Home


  • Namba Zetu Za Malipo

    Namba za malipo ya vitabu:

    Namba za lipa

    TIGO PESA: 19016638 Jina ni SONGAMBELE CONSULTANTS

    M-PESA: 5564517 jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

    Namba za kawaida

    AIRTEL MONEY: 0684408755
    TIGO PESA: 0655 848 392
    M-PESA: 0745 848 395

    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    NB: Kama namba ya malipo anatumiwa mtu ambaye yuko nje ya nchi. Iandikwe Kwa kuanza na +255

    Kwa hiyo namba zinazotumwa nje ya nchi zitakuwa
    Airtel money: +255 684 408 755
    TIGO PESA: +255 655 848 392
    M-PESA: +255 745 848 395

    KOTE Jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Kama malipo yatakuwa yanafanyika kupitia benki.

    Yafanyie kupitia

    1. CRDB BANK: 0150770710200
    2. NMB BANK: 22110047274

    Kote jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

  • Wasiliana na Godius Rweyongeza Sasa

    Habari yafuatayo ni mawasiliano Unayoweza kutumia kumpata GODIUS RWEYONGEZA

    Simu: +255 (0) 684408755

    Whatsap: +255 (0) 755848391

    Email: songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu vyake wasiliana Moja kwa Moja na +255 (0) 684408755 (more…)

  • usipofanyia kazi ndoto zako kuna mtu atakuajiri ili ufanyie kazi ndoto zake

    Rafiki yangu, watoto wadogo huwa wanaongoza kwa kuwa na ndoto kubwa sana. Ukiongea na mtoto yeyote yule mdogo atakwambia ndoto zake kubwa, tena kwa kujiamini.

    Ongea na MTU mzima sasa. UNAWEZA kutamani kuzaba baadhi ya watu vibao. Watu walewale ambao walikuwa na ndoto kubwa utotoni, kwa sasa hawana tena hizo ndoto kubwa.

    Ndoto ileile waliyokuwa nayo utotoni ukiwakumbushia wataanza kukupa sababu kibao kuonesha kwa Nini HAIWEZEKANI kufanyika.
    Watakwambia uchumi mgumu.
    Watakwambia vyuma vimekaza.
    Watakulerea sababu nyingine kibao.

    Rafiki yangu, wewe ni mmoja wa hao watu?

    Ndoto Yako. Naam ndoto Yako Ni kitu muhimu ambacho haupaswi kupoteza. Na ukiona umepoteza ndoto zako, ujue tu lazima Kuna MTU anaenda kukuajiri ili ufanyie kazi ndoto zake.

    Unajua kwa nini?

    Kwa sababu dunia haipendi kukaa na utupu. Popote pale kunapokuwa na utupu dunia inatafuta sababu ya kuhakikisha pamejaa.

    Kama sehemu Haina mazao Basi itakuwa na magugu.
    Kama sehemu ubongo hauna mawazo chanya, basi utakuwa na mawazo hasi.

    Kumbe na wewe usipofanyia kazi ndoto zako, lazima tu kutakuwa na mtu ambaye atakuajiri ili ufanyie kazi ndoto zake. Kama MTU hatakuajiri ufanyie kazi ndoto zake. Basi visingizio vitakumeza, kwenye kufanyia kazi ndoto zake.

    Sasa rafiki yangu, kuanzia leo amua kitu kimoja tu. Kufanyia kazi ndoto kwa kufa na kupona. Pambania ndoto zako rafiki yangu hata kwa kuanzia chini Sasa hivi.

    Kila la kheri

    Sasa kitu kikubwa cha kufanya leo ni wewe kuhakikisha kwamba unaanza kufanyia kazi.

  • Hivi ndivyo unapaswa kugawanya muda wako Kama una ndoto kubwa

    Rafiki yangu mpambanaji, bila shaka unaendelea vizuri kabisa. Hongera sana kwa hilo. Siku ya leo ningependa kuongea na wewe machache  rafiki yangu mwenye ndoto kubwa.

    Ukweli ni kuwa inachukua muda kufikia mafanikio makubwa: unapaswa kuyapambania mafanikio Yako makubwa Kama vile hakuna Kesho. Muda wako wewe mpambanaji unapaswa kuwa umegawanywa sehemu za muhimu tu.

    Muda wa kufanyia kazi ndoto zako. Hapa unafanya kila linalowezekana kuhakikisha umezipambania ndoto na malengo Yako kila wakati. Unafanya kazi kwa bidii na haurudi nyuma
    Inachukua Muda kufikia ndoto kubwa Ila inawezekana.

    PILI ni muda wa familia au watu wako wa KARIBU. Huu Ni muda mwingine ambao unapaswa kuwa KARIBU na familia yako au watu wako wa KARIBU.

    Ni hivyo tu. Vingine vilivyo nje ya hapo havipaswi kupata muda wako.
    Weka muda wako, NGUVU zako na Akili zako kwenye hivyo vitu viwili tu.

    Nina vitabu viwili vinavyokufaa sana wewe mpambanaji. Kwanza ni JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO

    Na pili Ni kitabu Cha mwongozo wa wapambanaji. Hustlers Guide. Hivi vitabu viwili hivi, vina mwongozo na kila kitu unachohitaji kujua kuhusu kufanyia kazi malengo na ndoto zako mpaka vikatimia. Cha kufanya hapa Ni kitu kimoja tu. Wasiliana nami kwa 0755848391 ili uweze kupata Nakala zako mapema.

    vitabu vyote viwili Ni 30,000/- kimoja ni hardcocopy (JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO) NA gharama yake Ni 20,000/-

    na mwongozo wa wapambanaji ni softcopy. Gharama yake ni 10,000/-. Vipate vyote, utanishukuru baadaye.

    Nakutakia kila la kheri.

  • Ufanyeje pale bidii yako inapotumika kama mtaji kwa watu wengine

    Siku moja kuna rafiki yangu aliniuliza swali, alitaka kujua kuwa unafanyaje pale ambapo unakuwa na bidii na watu wanajua kuwa una bidii ila wanataka wakutumie.

    Leo ningependa kujibu swali hili kwako wewe ambaye unaona kwamba una bidii na watu wanaitumia hovyo. Kwanza ningependa kwa kuanza kusema kwamba unapaswa kuwa na bidii kwenye kazi zako. hakikisha kazi yako yoyote ile unayogusa unaifanya kwa bidii, na siyo tu unaifanya kw abidii, bali unaifanya kwa ubora wa hali ya juu sana.

    Kama wewe unaona kwamba lazima bosi wako awepo ili ufanye kazi. HUFAI.

    Kama unaona kwamba bosi wako akitoka unapumua kwa nguvu kwa vile ametoke. Jua kwamba hufai.

    Kama muda wa kazi unachati, unaongea umbea na unajificha kwenye migongo ya watu wngine. Hufai pia.

    Rafiki yangu, wewe unapaswa kuwa mchapakazi wa hali ya juu sana. chapa kazi mara zote na sehemu zote, chapa kazi kwelikweli kiasi kwamba asipo mtu ambaye anapaswa kukuzidi kwenye kuchapa kazi.

    Na kwenye hii dunia kuna vitu viwili ambavyo haupaswi kuruhusu mtu yeyote akuzidi kwenye kuvifanya, vitu hivi ni kufanya kazi kwa bidii na kujituma.

    Kama kuna watu wanakuzidi kwenye hivyo vitu viwili. Basi funguka sasa hivi.

    SASA baada ya kuwa nimesema hayo yote kuhusiana na kuchapa kazi kwa bidii. Inawezekana kuna watu watataka kukutumia wewe kwa manufaa yao zaidi kwa vile wanaona unachapa kazi kw abidii.

    Na kama unasema watu wanakutumia, kwa lugha nyingine unamaanisha kwamba unafanya kazi kwa viwango vikubwa ukilinganisha na malipo ambayo unapata. Hivyo, unalipwa kiasi kidogo ukilinganisha na vile anavyopaswa kuwa analipwa.

    Laiti ungekuwa unalipwa vizuri usingesema hivyo.

    Kwa hiyo, kama unaona kwamba haulipwi kama vile unavyostahili unaweza kufanya yafuatayo.

    Kwanza, unaweza kuamua kuacha kazi ili uweze kuweka juhudi zako sehemu nyingine ambayo itakulipa kulingana na kazi yako. Huu ni ukweli ambao pengine hukuutegemea lakini unapaswa kuubeba na kuufanyia kazi bila yakuchelewa.

    Pili, kama unaona hiyo ni ngumu, basi unapaswa kuonana na bosi wako na kumwambia kuwa anapaswa kukuongeza malipo ili yaendane na viwango vya kazi unayoweka. Hapa nenda na vielelezo vyote ambavyo utahitaji kuonesha kwa bosi wako ili kuthibitisha hilo

    Na tatu na mwisho, ni kwenda kwa bosi mwingine ambaye anaweza kukulipa kiwango unachoona unastahili.

    Hayo ndiyo mambo matatu ambayo utahitaji kufanyia kazi rafiki yangu,ili kuhakikisha kwamba u

    KITU Kikubwa zaidi ni kwamba haupaswi kuja kuzama kwenye kukazania kulipwa na bosi wako na wakati huohuo thamani na ufanisi wako ukapungua. Muda wote huo, ufanisi wako unapaswa kuwa unaongezeka.

    Na hata wachezaji wa mpira huwa wanapandishwa viwango vya malipo kutokana na vile wanavyokuwa wanazidi kuwa bora zaidi kwenye kazi zao. Hivyo, kwa msingi huo basi, unapaswa kuongeza uchapaji wa kazi, ufanisi na ubora wa kazi bila kuacha ili kuendelea kupanda viwango

    Kila la kheri

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.

    Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.

    Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.

  • Karibu Kwenye Semina Ya Kufanya Makubwa Mwaka 2023: Fanikisha Ndani Ya Miezi Sita Kile Ambacho Wengine Huwa Wanafanya Kwa Mwaka Mzima

    Rafiki Yangu mpendwa, bila shaka unaendelea vizuri kabisa. Moja ya jambo la msingi kabisa ambalo unahitaji kuhakikisha kwamba umelifanya kwenye maisha yako ni kujenga utaratibu wakujifunza. Kujifunza kunaweza kuwa kupitia kusoma vitabu, kusikiliza mafunzo ya sauti au mafunzo ya vitendo pamoja na semina.

    Kwa kulitambua hili, mwaka huu tutakuwa na semina ya ana kwa ana ambayo itafanyika tarehe 24 juni. Itakuwa ni siku ya jumamosi na itafanyika hapa mkoani Morogoro.

    Lakini kabla sijajuelez zaidi kuhusu semina, ebu kwanza tuongee kuhusu uhitaji wa wewe kufanya makubwa.

    Eb u pata picha malengo uliyoyaweka ndani ya mwaka huu 2023, je, kuna hatua ambazo unaona unapiga? Je, unaona kwamba unaweza kuwa unapiga hatua zaidi lakini haujui ni kwa namna gani ambavyo unaweza kupiga hizo hatua zaidi?

    Je, unajiuliza ni vitu gani ambavyo vinahitajika kwako ili kuhakikisha kwamba unapiga hatua na kuweza kufanya makubwa, naam, makubwa sana.

    Nalijua hilo nap engine hilo siyo kwamba linakusumbua wewe peke yako, ni jambo ambalo linawasumbua wengi. mtu anakuwa na malengo, anaweka malengona anaanza kuyafanyia kazi, ila sasa mwisho wa siku mtu huyo anashindwa kuyafanyia kazi malengo yake mpaka kufikia mwisho. Ukifuatilia kwa undani unaweza kugunda kuwa kuna vitu viwili ambavyo vinamzuia mtu.

    Msukumo wa ndani wa kufanikisha kile alichopanga au

    Kukosa mbinu sahihi za kumwezesha kufanikisha malengo yake.

    Kwa kulitambua hilo, nimekuandalia semina ambayo inaenda kuchoche moto wa wa wee kufanya makubwa na kuweza kufanikisha malengo yako ndani ya mwaka 2023.

    Semina hii inaitwa SEMINA YA KUFANYA MAKUBWA, siyo kwa bahati mbaya, bali kwa sababu kuna maana yake.

    Kwenye hii semina tunaenda kujifunza namna ambavyo unaweza kufanikisha makubwa ndani ya miezi sita, wakati wengine huwa wanafanyia kazi hayo kwa miaka mmoja mpaka miaka miwili. Unaweza kujiuliza hili linawezekanaje. Kiufupi ni kwamba linawezekana maana tumekuwa tukililifanyia kazi kwa muda sasa, kinachofuata ni kuhamishia kile ambacho tumekuwa tukikifanyia kazi kwako ili na wewe uweze kukifanyia kazi kwa muda mfupi kuliko ambavyo umekuwa ukitegemea.

    Sambamba na hilo kwenye hii semina tunaenda kujifunza mambo mengine mazuri ambayo yatabadili maisha yako na mwelekeo wa maisha yako kiujumla.

    Tunaenda kujifunza juu ya safari ya kuelekea uhuru wa kifedha, kwenye hii semina tutaona namna ya kuianza safari hii hatua kwa hatua, tutaona namna ya kuendedelea na hii safari na hatimaye kuhakikisha kwamba hii safari inakamilika.

    Lakini siyo kwamba tutaishia hapo, tutaona namna ya kuamsha uwezo ulioala ndani yako na kuutumia kwa viwango vya juu ili uweze kufanikisha hayo yoooe ambayo tumekuambia.

    Kuna watu ambao huwa wanaogopa kwamba hivi vitu, vinaweza visifanye kazi. tutaona namna ya kuondoa hofu ya kufanyia kazi malengo na ndoto zako na namna ambavyo unaweza kuwa na maisha unayotaka baada ya kuwa umeondoa hiyo hofu.

    Hatutaishia hapo tu kwa wale walio kwenye mahusiano, tutaona namna ambavyo mnaweza kufanikiwa kifedha mkiwa kama wenza.

    Kiufupi hii semina itakuwa imejaa mengi kwa ajili yako. Na itakuwa ni semina ya siku nzima. Semina hii itaanza saa moja asubuhi na itamalizika jioni saa 12.

    Tutakuwa na siku moja nzima ambapo tutjitenge na uliwewengu na kukaa kwenye mazingira ambayo tutajifunza namna ya kupindua mambo mengi kwenye maisha yetu.

    Baada ya hii semina, kitakachofuata ni kuchukua hatua na kufanyia kazi yale tutakayokuwa tumejifunza.

    Hivyo, sasa naomba rasmi nichukue nafasi kukukaribisha kwenye semina hii ya kipekee.

    SEMINA HII ITAFANYIKA hapa morogoro,. Itafanyika siku ya jumamosi, na itakuwa ni semina ya siku nzima kuanzia saa moja asubuhi mpaka jioni. Chakula na bites vyote utapata kwenye hii semina.

    Gharama ya semina hii itakuwa ni shilingi 50,000/-

    Na mwisho wa kufanya malipo kwa ajili ya semina ni tarehe 15.6.2024

    Karibu sana kwenye semina ya kufanya makubwa mwaka 2023. Mwaka 2023 haturembi mwandiko!

    Kwa kumalizia ningependa kukumbusha mambo machache tu.

    • Semina itafanyika tarehe 24, Juni, 2023.
    • Itakuwa ni siku ya jumamosi
    • Itafanyika kuanzia saa moja asubuhi mpaka jioni saa 12
    • Gharama ya semina ni 50,000/-
    • Chakula na bites vitakuwepo.

    Cha kufanya ni wewe kuthibitisha malipo yako sasa hivi. zifuatazo ni namba ambazo zitatumika kufanya malipo ya semina.

    *NMB: 22110047274 JINA NI GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA*

    *Mpesa: 0755848391*

    *Airtel money: 0684408755

    *JINA NI GODIUS RWEYONGEZA*

    Kitu cha kufanya leo.

    Siku ya leo fanya kitu kimoja tu rafiki yangu.

    Tuma ujumbe wa kuthibitisha ushiriki wako kwenye semina. Tuma ujumbe huu kwenda whatsap

    0755848391  au bonyeza hapa

    Kisha niambie, utalipia kwa mpango gani.

    Utalipa kiasi chote kwa pamoja au takuwa unalipa kila wiki, au kila mwezi na kiasi gani utakuwa utakuwa unalipia?

    Tuma ujumbe wako hapa

    Mfano:

    *Mimi GODIUS RWEYONGEZA nathibitisha kushiriki semina ya mwezi wa sita*

    *Nitalipia kiasi chote kwa pamoja tarehe 15 MACHI, 2023.*

    *JIUNGE NA KUNDI LA WALIOTHIBITISHA KUHUDHURIA*

    https://chat.whatsapp.com/Je9AhwPiuwbGX3HeWTPGwG

    Karibu sana

  • Jinsi Ya Kujenga Mafanikio Makubwa Hata Kama Hauna Kitu

    Hapo zamani za kale, ili kujenga utajiri ulipaswa kuwa na ardhi kubwa, ng’ombe na vitu vingine vinavyoendana na hivyo. Ulipokuwa na vitu vya aina hiyo, hapo sasa ndipo watu walikuwa wanasema kwamba mtu fulani ni tajiri. Ila leo hii mambo yamebadilika.

    Baadaye ilikuwa inaaminika kwamba ili kujenga utajiri unapaswa kuwa walau na konekisheni na ndugu au mtu ambaye ni tajiri au ambaye anafanya kazi kwenye taasisi kubwa. ila leo hii mambo hayo yote yamebadilika, huhitaji kuwa na konekisheni wala ndugu yako ambaye anafanya kazi serikalini, huhitaji kuwa fisadi, huhitaji kuwa mashamba mengi wala ng’ombe elfu. Unahitaji kutumia kile ulinacho. Na kwa sababu hiyo, siku ya leo ninaenda kuandika makala ya kina inayoeleza namna ambavyo unaweza kufanikiwa kwa viwango vikubwa hata kama hauna kitu.

    Hatua ya kwanza ya kujenga mafanikio makubwa hata kama hauna kitu ni

    1. KUJUA KITU UNACHOPENDA NA KUANZISHA BIASHARA KWENYE KILE UNACHOPENDA

    Rafiki yangu, najua kuna vitu kadha wa kadha unapenda hivi kwako vinapaswa kuwa sehemu ya kuanzia. Haitoshi tu wewe kila siku kwenye kuangalia mechi kila siku, huku ukishangilia kwamba Mayele kafunga au hajafunga. Baala yake unapaswa kuangalia fursa iliyojicicha kwenye hicho kitu mbacho unapenda na namna ambavyo unaweza kuitumia hiyo fursa kufanya makubwa.

    Ukishajua kitu ambacho unapenda, basi acha kufanya mambo mengine yoyote yale, badala yake wekeza nguvu na muda wako kwenye hicho kitu unapenda.

    Jenga biashara kwenye hicho kitu. Jenga hata biashara ya kuanzia chini.

    2. ANGALIA RASILIMALI ZILIZO KWENYE MAZINGIRA YAKO UNAZOWEZA KUANZA KUTUMIA SIKU YA LEO

    Kuna rasilimali ambazo naamini unazo ambazo unaweza kuanza kutumia.unaweza ukawa unafikiria kufanya makubwa sana ambayo pengine hayajawahi kufanyika kwenye hii dunia, lakini unachopaswa kufahamu ni kwamba, hayo makubwa unaweza kuanza nayo kidogo kidogo na kwenda nayo hatua kwa hatua mpaka ukaweza kuyafanya kuwa makubwa zaidi.

    Kuna rasilimali nyingi zimekuzunguka ambazo unahitaji kuhakikisha kwamba umezitumia. Nguvu zako, muda wako, mazingira  yaliyokuzunguka na mengine mengi. Tumia hizi rasilimali kuhakikisha kwamba unafanya makubwa. Naam, makubwa sana.

    3. TOA THAMANI KUBWA TENA BURE

    Najua u ataka kulipwa tena kwa viwango vya juu. IlA NJIA NZURI YA wewe kuweza kulipwa ni kuanza na kile ulichonacho, ukiweza kufanyia kazi vizuri kile ulichonacho, utaweza kufanya makubwa sana. tumia kile ulichonacho kwanza.

    4. JIPE MUDA

    Kila kitu hakitaweza kufanyika ndani ya siku moja. unahitaji kujipa muda ili kuweza kujenga mafanikio ambayo unataka. Mafanikio makubwa hayajengwi ndani ya siku moja au wiki moja. badala yake ni kwamba yanachukua muda.

    5. JIJUE MWENYEWE

    Jijue mwenyewe ni vitu gani unaweza zaidi kuliko vingine. badala ya kupambana kufanya kila kitu, wekeza nguvu na muda wako kwenye vitu vichache ambavyo unaweza kuliko kufanya kila kitu  bila mpangilio.

    6. PAMBANA KWA BIDII

    Rafiki yangu, malengo yako na ndoto zako unapaswa kuzipambania kwelikweli bila ya kurudi nyuma. Na hili hakikisha kwamba unalifanyia kazi bila ya kurudi nyuma. Kiufupi. Hakikisha kwamba kila unapoamka mpaka unapoenda kulala, unakuwa umepambana na kupambana zaidi. ukiona imepita siku bila ya kufanya kitu chochote kwenye ndoto yako. Basi ujue hiyo siku umeipoteza.

    7. TUNZA MUDA WAKO VIZURI

    Muda ndiyo rasilimali pekee ambayo inaweza unayo bure na ambayo ukiipoteza unakuwa umeipoteza. Kwa hiyo basi, mara zote pambana kuhakikisha kwamba unautumia muda wako kwa uzuri na kwa weredi mkubwa kuhakikisha kwamba muda wako unakuwa wenye manufaa.

    Watu wanaofanikiwa sana na wale ambao hawafanikiwi sana wana muda uleule. Tofauti kati ya wale wanaofanikiwa sana na wale ambao wanakuwa na mafanikio ya kawaida ipo kwenye matumizi ya muda. Hivyo basi, ili uweze kufanya makubwa unapaswa kuhakikisha kwamba unautumia vizuri muda wako. Anza na dakika yako moja ya sasa, kisha pangilia saa lako moja la baadaye na kisha siku yako nzima. Muda wako ni rasilimali muhimu sana ambayo unapaswa kuitumia vizuri sana.

    8. PENDA MCHAKATO

    Mchakato ni muhimu zaidi kuliko lengo. Watu wengi huwa wanaweka malengo mwanzoni mwa mwaka, ila malengo ni kitu kimoja. Kufanyia kazi yale malenngo ndio jambo lenyewe haswa. Na hili ndilo ambalo ningependa ulifahamu siku ya leo

    9.ACHA KUJALI SANA KILE AMBACHO WENGINE WANAFIKIRIA

    Najua kuna mengi sana ambayo watu wengine wanafikiria. Acha kujali sana mambo ambayo watu wengine wanafikiria. Badala yake wekeza muda wako na nguvu zako kwenye kile unachofanya tu.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.

    Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.

    Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.

  • Kitu muhimu ambacho kila mtu anapswa kukifhamu

    Rafiki yangu, najua kuna vitu vingi ambavyo unahitaji kufahamu. Ila siyo kila kitu unachokifahamu kina manufaa chanya kwako. kwa mfano unaweza kufahamu kuwa kuna ajali fulani sehemu fulani, ila siyo kwamba hiyo ajali ina manufaa yoyote kwako. au kwa wewe kufahamu kuwa kuna vita sehemu fulani, hilo kwa kupande wako siyo kwamba linakuwa na matokeo chanya ambayo unaweza kuyatumia.

    Ila kwa upande mwingine kuna vitu ambavyo ni muhimu kwako kuvifahamu na baada ya kuvifahamu unapaswa kuhakikisha kwamba umetumia maarifa na kila kitu ulichokipata kwa manufaa zaidi. moja ya kitu ambacho wewe unahitaji kuhakikisha kwamba umekifahamu kwa undani zaidi ni THAMANI YAKO.

    kITABU CHA JINSI YA K UONGEZA THAMANI YAKO
    Karibu upate kitabu hiki cha kipekee sana. Gharama yake ni 30,000 tu

    Thamani ni kitu cha muhimu sana ambacho unahitaji kuhaikisha kwamba umekifanyia kazi, tena unahitaji kuhakikish kwamba unakifanyia kazi sasa hivi rafiki yangu

    Ukijua thamani yako, utaokoa mengi sana rafiki yangu.

    Thamani yako inakusaidia wewe kupangilia muda na kazi zako ambazo unafanya. hii ndiyo kusema kwamba badala ya kufanya vitu hovyohovyo, unakuwa unafanya vitu kwa ustaarabu na kwa utaratibu mzuri ambao umeupangilia. Kitu ambacho hujakipangilia hukifanyi.

    Pili kujua thamani yako kunakusaidia kujua vitu vya kukubali kwenye maisha yako na vitu ambavyo unapaswa kukataa. Siyo kila kitu unaweza kukifanya, kuna baadhi ya vitu unaweza kuvikubali na kuamua kuvifanya kwenye maisha yako, ila kuna baadhi ya vitu unapaswa kuacha kuvifanya ili uwekeze nguvu zako na muda wako kwenye kukuza thamani yako zaidi.

    Hii inakusaidia kuwekeza muda wako kwenye sehemu zenye nguvu na kuachana na sehemu ambazo hazina nguvu kwa upande wako.

    Rafiki yangu kama kuna sehemu ambapo wewe unapaswa kuwekeza muda wako na nguvu zako basi ni kwenye thamani yako. Hakikisha kwamba unaijua thamani yako kw aundani.

    Nimeandaa kitabu kizuri kwa ajili yako kitakachokusaidia wewe kwenye hili. Kitabu kinaitwa JINSI YA KUONGEZA THAMANI YAKO.

    Karibu sana uweze kujipatia nakala yako siku ya leo.

    Kupata nakala tuwasiliane kwa 0684408755 jina ni GODIUS RWEYONGEZA

  • Wewe unapenda kitu gani?

    Kati ya vitu vyote, nilipenda vitabu zaidi– Nikola Tesla

    Wewe unapenda kitu gani? Nadhani hili ni swali ambalo ukiuliza kwa vijana kama sisi wa siku hizi utapata majibu ya ajabu Sana.

    Kama unaweza kuvumilia *pressure,* Basi uliza hilo swali. Ila Kama una *pressure* ya haraka basi usiliuze labda Kama umechoka kula ugali. Hahaha

    Nakwambia hivyo, kwa sababu majibu utakayopata kutokana na swali Hilo yatakusikitisha sana.

    Mimi sitataja majibu  utakayopata, hivyo kaulize mwenyewe…..

    Utagundua mwanzoni nimeanza na nukuu ya Nikola Tesla ananasema Kati ya vitu vyote, vitabu ndivyo nilipenda zaidi.

    Sijajua wewe upande wako vipi.

    Leo nimeona nikusisitize zaidi huu ya umuhimu wa vitabu. Vitabu ni vya muhimu Sana kwenye maisha. Nakumbuka siku za nyuma niliwahi KUANDIKA kitabu kizima kinachoeleza NGUVU KUBWA iliyo kwenye Kusoma vitabu na jinsi ya kuitumia hiyo NGUVU kufanya makubwa.

    Nashauri na wewe usome hiki kitabu maana kina Mambo mengi mazuri sana ndani yake ambayo yatakunufaisha na wewe. Na ubora ni kwamba unaweza kukipata bure hapa

    Kwa kuwa vitabu vina Mambo mengi mazuri. Leo nataka nikwambie kwamba vitabu vina uwezo wa kukutoa kwenye ukilaza kuwa gwiji. Nikola Tesla ambaye nimeanza kwa kutoa nukuu yake hapo mwanzoni, alikuwa gwiji wa Aina yake.

    Alifanya Mambo mengi mazuri kwenye ulimwengu wa ugunduzi. Ni mmoja wa watu wanaoaminika kwamba waligundua redio.

    Lakini ukifuatilia nyuma yake unakuta kwamba alikuwa anapenda kusoma vitabu. Sijajua Hilo linakuwaje, Ila kila Mara ukifuatilia historia za watu waliofanya MAKUBWA, Kati ya Mambo mengi ambayo najifunza Kutoka kwa hao watu ni kusoma vitabu.

    Ninapoandika hapa nipo nasoma historia ya Mkurugenzi maarufu wa kampuni GE. Jack Welch, nadhani ukitafua Google wakurugenzi Bora wa nyakati zote, Ni lazima Jina la huyu jamaa ulikute.

    Lakini kinachonishangaza ni kwamba pamoja na mengine mazuri ambayo alifanya ila bado alikuwa anapenda kusoma vitabu.

    Hivyo, nadhani usomaji wa vitabu, unabaki kuwa ni moja ya jambo muhimu sana kwenye ulimwengu wa leo. Yaani, unabaki kuwa ni jambo la muhimu mno.

    Kati ya vitu vyote ambavyo utafanya, basi hakikisha kwamba unasoma na vitabu pia. Vitabu Ni muhimu Sana.

    Tenga muda hata kama Ni kidogo kuhakikisha unasoma vitabu.

    Pakua kitabu Cha bure hapa ili uweze kukisoma zaidi

    Kila la kheri

  • Hiki kitu kimoja tu kinaweza kukufanya ulipwe zaidi ya unavyolipwa Sasa

    Rafiki yangu, najua Mara kwa mara huwa nakwambia njia mbalimbali za kukusaidia KUONGEZA kipato chako.

    Nafanya hivyo kwa sababu nakupenda. Najua wazi kuwa haupaswi kutegemea chanzo kimoja cha kipato. Lakini pia najua wazi kuwa kama chanzo chako kimoja ni ajira Basi maana yake unapaswa kuhakikisha kwamba umepanbana na kuongeza vingie zaidi zaidi ili vitakavyokuingizia kipato bila Kokomo.

    Nadhani, kama Kuna mchezo ambao kila mmoja anapaswa kuufurahia hapa duniani Basi ni mchezo wa kuhakikisha kwamba   anaongeza kipato chake Mara kwa mara. Na hili linawezekana vizuri sana. Na ndio maana nimekuwa nasukumwa kukwambia njia mbalimbali za kuongeza kipato chako, na hata nimeandika vitabu kadha wa kadha vya kukusaidia kwenye hili Kama kitabu cha

    MAAJABU YA KUWEKA AKIBA
    JINSI YA KUONGEZA THAMANI YAKO na
    MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE.

    Sasa siku ya leo nataka nikwambie kitu kimoja ambacho kitakufanya wewe uweze kulipwa zaidi ya unavyolipwa sasa. Kitu hiki siyo kingine bali ni uhakika wa kutegemewa kufanya jambo na ukalifanya.

    Yaani, kwamba mtu anaweza kujiamini kwamba utafanya Jambo fulani, na kweli Hilo jambo ukalifanya bila shida yoyote.

    Hili ni jambo ambalo unapaswa kujijengea.
    Moja ya kitu ambacho kimekuwa kinanishangaza ni kuwa vijana wengi huwa wanaandika kwenye CV zao kuwa ni wachapakazi na wanaweza kufanya kazi hata kwenye msukumo mkubwa. Utakuta MTU ameandika kwenye CV yake kuwa “I can work under pressure”. Lakini Sasa njoo kwenye uhalisia. Huyo mtu hawezi kufanya hata za kawaida tu.

    Ulimwachia kazi na ukaondoka huyo mtu anakuwa siyo wa kutegemewa. Ni mpaka uwepo ndipo anaweza kufanya kazi. Kama haupo hawezi kufanya kazi.

    Ukiwa na tabia ya Aina hii huwezi kutegemea kulipwa zaidi kama ambaye anategemea kufanya kitu na anahakikisha kwamba amekifanya.

    Hivyo, Kuanzia siku ya leo nataka uwe mtu wa kutegemewa.
    Kutegemewa kufanya kazi na ukalifanya.
    Kutegemewa utawahi na ukawahi
    Kutegemewa kufanikisha kitu au vitu fulani na ukaweza kuvifanikisha.

    Rafiki yangu, inawezekana na ninakitakia kila la kheri.

  • Hiki kitu kimoja hakiwezi kukupa mafanikio unayotaka

    Watu wengi wanapenda kupata mafanikio kiasi kwamba ukiingia kwenye chumba Chenye watu kumi na Kuuliza wangapi wanapenda kufanikiwa? Utashangaaa kuona mikono zaidi ya kumi ikiwa imenyooshwa juu. Kwa Nini? Kwa sababu baadhi ya watu wanapenda Sana mafanikio kiasi kwamba wanakuwa tayari kunyoosha mikono miwili juu.

    Japo watu wengi wanapenda mafanikio, Ni wachache Sana ambao wanakuwa tayari kuchukua hatua na kuweka juhudi kupata mafanikio wanayotaka. Unakuta MTU anaendelea kufanya vitu kwa namna ileile waliyokuwa wanafanya babu zake Huku akitegemea kupata matokeo ya TOFAUTI.

    Hiki kitu Albert Einstein alikiita ujinga aliposema; ujinga ni kufanya vitu vilevile huku ukitegemea kupata matokeo ya TOFAUTI.

    Kumbe kwa mantiki hiyo ili upate matokeo ya TOFAUTI. Ni sharti. Na ninasema sharti uwe tayari kuchukua hatua za TOFAUTI.
    Hatua za kuanzisha biashara Kama ulikuwa hauna biashara.
    Hatua za kuongeza mauzo Kama tayari uneanzisha biashara
    Hatua za kujenga timu na kuwa na wasaidizi kwenye biashara. Huwezi kuendelea kufanya majukumu yooote kwenye biashara huku ukitegemea kupata matokeo ya makubwa.
    Hatua za KUTANGAZA biashara yako na nyingine nyingi.

    Ni kweli hatua hizi muda mwingine zinaogopesha.
    Ni kweli hatua hizi muda mwingine zinatufanya tusijisikie sawa. Ila zinapaswa kuchukuliwa Mara zote.

  • Vitu Saba vya KUZINGATIA unapokuwa na miadi na watu

    Rafiki yangu wa ukweli, siku ya leo Ningependa nikwambie vitu saba unavyopaswa KUZINGATIA pale unapokuwa na miadi na watu.

    Kwenye ulimwengu wa Biashara, miadi Ni jambo ambalo haliepukiki. Utahitaji kukutana na Wateja. Utahitaji kukutana na wasambazaji, utahitaji kukutana na washirika, utahitaji kukutana na wafanyakazi na wengineo wengi…

    Sasa yafuatayo ni mambo saba ya kuzingatia

    Kwanza. Unapokuwa na miadi na watu hakikisha kwamba unawahi kwenye miadi hiyo. Ikitokea kwamba una changamoto inayokuzuia wewe kufika eneo husika kwa wakati, basi wajulishe wahusika.

    Pili, unapokutana na watu usigawe umakini wako. NGUVU zako na Akili Yako yote iwe kwenye hiyo miadi.

    Tatu, usitumie simu Wala kifaa kingine wakati unaongea na watu.

    Nne, hakikisha unakuwa na kalamu na karatasi na andika yale ambayo wengine wanaongea. Chukua notsi. Hii itaonesha namna ulivyo makini kwenye kufanyia Kazi majukumu yako.

    Tano, usiingilie Kati mazungumzo ya mtu. Mwachie MTU nafasi ya kuongea mpaka mwisho Kisha ndiyo wewe uingilie kati.

    Sita, sikiliza umakini anavyosema mwingine. Haipendezi kuona kwamba mtu fulani anasema jambo fulani Tena kwa namna ya kueleweka halafu wewe unakazana Kuuliza. Hivi umesemaje hapo?

    Saba, vaa vizuri ili kuendana na mkutano husika.

    Rafiki yangu, hayo ndiyo mabo saba ya kuzingatia pale unapokuwa na miadi. Nikutakie wakati mwema rafiki yangu wa ukweli

    Jinsi Ya Kufanya Na Kukamilisha Majukumu Yako Kwa Wakati

    Ni Mimi rafiki yako
    Godius Rweyongeza
    0755848391

X