Home


  • Namba Zetu Za Malipo

    Namba za malipo ya vitabu:

    Namba za lipa

    TIGO PESA: 19016638 Jina ni SONGAMBELE CONSULTANTS

    M-PESA: 5564517 jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

    Namba za kawaida

    AIRTEL MONEY: 0684408755
    TIGO PESA: 0655 848 392
    M-PESA: 0745 848 395

    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    NB: Kama namba ya malipo anatumiwa mtu ambaye yuko nje ya nchi. Iandikwe Kwa kuanza na +255

    Kwa hiyo namba zinazotumwa nje ya nchi zitakuwa
    Airtel money: +255 684 408 755
    TIGO PESA: +255 655 848 392
    M-PESA: +255 745 848 395

    KOTE Jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Kama malipo yatakuwa yanafanyika kupitia benki.

    Yafanyie kupitia

    1. CRDB BANK: 0150770710200
    2. NMB BANK: 22110047274

    Kote jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

  • Wasiliana na Godius Rweyongeza Sasa

    Habari yafuatayo ni mawasiliano Unayoweza kutumia kumpata GODIUS RWEYONGEZA

    Simu: +255 (0) 684408755

    Whatsap: +255 (0) 755848391

    Email: songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu vyake wasiliana Moja kwa Moja na +255 (0) 684408755 (more…)

  • Kwa nini vijana wengi hawawekezi kwenye soko la Hisa, hatifungani na vipande

    Mwishoni mwa mwaka Jana nilipata kuhudhuria mkutano mkuu wa mwaka wa mfuko wa umoja kwa njia ya mtandao. Mkutano huu ulikuwa unafanyika kwenye ukumbi wa Mwalimu Nyerere UBUNGO lakini pia ulikuwa ulifanyika kwa njia ya mtandao. 
    Kitu kikubwa kilichokuwa kinaongelewa kwenye huu mkutano ilikuwa ni ripoti ya mwaka 2021/2022 ya mfuko wa umoja.

    Baada ya ripoti kuwasilishwa Kuna watu walionekana wanaguswa kwa namna mkutano mzima ulivyokuwa umejaa wazee na watu wenye umri wa kustaafu kwa asilimia kubwa.

    Hii ilitoa picha kuwa hawa watu ndio wawekezaji wakubwa kwenye mfuko, na hivyo vijana wameachwa nyuma.

    Swali kulikuwa kwa Nini vijana hawawawekezi?

    Sikumbuki Kama Kuna MTU alijibu hili swali, Ila leo Ningependa kukupa sababu chache tu kuonesha kwa nini vijana hawawekezi?

    Kwanza hawana elimu. Ujue elimu ndiyo inaondoa kiza na toongotongo machoni pa mtu na hivyo kumfanya awekeze.

    Kama hauna elimu sahihi, Basi jua waziwazi kabisa kuwa huwezi kuwekeza.

    Na ndio maana nimeamua kwa dhati kuhakikisha kwamba elimu hii ya uwekezaji naiweka kwenye maandishi kwenye kitabu hiki Cha kipekee cha MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE.

    Hakikisha unapata nakala yako siku ya leo kwa 20,000/- tu. Wasiliana nami kwa 0755848391

  • KUWA IMARA

    Tunaishi katika dunia ambayo haipendi vitu ambavyo siyo imara. Na hili jambo la KUWA imara halijaanza leo. Limekuwepo kwa siku nyingi sana.

    Vitu ambavyo vimekuwa imara kwa miaka mingi ya nyuma, ndivyo ambavyo viliendelea kuishi, huku vile ambavyo siyo imara vikidhoofu na kufa.

    Watu wanyonge, mimea minyonge, wanyama wanyonge havina nafasi kubwa ya kuishi Kama vile vitu ambavyo ni imara. Hivyo, na wewe unapaswa KUWA imara.

    Najua hiki kitu kinaweza kuonekana cha ajabu sana hasa kwa upande wako ukizingatia kwamba umezoea kuambiwa KUWA wewe Ni MNYONGE. Na hivyo kuna watu wanakutetea wewe na unyonge wako.

    Ninachotaka kukwambia ni kuwa, usikubali kuwa MNYONGE. Unyonge ni hali ya chini ambayo MTU yeyote hapaswi kuibeba.
    Unapaswa KUBEBA ujasiri, uthubutu, na sifa nyingine za aina hii.

    Unyonge haukai meza moja na ujasiri. Unyonge hauwezi kukaa meza moja na uthubutu. Unyonge hauwezi kukaa meza moja na utawala.
    Ukiwa MNYONGE unanyongwa na haki yako hupewi. Huo ndio ukweli.

    Kitabu: How to Win Friends and Influence People

    Hivyo, nataka ujiondoe kwenye hali ya unyonge kuanzia Leo hii na uanze kuwa jasiri, uwe imara.

    Kanuni ya Darwin
    Darwin na wanasayansi wengine waliotangulia kabla yake kama akina Lamark na wengine ambao wamefuata baada Yao wamethibitisha kuwa viumbe ambavyo huwa ni vinyonge huwa vinapotea na kutoweka kwenye uso wa dunia, huku vile ambavyo ni imara viking’aa na kufanya makubwa zaidi.

    Mfano wa kawaida ni kwenye wanyama. Ukiwa na mbuzi au kuku umewafuga. Halafu hao wanyama ukawawawekea chakula. Wanyama ambao ni imara watakuwa mstari wa mbele kula na hata watafukuza wale ambao siyo imara. Wale ambao siyo imara watafukuzwa na kukaa pembeni. Ni mpaka pale wanyama walio imara watakapokuwa wamemaliza kula ndio na wale wanyonge watakula. Kama chakula ni kidogo, Basi wanyama wanyonge wataishia kujiramba tu.

    Hiki kitu hata sisi kwetu wanadamu ,hujawahi kuona kwenye sherehe kinaletwa chakula watu wanakigombania? Unajua ni watu wa aina gani ambao huwa wanaishia kula chakula cha aina hiyo? Ni wale ambao huwa wanakuwa imara. Wanyonge wanakaa pembeni.

    Na hiki halitokei kwenye chakula tu, Bali hata kwenye tendo. Wanyama ambao siyo imara hawapati nafasi ya kufanya tendo na wanyama wengine. Kitu kinachofanya mbegu zao zisisambae Kutoka kizazi kimoja KWENDA kingine.

    Katika ulimwengu wa leo unahitaji kuwa imara.

    Achana na dhana ya kujiita MNYONGE kuanzia leo.
    Kuna watu wamekuwa wanakuita MNYONGE . Na hata wewe mwenyewe umekuwa unajiita MNYONGE. Rafiki yangu sikiliza, kuanzia leo hii kataa kuitwa MNYONGE. Na wala wewe mwenyewe usijiite MNYONGE.

    Anza kuishi kama MTU imara. Ongea Kama MTU ambaye yuko imara. Tembea kwa kujiamini kama MTU ambaye yuko imara. Kwa jinsi hiyo, utakuwa umetengeneza ulimwengu wako wa TOFAUTI na watu watakupenda.

    Utakuwa kama Moto. Moto ni hatari sana. Ukiugusa tu, unaungua. Lakini watu duniani kote wanaupenda kinachofanya watu wapende Moto ni kwa sababu ya uimara wake. Moto hautetereki kwenye uimara wake. Ukiingia kwenye kumi na nane zake unaungua. Ukitumia vizuri unakusaidia kutengeneza vitu vingine ambavyo ni imara. Mfano, ukiutumia kuunguza tofali unazifanya imara zaidi.

    Lakini ukiutumia vibaya unaunguza nyumba. Mbali na madhara yote ambayo Moto unaweza kufanya ila tunaupenda kwa sababu ya uimara wake. Tukiwa na baridi tunawasha Moto na kuusogelea karibu kwa sababu tunajua kwamba moto ni imara na hauyumbishwi na baridi. Hivyo tunausogelea ili tupate joto.

    Tukihitaji nyama choma, tunaenda kutafuta moto kwa mara nyingine. Tunajua moto ni imara na utatusaidia kugeuza nyama ya kawaida kuwa choma.

    Tukihitaji chakula, tunaufuata Tena Moto. Tunamenya ndizi zetu na kuziweka kwenye moto, noto unaturudishia ndizi zikiwa zimeiva.

    Huo ndio uimara wa Moto.

    Na wewe unahitaji kuwa imara pia

  • Maisha Yako Ni wajibu wako

    Maisha Yako Ni wajibu wako, usisubiri MTU aje akusaidie wewe kufanya vitu ambavyo wewe mwenyewe unapaswa kufanya.

    Ebu chukulia vitu vya kawaida tu Kama KUTUNZA muda
    Kuweka akiba
    Kuamka mapema
    Kufanya Kazi kwa bidii
    Kusoma vitabu na kufanyia kazi Yale unayojifunza.

    Je, hivi unahitaji mtu akusaidie kuvifanya? Na hivi unalalamika kwamba serikali haijavifanya kwa niaba yako? Hivi kweli uko siriazi na maisha yako?

    Chukua hatamu ya maisha yako kuanzia leo hii, maana maisha ni wajibu wako. Ukishinda ni juu yako. Ukishindwa ni juu yako pia.

    Kazi ya kufanya siku ya leo.
    Angalia vitu ambayo umekuwa unalalamikia Sana.
    Jiulize je, vipo ndani ya uwezo wangu?

    Kama. Vipo ndani ya uwezo wako, vifanye. Kama vipo nje ya uwezo wako, achana navyo.

    Kila la kheri.

  • Kitu Chenye Thamani Unachopaswa Kuwa Nacho Kuanzia Leo Hii

    Rafiki yangu ili uweze kuishi vizuri kwenye dunia ya sasa. Ni vizuri sana ukihakikisha kwamba una ujuzi wa kufanya jambo au kitu fulani.

    Hiki ni kitu ambacho wewe mwenyewe unaweza kujenga. Ujuzi wako unaweza kukutambulisha popote na kwa yeyote. Ujuzi wako unaweza kukulipa.

    Kama hauna ujuzi ni muda wako sasa wa kuhakikisha kwamba unaanza kujenga ujuzi. Badala ya wewe kupoteza muda kwenye mitandao ya kijamii ukiangakia vitu ambavyo havina manufaa, utumie muda huohuo kuhakikisha kwamba unajenga ujuzi wako.

    Utakuwa hujitendei haki kama unalalamika Kuwa maisha Ni magumu. Vyuma vimekaza halafu baada ya hapo unapoteza muda kwenye mitandao ya kijamii au kwenye vijiwe ukipiga stori. Badala ya kujenga ujuzi ambao utakulipa zaidi.

    Ubora wa ujuzi ni kwamba ukishakuwa nao unakuwa nao. Hakuna mtu yeyote ambaye anaweza kuuiba kwako.

    Hivyo basi rafiki yangu, kuanzia sasa chagua aina ya ujuzi ambao unaweza kujenga. Kwenye kitabu changu cha NGUVU YA KUCHUKUA HATUA YA KWANZA nimeeleza Aina 21 za ujuzi ambazo unaweza Kuwa nazo. Simaanishi kwaamba unapaswa Kuwa na Aina zote. Hapana.

    Badala yake unapaswa kuchagua Aina moja tu ya ujuzi na kukomaa na huo kwanza.

    Baadhi ya ujuzi unaoweza Kuwa nao ni Kama
    1. Kuchora
    2. Kuandika
    3. Kuongea na kuwasilisha mada watu wakakusikiliza (uneni)
    4. Graphics
    5. Kuuza

    Zipo Aina nyingi za ujuzi, Ila ujumbe wangu kwa leo ni kwamba chagua Aina moja tu ya ujuzi na hakikisha kwamba unakomaa na hiyo Aina ya ujuzi bila ya kurudi nyuma.

    Kila la kheri.

  • Kama Unatumia Nguvu Kubwa Kujitambulisha…

    Kama unatumia nguvu kubwa  kujitambulisha jua bado unapaswa kuweka nguvu kubwa kwenye kufanya kazi kwa bidii pia.

    Unajua kwa nini? Kwa sababu watu hawakujui.

    Pata picha Sasa hivi umepigiwa simu na
    Samia Suluhu Hassan
    Vile tu akijitambulisha kwako, hutahitaji KUANZA KUMWULIZA maswali mawili au matatu. Utakachofanya utaanza kumsikiliza anataka kusemaje?

    Lakinj he, vipi wewe kwa upande wako. Ukimpigia mtu mgeni ambaye hana namba Yako inakuwaje? Atakufahanu? Atasema ndio nakufahamu .. na KUANZA kukusikiliza unasemaje au utaanza kujitambukisha Mara tatu, tatu.

    Ukiona unatumia nguvu kubwa kujitambulisha, basi jua kazi unayo.
    Bado unapaswa kufanya kazi kwa bidii. Tena kwa bidii sana.

    Sasa kazi yako ya leo. Chukua namba kumi ngeni ambazo hujawahi kuzipigia. Watu ambao hawakujui.
    Wapigie simu.
    Je, unajitambulisha kilaini? Wanaelewa jina lako? Je, ulipowaambia bidhaa yako wameitambua haraka? Unaweza kufanya hivyo kwa watu wengine 100 nao wakakutambua wewe na bidhaa yako mapema.

    Kama siyo kaongeze bidii kwenye kazi.

    Imeandikwa na
    Godius Rweyongeza
    www.songambele.co.tz
    0755848391
    Morogoro-Tz

  • Tofauti Kati ya wale wanaofanya makubwa na wale wanaofanya vitu vya kawaida

    Kwenye kitabu cha 10X Rule Grant Cardone,  anasema kwamba tofauti pekee Kati ya wale watu wanaofanya makubwa na wale wanaofanya mambo ya kawaida imelala kwwnye  kanuni ya mara kumi zaidi.

    Kadiri ya kanuni hii Ni kwamba kama unataka kupata matokeo makubwa zaidi ya unavyopata sasa hivi, sharti uwe tayari kufanya vitu mara kumi zaidi ya unavyofanya sasa hivi.

    Unapaswa KUANZA kwa kuweka malengo MAKUBWA mara kumi zaidi.
    Unapaswa kuchukua hatua mara kumi zaidi.
    Unapaswa kwenda hatua ya ziada mara kumi zaidi.
    Kiufupi kwenye maisha yako unapaswa kuwa MTU wa mara kumi zaidi ili uweze kupata Yale unayotaka.

    Hivyo ndivyo unapaswa kuishi kwenye maisha yako.

    Unaweza usinielewe vizuri sana ninapokwambia kanuni ya mara kumi zaidi. Ila ngoja nikueleweshe kwa undani ZAIDI. Tuchukulie wewe ni mwanachuo. Unasoma chuo AA

    Na kuna notsi ambazo profesa alitoa Ila Sasa kwa bahati mbaya hizo notes umezipoteza.
    Ila unajua marafiki zako wanazo. Ila kwa bahati mbaya, unazihitaji hizi notes SAA tano usiku na marafiki zako wamelalala tayari. Sasa inafanyaje?

    Unaweza kuamua kumtumia Innocent ujumbe ili akutumie hizo notes halafu ukatulia. Japo utakuwa umefanya uamuzi mzuri wa kuomba notsi kwa Innocent. Ila inawezekana Innocent asiingie hewani usiku huo au hata akawa mbali na simu. Au akaona ujumbe wako Ila akaaanza kufanya Mambo mengine mpaka akasahau kukutumia notsi.
    Au hata akaona ujumbe wako Ila akawa Hana kifurushi Cha kukutumia hizo notsi.

    Hivyo, kama upo makini utatumia kanuni ya Mara kumi zaidi kuomba notsi.
    Utatuma kwa ujumbe wa kuomba notsi hizo kwa
    Innocent
    Janet
    Jeni
    Said
    Abdallah
    Joseph
    Ashura
    ……..yaani, kiufupi utatuma kwa watu wasiopungua kumi.

    Nakuhakikishia siyo wote watakujibu kwa wakati.
    Siyo wote watakutumia hizi notsi
    Na wengine wanaweza hata wasiwe nazo Kama wewe.
    Wengine watakuwa wanazitafuta Kama wewe
    Na wengine wataona Ila watasahau kukutumia.
    Ila hatakosa mmoja au wawili au watatu wa kukutumia notsi zako.

    Kwa jinsi hiyo, notsi zako utakuwa umezipata.

    Sasa huu mfano unafanya kazi kwenye vitu vingine kwenye maisha. Mara zote fikiri Mara kumi zaidi.
    Chukua hatua Mara kumi zaidi.
    Piga simu kwa wateja mara kumi zaidi
    Kutana na wateja Mara kumi zaidi
    Weka LENGO la kuuza Mara kumi zaidi.
    Soma vitabu Mara kumi zaidi ya wengine
    FANYA mazoezi Mara kumi zaidi

    Hii inakuweka kwenye eneo zuri Sana kuliko MTU ambaye anakuwa anafanya vitu kwa namna ya kawaida.
    Usiwe mtu wa kawaida. FANYA kazi Mara kumi zaidi

    Kila la kheri

  • Hii Ni Sanaa Unayopaswa Kuitumia Kila Siku Kwenye Maisha Yako

    Rafiki yangu, nipe dakika moja tu nikufundishe Sanaa unayopaswa kuitumia kwenye maisha Yako kuanzia leo hii.

    Wakati tunasoma Sekondari tulikuwa tunasikia stori kuwa masomo ya sayansi yanalipa sana. Hivyo, NGUVU kubwa tukaiweka huko

    Nilipoingia chuoni, ni kozi ya horticulture. Hapa kitu Cha kwanza kabisa unachofundishwa, unaambiwa kuwa horticulture is an art and sayansi. Halafu kumbe siyo sayansi ni science kwa kiingereza. Hahaha.

    Hii maana yake ni kwamba horticulture Ni Sanaa, lakini pia ni sayansi. Hapa ndipo nilianza kuuona umuhimu wa sanaa kwenye maisha. Maisha yanahitahi vyote viwili. Maisha yanahitaji sayansi na sanaa. Na vyote viwili tunavitumia kila siku bila kujali chuo ulisoma nini nala hukusoma Nini. Iwe ulikuwa mkali Sana kwenye fizikia kama Einstein, au ilikuwa MTU wa kawaida. Bado utaihitaji Sanaa. Na hata Kama ilikuwa hupendi sayansi kiasi ulikuwa unailaani, kwenye maisha ya kila siku, unaihitaji. Hivyo, vyote viwili tunavihitaji. Na kwa Leo nataka nikufundishe Sanaa moja Itakayokusaidia wewe Kufanikisha mengi

    Na Sanaa hii siyo nyingine, bali Ni kusikiliza.

    kusikiliza ni sanaa ambayo itakufikisha mbali Sana.

    Watu wanapenda kusikilizwa aisee. Naomba kwanza nieleweke kwamba Kuna TOFAUTI kubwa Kati ya kusikia na kusikiliza.

    Unaweza kumsikia MTU  ila ukawa hujamsikiliza. Kama MTU amewahi kuongea Jambo na ukawa umemwambia arudie japo alikuwa ameongea kwa sauti. Hapo jua wazi kuwa hukumsikiliza.

    Kumsikiliza MTU kunahitaji uweke umakini wake wote kwake

    Kuna watu unakuta kwamba hawana shida Wala tatizo lolote, wao wanachohitaji kwako ni kuwasikiliza na kuwapa umakini wako. Hivyo basi rafiki yangu, ninaomba kitu kimoja kwako kuwa msikilizaji.

    Yaani, unapokuwa unaongea na MTU, NGUVU zako na Akili Yako yote iweke kwake badala ya kutawanya nguvu zako.

    Inalipa sana kusikiliza.

  • Kama Kuna Kitu Unataka Kufanya Kifanye

    Badala ya kukaa na kusubiri MTU au watu fulani waje wakusaidie kufanya na kukamilisha kitu au jambo fulani, nakushauri kwamba Kama Kuna Kitu unataka kufanya. Kifanye. Ukiendelea kumsubiri mtu au watu fulani waje wakusaidie kukifanya ukweli Ni kwamba utasubiri sana na hawa watu unaweza usije kuwaona maisha yako yote.

    Kwenye hii dunia kuna watu wa aina tatu.
    Kuna wale ambao huwa wanatamani vitu, Ila huwa hawachukui hatua na kuvifanya.

    Kuna wale ambao huwa wanaona vitu vinafanyika na kuishia kuangalia na namna vinavyofanyika

    Mwisho Ni wale wanaochukua hatua kuhakikisha kwamba wamefanyia kazi vile wanavyotamani kufanya.
    Wewe unapaswa kuwa kwenye Aina ya tatu.
    Hawa ndio wale watu ambao huwa wakiamua jambo huwa wanalifanya bila kusita.
    Hawa ndio wale watu ambao huwa wapo tayari kuweka kazi inapohitajika ili waweze kupata matokeo wanayotaka.

    Dunia imekuwa hivi ilivyo Leo hii kwa sababu ya watu wanaochukua hatua.
    Leo hii naandika makala hii kwa kutumia simu simu ambayo imetengenezwa na watu wanaochukua hatua. Leo hii napanda gari lililotengenezwa na watu wanaochukua hatua.
    Hata Kama ukisikiliza muziki jua kuwa umetengenezwa na watu wanaochukua hatua.
    Kama unapendelea kuangalia tamthiliya, jua wazi kuwa zimetengenezwa na watu wanaochukua hatua.
    Na wewe kuwa tayari kuchukua hatua.
    Hakuna namna ambavyo unaweza kupata matokeo ya tofauti kama hutachukua hatua.

    Kama Kuna kitu ungependa kufanya Leo hii, Basi uchukue hatua na uanze kukifanya rafiki yangu.

    Naomba siku ya leo tukubaliane kitu kimoja tu. Na kitu hiki Ni wewe kufanya kile unachotamani kufanya bila kurudi nyuma kuanzia leo hii.

  • Hii Ndio Njia Pekee Ya Kuhakikisha Kwamba Unapata Upendeleo Popote Pale Utakapoenda

    Hii ndio njia pekee ya kuhakikisha kwamba unapata upendeleo popote pale utakapoenda

    Sisi binadamu huwa tunapenda sana kuonekana mbele ya watu kama watu wa thamani sana. Tunataka tukikuta sehemu fulani tusianze kupanga foleni, badala yake tupite kwenye hiyo foleni na kuhudumiwa.

    Tunapenda tukiwa kazini tupandishwe vyeo.

    Tunapenda tukiwa kwenye foleni, gari letu lipishwe lipite haraka ili tuwahi kufika.

    Sasa siku ya leo nataka nikuoneshe namna ambavyo unaweza kupata upendeleo sehemu yoyote ile utakapokuwa.

    Ndio namaanisha hilo.

    Na njia hii ya kupata upendeleo ni wewe kufanya kazi kwa bidii. Rafiki kufanya kazi kwa bidii kutakufanya upendelewe sehemu yoyote ile utakapoenda. Hakuna mwajiri ambaye huwa anapenda kukaa na wafanyakazi wazembe. Ila ukifanya kazi kwa bidii, mwajiri wako atakupendelea.

    Hakuna mtu ambaye yuko makini ambaye anapenda kukaa na watu wanazembea kwenye kazi zao.

    Hivyo basi, kuanzia leo hii, uamuzi wako uwe mmoja tu, kufanya kazi kwa bidii.

    Kufanya kazi kwa bidii kunaweza kukufanya ukae meza moja na wafalme. Na kwa jinsi hiyo utakuwa umesababisha watu wakupendelee.

    Kufanya kazi kwa bidii kuutakufanya ulipwe zaidi. hivyo, kwa jinsi hiyo, utakuwa umejipendelea.

    Kumbe basi kufanya kazi kwa bidii ni kujipendelea mwenyewe. Maana kabla mtu hajaona juhudi zako na kuzipia zawadi atahitaji kuona utendaji kazi wako.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.

    Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.

    Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.

  • Jinsi Ya Kubobea Kwenye Kitu Chochote

    Rafiki yangu habari ya leo. Bila shaka unaendelea vyama, siku ya leo ningependa kukwambia njia ambayo itakusidia wewe kuweza kubobea kwenye kitu chochote ambacho unafanya, na njia hii siyo nyingine bali ni kufanya kitu husika kwa marudio na mara kwa mara.

    Yaani, kama unataka kubobea kwenye kitu chochote kile usikifanye kitu  hicho mara moja kisha ukaacha, badala yake weka nguvu na muda wako mwingi kwenye hicho kitu kwa muda mrefu mpaka kieleweke.

    Watu wengi huwa wanapenda kubobea kwenye vitu ila sasa tatizo ni kwamba huwa wanajikuta kwamba wanafanya vitu vingi sana kwa wakati mmoja. Yaani, unakuta kwamba mtu anafanya kitu fulani siku ya leo. Halafu kesho yake hicho kitu anakisahau, kesho anapambana na kitu kingine, hivyo hivyo.

    Wewe unayesoma hapa nakupa mbinu ya kubobea kwenye kitu chochote kile. Na mbinu hii ya kubobea ni wewe kufanya kitu hicho kila mara bila kuacha.

    Tatizo la watu wengi wanafanya vitu vizuri kwa mazoea

    Ninaposema kwamba ufanye kitu kila mara, simaanishi kwamba ufanye kitu hicho kwa mazoea. Kuna tofauti kati ya kufanya hicho kitu kila siku na kwa moyo na kufanya kitu hicho kila siku kwa mazoea. Kuna stori ya mfanyakazi mmoja ambaye alienda kuomba kuongezea mshahara kwa bosi wake. Baada ya kupitia maombi yake, bosi alimwambia kwamba, hawezi kuwmongezea mshahara kwa sababu  huwa anafanya kazi siku moja kwa mazoea au kwa marudio. Yaaani, kwamba huyo mfanyakazi, alikuwa kila siku anaenda kazini kweli, ila hakukuwa na kitu cha tofauti ambacho alikuwa anafanya.

    Alikuwa anaenda kazini ili kupoteza muda. Nadhani umewahi kuwasikia wale watu ambao huwa wanasema kwamba ninapoteza muda tu. Kwako haipaswi kuwa hivi, yaani, usifanye kazi au kitu chochote kile kwa ajili ya kupoteza muda tu. Mara zote na siku zote hakikisha kwamba kila siku yako inakuwa ni bora zaidi ya jana. Yaani, usiweke mazoea kwenye kazi.

    Kila dakika ambayo unafanya kazi, weka nguvu, akili yako na kila kitu humo.

    Ebu tuchukulie mfano unataka kubobea kwenye uandishi.

    Unahitaji kuhakikisha kwamba unafanya mazoezi kila siku. Yaani, unapaswa kuandika kila siku. Huwezi kukaa tu kwenye kochi huku ukiw aunategemea kwamba siku moja utakuwaj akuwa mwandishi mbobevu bila ya kuchukua hatu aya ziada. Unataka kubobea kwenye uandishi kuanzia siku ya leo? Anza kuandika.

    Au labda tuseme kwamba unataka kubobea kwenye uwekezaji, unapaswa kuhakikisha kwamba unawekeza nguvu na muda wako kwenye kujifunza uwekezaji na kufanyia kazi yale unayojifunza kwa uhalisia.

    Unataka kubobea kwenye mchezo wowote. Unapatakiwa kila siku kufanya mazoezi ya kutosha kuhusiana na mchezo husika.

    Kwa jinsi hiyo rafiki yangu, utakuwa umejiweka kwenye nafasi ya kufanya makubwa na kwenda mbali zaidi kuliko pale ambapo utakuwa hufanyii kazi haya utakayojifunza.

    Kuna siku nilikuwa nasoma wasifu wa Kobe Bryant, kitu kikubwa nilichokuja kugundua kutoka kwake ni kwamba alikuwa mtu wa mazoezi na mazoezi ndiyo yalimfanya kuweza kufikia alipofikia. Nahakufanya hicho mara moja. bali alikifanya mara kwa mara mpaka akaweza kupata matokeo makubwa.

    Hivyo basi, nipende kusisitiza ujumbe muhimu kwako rafiki yangu ambaye unapenda kufika mbali. Kitu hiki kwamba kama unataka kubobea kwenye kitu chochote kile basi kuwa tayari kufanya kitu hicho mara kwa mara na marudio bila ya kuacha mpaka pale utakapopata matokeo unayotaka.

    Asante sana na nikutakie wakati mwema.

X