato, ilimradi tu wameanzisha Sasa zifuatazo Ni sifa za vyanzo vya kipato.

    Kwanza, vyanzo vyako vinapaswa kuwa kwenye sekta tofauti. Yaani, usitegemee sekta moja tu kwa ajili ya kukuingizia kipato. Mfano kipindi Cha Corona Kuna baadhi ya sekta zilikwama au kufungwa kabisa, lakini kipindi hichohicho sekta nyingine zilizidi kukua na kuwa na kuwa Bora ZAIDI. Sasa kwa MTU ambaye anategemea sekta Moja kwa ajili ya kuingiza kipato, na Kama sekta hiyo iliyumba basi, ni wazi kuwa MTU huyu Atakuwa aliyunva pia.

    Kwa hiyo basi, vyanzo vyako visiwe kwenye sekta moja.

    Kama ni kampuni au biashara, usiwe na bidhaa moja tu, maana Kuna baadhi ya bidhaa huwa zinauzika Sana kipindi fulani. Sasa ikitokea unategemea chanzo kimoja Cha kipato na kipindi hicho chanzo hicho kikakwama, Basi Ni wazi kuwa na wewe utakwama.

    Pili, Vyanzo vyako visikutegemee wewe kufanya kazi ili viingize kipato vyanzo vyako vyote rafiki yangu havipaswi kuwa vinakutegemea wewe kufanya kazi moja kwa moja ili uingize kipato.

    Ndio chanzo kimoja au viwili vinaweza Kuwa vinakutegemea wewe kufanya kazi moja kwa moja, ila kama unavyojua rafiki yangu. Kufanya kazi huwa juna ukomo. Unafanya kazi na unachoka. Kumbe basi, baadhi ya vyanzo vya kipato havipaswi kuwa vinakutegemea wewe ufanye kazi moja kwa moja ili uingize kipato. Vingine vinapaswa kuwa na uwezo wa kukuingizia kipato hata kama hufanyi kazi. Vingine unapaswa kufanya kazi Mara moja na vikulipe milele. Mfano mzuri ni Kama kuandika kitabu. Ukiandika kitabu, unafanya kazi Mara moja, Ila kipato kinachotokana na kazi hiyo ya Mara moja kinakuwa cha kudumu maisha yako yote.
    Au kutengeneza video kama YouTube. Ukishaitengeneza video hii ndio unakuwa umeitengeneza.

    Makosa kwenye vyanzo vingi vya kipato

    Kosa la kwanza huwa ni kuanzisha vyanzo vyote vya kipato kwa wakati mmoja.
    Kutegemea na Aina ya chanzo Cha kipato, baadhi ya vyanzo vya kipato haviwezi kuanzishwa kwa wakati mmoja. Kuna baadhi ya vyanzo vinapaswa kuanzishwa kwa nyakati tofauti, ili kukupa wewe mwanya wa kujenga chanzo kimoja kwa uhakika kwanza.

    Kosa la pili huwa Ni kuchanganya hela kutoka kwenye kila chanzo. Wengi wanapopokea hela kutoka kwenye vyanzo mbalimbali huwa wanazichanganaya na kuzitumia bila ya mwelekeo wowote. Hivyo basi, nashauri uwe na utaratibu wa kutofaytisha hela zinazotoka kwenye chanzo kimoja na hela zinazotoka kwenye chanzo kingine.

    Na ikiwezekana kabisa uwe na malengo kwamba fedha itakayotoka sehemu fulani, nitaielekeza kwenye kufanyia kazi Jambo fulani wakati fedha ambayo itatoka kwenye chanzo kingine utafanya jambo jingine.

    Tatu ni kutoa hela kwenye chanzo kimoja na kuiweka kwenye chanzo kingine.
    Ni wazi kuwa pale unapoakzisha chanzo fulani Cha kipato, unakuwabunaweka fedha. Ila inabidi ifikie hatua ambapo wewe utakuwa huweki fedha, badala yake chanzo kiwe kinakupa wewe kipato.

    NI VYANZO KIASI UNAPASWA KUWA NAVYO.


    Hili nalo neno! Tafiti mbakimbali zimeonesha kuwa vyanzo vinne mpaka vitano, vinatosha sana kukufanya uishi maisha mazuri.

    Kumbe basi idadi yako ya kwanza ya vyanzo vyako vya kipato ipiganie iwe nne mpaka saba. Na Hivi viwe vyanzo vya uhakika.


    Mpango wako wa kuongeza kipato Cha ziada mwaka 2023 ukoje? Unafanyaje ili kuhakikisha unakuwa na chanzo kingine Cha ziada?

    Karibu kwenye Semina ya kufungua mwaka 2023. Semina hii itaendeshwa kwa njia ya mtandao na imelenga kuhakikisha inakupa wewe mbinu za kuongeza kipato chako mara mbili mpaka mara kumi zaidi.

    Semina hii itadumu kwa siku 15 kuanzia Januari 15 mpaka tarehe 30.
    Kwa siku zote hizo 15 utalipia 15,000/- tu.

    Unataka kuongeza kipato chako Mara mbili mpaka Mara kumi zaidi ndani ya mwaka 2023, Basi jiunge kwenye Semina hii.

    Karibu sana

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.

    Godius Rweyongeza ni mwandishi wa vitabu zaidi zaidi ya 20. Na ni mwendeshji wa mtandao wa Songambele. Amekuwa akiandika kwenye huu mtandao huu tangu mwaka 2016. Kitabu chake cha Kutoka Sifuri Mpaka Kileleni kimekuwa #1Best Seller kwa muda sasa kwenye mtandao wa GETVALUE

    Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.

    Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.

    Mtandaoni, vitabu vyake unaweza kuvipata kupitia mtandao wa GETVALUE kwa KUBONYEZA HAPA

  • Jinsi Ya Kufungua akaunti ya mfuko wa FAIDA (FAIDA FUND)

    Juzi niliandika makala kuhusu mfuko wa FAIDA (FAIDA FUND). Swali ambalo nilipokea kutoka kwa wengi waliosoma makala hii lilikuwa ni kwa namna gani naweza KUFUNGUA akaunti kweye mfuko huu wa FAIDA.

    KITU hiki kimenisukuma nikuandalie Makala nyingine kukuonesha ni kwa namna gani unaweza KUFUNGUA akaunti kwenye mfuko huu wa FAIDA. Unajua unawezaje kufungua akaunti.

    Fanya yafuatayo.

    BONYEZA *152*00# kwenye simu yako.

    Kisha chagua namba 1 kama inavyoonekana hapo chini

    Baada ya hapo chagua namba 6 Kama inavyoonekana hapo chini

    kisha chagua namba 1 tengeneza akaunti ya binafsi.

    Baada ya hapo utaweka majina yako kamili

    Kisha utaweka tarehe, mwezi na mwaka wa kuzaliwa

    Ukibonyeza hapa, kuna hatua zaidi, utapata. Zifuate Mpaka mwisho ili ukamilishe kusajili akaunti yako.

    Ukishasajiri akaunti yako, endelea mbele kwa kuhakikisha unaweka kiasi kisichopungua elfu kumi kwenye akaunti. Kwa kufanya hivyo, utakuwa umefungua akaunti.

    kila la kheri

    Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.

    Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.

    Mtandaoni, vitabu vyake unaweza kuvipata kupitia mtandao wa GETVALUE kwa KUBONYEZA HAPA

  • Kitu Kimoja Kinachopaswa Kukufanya Usome Vitabu Vya Hardcopy badala ya Softcopy

    Rafiki yangu, linapokuja suala la softcopy au hardcopy watu wamekuwa wanakuwa na mtazamo tofauti. Wapo wanaopendelea hardcopy na wapo wanaopendelea softcopy na wengine wanapendelea audiobook kama huyu hapa

    Kwa upendeleo wowote atakaokuwa nao mtu, hakuna ambaye anakuwa sahihi wakati mwingine akiwa hayuko sahihi. Kitu kikubwa sana ni kupata maarifa yaliyo kwenye kitabu na kuyafanyia kazi.

    Ila siku ya leo ninapenda nikwambie sababu hii moja ambayo inapaswa kukusukuma wewe kupata vitabu vya nakala ngumu au audiobook na siyo softcopy.

    Na sababu hii ni kwamba, kama una watoto au mtoto mdogo. Hii ni sababu kubwa kwa nini unapaswa kununua vitabu vya nakala ngumu au vitabu vilivyosomwa (audiobook).

    Ili unielewe vizuri hapa naomba nieleze kwa undani kidogo, mtoto mdogo ana tabia ya kuiga kile ambacho mzazi anakuwa anafanya.

    Unapokuwa unasoma kitabu kwenye simu, mtoto anakuwa hajui kama unasoma kitabu au husomi kitabu. Kitu hiki kinamfanya mtoto awe anapenda kushika simu. Ila unapokuwa unasoma kitabu cha kushikika (hardcopy), mtoto anakuwa anaona. Kitu hiki kinamfanya mwanao apendelee zaidi kushika kitabu cha nakala ngumu na hivyo kumjengea tabia ya kuanza kusoma vitabu mapema.

    Hivyo, kama wewe ni mzazi, sambamba na kusoma vitabu vya nakala laini (sofcopy/ebooks), hakikisha unakuwa na nakala ngumu kadhaa pale nyumbani kwako. Pale ambapo utakuwa na mtoto,  usisome kitabu kwenye simu, badala yake soma kitabu cha nakala ngumu.

    Mpe na mtoto kitabu ashike, ili aanze kuzjenga tabia ya kusoma vitabu mapema sana.

    Unatakiwa pia kupenda vitabu vya kusikiliza unapokuwa na mtoto. Kwanza inasaidia kumwongezea mtoto misemo ya ziada. Na tafiti zinaonesha kwamba watoto wanaokuwa wanaojifunza misemo mingi, huwa wanajiamini mbele ya watu kuliko ambao wanakuwa na misemo kidogo. Lakini pia watoto wanaokuwa na misemo mingi huwa ni wawasilishaji wazuri wa mada. Ssa wewe hupendi mwanao awe mwasilishaji mzuri wa mada? Naamini wewe ni kama mimi, na ungependa mwanao awe gwiji wa kuongea na kuwasilisha mada mbele za watu kwa kujiamini na bila uoga wowote.

    Watu wengi huwa wanapenda pale ambapo huwa wanaona  mtoto mdogo anasimama mbele ya watu na kuongea kwa kujimini. Wengi hupiga makofi na kumpongeza kwa namna ambavyo wanaweza, ikiwa ni pamoja na kutoa zawadi ya pesa.

    Naamini na wewe unaweza kumlea mwanao hivyo, kwa kuanza kumjengea misingi sahihi sasa hivi.

    Nakutakia siku njema

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.

    Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.

    Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.

  • Jinsi ya kupata matokeo ya tofauti mwaka 2023

    Kuna kitu kimoja nakijua kuhusu wewe rafiki yangu. Na kitu hiki ni kwamba mwaka 2023, ungependa kupata matokeo ya tofauti. Matokeo ya tofauti kwenye kila eneo ambalo utakuwa ukilifanyia kazi.

    Kama unataka kupata matokeo ya tofauti mwaka 2023, basi hakikisha kwamba unakuwa tayari kufanya vitu vya tofauti. Yaani, vitu ambavyo hujawahi kufanya siku za nyuma.

    Huwezi kutegemea kupata matokeo ya tofauti mwaka 2023, huku ukiwa unaendelea kufanya vitu vile vile bila ya kubadilika.

    Ni lazima uwe tayari kufanya hivi vitu vya tofauti, labda swali la kujiuliza ni vitu gani vya tofauti ambavyo naweza kufanya mwaka 2023 vikanipa matokeo ya tofauti.

    VIfuatavyo ni vitu vitatu vya tofauti ambavyo unaweza kufanya mwaka 2023, vikakupa matokeo ya tofauti kwenye kipato chako, kwenye uwekezaji, kwenye afya yako, kwenye watu unaokutana nao na kwenye kila kitu unachofanya. Kiufupi kama unataka kuufanya mwaka 2023, uwe mwaka wa baraka na kila kitu utakachogusa basi kibadilike kuwa dhahabu, basi hakikisha kwamba unafanyia kazi yafutayo.

    Kwanza hakikisha kwamba una malengo ambayo unayafanyia kazi. rafiki yangu, bila malengo makubwa mwaka 2023, hutaweza kutoboa. Kwa hiyo, kama kuna kitu ambacho unapaswa kuanza nacho mwaka 2023, basi ni kuhakikisha kwamba unaanza kwa kuweka malengo. Weka malengo na yafanyie kazi.

    Pili, kuwa tayari kuchukua hatua. Rafiki yangu, bila ya kuchukua hatua, malengo uliyojiwekea hayataweza kutimia. Ni lazima uwe tayari kuchukua hatua hata kama ni kidogo.

    Wengi hufikiri kwamba ili wafanikishe malengo yao, basi wanapaswa kusuburi siku moja ya mwisho wa mwaka ambapo malengo yao yatatimia, ukweli ni kwamba malengo makubwa huwa hayatimii kwa siku moja ya mwisho wa mwaka. Badala yake yale unayokuwa unayafanya kila siku, kila kukicha ndiyo yanakupelekea wewe kwenye kufanikisha malengo yako au kufeli kwenye kufanyia kazi malengo yako. Ndio maana nimekuandalia kitabu murua kabisa cha NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA. Ukipata kitabu hiki, utajifunza na kuona ni kwa namna gani unaweza kufanyia kazi malengo makubwa kwa kuanza kidogo kidogo.

    Mambo madogo madogo unayoyafanyia kazi leo hii, yana uwezo wa kukuletea matokeo makubwa. Hakikisha kwamba unapata nakala ya kitabu hiki cha kipekee leo hii. Nakala yako ni 20,000/- tu. na utatumiwa popote pale utakapokuwa nchini.

    Tatu ni kukaa na watu sahihi. Watu sahihi rafiki yangu watakufanya uweze kupiga hatua na kufika mbali. Hivyo basi, kama unataka kuufanya mwaka 2023, uwe  mwaka wa kipekee hakikisha kwamba unaungana na timu ya watu sahihi. Kuna timu ya watu sahihi ambayo unahitaji kujiunga nayo mwaka 2023, na timu hii ni ya watu ambao wamejiunga na semina ya kufungua mwaka 2023. Ukijiunga na timu hii utakutana na watu sahihi ambao wana mtazamo chanya kama wewe.

    hawa wote utakutana nao, endapo tu utajiunga na semina ya kufungua mwaka 2023.

    Karibu kwenye semina hii ya kipekee sana.

    Kila mwanzo mwa mwaka na katikati mwa mwaka huwa Kuna semina ambayo huwa naiendesha.

    Mwakani wakati wa kufungua  mwaka mpya tunatarajia kuwa na semina ya kufungua mwaka ambayo itafanyika kuanzia tarehe 15.

    Na itadumu kwa siku 15 mfululizo. Semina hii ya kipekee ambayo itafanyika kwa njia ya mtandao, inalenga kukupa maelezo ya kina yatakayokusaidia kuuanza mwaka mpya kwa mtazamo sahihi na kuuweza kuufanikisha kwa viwango vikubwa sana. Semina hii inaitwa JINSI YA KUONGEZA THAMANI YAKO 2023.
    Kwenye Semina hii utajifunza Mambo
    1. Namna ya kuongeza thamani yako
    2. Namna ya kuongeza kipato chako mara mbili mpaka mara kumi zaidi
    3. Njia za kuweka malengo na kuyafanyia kazi kwa usahihi ndani ya mwaka 2023.
    3. Nguvu ya vitu vidogo kwenye kuongeza thamani yako binafsi na mengine mengi

    Hii Ni semina ya siku 15 mfululizo ambayo imeshiba mambo ya msingi sana yanayokufaa wewe na yatakayokusaidia wewe kuuanza mwaka kwa usahihi na kupiga hatua na kufika mbali.

    Katika siku hizi 15 utapata masomo 15 yaliyoandaliwa kwa kina na ambayo yatakusaidia wewe kuanza KUONGEZA THAMANI YAKO ndani ya mwaka 2022.

    Ni matarajio yangu kuwa baadaa ya semina hii, utakuwa na mbinu za kukusaidia wewe kuongeza thamani yako binafsi na kipato chako walau Mara mbili zaidi

    Hakikisha kwamba haukosi Semina hii, ya kipekee sana

    Semina itafanyika lini?
    Itaanza tarehe 15 Januari na itadumu kwa siku 15

    Semina itafanyika wapi?
    Semina itafanyika mtandaoni (WhatsApp) kwenye kundi maalumu la WhatsApp.

    Je, Kuna ada ya kujiunga na Semina.
    Ndiyo ada ipo. Ada ya semina ni 15,000/- tu. Kwa kila mshiriki kwa siku zote za semina.
    Mwisho wa kulipia ni tarehe 10 Januari.

    Njoo uuanze mwaka wako kwa kiusahihi na kwa kupata mwongozo utakaokusaidia kuufanyia kazi mwaka mpya kutokea kwenye nafasi nzuri.

    Kuthibitisha ushiriki wako. Tuma malipo yako kwenye Namba ya simu 0755848391 jina ni GODIUS RWEYONGEZA.

    Karibu sana

    Whatsap group la semina: https://chat.whatsapp.com/FbzmwEVkObKIuqeR4pIZmu

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza
    Unaweza kusoma makala na mafunzo yake zaidi kwenye blog yake ya SONGAMBELE (www.songambele.co.tz)

  • Faida Tatu KUBWA unazopata pale unapowekeza kwenye hisa

    Kitabu hiki kinapatikana kwa elfu tano tu (sotfcopy0
    Kitabu hiki kinapatikana kwa elfu tano tu (sotfcopy)

    Rafiki yangu, umewahi kuwaza kwamba ukiwekeza kwenye hisa utanufaika na kitu gani?

    Kuna faida nyingi za kuwekeza kwenye hisa, ila kwenye hii makala ya siku ya leo ningependa kuongelea faida mbili kubwa kwa haraka

    Faida ya kwanza ya kuwekeza kwenye hisa ni kupata ongezeko la thamani.  Ongezeko la thamani ni pale unaponunua hisa kwa bei ya chini na baadaye kuja kuiuza kwa bei ya juu.

    Mfano mwaka, 2022 hisa za CRDB zilikuwa zinauzwa na kununuliwa kwa bei ya shilingi 150. Sasa hivi hisa hizohizo zinauzwa shilingi 380. Hii ndio kusema kwamba aliyenunua hisa kipindi hicho cha mwaka 2020 kwa shilingi 150, sasa hivi kila hisa yake ina thamani ya shilingi ya 380. Kumbe hapa kila hisa ina ongezeko la thamani la shilingi 230 na zaidi.

    Na hiyo ni pesa ambayo imeongezeka bila ya wewe kutoa jasho wala kufanya kazi yoyote ile. Ulichofanya wewe ni kuwekeza fedha yako tu.

    Hii ndiyo faida kubwa ambayo watu wanaomiliki hisa huwa wanaipata.

    Faida nyingine ambayo utaipata kama utamiliki hisa ni  GAWIO. Gawio ni faida ambayo wanahisa wanapata. Faida huwa inapatikana kulingana na wingi wa hisa ambazo mtu anakuwa anamiliki kwenye kampuni husika. Kumbe basi, hisa ni kitegauchumi ambacho kila mtu anapaswa kuwa nacho na anapaswa kukimiliki.

    3. Hisa ni kipimo cha utajiri. Leo hii dunia inamfahamu Elon Musk kama tajiri mkubwa duniani. Ila tajiri huyu siyo kwamba ana mabilini yote ya fedh mfukoni. Utajiri wake uko kwenye hisa anazomiliki kwenye makampuni ya TESLA, SPCAEX na makampuni mengine. Kumbe hisa, ni kipimo cha utajiri wa mtu husika. Na wewe tunaweza kupima utajiri wako kwa kuangalia vitegauchumi ulivyo navyo ikiwa pamoja na hisa unazomiliki..

    Rafiki yangu, kama bado hujawa na kitega uchumi hiki cha kipekee basi hakikisha kwamba unakuwa nacho.

    PATA KWANZA NAKALA YA KITABU CHA MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE. Hiki kitabu kitakupa mwongozo wewe wa kuweza kuanza kuwekeza kwenye hisa, hatifungani na vipande.

    Kitabu hiki kinapatikana kwa elfu tano tu (sotfcopy0
    Kitabu hiki kinapatikana kwa elfu tano tu (sotfcopy)

  • Njoo Uongeze Kipato Chako Mara Mbili Zaidi Mwaka 2023

    Kuna kitu kimoja nilicho na uhakika nacho juu yako rafiki yangu…Kitu hiki ni kwamba, ungependa kuongeza kipato chako walau mara mbili zaidi ndani ya mwaka 2023! Na hiki ni kitu ambacho ningependa kukusaidia ukifanikishe ndani ya mwaka 2023!

    Kuanzia tarehe 15 januari 2023, tutakuwa na semina ya kufungua mwaka mpya 2023, lengo kubwa la semina hii, ni kukupa mbinu za kukusaidia wewe kuweza kuongeza kipato chako walau mara mbili zaidi ya kilivyo sasa.

    Kwa mbinu tutakazoona kwenye hii semina, ni uhakika kwamba unaenda kuongeza kipato hako walau mara mbili zaidi ndani ya mwaka 2023!

    Hii semina siyo ya kukosa hata kidogo.

    Semina hii itaanza tarehe 15  januari na itadumu kwa siku 15 mfululizo.

    Gharama ya semina hii ni 15,000/- tu. sawa na shilingi elfu moja kwa kila siku ambayo utahudhuria semina. Ili kuhudhuria semina hii ya kipekee utapaswa kulipia hiki kiasi cha shilingi 15,000/- tu. namba ya malipo ni 0755848391 jina ni GODIUS RWEYONGEZA. Ukifanya malipo, utakuwa umethibitisha ushiriki wako kwenye semina

    Wahi sasa maana nafasi kwenye hii semina ni chache kwa watu maalumu tu!

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.

    Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.

    Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.

  • Mfuko wa FAIDA (FAIDA FUND): Unawekeza au Huwekezi?

    Watumishi Housing Investment (WHI) wameanzisha mfuko wa uwekezaji wa pamoja ambao wanauita MFUKO WA FAIDA au kama unaielewa vizuri lugha ya kigeni basi unasema FAIDA FUND. Mfuko wao ni mfuko ulio wazi (open-endend). Kama bado hujasoma kitabu changu cha maajabu ya kuwekeza kwenye hisa, hatifunagni na vipande lazima tu utakuwa unajiuliza mfuko ulio wazi maana yake ni nini?

    Mfuko ulio wazi ni mfuko ambao pale unapotaka kununua vipande meneja wa mfuko anakutengenezea vipande vyako. Na pale unapotaka kuuza vipande meneja wa mfuko ananunua vipande vyako.

    Yaani, tuchukilie mfano, mimi naanzisha mfuko wa uwekezaji wa pamoja. Na watu mnakusanyika kununua vipande, labda kipande kimoja ni shilingi mia moja. na watu wa kwanza, mnanunua vipande elfu moja (1000). Mfuko hapo hapo utakuwa na vipande elfu moja. Labda baada ya siku kumi za kununua vipande anatokea mmoja ambaye anataka kuuza vipande vyake 200. Anauza vipande na mimi meneja wa mfuko nanunua hivyo vipande na kumpa hela yake. Mfuko unabaki na vipande 800. Wakati kesho yake anatokea mwingine ambaye anataka kunununua vipande mia tano. Na huyo anaunua vipande na hivyo vipande vya mfuko sasa vinakuwa 1300/-.

    Kwa hiyo, mfuko ulio wazi huwa una sifa ya kuongezeka kwa vipande pale wanunuaji wanaponunua na kupungua kwa bei pale wauzaji wanapouza.

    Mfuko ulio wazi (open ended) ni tofauti kabisa na mfuko uliofungwa (closed ended) ambao wenyewe huwa una idadi ya kamili ya vipande, na idadi hiyo huwa haiongezeki wala kupungua. Kama mfuko una vipande 1000. Vinabaki kuwa hivyo hivyo tu miaka yote. Ili ununue vipande kwenye mfuko uliofungwa, lazima awepo mtu anayeuza. Na ili uuze, lazime kuwepo anayenunua. Utagundua kitu hiki ni tofauti na mfuko ulio wazi ambao meneja wa mfuko ndiye ananunua au kukuuzia vipande. Kama huelewi, hakikisha unapata kitabu changu cha MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE kwa 20,000 tu, nakala ngumu, na 10,000 tu nakala laini (softcopy).  Kipate kitabu hiki kwa ajili ya kuongeza maarifa zaidi pia kuhusu eneo hili la uwekezaji.

    Kitabu hiki kinapatikana kwa elfu tano tu (sotfcopy0
    Kitabu hiki kinapatikana kwa 20,000/- tu

    Mimi niache niendelee mbele kuuongelea mfuko wa FAIDA ulioanzishwa na WHC.

    Mfuko upo chini ya WHI ambao wamesajiliwa na kisheria chini ya soko la mitaji (CMSA).

    Madhumuni ya mfuko

    •   Mfuko huu   ni    mpango    ulio    wazi unaotoa fursa nyingine ya uwekezaji kwa Watanzania hasa wa kipato cha kati na cha chini kupitia uwekezaji katika vipande ili kupata mapato shindani kupitia ukuaji wa mitaji.

    • Kuwajengea watanzania utamaduni wa kuwekeza katika Masoko ya Fedha na Mitaji na kuweka akiba.

    Anayestahili kuwekeza kwenye huu mfuko

    Mfuko huu unatoa mwanaya wa mtu yeyote, (ambaye ni mtanzania au wa nje ya nchi) kuwekeza kwenye mfuko huu. Lakini pia taasisi kama benki, mifuko ya pension, taasisi za kiserikali,  taasisi zisizo za kiserikali, taasisi za kijeshi, makampuni n.k.

    Kiwango cha chini cha kuwekeza kwenye mfuko huu

    Kiwango cha chini cha kuwekeza kwenye huu mfuko ni elfu kumi, pale unapofungua akaunti mara ya kwanza. Baada ya kufungua akaunti, unaweza kuendelea kuwekeza zaidi kwenye huu mfuko kwa kuongeza kiwancho cha chini kabisa cha shilingi elfu tano.

    Kiwango cha juu cha kuwekeza

    Hakuna kiwango cha juu cha kuwekeza. Kwa hiyo, kama una mabilioni ya kuwekeza, unaweza kuyawekeza bila shida yoyote kwenye huu mfuko. Lakini bado kama huna mabilioni makubwa sana, unaweza kuendelea na utaratibu wako wa kuwekeza kwenye huu mfuko kadiri utakavyojiwekea, kwa kuweka kiwango cha chini kabisa cha elfu tano (5,000/-) kila utakapohitaji kuwekeza.

    Gharama za kujiunga na mfuko (Entry load)

    Kwa kawaida huwa ukitaka kununua hisa, huwa kuna gharama ambayo mtu unalipia ili kununua hisa. Na pale unapotaka kuuza hisa zako, kuna gharama ambazo unakatwa. Hizi gharama kwa Kiswahili tunaweza kuziita tozo za kiujiunga (entry load) au tozo za kujitoa (exit load).

    Wakati wa kujiunga na mfuko huu au wakati wa kujitoa kwenye huu mfuko, hakuna gharama yoyote ile ya kujiunga au kujitoa.

    Thamani ya kipande

    Thamani ya mwanzo ya kipande ni Tsh 100/=. Hii itatumika wakati wa mauzo ya awali na baada ya hapo kipande kitauzwa kulingana na thamani halisi.

    Ambapo kipande kitapanda au kushuka kulingana na mwenendo wa soko kwa wakati husika.

    NB: Mpaka sasa hivi mfuko upo kwenye hatua za awali za kuuza vipande vyake. Hivy, kama unasoma ujumbe huu kabla ya tarehe 31 Disemba, unaweza kununua vipande kwa bei ya awali ya vipande.

    Ukwasi

    Uuzaji wa vipande utafanyika kila siku baada ya mienzi mitatu tangu kumalizika kipindi cha mauzo ya awali. Mfuko utatuma malipo ya mauzo ya vipande ndani ya siku tatu za kazi baada ya kupokea maombi katika Makao Makuu ya Watumishi Housing Investments. Fedha za mauzo zitatumwa moja kwa moja katika akaunti ya benki ya mwekezaji au simu ya mkononi iliyosajiliwa.

    Sera za uwekezaji kwenye mfuko

    Mfuko utawekeza katika masoko ya fedha kwa asilimia 100%. Kiwango cha uwekezaji katika masoko ya fedha na Dhamana kitalenga kupata mapato makubwa katika soko.

    Muda wa kuendesha mfuko

    Mfuko huu ni wa kudumu kwa mujibu wa Waraka wa Makubaliano.

    Faida za kikodi

    Kwa mujibu wa sheria za nchi,mgawanyo wa mapato ya Mfuko yamesamehewa kodi ya mapato kwa wawekezaji.

    Hayo ni baadhi ya mambo ambayo nimekuandalia kuhusu  mfuko huu.

    NB: 1. Kabla hujachukua hatua ya kuwekeza kwenye huu mfuko, nashauri uhakikishe umesoma kitabu changu cha MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE ili uweze kuelewa zaidi dhana ya uwekezaji.

    2. Mwandishi wa makala hii hauhusiki kwa vyovyote vile na faida au hasara utakayopata kutokana na uwekezaji utakaoufanya kwenye huu mfuko. Ni muhimu kuhakikisha kwamba umepata ushauri wa watalaam kabla ya kufanya uwekezaji.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.

    Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.

    Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.

  • SEMINA YA KUFUNGUA MWAKA: Karibu kwenye Semina ya kufungua mwaka 2023

    Kila mwanzo mwa mwaka na katikati mwa mwaka huwa Kuna semina ambayo huwa naiendesha.

    Mwakani wakati wa kufungua  mwaka mpya tunatarajia kuwa na semina ya kufungua mwaka ambayo itafanyika kuanzia tarehe 15.

    Na itadumu kwa siku 15 mfululizo. Semina hii ya kipekee ambayo itafanyika kwa njia ya mtandao, inalenga kukupa maelezo ya kina yatakayokusaidia kuuanza mwaka mpya kwa mtazamo sahihi na kuuweza kuufanikisha kwa viwango vikubwa sana. Semina hii inaitwa JINSI YA KUONGEZA THAMANI YAKO 2023.
    Kwenye Semina hii utajifunza Mambo
    1. Namna ya kuongeza thamani yako
    2. Namna ya kuongeza kipato chako mara mbili mpaka mara kumi zaidi
    3. Njia za kuweka malengo na kuyafanyia kazi kwa usahihi ndani ya mwaka 2023.
    3. Nguvu ya vitu vidogo kwenye kuongeza thamani yako binafsi na mengine mengi

    Hii Ni semina ya siku 15 mfululizo ambayo imeshiba mambo ya msingi sana yanayokufaa wewe na yatakayokusaidia wewe kuuanza mwaka kwa usahihi na kupiga hatua na kufika mbali.

    Katika siku hizi 15 utapata masomo 15 yaliyoandaliwa kwa kina na ambayo yatakusaidia wewe kuanza KUONGEZA THAMANI YAKO ndani ya mwaka 2022.

    Ni matarajio yangu kuwa baadaa ya semina hii, utakuwa na mbinu za kukusaidia wewe kuongeza thamani yako binafsi na kipato chako walau Mara mbili zaidi

    Hakikisha kwamba haukosi Semina hii, ya kipekee sana

    Semina itafanyika lini?
    Itaanza tarehe 15 Januari na itadumu kwa siku 15

    Semina itafanyika wapi?
    Semina itafanyika mtandaoni (WhatsApp) kwenye kundi maalumu la WhatsApp.

    Je, Kuna ada ya kujiunga na Semina.
    Ndiyo ada ipo. Ada ya semina ni 15,000/- tu. Kwa kila mshiriki kwa siku zote za semina.
    Mwisho wa kulipia ni tarehe 10 Januari.

    Njoo uuanze mwaka wako kwa kiusahihi na kwa kupata mwongozo utakaokusaidia kuufanyia kazi mwaka mpya kutokea kwenye nafasi nzuri.

    Kuthibitisha ushiriki wako. Tuma malipo yako kwenye Namba ya simu 0755848391 jina ni GODIUS RWEYONGEZA.

    Karibu sana

    Whatsap group la semina: https://chat.whatsapp.com/FbzmwEVkObKIuqeR4pIZmu

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza
    Unaweza kusoma makala na mafunzo yake zaidi kwenye blog yake ya SONGAMBELE (www.songambele.co.tz)

X