Home


  • Aina Tano (05) Za Ujuzi Unazohitaji Ili Kuwa Milionea Kwenye Ulimwengu Wa Leo

    Kwenye makala niliyotuma kwa watu wa nguvu ambao huwa wanapokea makala zangu kwa njia ya email jana. Niliandika kwamba zama zimebadilika na wewe unapaswa kubadilika. Kama hujajiunga na mfumo wetu wa kupokea makala kwa njia ya barua pepe nina hakika huo ujumbe hukuuona,  hivyo, leo nimelazimika kuuweka huo ujumbe kwenye blogu yetu hapa ili na wewe uweze kuuona na kikubwa zaidi ni kwamba uweze kunufaika nao. Hivyo unaweza kuusoma kwa kubonyeza hapa rafiki yangu.

    Sasa baada ya jana kukwambia kwamba zama zimebadilika, basi leo nataka nikwambie aina saba za ujuzi unaopaswa kuwa ili uweze kutoboa kwenye ulimwengu wa leo ambao umebadilika sana.

    SOMA ZAIDI: Vitu Viwili Ambavyo Havitapitwa na wakati kwenye zama hizi

    Unashangaa ee!

    Usishangae! Unapaswa kuzoea kitu hiki, kwa sababu ulimwengu wa leo umebadilika sana. Kwenye uliwengu wa leo umilionea ni neno ambalo unapaswa kulitumia sana, na hata wewe unapaswa kupambana sana kuhakikisha kwamba unaufikia walau umilionea kama siyo ubilionea.

    Sasa ujuzi huu ndiyo utakufanya wewe utobe.

    1. Ujuzi wa kuongea mbele ya watu wa  kuwasilisha mada au kitu unachofikiria

    kuna watu wengi wana vitu vizuri sana ndani yao. ila vitu wanashindwa kuvifikisha kwa watu kutokana na kukosa ujuzi sahihi wa kuwasilisha kile walichonacho. Naomba unisikilize mimi kwenye hili. Kwenye uliwengu wa leo unahitaji sana ujuzi wa kuongea mbele ya watu.

    Hata kama umeajiriwa. huu ujuzi ni muhimu kwako, maana ujuzi huu pekee tu unaweza kukufikisha kwenye umilionea. Dunia ya leo bado inawapenda sana watu ambao wanaweza kusimama mbele ya watu na kuwasilisha mada kwa namna ambayo inaeleweka.

    Naamini, wewe ni kama mimi huwa hupendi mtu anayesimama mbele ya watu kuongea na kuanza kumung’unya maneno. Au mtu anayesimama na kuwasilisha mada kama vile anaogopa dunia itammeza.

    Huwa siwapendi watu wa aina hii. Ila ukifuatilia wengi ambao huwa wanaoongea mbele ya watu, huwa wanaongea kwa namna ya kipumbavu kama hii.

    Rafiki yangu, unahitaji kujitofautisha. Kuanzia leo hii anza kujenga ujuzi wa kusimama mbele ya watu na kuongea. Uongee na watu wawe na shauku ya kukusikiliza wewe ukiongea. Siyo unaongea mpaka unaboa watu wanaanza kutafuta simu zao ziko wapi ili wachati.

    huu ni ujuzi ambao haufundishwi shuleni, ila ni ujuzi ambao unahitaji kujifunza ili uweze kula mema yanchi. Nakwambia rafiki yangu, kamwe, usije ukafanya kosa la kuishi bila ya huu ujuzi.

    anza leo kujifunza ujuzi huu baada ya kusoma hapa. Kuna kozi kibao mtandao ambazo unaweza kusoma na zikakusaidia kupata ujuzi huu. Ukweli ni kwambaa kama kuna ukomo ambao utakuzia, basi utakuwa ni ukomo ambao umejiwekea mwenyewe.

    2. ujuzi wa kuanzisha na kusimamia na kukuza biashara

    Huu ni ujuzi ambao unauhitaji rafiki yangu. kwenye ulimwengu wa leo kuwa na biashara ni moja ya hitaji la muhimu sana.

    Najua unaweza kuwa unasema kwamba ajira peke yake inanitosheleza.

    Ninachotaka kukwambia ni kwamba kama unataka kufikia kiwango cha  kuwa na fedha ambacho kitakupa uhuru. Basi kuwa na biashara ni lazima.

    Ni kweli ajira inakupa kipato. Ila nina  uhakika kipato chako hakiwezi kuwa kikubwa sana kiasi cha kukufanya uweze kufurahia mambo mengine matamu yaliyo kwenye hii dunia.

    Lakini pia kipato cha ajira pekee, nina hakika hakitoshi kukufanya wewe uweze kuwekeza na kufanya mambo mengine ya kipekee.

    Kwa Tanzania, asilimia kubwa ya wafanyakazi wanalipwa chini ya milioni moja kwa mwezi. Hiki kiasi kinaweza kukutosha tu kula, kunywa na kufanya mambo mengine ya kawaida. Ila hakiwezi kukutosha wewe kufanyia kazi ndoto zako mpaka kuweza kuzifikia. Na hapa ndiyo maana, unahitaji kuwa na biashara

    Ubora wa biashara ni kwamba inaweza kukupa kipato kisicho kuwa na kikomo.

    Kadiri utakavyoweka juhudi kubwa kwenye biashara yako ndivyo ambavyo utaweza kuongeza kipato chako zaidi.

    Kwa hiyo nakushauri rafiki yangu uweze kuanzisha biashara. Hata kama ni kijibiashara kidogo, anza na hicho.

    Kama umeajiriwa, tumia muda wako wa ziada baada ya kutoka kazini au kabla ya kwenda kazini kwa ajili ya kufanyia kazi biashara yako.

    Rafiki, usiridhike na hayo maisha. Maisha yanabadilika kila kukicha. Hivyo, kwa vyovyote vile, pambana kuhakikisha kwamba unaanzisha hata kijibiasahra kidogo ambacho kitakupa kipato bila ukomo.

    SOMA ZAIDI:

    Tatu jifunze ujuzi ambao unaweza kukuingizia kipato cha milioni moja na zaidi

    Kama nilivyoandika kwenye makala ya jana. Kuna aina fulani za ujuzi kwenye ulimwengu wa leo ambao ukiwa nao, unaweza kukuingizia kipato cha milioni  moja na zaidi. na hii syo kwa mwezi, siyo kila baada ya siku mbili au tatu. Bali ni kwa siku moja. aina hizi za ujuzi zipo rafiki yangu, chagua aina walau moja ya ujuzi wa aina hii kisha anza kuujenga.

    Kabla sijakupa mifano ya aina  hii ya ujuzi nataka wewe mwenyewe uweze kutafakari kuhusu watu ambao unawafuatilia sana kwenye mitandao ya kijamii.

    Hivi watu wa aina hii ni wapi? Wana kitu gani ambacho kinakufanya uwafuatilie. Ukifuatilia kwa umakini utagundua kuwa baadhi ya hawa watu wana huo ujuzi ndio maana hata wewe unawafuatilia. Inawezekana ni ujuzi wa kuongea mbele ya watu na kuwasilisha mada zao kwa ustadi wa hali ya juu sana, inawezekana ni ujuzi wa kuandika, inawezekana ni ujuzi wa kuuza, unaweza pia kuwa ni ujuzi kuunda timu sahihi ya watu, unaweza kuwa ni ujuzi wa kung’ang’ania kitu kimoja mpaka kieleweke au ujuzi wa kuburudisha.

    Kwa vyovyote vile ebu na wewe chagua ujuzi wako ambao unataka kuwa nao maishani. Kisha anza kuujenga.

    Tena unaweza kuwa aina mbli za ujuzi na kuziunganisha na kuwa kitu kimoja. Hiki kitu kitalaamu kinaitwa skill sexing au idea sexing. Unaweza kukisoma zaidi kwa kubonyeza hapa

    SOMA ZAIDI: Kitu kimoja ambacho watu hawajui kuhusu uwekezaji

    Nne, jifunze kusema hapana kadiri uwezavyo

    Huu ni ujuzi ambao unapaswa kuwa nao pia. Maana kama utafuata mbinu ambazo nimekueleza hapa, muda siyo mrefu wewe utakuwa ni mtu wa viwango vingine. muda siyo mrefu kila mtu atakuwa anahitaji muda wa kuwa na wewe.

    Sasa hapa, unahitaji kuwa bahili wa muda wako. Unakuwa bahiri siyo kwa ubaya bali kwa uzuri. Ili uweze kuwekeza muda wako kwenye kufanya kazi za maana kwako na kuachana na kazi ambazo hazikujengi wala kukuongezea kitu chochote.

    Kwa hiyo, kama unataka kuujenga umilionea, jifunze kusema hapana nyingi kwa vitu ambavyo siyo vya muhimu kwako na vitu mbavyo havikusogezi wewe kwenye kufanikisha lengo lako. Badala yake wekeza muda wako huo kwenye kufanyia kazi malengo na ndoto zako mpaka uweze kuzikifia.

    SOMA ZAIDI: Huyu Ni Mtu Ambaye Lazima Utamwambia Hapana

    Tano ujuzi wa kuwekeza

    Huu ni ujuzi mwingine ambao unauhitaji. Rafiki yangu unahitaji uwe na ujuzi wa kuwekeza ili uweze kutunza fedha zako unazopata kwa uzuri na kwa namna ambayo itakusaidia wewe kuendelea kukuza utajiri wako.

    Nimeandika zaidi kuhusu uwekezaji na hasa uwekezaji kwenye hisa kwenye kitabu cha maajabu ya kuwekeza kwenye hisa, hatifungani na vipande. Unaweza kukipata hicho kitabu kwa kufuata maelekezo haya hapa

    maelekezo ya kupata kitabu cha MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE haya hapa

    Au unaweza kuwasiliana moja kwa moja na +255 684 408 755 sasa.

    SOMA ZAIDI: 

    Najua kuwa ungependa kupata ushauri wa karibu zaidi moja moja kwa moja kutoka kwangu. Nitafute tuone ni lini nitakuwa na muda, ili nikupangie ratiba ya kuongea na wewe. Utalipia kiasi kidogo tu.

    Saa moja ni laki moja mazungumzo kwa njia ya mtandao.

    SAA MOJA NI LAKI MBILI NA NUSU MAZUNGUMZO YA ANA KWA ANA. Malipo yanafanyika kwanza, kisha unapewa tarehe (appointment) tutakapoweza kuongea

    Tumia namba ya simu +255 755 848 391 kuwasiliana nami.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza ambaye anaishi Morogoro nchini Tanzania.

    Unaweza kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza kupitia youtube channel yake hapa

    Kwa ushauri niandikie songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu ambavyo ameandika Godius Rweyongeza, wasiliana naye kwa +255 684 408 755 na orodha ya vitabu vyenyewe unaweza kuiona HAPA. Chagua unachopenda, kisha twanga,  +255 684 408 755

    Kujiunga na programu yetu ya uandishi. Wasiliana na +255 678 848 396

    For Consultation only: +255 755 848 391  au godiusrweyongeza1@gmail.com

  • ZAMA ZIMEBADILIKA: MAISHA YAMEBADILIKA PIA

    Leo kwenye status ya moja za rafiki yangu aliweka picha ikionesha jinsi bei za vyakula zilivyokuwa chini siku za nyuma. Unaweza kuona mwenyewe picha yenyewe hapa👇🏿👇🏿

    Ukiangalia hapo utagundua bei zilikuwa chini kweli!
    Maziwa yalikuwa shilingi 100. Bei ya maji ya kandoro kwa sasa 🙈! Sijui maji ya kandoro kipindi hicho yalikuwa yanauzwa shilingi ngapi🤔.

    Au basi..

    Kitu kikubwa ninachotaka kukwambia leo ni kwamba Zama Zimebadilika! Na bado zitazidi kubadilika.

    Wewe pia unapaswa kubadilika.

    Najua wengi wanapenda mabadiliko ila ambao wako tayari kuchukua hatua kupata hayo mabadiliko ni wachache sana, yaani, wachache mno.

    Kitu cha kufahamu ni kuwa mabadiliko kwenye maisha lazima yatatokea.
    Wewe unapaswa kuwa sehemu ya mabadiliko hayo.

    Na njia nzuri ya kufanya mabadiliko Ni kutumia nguvu ya vitu vidogo.

    Hii Ni falsafa kubwa ambayo nimeeleza kwenye kitabu changu cha NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA.

    …..njoo ujipatie nakala ya kitabu hiki. Nina hakika hutajutia maishani mwako.

    Uwekezaji wa kitabu hiki ni moja ya uwekezaji wa kipekee ambao unaweza kuufanya.

    Ukiitumia NGUVU hii ya VITU VIDOGO hakuna ambacho kitakushinda hapa duniani.

    Ebu chukua hatua leo. Upate nakala yako leo rafiki yangu.
    Nakala moja gharama take Ni 20,000/-

    Tuma fedha Sasa kwa 0755848391 jina ni GODIUS RWEYONGEZA

  • Hivi Ndivyo Tunaweza Kufanya Biashara Za Kitanzania Zikue Zaidi

    Kwa Dakika moja Tu Leo Nataka Nikwambie Ni Kwa Namna Gani Unaweza Kufanya Biashara ya Rafiki Yako Ikue Zaidi Na Zaidi Ya Ilivyokuwa Mwanzo.

    Njia hii ni kununua kwake. Hii ndio njia bora nay a kipekee sana. Maana kwa jinsi hiyo utamfanya mwenye biashara apate kipato cha kumwezesha kuikuza biashara yake

    Kwa hiyo badala ya kukaa kwenye kikjiwe na kupiga majungu. Badala ya kumakatisha tamaa mpambanaji, ebu sikiliza, nenda kanunue kwake. Hicho ni kitendo cha kiungwana ambacho unaweza kufanya na kufanya biashara ya rafiki yako ikue.

    Ifikie hatua watu tuache kuagiza bidhaa kutoka nje ya nchi. Tununue bidhaa kutokea hapahapa kwetu. Na njia ya kufanya hivi ni kumsapoti mwezako anayefanya kitu kizuri

    Ni hivyo tu.

    Kama umeilewa hii makala basi nenda kamsapoti mwenzako badala ya kupiga majungu.

  • Kitu Kimoja Cha Kufanya Unapokutana Na Watu

    Unaendeleaje rafiki yangu mpendwa. Siku ya leo ningependa tujadili kitu kimoja cha kufanya unapokutana na watu. Kitu hiki ni kubadili maisha yao na Kuyafanya kuwa bora zaidi kuliko ulivyowakuta.

    Yaani, kuwainua na kuwafanya wajisikie vizuri ZAIDI Kuliko pale walipokuwa hawajakutana na wewe.

    Hii Ni moja sifa ya viongozi na watu wote WALIOFANIKIWA.

    Kwa hiyo kila ukikutana na mtu, angalia ni kitu gani unaweza  kufanya kumwacha bora zaidi ya vile ulivyokuta mwanzoni?

    Kuwa sehemu ya kusambaza upendo,  na furaha. Kuwa mtu wa kuhamasisha watu. Kuwa mtu wa kuwaacha watu Bora ZAIDI ya vile ulivyokuta. Hivi ndivyo viongozi wote wakubwa wanavyofanya.

    Ukikutana nao unapata hamasa ya kwenda kufanya kazi kwa ubora ZAIDI.

    Siyo kwamba wanakukatisha tamaa.
    Siyo kwamba wanakufanya ujisikie wa chini Kuliko wao. Bali wanakuwa nyuma yako kuhakikisha kwamba wanakusuma uende mbele zaidi.

    Kila la kheri.

  • App mbili ambazo kila mfanyabiashara anapaswa kuwa nazo

    Kuna app mbili ambazo kila mfanyabiashara anapaswa Kuwa nazo.

    1. Thl accounting
    Hii inakusaidia kutunza hesabu zako zote za biashara. Na bidhaa ZAKO zote ulizonazo kwenye Biashara yako, itakuonesha bidhaa zinazokaribia kuisha au zilizoisha, itakusaidia kutengeneza invoice, itakusaidia kutunza hesabu za mauzo, mapato mpaka matumizi.
    Hata Kama uko mbali bado unaweza kuona mwenendo wa  biashara yako. Kitu hiki Ni muhimu Sana kwako wewe mfanyabiashara.

    Rafiki yangu, hii ni moja ya app ambayo nakushauri Sana uwe nayo kwenye biashara yako. Itakusaidia kufanya mengi kwa manufaa.

    2. Beem
    Hii inakusaidia kutuma SMS kitalaam. Yaani, unatuma sms zenye jina la biashara. Kama umewahi kuona SMS za voda, Tigo au halotel wanazotuma. Sms ambazo huwa zinakuja kwa msomaji Ila hawezi kujibuoja kwa moja. Badala yake unaweza kumwekea link au namba ya kujibu. Kama hii hapa

    Hii Ni muhimu kwako mfanyabiashara.
    Kwanza utafanya biashara yako ionekane kitalaamu zaidi.

    Lakini pia utafanya wateja wakuamini. Kuna wateja wakiona tu kuwa unaweza kutuma jumbe za aina hiyo, watashawishika na kuona wewe unawafaa zaidi.

    Unaweza kuwatumia wateja SMS za kuwajulia Hali
    SMS za kuwakaribisha kununua
    Ofa za sikukuu na kawaida
    Mzigo mpya unaposhuka
    N. K.

    Hizo ndizo app mbili ambazo ni lazima kila mfanyabiashara awe nazo.

    Kama ungependa kujifunza zaidi namna bora ya kuzitumia, Basi usisite kuwasiliana nami kwa 0755848391

    Karibu sana.

  • Ni makosa Yapi Kati Ya Haya Matatu Umewahi Kuyafanya Maishani Mwako?

    1. Kuwa na wazo la BIASHARA au uwekezaji Ila ukachelewa na baadaye watu wengine wakalifanyia kazi

    Umewahi Kuwa na wazo la BIASHARA ambalo ulikuwa ukifikiria kulifanyia kazi Ila ukachelewa kulifanyia kazi. Baadaye likafanyiwa kazi?

    2. Kuweka Mipango mikubwa mwanzoni mwa mwaka ambayo hukuwahi kufanyia Kazi?
    Au labda umewahi Kuwa na mpango mkubwa sana, mwanzoni mwa mwaka. Mpango  wa kuanza kusoma
    Mipango ya kupanda miti
    Mipango ya Kujenga n.k Ila hukuwahi kuifanyia kazi?

    3.  Kuwa na kazi kubwa ambayo ulisubiri kuifanya siku ya mwisho.

    Au pengine umewahi kupewa kazi ya kufanya ofisini, ukaisubirisha mpaka siku za mwisho mwisho ndio ukaja kuifanya na baadaye ukawa uneifanya hovyo.

    Kama umewahi kufanya kosa lolote hapo na kama bado Kuna kosa unafanya hapo, maana yake umekuwa unasubiri kufanya kitu kikubwa kwa wakati mmoja. Yaani, umekuwa unasubiri ufanye kitu kwa mapinduzi badala ya kufuata mfumo wa mageuzi.

    Unajua mapinduzi ni Nini.

    Mapinduzi ni mabadiliko ambayo huwa yanatokea ndani mfupi Sana. Yanaweza kuchukua sekunde, dakika au siku chache. Ila yakitokea huwa yana tabia ya kurudiwa tena.

    Ila mageuzi kwa upande mwingine huwa yanachukua muda. Miaka na miaka. Ila yakitokea, huwa yametokea na huwa hayarudi nyuma.

    Sasa wewe kwenye maisha yako unahitaji mageuzi. Kufanya vitu hata kama ni kidogokidogo bila ya kurudi nyuma. Na hapa ndipo unahitaji mwongozo wa kitabu cha NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA.

    Hiki kitabu kimeeleza kwa kina, namna unavyoweza kuitumia NGUVU Hii ya VITU VIDOGO kufanya MAKUBWA.

    Hakikisha unapata nakala yako leo hii. Nakala moja ya kitabu hiki ni 20,000/- tu.

    Na unatumiwa popote pale ulipo duniani.
    Audiobook na softcopy pia vipo.
    Fanya malipo kwa 0755848391 Sasa ili utumiwe  nakala yako.

    NAKUKUMBUSHA TU: Endapo hutachukua hatua ya kupata kitabu hiki cha NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA miaka mitano ijayo utakuwa unaendelea kufanya makosa hayahaya Tena kwa kuyarudia.

    Na hicho kitu ndicho Albert Einstein alikiita ujinga pale aliposema, “ujinga Ni kurudia kufanya Mambo yaleyale huku ukitegemea kupata matokeo ya tofauti.”

    Chukua hatua sasa. Pata nakala yako kwa elfu 20,000 tu. Tuma fedha kwa namba 0755848391

    Umekuwa nami
    Godius Rweyongeza
    Morogoro-Tz
    +255755848391

    Karibu sana

  • Njia hii itakusaidia kufanya majukumu yako kwa mwendelezo na kuchana na kughairisha (Seinfeld Calendar)

    Nadhani imewahi kukutolea maishani kwamba unapenda kuanzisha kitu na kukifanyia kisha baada ya muda kidogo unaachana nacho. Au baadaye unaanza kujiambia kwamba nitakifanya kesho au wiki ijayo.

    SIKU ya leo Nina mbinu ambayo inafahamika kama  Seinfeld Calendar.
    Kuifahamu Seinfeld Calendar ngoja kwanza tujue  Seinfeld mwenyewe alikuwa nani kiufupi.

    Huyu alikuwa ni mwigizaji ambaye kwa miaka mingi alikuwa akitengeneza maigizo yaliyokuwa yanakonga nyoyo za watu. Watu walishangaa kwa nini alikuwa hashuki kwenye chati.

    Sasa SIKU moja ndipo alipoeleza hii Siri take ya mafanikio. Akisema kwamba, Siri kubwa ya mafanikio yake ni kuwa huwa anaandika maigizo kila SIKU. Kadiri anavyoandika ndivyo anapata hamasa na mawazo mapya ya kuigiza kila SIKU.

    Aliendelea kwa kusema kwamba yeye huwa ana kalenda kubwa ambayo huwa anaiweka chumbani kwake au sehemu yoyote ambapo inaonekana. Halafu anakuwa na mark pen kubwa nyekundu.  Kwenye kalenda  anaweka  X kubwa SIKU ya mwisho ambayo anataka igizo lake liwe limekamilika.  Halafu anaanza kulifanyia kazi Sasa.


    Kila siku anapofanya kazi anaweka X kubwa. Muda siyo mrefu anakuwa ameweka X nyingi, kiasi kwamba mchakato wake unakuwa Ni kupongeza X ZAIDI kwenye kalenda. Anasema kadiri inavyokaribia siku ya mwisho ya kukamilisha jukumu, ndivyo anakuwa anajisukuma zaidi ili kukamilisha jukumu husika. Huku akifurahia mchakato wa KUWEKA X ZAIDI kwenye kalenda.

    Rafiki yangu, una jukumu kubwa? Unataka liwe limekamilika Mpaka siku gani? Basi chukua kalenda leo. Weka X kwenye tarehe ambapo ungependa kukamilisha jukumu lako. Kisha anza kulifanyia kazi kuanzia Leo ukiweka X moja baada ya nyingine.

    Kila la kheri
    Godius Rweyongeza (songambele)
    0755848391
    Morogoro

  • Kama Wewe Ni Mpenzi wa Kuandika kwenye Status Za WhatsApp Basi Leo Kuna kitu Nataka Nikwambie.

    Siku hizi imekuwa ni rahisi kuandika mtandaoni. Status za WhatsApp, Facebook na maeneo mengine.

    Kitu hiki kinawafanya watu waandike jumbe fupi Ila nzuri ambazo huwa zinapotea baada ya muda.

    Kwa mfano, mtu anaandika status ya WhatsApp, lakini  inapotea baada ya saa 24. Ule ujumbe wake mzuri alioandika unapotea na hauonekani Tena. Na wengi wanaoandika kwenye status huwa hawatunzi kumbukumbu za kile walichoandika. Kwa hiyo baada ya mwaka akitaka kurejea alichoandika mwaka mmoja uliopita. Kinakuwa hakipo! Halafu eti ninasema baada ya mwaka. Mwaka wote huo.
    Hata baada ya saa 24. Ebu fikiria jumbe nzuri ngapi zinapotea tu kama upepo kila siku. Jumbe ambazo watu wanaweka WhatsApp na bado hazimnufaishi mtu yeyote.

    Kama wewe ni mpenzi wa kuandika kwenye status za WhatsApp Basi leo Kuna kitu nataka nikwambie.

    Unaonaje badala ya kuandika jumbe zako hizo nzuri na kuziweka WhatsApp tu Ambapo zinapotea baada ya saa 24 ukiziweka  sehemu Ambapo hazipotei Kama kwenye blogu.  Unaweza hata kutengeneza blogu ya bure mtandaoni. Ukawa unaziweka  huko kwa ajili  ya kumbukumbu ya baadaye.

    Unaonaje badala ya kuandika status fupi za WhatsApp ukiandika makala ndefu ya kuweka kwenye blogu, halafu ukatoa kipande tu cha kuweka status Kama kawaida yako.

    Unaonaje ukiendeleza jumbe zako fupi na kuzifanyia KUWA kitabu?
    Siyo kwamba huwezi kuandika kitabu. Unaweza vizuri tu, Mimi nina hakika ukijumuisha status zako zote ambazo umekuwa unaandika whatsap kwa miaka sasa, utakuwa umeshaandika kitabu kikubwa. Sasa kwa nini usiamue kuanzia hapa kuandika kitabu chako.

    Nina uhakika Kati ya wote watakaosoma ujumbe huu, wengi wataupuuzia, mmoja ataufanyia kazi na baada ya mwaka atatoa kitabu chake. Na nitamwandika  hapa jamvini. Sasa kwa nini mmoja huyo asiwe wewe?

    Ebu chukua HATUA.
    Najua utakuwa unakwama kwa kujiuliza, nawezaje kuanza kuandika kitabu? Jibu ni rahisi sana. Hakikisha unapata kitabu cha NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA (Hardcopy) na kitabu cha JINSI YA KUWA MWANDISHI MBOBEVU (softcopy). Kuvipata hivi Vitabu wasiliana nami kwa 0755848391

    Hivi vitakupa mwongozo wote unaouhitaji.

    Kila la kheri.

  • Hiki ni kitu ambacho unapaswa kukitafuta kwa nguvu zako zote

    Ni kitu gani hiki….
    Ni kutafuta kuwaelewa wengine kabla ya kutaka kueleweka.

    Kwenye maongezi ya kila siku kila mtu huwa anapigana kuhakikisha kuwa anaeleweka kwenye kile anachofanya.

    Hiki kitu tu huwa kinasababisha ubishi mkubwa. Ninachotaka kukwambia leo ni kwamba tafuta kuwaelewa wengine kwanza kabla wewe hujaeleweka. Hilo litakusaidia sana maana ukishajua upande mwingine unataka nini itakuwa rahisi kwako kuweza kuwasilisha hoja yako na kuongea nao  waweze kukubaliana na wewe.

    Hilo ndilo Jambo la msingi na KUBWA Sana ambalo unapaswa kupambania kila mara. Maana watu wengi huwa wanapenda kueleweka wao kwanza wakiwa hawataki kuwaelewa wengine. Sikiliza, kama hujawaelewa wengine, hata ukishinda kwenye mjadala bado ushindi wako haitakuwa wa maana. Hivyo Mara zote tafuta kuelewa watu kwanza kabla ya kueleweka.

  • Business to Business (B2B) Ni Nini?

    Business to business ni mfumo wa BIASHARA unaofanyika kati ya Kampuni na Kampuni au kati ya BIASHARA moja na nyingine.

    Yaani, Kampuni inatengeneza bidhaa kwa ajili ya kuuza kwa Kampuni nyingine na siyo kwa walaji wa mwisho.

    Kampuni nyingine zinaweza kuwa na bidhaa za aina mbili. Bidhaa moja ya kuuza kwa walaji wa mwisho na bidhaa nyingine kwa kampuni nyinginezo.

    Au bidhaa moja inaweza kuuzwa kwa watu kwa bei tofauti. Walaji wa mwisho wakauziwa kwa bei ya juu kidogo wakati biashara au kampuni ikiiuziwa kwa bei ya chini.

    Mfano bidhaa ya inayouzwa elfu ishirini kwa walaji wa mwisho inaweza kuuzwa elfu kumi na tano au chini kwa biashara nyingine.

    Hiyo ndiyo business to business (B2B)

X