Category: Uncategorized

  • Maswali Matatu (03) ya Kukusaidia Kuwa Tajiri

    Utajiri hauwezi kuja kwa siku moja labda ikitokea ukashinda kwenye bahati na sibu au ukapata mali za kurithi. Watu waliofanikiwa huwa hawajengi uchumi binafsi kwa siku moja bali ni mpango wa mda mrefu wa kukuza na kudumisha mali zao. Haijalishi kipato chako ni kidogo au kikubwa ni muhimu kujua na kutambua njia unayotaka kuchukua ili…

  • Ukweli Kuhusu Safari ya Mafanikio

    Safari ya ya mafanikio sio ya mchezo mchezo, bali safari ambayo hukuitaji uwe makini na ujiandae sawasawa na kujitoa. Kama utaanza safari ya kimafanikio bila kujitoa sawasawa, na kujiandaa pale utakapokutana na vikwazo mbalimbali kama vile kukata tamaa, kukatishwa tamaa, kupingwa, na visingizio utakwama. unahitaji uwe umejipanga kisawasawa. Unahitaji kuwa umeweka malengo na mipango ya…

  • Nguzo Muhimu Unayohitaji Kufikia Mafanikio.

    Watu wengi sana wamekuwa wanafikiri safari ya mafanikio ni rahisi sana, na hivyo huingia katika biashara kwa kuwa na mtazamo wa kupata mafanikio tu. Pale inapotokea vikwazo vya aina mbalimbali njiani ndipo mtu huona ugumu wa kazi na kuamua kuacha. Safari ya mafanikio sio rahisi wala sio safari ya kubashiri, au kubahatisha. Unapoamua kuanza safari…

  • Zifahamu Sheria za Asili za Kuwa Tajiri

    Katika maisha ya kawaida kuna sheria nyingi zimetuzunguka na inabidi tuzifuate. Katika mazingira yetu kuna sheria za serikali za mitaa, sheria za serikali kuu na pengine sheria za kimataifa. Zote hizi huwa inabidi zifuatwe na ikitokea umezivunja basi kuadhibiwa huwa kunafuata. Adhabu hutolewa kulingana nabsheria ulizozivunja. Vilevile sheria za asili zimekuwepo zipo na zitaendelea kuwepo.…

  • Kwa Nini Kuzaliwa Maskini sio Dhambi Lakini Kufa Maskini ni Dhambi

    “Kuzaliwa maskini sio dhambi lakini kufa maskini ni dhambi” hii ni kauli maarufu iliyotolewa na blionea Bill Gates. Tunapozaliwa hakuna ambaye huwa anachagua azaliwe wapi na azaliwe na nan. Ni bahati tu kwamba kila mmoja huwa anajikuta kazaliwa katika mazingira ambayo yumo. Haijalishi ni katika mazingira ya kitajiri au kimasikini bado kote ni bahati tu.…

  • Je, Wajua kwamba Mlango Mmoja Ukifungwa , Milango Saba Inafunguliwa.

    Habari za leo ndugu msomaji wa SONGA MBELE BLOG ni imani ya yangu unaendelea vyema katika safari ya kuelekea mafanikio.  Hongera sana na karibu katika mada ya leo. Yawezekana unaona hauna, bahati. Yawezekana ukafikiri labda umelogwa.Katika safari ya mafanikio kuna mambo mengi sana utakutana nayo. Hakuna njia nyoofu katika kuelekea mafanikio. Na kama hii njia…

  • Jinsi ya Kuweka Usawa Katika Mapato na Matumizi.

    Ni muhimu sana kujifunza mbinu za kuweka usawa mapato na matumizi, haijalishi uko kwenye hali gani kiuchumi. Watu wengi hawatilii maanani suala la kuwa na bajeti, huku wakisema suala la kuwa na bajeti mpaka pale watakapokuwa  wamekuza kipato. Lakini ili ukuze kipato bajeti ni muhimu sana. Kile kinachoitwa bajeti ni usawa kati ya mapato na…

  • Jinsi ya Kuepukana na Kauli Hizi Tatu (03) za Kukatisha Tamaa

    Kwa kawaida mtu ukitaka kufanya jambo fulani la maana basi kila mmoja huwa anakuja na kauli zake na mtazamo wake. Wako baadhi ambao hutoa kauli fulani ambazo hulenga kukukatisha tamaa ili usiendelee na kwa wengine kauli hizi, huwakatisha tamaa kweli na kuwafanya wasiweze kuendelea mbele kwelikweli. Baadhi ya kauli hizo ni kama ifuatavyo. 1. Unapoteza…

  • Zifahamu njia za Kufanya Pesa Ikufanyie kazi

    Moja ya tofauti kubwa sana kati ya matajiri na maskini ni kwamba matajiri hutengeneza faida na maskini hutumia faida. Ni muhimu sana kufahamu kwamba hela ni kifaa ambacho kinaweza kukusaidia kufikia malengo yako. Ili wewe uweze kufikia uhuru wa kiuchumi unahitaji  kuanza kuitumia pesa ikutengenezee pesa sio wewe ufanye kazi ili upate pesa. Hapa kuna…

  • Mambo Saba (07)Ambayo Watu Waliofanikiwa Huwa Wanaepuka Kufanya

    Nikiongea na rafiki zangu, wengi huonekana wamekata tamaa na wanahisi hawajabahatika kufikia malengo yao. Wengine wanahisi wamerogwa au kuna watu wanawachezea. Wanahisi wamekwama kiasi kwamba hawajui wafanye nini. Mimi kitu cha kwanza ambacho hufanya ni kuangalia vitu ambavyo hupoteza muda wao na kuwafanya wakwame. Vitu ambavyo huingia katika njia yao ya mafanikio. SOMA ZAIDI: Kupe Hawa…

  • Kupe Hawa Wanne (04) Wananyonya Muda Wako Kila Siku.

    Je ni siku gani imekuwa ya matokeo makubwa sana kwako. Je, ni wiki gani imekuwa ya matokeo makubwa sana kwako? Ni mwezi gani umekuwa wa matokeo makubwa sana kwako? Watu wengi hupoteza mda wao wakifanya mambo ambayo hayaongezi  thamani kwao. Mambo baadhi ambayo hupoteza mda wako ni intaneti, kujaribu kubadili mambo nje ya uwezo wako,…

  • Ufahamu Uovu wa Lazima Kwenye Maisha Yako

    Habari za leo ndugu msomaji wa SONGA MBEL ni imani yangu unaendelea vyema katika hatua za kuelekea mafanikio. Leo tunaenda kuona jambo moja la lazima katika maisha yetu ambalo haliepukiki. Jambo hili ni kufikiri.   Kufikiri ni uovu usioepukika katika maisha yetu. Tunafanya hivyo muda wote, kila siku. Wanasayansi wanasema hatuachi kufikiri mda wote. Hata kama tumelala…

  • Yafahamu Mambo Manne (04) Ambayo Huwezi Kujifunza Shuleni.

    Habari za leo ndugu msomaji  wa SONGA MBELE BLOG. Ni imani yangu unazidi kupiga hatua katika kutafuta na kufikia mafanikio. Leo tunaenda kuona mambo ambayo huwezi kujifunza shuleni. Haijalishi umesoma hadi chuo kikuu au hujafika. Kuna utofauti mkubwa kati ya masomo yanayofundishwa shuleni na vyuoni, Na yale unayonifunza kutokana na maisha. Haya hapa ndo mambo…

  • Kama Hawa Wameweza Kwa Nini Wewe Usiweze;Usikate Tamaa Songa Mbele.

    Habari za leo ndugu msomaji wa songambeleblog.blogspot.com Ni imani yangu unaendelea vyema katika hatua ya kuimarisha maisha yako na kufikia mafanikio. Leo tunaenda kuangalia jambo muhimu sana katika maisha yako ambalo linaweza kuwa limekutokea au unaweza kukutana nalo ktika safari ya kutafuta mafanikio Jambo lenyewe ni kukata tamaa. Hili huweza kutokea baada ya kujaribu jambo flani na…

  • Faida 6 za Kusoma Vitabu na Makala za Kuelimisha.

    Habari za leo msomaji wa songambeleadress.blogspot.com ni imani yangu kuwa unaendelea vyema katika hatua za kuweza kufikia malengo uliyojiwekea Leo ningependa tujue umuhimu wa kusona vitabu na makala za kuelimisha, lakini pia tujifunze na kuanza kujisomea vitabu. 1.Unapata kujua mambo mapya.Kupitia kusoma unapata kujua vitu vipya,taarifa mpya na mbinu mpya za kutatua matatizo Ili uweze kupata yote…

  • Wafanyabiashara Waliofanikiwa Wanavyotunza Muda

    Ili ufanikiwe katika biashara unahitaji kutunza mda.Kama hutatunza mda sio tu kwamba utapoteza malengo lakini pia utapoteza wateja,hela,na pia unaweza kupoteza na biashara. Hapa kuna mambo matatu ambayo unaweza kuchukua ili kutunza mda wako.1.kuwa na mpango. Unahitaji kujua kile ambacho unataka kufikia na mda ambao unataka kiwe kimekamilika. Kuwa na mpango kutasaidia sana wewe kufikia…

  • Mambo Muhimu Ya Kuzingatia Wakati wa Kuanzisha Biashara

    Wakati hali mbaya kiuchumi na mshahara kidogo  kwa walioajiriwa vikipamba moto, wazo la kuanzisha biashara na kuwa bosi wako mwenyewe linaweza kuwa bora zaidi.Hapa kuna mambo muhimu ya kuzingatia wakati wa kuanzisha biashara 1.WazoKatika kila wazo zuri la biashara ulilo nalo kuna mamia ya watu wana wazo hilohilo. Jambo muhimu la kuzingatia ni kama wazo…

  • Jinsi Ya Kuepuka Kujiua Mwenyewe Kiakili

    Kujiua mwenyewe kiakili ni pale ubongo unapojirarua mwenyewe. Mwili unataka kufanya jambo fulani lakini ubongo ushakata tamaa na unaamua kujiua. Kila kitu tunachofikiria kinaweza kukujenga au kukubomoa.Kina uwezo wa kukutoa sehemu ya chini kimaendeleo na kukupeleka sehemu ya juu.Uko ulivyo kwa sababu ya jinsi unavyofikria,ukijisemea mimi  ni maskini Au hiki sikiwezi Au mimi ni mvivu…

  • Ijue Siri Ya Babiloni Kuwa Mji Tajiri Kuliko Yote Duniani

    Babiloni ulikuwa mji katika sehemu ya Mesopotamia. Mji huu ulikuwa sehemu ambayo ni kame na hivyo haukuwa na mvua za kutosha ili kuweza kuendesha shughuli yoyote ya kilimo. Chanzo pekee cha maji kilikuwa ni mto Euphrates. Watu wa Babiloni waliweza kuchimba mifereji kuingia mjini mwao na hivyo kuendesha shughuli zao za kuwaingizia kipato. Jambo kubwa…

  • Mbinu Muhimu Ya Kujenga Mafanikio Katika Biashara

    Wajasiriamali wana mchango katika maendeleo ya uchumi wa nchi yetu. Wajasiriamali ni chimbuko la vipato ambavyo husaidia kujenga uchumi wa watu kupitia biashara zao. Wajasiriamali wanatoa ajira kwa vijana wengi na hivyo kuwasaidia kupata kipato chao na kupata kitu cha kuweka mkono kinywani. Kuna mbinu mbalimbali ambazo wajasiliamali wanaweza kuzitumia ili kujenga mafanikio katika biashara…

X