Home


  • Namba Zetu Za Malipo

    Namba za malipo ya vitabu:

    Namba za lipa

    TIGO PESA: 19016638 Jina ni SONGAMBELE CONSULTANTS

    M-PESA: 5564517 jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

    Namba za kawaida

    AIRTEL MONEY: 0684408755
    TIGO PESA: 0655 848 392
    M-PESA: 0745 848 395

    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    NB: Kama namba ya malipo anatumiwa mtu ambaye yuko nje ya nchi. Iandikwe Kwa kuanza na +255

    Kwa hiyo namba zinazotumwa nje ya nchi zitakuwa
    Airtel money: +255 684 408 755
    TIGO PESA: +255 655 848 392
    M-PESA: +255 745 848 395

    KOTE Jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Kama malipo yatakuwa yanafanyika kupitia benki.

    Yafanyie kupitia

    1. CRDB BANK: 0150770710200
    2. NMB BANK: 22110047274

    Kote jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

  • Wasiliana na Godius Rweyongeza Sasa

    Habari yafuatayo ni mawasiliano Unayoweza kutumia kumpata GODIUS RWEYONGEZA

    Simu: +255 (0) 684408755

    Whatsap: +255 (0) 755848391

    Email: songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu vyake wasiliana Moja kwa Moja na +255 (0) 684408755 (more…)

  • Maswali Unayopaswa kuwauliza watu waliofanikiwa

    Ukikutana na mtu ambaye amefanikiwa, usitoke bure kwake. Kuwa mdadisi ili uweze kujua ni kitu gani ambacho kimeweza kumpa mafanikio makubwa.

    Yafutayo ni maswali ambayo unapaswa kuwauliza watu waliofanikiwa?

    1. Imekuwaje umefanikiwa wakati wengine huona siyo rahisi kufanikiwa maishani?

    2. Unawezaje kuendesha miradi mikubwa wakati mimi nahangaika na miradi midogo?

    3. Nini siri ya mafanikio yako?

    4. Ni kitu gani kinakupa hamasa ya kuendelea zaidi?

    5. Ulianza anzaje? Je, tangu unaanza maisha ulikuwa hivi?

    6. Una mipango gani miaka 10 ijayo?

    Usichoke kuuliza maswali. Kila unapokutana na mtu aliyefanikiwa jua kuwa kuna vitu vingi vya kujifunza kutoka kwake. Hivyo basi, kuwa tayari kumuuliza, kitu ambacho kimeweza kumfanya afanikiwe.

    Hiki Kitu kitakupa nguvu zaidi wewe na kukufanya usonge mbele zaidi.

    Kwanza, utaona kwamba mafanikio siyo kitu cha watu wachache. Na wewe pia unaweza kufanikiwa.

    Lakini pia utaona kwamba na wewe ndoto zako zinawezekana. Kama huyu kaweza na mimi nitaweza.

    Tatu, utaona kuwa unaweza kuanzia popote ulipo na bado ukatoboa kwenye maisha.

    Nne, utapata ule mtazamo halisi wa kimafanikio kutoka kwa mtu aliyefanikiwa.

    Mimi nakutakia kila la kheri.

    1.KUMBUKA kwamba mafanikio ni haki yako ila tofauti na haki nyingine. Mafanikio hayadaiwi mahakamani. Unapaswa kupambana kuhakikisha kwamba unayapata.

    2. Ukitaka kupata matokeo yasiyo ya kawaida, sharti ukubali kufanya vitu ambavyo siyo vya kawaida.

    3. Ukitaka kupata matokeo ambayo hujawahi kupata, sharti ukubali kufanya vitu ambavyo hujawahi kufanya.

    Kila la kheri.
    Godius Rweyongeza
    0755848391
    Morogoro-Tz

  • Je, kizazi kijacho cha Mabilionea wa Afrika kitatokea wapi?

    Takwimu zilizotolewa na gazeti la Forbes ni kwamba karibia bilionea mmoja anatengenezwa kila baada ya dakika moja. Hii Ndio kusema kwamba fursa za kutengeneza mabilionea zaidi zinazidi kuongezeka.

    Nafasi ya wewe kutengeneza ubilionea pia ipo, lakini endapo tu utaifahamu na kuiishi misingi na kanuni za kibilionea.

    Sababu Tano Kwa Nini Afrika Ndiyo Eneo Pekee Unapoweza Kutengeneza Mabilioni ya Fedha Zaidi Ya Eneo Jingine Hapa Duniani

    Kwa leo ninataka nikuelekeze eneo ambapo mabilionea wajao wa Afrika watatokea. Yapo maeneo 11 kama ambavyo nimeyaeleza kwenye kitabu Cha SEKTA 11 ZA KUTENGENEZA MAMILIONI YA FEDHA TANZANIA ila kwa Leo na kwa ufupi sana nataka nizungumzie eneo moja tu.

    Kilimo. Afrika imebarikiwa kuwa na ardhi nzuri yenye kilimo.

    Idadi ya watu Afrika inazidi kuongezeka kila siku. Na watu hawa wanahitaji kula.

    Mambo mengine yanaweza kubadilika ila kula kutabaki palepale. Pengine MATUMIZI ya mtandao wa intaneti yanaweza kubadilika ila hatutaacha kula.

    Idadi ya watu duniani kwa ujumla pia inazidi kuongezeka na ongezeko hili linahitaji chakula pia.

    Kwa misingi hiyo basi, sisiti kusema kwamba kilimo ni mojawapo ya eneo ambalo linaenda kutengeneza mabilionea wapya Afrika. Kwenye ebook ya SEKTA 11 ZA KUTENGENEZA MAMILIONI YA FEDHA TANZANIA nimeeleza kwa kina hili.

    Ila kwa hapa itoshe tu kusema kuwa kilimo Ni SEKTA muhimu sana ya kuangalia kwa jicho la pili.

    Ndio maana mimi nimeshaanza harakati zangu za kuhakikisha kwamba natengeneza mabilioni yangu huku.

    Mfano mzuri tu hapa Tanzania. Kuna mazingira yanayoruhusu kuzalisha karibia kila zao. Lakini cha ajabu ni kuwa unaweza kwenda supermarket na kukuta kuna mazao ya nje ya nchi yanauzwa.

    Wewe kama kijana unaweza kuchagua baadhi ya mazao na kukomaa nayo, ukayazalisha kwa viwango vizuri kiasi cha kuweza hata kusafirisha nje ya nchi.

    Hivyo, ukaliteka soko la ndani na nje ya nchi. Upo tayari kwa ajili ya hii safari.MAFUNZO ZAIDI

  • Kama Bado Hujapata Nafasi Ya Kushiriki Darasa La Uandishi Kwa Mwaka 2022 Chukua Hatua Sasa Hivi

    Tunategemea kuwa na darasa rasmi la uandishi kwa mwaka 2022. Darasa hili la kipekee litaanza rasmi tarehe 16 machi.

    Kama ulikuwa huna habari basi taarifa rasmi  ilitolewa HAPA HAPA na BAADAYE ikatolewa hapa.

    Idadi ya watu ambao watashiriki kwenye darasa hili hapa la kipekee Ni kumi tu, na nafasi zinazidi kupungua kila kukicha. Hivyo, kama hujachukua hatua ya kujiunga, fanya hivyo leo.

    Kuna kitu gani cha kipekee kwenye hii semina?

    Kozi hii ni ya waandishi, siyo wale wanaojiita waandishi, ila waandishi wanaoandika, hicho ndiyo kitu Kikubwa tunachopambana nacho kwenye hii kozi. Hata kama hujawahi kuandika,

    Mpaka kozi inafikia mwishoni utakuwa tayari umeshaandika, siyo mara moja, siyo mara mbili, ila utakuwa umeandika kiasi cha kuweza kumaliza kitabu chako.

    Hiki ni kitu siyo tu ambacho nakwambia kwa nadharia, ila ni kitu ambacho watu wengine wamekifanyia kazi kwa mafanikio makubwa, Nina uhakika kama upo siriazi pia utaweza kukifanyia kazi.

    Sasa kama kuna watu wametumia mbinu hizi ninazofundisha kuandika na kukamilisha vitabu vyao, unadhani wewe utashindwa?

    Kozi imeandaliwa katika mfumo wa kukufanya uandike na ukamilishe lengo lako ndani ya muda wa kozi. Ukijiunga na kozi tutawasiliana na kuweka mpango. Utaweza kuandika hata kama hujawahi kuandika.

    Hivyo kwa mara ya kwanza baada ya kuhudhuria kozi hii utakuwa mwandishi. Yale masuala ya kujiita mwandishi mtandaoni wakati hata hujawahi kuandika kwishney.

    Kozi hii ina mwongozo uliokamilika na ina kila kitu unachohitaji kujua kuhusu uandishi.

    Mbali na hilo kwenye kozi hii:

    👉Utaandika kitabu chako na kitakamilika ndani ya siku 30.

    👉 Nitakusimamia na kusoma kazi zako unazoandika kila siku na kukusaidia kuziboresha.

    👉 Nitakufungulia blogu ya bure.

    👉 Utajifunza mengi kutokana na yale wanayoandika wenzako na maoni nitakayokuwa natoa kuhusu kazi za wenzako.

    👉 Utapata kitabu Cha JINSI YA KUWA MWANDISHI MBOBEVU NDANI YA SIKU 30 bure.

    👉 Utapata jarida lenye hatua 15 za kufuata ili kuandika magazetini.

    👉 Utapata mafunzo ya audio zaidi ya 10. Yakiwemo mahojiano na waandishi wakubwa hapa nchini.

    👉 Utaungana na waandishi wengine wanaoandika na kujifunza mengi kutoka kwao.

    Nafasi kwenye kozi hii ni 10 tu. Hivyo, kama unataka kuhudhuria kozi hii, sharti uwahi kujihakikishia nafasi yako kabla hazijaisha.

    Na gharama za kuhudhuria darasa hili la kipekee itakuwa ni laki mbili (200,000/) tu. Jihakikishie nafasi yako Sasa hivi kwa kuwasiliana na 0755848391 kabla nafasi hazijaisha.

    NAKUKUMBUSHA TU: kozi hii ni ya siku 30 tu, na huna kitu chochote cha kupoteza. Endapo utajiunga na kozi hii ila katikati mwa kozi au mwishoni ukaona kuwa haifai, utanipigia simu nami nitakurejeshea fedha yako bila kukuuliza maswali yoyote.

    Hivyo, jisajili sasa hivi kwa kuwasiliana na 0755848391.

    Nafasi zimebaki chache.

  • Umuhimu Wa KUWEKEZA Kwenye Hisa

    Kwa Tanzania kumekuwepo na hiki Kitu kinaitwa Vicoba na michezo. Wengi wamekuwa wanaweka fedha zao kwenye hii michezo, ambapo muda mwingine wanalizwa kwa kutopewa fedha zao.

    Na muda mwingine wanaweka fedha kwa pamoja BAADAYE zinaibiwa na mtu mmoja, wahusika walio wengi wanaishia kulia. Nadhani huku ni kuangamia kwa kukosa maarifa. 

    Kuelewa a kuhusu hisa na HATIFUNGANI unaweza kuanza na e-book ya MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE kwa elfu 5 tu.

    Hivi wewe ushawahi kusikia kitu kinachoitwa hisa?

    Hivi umewahi kujiuliza kwa nini unapaswa KUWEKEZA KWENYE HISA HATIFUNGANI au VIPANDE? Zina faida gani hizi hisa?

    Kuna faida nyingi za KUWEKEZA kwenye HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE.

    Kwa keo nimeona nikukaribishe uweze kumsikiliza Ezden Jumanne akizungumzia umuhimu wa KUWEKEZA KWENYE HISA HATIFUNGANI NA VIPANDE.

    Video hii hapa.

    VIDEO: UMUHIMU WA KUWEKEZA KWENYE HISA

    Kupata e-book ya MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA HATIFUNGANI NA VIPANDE basi lipa elfu 5 kwa 0684 408 755 jina ni GODIUS RWEYONGEZA ili uipate.

    SOMA ZAIDI: Ninawezaje kununua hisa na ninatakiwa kuwa na shilingi ngapi?

    Inawezekana Wewe Kuwa Mwekezaji

    Umekuwa nami
    Godius Rweyongeza
    0755848391
    Morogoro-Tz

    Baada ya hapo nitakutumia ebook hii kwa WhatsApp au telegram au kwa baruapepe.

  • Kama Unataka Kubadili Dunia Fanya Haya Hapa

    Unaendeleaje rafiki yangu

    Nimekutana na watu wengi wanaopenda kubadili dunia. Hata hivyo, cha kushangaza wamekuwa hawachukui hatua.

    siku leo, nimeona siyo vibaya, ngoja nikuandalie kitu kuhusu mabadiliko, kama unataka kubadili dunia fuatilia haya mafunzo.

    1. Kama unataka kubadili dunia, tandika kitanda chako vizuri.(KITABU)

    Huu ni uchambuzi wa kitabu cha Make Your Bed kilichoandikwa na William H. McRaven

    Huyu alikuwa mwanajeshi wa jeshi la majini la Marekani. Siku moja alialikwa  kwenye chuo kutoa hotuba siku ya mahafali.

    Pale chuoni akawa ametoa hotuba inayojulikana kama “tandika kitanda chako”. kama unataka kubadili dunia, fanya haya mambo..

    Kwenye hiyo hotuba alieleza Mambo 10 . Baadaye hiyo hotuba yake tu ilikuwa maarufu kiasi kwamba akaamua kuandika kitabu.

    Kwenye chambuzi huu utakutana na haya mambo 10 yakiwa yameelezwa
    BONYEZA HAPA kuiona.

    uchambuzi wa kitabu Cha make your bed

    2. Kama unataka kubadili dunia ifahamu NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA (kitabu)

    Hiki ni kitabu ambacho nipo nashughulika nacho nyuma ya pazia kwa sasa. Ila tayari nimeandika makala kadha wa kadha kwenye blogu hii
    Ebu zisome hapa

    1. NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA
    2. Jinsi Vitu Vidogo Vinavyoweza Kukupa Vikubwa (Mfano Kutoka KWENYE Biblia) Sehemu ya kwanza
    3. Vitu Nane (08) Vidogo Ambavyo Unaweza Kuanza Kufanya Leo, Vikaongeza Thamani Yako Na Ya Watu Wengine

    Leo niliona nukupe mwongozo wa kukusaidia kufanya makubwa na hata kubadili dunia.

    Kupata vitabu Vyangu BONYEZA HAPA

  • Je, Viwanja Vya Zama Hizi Vimehamia Mtandaoni

    Leo nimeona nifunguke mambo ya muhimu sana baada ya kuona kwamba dunia inazidi kubadilika kwa Kasi sana wakati Watanzania wenzangu wakiwa wanaendelea kuishi kama vile hakuna kinachotokea.

    Zamani ilikuwa kwamba mtu akiwa na mashamba makubwa au viwanja basi alikuwa anahesabika kuwa ana utajiri mkubwa sana. ila siku hizi hali inaonekana kama imebadilika.

    Nadhani wewe mwenyewe unaweza kujionea mwenyewe.

    Kwenye orodha ya matajiri wakubwa duniani, matajiri wangapi wanamiliki viwanja au majumba.  Ebu kwa mfano tuchukue ile kumi bora ya matajiri duniani, ni wangapi wanamiliki viwanja au majumba.

    Utagundua kwamba wengi wanamiliki biashara za mtandaoni/intaneti.

    Orodha ya matajiri wakubwa duniani kwa sasa

    Hapa siyo kwamba nataka kusema biashara ya uwekezaji kwenye majengo siyo muhimu. Ila pia nataka hiki kitu ukiangalie kwa jicho la pili. Kama bado hujaweka biashara yako mtandaoni,basi ni muda wako wa kufanya hivyo.

    Biashara ambazo zilikuwa zinafanya vizuri kabla ya intaneti, zilifanya vibaya pale  ziliposhindwa kuhamia mtandaoni. Mfano mzuri ni  kampuni ya Walmart.

    Kuna watu hata hawaijui Walmart ila wanaijua AMAZON. Ujue Amazon ni kampuni ya juzi juzi ila Walmart walikuwepo kabla ya Amazon.

    Kitu wanachofanya Amazon leo hii, kilishafanywa na Walmart kwa zaidi ya miaka 30 wakati Amazon inaanza. Kama ulikuwa hujui ni kwamba Amazon ilianzishwa mwaka 1994 wakati Warmart ilianzishwa mwaka 1962.

    Kwa kipindi hicho chote sisiti kusema kwamba tayari Walmart walikuwa na uzoefu mkubwa kwenye biashara kuliko Amazon wakati amazon inaanza. Sisiti kusema kwamba Walmart walikuwa na rasilimali za kutosha na hata ushawishi mkubwa.

    SOMA ZAIDI: ZAMA ZIMEBADILIKA

    Kuna kitu gani sasa kilichotokea?

    Walichofanya Amazon ni kudandia teknolojia; wakati Walmart wakiendelea kushikilia njia za zamani Amazoni wakakimbilia mtandaoni. Na huo ndio ulikuwa mwanzo wa Daudi kumpiga Goliath.

    Unaifahamu stori ya Daudi na Goliath wewe? Niache kwanza niendelee…

    Na hiki ndicho nakiona kwa wabongo na waafrika wengi.  Wanaendelea kushikilia ile dhana kwamba zamani mambo yalikuwa yanafanyika hivi wakati mambo yameshabadilika. Shauri yako.

    Leo nataka usanuke na uhamishie biashara yako mtandaoni.

    Kwa kukusadia nitaongelea mambo matatu yatayokuwa ya msaada kwako.

    Mosi, fungua blogu au tovuti

    Pili, andikisha biashara yako kwenye Google my business

    Tatu, Tengeneza kurasa za Facebook Instagram na Twitter

    Haya Sasa tuone maelekezo ya kila kimoja, lakini kwanza hakikisha umejipatia nakala ya kitabu cha bure hapo chini kishauendelee

    Fungua Blogu Au Tovuti.

    Hapa hakikisha kwamba umefungua blogu au tovuti. Na hili nalisema kwa aina yoyote ile ya biashara, kipaji au shughuli unayofanya. Kwa biashara yoyote ile uliyonacho hakikisha kwamba umefungua blogu na kwenye hiyo blogu, hakikisha kwamba kuna mawasiliano yako na taarifa zote za muhimu inazohusiana na kile unachofanya.

    Na hakikisha kwamba, unaweka taarifa za mara kwa mara kwenye blogu yako ambazo zitawafanya watu wawe wanakuja kuitembelea mara kwa mara.

    Blogu na tovuti zimekuwepo kwa muda mrefu na umaarufu wake hauishi, ukilinganisha na mitandao mingine ya kijamii. Mitandao ya kijamii huwa inakuja na kupoteza umaarufu wake ila blogu, zinabaki na umaarufu wake kila wakati. hivyo, zitumie vyema blogu

    Hili litakusaidia wewe pale watu watakapokuwa wanatafuta taarifa, uweze kuonekana na hivyo kuiunganisha biashara au kipaji chako na watu wenye uhitaji nayo. Sijui hapo umenielewa au nirudie tena

    Unachopaswa kufahamu ni kuwa siku hizi mtu akihitaji kitu sehemu ya kwanza kabisa anapokimblia ni mtandaoni ili kuktafuta hicho kitu. Sasa kama wewe umeweka hicho kwenye mtandao, itakuwa rahisi kwa watu kukutafuta na kukupata. Na eneo la kwanza kwako kuanzia ni kwenye blogu au tovuti.

    Kwa wale mtakaojiandisha na darasa maalumu la uandishi kwa mwaka huu, nitawafungulia blogu bure kabisa. kwa maelezo zaidi SOMA HAPA

    SOMA ZAIDI: Ninahitaji watu 10 Nami nitawafanya kuwa waandishi wabobevu ndani ya siku 30

    Fungua ukurasa wa GOOGLE MYA BUSINESS

    Eneo la pili la kuweka biashara au kipaji chako ni GOOGLE MY BUSINESS. Huu ni ukurasa ambao unautengenza bure kabisa. ukiwa na GMAIL Unaweza kutengeneza ukurasa huu na kuorodhesha kipaji chako huko kama biashara.

    Google huwa wanaonesha vitu mtandaoni kulingana na umuhimu wake, lakini pia eneo ulipo. Unapoweka kipaji au biashara yako kwenye google my business maana yake, watu watakapokuwa wanatafuta kitu kinachoendana na kile unachofanya, wewe utapewa kipaumbele.

    Google my business inaitwa local business directory, yaani inawasaidia kuonesha watu taarifa kwenye maneo yaliyo karibu yao. Kwa hiyo badala ya watu wahangaike kwenda sehemu ya mbali kumtafuta mbunifu wa nguo kama wewe, ukiwa umeweka kipaji au biashara yako huko, wataanza kukuona wewe.

    Na wakikuona wewe watakutafuta ili uwasaidie kwenye kuwatengenezea magauni safi ya pasaka! Sijui unanielewa hapo!

    Kwa hiyo cha kufanya sasa hivi, pakua app ya google my business, kisha orodhesha kipaji chako huko kama biashara. NI BURE

    Sasa kila kitu kipo wazi. Ushindwe wewe tu.

    Siku nyingine nitaandaa video inayoonesha nammna ya kujiandikisha google  my business. Ili usipitwe na hili hakikisha umejiunga na mfumo wetu wa kupokea makala kwa njia ya barua pepe. Jiunge sasa hivi kwa kujaza taarifa zako hapo chini.

    Mitandao Ya Kijamii

    Najua wengi watakwambia fungua ukurasa wa facebook, twitter au instagram, ila kama ulivyoona, mimi kwangu kurasa za mitandao ya kijamii siyo nambari moja wala nambari mbili. bali zinakuja kwenye nafasi ya tatu. Na hapa siwezi kukwambia kwamba fungua ukurasa wa facebook au instagram, badala yake ninchoshauri uchague eneo kulingana na kipaji chako kilivyo.

    Instgaram ni mtandao ambao unaendana na picha. Hivyo ukiamua kuwa instagram hakikisha kwamba utakuwa mtu wa kutupia picha mara kwa mara.

    Twitter ni mtandao ambao unahitaji ujieleze kwa maneno kidogo tu.

    Facebokk picha na maneno vyote vinaenda tu. sasa wewe chagua wapi panakufaa zaidi kulingana kipaji ulichonacho.

    Kama wewe kipaji chako ni kinahusisha kurekodi video unaweza kufikiria kuhusu kutengeneza akaunti ya youtube.

    Kama wewe unarekodi mafunzo kwa njia ya audio unaweza kuchagua platform za audio kama anchor, spotfy na nyinginezo.

    SOMA ZAIDI: Faida Za Kuwa Na Blogu Ambazo Hakuna Mtu Amewahi Kukwambia

    umekuwa nami GODIUS RWEYONGEZA

    0755848391

    [block rendering halted]

  • Kwa Nini Mpaka Sasa hivi huanzishi biashara yako?

    Ngoja kwanza! Si ulisema mwaka 2020 kwamba utaanzisha biashara? Ilikuwaje? Nakumbuka mwaka 2021 ulisema ndio mwaka wako wa kufanya makubwa! Uliishia wapi? Mbona hilo wazo lako la kuanzisha biashara unarudia kulisema kila mwaka huku ukiwa huchukui hatua?

    Siku ya leo nataka nikudadavulie vitu vinavyokuzuia wewe kuanzisha biashara yako mwaka hadi mwaka na hatua unazoweza kuchukua.

    MOJA: MSHAHARA

    Mshahara unaondelea kuupokea kila mwezi unaona kwamba utaendelea kuwepo mwaka hadi mwaka, hivyo huoni haja ya kuanzisha biashara au chanzo kingine cha kipato.

    Ninachotaka ufahamu ni kwamba, mambo yanabadilika kila siku. Ajira yako ya leo, inaweza isiwepo kesho. Hivyo basi ni muhimu sana uanzishe biashara.
    Kuna sababu nyingi kwa nini unapaswa kuanzisha biashara, mojawapo ikiwa ni pamoja ni kujitengenezea uhuru wako mwenyewe.

    Na uhuru huu unaweza kuupata zaidi kwenye biashara yako utakayoanzisha.

    SOMA ZAIDI: USHAURI: Jinsi ya kuanzisha Biashara Ukiwa Umeajiriwa Bila Bosi Wako Kujua

    PILI: UOGA

    Najua, umekuwa unaogopa kwa muda sasa, hivi nikianzisha biashara, itakuwaje?

    Ninachotaka ufahamu ni kuwa watu ambao wewe unawaogopa, wao pia kuna vitu vyao wanaogopa na pengine wanakuogopa wewe. Usikwamishe ndoto zako kwa sababu ya watu waliokuzunguka au hofu ya watu.

    TATU: HUTAKI KULIPA GHARAMA

    Biashara siyo kitu cha mchezo mchezo. Ukianzisha biashara kuna vitu ulikuwa unafanya, utapaswa kuachana navyo na kuna vitu ulikuwa hufanyi utapaswa kufanya.
    Ulikuwa husomi wala kujifunza utapaswa kuanza kusoma na kujifunza.
    Ulikuwa hutaki kuongea na watu, utapaswa kuwapigia wateja na kuongea nao vizuri ili waweze kuja kwako kununua zaidi.

    Kuwa tayari kulipa gharama maana mtaka cha uvunguni sharti ainame. Ukitaka kula vinono, sharti ukubali kulipa gharama kwanza.

    NNE: UNASUBIRI MPAKA UWE NA MTAJI WA KUTOSHA.

    Yaani, nadhani hiki ndicho kilipaswa kuwa kigezo nambari kwako.

    Kila siku na kila mwaka unaendelea kusema kwamba unazichanga, sijui utaendelea kuzichanga mpaka lini.

    Unasubiri mpaka uwe na mtaji wa milioni 200 ndio uanzishe biashara si ndio?

    Kwa nini usianze sasa hivi kwa kutumia huo mtaji ulio nao. Una mitaji mingi sana imekuzunguka, unaijua?

    Ebu rusha elfu mbili tu leo, nikurushie ebook inayozungumzia MITAJI 8 ILIYOKUZUNGUKA NA JINSI YA KUITUMIA.

    Changamka sasa rusha kwa 0684 408 755 jina ni GODIUS RWEYONGEZA. Hii ni bei ya ofa

    TANO: UNAOGOPA KUSHINDWA

    Najua kuwa ukianzisha biashara, lazima tu watu wengi watajua kuwa umeanzisha biashara.

    Na hasa watu wako wa karibu. Ndugu, jamaa na marafiki. Sasa unachoogopa ni endapo biashara ikifeli itakuwaje?

    Si unajua huwa hatupendi kuonekana tumeshindwa, badala yake tunapenda kuonekana tunashinda kwa kila kitu?

    Ninachotaka nikwambie ni kuwa japo biashara haina guarantee kuwa itafanikiwa kwa asilimia 💯. Ila utajifunza sana kwenye kuanzisha na kukuza biashara kuliko unavyoweza kujifunza sehemu yoyote.

    Hata biashara ikifeli, bado somo utakaloondoka nalo hapo ni kubwa kuliko unavyoweza kufikiri.

    Hata hivyo, kufeli ni sehemu ya maisha.  Nyuma ya ushindi wowote ule Kuna kushindwa, kushindwa, kushindwa. Usiogope SONGAMBELE

    Tulipokuwa wadogo, tulijaribu vitu vingi sana na kufeli kwenye vitu vingi pia. mfano kwenye kutembea tu, mtoto anajaribu mara nyingi sana kutembea huku akianguka na kuinuka.

    Hakuna mtu ambaye huwa anamcheka mtoto kwa sababu eti anaanguka. ila sote huwa tunajua kwamba kadiri anavyoanguka ndivyo anakuwa anakaribia kwenye ushindi. kwa hiyo kuanguka kwako, ni sehemu tu ya kuelekea kwenye ushindi.

    Kupata kitabu hiki wasiliana na 0755848391 sasa

    SITA: UMEZUNGUKWA NA WATU WENGI AMBAO HAWANA MTAZAMO WA KIBIASHARA

    Ukizungukwa na watu ambao hawana mtazamo wa kibiashara, hata kama unapenda biashara kiasi gani, usitegemee kuanzisha biashara.

    Watakukatisha tamaa na wataongea vitu ambavyo mwisho wa siku vitakufanya ushindwe kwenda hatua ya ziada na kuanzisha biashara.

    Kama unataka kuanzisha biashara, ungana na timu ya watu sahihi.

    SABA: KUNA WATU UNAWATEGEMEA

    Una wazazi, mjomba au ndugu unayemtegemea akupe kila kitu. Hivyo, unadhani kila kitu kitaendelea kuwa hivyo maisha yako yote.

    Unadhani, ataendelea kukulipia bili ya umeme na wewe unachaji simu yako tu ili uchati.

    Unadhani ataendelea kukupa chumba cha kulala maisha yako yote, milele na milele, Amina.

    Funguka. Itumie hiyo kama fursa, kwa kuwa una mtu ambaye anaweza kukusaidia basi tayari una sehemu ya kusimamia.

    Kuna watu wanakutamani ila wewe hujui tu. Wengi wanatamani wangekuwa kama wewe, shauri yako!

    NANE: UNADHANI UMEZEEKA SANA AU BADO KIJANA SANA

    Kitu kingine unafikiri labda umri wako bado sana kiasi kwamba huwezi kuanzisha biashara, na pengine labda unadhani kuwa umri wako umeenda sana.

    Nakumbuka niliwahi kuongea na kijana wa miaka 35 tu, akawa ananiambia umri wake umeshaenda, hawezi tena kufanikiwa.

    Kama wewe unadhani umri wako bado sana unakosea . Unapaswa kuanza ukiwa bado na nguvu kama kijana.

    Vipi ukiambiwa Warren Buffet alianza kuwekeza akiwa na umri wa miaka 11? Na bado leo hii anasema kwamba anaona alichelewa kuanza. Siyo kwamba muda wako bado, Anza sasa hivi.

    Kama unadhani umri wako umepita. Unakosea pia. Vipi ukiambiwa aliyeanzisha KFC aliianzisha baada ya kustaafu?

    Siyo kwamba muda umeenda; muda mzuri wa kupanda mti ulikuwa miaka 20 iliyopita muda mzuri zaidi wa kupanda miti ni sasa.

    Pichani ni Cornel Sanders aliyeanzisha mgahawa wa KFC akiwa na umri wa miaka 65

    TISA: MAJUKUMU YA SASA YANAKUBANA

    Unasema kwamba majukumu ya sasa yanakubanabsana kiasi huwezi kuanzisha biashara. Na ni ukweli kuwa biashara inahitaji muda pia.

    Wewe kwa upande wako unaweza kuona upo sawa, ila mimi naona tatizo hapo. Kwa nini? Kwa sababu japo biashara mwanzoni itakuhitaji sana, ila mwisho wa siku lengo la biashara ni kutupa uhuru.

    Maana yake kama kweli uko siriazi kufanya biashara inapaswa baada ya muda upate uhuru, biashara ijiendeshe yenyewe, wewe upate uhuru na muda wa kufanya mengine.

    Najua kwako hili ni gumu kumeza kwa sababu hujawahi kuona washikaji zako wakifanya hivyo. Ila huoni walau hata kwa bosi wako?

    Sasa hata kama upo bize hakikisha unaanzisha biashara, anza na biashara hata za mtandaoni, soma ebook ya MITAJI 8 ILIYOKUZUNGUKA NA JINSI YA KUITUMIA

    Kama unaona upo bize na huwezi kuanza biashara. Nashauri pia ujiunge na programu yetu ya mafunzo zaidi ambapo utapata nafasi ya kuwa karibu na mimi kwa mwaka mzima. Nitakusaidia na kukushika mkono mpaka uanzishe na kuendesha biashara kwa muda ziada. BONYEZA HAPA kujiunga.

    kupata mafunzo zaidi BONYEZA HAPA

    KUMI: HUPATI RUHUSA KUTOKA KWENU

    Pengine labda ndugu zako wa karibu hawataki kabisa kusikia habari za wewe kuanzisha biashara. Kama mazingira yako ndiyo haya

    Basi utapaswa kukaa nao na kuongea nao kwa kina kuhusiana na biashara. Walekeze kwa nini unataka kuanzisha biashara. Waeleze ndoto zako kubwa ulizonazo kuhusu biashara.

    Ongea nao, bwana bro au sista, iko hivi, mimi siku zote hizi unaniona hapa, nina ndoto kubwa za kuanzisha biashara, najua kweli kuwa biashara siyo kitu ambacho unapenda ila mimi binafsi ni kitu ambacho naona kwamba napenda na ninaona naweza kusaidia watu na familia kupitia hapo…

    Kama kuna uoga au hofu ambayo wanayo iongelee kwenye maongezi yako na namna ambavyo utaweza kufanya biashara yako bila ya kuwasababishia hiyo hofu.

    Ikiendelea kushindikana pengine unaweza kutakiwa kutoka nyumbani, kama upo nyumbani kwenu lakini.

    KUMI NA MOJA: HUNA MTAJI FEDHA

    Pengine labda kinachokukwamisha wewe kuanzisha biashara yako ni kukosa mtaji fedha.

    Kama shida yako ni mtaji fedha, basi utapaswa kuanza utaratibu wa kuweka akiba. Weka akiba kutokana na kipato chako cha sasa.

    Kama huna kazi kabisa, basi kuanzia leo unapaswa kufunguka. Tafuta kazi au kitu chochote kile cha kuuza kuanzia leo. Angali akwenye jamii yako ni kitu gani ambacho unaweza kuanza kuuza. Lakini pia unapaswa kujua ni mtaji kiasi gani ambao unauhitaji.

    Nashauri sana, sana uhakikishe umesoma ebook ya MITAJI 8 ILIYOKUZUNGUKA NA JINSI YA KUITUMIA itakusaidia hata kama huna mtaji upate sehemu ya kuanzia. Kupata ebook hii Tuma elfu 5 sasa hivi kwenda 0684 408 755 jina ni GODIUS RWEYONGEZA ili kupata ebook hii

    umekuwa nami GODIUS RWEYONGEZA

    0755848391

    [block rendering halted]

  • Dhana Ya Riba Mkusanyiko Kwenye Kipaji

    Hakikisha unasoma: Kipaji Ni Nini?

    Mwanasayansi Albert Einstein aliwahi kunukuliwa akisema “riba mkusanyiko (compound interest) ni moja kati ya maajabu saba ya dunia”.

    Dhana ya riba mkusanyiko imejengwa kwenye msingi kwamba vitu vidogo vidogo vidogo vinapokusanywa kwa pamoja kwa kipindi kirefu, basi inafikia hatua ambapo vitu hivyo vinatengeneza kitu kikubwa.

    Ukitaka kunielewa vizuri zaidi nikupe tu mfano wa mtu aliyekuwa na mpango wa kuingia kwenye biashara ya nyumba za kupangisha ila hakuwa na mtaji.

    Mtu huyu alikuwa ana uwezo wa kuingiza fedha kidogo kila mwezi. Hivyo, kwenye hiyo fedha kidogo alikuwa anawatafuta watoto waliokuwa wanaenda kuokota matofali yaliyopasuka kidogo kwa ajili yake, kisha anawalipa.

    Watu walikuwa wanamwona kama mtu asiyekuwa na akili, ila yeye ndani kabisa alikuwa anajua wazi ni kitu gani ambacho alikuwa anataka kufanya.

    Walipokuwa wanafikisha kiasi kikubwa cha matofali alikuwa anajenga jengo lake kwa kutumia hayo matofali ila sasa akiwa ameyaweka vizuri.

    Alianza kujenga vyumba vidogodogo, kisha baada ya muda akawa ameanza kujenga nyumba kubwa na akawa ameanzisha kiwanda chake cha kufyatua matofali.

    Dhana ya riba mkusanyiko inafanya kazi hivi pia, kwenye kipaji. Unaweza kuona kama kufanya mazoezi leo hakutakuwa na maana.

    Ila ukweli ni kwamba, kipaji chako hakijengwi kwa siku moja kama ambavyo huwezi kujenga misuli yako ndani ya siku moja. Badala yake ule mkusanyiko wa vitu na mazoezi ambayo unakuwa unafanya kwa ajili ya kipaji chako ndio kwa pamoja unaleta matokeo makubwa.

    Kwa hiyo, jitoe kila siku kuhakikisha unakifanyia kazi kipaji chako. Kama itatokea kuwa unaenda kulala, ila ukakumbuka kuwa siku hiyo hukufanya kitu ili kukuza kipaji chako, hairisha kulala kwa dakika hata kumi, ili kwanza ufanye kitu kinachoendana na kipaji chako.

    Njia nzuri ya kufanyia kazi kipaji chako ni kuhakikisha kuwa unaweka muda kwenye ratiba yako ambao utautumia kufanyia kazi kipaji chako. Na muda huo ukifika acha kila kitu. Weka nguvu kwenye kipaji chako kwanza.

    Naipenda sana hadithi ya hekalu kubwa hapa duniani.

    Taj Mahal, lilijengwa kwa miaka 22. Na kila siku kuna kitu cha kipekee ambacho kilikuwa kinaongezwa, siku nyingine tofali. Siku nyingine jiwe, siku nyingine nondo n.k .

    Baada ya miaka 22 ya kulifanyia kazi lile jengo kila siku, ndio likatokea kuwa ni jengo bora.

    Na wewe kipaji chako kinaweza kuchukua muda kuanza kukulipa au kutambulika, usiogope.

    Endelea kukifanyia, siku nguvu ya riba mkusanyiko ikikaa pamoja, utafurahi sana.

    Kupata Vitabu Vyangu BONYEZA HAPA au piga 0755848391

    soma zaidi: Kipaji Ni Nini?

    Mambo Matatu Usiyoyafahamu Kuhusu Kipaji

    KUZA KIPAJI CHAKO

    Muda sahihi Unaopaswa Kuendeleza Kipji chako

  • Mafanikio Sio Ajali

    Mafanikio siyo kitu kinachotokea mara moja kama ajali, bali ni kitu ambacho kinatokea kwa kuandaliwa kila siku.

    Kwa hiyo mafanikio yako unapaswa kuyaandaa kila siku. Usisubiri ije itokee siku moja ambapo utaamka ukiwa umefanikiwa. Ishi kila siku yako kwa mafanikio.

    Maana mkusanyiko wa siku moja moja ndio unaleta mafanikio makubwa.

    Soma zaidi: Nguvu Ya Riba Mkusanyiko

    Kupata Mafunzo Zaidi BONYEZA HAPA

  • Tai Anatufundisha Somo Hili Kubwa Kuhusu Maisha Ya Mafanikio

    Tai Anatufundisha Somo Hili Kubwa Kuhusu Maisha Ya Mafanikio

    Siku ya leo nataka tujifunze kutoka kwa tai. Kuna mengi ya kujifunza Kutoka kwa tai ila kwa leo acha twende na hili.

    Tai akitaka kumla nyoka anamnyanyua kwa nguvu na kwa spidi kali ambayo nyoka hawezi kuhimili mpaka juu, Kisha anamwachia.

    Nyoka akiwa bado hajaelewa kinachoendelea tai anamdaka haraka kabla hajadondoka chini na kupanda naye juu zaidi katika mazingira ambapo tai anajisikia huru kufanya chochote.

    Kisha anamrarua nyoka…

    Anaweza kufanya hivyo kwa nyoka yeyote bila kujali ukubwa wa nyoka husika.

    SOMO: Kila mtu ana eneo lake la kujidai. Kwa tai eneo lake la kujidai Ni huko angani. Akipigana na nyoka wakiwa ardhini, lazima tu atafeli, ila akimchukua juu nyoka hana ujanja.

    Wewe pia unapaswa kufahamu eneo lako la kujidai. Kisha litumie kwa manufaa yako.

    SOMA ZAIDI:

    Kupata ebooks nzuri za kusoma BONYEZA HAPA

X