-
Usiache Kufanya Mazuri Kwa Sababu Umezungukwa Na Watu Wanafanya Mabaya
Kama umezungukwa na watu ambao wanafanya vitu ndivyo sivyo. Usikubali kuachana na tabia yako nzuri na kuanza kufanya vitu ambavyo havieleweki. Mara zote na sehemu zote hakikisha kwamba unafanya mazuri hata kama umezungukwa na watu ambao wanafanya vitu vibaya..
Usikubali kuwa sehemu ya kuendeleza ubaya. Badala yake sambaza upendo wa kufanya mazuri.
Unaweza usione matokeo ya kile unachofanya kwa muda mfupi. Ila uhakika ni kwamba baada ya muda matokeo hayo unaenda kuyaona.
Kwa hiyo endelea kuonesha wema wako.
Asili huwa huwa haisahau. Siyo kwamba utafanya mazuri na yatasahaulika. Hapana, hayo mazuri kuna watu wanaona hata kama watakuwa ni wachache. Na hata kama wengine watajidai kama hawaoni, ila watakuwa wanaona.
Kuna siku utapata matokeo ya mbegu zako hizi za wema unazopanda.
-
Hivi Ndivyo Na Wewe Unaweza Kuandika Kitabu Historia Ya Maisha Yako Kama Sugu
Miongoni mwa watanzania ambao wameandiaka vitabu vya historia ya maisha yao ni Sugu. Kitabu chake kinaeleza historia ya maisha yake kuanzia alipozaliwa mpaka anaingia bungeni mwaka 2010. Kina mambo mengi mzuri na ya kujifunza kwelikweli. Nashauri kama hujasoma kitabu cha Sugu, kinachoitwa Maisha na muziki ukisome. Utajifunza mengi sana ndani ya hiki kitabu. Tunaweza pia kuwasiliana kwa 0755848391 ili nikutumie nakala ya kitabu chako kwa bei chee tu.
Sasa baada ya kusema hayo tuone ni kwa namna gani wewe pia unaweza kuandika kitabu cha kwako.
Watu wengi wanafikiri kwamba kuandika kitabu kikubwa na kizuri kama hicho basi ni kazi kubwa. Hapana. Kuna njia mbili za kuandika kitabu kama hicho.
Kwanza ni kuanza kukiandika kidogo kidogo. Yaani, unakiandika hatua kwa hatua. Kwa mfano leo hii, tena sasa hivi unaweza kuamua kuanza kuandika historia ya maisha yako kwa kuandika jina lako na sehemu ulipozaliwa. Kesho ukaongeza kitu kingine kwa kuandika sehemu ulipokulia. Siku nyingine ukaandika namna ulivyosoma shule ya msingi. Siku nyingine ukaandika masomo uliyokuwa unapenda shule ya msingi. Siku nyingine ukaandika kuhusu ile siku uliyotoroka shuleni mwalimu akakuchapa.
Muda siyo mrefu utakuta kwamba kitabu chako kinazidi kusogea na mara kitabu chako kitakuwa kimeisha. Kitachukua muda kukikamilisha. Lakini nina hakika huu mchakato utaufurahia sana. kila siku utakuwa ukiandika maneno kidogo. Hata kama ni maneno 1000 tu, lakini utakuwa umeyaandika na yatakuwepo kwenye kitabu chako bila shida yoyote ile. Nashauri sana kama una mpango wa kuandika basi usisite kuanza kuandika sasa hivi, tena leo hii. anza tu hata kama ni kidogo
Bado huna uhakika ni kitu gani ambacho unaweza kufanya? Basi wasiliana name kwa 0755848391 ili niweze kukupa mwongozo na kukushikamkono wakati unaandika kitbu chako. Nimesaidia wengi wanaoandika vitabu vya historia ya maisha yao. Wewe unaenda kupata msaada pia. Karibu.
Njia ya pili ya kuandika kitabu cha historia ya maisha yako. Na hii ni kama uko bize tu. kama hauko bize tumia njia ya kwanza, itakufaa sana. Kwa njia hii ya pili, maana yake unatafuta mtu ambaye anaweza kukusaidia kuandika na kupangilia matukio ya kitabu chako. Unakuwa unawasiliana naye, na yeye anakusaidia kupangilia matukio ya kitabu chako mpaka kinakamilika.
Unampa taarifa kwa njia ya sauti.
Mnafanya mahojiano. Na hata anawahoji watu wako wa karibu kidogo, kisha anakusaidia kuandika kitabu kilichopangiliwa vizuri na kinachosomeka.
Hizo ndizo njia mbili unazoweza kutumia kwenye kuandika kitabu chako.
Kitu kimoja muhimu sana kwenye hili hapa ni kwamba unapaswa kuandika kitabu chako. Usikubali kuacha historia ya maisha yako bila kuandikwa kwenye kitabu. Kamwe usikubali kitu kama hiki kitokee kwenye maisha.
Historia ya maisha yako, itawanufaisha sana wanao mpaka wajukuu wako.
Kila la kheri.
-
Maswali Yanaoulizwa Mara Kwa Mara Kuhusu Semina Ya Uwekezaji Kwenye Hisa
Unaendeleaje mwekezji siku ya leo ningependa kujibu maswali ambayo watu wamekuwa wanauliza mara kwa mara kuhusu semina ya uwekezaji kwenye hisa?1. Semina itaendeshwa wapi?Semina itaendeshwa kwa njia ya mtandao kupitia kundi maalumu la whatasap. Na inaenda kudumu kwa siku 10 mfululizo. Yaani, kuuanzia tarehe 1.8.2022 mpaka tarehe 10.8.20222.Je, atakayehudhuria semina atajifunza vitu gani kwenye hii semina?Hii ni semina ya uwekezaji kwenye hisa. Hivyo, mtu yeyote ambaye atahudhuria hii semina atapata elimu yote ya msingi kuhusu uwekezaji kwenye hisa.Hiyo mwisho wa semina hii nategemea kuwa kila mshiriki
atakuwa anajua maana ya hisa, hatifungani na VIPANDE.
Viashiria vitakavyokuonesha kwamba hapa unapaswa kununua hisa au unapaswa kuuza hisa zako.
Atakuwa anajua namna ya kuchambua kampuni moja baada ya nyingine na hivyo kufanya uamuzi bora juu ya kampuni ya kuwekeza.
kila mshiriki atapata maelekezo ya kufungua akaunti ya kuwekeza na matarajio yangu kuwa kabla semina Haijaisha wengine watakuwa wameshaanza kuwekeza
kila mshiriki atajua namna ya kutumia simu yake katika UWEKEZAJI kwenye soko la hisa na vipande.
Atajua kuhusu mnada wa dhamana za SERIKALI na namna ambavyo anavyoweza kununua dhamana hizi.Halafu tutaona kati ya hisa, hatifungani kipi unaweza kuanza nacho na namna ya kutumia vitu vyote vitatu kutengeneza utajiri.3. Je, kuna vitu vingine ambavyo mtu akayehudhuria semina atapata.Ndio vipo. Sambamba na kuhudhuria semina hii ya kipekee unaenda kupata kitabu cha bure tena hardcopy ya kitabu cha JINSI YA KUWEKA AKIBA NA KUANZA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE.Hiki kitabu utakipata bure bila ya kuongeza gharama ya ziada.4. JE, Kuna gharama ambazo zitahusika kwenye kuhudhuria seminaNDIO GHARAMA ZIPO, na gharama hizi ni shilingi 21,000/- tu. Ukilipia hiki kiasi utaweza kuhudhuria semina ya siku 10. Na utapata bonasi ya kitabu cha JINSI YA KUWEKA AKIBA NA KUANZA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE5. Je, kitabu kinatumwaje kwa watu wa mikoani? Je, kuna Gharama za ziada ya kutumaKitabu kitatumwa kwa basi MPAKA mkoani na hakuna Gharama ya ziada inahohitajika ili utumiwe kitabu.Hii nimesema Ni bonasi unaipata kwa kuhudhuria semina. Hivyo huchajiwi Gharama ya ziada. Wewe Ukilipia 21,000/ tu ya semina unakaa mkao wa kula. bure.Kumbe kwa kuhudhuria semina hii Ni Kama unaua Ndege wawili kwa jiwe moja.Unapata mafunzo ya kina kuhusu UWEKEZAJI kwenye HISA. Na bado unapata kitabu bonasi ya kitabu cha JINSI YA KUWEKA AKIBA NA KUANZA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE.6. Kitabu nitakachopata kinaendana na masuala ya hisa?Ndiyo. Kinaitwa JINSI YA KUWEKA AKIBA NA KUANZA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE.Thibitisha kuwa utahudhuria semina hii ya kipekee kwa kutuma ujumbe kwenda 0684408755 Karibu sana.Jiunge na kundi letu la uwekezaji kwenye hisa hapa -
Hivi Ndivyo Elfu moja inaweza kukusaidia kuhudhuria semina ya uwekezaji kwenye hisa
Unaendeleaje rafiki yangu wa ukweli. Mimi kwa upande mwingine huku naendelea vizuri kabisa.
Wiki ilyopita nilitangaza juu ya uwepo wa semina ya uwekezaji kwenye hisa.
Semina hii ya kipekee itaendeshwa kwa njia ya mtandao wa whatsap kupitia kundi maalumu la semina.
- Itadumu kwa siku 10 na kila siku itakuwa ni siku ya mafunzo kwako.
- Baada ya semina utapata kitabu (hardcopy) cha JINSI YA KUWEKA AKIBA NA KUANZA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE. Hii ni nakala ambayo kila atakayehudhuria semina hii ataipata, mwishoni kabisa mwa semina
- Jina lako litaandikwa kwenye kitabu utakachopokea. Ningependa kuandika jina lako kwenye hiki kitabu kinapotoka, na jina lako litaendelea kuwa kwenye hiki kitabu vizazi hadi vizazi.
Njoo rafiki yangu uhudhurie semina hii ya kipekee, ujifunze mbinu za kuwekeza kwa faida.
Gharama ya semina hii ni 21,000/- tu. Na kitabu cha JINSI YA KUWEKA AKIBA na kuanza kuwekeza utakipata bila gharama ya ziada. Utakipata kwa gharama hiyohiyo ya 21,000/-
Kuna njia mbili za kulipia semina hii.
Moja ni kulipia moja kwa moja fedha yote kwa mkupuo. Unalipa kwa namba ya 0684408755 jina ni GODIUS RWEYONGEZA.
Au unalipa kidogokidogo.kwa kiwango utakachojiwekea wewe.
Kiwango cha chini kabisa unaweza kuanza kulipa elfu moja kila siku kuanzia leo hii. Ambapo baada ya siku 20 utakuwa umekamilisha malipo. Karibu sana. Hakikisha kwamba kwa vyovote vile unahudhuria semina hii ya kipekee rafiki yangu. mwambie na rafiki yako.
Ni mimi Godius Rweyongeza (Songambele)
0755848391
Morogoro-Tz
-
Vitu Viwili Ambavyo Havitapitwa na wakati kwenye zama hizi
Tuna facebook, twitter na mitandao mingine ya kijamii. Kila mtu anakazana sana kuhakikisha kwamba kwenye hii mitandao anakuwa na wafuasi wengi
Hata hivyo, ukweli ni kwamba hii mitandao huimiliki wewe. Muda wowote ule wanaomiliki hii mitandao wanaweza kufanya chochote na watu wazuri wanaofuatilia kazi zako wakashindwa kuziona tena. Hii ni mbaya sana.
Instagram wanaweza kukufungia leo na watu wote ambao wanafuatilia kazi zako huku wakashindwa kuona vitu vizuri wanavyopata kutoka kwako.
Facebook na majukwaa mengine yote yanaweza kukufungia na watu wakakosa vitu vizuri kutoka kwako. Unakumbuka kilichomtokea Trump?
Ila kuna vitu viwili ambavyo kwenye zama za leo ni uhakika hakuna mtu anaweza kukuzuia ukiwa navyo.
Kwanza ni email list

Hawa ni watu wanaokuwa wamejiunga na mfumo wako wa kupokea mafunzo kwa njia ya baruapepe. Unaweza kupoteza wafuasi wako wa facebook, instagram au sehemu nyingine lakini hawa huwezi kuwapoteza. Hawa watu ni wako na umiliki wa haya mawasiliano unakuwa nayo wewe wala siyo Zuckerberg au mtu mwingiine.
Halafu isitoshe barua pepe ni kitu binafsi. Unapokuwa unawasiliana mtu kwa njia ya barua pepe unakuwa unawasiliana naye yeye kama yeye. Hivyo, inakuwa rahisi kujenga uhusiano wa karibu na watu wako. Kwa sababu wanaweza kufunguka kwako chochote na wewe unaweza kufunguka kwao chochote. Kwa hiyo mnajenga uhusiano wa kudumu.
Baruapepe za watu unakuwa nazo wewe, siyo kwamba wanakuwa nazo facebook au instagaram ambao wanaweza kusepa na followers wako muda wowote.
Kwa hiyo rafiki yangu, japo unajenga wafuasi kwenye hii mitandao. Ebu fikiria pia kuhusu namna unavyoweza kujenga email list yako. Mfumo wa kupokea makala kwa njia ya barua pepe ambapo watu wako watakuwa wanapokea mafunzo kwa njia ya baruapepe.
Unaweza kuanza kujenga huu mfumo kupitia jukwaa kama mailchimp, mailmunch, mailerlite na nyinginezo nyingi zilizopo. Chagua moja na komaa hiyo kwa kuanzia.
Pili Ni Tovuti Au Blogu

Hki ni kitu kingine ambacho wewe mwenyewe una umiliki nacho na wala siyo facebook wala twitter. Hawana mamlaka yeyote huku.
Ebu chukulia mfano wa kawaida tu. ukiandika status ya whatsap inapotea baada ya saa 24.
Leo hii kuna vitu ambavyo uliandika kwenye instagrama yako mwaka 2020 ila unavitafuta na huwezi kuvipata. Na isitoshe hakuna namna ambavyo unaweza kumwambia mtu arejee masomo yako ya nyuma ii kujifunza na kunufaika zaidi. Ila mimi kwenye blogu hapa naweza.
Mfano, soma hili somo nililoandika siku za nyuma kwa KUBONYEZA HAPA
Unaona ee! Hiki kitu kwenye blogu nakifanya ndani ya sekunde tu na kinaisha, ila ukitaka kufanya hivi facebook, inabidi utenge masaa ya kutafuta kile ulichoandika siku za nyuma.
Ukibahatika kukiona ndio unaweza kumwonesha mtu akiangalie. Rafiki yangu naomba unisikilize kwenye hili
Kuwepo facebook, kuwepo instagram, ila kitu kimoja tu ni kwamba usiache kuwa na blogu yako pamoja na email list maana hivi ni vitu viwili ambavyo unaweza kumiliki mtandaoni.
Hii ni maalumu kwa ajili yako wewe unayefanya biashara kwa njia ya mtandao na unataka kujenga mtandao wa watu utakaodumu nao bila kuwapoteza. Na ngoja nikwmabie kitu. Hivi
Kila la kheri
Umekuwa name Godius Rweyongeza (Songambele)
0755848391
Morogoro-Tz
-
KITABU CHA MY STORY kipo, hivi ndivyo unaweza kukipata

KUPATA KITABU HIKI, tuma baruapepe kwenda songambele.smb@gmail.com Rafiki yangu mpendwa unaendeleaje. Kwenye mojawapo ya makala ambazo nimewahi kuandika hapa siku za nyuma nilieleza kuwa nina kitabu cha MY STORY cha Mohmmed Ibn
Sasa watu wengi wamekuw wananiomba niwatumie hiki kitabu, leo nimeona nikwambie kwamba unaweza kupata hiki kitabu. Kama utakaitaka basi nitumie ujumbe kwa njiaa ya baruapepe ili nikutumie.
Baruapepe yangu ni godiusrweyongeza1@gmail.com au songambele.smb@gmail.com
Kichwa cha habari andika KITABU CHA MY STORY
-
Njoo rafiki yangu ujifunze mbinu za kuwekeza kwa faida.
Unaendelea rafiki yangu. Bila shaka kila kitu kipo Safi kwa upande wako.
Mimi huku naendelea vyema.
Nilikuwa najiuliza, Hivi umeshajiunga na semina ya uwekezaji kwenye HISA ambayo itaendeshwa kwa njia ya mtandao kuanzia tarehe 1.8.2022?
Kama ulikuwa hujui Ni kwamba kwenye semina hii ya kipekee, unaenda kujifunza mengi kuhusu uwekezaji kwenye HISA
Baada semina hii utaanza moja kwa moja kuwekeza.
Semina hii ya kimtandao, itadumu kwa siku 10. Na baada ya semina unaenda kupata kitabu (hardcocopy) bila gharama ya ziada.
Gharama ya semina hii Ni 21,000/- tu.
Ambapo
Utapata mafunzo ya semina kwa siku 10. Mafunzo yatatolewa kwa mfumo wa Makala, sauti na video
Utapata kitabu (Hardcopy) Cha JINSI YA KUWEKA AKIBA NA KUANZA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE.
Jina lako litaandikwa kwenye kitabu pia. Kila mshiriki wa semina jina lake litaandikwa kwenye hiki kitabu hiki.….nisingependa usikose semina hii ya kipekee. Ebu thibitisha ushiriki wako kwa kulipia leo hii.
Malipo yote yanafanyika kupitia Namba ya simu (Airtel money) 0684408755 jina ni GODIUS RWEYONGEZA
Ukishalipia wewe unabaki kusubiri mafunzo haya ya kipekee sana.
-
Hii dhana ambayo kila kijana anapaswa kuachana nayo

Vijana tupambane, ifike hatua haya mabango yaondolewe mitaani kwetu. Vijana wanapokuwa wanafikiria kuanzisha kitu, kitu Cha kwanza wanafikiria kupata mtaji au msaada. Nakumbuka wakati naanza chuo mwaka 2016 nilimwambia rafiki yang hivi, mpaka nahitimu chuo nataka niwe na uwezo wa kuajiri vijana kumi”. Yeye aliniambia “mpaka nahitinu chuo nitakuwa nimetafuta na kupata wadhamini kumi”
Sasa nadhani vijana tunapaswa kubadili fikra zetu.
Tubadili namna tunavyofikiri maana mitaji mingine tayari tunayo.
Una nguvu zako. ZITUMIE hizi kuchapa kazi
Una akili itumie kubuni vitu
Una kipaji, kitumie.
Una muda, utumie
Una ujuzi/elimu itumie pia.Kwa vyovyote vile, usikubali kuendelea kubaki ulivyo. Nakubaliana na Martin Luther King Jr aliyesema kwamba, Kama huwezi kupaa, kimbia. Kama huwezi kukimbia tembea, Kama huwezi kutembea Basi tambaa Ila kwa vyovyote vile usikubali kubaki ulivyo. Pambana uwezo unao.
Tuachane na dhana ya kwamba Kuna mtu atasimamia na kufanya vitu kwa niaba yetu.
Maisha yako ni wajibu wako kijana. Ukiendeleza kusubiri misaada kutoka sijui wapi ili ufanikishe malengo yako. Utasubiri Sana.Anza hata kidogo
Fanya Kitu
Wanaopata bahati Ni wale walio kwenye mwendo siyo wale wanaokaa vijiweni tu wakisubiri bahati. -
Namna ya kukabiliana na ukosefu wa ajira kwa vijana. Njia Saba Zilizothibitishwa (Njia Namba 2, 4 na 7 ni muhimu sana)
Mwishoni mwa mwezi uliopita nilisafiri kwenda Dar kutembea. Nikiwa Dar nilipata nafasi ya kuongea na mmoja wa rafiki zangu. sijui ilikuwaje lakini kwenye maongezi yetu kuna sehemu tulifika tukaanza kuongelea suala zima la ajira, na hapo ndipo akawa ananiambia kwamba yeye alihitimu mwaka 2006 na kupata ajira miezi mitatu baada ya kuhitimu.
Kwa maneno yake akawa ameianiambia, “siyo kama ninyi vijana wa siku hizi mnahitimu na kukaa mtaani miaka na miaka bila kupata ajira”. Aliendelea kuniambia na hiyo miezi mitatu aliyokaa bila kupata ajira ni sawa na alichelewa kupata ajira.
Siku hizi hali ni tofauti. Vijana wanaozidi kuhitimu kila mwaka ni wengi ila wanaoajiriwa ni wachache sana. Kilio kikubwa cha vijana sasa hivi ni ajira. Sasa nini kifanyike ili kuondokana na hali kama hii?
Sasa viafuatavyo ni vitu ambavyo kwa leo ningependa kushirikisha kuonesha ni kwa namna gani tunaweza kuondokana na tatizo la ajira
Moja. Kufanya kazi kwa bidii kunaweza kukukutanisha meza moja na wafalme
Ukisoma CV za vijana wengi wanajinadi kamawachapakazi na wanaofanya kazi kwa bidii. Na ambao wapo tayari kufanya kazi kwenye mazingira na hali yoyote. (nasema ukisoma CV za vijana wengi kwa sababu mimi mwenyewe hata CV ya kuombea kazi sina na sina mpango wa kutengeneza moja. nataka matendo yangu na kazi zangu tu ziongee mbele ya watu.
Lakini kitu cha kushangaza ni kwamba, vijana hawa hawa ambao wanajinadi kwamba wanaweza kufanya kazi kwa bidii wakiajiriwa hawafanyi kazi kwa bidii. Mwajiri asipokuwepo hawawezi kujisimamia na kuchapa kazi badala yake wanachapa soga.
Ongea na mwajiri yeyote, atakwambia asilimia kubwa ya tatizo analokumbana nalo kwa vijana wa siku hizi anaowaajiri ni uzembe. Mtu hataki kujituma na kufaya kazi kwa bidii.
Inaweza kushanganza ila ni kweli, kijana ameajiriwa anatumia muda mwingi facebook na instagram kwa siku kuliko anavyoutumia kweye kazi yake, asa unashangaa hivi huyu ameajiriwa na kampuni ya facebook au nini kinaendelea.
USHAURI WANGU: vijana wenzangu tupende kufanya kazi kwa bidii. Tukipewa kazi tuifanye kwelikweli kwa viwango vya juu. Kazi ni moja ya kitu ambacho kinaweza kukuinua juu, juu sana. nimekuwa nikiandika mara kwa mara humu kuwa kazi inaweza kukufanya ukutane meza moja na wafalme. Kazi inaweza kukuinua juu.
Ninachojua ni kwamba, unaweza ukawa hauna elimu kubwa, unaweza ukawa hauna ujuzi mkubwa, unaweza ukawa hauna konekisheni kubwa, ila kazi tu ikakuinua.
Sidhani kama kuna mwajiri anachukuia mtu anayefanya kazi kwa bidii. Mtu anayejituma na kufanya kazi kwa viwango vya juu. Hakuna mwajiri wa aina hii. kwa hiyo vijana tupende kazi.
SOMA ZAIDI: WANAOSHEREKEHEA KUHITIMU CHUO TUWAAMBIE UKWELI? AU TUWAACHE KWANZA WAFUMUE NYWELE ZAO ZA GRADUATION?
Mbili, tuwaambie vijana watembee na ujuzi mtaani na siyo Vyeti
Dunia ya sasa hivi imebadilika sana. Kuna kazi au ajira zilizokuwepo siku za nyuma, ila siku hizi hazipo au la zinaelekea kuisha. Siku hizi kuna hizi mashine ambazo zinaweza kufanya kazi ya watu wawili mpaka kumi au hata zaidi kwa wakati mmoja. Kwa hiyo, mashine moja inakula ajira za watu kumi
Na sasa hivi kuna mshine zinatibu,
Mashine ambazo zinafanya kazi za kihasibu
Mashine ambazo zinafanya kazi za kilimo mpaka mapishi.
na mashine hizi haziitishi mgomo, mashine hizi haziombi kufanya kazi kwa saa chache zinafanya kazi saa 24 siku saba za wiki. Ebu chukulia mfano wa ATM benki. Hii mashine kila siku inafanya kazi, haina likizo na wala haitakuja kulilia likizo hata siku moja, haiwezi kugoma na wala haiwezi kudai ongezeko la mshahara. Gharama pekee inayotumika kwenye hii mashine ni gharama ya kuinunua na gharama za maintainace.
Sasa ili kijana uweze kuishi kwenye ulimwengu huu wa mashine unapaswa kujitofautisha.
Nakumbuka siku moja wenye mtandao wa Quora Kuna mtu aliuliza, nawezaje kuwa Kama Elon Musk, Jeff Bezos au Bill Gates? Justin Musk ambaye ni mke wa zamani wa Elon Musk, alijibu kwa kusema HUWEZI. Ila kama unataka kufikia kwenye viwango walivyofikia basi chagua kitu kimoja kisha bobea kwenye hicho kitu kiasi kwamba hakuna mtu ambaye anaweza kubobea kwenye hicho kitu kama wewe. Kisha baada ya hapo bobea kwenye kitu kingine. Mfano, bobea kwanza kwenye uhasibu kisha bobea kwenye kompyuta. Baada ya hapo unganisha hivyo vitu viwili kutengeneza kitu kimoja.
Alimalizia kwa kusema, uliweza kufanya hivyo, nakuhakikishia hakuna mtu hata mmoja ambaye anaweza kukufikia kwenye kitu utakachofanya. Na wala hakuna mashine itaweza kuchukua kazi yako.
NDIYO MAANA vijana tunapaswa kutembea na ujuzi mtaani. Mwenye ujuzi halali njaa, mwenye cheti mhhh!
Sasa na wewe Unapaswa kubobea. Dunia ya leo bado inawapenda sana wabobevu na inawalipa vizuri ukilinganisha na watu wa kawaida. Sasa swali langu kwako, unaemda kubobea katika nini?
Kama ungependa kubobea kwenye uandishi hakikisha unajipatia nakala ya kitabu hiki Cha JINSI YA KUWA MWANDISHI MBOBEVU NDANI YA SIKU 30. Bonyeza hapa.
Tatu, vijana tuwe waaminifu
Kuna akili ambazo vijana wengine wanakuwa nazo, zinakuwa siyo nzuri. Mtu anawaza aajiriwe halafu aanze kupiga cha juu. Yaani, aanze kuiba. Uaminifu ni mtaji mkubwa. Watu wanapenda kufanya kazi na waaminifu. Uaminifu ni kitu muhimu bila kujali umeajiriwa au umeajiajiri
Siku za nyuma hapahapa kwenye hii blogu niliwa hia kuandika namna ambavyo kijana mmoja alikusanya vijana wengine na wakaunda kampuni huku wakimshirikisha mmwekezaji. Wazo lao lilikuwa ni kulima mboga mboga, kwa kuanzia na nyanya na mboga nyinginezo.
Walikubaliana na mwekezaji kuwa wao wangekuwa na asilimia sitini ya umiliki wa kampuni (walikuwa vijana watano) na mwekezaji angepata asilimia 40.
Wakati taratibu za kusajili kampuni zikiendelea, mwekezaji alimpa kiongozi wao milioni saba. Mradi ulikadiriwa kuwa wa milioni 30. Kijana alipopokea hela akatokomea kusikojulikana.
Kama vijana tunahitaji kuwa waaminifu kwenye kazi zetu.
waaminifu kwa wale tunaofanya nao kazi
Waaminifu kwa kwenye bidhaa zetu. Ukimuuzia mtu bidhaa, umuuzie bidhaa inayoendana na hela aliyotoa. Kiuhalisia bidhaa yako inapaswa kuwa na thamani zaidi hata fedha inayotoka. Hiki kitu ndicho tupambane nacho. Bila uaminifu, sahau kuhusu mafanikio yoyote yale maishani mwako.
SOMA ZAIDI: Jinsi Ya Kuanzisha Biashara Bila Mtaji Tanzania
Nne;KIJANA FANYA KITU
Huwa napenda kuwaambia vijana wenzangu kuwa haifai wewe kuendelea kulalamika tatizo la ajira huku ukiwa umekaa kwenye kochi. Ebu fanya kitu chochote kile ambacho ni halali na kinaweza kukuingizia kipato.
Usikae tu na kujiita msomi, huku ukiwa huna hata kitu chochote cha kukuingizia kipato.
Fanya chochote
Uza karanga
Uza madazi, vitumbua n.k.
Najua vitu kama hivi kwa wasomi wengi ni kichekesho, kwa sababu wengi wanapenda wakae kwenye ofisi yenye kiyoyozi. Yaani, mtu amehitimu halafu aanze kuuza mandazi. Inaonekana ajabu kweli.
Ila ushauri wangu kwako kijana mwenzangu ni huu: Fedha zako wanazo watu wengine.Hapo hapo ulipo kuna watu wana fedha zako, ila huwezi kuzichukua hizo fedha kwa nguvu, huo utakuwa ni wizi.
Njia nzuri ya wewe kupata fedha ni kuwapa kitu wanachotaka. Na moja ya kitu ambacho wanataka ni chakula. Kwa hiyo unaweza kuwapa hicho ili wakupe fedha. Ndiyo maana hapo juu nikasema kwamba unaweza hata kuuza mandazi au vitumbua.
Najua wazi kuwa una malengo ya kuwa kwenye ofisi kubwa yenye kiyoyozi, ila hilo kwa saas awacha tuliweke pembeni. Pambana kwanza upate hela.
Najua siyo kitu cha viwango vyako ila kwa kuwa ni halali kinaweza kukufikisha mbali.
Ngoja sasa nikwambie siri ambayo hakuna mtu alikuwa amefikiria kukwambia. SIri yenyewe ni hii. vitu vidogo vina hela aisee! Shhhh! Usimwambie mtu.
Mtu akiwa akiwa ananunua kitu cha shilingi mia moja kama kitumbua. Hajiulizi mara mbilimbili. Anatoa mia au mia mbili na wewe unampa kitumbua chako, na kuendelea mbele.
Lakini ukiwa unauza kitu cha elfu kumi. Aisee, mtu atajihoji sana sana kabla ya kutoa hela yake. Ndiyo maana unaona hata matajiri wakubwa bado wanatengeneza vitu vya hela ndogo kama pipi na kiberiti.
SOMA ZAIDI: Kama Unataka Mali: Maeneo Matano Unapoweza Kupata Mali Halali…
Tuseme kwa mfano umeamua kuuza vitumbua vyako, unaweza kuungana na mwezako. Mkatengeneza ofisi yenu ya uongo na ukweli.
Au kama huoni mwenzako wa kuungana naye, basi unaweza kuajiri kijana mmoja.
Akawa anatengeneza vitumbua halafu wewe unasambaza. Tafuta basikeli hata ya kuazima. Zunguka mitaani, na kwa siku mnajiwekea lengo la kuuza vitumbua 300 mpaka 500. Hiyo ni sawa na elfu 30 mpaka 50 kila siku. Ukitoa gharama uliyoweka kwenye hivyo vitumbua hukosi cha kwako kila siku. Rafiki yangu, miaka mitano mpaka kumi ijayo, tutakuwa hatuongelei kijana wewe ambaye hukuwa na ajira, bali kijana wewe uliyetengeneza ajira za watu. hivi ndivyo watu waliofanya makubwa walivyoanza.
Hivi kweli hata mtaji wa kuanzisha biashara ya karanga kweli utakosa?
Hivi hata mtaji wa vitumbua utakosa kweli rafiki yangu? kweli..
Kama hauna huo mtaji ila una simu kubwa ambayo unaitumia kusoma hii makala. Uza hata hiyo simu kwanza upate mtaji, kisha chapa kazi. siku za mbeleni utanunua simu nyingine.
Nimeeleza zaidi kuhusiana na suala zima la mtaji kwenye kitabu changu cha NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA. Kiufupi hiki kitabu unapaswa ukipate na ukifanye kuwa mwongozo kwako, kwa sababu kimeeleza ni kwa namna gani unaweza kutumia nguvu ya vitu vidogo kwenye kila eneo la maisha yako. Na vile unaanzia chini kabisa, basi unahitaji hiki kitabu kama mwongozo wako wa kukusaidia kufanyia mpango kazi wako mpaka ukufikishe kileleni.

Tano: Geuza kitu ulichosomea kuwa ajira
Hivi kwa nini tunasoma? Hizi shahada za awali hizi ni za nini? Haoa naweza kuwa mtazamo tofauti na walio wengi. ila huu ndiyo mtazamo wangu na hiki kitu ndiyo mimi nasimamia. Mimi naamini kwamba, tunasoma ili tuje kutatua matatizo yaliyo kwenye jamii zetu. Tunasoma ili kuja kutengeneza ajira.
Kwa hiyo kwa kitu ambacho umesoma, angalia ni kwa namna gani unaweza kukitumia hicho kitu kwenye jamii yako kusaidia watu.
Umesomea sheria, je, hiyo inawasaidiaje watu waliokuzunguka.
Wewe ni mtalaamu wa kilimo, watu waliokuzunguka wananufaika na utalaamu wako?
Ni mtaalamu sijui wa IT, huo utalaamu wako unauletaje kwenye mazingira yetu ya huku mtaani. Kuna vitu unajua na unaweza kuwa unavichukulia poa, ila watu huku mtaani wanavihitaji sana.
Umesomea masuala ya biashara, wasaidie watu kukuza biashara zao. Zile mbinu ulizojifunza chuoni onogea na watu wenye biashara ndogo huku mtaani ili wazitumie. Hawajui hata namna hata namna ya kutunza hesabu zao za kibiashara, kila siku wanasema kuna chuma ulete anachukua fedha zao. Wasaidie kwenye hilo.
Wasaidie kuwafikia wateja. Wakiona mbinu zako hizo zinawasaidia baadaye ukisema kwamba wakulipe ili mfanye kazi zaidi, watakuwa tayari. Maana watajua unaenda kuwasaidia zaidi.
Kijana msomi, ebu badilisha elimu yako kuwa ajira yako basi. Ebu wasidie watu waliokuzunguka kwanza, watu hao hao watakuwa tayari kukulipa, maana wewe ukiwapa mbinu za kuwainua hawawezi kukuacha.
SOMA ZAIDI: Cha kufanya pale wenzako wanapokuzidi elimu, kipaji, ujuzi konekisheni n.k.
Sita, Vijana tujitangaze
Kama una ujuzi au una kitu chochote ambacho unajua kinaweza kusaidia watu , kitangaze watu wakijue. Kuwa na bidhaa nzuri bila kuitangaza kwa watu ni sawa na kujinongongeza mwenyewe kwa kumwambia binti kuwa nakupenda kwenye giza.
Ukiwa na bidhaa,
Saba; Vijana tushikane mkono
Njia pekee ambayo tunaweza kusaidia vijana kuondokana na hili tatizo la ajir ni kuwashika mkono au kwa lugha ya mtaani kuwaungisha pale wanapokuwa na bidhaa au wnapoonesha juhudi za kufanya kitu fulani. Tusapoti juhudi za vijana wenzetu.
Ni kweli mtu anaweza kuwa ameanza kwa kufanya kitu kwa udogo, ila tukizidi kumsapoti kitakua.
Hapa naongea na ninyi nyote wenye tabia za kupenda vitu vya nje ya kudharau vitu vya ndani. Utasikia mtu anasema, aah, kitu chenyewe kimetengenezwa na mtanzania. Wabongo hakuna kitu chochote.
Tukisapotiana sisi vijana tutafika mbali.
Moja ya ndoto yangu kubwa ni kuona watu wakiacha kwenda China kutafuta bidhaa. Badala yake vitu hivyo wavipate hapa nchini. Mfano, badala ya mtu kwenda china kununua nguo, kwa nini vijana wa kitanzania tusitengeneze nguo na kuziuza hapa kwa bei sawa na ile ya china.
Kuna vijana wengi wanashona nguo. Ila je, tunawasapoti.
Tunataka wainuke.
Jamani, tuwasapoti watu wanaofanya vitu.
Mtu akianzisha mgahawa kanunue chakula kwake
Mtu akilima mboga, nunua kwake.
Mtu akiinua kipaji chake, kisapoti
Tatizo la watu ni kwamba unaweza kuwa unapambana na bado wanataka wakija kwenye biashara yako uwape vitu bure. Mtu umepambana na kupata mtaji wako na sasa umefungua duka,, wanataka wakija kwako uwape vitu bure tu. Wengine wanakopa na kulipa hawalipi. Hivi kweli, tutafika kwa namna hii?
Vijana tusapotiane.
Tena inabidi tuanze kusapotiana kwa vitendo kuanzia sasa hivi. Ebu shirikisha hii makala kwenye makundi mengine ya whatsap ili vijana wengi wasome ujumbe huu. hakikisha kwamba hakuna kijana unayemjua ambaye hajasoma huu ujumbe.
Subscribe kwenye channel yangu ya youtube pia. Enhee, hapo naona sasa umeanza kunielewa kwenye dhana nzima ya kusapotiana.
Nakaukaribisha pia upate vitabu vyangu vya NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA na JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO kila kitabu ni elfu ishirini (20,000). Ukituma 40,000/- tu unapata vitabu vyote viwili na nikakusafirishia bure.

Karibu sana
umekuwa nami Godius Rweyongeza
Kupata makala zaidi kutoka kwangu weka mawasiliano yako hapa chini ili uendelee kujifunza zaidi kutoka kwangu kila siku. Jaza taarifa zako hapa
Kwa mawasiliano na mimi tafadhali usisite kutuma ujumbe kwa Email: songambele.smb@gmail.com
Whatsap +255755848391
For Booking: songambele.smb@gmail.com
-
Karibu kwenye semina ya uwekezaji kwenye Hisa
Habari ya leo rafiki yangu. bila shaka unaendelea vyema kabisa. karibu kwenye semina ya uwekezaji kwenye hisa. Hii ni semina ya kipekee sana ambayo itaendeshwa kwa njia ya mtandao kuanzia tarehe 1 Agosti 2022. Katika semina hii ya kipekee unaenda kujifunza kila kitu unachohitaji kujua kuhusu uwekezaji wa hisa.
Semina hii ya kipekee itadumu kwa siku 10 mfululizo na itaendeshwa kwa njia ya mtandao. Kwa siku hizi 10 utapata mafunzo ambayo yatatolewa kwa njia ya maandishi, sauti na video.
Kwenye semina hii unaenda kujifunza kila kitu unachohitaji kujua kuhusu uwekezaji wa hisa na kikubwa zaidi ni kwamba utapata nakala moja (hardcopy) ya kitabu cha MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE
Gharama za semina hii ni 21,000 tu. Namba ya malipo ya semina ni 0684408755
Jiwekee nafasi yako kwa kulipia leo.
Ni Mimi
Godius Rweyongeza
0755848391
Morogoro-Tz