Home


  • Kitabu Hiki Kinahusu Nini?

    Mara kwa mara napokea maswali kuhusu kitabu Cha MAAJABU YA KUSOMA VITABU. Maswali haya yanatokabkwa wale ambao hawajakisoma na wanapenda kujua kwa ufupi kinahusu Nini?

    Unaamzaje kumweleza mtu juu ya kitabu kilichosaidia maelfu ya watu KUJENGA tabia ya ya KUSOMA vitabu?

    Nadhani kwa ufupi kitabu hiki kinaeleza

    NGUVU YA KUSOMA VITABU na JINSI vitabu vinavyoweza kukuinua.

    JINSI vitabu vinavyoweza kukusaisia kuongeza THAMANI Yako.


  • Utajiri ni haki yako ya msingi

    Utajiri ni asili lyako, hivyo usiogopeshwe na wala usidanganywe na mtu yeyote anayekwambia kwamba utajiri siyo saizi yako au siyo kitu unachopaswa kuwa nacho.

    Fursa za kuwa tajiri zipo kwa usawa kwa kila mmoja. Zitumie hizo fursa vizuri haswa.

    Utajiri hauna ubaguzi.

    Haumpendelei mmoja na kumbagua mwingine. Unatoa fursa kwa usawa kwa watu wote

    Unapawa kuupenda utajiri na wenyewe utakupenda maana kitu ambacho hukipendi hakiwezi kukupenda hata kidogo.

  • Vitabu vipya vya GODIUS RWEYONGEZA

     

    Godius Rweyongeza amezindua vitabu vipya.

    Na Kwa kuwa ndiyo kwanza amevizindua basi vitakuwa vinapatikana Kwa ofa. Chagua vitabu vitatu kati ya hivyo, utumiwe vitabu hivyo Kwa bei ya ofa Sasa hivi


    Vitabu vyenyewe ni:


    1. TENGENEZA PESA KWA KILE UNACHOJUA

    2. NGUVU YA KUFIKIRI KWA UKUBWA

    3. FURSA AMBAZO VIJANA WA SIKU HIZI WANACHEZEA na jinsi ya kuzitumia Kwa manufaa

    4. AINA 10 ZA UJUZI AMBAO KILA MFANYABIASHARA ANAPASWA KUWA NAO

    5. JINSI YA KUTOA NA KUPOKEA MREJESHO (kitabu Cha kwanza)

    6. USIMAMIZI WA FEDHA BINAFSI: Kanuni za kusimamia fedha, KUWEKA bajeti na kujenga utajiri

    7. NGUVU YA KUFANYA MAAMUZI

     

    Chagua vitabu vitatu kati ya hivyo. Lipia Elfu kumi upate vitabu vitatu Sasa


    Lipia 20,000/- upate vyote sita. Hii ofa mwisho ni jumapili hii


    Namba ya malipo ni 0684408755

  • Jambo Moja Kubwa La Kujifunza Kutoka Kwa Kampuni ya Alibaba

    Picha hizi hapo ni picha za matangazo ya kampuni ya Alibaba ambayo binafsi nimekutana nayo mara kwa mara kwenye mitandao ya kijamii.

    Mtandao wa alibaba ni moja ya mtandao ambao unawekeza sana kwenye mtangazo. Ukiingia google unakutana na matangazo yao.

    Ukiingia youtube, unakutana na matangazo yao.

    Ukiingia facebook, matangazo yao pia yapo,

    Ukiwa instagrama matangazo yao yapo.

    Na hata kwenye messenger wapo.

    Yaani, alibaba hawana dogo.

    hawadharau mtandao.

    Wakijua kwamba sehemu fulani kuna watu, basi na wenyewe wapo.

    Kitu kikubwa ambacho tunaweza kujifunza kwao ni kutumia kila njia kuwafikia wateja.

    Ni kweli najua kwamba unaweza usiwe na bajeti kubwa kama hiyo ya alibaba, lakini bado hili halimaanishi kwamba unapaswa kurudi nyuma kwenye kuitangaza biashara yako.

    Endelea kuitangaza biashara yako bila ya kurudi nyuma kila kukicha.

    Tumia kila njia ambayo unaweza kutumia.

    SMS

    WHATSAP

    SIMU ZA KAWAIDA

    MITANDAO YA KIJAMII

    Unapokutana na watu

    Maonesho mbalimbali

    Watu maarufu

    Content creators

    Yaani, kama kuna njia ambayo unaweza kutumia, itumie.

    Uwe na siku njema.

    Hii picha inaonesha bajeti ya alibaba kwenye matangazo tu kila mwaka

    Najua kuwa ungependa kupata ushauri wa karibu zaidi moja moja kwa moja kutoka kwangu.

    Nitafute tuone ni lini nitakuwa na muda, ili nikupangie ratiba ya kuongea na wewe. Utalipia kiasi kidogo tu.

    Saa moja ni laki moja mazungumzo kwa njia ya mtandao.

    SAA MOJA NI LAKI MBILI NA NUSU MAZUNGUMZO YA ANA KWA ANA. Malipo yanafanyika kwanza, kisha unapewa tarehe (appointment) tutakapoweza kuongea.

    Tumia namba ya simu +255 755 848 391 kuwasiliana nami.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza ambaye anaishi Morogoro nchini Tanzania.

    Unaweza kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza kupitia youtube channel yake hapa

    Kwa ushauri niandikie songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu ambavyo ameandika Godius Rweyongeza, wasiliana naye kwa +255 684 408 755 na orodha ya vitabu vyenyewe unaweza kuiona HAPA. Chagua unachopenda, kisha twanga,  +255 684 408 755

    Kujiunga na programu yetu ya uandishi. Wasiliana na +255 678 848 396

    For Consultation only: +255 755 848 391  au godiusrweyongeza1@gmail.com

  • Leo ni Siku ya Wafanyakazi Duniani!

    Asanteni na hongereni nyote kwa kujituma na kujitolea kila siku katika kazi na majukumu mnayofanya.

    Nyie ndiyo mnafanya taifa letu kuzidi kuwa Bora zaidi. Juhudi zenu zinathaminiwa sana na zinastahili pongezi kubwa mno!

    Tunathamini sana mchango wenu katika ufanisi maendeleo ya nchi yetu. Hongera kwa kazi nzuri mnayofanya! 🎉

    Leo Nina OFA Kwa ajili Yako wewe mfanyakazi Bora kuwahi kutokea✅✅ Pata vitabu hivi Kwa 20,000/-

    1: JINSI YA KUONGEZA THAMANI YAKO

    2: VYANZO VINGI VYA KIPATO

    3: MAAJABI YA KUWEKA AKIBA.

    4: JINSI YA KUTENGENEZA MSHAHARA NJE YA MSHAHARA ILI ufungue milango mipya ya fursa na mafanikio katika maisha yako ya kazi.

    Kupitia ujuzi mpya na ufahamu, tunaweza kujenga jamii yenye nguvu zaidi na maisha bora kwa kila mmoja wetu.

    Heri ya Sikukuu ya Wafanyakazi* Kupata nakala hizi, Lipia 20000 upate Soft copy zote nne. Namba ya malipo ni 0684408755: GODIUS RWEYONGEZA 👏🏼👏🏼

  • Kwa Nini Unapaswa Kuwa na Fikra za Kuwa Bilionea

    Rafiki yangu mpendwa, salaam.
    Leo nataka Nikwambie sababu kuu Kwa Nini Wewe unahitaji kuwa na fikra za kuwa bilionea.

    Wengi wakifikiria juu ya hili Huwa wanaogopa sana na kuona kama kitu ambacho haiwezekani, ila ukweli ni kuwa kile anachofikiria mtu ndiyo anakuwa.

    Kama Leo hii unaingiza KIPATO chochote, hata kama ni kidogo, una nafasi kubwa ya kutengeneza mabilioni ya PESA hapo baadaye.

    • Ukweli ni kuwa mabilioni ya PESA yanaanza na PESA kidogo TU hizi ambazo unaingiza Leo hii. Hiki kitu unaweza kukiona kama Cha kipumbavu hivi
    • Ila ngoja nianze Kwa KUELEZA hiki kitu Kwa namna ya kawaida TU.
    • kama unaingiza Elfu kumi Kwa siku, mfano, kiasi hiki kidogo kama kilivyo, kinaweza kuwa tiketi ya wewe kuingiza mamilioni zaidi. Ni wazi kuwa ukipambana hii Elfu kumi Kwa siku, baada ya muda inaweza kuwa laki Moja Kwa siku. Au na hapo unataka kunikatalia😁😁.

    Ukishagundua namna ya kuingiza laki moja kwa siku, unaweza pia kuingiza milioni Moja Kwa siku.

    Hivyohivyo kuendelea mpaka milioni kumi, mpaka milioni 100 ma zaidi ..

    Na hiyo ndiyo inaweza kuwa tiketi yako ya kufikia ukuu na ubilionea unaoutaka.

    RAI yangu Usifikirie kiudogo rafiki yangu Mara zote fikiria Kwa ukubwa.

    Ni Bora uwe na fikra za kuwa na mabilioni ya PESA, Ili ikiotokea hujafikia, walau uwe sehemu nzuri zaidi. Kuliko kuwa fikra ndogo ambazo ikitokea hujafikia kabisa utafeli vibaya sana.

    Sasa baada ya kusema hayo wacha nikupe sababu yangu Kwa Nini unapaswa kufikiri katika mabilioni. Na kumbuka hapa ninaposema ubilionea simaanishi Kwa PESA za Tanzania. Namaanisha ubilionea Kwa Dola.

    • Siku za nyuma niliwahi KUELEZA hapa kuwa ubilionea haupimwi Kwa shilingi, Bali Kwa Dola Marekani. Ndiyo kipimo kinachotumika kupima utajiri Kwa Sasa
    •  SOMA ZAIDI HAPA Bilionea Ni Mtu Wa Aina Gani?
    • Hapa kuna sababu kumi kwa nini unapaswa kuwa bilionea: SABABU YA KUMI NA KUMI NA MOJA NI NZURI ZAIDI

    1. Uwezo wa Kubadilisha Maisha: Kama bilionea, utakuwa na uwezo wa kubadilisha maisha ya watu wengi kwa kutoa fursa za kazi, elimu, na huduma za kijamii.

    2. Uhuru wa Kifedha: Kuwa bilionea kutakupa uhuru wa kifedha ambao utakuruhusu kufanya chochote unachotaka bila wasiwasi mkubwa wa fedha.

    3. Nguvu ya Kufanya Mabadiliko: Kwa kuwa na utajiri mkubwa, utakuwa na uwezo wa kushawishi sera na kufanya mabadiliko makubwa kijamii na kiuchumi.

    4. Fursa za Uwekezaji: Kama bilionea, utakuwa na fursa za kuwekeza katika miradi mbalimbali na hivyo kuongeza utajiri wako na kusaidia katika maendeleo ya jamii.

    5. Kuwa Na Athari ya Muda Mrefu: Kwa kuwa bilionea, unaweza kujenga athari ya muda mrefu ambayo itaendelea kuathiri vizazi vijavyo kupitia miradi na taasisi za kijamii utakazozianzisha.

    6. Kuboresha Ubunifu na Teknolojia: Utajiri wako unaweza kuwekezwa katika kuboresha ubunifu na teknolojia, kusaidia katika kuleta maendeleo makubwa kwa binadamu.

    7. Kuwa Mfano wa Kuigwa: Kama bilionea, utakuwa mfano wa kuigwa kwa vijana na watu wengine, kuwahamasisha kufanya kazi kwa bidii na kufikia malengo yao.

    8. Kupata Fursa za Kusafiri na Kujifunza: Utajiri wako utakuruhusu kusafiri na kujifunza mambo mbalimbali duniani kote, kuongeza ufahamu wako na mtandao wa kijamii.

    9. Kufurahia Maisha: ubilionea utakuruhusu kufurahia maisha na kutimiza ndoto zako bila kikwazo cha kifedha.

    10. Ubilionea itaonesha ni Kwa namna gani umeweza kutoa THAMANI kubwa Kwa watu. Ni Kwa namna gani umeweza kuleta mchango chanya Kwa jamii kiasi kwamba jamii umekuwa tayari kutoa Fedha na kupata huduma au bidhaa zako ambazo zimekufikishabkwenye ubilionea

    11. Ni kwa sababu wewe umeubwa Kwa mabilioni.

    • Kama wewe ni mwanaume, wanasanyansi wananiambia kwamba mwili wako una seli bilioni 36.Seli trilioni 36 ni sawa na seli bilioni 36 mara Elfu Moja
    •  Kama wewe ni mwanamke wanasayansi wananiambia kuwa mwili wako una Trilioni 28. Seli trilioni 28 ni sawa na seli bilioni 28 mara Elfu Moja.

    Huo ndiyo mwili wako. Hauna mamia ya seli, Wala siyo Malaki au mamilioni, ni mabilioni.

    Anza kufikiri Kwa mabilioni wewe!

    Ukiachana na seli hizo ambazo unazo Kwa maelfu ya mabilioni.

    Wanasanyansi wananiambia Kuna hiki kitu kinaitwa Neurons. Hizi wanasema unazo bilioni 100 na zimeunganishwa zenyewe Kwa zenyewe bilioni 100 mara 1000.

    Na hii ndiyo sababu kwa nini unapaswa kufikiri Kwa mabilioni.

    Enewei Kwa Leo inatosha au unasemaje? Tukutane Dar Es Salaam Ubungo; Landmark hotel tarehe 29 JUNI

    Soma tarehe vizuri👆🏿

    Tutaanza mapema saa 1 mpaka jioni saa 1 jioni. Itakuwa ni siku yetu Moja ya kukaa pembeni, kujifunza Kwa kina, Kisha tutachukua kubwa zaidi baada ya hapo.

    Kundi la wahudhuriaji wa semina hili hapa

    https://chat.whatsapp.com/CAdCnW82i8N0clD2fDvn7v

    SOMA ZAIDI: 

  • NGUVU YA KUANZA

    Habari na karibu sana kwenye video hii ya siku ya leo ambapo tunaenda kuwa tunaongelea nguvu ya kuanza na jinsi ambavyo tunaweza kuitumia nguvu hii ya kuanza kwa manufaa kwenye mambo mbalimbali na kazi mbalimbali ambazo tunafanyia kazi kwenye maisha yetu ya kila siku.

    Unaenda kujifunza nguuv ya kuanza kwenye maisha na jinsi ambavyo unaweza kuitumia nguvu hii kwa manufaa kwenye maisha ya kila siku. Unafahamu kuitumia nguvu ya kuanza kulivyo na manufaa na vitu gani ambavyo umekuwa unakosa kwa kutochukua hatua kwenye kuanza?

    Tuambatane moja kwa moja mpaka mwisho ili uweze kujifunza mengi kwenye video hii Jifunze zaidi hapa

  • Utt ni Nini?

    Pata hiki kitabu kwa 20,000 hardcopy na 10,000 softcopy

    1. Utt ni Nini?

    2. Ina faida gani?

    3. Nani anaruhusiwa kuwekeza?

    4. Unafunguaje akaunti? 5.

    Nikiwa mkoani nafunguaje akaunti?

    6. Kiasi gani Cha pesa unahitaji ili kuanza kuwekeza utt?

    7. Mfuko upi mzuri utakaonipa mrejesho mzuri? 8. Kwani utt na hisa utofauti wake ni Nini?

    9. Mfuko wa Hatifungani wa utt ni sawa na kuwekeza kwenye Hatifungani?

    10. Kama ndiyo KWANZA niwekeze wapi? Kwenye hisa, Hatifungani au vipande?

    Maswali haya na mengine mengi, yamejibiwa kwenye kitabu Cha MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE.

    Jipatie nakala Kwa 25,000/- Lipia sasa Kwa namba hii 0684408755 jina kitatoka GODIUS RWEYONGEZA Unaipata popote ulipo duniani✅

  • Hii Ndiyo Gharama Halisi Unayopaswa Kulipa Ili Kufanikiwa Kwenye Biashara

    Nyuma ya ushindi wa biashara kuna vitu ambavyo unapaswa kufanya ili uweze kuisogeza biashara yako mbele. Baadhiya hivi vitu vinahitaji ujitoe, kuliko mtu yeyote.

     

    #1. Kuchelewa kulala, hii mojawapo ya gharama ambazo unapaswa kulipa kama mfanya biashara katika kujenga biashar ayako. Kuna nyakati nyingi ambazo utahitaji kutumia muda mwingi kazini kwa ajili ya kukamilisha jambo fulani ambalo liko mbele yako. Kuwa tayari kulipa gharama hii pale itakapohitajika

     

    #2. kuamka mapema

    mmbali na kuwa utapaswa kulala umechelewa, kuna nyakati utakuwa wa mwisho kulala na wa kwanza kuamka. Yaani, hapo umelela saa sita au saa saba, na saa kumi kamiili alfajiri upo macho na kazi inaendela. Kuwa tayari kw aajili ya hili, ila kama hujaanza biashara usiogope.

     

    #3. Kuweekeza katika wewe

    Hi ini gharama nyingine muhimu sana ambayo unapaswa kuilipa. Ukweli ni kuwa biashara itakuwa kulingana na vile uyakavyokuwa unakua wewe. Kama wewe hukui, biashara haitakua pia.

    kama wewe unadorora vile vile biashara itadorora.

     

    #4. KUWEKEZA pesa

    Hiki ni kitu kingine muhimu ambacho kama mfanyabishara utapaswa kukifanya. Unahitaji kuwkeza fedha zako. Kuna maeneo muhimu ambayo mfanyabishara yeyote makini anapaswa kuwekeza fedha zake.

    Eneo la kwaza ni kuwekeza fedha kwenye biashara yako. Hili ni eneo la kwanza kabisa ambalo unapaswa kuwekeza fedha zako kama mfanyabiashara.

    Eneo la pili ambapo unapaswa kuwekeza fedha zako ni kwenye hisa, hatifungani na vipande kupitia soko la hisa la Dar Es Salaam

    Na eneo la tatu ni kuwekeza kwenye elimu na kujifunza.

     

    Hayo ndiiyo maeneo ambayo kama  mfanyabiashara unapaswa kuwekeza fedha zkao.

    Najua kuwa ungependa kupata ushauri wa karibu zaidi moja moja kwa moja kutoka kwangu. Nitafute tuone ni lini nitakuwa na muda, ili nikupangie ratiba ya kuongea na wewe. Utalipia.

    Saa moja ni laki moja mazungumzo kwa njia ya mtandao.

    SAA MOJA NI LAKI MBILI NA NUSU MAZUNGUMZO YA ANA KWA ANA. Malipo yanafanyika kwanza, kisha unapewa tarehe (appointment) tutakapoweza kuongea

    Tumia namba ya simu +255 755 848 391 kuwasiliana nami.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza ambaye anaishi Morogoro nchini Tanzania.

    Unaweza kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza kupitia youtube channel yake hapa

    Kwa ushauri niandikie songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu ambavyo ameandika Godius Rweyongeza, wasiliana naye kwa +255 684 408 755 na orodha ya vitabu vyenyewe unaweza kuiona HAPA. Chagua unachopenda, kisha twanga,  +255 684 408 755

    Kujiunga na programu yetu ya uandishi. Wasiliana na +255 678 848 396

    For Consultation only: +255 755 848 391  au godiusrweyongeza1@gmail.com

     

  • Njia za Kweli za Kuwathibiti Wakatisha Tamaa

    Kuna watu wengi wanaokatisha tamaa kwenye maisha yetu ya kila siku. Hata hivyo, ni muhimu sana, kuwa kujua njia ya kujikinga na wakatisha tamaa. kama ambavyo kuna mavazi ambayo ni bullet proof, hivyohivyo kuna njia ambazo ukizitumia naweza kuthubutu kuziita, kukatishwa tamaa proof, yaani njia hizi zitakufanya uzidi kusongambele hata katikati ya wakatisha tamaa. Utakuwa hushikiki, na mara zote utakuwa na malengo na ndoto kubwa ambazo unazipambania

    Ngoja kwanza nikuchane ukweli, 

    Ukweli wa kwanza ni kwamba kama unakata tamaa kwa sababu ya watu wanaokukatisha tamaa, basi wewe hutakuja kufanikiwa. Maana tunavyoyaendea mafanikio makubwa ni kwamba kuna watu watatishika na mafanikio yetu ambayo tunayafanyia kazi. Na wengine watakukatisha tamaa kwa sababu tu wanaogopa zile hatua kubwa ambazo unachukua, kitu pekee watakachoona wanaweza kufanya ni kukukatisha tamaa.

    Ukweli namba mbili ni kwamba kama unatakatishwa tamaa na watu, maana yake hauko bize kiasi cha kutosha, na hasa kama maneno na kauli ambazo watu wanatoa juu yako.

    Ukweli ni kuwa unapaswa kuwa bize mara zote kuliko hata ubize wenyewe. Hakuna kitu kingine nje ya kazi zako na majukumu yako ambacho kinapaswa kukukwamisha wewe wala kukurudisha nyuma

    Ukweli nambari tatu, kuna watu wamejipa kazi ya kukatisha tamaa wengine. Hivyo, waache wafanye kazi zao, na wewe kazi yako iwe ni kupambania malengo na ndoto zako kubwa.

    Ukweli nambari nne, mti unaopigwa mawe ni mti wenye matunda.

    Kiufupi ujumbe wangu ninaotaka kukwambia wewe ni kwamba haupaswi kuwa mtu wa kurudi nyuma na wala haupaswi kukatishwa na kitu chochote. kile kwenye maisha yako.

    sasa ili usikate tamaa kuna silaha muhimu ambazo unapaswa kuwa nazo ambazo zitakusaidia sana kuhakikisha kwamba unasongambele.

    SILAHA YA KWANZA: Kuwa na ndoto kubwa kama vile utaishi milele. rafiki yangu unapaswa kuwa na ndoto kubwa ambazo unazifanyia kazi, na zifanyie kazi mara zote bila ya kurudi nyuma, zifanyie kazi ndoto zako leo kama vile unaenda kufa kesho.

    SILAHA YA PILI: Mara zote kuwa kwenye ratiba ya kufanyia kazi malengo na ndoto zako kubwa. Kamwe usirudi na usikubali kurudishwa nyuma na mtu au kitu chochote kile. Usipokuwa bize na ndoto zako, hakuna mtu hata mmoja ambaye atakuwa bize na ndoto zako. Kumbuka ile nukuu ya madebe tupu huvuma

    SILAHA YA TATU: Hakikisha mara zote umepangilia ratiba zako kwa umakini kiasi kwamba unakuwa hauna muda wa kupoteza.  Hii ni silaha kubwa sana kwa sababu, itakufanya uwe biza na maisha yako na uachane na mambo ya wengine.

    na ukweli ni kuwa una mambo mengi ya kufuatilia juu ya maisha yako kuliko kufuatilia maisha ya watu wengine

    SOMA ZAIDI: 

    Najua kuwa ungependa kupata ushauri wa karibu zaidi moja moja kwa moja kutoka kwangu. Nitafute tuone ni lini nitakuwa na muda, ili nikupangie ratiba ya kuongea na wewe. Utalipia kiasi kidogo tu.

    Saa moja ni laki moja mazungumzo kwa njia ya mtandao.

    SAA MOJA NI LAKI MBILI NA NUSU MAZUNGUMZO YA ANA KWA ANA. Malipo yanafanyika kwanza, kisha unapewa tarehe (appointment) tutakapoweza kuongea

    Tumia namba ya simu +255 755 848 391 kuwasiliana nami.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza ambaye anaishi Morogoro nchini Tanzania.

    Unaweza kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza kupitia youtube channel yake hapa

    Kwa ushauri niandikie songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu ambavyo ameandika Godius Rweyongeza, wasiliana naye kwa +255 684 408 755 na orodha ya vitabu vyenyewe unaweza kuiona HAPA. Chagua unachopenda, kisha twanga,  +255 684 408 755

    Kujiunga na programu yetu ya uandishi. Wasiliana na +255 678 848 396

    For Consultation only: +255 755 848 391  au godiusrweyongeza1@gmail.com

X