-
Kitu Hiki Ndicho Kinawafanya wengi washindwe kufanya makubwa
Habari ya leo rafiki yangu, bila shaka unaendelea vyema kabisa.
Leo ningependa nikwambie kitu ambacho kimekuwa kinawakwamisha watu wengi na kuwafanya washindwe kufanikisha makubwa . Kitu Hiki siyo kingine bali ni kukosa malengo makubwa ambayo wanayafanyia kazi kwenye maisha yao.
Ili uweze kunielewa vizuri hapa naomba nianze kwa kukupa mfano wa kawaida tu, unaweza kukuta MTU anadaiwa hela.
Anapambana kwa nguvu zake zote kutafuta pesa ili alipe deni lake.Na kweli pesa anapata na deni analilipa, Ila akishamaliza kulipa deni anakosa msukumo wa kuendelea kupambana na kutafuta pesa zaidi ili kununua Uhuru wake wa Kifedha.
Au unaweza kukuta mtu anatembea kinyonge. Lakini inapotokea hatari ya ghafla, MTU huyo anaruka na kukimbia Kama vile siyo yeye.
Huu uwezo tulionao siyo TU tuitumie wakati wa hatari peke yake, bali tuitumie pia muda mwingine ambao siyo wa hatari pia. Kwa ajili ya kufanya makubwa
Kinachowafanya wengi washindwe kuutumia huu uwezo mkubwa Ni kwa sababu hawana malengo. Unapokuwa hauna malengo, maana yake unashindwa kujisukuma maana hauna kitu chochote cha kukusukuma.
Rafiki yangu Mara zote kuwa na melengo ambayo unayafanyia kazi. Malengo yawe makubwa na yakusukume muda wote kujituma na kufanya kazi kwa bidii.
Kama hauna malengo basi kaa chini Uweke malengo sasa.
Malengo ni Moto wa kukusukuma wewe kufanya Yale ambayo wengine wanaona kama hayawezekani.
Tenga muda leo hii ukae chini Uweke malengo. Muda huu ni uwekezaji ambao unaufanya. Kwa ajili ya kesho yako.
Nataka tu ufahamu kuwa bila ya kuwa na malengo, hutajisukuma kufanya kitu Cha maana.
-
Jinsi ya kupata mafunzo yenye hadhi ya chuo
Brian Tracy anasema kuwa muda ambao tunautumia kwa siku tukisafiri na Kutembea kutoka eneo moja kwenda jingine, ukiuunganisha baada ya mwaka mmoja Ni sawa na semester moja ya chuo!
Hii ndio kusema Kuwa ukiutumia vizuri huu muda, kujifunza. Baada ya mwaka utakuwa umepata kozi yenye hadhi ya semester ya chuo.
Nataka hili likutafakatishe uanze kuona Ni kwa namna gani umekuwa unapoteza muda mwingi ambao huutumii wakati wa safari na wakati unatembea. Muda ambao kwako ungeweza kuwa muda wa kujifunza na kupata mafunzo yenye hadhi ya kozi ya chuo.
Na nitafurahi ukianza kuutumia vizuri huu muda.
Kwa kulifahamu hili, Ni nimekuandalia vitabu vyangu kwa mfumo wa sauti (Audiobook) ili uweze kuutumia muda wako wa safari kusikiliza Audiobook hizi.
Na hiki ndicho kitu ambacho nataka tufanye siku ya leo.
Pata Audiobook zangu tatu kwa kulipia Audiobook moja tu.
Kwa kawaida Audiobook moja huwa naiuza kwa shilingi 20,000/- kwa hiyo Audiobook tatu ni sawa 60,000/-
Ila Leo hii nataka ulipie Audiobook moja.nikupe nyingine mbili bure kabisa
Audiobook zilizopo Ni pamoja na
1. NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA
2. JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO
3. MAISHA NI FURSA: ZITUMIE ZIKUBEBE
Lipia Audiobook moja siku ya leo. Upate nyingine mbili bure.
Karibu
Namba ya malipo ni 0755848391
Jina ni GODIUS RWEYONGEZA
Karibu.
-
Leo ni siku ya waandishi duniani: Mambo mawii unayopaswa kufahamu
Habari ya siku ya hii ya kipekee sana rafiki yangu. leo ni siku ya waandishi duniani. Mimi ni kiwa mmoja wa waandishi, hii siku inanihusu sana. lakini pia inakusu wewe, maana hakuna mwandishi bila msomaji. Hivyo, siku ya leo ni siku yetu sote. Kwa hiyo, nitakuwa sijakosea kusema kwamba kheri ya siku ya waandishi kwako!
Sasa kwenye siku hii ya waandishi kuna mambo yafuatayo ambayo ningependa uweze kuyafahamu.
Kwanza, ni kuwa tumia saa chache zilizobaki, kuhakikisha kuwa unaandika ujumbe mfupi kwa mwandishi umpendaye. Mtumie ujumbe wa kumpongeza ili kumtia moyo kwa kazi yake nzuri anayofanya.
Pili, kujinyakulia kitabu cha jinsi ya kuwa mwandishi mbobevu. Mwakani ningependa kuona kitabu chako ili wakati tunasherehekea waandishi mwaka 2023. Na wewe uwe kwenye hiyo orodha.
Ndiyo maana nataka na wewe ujinyakulie ofa ya kitabu cha JINSI YA KUWA MWANDISHI MBOBEVU. Gharama ya kitabu hiki ni 5,000/- ila kwa leo tarehe 1 na kesho tarehe 2, utakipiata kwa 4,000/.
Lengo langu nataka mwakani, wewe uwe miongoni mwa waandishi tutakaosherehekea sikukuu yao.
Tuma 4,000/- tu kwa 0755848391 jina ni GODIUS RWEYONGEZA ili niweze kukutumia kitabu hiki. Usichelewe maana muda wa ofa ni mchache sana, na ofa hii haitajirudia tena.
-
Usipokata tamaa…
Mwisho wa siku usipokata tamaa, ukiendelea kuweka juhudi na kujituma bila kurudi nyuma, matokeo utayaona.
Kwa hiyo ujumbe wangu kwako siku ya leo Ni kuwa endelea kuweka juhudi zaidi kwenye Kazi. Yajayo yanafurahisha.
-
Vitu viwili ambavyo huwafanya watu washindwe kupiga hatuaRafiki yangu, bila shaka unaendelea vyema.
Rafiki yangu, bila shaka unaendelea vyema. Mimi hapa nilipo, niko sawa kabisa. Kuna vitu viwili kwenye maisha ambavyo huwafanya watu washindwe kufanikisha malengo na ndoto zao.
Lengo la mimi kukwambia vitu hivi ni kuwa wewe unapaswa kuvifahamu hivi vitu viwili na kuviepuka, la sivyo utaishi maisha ya kawaida Kama ambavyo watu wengine wanaishi.
Vitu hivyo viwili Ni
Moja KUTOKUWA NA MALENGO AU NDOTO KUBWA
Wengi wanaamka kila siku na kwenda kufanya kazi. Ila hawana malengo na ndoto Kubwa zinazowasukuma. Hiki Ni kitu kibaya, maana bila malengo na ndoto Kubwa ambazo zinakusukuma, utakosa motisha ya kufanya makubwa. Na hivyo, hutaweza kufika mbali kwenye maisha. Rafiki, yangu, Kama hauna malengo, Basi Leo hii, kaa chini na uweke malengo ambayo utaanza kuyafanyia kazi.Kwenye maisha yako, rafiki yangu, hakikisha Mara zote una malengo au ndoto kubwa unazozifanyia kazi. Malengo ni ramani ya kule unapotaka kuelekea. Kwenye maisha hakuna ambaye huwa anapanga kushindwa , Bali watu hushindwa kupanga. Nakuomba kitu kimoja tu rafiki yangu, usishindwe kupanga
Pili, ni KUTOKUWA TAYARI KULIPA GHARAMA
Siku hizi watu wengi wanapenda Ssna njia za mkato ili kupata mafanikio ya haraka . Rafiki yangu, njia ya mafanikio inakuhitaji ulipe gharama.
Na zipo gharama sita ambazo utapaswa kulipa kama ambavyo nimezianisha kwenye kitabu changu Cha jinsi ya kufikia ndoto zako.
Kitu kikubwa unachohitaji kujua ni gharama kiasi gani upo tayari kulipa ili kufikia mafanikio unayotaka. Kama hauko tayari kulipa gharama ujur hutaweza kufikia ndoto na malengo makubwa.Unaweza kupata Audiobook ya kitabu Cha Jinsi ya kufikia NDOTO ZAKO leo hii kwa kulipia 20,000/- tu. Nitakutumia Audiobook hii pamoja na Audiobook nyingine mbili bure kabisa
Audiobook nyingine mbili nitakazotumia bure Ni
1. NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA
3. Maisha Ni FURSA: ZITUMIE ZIKUBEBERafiki yangu, lipia Audiobook moja upate mbili bure
Vitu viwili ambavyo huwafanya watu washindwe kupiga hatua
Rafiki yangu, bila shaka unaendelea vyema. Mimi hapa nilipo, niko sawa kabisa. Kuna vitu viwili kwenye maisha ambavyo huwafanya watu washindwe kufanikisha malengo na ndoto zao.
Lengo la mimi kukwambia vitu hivi ni kuwa wewe unapaswa kuvifahamu hivi vitu viwili na kuviepuka, la sivyo utaishi maisha ya kawaida Kama ambavyo watu wengine wanaishi.
Vitu hivyo viwili Ni
Moja KUTOKUWA NA MALENGO AU NDOTO KUBWA
Wengi wanaamka kila siku na kwenda kufanya kazi. Ila hawana malengo na ndoto Kubwa zinazowasukuma. Hiki Ni kitu kibaya, maana bila malengo na ndoto Kubwa ambazo zinakusukuma, utakosa motisha ya kufanya makubwa. Na hivyo, hutaweza kufika mbali kwenye maisha. Rafiki, yangu, Kama hauna malengo, Basi Leo hii, kaa chini na uweke malengo ambayo utaanza kuyafanyia kazi.Kwenye maisha yako, rafiki yangu, hakikisha Mara zote una malengo au ndoto kubwa unazozifanyia kazi. Malengo ni ramani ya kule unapotaka kuelekea. Kwenye maisha hakuna ambaye huwa anapanga kushindwa , Bali watu hushindwa kupanga. Nakuomba kitu kimoja tu rafiki yangu, usishindwe kupanga
Pili, ni KUTOKUWA TAYARI KULIPA GHARAMA
Siku hizi watu wengi wanapenda Ssna njia za mkato ili kupata mafanikio ya haraka . Rafiki yangu, njia ya mafanikio inakuhitaji ulipe gharama.
Na zipo gharama sita ambazo utapaswa kulipa kama ambavyo nimezianisha kwenye kitabu changu Cha jinsi ya kufikia ndoto zako.
Kitu kikubwa unachohitaji kujua ni gharama kiasi gani upo tayari kulipa ili kufikia mafanikio unayotaka. Kama hauko tayari kulipa gharama ujur hutaweza kufikia ndoto na malengo makubwa.Unaweza kupata Audiobook ya kitabu Cha Jinsi ya kufikia NDOTO ZAKO leo hii kwa kulipia 20,000/- tu. Nitakutumia Audiobook hii pamoja na Audiobook nyingine mbili bure kabisa
Audiobook nyingine mbili nitakazotumia bure Ni- NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA
- Maisha Ni FURSA: ZITUMIE ZIKUBEBE
Rafiki yangu, lipia Audiobook moja upate mbili bure
-
Vitu viwili ambavyo hakuna MTU anapaswa kukuzidi
Rafiki yangu, SIKU ya leo ningependa kukwambia vitu viwili ambavyo hakuna MTU anapaswa kukuzidi kwenye kuvifanya. Vitu hivi ni
1. Kufanya kazi kwa bidii
Acha watu wakuzidi kwenye mambo mengine yote ila wasikuzidi kwenye kufanya kazi kwa bidii.Kufanya kazi kwa bidii kupo ndani ya uwezo wako. Kwa hiyo kuanzia leo, acha watu wakuzidi kwenye vitu vingine Ila siyo kwenye kufanya kazi kwa bidii.
2. Kujifunza kwa bidii
Hiki Ni Kitu kingine ambacho hakuna mtu yeyote anapaswa kukuzidi kwenye kufanya. Hakikisha mara zote unazama kwenye kujifunza na kuelewa vitu kwa kiasi ambacho hakuna mtu mwingine mwenye elimu na uelewa mkubwa kukuzidi wewe.Kila SIKU jifunze. Jifunze kwa kusoma vitabu, jifunze kwa kuhudhuria semina na maonesho, jifunze kwenye kozi na maeneo mengine.
Mara zote jifunze rafiki yangu. Hakuna mtu yeyote ambaye anapaswa kukuzidi kwenye kujifunza hata siku moja.
NB: Kwa kuanzia, hakikisha umepata audiobook zangu tatu ili uanze kuzisikiliza. Audiobook zenyewe ni
- JINSI YA KUIFIKIA NDOTO ZAKO
- NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA
- MAISHA NI FURSA: ZITUMIE ZIKUBEBE
Kila audiobook Ni 20,000/- Ila Leo nakupa ofa. Lipia audiobook moja nikupe audiobook nyingine mbili bure.
Badala ya 60,000/- utaipia elfu 20,000 tu, nami nitakupa audiobook zote tatu.lipia Sasa kwa 0755848391 jina ni GODIUS RWEYONGEZA. Baada ya hapo, nitakutumia audiobook zako.
Umekuwa nami rafiki yako,
Godius Rweyongeza
0755848391 -
FANYA MAZOEZI
Siku moja nilikuwa nasoma makala mtandaoni, kwenye makala hiyo mwandishi akawa amesema kwamba Michael Jackson ambaye ni gwiji kwenye muziki wa hiphop alikuwa ni mmoja watu waliokuwa wanafanya mazoezi kwa muda mrefu sana kabla ya kuonekana mbele ya watu. Kwa baadhi ya watu kitu hiki kilionekana cha ajabu sana, Ukilingananisha na kuwa Michael Jackson alikuwa akiimba na kucheza kwa namna ambayo ilikuwa inaonenekana ni njia ya asili. Inawezekanaje gwiji kama Michael Jackson awe anafanya mazoezi kwa muda mrefu hivyo?
Na hiki ni siri ambayo nimegundua vijana wengi hawaielewi. Wapo wanaodhani kuwa ukishakuwa na kipaji peke yake basi anaweza kulala na kila kitu kikajipanga.
Kama kuna kitu unapaswa kufahamu kwenye maisha yako ni kujua kwamba mazoezi ni jambo moja muhimu sana ambalo utapaswa kulifanyia kazi kwenye maisha yako. Tena utahitaji kuhakikisha kuwa unafanya mazoezi ya mara kwa mara kwenye kitu ambacho unafanya, kiasi cha kuweza kufikia ubobezi kwenye hicho kitu.
Kila eneo lina vitu vyake vya kufanyia mazoezi. Kwa mwanasheria kuna vitu vyake ambavyo anapaswa kufanyia kazi maeozi.
Mazoezi yanakujenga, mazoezi yanakuimarisha na njia ya wewe kupanda kutoka hapo ulipo kwenda unapotaka kwenda ni kufanya mazoezi.
Tujifunze kwa wachezaji wa mpira wa miguu
Wachezaji wa mpira wa miguu ni miongoni mwa watu ambao wanafanya mazoezi bila kuchoka. Kipindi ambacho ligi inakuwa imepumzishwa wenyewe wanaenda mpaka kambini. Na kambi hii inakuwa ni maalumu kwa ajili ya kufanya mazoezi ili waweze kufanya vizuri kwenye mashidano yanayofuata. Na siyo hilo tu, hata baada ya kuwa wamaenda kwenye mashidano huwa hawaachi kuanya mazoezi. Hiki kitu ndicho na wewe unapaswa kuwa nacho pia kwenye kazi na vile unavyofanya. Jijengee utaratibu wa kufanya mazoezi kwenye kazi au kitu unachofanya. Hakikisha kwamba unafanya mazoezi bila ya kuchoka.
Mazoezi yanakuimarisha. Kadiri unavyokuwa unazidi kufanya mazoezi ndivyo unazidi kuimarika na kubobea zaidi.
Mazoezi yanakuondolea hofur woga na wasiwasi. KILA MARA ukifanya mazoezi unairmarika na kukielewa kitu husika.
Ebu fikiria unataka kuwa muongeaji mzuri mbele ya watu. (by the way, kuongea mbele ya watu ni kitu ambacho kinawashinda watu wengi sana na ni kituambacho unahitaji ukifahamu kwa uzuri sana).
Sasa kitu hiki unaweza kukifanyia mazoezi kwa kuhakikisha kwamba kila siku unatenga nusu saa tu ya kufanya hivi. Kwenye hii nusu saa unaamua kuwa unaongea mbele ya watu na kuwasilisha mada yako ambayo umeandaa. Au hata kama hakuna mtu ambaye yuko mbele yako.
-
Hii ndiyo sababu kuu kwa nini unapaswa kutoa thamani kubwa kuliko mteja anavyokulipa

Ni miaka kama mitano hivi imepita tangu nimegundua kanuni moja muhimu sana ambayo nimekuwa naitumia kwenye kila kitu ninachofanya. Na kanuni hii siyo nyingine bali ni kutoa thamani kubwa zaidi kwa mteja kuliko mteja anavyolipia.
Tangu nimegundua kanuni hii nimekuwa naitumia kwenye vitabu vyangu vyangu vyote. Ambacho nimekuwa nafanya ni kuwa, kwa kitabu ambacho mteja analipia elfu ishirini, nahakikisha kwamba kinakuwa na thamani ya laki mbli na zaidi. hivyo, namwuzia mteja kitabu chenye thamani ya laki mbili na zaidi kwa elfu ishirini tu.
Nafanya hivi siyo kwamba ninakuwa sijui, bali kwa sababu nataka mtu yeyote yule anayenunua kitabu au kupata huduma yoyote kwangu, apate thamani mara kumi zaidi na vile ambavyo analipia.
Hii ni kanuni muhimu sana ambayo na wewe unapaswa kuizingatia na kuanza kuitumia kuanzia leo hii kwenye biashara yako. Hakikisha kwamba bidhaa au huduma unayoitoa kwa mteja inakuwa na na thamani mara kumi zaidi ya vile ambavyo anavyolipia.
Tumia hii kanuni hata kwenye kazi. hakikisha kwamba unafanya kazi kwa viwango vikubwa mara kumi zaidi kuliko watu wengine wanavyofanya. Jitume mara kumi zaidi ya wengine. Soma vitabu mara kumi zaidi yaw engine. Jibrand mara kumi zaidi ya wengine. Hiki kitu kitakusaidia wewe kuweza kujenga jina lako na hata kujitofautisha.
Unapaswa kufanya hivi, kwa sababu katika ulimwengu wa leo ni watu wachache sana ambao wanafanya hivi. Wengi wanapenda njia za mkato za kupata mafanikio ila hawapendi kuweka kazi. kufanya kazi zaidi ya vile wanavyolipwa kujituma na kuwapa wateja thamani.
Ukiweza kufanya hivi, maana yake utawateka wateja wako na kuwafanya waendelee kupata huduma kwako na hivyo kujenga jina katika namna ya kipekee ambayo hakuna mtu mwingine anaweza kujenga jina kama wewe.
Kazi yako ya kufanya kuanzia leo hii ni kuanza kutoa thamani mara kumi zaidi ya vile unavyolipwa. Jiulize ni bidhaa ipi haitoi thamani mara kumi zaidi ya vile ninavyolipwa? Kama kuna bidhaa ya aina hiyo, basi anza kuiboresha ili iweze kutoa thamani kubwa zaidi kwa mteja kuliko vile anavyokulipa.
-
Hii ni tabia muhimu unayopaswa kuanza kuishi nayo kuanzia leo hii. (usishike simu kama kitu cha kwanza unapoamka asubuhi, na wala usishike simu kama kitu cha mwisho kabla ya kwenda kulala).
Siku zinazidi kusogea kwelikweli. Mwaka uliokuwa mpya sasa hivi, tumeshaanza kuuaga taratibu. Siku siyo nyingi utaingia mtaani na kuanza kuzisikia nyimbo za krismasi zikipigwa. Ukiona hivyo, ujue kwamba mwaka unazidi kusogea na na siku siyo nyingi tutakuwa tunauaga. Lakini kabla mwaka huu haujaisha, kuna tabia ambayo ningependa uanze kuifanyia na kuachana nayo
TABIA YA KUTOSHIKA SIMU YAKO KAMA KITU CHA KWANZA UNAPOAMKA ASUBUHI
Kuna siku kulikuwa na kichekesho fulani hivi, kuwa mtu anaamka asubuhi kabla hata hajajua kama kichwa chake kimeshikana kiwiliwili chake anakuwa tayari ameshashika simu yake. Japo ni kichekesho ila kina ukweli mkubwa sana ndani yake. Asilimia kubwa ya watu, asubuhi kabla hata hajatoka kitandani, anakuwa tayari ameshika simu yake.
Na ukifuatilia ni kitu gani cha msingi ambacho huyu mtu anakuwa anafanya na simu yake, huwezi kukiona, zaidi zaidi utakuta kwamba anajibu SMS hata zisizokuwa na maana. Au anaingia kwenye mitandao ya kijamii kuangalia watu wamekoment nini kwenye kitu alichopost jana yake. Sasa rafiki yangu, kuna kitu kimoja ambacho ningependa uweze kufahamu. Na kitu hiki syo kingine bali ni wewe kuepukana na kushika simu kama kitu cha kwanza unapoamka asubuhi.
Ukiamka asubuhi, anza kwa kushukuru kwa kuiona siku nyingine mpya. Baada ya hapo anza kutahajudi.
Kisha jiambie kauli chanya, kauli kama
- Mimi ni bilionea.
- Mimi ni sumaku ya fedha na fedha zinanifuata
- Mimi ni mshindi na nimezaliwa kushinda.
- Mimi nastahili kupata vitu vizuri na vizuri vimetengeezwa kw ajili yangu. Na nyinginezo nyingi.
Katika huu muda hakikisha kwamba unapata maji ya uvuguvugu, kisha toka nje uvute pumzi kwa nguvu na ikiwezekana kukanyaga chini kwenye udongo il kuungana na asili na kufanya mazoezi. Baada ya hapo soma walau kwa dakika 20 tu.
Itapendeza sana kama saa moja la kwanza baada ya wewe kuamka kama hutashika simu kabisa.
Hii ndio kusema kwmaba ndani ya saa lako moja hili utakuwa umeweza kufanya makubwa, ikiwa ni pamoja na kupangilia asubuhi yako kwa kuweka to do list. Ukitoka hapo sasa unaweza kuendelea na mambo mengine.
Hivyo hivyo wakati wa kulala. Usishike simu kama kitu cha mwisho kabisa kabla ya kulala. Tafiti nyingi zinaonesha kuwa unapaswa kushika simu walau saa mbili kabla ya kulala. Hii ni kwa sababu simu, ina mwanga ambao unaingiliana na usingizi. Hivyo, unaweza kujikuta kwamba unakosa usingizi muda mwingine, kumbe kinachokukosesha usingizi siyo kingine bali ni simu yako.
Rafiki yangu, najua wazi kuwa simu ina manufaa mengi ila ninachokuomba ni kitu kimoja tu. Usishike simu kama kitu cha kwanza unapoamka asubuhi, na wala usishike simu kama kitu cha mwisho kabla ya kwenda kulala. Kila la kheri.
-
Je, kuuza vitu vya bei rahisi ni njia kutengeneza fedha nyingi kwa sababu bidhaa zinatoka kwa haraka?
Mara kwa mara nimekuwa naandika kwenye blogu yangu na kutolea mfano namna ambavyo Bakhresa na Mo Dewji wanauza bidhaa za bei ya chini. mfano watu hawa unakuta wanauza mpaka viberiti, chumvi, pipi na vinginevyo ambavyo vinauzwa shilingi 50, 100, 200 mpaka 500.
Nimekuwa nikitumia mfano huu kuhamasisha vijana mbalimbali kwamba wasidharau fedha kwenye maisha, badala yake kama mtu haoni sehemu yoyote ile ya kuanzia kwenye maisha kabisa, basi unaweza kuanza hata kwa kuuza kitu chochote kile cha bei ya chini kwa watu.
Lengo likiwa ni kwamba kijana aanze kujishughulisha na hata kuingiza kipato. Nimekuwa nasema hivi kwa sababu, kwa mtu anayeanza, ni rashisi sana kwenda kwa watu kuuza bidhaa ya bei rahisi kuliko kwenda kwa watu kuuza bidhaa ya bei kubwa.
Mtu anaponunua bidhaa ya bei ya chini labda (elfu moja), hajiulizi mara mbilimbili kama anapaswa kutoa fedha yake mfukoni au anapaswa kuendelea na maisha mengine. Tofauti na mtu anayenunua bidhaa ya laki moja. huyu kidogo ataanza kujiuliza na utahitaji kutumia nguvu kumshawishi.
Sasa nadhani kutokana na msisitizo wangu huu wa kusisitiza vijana kuanza hata kuuza bidhaa za bei ya chini, umemfanya rafiki yangu kuuliza swali kama linavyoonekana hapa chini,
Anasema je, kuuza bidhaa za bei rahisi ni njia rahisi ya kuvutia wateja na unaweza kutengeneza pesa nyingi pia kwa sababu huenda bidhaa zinatoka kwa haraka??
Jibu ni hapana.
Kuna njia kadha wa kadha za kutengeneza fedha na kuufikia utajiri kwa hiyo sidhani kama hii ni njia RAHISI.
Unapokuwa unauza bidhaa za bei ndogo maana yake unavutia wateja wengi na matatizo yako yatakuwa mengi pia. Iko hivi, ukiuza bidhaa ya shilingi mia moja, utatakiwa kuuza kwa watu 100 ili ufikishe elfu kumi. Wakati huohuo mtu anayeuza bidhaa ye elfu tano, atatakiwa kuuza kwa watu wawili tu ili afikishe hiyo elfu kumi. Na kama unavyojua kushughulikana watu hakuwezi kukosa changamoto. Kwa hiyo, changamoto anazokuwa nazo mtu ambaye anauza bidhaa kwa watu mia moja ni tofauti kabisa na changamoto anazokuwa nazo mtu anayeuza bidhaa kwa watu wawili.
Kuuza bidhaa za baei rahisi ni njia ya kuanza nayo kwa ajli ya kukuweka kwenye mwendo, lakini siyo kwamba ndiyo mwanzo na mwisho. Hata Bakhresa mwenyewe siyo kwamba anauza pipi ya 100 kama pipi ya 100. Badala yake hizo pipi zake anaziuza kwa jumla kwa watu wanaoenda kuuza kwa rejareja huko mtaani. Hivyo, yeye hashughuliki moja kwa moja na wale wateja wengi wanaonunua pipi ya 100. Bali wateja wachache wananunua mzigo wa bei kubwa.
Kwa uzoefu wangu, wateja wanaoununua vitu vya bei rahisi huwa ni wasumbufu sana ukilinganisha na wateja wanaonunua vitu kwa bei kubwa.