Home


  • Namba Zetu Za Malipo

    Namba za malipo ya vitabu:

    Namba za lipa

    TIGO PESA: 19016638 Jina ni SONGAMBELE CONSULTANTS

    M-PESA: 5564517 jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

    Namba za kawaida

    AIRTEL MONEY: 0684408755
    TIGO PESA: 0655 848 392
    M-PESA: 0745 848 395

    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    NB: Kama namba ya malipo anatumiwa mtu ambaye yuko nje ya nchi. Iandikwe Kwa kuanza na +255

    Kwa hiyo namba zinazotumwa nje ya nchi zitakuwa
    Airtel money: +255 684 408 755
    TIGO PESA: +255 655 848 392
    M-PESA: +255 745 848 395

    KOTE Jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Kama malipo yatakuwa yanafanyika kupitia benki.

    Yafanyie kupitia

    1. CRDB BANK: 0150770710200
    2. NMB BANK: 22110047274

    Kote jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

  • Wasiliana na Godius Rweyongeza Sasa

    Habari yafuatayo ni mawasiliano Unayoweza kutumia kumpata GODIUS RWEYONGEZA

    Simu: +255 (0) 684408755

    Whatsap: +255 (0) 755848391

    Email: songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu vyake wasiliana Moja kwa Moja na +255 (0) 684408755 (more…)

  • Mwaka Huu Ni Wangu Kufanya Makubwa

    Mwaka Huu Ni Wangu Kufanya Makubwa

    Kila mwanzoni mwa mwaka watu wengi huwa wanaweka malengo makubwa ya kufanyia kazi. utasikia mtu anasema kwamba mwaka huu ni mwaka wangu wa kufanya makubwa. utasikia mwingine anasema kwamba mwaka huu lazima tu nifanye makubwa. ila sasa cha kushangaza

    Unakuta kwamba siku zinakuwa zinazidi kupita kiasi kwamba inafikia hatua huyo mtu anashindwa kufanyia kazi lengo lake la mwaka.

    Kinachokwamisha watu wengi ni kwamba wengi wanaweka mipango na malengo makubwa ila wanakuwa hawachukui hatua kuhakikisha kwamba wameweza kufikia malengo na ndoto zao.

    Hivi wewe ni miongoni mwa hawa watu rafiki yangu?

    Ninachotaka kukwambia ni kwamba mafaniko makubwa huwa hatatokei mara moja tu yaani, mwishoni mwa mwaka. Badala yake ni mchakato wa vitu vidogovidogo unavyokuwa unafanya kila siku.

    Hivi vitu vidogo vidogo unavyofanya kila siku, baadaye vinaunganika na kutengeneza kitu kikubwa.

    Ebu fikiria kila siku ukiwekea utaratibu wa kufanya kitu hata kama ni kidogo, ni uhakika kuwa mpaka mwisho wa mwaka lengo lako lililokuwa kubwa utakuwa umelisogeza mbali pangine hata kulifikisha na kupita makadirio yako.

    Hiki kitu hakiwezi kukushinda.

    Kwa siku zilizobaki kumaliza mwaka huu. anza kufanya kitu hata kama ni kidogo tu kila siku kuelekea kwenye lengo lako kuu. Kila siku fanya kitu hata kama ni kimoja tu. uhakika ni kuwa baada ya mwaka utakuwa umeweza kufanya siyo hicho kitu kimoja, badala yake utakuwa umeweza kufanya makubwa.

    Haijalishi umeajiriwa

    Uko bize sana au

    Bosi wako anakubana.

    Huwezi kukosa hata dakika kumi na tano tu kwa siku za kufanya kitu cha kwako hata kama ni kidogo. rafiki yangu, endelea kuipambania ndoto yako mpaka kieleweke. Usikubali kurudi nyuma kwa namna yoyote ile.

    Bila kuongeza la ziada, naomba niishie hapo……..

    Kitu kimoja cha ziada kuhusu kitabu cha nguvu ya vitu vidogo kuelekea mafanikio makubwa.

    Najua hapa kwa vile nimeongelea kitabu unaishia hapa na kucha kusoma zaidi. hahahaha

    Unaanza kufikiria huyu jamaa hapa anaongelea pesaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa

    Enewei, hiki kitabu ni muhimu kwako rafiki yangu…..

    Ni muhimu mno.

    Kama kuna kitabu kimoja unachopaswa kusoma mwaka 2022 basi ni hiki. Sikisifii kwa sababu nimekiandika mimi bali kwa sababu waliokisoma wengine wamethibitisha hilo.

    Ebu ona maoni haya hapa chini

    Umeona ee….

    Sasa, kitabu hiki ni 20,000 tu za kitanzania au dola kumi (10) kama upo nje ya nchi.

    Utaongeza gharama kidogo za usafiri kulingana na sehemu ulipo nami nitakutumia hiki kitabu. Ninatuma popote pale duniani.

  • Njia pekee ya itakayokuhakikishia wewe kupata matokeo ya tofauti

    Siku za nyuma niliandika makala niliyoipa kichwa cha Kama Unataka Mali: Maeneo Matano Unapoweza Kupata Mali Halali…

    Kwenye makala hii nilieleza mbinu mpya za kupata Mali. Najua kwamba wengi tulisoma shairi la kama mnataka Mali mtazipata shambani, Ila sasa je, siku hizi na zama hizi tunazoishi,  bado tunapaswa kutegemea Mali kutoka shambani? Hapo ndipo nilikueleza hizo mbinu za kukuaidia kupata Mali kwenye hizi zama.

    Sasa siku ya leo nina kitu Kimoja. Leo nataka nikwambie Kuwa kama unataka kupata matokeo ya tofauti. Rafiki yangu sharti unapaswa kukubali kufanya vitu vya tofauti.

    Huwezi kuendelea kufanya vitu vilevile kila siku huku ukitegemea kupata matokeo ya tofauti.

    Matokeo ya tofauti hayapo kwenye kufanya vitu vilevile kila siku. Kama unataka kupata matokeo ya tofauti, sharti ukubali kufanya vitu vya tofauti kwanza.

    Kama unafanya kile ambacho kila mtu anafanya, utapata matokeo ambayo kila mtu anapata. Njia pekee ya wewe kupata matokeo ambayo hujawahi kupata Ni kufanya vitu ambavyo hujawahi kufanya.

    Kama umeajiriwa, unaenda kazini muda ambao kila mtu anaenda kazini na muda wa kutoka unakukuta getini. Ujue wazi kuwa hutapata matokeo ya tofauti maishani mwako. Fanya kitu Cha tofauti, wahi kazini, fanya kazi kwa bidii, chelewa kidogo kutoka, pangilia ratiba zako.

    Kama umejiajiri unafungua biashara au unaenda kazini unapotaka na kutoka unapojisikia, jua wazi kuwa hutakuja kupata matokeo ya tofauti. Sikiliza, Anza kwenda tofauti. Jitume kufanya kazi zaidi ya saa 15 kila siku. Kumbuka siyo saa 15 za kuwa macho na kuperuzi mtandaoni. Ni saa 15 za kazi siriazi.

    Rafiki yangu, popote pale ulipo. Pambana kufanya kazi kitofauti na vile ulivyozoea.

    Ukiendelea kufanya kazi kwa namna ulivyozoea nakuhakikishia kuwa hakuna MUUJIZA wowote utakaouona maishani mwako.

    Kila la kheri.

  • Endelea Kupambania Ndoto Na Lengo Lako

    Kama una lengo na ndoto kubwa ambayo unaifanyia kazi. Endelea kupambania ndoto yako na lengo lako kila siku. Usirudi nyuma kwa kuanza kujilinganisha na watu wengine.

    Sikiliza kila siku jiboreshe wewe mwenyewe.
    Jifanyie tathimini kila mara kuangalia umatoka wapi, uko waapi unaelekea wapi.

    Jisukume kila mara kufanya zaidi. Ila usijilinganishe na MTU mwingine.

    Hakuna mtu mwingine mwenye lengo na ndoto Kama zako.

    Kabisa….

    Kila mtu anapambana na hali yake…

    Kitu pekee ambacho unapaswa kuchukua kutoka kwa Watu Ni mbinu na namna ambavyo wanainuka kutoka eneo moja kwenda jingine na kusongambele.

    Ila siyo kujilinganisha nao.

    Kisa eti fulani kanunua gari Basi na wewe ukimbizane na gari

    Kisa eti fulani kajenga NYUMBA Basi na wewe ukajenge.

    Sikiliza, tulia na ndoto yako na vipaumbele.
    Ukifuata kile ambacho wengine wanafanya Hutakata uishi maisha yako kama wewe. Utaishi maisha ya kuiga tu siku zote na sehemu zote. Hakuna haja ya wewe kuiga maisha.

    Ishi maisha yako
    Jitathimini kila mara
    Fanyia kazi uliyopata kutoka kwenye tathimini yako.
    Songambele.
    Tukutane kwenye jukwaa la wanamafanikio.

  • Hiki kitu ndicho kinafanya watu wanakuchukulia poa

    Umewahi kujiuliza kwa Nini watu wengi wanakuchukulia poa.

    Kuna sababu nyingi zinaweza kuwa zinasababisha hiki ila sababu ya kuu unaweza kuwa Ni wewe umewafanya wakuchukulie poa.

    Inawezekana kuna kipindi ulitakiwa kutoa huduma fulani kwao ila hiyo huduma hukuitoa vizuri.

    Inawezekana ulijishusha viwango kwa kutaka kupata kitu fulani wakati hukupaswa kujishusha

    Na pengine inawezekana ni kwa sababu ya mtazamo  wa MTU tu. Yaani, akiaakuangalia anakuchukulia poa.

    Unachopaswa kujua ni kuwa siyo kazi yako kuanza kuwaambia watu kuwa msinichukulie poa.

    Badala yake nenda kafanye kazi. Acha matendo yako yaongee kiasi kwamba hata wale wanaokuchukulia poa waanze kuona thamani yako.

    Anza leo.
    Chukua hatua hata Kama ni ndogo kwa ajili ya kuongeza thamani yako.

    Kazi utakayofanya, ifanye kwa ubora.
    Ongeza kipato chako
    Kuwa bize na maisha yako badala ya kufuatilia maisha ya watu wengine.
    Acha kutuatilia maneno wanayosema wengine.
    Nguvu zako zote ziweke kwenye kazi.

    Kwa jinsi hii itakuwa umekataa kuchukuliwa poa kwa vitendo na siyo kwa maneno. Endelea kupambana, watakuona ukivuka ng’ambo.

  • Vitu vizuri huchukua muda

    Mfano hupandi mti wa mwembe leo naa kuvuna kesho. Hapana.
    Unachukua muda.

    Utamwagilia mbegu
    Utapalilia kuondoa majani ili mhegu iweze kuendelea kukua.

    Ila walau haitachukua siku moja wala siku mbili. Itachukua muda. Kwa miembe ya kisasa inachukua siyo chini ya miaka mitatu na nusu.

    Kwa miembe ya kawaida inachukua miaka Saba na zaidi.

    Inashangaza kuona watu wako tayari kuvumilia miaka saba kabla ya kuvuna maembe lakini hawako tayari kuvumilia miaka saba kabla ya kufikia ndoto au lengo kubwa walilojiwekea.

    Watu wapo tayari kusoma shuleni kwa miaka 16-20 au zaidi kabla ya kuanza kufurahia matunda ya elimu. Lakini hawako tayari kuvumilia miaka saba mpaka kumi kabla biashara yao haijaleta matunda makubwa.

    Hiki kitu kinapelekea watu kukimbilia fursa zisizokuwepo.
    Leo hii wakiambiwa kuna fursa ya kuweka laki moja kesho kuvuna laki mbili wanaikimbilia.

    Rafiki yangu nisikilize kwa kitu kimoja tu.
    Kwa lengo lako au ndoto yako uliyonayo. Utaweza kuifikia iwapo tu utaifanyia kazi hatua kwa hatua.

    Tumia nguvu ya vitu vidogo Kwenye kufanyia kazi ndoto zako.

    Ndiyo maana nimekuandalia mwongozo wa kitabu hiki Cha kipekee.

    NGUVU ya VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA.
    Kitabu hiki Cha kipekee kinapatikana kwa 20,000/- tu.

    Unatumiwa popote pale ulipo. Sasa cha kufanya leo hii unapaswa kufanya hivi
    Wasiliana na 0755848391 ili uweze kupata kitabu chako. Utatumiwa popote pale ulipo

  • Fanya Hiki Unapokuwa Huna Kitu

    Kama huna kitu chochote kile Cha kupoteza basi pambana. Pambania ndoto na malengo yako kila siku na kila Mara bila kurudi nyuma.

    Maana huna kitu chochote cha kupoteza.
    Huna hela
    Huna ujuzi
    Huna konekisheni

    Hivyo njia pekee ya wewe kutoboa ni Kuendelea kupambana bila ya kurudi nyuma hata kidogo.

    Ipambanie ndoto yako mpaaka uifikie.

    Nakushauri Sana usome hiki kitabu Cha NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA
    Nitakuonesha Ni kwa namna gani unaweza kuanza kidogo mpaka ikafikia hatua ukafanya makubwa.

    Karibu sana

  • Zawadi Tano Nzuri Unazoweza Kutoa Kwa Uwapendao

    Mara kwa mara huwa tunapenda Kutoa zawadi za gharama kubwa ili kuwaonesha watu Kuwa tunawapenda. Zawadi kama gari ndio zinaonekana zawadi zenye maana kubwa Sana..

    Leo hii ningependa nikuoneshe zawadi Tano Nzuri ambazo unaweza kutoa kwa watu zikawa na maana kubwa Sana. Zinaweza zisionekane za thamani machoni pa watu ila aliyepewa zawadi husika akiichukua na kuitumia. Uhakika ni kuwa hii zawadi Ina uwezo wa kumfikisha mbali sana.

    Zawadi  ya kwanza ni zawadi ya kitabu.
    Ebu jiulize kwanza, wewe umewahi kupewa zawadi ya kitabu? Umewahi kuona MTU anatoa zawadi ya kitabu?
    Umewahi kufikiri kutoa zawadi ya kitabu?

    Zawadi ya kitabu siyo zawadi maarufu sana. Kwa Nini? Kwa sababu tumeambiwa kwamba ukitaka kumficha mwafrika kitu, basi niandike kwenye kitabu.

    Ila ukimpa mtu zawadi ya kitabu unakuwa umempa hazina kubwa sana. Kwenye kitabu kuna maarifa ambayo yanaweza kusaidia kumwinua mtu huyo

    Zawadi ya pili ni zawadi ya wazo
    Wazo moja linaweza kumwinua rafiki yako au MTU yeyote kutoka sehemu alipo kwenda sehemu nyingine.

    Kwa hiyo Kama mtu akikuomba msaada Basi mpe msaada wa wazo. Nasema Kama mtu akikuomba kwa sababu, watu huwa hawathamini mawazo. Watu wanathamini Sana fedha, hivyo usijitoe ufahamu tu wa kuwa unatoa zawadi ya mawazo yako bure kwa watu ambao hawayafurahii na hawatayatumia. Ila mtu akikuomba wazo, wewe mpe.

    Mimi mwenyewe kama una wazo lolote la kuniambia unaweza kuniambia. Napokea mawazo na Kuyafanyia kazi. Ebu nipe wazo/pendelezo lako Sasa Hivi
    Baruapepe:
    godiusrweyongeza1@gmail.com
    Simu/SMS/WhatsApp 0755848391
    Nitalipokea wazo lako.

    Zawadi ya tatu ni zawadi ya kumfundishaa mtu ujuzi
    Tunaishi kwenye ulimwengu ambapo ujuzi Ni kitu muhimu sana. Ukiwa na ujuzi wako na ukautumia vizuri. Huo ujuzi utakufikisha mbali.

    Ndio maana kwenye ulimwengu wa Leo tunapaswa pia kutoa zawadi za kufundisha watu ujuzi fulani…

    Ujuzi wa kufanya kitu fulani
    Ujasiriamali
    Uwekezaji
    Uchambuzi
    Kuna aina nyingi za ujuzi.

    Kuna soft skills na hard skills. Ila ujuzi wowote ule ni ujuzi tu, Kama unaweza kumfundisha mtu ujuzi, mfundishe.

    Na hapa naomba nieleweke kwa kitu Kimoja. Ujuzi aliokuwa anahitaji babu yako kuishi kwenye kipindi chake siyo ujuzi unaouhitaji wewe leo hii. Zama za sasa zimebadilika. Zamani walihitaji kuwa na ujuzi wa kuwinda, ujuzi wa kutengeneza moto, ujuzi wa kujua viashiria vya mazingira ya hatari n.k.

    Kwenye ulimwengu wa leo hali ni tofauti. Unaweza kuwa na ujuzi ambao watu wanauchukulia poa Ila ukakuingizia kipato kikubwa sana.

    Zawadi ya nne ni zawadi ya konekisheni.
    Kama kuna mtu anafanya kitu, zawadi pekee Unayoweza kumpa ni konekiaheni ili kitu chake kiweze kujulikana zaidi. Kama mtu ana mgahawa, mpe konekisheni ya watu zaidi wa kununua kwake.
    Kama mtu ni msusi, mpe konekisheni ya watu zaidi watakaosuka kwake.

    Kiufupi Kama Kuna MTU anafanya Jambo fulani zuri. Mpe konekisheni ya watu zaidi ambao wanaweza kupata bidhaa au huduma kwake. Hii Ni Zawadi kubwa Unayoweza kutoa. Maana ukimletea mtu mteja mmoja na akamhudumia huyo mteja mmoja vizuri. Ukweli ni kwamba huyo mteja mmoja Anaenda kununua kwake Mara nyingi zaidi na ataleta wengi zaidi

    Sasa hii si zawadi nzuri na ya kipekee?

    Zawadi ya tano ni zawadi ya kuwekeza kwenye HISA
    Mpe mtu zawadi ya hisa, hatifungani au VIPANDE. Hii Ni hazina kubwa sana.

    Ukimpa mtu zawadi ya hisa unakuwa unempa umililiki wa kampuni.

    Karibu sana kwenye semina ya uwekezaji kwenye HISA. Hili ni kundi la mapokezi.

    Semina hii itafanyika kwa njia ya mtandao (online) kupitia kundi maalumu la WhatsApp.

    Kwenye semina hii utajifunza mengi kuhusu uwekezaji kwenye HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE

    Na baada ya semina utapata kitabu (Hardcopy/audiobook) Cha JINSI YA KUWEKA AKIBA NA KUANZA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE.

    Kitabu hiki utakipata bila kuongeza Gharama ya ziada.

    Gharama ya semina ni elfu ishirini na moja 21,000/- tu.

    Namba ya malipo kwa Ajili ya semina ni 0684408755 jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Karibu sana
    Ni Mimi Godius Rweyongeza
    0755848391
    Morogoro-Tz

  • Mfuatilie huyu jamaa kwa mwezi mmoja tu, wewe mwenyewe utaniambia utakachoona

    Tunaishi katika dunia ambapo watu wanapenda kufuatilia sana maisha ya watu wengine. MTU anaweza kushinda mtandaoni akifuatilia maisha ya watu mbalimbali
    Wasanii
    Wachumba fulani
    Wachungaji n.k.

    Ila Kuna jamaa mmoja ambaye umekuwa unasahau kufuatilia. Na jamaa huyu siyo mwingine bali ni wewe mwenyewe.

    Rafiki yangu, kwa kitu chochote kile unachofanya. Penda Sana kujifuatilia wewe mwenyewe zaidi ya unavyofiatilia maisha ya watu wengine.

    Jijue maisha yako kwa uzuri.
    Jua wapi unapotezea muda wako mwingi zaidi ili uweze kuwekeza muda huo kwenye vitu vya maana.
    Jua ujuzi gani hauna sasa hivi, ili uanze kuujenga.
    Jua  konekisheni ambazo hauna ili uanze kuzijenga.
    Jua afya yako ikoje, ili uiboreshe.
    Jua maarifa unayohitaji sana sasa hivi, ili uweze kuyajenga.
    Jua changamoto zinazokukabili ili uweze kuzitatua.
    Jua ulivyofanya vizuri leo ili uweze kujipongeza
    Jua ulipokosea leo ili uweze kujirekebisha.

    Ukifuatilia maisha yako na kujiwekeaa nadhiri ya kuyaboresha maisha yako kila siku. Basi ni wazi kuwa baada ya muda maisha yako yatakuwa yanazidi kuboresheka na kuwa bora zaidi na zaidi.

    Rafiki yangu, jitahidi sana kufuatilia maisha yako na ili uweze kuyaboresha na Kuyafanya kuwa bora zaidi.

  • Vitu Vitano Unavyopaswa Kutembea Navyo Kila Mahali

    Ni vitu gani huwa unaambatana Navyo kila mahali unapoenda. Je, ni simu, kitabu au Nini? Leo hii ninakuletea orodha ya vitu Vitano Unavyopaswa kuambatana Navyo kila mahali na ubora Ni kuwa havina gharama ya ziada kuvifanya

    Kujiamini. Jiamini kwenye kila kitu unachofanya. Kama unafanya kitu ambacho hakikufanyi ujiamini, basi hapo kuna mawili.
    Achana nacho usikifanye kabisa ili uweze kufanya kitu kingine kitakachokufanya ujiamini. Au Anza kujiamini kuanzia leo hii.

    Upendo wa Kazi.

    Rafiki yangu, tembea na upendo wa Kazi kila mahali. Yaani, kazi unayoifanya ifanye kwa moyo wako wote bila kijibakiza.
    Kama huwezi Kuwa na upendo kwenye Kazi yako unayofanya sasa hivi una machaguo mawili moja Ni kuachana nayo na usiifanye kabisa ili uweze kutafuta kitu ambacho unakipenda au chagua kitu ambacho unakipenda na ufanye hicho.

    Tabasamu
    Haikugharinu kitu chochote kutabasamu popote pale utakapokuwa. Kama kuna kitu ambacho unapaswa kukifanya kila marra Basi Ni kutabasamu
    Anza leo hii

    Kuwaacha wengine zaidi ya ulivyowakuta

    Jitahidi sana kila mara Unapokutana na mtu kuhakikisha kwamba unamwongezea kitu cha ziada
    Kwenye mazingira yetu tumezungukwa na wakatisha tamaa wengi. Watu ambao wanarudisha maisha ya watu nyuma zaidi.

    Sasa unaonaje na wewe badala ya Kuwa mkatisha tamaa, ukiwa MTU wa kuwapa watu matumaini. Mara zote watie watu moyo na ONGEA maneno ya kuwainua ili waweze kufanya kazi na shughuli zao kwa ubora ZAIDI ya wanavyofanya.

    Kama hujapenda kitu badala ya kumkatisha tamaa anayekifanya, toa mbinu ya kukiboresha. Ila siyo kuishia tu kulalamika.

    Kila mtu anaweweza kulalamika. Kulalamika siyo Bei kubwa, ndiyo maana kila mtu anaweza kufanya hivyo, wewe jitofautishe kwa kuachana na kulalamika.

    Maneno yako.
    Mara zote tembea na maneno chanya. ONGEA kile unachomaanisha. Maneno yanaumba. Usijitamkie maneno mabaya na Wala usiseme maneno mabaya kwa wenzako. Weka nuvu kubwa kwenye kusema maneno chanya na kuwahamisha watu wengine ili waweze kufanya kile wanavyofanya kwa ubora ZAIDI.

    Tunahitaji tutengeneze dunia ya tofauti na hii dunia hatuwezi kuitengeneza kwa Kuwa na watu ambao wanalalamikia kila kitu.

    Hivyo, Ni vitu Vitano ambavyo unapaswa kutembea mavyo kila mahali na kila siku.

    Kila la KHERI.

    Umekuwa nami,

    Godius Rweyongeza

    0755848391

    Morogoro-Tz

  • Je, bado na wewe ni mshamba wa fursa?

    Kila mara huwa wanakuja watu kwa kusema kwamba kitu fulani kinalipa ukilinganisha na kitu kingine. hiki kitu ndio kinanifanya leo hii intake kukuuliza, hivi na wewe bado ni mshamba wa fursa.

    Hkauna fursa moja ambayo unaweza kusema kwamba inalipa zaidi kuliko nyingine.

    Kila ulimwona mjomba amenunua gari kupitia fursa fulani, haimaanishi kwamba na wewe ukimbilioe huko.

    Moja ya stori ambayo imekuwa ikipagawisha watu kwenye kilimo ni stori KILIMO CHA TIKITI.

    Watu wengi wamekuwa wakikimbilia kulima tikiti kwa kujua kwamba tikiti linalipa sana. wapo ambao wamekuwa wanafanikiwa kwa viwango vikubwa huku wengine wakiangukia pua.

    Ujumbe wangu kwako siku ya leo ukiona mtu kafanikiwa kwenye fursa fulani, badala ya kukimbilia kuiga na kufanya kama alivyofanya, jiulize maswali yafuatayo.

    Je, amekuwa akiifanyia kazi hii fursa hii kwa miaka mingapi?

    Hiki kitu kitakusaidia kujua nje ndani kuhusiana na fursa husika na hivyo kujua  muda na nguvu utakazopaswa kuweka. Wengi  wanaposikia kuhusu fursa wanadhani kuwa ni kitu ambacho utafanya kwa siku moja na kitu hicho kikaleta matokeo makubwa. wengi unaowaona wamefanikiwa kwenye fursa fulani, wamekuwa wakizifanyia kazi hizo fursa kwa miaka mingi mpaka leo hii unaona tayari wamefanikiwa. Na hiki kitu kimewafanya waijue fursa husika nje ndani, kiasi kwamba inafikia hatua wanafanya maamuzi ambayo yanawasaidia kufika kule wanapotaka.

    Ni msimu gani zao hili linafanya vizuri?

    Kama umemwona mtu amefanikiwa kwenye kilimo. Na wewe unataka kuingia kwenye kilimo. Usiingie kichwa kichwa, la sivyo utakuja kuangukia pua. Kabisaaa. Badala yake jiulize ni  msimu gani zao lipi huwa linakuwa na bei ya juu. Hili lipo karibia kwenye kila zao. Hivyo, ni muhimu kwako kutambua hiki kitu, la sivyo utaingia kwenye kilimo kichwa kichwa halafu utaangukia pua.

X