Home


  • Namba Zetu Za Malipo

    Namba za malipo ya vitabu:

    Namba za lipa

    TIGO PESA: 19016638 Jina ni SONGAMBELE CONSULTANTS

    M-PESA: 5564517 jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

    Namba za kawaida

    AIRTEL MONEY: 0684408755
    TIGO PESA: 0655 848 392
    M-PESA: 0745 848 395

    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    NB: Kama namba ya malipo anatumiwa mtu ambaye yuko nje ya nchi. Iandikwe Kwa kuanza na +255

    Kwa hiyo namba zinazotumwa nje ya nchi zitakuwa
    Airtel money: +255 684 408 755
    TIGO PESA: +255 655 848 392
    M-PESA: +255 745 848 395

    KOTE Jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Kama malipo yatakuwa yanafanyika kupitia benki.

    Yafanyie kupitia

    1. CRDB BANK: 0150770710200
    2. NMB BANK: 22110047274

    Kote jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

  • Wasiliana na Godius Rweyongeza Sasa

    Habari yafuatayo ni mawasiliano Unayoweza kutumia kumpata GODIUS RWEYONGEZA

    Simu: +255 (0) 684408755

    Whatsap: +255 (0) 755848391

    Email: songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu vyake wasiliana Moja kwa Moja na +255 (0) 684408755 (more…)

  • Ukifanya Hiki Kitu Kimoja Tu Utafanikiwa Sana

    Rafiki yangu wa ukweli, kuna kitu kimoja ambacho endapo utakifanyia kazi, ni wazi kuwa utafanikiwa, tena siyo kwa viwango vya chini, bali utafanikiwa kwa viwango vya juu sana.Unaweza kuwa unajiuliza hili linawezekanaje maana kila siku najifunza kuhusu mambo mengi ya kufanya ili kufanikiwa.

    Kitu kikubwa unachohitaji wewe siyo kufanya mambo mengi ili ufanikiwe, bali unahitaji kujithibiti wewe mwenyewe na kuhakikisha kwamba umekuwa na nidhamu kwenye yale unayotakiwa kuyafanya na kuyafanya bila ya kukosa. Ukiweza kufanya hili, ujue utafika mbali sana/

    Hii ni kutokana na ukweli kuwa asilimia kubwa ya vile vitu vya msingi unavyotakiwa kufanya kwa ajili ya mfanikio yako, tayar unavijua.

    Najua unajua kwamba unahitaji kuweka akiba. Kwa hiyo wewe unachohitaji sasa hivi siyo kuambiwa kwamba weka akiba. Unajua vizuri tu. unachohitaji ni nidhamu ya kuweka akiba bila ya kuacha.

    Tayari unajua kwamba unapaswa kufanya kazi kwa bidii. Unachihitaji wewe siyo kuambiwa tena kwamba fanya kazi kwa bidii. Bali ile nidhamu ya kufanya kazi kwa bidii.

    Tayari unajua kwamba mafanikio makubwa hayaji ndani ya siku moja. bali ni matokeo ya vile vitu vodogovidogo unavyokuwa unafanya kila siku na unavifanya kwa mwendelezo bila ya kuacha.

    Kwa hiyo, unachihitaji wewe siyo kusubiri uwe na mabilioni ya fedha kwenye akaunti yako ili uwe bilionea, bal unajua wazi kuwa kuweka akiba hata kama ni kidogokidogo kwenye akaunti yako kila siku, kutekupeleka wewe kwenye ubilionea huo

    Kumbe basi rafiki yangu, unachohitaji wewe siyo vitu vingi sana ili ufanikiwe. Unahitaji kitu kimoja tu. na kitu hiki ni nidhamu ya kuamua kufanya jambo na ukahakikisha kwamba hilo jambo unalifanya kwelikweli.

    Sasa ninachotaka kutoka kwako siku ya leo ni kitu kimoja tu. Nataka uniambie ni kitu gani kimoja ambacho utakuwa unafanya na utakufanya kwa msimamo kila siku bila ya kuacha. Halafu, mimi nikusaidie kukufuatilie kwenye hilo, ukifanye hicho kitu mpaka uifanikishe.

    Hilo ndilo jambo kubwa sana ambalo nilitaka kukwambia siku ya leo. Naomba nikutakie kila la kheri.

    Kitu kimoja cha ziada, ningependa tu kukumbusha kuwa semina yetu ya ana kwa ana ambayo itafanyika Morogoro mwezi wa sita, ndio hiyo hapooo inakaribia.

    Nichukue nafasi hii kukukaribisha kwenye semina hii ya kipekee sana.

    Kitu kimoja cha kufanya ni wewe kuhakikisha kwamba unajiandikisha kwa ajili lya kuhudhuria semina hii. Fanya hivi. TUMA UJUMBE unaothibisha kwamba utashiriki kwenye hii semina kwa whatsap Namba 0755848391.

    Ada ya semina ni 50,000/-

  • Tumezindua audiobook mpya, haya hapa ni mambo ya msingi ambayo unahitaji kuyajua.

    Rafiki yangu mpedwa kwa mara ya kwanza kabisa mwaka jana tulizindua audiobook ya kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO. ilikuwa ni audiobook ya kwanza ya kiswhili, Tanzania kama siyo Afrika Mashariki nzima. Watu wengi waliichangamkia hii audiobook, kitu kilichonifanya nione kwamba kuna uhitaji mkubwa wa hizi audiobook, kutokea hapo tumeendelea kutengeneza audiobooks za vitabu tofautitofauti. Ambapo mpaka sasa hivi tumetengeneza audiobooks zifuatazo.

    1. JINSI YA KUFIKIA NZOTO ZAKO ina urefu wa saa 2 dakika 57 (sample ya audiobook hii iko hapa chini)

    Hii ni sample ya audiobook, audiobook kamili ipo na ina urefu wa saa 2 dak 57. TUwasiline kwa 0687408755

    2. NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKA MAFANIKIO MAKUBWA (ina urefu wa saa 3 dakika 37) pamoja (sample ya audiobook hii iko hapa chini)

    3. MAISHA NI FURSA: ZITUMIE ZIKUBEBE ina urefu wa saa 5 dakika 06 (sample ya audiobook hii iko hapa chini)

    Audiobook ya kitabu cha maisha ni fursa, tuliizindua mwishoni mwa mwaka jana.

    Kitu kimoja ambacho nimekuja kugundua kwenye utengenezaji wa audiobooks ni kwamba watu ambao wanaonja utamu wa kusikiliza vitabu kwa sauti, hawataki kuacha hata kidogo. Hili nimeliona mwenyewe, maana wale waliopata kusikiliza audiobook hizo tatu hapo juu, wamekuwa wakinipigia au kunitumia jumbe kila mara kutaka kupata audiobooks nyingine zaidi.

    Na kitu hiki kimenisukuma kuandaa audiobook nyingine mpya na hivyo leo nina furaha kubwa sana kukutangazia kuwa tumezindua audiobook ya kitabu cha JINSI YA KUONGEZA THAMANI YAKO.

    Audiobook hii ni ya kipeke sana na ambayo nashauri uhakikishe kwamba umeipata, tena sasa hivi.

    Ina urefu wa saa 4

    Imesomwa na Fadhil Kirundwa ambaye amekuwa anasoma audiobooks zetu za siku za nyuma.

    Unaipata kwa telegram

    Na gharama yake ni 15,000/-.ila habari njema ni kwamba endapo utafanya malipo siku ya leo. Basi hii audiobook utaweza kuipata kwa ofa ya shilingi 10,000/- tu. Malipo yote yafanyike kupitia namba ya simu ya 0684408755 jina ni GODIUS RWEYONGEZA.

    Ukishafanya malipo. Tuma ujumbe kwa namba hiyohiyo ili uweze kutumiwa audioboook yako.

    Utapokea audiobook yako ndani ya dakika tano tu baada ya kuwa umefanya malipo. Karibu sana.

  • Mabilioni yayeyuka upatu mpya

    Hiki kichwa wala hata siyo mimi niliyekitunga, kilikuwa ni kichwa kwenye gazeti la mwananchi juzi. Ni moja ya habari ambayo imetikisa kwenye vyombo vya habari, na kwenye mitandao ya kijamii. Swali ambalo unaweza kuwa unajiuliza ni kuwa inawezekanaje watu wanalizwa kila mara kwa kutapeliwa na bado wanazidi kutapeliwa?

    Utapeli hautaisha hapa duniani.

    Moja kati ya matapeli wakubwa sana ambao waliwahi kuishi hapa duniani, ni bwana mmoja ambaye anajulikana kwa jina la Ponzi. Huyu jamaa alifanya utapeli wake miaka ya 1920

    Huu ulikuwa ni mradi ambao ulikusanya pesa nyingi za watu na baadaye jamaa akawa ameyeyuka na pesa za watu.

    Mpaka leo hii michezo ya upatu mingi imekuwa inajulikana kwa jina la PONZI SCHEME. Ikichukua jina la tapeli mkubwa sana kuwahi kutokea hapa duniani. Kabla ya huyu jamaa utapeli ulikuwa ukifanyika na hata baada ya utapeli huo mkubwa alioufanya, bado utapeli umekuwa unafanyika. Kwani mwaka 2008,  tapeli mwingine mkubwa  kwa jina la Bernoff alikuwa ametapeli watu zaidi ya dola bilioni 64.

    Huu nao ulikuwa ni utapeli mkubwa sana.

    Naweza kuonekana naongelea utapeli unaoendelea kwenye nchi za watu wengine, halafu ikaonekana kama vile hapa kwetu hakuna uutapeli unaonendelea.  Hapa kwetu pia utapeli umekuwa unaendelea kwa wingi sana.

    Nadhani, mara ka mara umekuwa unasikia watu wanavyotapeliwa.

    Juzijuzi tu hapa kulikuwa na watu wanaitwa Kaylinda, hawa waliyeyuka na pesa nyingi za watu pia. Sasa juzi tena gazeti la mwananchi lililipoti taarifa ya mabilioni ya watu kulizwa kwa mabilioni yao kupelekwa.

    Unachopaswa kufahamu mpaka hapa ni kwamba utapeli upo na utaendelea kuwepo kwa miaka yote ambayo binadamu atakuwa hapa duniani.

    Hii hapa ni sababu kwa nini utapeli utaendelea kuwepo hapa duniani.

    Kwanza unajua kwa nini watu huwa wanatapeliwa?

    Watu huwa wanatapeliwa kwa sababu wanapenda kupata faida kubwa ndani ya muda mfupi, au huwa wanataka kupata fedha nyingi ndani ya muda mfupi na bila ya kufanya kazi. Hiki ndicho chanzo cha watu kutapeliwa. Na ndio maana watu wataendelea kutapeliwa.

    Watu wataendelea kutapeliwa kwa sababu wanapenda hivyo vitu viwili nilivyoanisha hapo juu. Faida kubwa kutokana na uwekezaji wao, tena ndani ya muda mfupi pamoja na pesa nyingi tena bila ya kutoa jasho.

    Sasa kwa kuwa matapeli wanayajua hayo mambo mawili, wakija kukutapeli wanaanzia hapo.

    Wanakuahidi kukupa fedha nyingi ndani ya muda  mfupi, tena bila ya kufanya kazi au kutoa jasho.

    Kwa kuwa watu wanataka kuwekeza na kupata mrejesho mkubwa, hapo ndipo wanaanza kuchutapeliwa.

    Viashiria kwamba hapa uwekezaji fulani ni upatu

    1. Unaambiwa kwamba ufanye uwekezaji na hakuna hatari yoyote ile kwenye uwekezaji huo.

    Kila uwekezaji una hatari zake, ukiona mtu anaanza kukwambia uwekezaji fulani hauna hatari yoyote, basi ujue kwamba hicho ni kiashiria cha kuwepo cha mchezo wa upatu.

    2. wanatoa mrejesho mkubwa kwa watu wawekezaji wa kwanza ili kuwavutia watu kuwekeza zaidi. unachoopaswa kujua wewe kama mwekezaji ni kwamba hakuna uwekezaji ambao huwa unatoa mrejesho mkubwa tu mara zote. kuna wakati mrejesho unaweza kuwa ni mkubwa na muda mwingine ukapungua. Ila ukiona unaambiwa ukiwekeza utapata mrejesho mkubwa tu, au ukiona watu wanapewa mrejesho mkubwa tu kila mara. Basi hapo ujue kuwa kiashiria cha utapeli.

    3. shughuli zinazoleta kipato hazijulikani. Yaani, wewe unaambiwa weka laki moja leo na kesho tutakupa laki mbili, lakini ukiwauliza ni shughuli gani ambazo zinawapa hicho kipato kwa haraka hivyo, wanakuwa hawako tayari kuziweka wazi. Ila wewe unaambiwa, wewe wekeza tu uone….

    Ukiona hivyo, ukiwekeza tu ujue utaona kwelikweli…

    Sasa ufanyeje ili kuepukana na kutapeliwa?

    Rafiki yangu, hivi nilikwambia kwamba watu wamekuwa wanatapeliwa na wataendelea kutapeliwa kwa siku zote ambazo binadamu anaendelea kuishi. Ndio, sijakosea kwenye hili, na kuthibitisha hili wewe mwenyewe unaweza kujaribu kuorodhesha utapeli ambao umewahi kusikia au kuona kwa macho yako tangu umekuwa na akili timamu. Tuachane na tangu umekuwa na akili timamu, tuchukue tu hata miaka mitano iliyopita. ni mara ngapi umesikia watu wametapeliwa. Ni mara nyingi sana. na hao ni wale ambao walitangazwa kwenye vyombo vya habari, kuna wale amba habari zao hazisikiki kwenye vyombo vya habari, na hao ni wengi pia.

    Ssa ufanyeje ili kuepukana na kutapeliwa?

    Yafuatayo ni mabo ya kuzingatia.

    Kwanza usikurupuke kuwekeza. Kisa unaona watu wengi wanakimbia kuwekeza na wewe unakimbia tu kuwekeza.

    Pili, wekeza kwenye uwekezaji unaoeleweka. Kama kitu hukielewi, usiweke hela yako hata kama wanakuahidi kukupa hela mara elfu moja ya ile uliyoweka. Warren Buffet ni mmoja wa matajiri wakubwa sana hapa duniani, na anafanya uwekezaji. Lakini kitu kikubwa sana kuhusu gwiji wa uwekezaji ni kwamba huwa hawekezi kwenye vitu ambavyo havielewi. Yeye huwa anawekeza tu kule anapokuelewa.Hiki kitu kimefanya watu wengi wamseme sana, ila yeye kwa upande wake ameendelea kusimamia msimamo wake huo bila kuteteleka. Mfano, moja ya  msimamo wake ni msimamo wake wa kutowekeza kwenye makampuni ya mitandao ya intaneti. Ni aina ya biashara ambayo alikuwa haielewi, na hivyo hajawekeza huko. Ndio kuna watu wamewekeza na wanapata faida nzuri, ila yeye haelewi, hivyo, hata haweki nguvu kwenye hayo makampuni.

    WEWE pia kwa upande wako unapaswa kuwa hivyo, usiwekeze kwenye kitu ambacho hukijui.

    Tatu, Wekeza kwenye uwekezaji uliorasimishwa na serikali kama uwekezaji kwenye HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE unmerasimishwa na unaendeshwa chini ya soko la HISA LA DAR ES SALAAM. Kuelewa zaidi kuhusu hisa, hatifungani na vipande basi soma kitabu cha MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE. Hiki ni kitabu ambacho kimewasaidia watu wengi, na wewe kitakusaidia pia. Kipate hiki kitabu kwa manufaa yako.

    Pata hiki kitabu kwa 20,000 hardcopy na 10,000 softcopy

    Sambamba na hicho kitabu, kuna kitabu kingine muhimu sana ambacho unapaswa kuchukua. na kitabu hiki siyo kingine bali ni hiki hapa

    Kipate kitabu hiki kwa manufaa yako

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.

    Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.

    Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.

  • Hii ndiyo njia rahisi ya wewe kujipoteza

    Rafiki yangu, kama kuna njia rahisi ya wewe kujipoteza ni kufanya vitu kama ambavyo kila mtu anafanya. sote tunajua kwamba vitu ambavyo watu wengi huwa wanafanya huwa siyo sahihi. Na njia ya pekee ya wewe kuishi maisha ya kawaida, ni wewe kufanya vitu kama ambavyo kila mtu anafanya.

    Hii ni njia ambayo haifanyi kazi, na laiti kama hii njia ingekuwa inafanya kazi maana yake watu wengi wa kawaida wangekuwa matajiri wakubwa sana au la wangekuwa na mafanikio ambayo siyo ya kawaida. Lakini hali siyo hivyo.

    Kumbe vitu ambavyo watu wengi wafanya siyo sahihi. Na kitu kufanywa na watu wengi hakikifanyi kuwa sahihi.

    EBU KWA MFANO tuchukulie tu maisha ya kawaida ambayo mtu anaishi. Anaambiwa kwamba nenda shule usome kwa bidii, na kweli anaenda shule anasoma kwa bidii, kisha baada ya shule anatafuta kazi. tuchukulie huyu mtu amepata kazi, baada ya hapo anaenda kazini. Akifika kazini, anaambiwa kwa kuwa sasa una mshahara, wewe unaweza kupata mkopo ambao utakufaa.

    Anachukua mkopo.

    Wakati huohuo, anakuta kwamba kuna sheria ambayo inamtaka kujiunga na mashirika ya MAFAO, hivyo anaanza kuaminishwa kwamba ukiweka hela yako, hutahitaji kushughulika na pesa zako tena. Na wala hutahitaji kujiandaa kwa ajili ya kuja kustaafu, badala yake sisi, tutakufanyia kila kitu.

    Anaanza kuishi maisha yake kihivyo, mpaka anafikia miaka ya kustaafu ambapo anakuja kupewa MAFAO yake, hapo ndio anagundua kwamba hayatoshi. Muda huu sasa ndio anaanza kufunguka ili aweze kutafuta ajira na kazi nyingine.

    Habari njema ni kwamba unaweza kujiondoa kwenye huu mnyororo wa watu wengi, na kujiweka kwenye mnyororo wa watu uwachache.

    Kwenye jamii yoyote ile huwa kuna wachache waliofanikiwa. Na hawa watu ukiwafuatilia, utagundua kitu kimoja kutoka kwao. Kitu hiki ni kufanya vitu kwa namna ya upekee, tofauti na watu wengine

    Hawa ndio wale ambao utakuta wanajilipa wenyewe kila baada ya kuwa wamepata kipato chao.

    Hawa ndio wale ambao utakuta kwamba wanawekeza na kuchukua kiasi cha fedha na kukifanya kiwafanyie kazi.

    Hawa ndio wale ambao huwa hawanunui vitu kuwaridhisha watu wengine. Badala yake huwa wananunua kutokana na uhitaji wao kwa wakati husika.

    Rafiki yangu, ninachotaka kukusisitiza siku ya leo ni kwamba wewe unaweza kujiingiza kwenye kundi la watu wachache sana ambao wanafanya makubwa. Na hili linawezekana vizuri sana. Ila utahitaji kuzingatia yafuatayo.

    Kwanza, utahitaji kujisukuma kwenye kila kitu unachofanya. Na kuhakikish kwamba hicho kitu unakifanya kwa namna ya utofauti ukilinganisha na watu wengine. Jisukume kwenye kitu chochote unachofanya na hakikisha kwamba kila unachofanya, unakifanya kwa viwanvo vikubwa sana. Naam, unakifanya kwa viwango vikubwa sana kuliko ambavyo umewahi kukifanya.

    Kiasi kwamba mtu yeyote atayeona kazi yako, aseme kweli hii kazi imefanywa na mtu fulani.

    Pili, utahitaji ujiepushe na mambo mengine yote ambayo hayachangii kwenye kufikia ndoto zako. na hapa namaanisha mambo mengine yote. Kama umekuwa unaangalia runinga kila siku. Kuanzia sasa hivi, anza kujiuliza, hivi runinga inasaidiaje kwangu kwenye kufikia ndoto zangu. Ukifuatilia kwa umakini utagundua kwamba, runinga haina manufaa yoyote yale kwako. Hivyo, unaweza kuiweka pembeni ili uweze kufanyia kazi majukumu yale machache ambayo yatakuwa na manufaa kwako.

    Kama umekuwa unafuatilia maisha ya watu wengine, jiulize ni kwa namna gani kufuatilia maisha ya watu wengine kumekuwa na manufaa kwangu? Utagundua kwamba kufuatilia maisha ya watu wengine hakuna manufaa yoyote yale kwako. Hivyo, badala ya wewe kuanza kufuatilia maisha ya watu wengine, weka nguvu sasa kwenye kujifuatilia wewe mwenyewe. Weka nguvu kwenye kufuatilia mipango yako na mambo mengine ambayo yanakuhusu wewe mwenyewe.

    Tatu, usiige maisha. Uwepo wa mtandao wa intaneti na mitandao ya kijamii. Uwepo wa runinga na vitu vingine umewafanya vijana wengi waishi maisha ya kuigiza kwa wingi kuliko uhalisia. Wengi watanunua vitu hata kama hawahivitaji. Wanasahau kwamba Warren Buffet anasema sheria kuu mbili unazopaswa kuziangatia ni moja, kutokupoteza fedha. Na mbili ni kutosahau sheria ya kwanza.

    Rafiki yangu, kwa leo ningependa niishie hapo. Naamini kuna kitu utakuwa umepata kutoka kwenye hii makala ya leo. Kama wewe umeweza kunufaika hata kwa kupata kitu kimoja tu unachoweza kufanyia kazi. basi kuna wengine wanaweza kunufaika pia. Ebu washirikishe rafiki zako wawili tu hii makala ili na wao waweze kuisoma na kunufaika nayo.

    Chagua kimoja, kisha nicheki kwa 0755848391 ili uweze kupata nakala ya kitabu chako.

    Bila kuongeza kitu cha ziada. Nikutakie siku njema sana.

  • Kinachokukwamisha wewe ni hiki hapa

    Rafiki yangu, umewahi kujiuliza ni kitu gani kinakukwamisha wewe kuweza kufanya makubwa. Kama kuna kitu kinakukwamisha wewe na watu wengine wengi, basi kitu hiki ni kufanya kazi kama vile una muda wote hapa duniani. Yaani, unaanza kufanya jukumu lako bila ya kuwa na lengo wala mwelekeo wowote. Kitu kinachokufanya ufanye jukumu hilo kwa muda mrefu sana kuliko unavyokuwa unatazamia.

    Unaweza usijue hili. Kwa sababu kama hauna mpango, utaona uko sahihi kwa kile utakachokuwa unafanya. Ila nikuhakikishie kwamba ukiwa na mpango, rafiki yangu, mambo yako, utayafanya vizuri, kwa kujisukuma na kujituma zaidi.

     Ninachotaka ufahamu ni kuwa kama unataka kuutumia muda wako vizuri na kwa manufaa makubwa sana, basi unapaswa kuwa na ukomo kwenye muda wako.

    1. kuanzia unapoamka asubuhi, hakikisha kwamba unapangilia siku yako kwa kuweka majukumu yote utakayoyafanya ndani ya hiyo siku. Usikubali kuipitisha siku bila ya wewe kuwa na mpango ambao unaoufanyia kazi ndani ya hiyo siu

    2. Muda ambao wewe unautumia kupangilia siku yako au wiki yao, siyo kwamba huo muda unakuwa unaupoteza. Hapana, badala yake huo muda unakuwa unautumia kwa manufaa makubwa. Hivyo, usije kusema kwamba nimepoteza muda kwa kupangilia siku yangu. Badala yake unakuwa umeokoa muda, maana muda ambao hapo baadaye ungekuja kuupoteza utauokoa kwa kufanya majukumu ya maana.

    3. Ukishapangilia siku yako, kinachofuata ni wewe kufuata huo mpangilio wako ambao umeuweka kama ulivyo. Kufanya majukumu yako muda ambao unapaswa kuyafanya bila kuacha, kitu hiki kitakufanya uweze kuutumia muda wako kwa manufaa makubwa.

    Asante sana, nikutakie siku njema rafiki yangu.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.

    Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.

  • Jinsi ya kuwa mtu mwenye msaada kwa wengine

    Huwa inatokea kwamba mtu anasoma makala yangu ambayo niliandika siku nyingi za nyuma, kisha mtu huyo anasema kwamba hiyo makala imemsaidia sana.

    Mfano leo hii wakati naandika makala hii nimeagalia maoni kwenye blogu kwenye makala za nyuma nimeona kwamba, maoni ya jana yaliwekwa kwenye makala ya ambayo mimi niliandika mwaka jana mwezi wa 11.

    kwangu hiki siyo kitu cha kushangaza kwa sababu wakati mwingine unaweza kukuta mtu kaweka maoni kwenye makala ambayo niliandika hata miaka mitano iliyopita.

    wakati mwingine mimi nakuwa nimeshaandika na kusahau kuwa niliandika hiyo makala.
    lakini andikko hilo linakuwa lenye msaada kwa mwingine.

    KITU HIKI ndicho kinanileta kwenye ujumbe wa leo ambao ningependa kukwambia. NA UJUMBE huu ni kwamba, kamwe usipitishe siku bila ya kufanya kitu ambacho utaona kwamba kinaongeza thamani kwa watu wengine. Kila siku fanya kitu ambacho kitaongeza thamani kwenye maisha ya mtu mwingine. Hiki kitu kinaweza kisisaidie mtu uliyemlenga leoleo. lakini kwa sababu umekifanya, kinaweza kumfikia huyo mtu hata baada ya miaka kadhaa.

    sasa swali langu kwako siku ya leo ni kuwa ni kitu gani ambacho unaenda kufanya ambacho kitakuwa chenye msaada kwako na kwa wengine hata kwa siku zijazo.

    USIWE mbinafsi kwa kutaka kufanya vitu ambavyo vitakunufaisha wewe tu.
    Asante sana na kila kheri

  • Epuka hiki Kitu kama unataka kufanya makubwa

    /

    Rafiki yangu, najua unataka kufanya makubwa kwenye maisha yako. Hongera sana kwa kuwa na ndoto kubwa sana.
    Ebu kwwanza, kabla sijakwambia kitu cha kuepuka kama unataka kufanya makubwa. Naomba kwanza uandike malengo yako na ndoto zako hizi kubwa chini. Ziandike kabisa, ili ujue ni kitu gani unataka kufanikisha kwenye maisha yako.

    Hongera kwa kuweza kufanyia kazi hilo.
    Sasa kwa kuwa una malengo na ndoto kubwa hivyo, kuna kitu kimoja ningependa ukifanyia kazi siku ya leo. Na kitu hiki siyo kingine bali ni kuhakikisha kwamba unajituma na unafanya vitu vya tofauti. Huwezi kuendelea kufanya vitu vilevile kila siku huku ukitegemea kupata matokeo ya tofauti.

    Ni lazima uwe tayari kujisukuma kidogo, ni lazima uwe tayari kufanya mambo ya tofauti, ili uweze kupata matokeo ya tofauti ambayo hujawahi kuyapata.

    Hiki ndicho kitu kikubwa sana ambacho ninataka kukwambia siku ya leo rafiki yangu.

    Kifanyie kazi hiki, utanishukuru kesho.

    Kila la kheri

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.

    Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.

    Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.

    uNGEPENDA KUPATA HIVI VITABU, TWANGA 0755848391

  • Jinsi ya kunufaika na muda wako wa safarini

    Kwa namna moja au nyingine KATIKA maisha yetu ya kila siku Kuna kusafiri.
    Unaweza kuwa unasafiri umbali mrefu sana kama kutoka mkoa mmoja KWENDA mwingine.

    Lakini muda mwingine Unaweza kuwa unasafiri eneo fupi tu. Dakika kumi, kumi na tano au SAA moja.

    Bila kujali, umbali unakwenda, Bado safari Ni safari na muda huu unapokuwa unatoka eneo moja kwenda jingine Unaweza kuutumia kwa manufaa.

    Huu muda wa Kutoka eneo moja kwenda jingine ukiuunganisha kwa siku, kwa wiki na kwa mwaka utajikuta kwamba unapata muda mwingi sana. Brian Tracy anasema kwa mwaka mmoja muda ambao MTU anakuwa safarini ni sawa na mhura mmoja wa chuo.

    Kumbe huu muda huu ukiutumia vizuri ni wazi kuwa utajifunza mengi, na pengine hata kitu ambacho umekuwa unatamani kujifunza kwa siku nyingi utakielewa.

    Ebu chukulia umekuwa unatamani kujifunza uandishi kwa siku nyingi. Ukaamua tu kuhakikisha unautumia muda ule wa safari kusikiliza vitabu na kozi za uandishi, na Kisha ukawa unatenga dakika chache tu za kuandika kila siku. Ni wazi kuwa baada ya muda utabobea.

    Au kama umekuwa unapenda kujifunza mauzo. Unaweza kuutumia muda huu wa ziada kusikiliza mafunzo ya sauti ya mauzo ambayo yatakufanya uweze kubobea kwenye mauzo.

    Kumbe basi, wito wangu kwako Ni mmoja TU rafiki yangu, kuanzia Leo hii, hakikisha kwamba unautumia vizuri Sana muda wako wa safari.
    Utumie kujifunza na hasa kujifunza kwa kusikiliza mafunzo ya sauti. Yaani, Audiobooks

    Hizi zitakupa maarifa yenye manufaa makubwa.

    Rafiki yangu, tunahitaji kuleta mapinduzi kwenye jamii zetu. Na hatuwezi kuleta mapinduzi kwa kuendelea kufanya Mambo Yale Yale ambayo tumekuwa tunafanya kila siku. Badala yake fanya mambo ya TOFAUTI kidogo kabisa. Kama kusikiliza mafunzo ya maana wakati wengine wanapoteza muda huo kwa kuchati, kusikiliza miziki na vinginevyo.

    Kila la kheri

    Kisha andika AUDIOBOOKS

  • Unataka kufanya vitu vya tofauti? Siri hii hapa

    Watu wanaofanya vitu vya tofauti siyo kwamba ni watu ambao wameshuka kutoka mbinguni. Siyo watu ambao wana vitu vya kipekee kukuzidi wewe. Siyo watu ambao wana elimu kubwa kulliko wewe. Isipokuwa ni kuwa wana sifa moja kubwa ambayo inawatofautisha wao na wewe.

    Na sifa hii siyo nyingine, bali ni sifa ya kuamua kufanya jambo na kuhakikisha kwamba wanalifanya bila ya kurudi nyuma.

    Hii ni sifa ambayo na wewe unapaswa kuwa nayo pia rafiki yangu.

    Kuazia leo hii fahamika kama mtu ambaye akiamua kufanya jambo analifanya kweli.

    Na kwa sababu ninataka ufahamike hivyo kuanzia leo hii. Nataka uanze kuchukua hatu akuanzia sasa hivi.

    Ebu sasa hivi andika chini jambo ambalo unaamua kufanyia kazi kuanzia leo hii.

    Kisha nenda kalifanyie kazi kuanzia leo hii.

    Lifanyie kazi kila siku kwa siku zijazo mfululizo bila kuacha.

    Jipe walau changamoto ya kufanya hilo jambo kwa siku 100 zijazo bila ya kuacha. Ukiweza kufanya hili jambo kwa siku hizi 100 bila kuacha, ni wazi kuwa utakuwa umeweza kujijengea nidhamu kubwa sana. lakini pia utakuwa umejenga njia nzuri yaw ewe kuweza kulifanya hilo jambo.

    Na baada ya hapo utakuwa hauzuiliki wala kurudi nyuma hata kidogo

    Chukua hatua leo hii

    Kila la kheri

  • Siri itakayokuwezesha wewe kufanya makubwa

    Rafiki yangu wa ukweli, sina shaka wiki yako umeianza vizui sana. Hongera sana kwa kazi.

    Siku ya leo ningependa tu kukwambia kuwa kama unataka kufanya makubwa kuna vitu muhimu sana ambavyo unapaswa kuzingatia nakuhakikisha kwamba umevifuata. Vitu hivi ni pamoja na na wewe kufanya majukumu makubwa kwanza asubuhi kabla hujafanya kitu kingine.

    Kama una majukumu mawili, basi nguvu yako kubwa unapaswa kuilekeza kwenye jukumu ambalo ni kubwa kwa upande wako.. Yaani, lile jukumu ambalo usipolifanya, litakuwa na madhara makubwa aidha ya muda mfupi au ya muda mrefu kwa upande wako. Ni jukumu ambaloendapo likifanyika kwa ukamilifu, litaleta matokeo mazuri. Haya majukmu mengine yanaweza kusubiri lakini hili halipaswi kusubiri.

    Mara nyingi watu wengi huwa wanaliogopa na kulikwepa hili jukumu. Kitu ambacho huwa kinawafanya wakimbilie kufanya majukumu madogo madogo ambayo hayana nguvu huku wakiacha majukumu ambayo yana nguvu. Ninachotaka kukwambia siku ya leo ni kwamba, kama uanataka kufanya makubwa. kuwa tayari kufanyia kazi majukumu ambayo muda mwingine yanaonekana ni magumu.

    Ni kwa sababu haya majukumu ndiyo ambayo yanaweza kukusogeza wewe kule unapotaka kufika.

    Haya majukumu japo yanaogopesha lakini ndiyo ambayo yatachangia kwenye kulipwa kwako kwa asilimia 80, ukilinganisha na majukumu ambayo ni asilimia 20 ambayo siyo ya muhimu sana ambayo unakuwa unafanya.

    Kazi yako siku ya leo ni kujua ni kuhakikisha kwamba unayajua majukumu yako ambayo ni ya muhimu sana, kisha kuyafanya hayo kwanza kbla hujafanya majukumu mengine.

    Kwenye mambo 10 ambayo unapaswa kufanya leo, siyo yote yana umuhimu na nguvu sawa. Ni baadhi tu, au machache kabisa ambayo yana nguvu kubwa. wekeza kwenye haya machache.

    Kila la kheri

X