Home


  • Namba Zetu Za Malipo

    Namba za malipo ya vitabu:

    Namba za lipa

    TIGO PESA: 19016638 Jina ni SONGAMBELE CONSULTANTS

    M-PESA: 5564517 jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

    Namba za kawaida

    AIRTEL MONEY: 0684408755
    TIGO PESA: 0655 848 392
    M-PESA: 0745 848 395

    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    NB: Kama namba ya malipo anatumiwa mtu ambaye yuko nje ya nchi. Iandikwe Kwa kuanza na +255

    Kwa hiyo namba zinazotumwa nje ya nchi zitakuwa
    Airtel money: +255 684 408 755
    TIGO PESA: +255 655 848 392
    M-PESA: +255 745 848 395

    KOTE Jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Kama malipo yatakuwa yanafanyika kupitia benki.

    Yafanyie kupitia

    1. CRDB BANK: 0150770710200
    2. NMB BANK: 22110047274

    Kote jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

  • Wasiliana na Godius Rweyongeza Sasa

    Habari yafuatayo ni mawasiliano Unayoweza kutumia kumpata GODIUS RWEYONGEZA

    Simu: +255 (0) 684408755

    Whatsap: +255 (0) 755848391

    Email: songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu vyake wasiliana Moja kwa Moja na +255 (0) 684408755 (more…)

  • KUZA KIPAJI CHAKO

    Kipaji ni mauwezo fulani hivi ya asili ambayo mtu unazaliwa nayo na yanakuwezesha kufanya vitu kwa namna ya upekee sana.

    Mauwezo haya yanakutambulisha kwa watu kwa sababu hakuna mwingine ambaye anakuwa nayo. Na wala ya kwako hayawezi kulinganishwa na ya mtu mwingine. 

    Sasa nikuulize wewe, kipaji chako unakifahamu?

    Ni kipi? Na je unakifanyia kazi?

    Hakikisha unakitumia vizuri kipaji chako maana, siku ya mwisho utaulizwa namna ulivyokitumia kipaji chako๐Ÿ˜€๐Ÿ˜€.

    Kujua namna nzuri ya kugundua na kutumia kipaji chako hakikisha umesoma kitabu cha KUTOKA SIFURI MPAKA KILELENI. Sura ya KUMI imeeleza kwa kina jinsi ya Kugundua kipaji chako, kukinoa na kukitumia kwa manufaa. Fungua ukurasa wa 52 kwenye kitabu ujionee mwenyewe.

    Kama huna kitabu hiki, rusha elfu 10 leo ili uweze kukipata. Nitakutumia na vitabu vingine vitatu ambavyo ni

    1. MAISHA NI FURSA: ZITUMIE ZIKUBEBE

    2. MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE

    3. SEKTA 11 ZA KUTENGENEZA MAMILIONI YA FEDHA TANZANIA

    Rusha sasa hivi kwa 0684 408 755 jina ni GODIUS RWEYONGEZA

  • Usiende Chuo Kusomea Uandishi Wa Vitabu; Badala Yake Fanya Hivi

    Siku kadhaa zilizopita nilipokea simu ya mtu aliyekuwa anataka nimwambie chuo kizuri kinachonoa Waandishi Wa Vitabu.

    Nilimjibu vizuri tu, ila hakuridhika na majibu yangu kwa maana yalipingana na kile alichokuwa anaamini kwa asilimia 100. Yeye alitaka kwenda chuo, asomee uandishi na apate cheti. Cheti cha nini sasa? Najua, jamii yetu imezoea kwamba ukiwa na cheti basi hapo unakuwa umefaulu na unaenda ku-win maisha.

     Baada ya siku kama tatu hivi nilipokea ujumbe huu hapa chini kutoka kwa mtu mwingine.

    Nadhani huyu alinifafuta na tuliongea kwa kina kuhusu hili.

    . Simshauri kwa Sasa apoteze fedha zake kwenda chuo kwenda kusomea UANDISHI. 

    Kuna kozi nyingi ambazo anaweza kusoma mtandaoni tena akiwa nyumbani, na akiwa anaendelea na shughuli zake za sasa. 

    Ni sawa kuingia darasani, ila kwa sasa asifanye hivyo.

    Afanye yafuatayo.

    1. Aanze kuandika

    2. Amtafute โ€˜mentor’ wa kumsaidia.

    3. Aoneshe kazi zake anazoandika aidha mtandaoni au kwa watu wake wa karibu.

    4. Apokee mrejesho wa kazi zake na aufanyie kazi.

    5. Atumie mrejesho anaoupata na mafunzo anayopata kuboresha uandishi wake zaidi.

    Kuna mengi ila kwa sasa hayo yanatosha.

    Najua ushauri huu ataupuuza. Ila walau ninachofahamu kwa sasa atapoteza muda wake kwenda kujifunza uandishi kwa ajili tu ta kupata CHETI ambacho mwisho wa siku hakitamsaidia chochote.

    Ngoja nieleze kitu zaidi hapa. Waandishi hawafahamiki Kama waandishi kwa sababu wanaVYETI. Waandishi ni waandishi kwa sababu wanaandika.

    Mimi siyo mwandishi kwa sababu Nina cheti; HAPANA. Sijawahi hata siku moja kuona mtu ananiuliza cheti changu cha kuwa mwandishi kipo wapi๐Ÿ˜Š๐Ÿ˜Š. 

    Kitu kingine ni kwa kuwa nguvu yake kubw ipo kwenye cheti kuliko kufahamu zaidi mchakato wa kuandika na kubobea kwenye uandishi, ataweka NGUVU kwenye kupata CHETI na atapata, ila hatakuwa mwandishi mzuri. Na hicho ndiyo kuantokea pia kwenye mfumo wa elimu. Wahitimu wengi wanahitimu na vyeti vizuri ila ujuzi SIFURI kutokana na ukweli kuwa waliweka nguvu kubwa kwenye VYETI kuliko kupata ujuzi.

    ๐Ÿ–Š๏ธ๐Ÿ–Š๏ธ๐Ÿ–Š๏ธ๐Ÿ–Š๏ธ๐Ÿ–Š๏ธ๐Ÿ–Š๏ธ

    Nashauri asome kitabu changu cha JINSI YA KUWA MWANDISHI MBOBEVU NDANI YA SIKU 30 ambacho kimeeleza kila kitu anachohitaji kujua kuhusu uandishi๐Ÿ‘‡๐Ÿ‘‡

    Au awasiliane nami kwa 0755848391

  • FANYA UAMUZI SASA

    Bila kujali upo katika hali gani, Kuna wakati unapaswa kufanya UAMUZI kwamba sasa mimi nitaanzia hapa na nitaendelea mbele 

    Kataa kabisa kuendelea kusema kwamba sina mtaji

    Kataa kuendelea kulalamikia ugumu wa maisha.

    Chagua kuanzia hapo ulipo, miaka 10 ijayo utajishukuru kwa uamuzi huu.

    Amua Sasa kupata vitabu vitano kwa elfu kumi tu. Hii ofa mwisho wake ni  Leo hii

    Vitabu vyenyewe ni

    1. MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE.

    2. MAISHA NI FURSA ZITUMIE ZIKUBEBE

    3. SEKTA 11 ZA KUTENGENEZA MAMILIONI YA FEDHA TANZANIA 

    4. KUTOKA SIFURI MPAKA KILELENI

    5. Cha tano utachagua mwenyewe kutoka kwenye orodha ya vitabu vyangu hapa

    https://www.getvalue.co/home/seller_collection/393

    Utalipia kwa Airtel money namba 0684 408 755

    Changamka sasa. Hii ni ofa ya Leo tu

  • Kinachotokea Unapokuwa Na Ndoto Kubwa

     Jana niliandika makala yenye vitu 9 ambavyo hupaswi kuchoka kufanya. Mmoja wa wasomaji wa amkala hiyo alinibu kwa kusema hivi

    Nami nikawa nimemjibu pia kwa ujumbe huu hapa chini

    Ni kweli unapokuwa unapambania ndoto kubwa watu watakuona mtu wa ajabu sana. 

    Watakuona kichaa, utaambiwa umechnganyikiwa na mambo mengine mengi.

    Na hili linawatokea watu wote wenye ndoto kubwa. 

    Kuwa na ndoto kubwa ni sawa na kucheza muziki ukiwa na earphone masikioni. Wengine hawausikii huo muziki ila kwako unakuwa umenoga. Wanaokuona unacheza watakuona kichaa tu, kwa sababu muziki unaocheza kwao hauna maana.

    Ndio  maana Steve Jobs anasema kwamba, watu wenye kichaa cha kutosha kiasi cha kufikiri wanaweza kuibadili ndio ambao huibadili. Kuna wakati unapokuwa na ndoto kubwa, unapaswa kukubali tu kuonekana kichaa.

    Nashauri sana usome kitabu changu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO. Kina mengi ya kueleza kuhusu ndoto.

  • Vitu 9 ambavyo hupaswi kuchoka kufanya

    Katika maisha Kuna vitu hata iweje huwezi kusema umechoka kuvifanya. Huwezi kusema nimechoka kupumua, maana ykiacha kupumua tu huo ndio mwisho wako. Huwezi kusema nimechoka kula, wala huwezi kusema nimechoka kulala, kuanzia leo sitalala tena. Ni vitu vya asili ambavyo mwili wako unahitaji ili uendelee kuwa imara zaidi.

    Wewe pia Kuna vitu unapaswa kujiwekea utaratibu wa kuvifanya bila kuchoka. Ifuatayo ni orodha ya vitu ambavyo hupaswi kuchoka kufanya.

    1. Usichokwe kuweka akiba wala kuwekeza.

    2. Usichoke kusoma vitabu maana vutakusaidia kuongeza maarifa, ufahamu na kipato.

    3. Usichoke kusamehe maana kutosamehe kunakuumiza wewe mwenyewe.

    4. Usichoke kuongeza kipato chako.

    5. Usichoke kutengeneza bidhaa bora zaidi

    6. Usichoke kutoa huduma nzuri

    7. Usichoke kushukuru

    8. Usichoke kusema ukweli

    9. Usichoke kuisimamia ndoto yako.

    Rafiki yangu, hivyo ni baadhi ya vitu ambavyo hupaswi kuchoka kuvifanya. Unaweza kuongeza vingine zaidi.

    Je, umeshapata vitabu vipi vya kwangu vya kiswahili.

    Chagua vitano Leo kwa elfu kumi tu.

    Ingia hapa uchague 

    https://www.getvalue.co/home/seller_collection/393

    kisha ulipie elfu kumi kupata vitabu hivyo vitano.

    Lipia kwa Airtel money 0684 408 755 jina ni GODIUS RWEYONGEZA

  • FANYA UNACHOPENDA

     

    Mara nyingi watu hupenda kufanya kazi fulani kwa sababu aidha ya kifedha au kutafuta umaarufu au pengine kwa kulazimishwa na wazazi.

    Lakini kazi hizi huwa hawazifanyi kutoka moyoni au Wala huwa haziwapi motisha. Ni muhimu sana ufanye kitu unachopenda kuliko kulazimisha au kulazimishwa kufanya kitu usichopenda.

    Kama ni fedha au umaarufu utaupata kwa kufanya usichopenda, ila ndani mwako utakuwa unahisi kama kuna kitu hakiko sawa mara zote. Na kitu hiki kikiendelea kwa muda mrefu utajikuta ukiishi kama vile huishi. Yaani, utakuwa mtupu.

    Ndiyo maana Benjamin Franklin aliwahi kusema kwamba kuna watu wanakufa wakiwa na miaka 25 na kuzikwa wakiwa na miaka 75. Mojawapo ya kitu kinachowafanya watu wafe wakiwa na miaka 25 ni kwa sababu wanafanya kitu wasichopenda. Hivyo, wanapita tu kwenye maisha wakiwa wanafanya kazi au kitu ambacho hakiwapi ukamilifu wa ndani.

    Kazi ya kufanya leo. Tafuta kitu au kazi unayopenda na Anza kufanya hiyo. Inaweza ikawa haikulipi vizuri leo ila baada ya muda itaweza kukulipa vizuri kwa sababu utakuwa unaifanya kutoka moyoni tena kwa nguvu na akili zote.

    Kazi usiyoipenda utaifanya sawa, lakini inaweza kwa kuwa haitoki moyoni, ufanisi kwenye hiyo kazi utakuwa ukipunguka kidogo kidogo bila ya wewe kujua. Mwisho wa siku utajikuta  umeingia pabaya.

    GODIUS RWEYONGEZA

    0755848391

    Morogoro-Tz

  • Kitu hiki lazima tu kitokee maishani mwako

     

    Kuna vitu katika maisha lazima tu vitokee. Vinatokea uwe unavipenda au huvipendi. Vyenyewe vinatokea tu.


    Jua linachomoza na kuzama, bila kujali unapenda au hupendi.
    Dunia inajizungusha kwenye mhimili wake, bila kujali una chuki nayo au unaipenda.
    Ukiruka juu, sharti utarudi chini bila kujali unapenda au hupendi.

    Mojawapo ya kitu kingine ambacho lazima kitokee kwenye maisha ni mabadiliko. Uwe unapenda au hupendi mabadiliko lazima tu yatatokea.

    Ndio maana unaona kila zama huwa zina matajiri ambao huwa wanatengeneza mabilioni ya fedha ya kutumia fursa ya mabadiliko fulani vizuri.

    Mansa Musa alikuwa tajiri mkubwa kuwahi kutokea duniani kwa sababu alitumia fursa ya kuuza chumvi na dhahabu enzi zake vizuri. Unaweza kushangaa chumvi?!! Ilimtajirishaje mtu?? Ukweli ni kwamba kipindi chake chumvi ilikuwa dili kubwa Kama ambavyo miaka ya 1800 viwanda vilikuwa dili kubwa pia.

    Kitu Kikubwa ninachotaka ni wewe kuhakikisha unasoma mabadiliko na kuyatumia kwa manufaa.

    Ni hayo tu
    NAKUKUMBUSHA TU. Kama hukupata nakala ya kitabu cha MAiSHA NI FURSA: ZITUMIE ZIKUBEBE kwa elfu sita tu (6,000/-) changamka utumie fursa hii leo hii. Kuanzia mwezi ujao kitabu kitarudi kwenye bei yake ya elfu kumi.

    Hivyo kipate Leo kwa elfu sita tu. Cha kufanya Sasa. Tuma elfu sita (6,000/-) kwa MPESA 0755848391 au Airtel money 0684 408 755
    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA.

    CHANGAMKA SASA.

  • Madhara Ya Kuwa Na Mahusiano Na Mtu Zaidi Ya Mmoja

     

    Kama una ndoto kubwa na umekuwa na mpango wa kuja kuwa na mahusiano na watu wawili, au tayari una mahusiano na watu wawili ni bora ukauhairisha au kuondoa kabisa huo mpango. Yafuatayo ni mdhara ya kuwa na mahusiano na zaidi ya mtu mmoja.

    Kwanza utapoteza nguvu zako nyingi kwa watu hao ambao umeingia nao kwenye mahusiano. Hizi ni nguvu ambazo ungeweza kuzitumia kufanya kazi zako za maendeleo.

    Pili, utapoteza muda wako ambao ungeweza kuutumia kufanikisha NDOTO zako.

    Tatu, utapoteza fedha ambazo zingekusaidia kufanikisha NDOTO zako kubwa. Na kama unavyojua muda ni mali.

    Hayo ni madhara ya kuwa na mahusiano na zaidi ya mtu mmoja. Epuka kitendo hiki kwa nguvu zako zote.

  • Kitabu cha KUTOKA UMASIKINI MPAKA MAFANIKIO CHA ERICK SHIGONGO.

    Kwenye kitabu hiki Erick Shigongo ameeleza historia ya maisha yake na kutoa mafunzo kadha kadha kuhusu maisha

    Kitabu hiki ni kizuri sana, nashauri kila mwenye kiu ya mafanikio makubwa akisome. Utajifunza mengi kuhusu kutoka umasikini mpaka mafanikio makubwa kupitia stori ya Erick Shigongo ambaye maisha yake yalikuwa duni sana, kuliko hata wewe ila akaweza kupasua anga na kufikia viwango vikubwa.

    Utajifunza na kuona ni kwa jinsi gani na wewe unaweza kufanikiwa pia kupitia mbinu mbalimbali alizoshirikisha mwandishi huyu.

    Moja ya kitu ambacho nakikumbuka sana kutoka kwenye kitabu hiki ni kauli inayosema kwamba; Kuna watu kwa tabia zao wataendelea kuwa masikini na Kuna watu kwa tabia zao hata waukimbie utajiri, utazidi kuwafuata tu.

    Leo nimeona nikushirikishe hili ili na wewe ujitathimini tabia zako. Hivi ni kweli wewe ukiamua kuukimbilia utajiri utakufuata kweli au utaendelea kuwa masikini tu kutokana na tabia zako?

    Jiulize una tabia gani. Na je, hizo tabia zinakupeleka wapi?

    Soma zaidi:

    Watanzania Tujenge Utaratibu Wa Kukubali Vitu Vyetu.


    UCHAMBUZI WA KITABU CHA SUGU; MAISHA NA MUZIKI. Mambo 14 niliyojifunza kwenye kitabu hiki kinachoeleza Maisha ya Sugu Kutoka Mtaani Mpaka Bungeni

     

    Kila la kheri.

    GODIUS RWEYONGEZA
    Morogoro-Tz

  • Fursa iliyotengeneza mabilionea kwenye karne ya 21

     

    Madalali ni watu ambao wamekuwepo kwa siku nyingi sasa. Kazi yao kubwa imekuwa ni kuunganisha eneo moja lenye bidhaa na jingine lenye uhitaji.

    Kama una uhitaji wa chumba cha kupanga unamwona dalali anayekuunganisha kilipo.

    Kiufupi wenyewe wamekuwa wanaingia katikati ya mlaji na mzalishaji.

    Kwenye karne ya 21 udalali ndio umetengeneza mabilionea kwa wingi. Mtandao wa amazon na alibaba ni ya kidalali inayounganisha  kati ya wazalishaji na walaji wa mwisho wa bidhaa.

    Mtandao wa Uber ni wa kidalali pia. Unaunganisha kati ya wenye teksi na wasafiri.

    Google pia ni mtandao wa kidalali, unaunganisha mwenye taarifa na mwenye uhitaji nazo.

    Ukiangalia mitandao yote hiyo imetengeneza mabilionea wakubwa. Hivyo, kwenye karne hii ya 21 ukitaka kuwa bilionea, basi kuwa dalali wa kidigitali. Unganisha watu na huduma wanayoihitaji.

    Kila la kheri.

    Umeshapata kitabu cha MAiSHA NI FURSA: ZITUMIE ZIKUBEBE

    Kama bado fanya hivi, tuma elfu sita (6,000/-) kwa 0755848391 jina ni GODIUS RWEYONGEZA Sasa ili upate kitabu hiki cha kipekee sana.

X