Home


  • Namba Zetu Za Malipo

    Namba za malipo ya vitabu:

    Namba za lipa

    TIGO PESA: 19016638 Jina ni SONGAMBELE CONSULTANTS

    M-PESA: 5564517 jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

    Namba za kawaida

    AIRTEL MONEY: 0684408755
    TIGO PESA: 0655 848 392
    M-PESA: 0745 848 395

    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    NB: Kama namba ya malipo anatumiwa mtu ambaye yuko nje ya nchi. Iandikwe Kwa kuanza na +255

    Kwa hiyo namba zinazotumwa nje ya nchi zitakuwa
    Airtel money: +255 684 408 755
    TIGO PESA: +255 655 848 392
    M-PESA: +255 745 848 395

    KOTE Jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Kama malipo yatakuwa yanafanyika kupitia benki.

    Yafanyie kupitia

    1. CRDB BANK: 0150770710200
    2. NMB BANK: 22110047274

    Kote jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

  • Wasiliana na Godius Rweyongeza Sasa

    Habari yafuatayo ni mawasiliano Unayoweza kutumia kumpata GODIUS RWEYONGEZA

    Simu: +255 (0) 684408755

    Whatsap: +255 (0) 755848391

    Email: songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu vyake wasiliana Moja kwa Moja na +255 (0) 684408755 (more…)

  • Email List Ni Nini?

    Ila swali lilikuwa email list nini? Kujibu Hilo swali naomba usome hapa chini

    Email list ni mfumo wa kukusanya mawasiliano ya watu wanaofuatilia kazi zako. Ambapo kila anayesoma na kupenda Makala zako, anaweza kukuachia email take na wewe ukaendelea kuwasiliana naye kwa kumtumia Makala zaidi kwenye email yake moja kwa moja.

    Kuna sababu nyingi kwa Nini unapaswa kuwa na email list Ila hapa sitazitaja zote

    1. Siyo kila mtu anayetembelea blog yako leo, ataendelea kuitembelea kila siku. Baadhi ya watu watakuja kwenye blogu yako kwa shida maalumu, wakishasoma kitu chako, wataondoka na kukusahau. Ila endapo huhu mtu atakuwa amekuachia email yake. Ni rahisi kwako kuwasiliana naye kwa baadaye kwa njia ya baruapepe na kumfanya aendelee kufuatilia kazi zako zaidi.
    2. Lakini pia email list inakusaidia kuanza kutengeneza jumuiya ya watu wanaokuamini zaidi, ili ikifikia hatua ambapo wewe utakuwa na bidhaa, hawa watu ndio watakuwa wa kwanza kununua kwako

  • Jinsi Nilivyoandika Kitabu Kilichosomwa Sana Kuliko Vitabu Vyote Tanzania

    Nakumbuka mwaka 2019 kulikuwa na kijitabu kidogo hivi kilikuwa kinazunguka mtandaoni. Kijitabu hiki kilikuwa kinajulikana kama Baharia.

    Kilikuwa kinazungumzia mambo kadha wa kadha ambayo baharia anafanya.

    Kijitabu hiki kilizunguka sana, sana. Binafsi sikukisoma, Ila watu wengi ninaowafahamu mimi walikisoma hicho kijitabu. Kwa hiyo mada yao kubwa kwenye mazungumzo ikawa imekuwa BAHARIA.

    Yaani, ulikuwa huwezi kupitisha nusu saa bila kusikia mtu akisema kuhusu Baharia.

    Kwa sababu nilikuwa nimezungukwa na watu wengi waliosoma kijitabu kwa wakati huo, nikipata kujua kuhusu uwepo wa kijitabu hicho. Na hata baadhi ya vitu kwenye kijitabu hicho nilisikia watu wakiviongelea…

    Wewe vipi ulikisoma?

    Kama nakuona vilee….

    Sasa katika kipindi hiki nilikaa nikajiuliza. Kama hiki kijitabu (ambacho mimi niliona hakina ujumbe wa maana)  kinaweza kusomwa hivi, basi na Mimi naweza kukaa chini, nikaandika kitu cha maana kikasomwa na kusambaa sana kama hiki kijitabu….

    Nilitafakari sana hili…
    Ila sikujua niandike nini… Nilikuwa najiuliza hivi hiki kijitabu kina sifa gani ambazo zimekifanya kisomwe Sana.

    Baada ya siku chache nikaamua kuandika kitabu kuhusu usomaji wa vitabu.

    Kitabu hiki nilishaanza kukiandika muda kabla hata kusikia habari za BAHARIA. Ila nilikuwa nakiandika kwa mfumo wa hadithi. Na baadaye ile hadithi ilipotea nikiwa katikati baada ya kupoteza simu yangu..

    Baada ya tafakari ya kina, nikaamua kurudia kuandika kitabu hiki, Ila zamu hii sikutaka kuandika hadithi kama ilivyokuwa mwanzoni.

    Nikaanza kuandika. Sikumbuki nilitumia muda kiasi gani kuandika hiki kitabu, Ila nadhani nilikiandika siku za wikendi kikakamilika.

    Nikakitengeneza vizuri, halafu nikamfuata mshikaji wangu Magambo kumpasha habari. Nikampa nakala aisome,

    Wakati nasubiri mrejesho wake nikaamua kuwa kitabu kile nikitoe na nikigawe bure, Kama ambavyo nilikuwa nimepanga tangu mwanzo

    Kilichotokea ni historia.

    Kitabu hiki ambacho mwanzoni kilikuwa kinajulikana kama MAAJABU YA VITABU, na Sasa hivi kinaitwa MAAJABU YA KUSOMA VITABU kimesomwa na watu wengi tangu hiyo Septemba 2019.

    Kimezungumzia kuhusu usomaji wa vitabu tu! Na kimekuwa kikitolewa bure tangu 2019 mpaka leo hii.
    Kiukweli wengi wamekisoma, na sasa nina toleo la 2 kitabu hiki. Pamoja na marekebisho yake.

    Wewe pia unaweza kupata zawadi ya nakala yako HAPA CHINI

    Mpaka sasa kitabu hiki, kimekuwa kuwa mwongozo wa usomaji wa vitabu kwa watu wengi. Lakini kwa watu ambao hawajawahi kusoma kitabu changu chochote, huwa nawashauri waanze na hiki cha bure, halafu ndio waje kununua.

    Vyote hivi viwili utavipata kwa bei ya 8,000/- tu badala ya bei yake halisi. Tuma fedha kwa 0684408755 jina ni GODIUS RWEYONGEZA


    Ni mimi rafiki yako
    Godius Rweyongeza
    0755848391
    Morogoro-Tz

  • JINSI YA KUANZISHA BLOG

    Habari ya leo rafiki yangu. Siku ya leo ningependa kukuelezea ni kwa namna gani unaweza kufungua blog.

    Kwanza labda nianze kwa kusema kwamba ulimwengu wa sasa hivi umebadilika. Kwenye ulimwengu wa leo mtu anapokuwa na wazo, au dukuduku sehemu ya kwanza kabisa anapokimbilia ni mtandaoni kutafuta kitu hicho.

    Hiki kitu kimejenga utagemezi kwa watu, maana watu hawawezi kuishi tena bila mtandao. Na hizi taarifa za mtandaoni ambazo tunatafuta kila siku, zinawekwa na watu. Hazishuki kutoka mbinguni na wala haziwekwi na roboti (japo zipo baadhi zinazowekwa na roboti)

    Usije ukafiri kwamba kuna watu wa aina fulani tu, ambao ndio wamebarikiwa kuweka vitu mtandaoni, na wengine hawajabarikiwa. Unachopaswa kufahamu ni kuwa, kila mtu kabarikiwa kwa namna yake.
    Kwa hiyo na wewe huwezi kukosa kitu cha kuweka mtandaoni.

    Ni sifa gani napaswa kuwa nazo ili kiandike na kuweka vitu vyangu mtandaoni?

    Kama wewe una ujuzi fulani, basi ujue kabisa kuwa una sifa za kukuwezesha kuweka vitu mtandaoni.

    Kama wewe unapenda kufuatilia baadhi ya vitu kwa kina, labda kufanya utafiti au kujifunza. Ujue kabisa kuwa una sifa za kukuwezesha vitu mtandaoni.

    Kwa hiyo kiufupi, elimu yako, ujuzi wako, udadisi wako, Ubunifu wako, kipaji chako, n.k. vinapaswa kuwekwa mtandaoni.

    Je, niweke vitu vyangu mtandaoni kwa njia gani?
    Mtandao umekuja na fursa nyingi. Unaweza kutumia njia ya sauti kufikisha ujumbe wako (podcast)
    Unaweza kutumia njia ya video kufikisha ujumbe wako
    Unaweza kutumia njia ya maandishi (Makala)
    Unaweza kutumia njia ya michoro na picha

    Furaha unayoipata kwa kujua kuwa na wewe unaweza kuweka vitu vyako mtandaoni

    Kwa hiyo njia zipo nyingi, nyingi sana.

    Ni eneo gani sasa naweza kuweka kitu changu nilichoandaa?
    Kwanza kabisa ningependa ufahamu maeneo matano ambayo watanzania wanapenda kutembelea. Yaani, mitandao maarufu hala nchini. Hizi takwimu zinatolewa na mtandao wa Alexa na zinaweza kukusaidia kujua wapi walipo watanzania wengi ili uwawekee vitu vyako huko.

    Mtandao wa kwanza kwa kutembelewa ni GOOGLE
    Wa pili ni YOUTUBE
    Wa Tatu ni Facebook
    Wa nne
    Na wa tano

    Orodha ya mitandao mingine inayitembelewa zaidi unaweza kuiona hapa chini kwenye picha

    Mitandao inayotembelewa zaidi nchini Tanzania

    Imekuwepo mitandao ya kijamii kadha wa kadha ambayo watu wamekuwa wakiikimbikia na kuitumia kama Facebook, twitter, Instagram. Hii mitandao iko vizuri na imerahisisha Mambo mengi linapokuja suala zima la mawasiliano.

    Ila kama una mpango wa kuweka mawazo yako mtandaoni katika namna ambayo itadumu kwa kipindi kirefu. Basi hii mitandao ya kijamii haifai. Mitandao ya kijamii ina watu ambao wanaweza kusoma au kufuatilia kazi zako. Ila kudumu ya wewe kuweka taairfa zako.

    Lakini pia mpangilio wake ni ule ambao unatoa taarifa mpya kwanza huku za zamani zikiwa hazipewi kipaumbele. Breaking news, ndizo zinakaa juu.


    Na umiliki mtandao uko wa MTU mwingine. Wewe unaysoma hapa najua haumiliki twitter labda kama wewe ni Elon Musk,
    Haumiliki Facebook wala WhatsApp labda kama wewe ni Mark Zuck.

    Ndio maana unahitaji kuwa na kitu Cha kwako, nafasi yako mtandaoni ambayo unazomi Na sehemu ya kuanzia ni kwenye blog.

    JINSI YA KUTENGENEZA BLOGU

    Kuna aina mbili za blogu. Blogu za bure na za kulipia.

    Blogu za bure pia zipo za aina mbili

    1. WordPress (mfano wa blogu hii unaweza kuwa ni (jinalako.wordpresa.com)
    2. Blogger mfano wa blogu ya Aina hii, unaweza kuwa ni (jinalako.blogspot.com)
    3. Blog za bure, hauzimiliki wewe moja kwa moja. Zinakuwa chini ya kampuni uliyofungulia, na waweza kuifunga muda wowote wakitaka. Ila kwa mtu yeyote anayeanza, anaweza kuanza na blogu za bure.

    Blog za kulipia kwa upande mwingine zinakuhitaji utoe fedha mfukoni ili kutengeneza blog. Na ukishaitengwneza inakuwa ya kwako na wewe ndiye unakuwa mmiliki halali. Yaani, tuseme unakuwa na sehemu yako mtandaoni. Kaa ambavyo google wana sehemu yao au Facebook wana sehemu yao.

    Na wewe utakuwa na sehemu yako mfano jinnalako.com au jinalako.co.tz

    Mpaka haponina uhakika utakuwa umepata kujifunza mengi. Kama utataka kufungua blogu ya bure Basi tembelea

    ukikwama utaniambia

    Ni mimi rafiki yako
    Godius Rweyongeza
    0755848391
    Morogoro-Tz

  • Ni Nani Huyu Anaenda Kukupigia Push-Up?

    Hakuna mtu ambaye anaenda kupambana kwa ajili yako. Kufanya kazi ambazo unapaswa kufanya, kufikia mafanikio ambayo unataka wewe.

    Hakuna mtu wa aina hiyo.

    Wewe mwenyewe ndiye unapaswa kupambana kwa ajili yako, mwenyewe.

    Jua malengo ambayo unapaswa kuyafanyia kazi.
    Kisha yafanyie kazi bila ya kuchoka.

    Maisha haya ni mafupi na siyo ya kupoteza.

    Yatumie vizuri kupambana kwa ajili ya ndoto zako.

    Ni jana tu niliokupa ofa ya kupata vitabu vyangu viwili kwa bei ya ofa. Vitabu vyenyewe ni kitabu cha
    MAISHA NI FURSA: ZITUMIE ZIKUBEBE pamoja na kitabu cha
    AKILI YA DIAMOND: Mambo 50 Ya Kujifunza Kutoka Kwa Diamond Platnumz Kuhusu Kipaji, Ubunifu Na Mafanikio.

    Gharama ya vitabu hivi vyote viwili Ni zaidi ya 25,000. Ila leo nataka nikupe ebooks zake kwa 8,000/- tu.

    Upo tayari? Lipia sasa hivi nikutumie ebooks hizi za kipekee sasa.

    Kumbuka: Ebook hizi utazipata kwa 8,000/- tu badala ya 25,000+

    Ni mimi rafiki yako
    Godius Rweyongeza
    0755848391
    Morogoro-Tz

  • UKIANGUKA SIMAMA TENA

    Usijivunie kuwa hujawahi kushindwa, bali jivunie kuwa ulisimama tena baada ya kuwa umeanguka-Ralph Waldo Emerson

    Ni vibaya kushindwa, ila ni vibaya kama hujwahi kujaribu na kushindwa-Theodore Roosevelt

    Mtu pekee ambaye hajawahi kufanya makosa ni yule ambaye hajawahi kufanya chochote-Theodore Roosevelt

    Sikushindwa mara 10,000 bali nilijifunza njia 10,000 za kufanya kitu kwa usahihi-Thomas Edison

    Mambo yakienda vibaya, yaache yaende peke yake-

    Mtu aliyeshindwa kuliko wote ni yule ambaye hajawahi kujaribu kitu-Dr. Larry Kimsey

    Ili mtoto aweze kutembea vizuri na kuwa mbobevu, basi anapaswa kuanza kwa kuanguka na kusimama tena na kuanguka tena. Hakuna mtu ambaye huwa anamcheka mtoto kwa sababu ameanguka chini wakati akijaribu kutembea. Kila mtu huwa anafurahia kwamba mtoto huyu ameweza kujaribu kutembea, japo ameanguka. Hiyo ni ishara kwamba huyu mtoto ana uhai ndani yake.

    Ila mtoto ambaye hata haoneshi dalili za kutembea ni wazi kuwa anawatia mashaka wazazi wake. Sasa hili linapaswa pia kuwa kwako.

    Ukiona kwamba hauna changamoto wala hujashindwa kwa lolote, basi fahamu kuwa kuna sehemu unakosea. Kuna hatua hauchukui. Kufanikisha ndoto zako sio kitu rahisi.

    Kuna mtu mmoja aliwahi kunukuliwa akisema kwamba; nilipogundua kwamba katika vitu tisa ninavyofanya ninafanikisha kitu kimoja tu, basi niliongeza juhudi katika vile vitu ambavyo nilikuwa nafanya.

    Pengine na wewe unaweza kukuta kwamba unapaswa kufanya vitu mara kumi ili kufanikiwa kwa kishindo mara moja. Usichoke kuinuka hata baada ya kuanguka na kuendelea mbele.

    Kitu pekee unachopaswa kuondoka nacho kwenye kuanguka kwako ni somo la kufanyia kazi. Kumbuka kwamba kushindwa sio mwisho wa safari bali unakuwa unajifunza njia sahihi za kufanikisha hicho kitu. Mafanikio ni asilimia 1 ya kushindwa ambako ni asilimia 99, kama alivyowahi kusema Thomas Edison mgunduzi wa karne ya 21.

    Sasa inashangaza kwenye maisha ya kila siku kwamba kuna watu ambao wanaogopa kuanguka na hivyo kuficha makosa ili wasionekane kwamba walishindwa au kuna wakati walifanya uamuzi mbovu. Hata ukiangalia wasifu wa watu mbalimbali, huwa ni wasifu chanya wakionesha vitu ambavyo watu hao wameweza kufanikisha na kufanya kwa ubora na huku wakiepuka kutaja vile vitu ambavyo walifanya hovyo. Ila ukweli ni kuwa hata kwa vile vitu ambavyo huwa unafanya hovyo, huwa kuna kitu cha kujifunza na kuchukua hatua.

    Hivyo, ukianguka au ukifanya kitu hovyo, usianze kutafuta sehemu ya kujificha ili usionekane. Badala yake jiulize ni kitu gani ambacho umejifunza kutokana na kuanguka huko, kitu ambacho kitakusaidia wewe kusonga mbele na kufanya mambo mengine makubwa zaidi. Ukijifunza kutokana na kushindwa kwako unakuwa hujashindwa. Kitu kingine unachopaswa kufahamu ni kuwa kushindwa ni tukio ila sio wewe. Pia, unapaswa kufahamu kuwa kuna watu wengi ambao hata hawajajaribu kufanya hicho ulichoshindwa.

    Baba mkubwa wangu aligombea udiwani 2010 akashindwa, aligombea tena 2015 akashindwa, alirudia tena 2020 na kushindwa. Watu wengi walikuwa wanamcheka na kusema kwamba anapoteza muda na fedha zake. Hata hivyo, nilikuja kugundua kuwa asilimia kubwa ya watu waliokuwa wanamcheka kuwa ameshindwa na anapoteza fedha zake hawakuwa watu ambao wangeweza kuchukua hatua kama zake. Hivyo, kwangu alikuwa mshindi mara mia zaidi ukilinganisha na hawa watu waliokuwa wanakaa vjiweni kumbeza.

  • Maisha Ni Fursa: Zitumie ZIKUBEBE

    Unaendeleaje rafiki yangu wa ukweli. Jana nilikutana na kichekesho fulani hivi mtandaoni. Jamaa mmoja alikuwa akizungumzia kuhusu mfumuko wa bei unayoendelea Sasa hivi.

    Hivyo akawa amesema maneno haya:

    Jamani jamani, mtuonee huruma mnapandisha vitu mno. Mafuta mnapandisha, gesi mmepandisha, uchumi mmepandisha, mtapandisha hadi mapepo……..

    Baada ya kuangalia hiki kichekesho, nilijiuliza hivi Kuna fursa yotote kwenye mfumuko huu wa bei. Kuna fursa yotote hapa?

    Nikakumbuka kitabu changu cha MAISHA NI FURSA: ZITUMIE ZIKUBEBE nilichoandika miezi kadhaa nyuma.

    Nikaona kweli hapa Kuna fursa…Na hiki kitu ndiyo kimenifanya nikutumie ujumbe sasa hivi …….Nataka nikwambie kwamba MAISHA NI FURSA, ZITUMIE ZIKUBEBE. Na kwa sababu hiyo nataka nikupe ofa ya kupata kitabu hiki.

    Kwa kawaida kitabu hiki kinauzwa kwa gharama ya 10,000 (ebook).Sasa wewe utalipia 8,000 tu. Lakini siyo tu kwamba utapata ebook ya kitabu hiki peke take.Bali pia nitakutumia na ebook ya AKILI YA DIAMOND: E-BOOK hii imezungumzia MAMBO 50 YA KUJIFUNZA KUTOKA KWA DIAMOND PLATNUMZ KUHUSU KIPAJI, UBUNIFU na MAFANIKIO.

    Kina Mambo 50 tu, ila ni Mambo konki!

    Kwa hiyo kwa elfu 8 unaenda kupata ebook hizi mbili za kipekee

    MAISHA NI FURSA ZITUMIE ZIKUBEBE pamoja na

    AKILI YA DIAMOND: Mambo 50 Ya kujifunza kutoka kwa Diamond Platnumz kuhusu Kipaji Ubunifu na Mafanikio.

    Amua sasa kupata ebook hizi mbili za kipekee kwa bei ya ofa ambayo haitajirudia tena. Utatuma fedha kwa 0684408755 jina ni GODIUS RWEYONGEZA, halafu utanitaarifu kwa namba hiyohiyo.

  • Zawadi Yako Kama Hutakata Tamaa


    Rafiki yangu, unapofanya  kitu kikaenda ndivyo sivyo, usikate tamaa.

    Kwa sababu kadiri unavyokosea ndivyo unazidi kuwa imara zaidi.

    Makosa ni mwalimu mzuri kama utayatumia vizuri.  Ndio maana wahenga wetu wanasema kufanya kosa siyo kosa. Kosa ni kurudia kosa.

    Ukirudia kosa maana yake hukukifunza chochote na wala hukupata funzo lolote kutokana na kosa la kwanza.

    Na ukiendele kurudia kosa lilelile kila Mara, huwezi kupiga hatua kubwa kimaisha.

    Sasa labda nikuulize wewe makosa ambayo huwa yanatokea kila siku kwenye maisha yako, huwa yanakuimarisha au huwa yanakubomoa?

  • Wazo Bora La Biashara

    Najua kila mtu anapenda kupata wazo zuri la biashara. Ukweli ni kwamba WAZO ZURI LA BIASHARA NI LILE AMBALO UNAWEZA KUFANYIA KAZI KWA SIKU 365 BILA KUCHOKA. Usipolifanyia kazi wazo lako, ujue utalinyima uhai.

    Ebu fikiria mtu ana wazo la kuchonga sanamu fulani, halafu hilo wazo akakaa nalo kichwani mwake.

    Unadhani wewe utaiona hiyo sanamu? Jibu ni hapana, kwa sababu sanamu hiyo haijachongwa. Kuchonga sanamu ni kuipa uhai, na hivyo kuifanya ionekane kwa watu wengine. Raha ya wazo sharti ulifanyie kazi na kufanyia kazi wazo lako.

    unafanya wazo liwe bora.

    Najua kitu hiki kinaweza kukushangaza kutokana na ukweli kuwa umeaminishwa kuwa wazo zuri la biashara ni lile ambalo linalipa. Labda nikuulize kuwa unajuaje wazo linalolipa na ambalo halilipi? Kwa hapa unaweza kujitetea na kusema wazo la kuanzisha mtandao kama Google, Facebook, au wazo la kutengeneza simu janja ni wazo ambalo lilikuwa linalipa pia. Ukweli ni kuwa mawazo haya yote yalikuwa hayana maana yoyote. Ni mpaka pale yalipofanyiwa kazi.

    Steve Jobs aliifanyia kazi iPhone kwa zaidi ya miaka miwili na nusu kabla haijaonekana kwenye uhalisia. Wazo la kuanzisha facebook halikuwa hata wazo bora, ni mpaka pale lilipofanyiwa kazi.

    Wazo la kuanzisha kampuni ya cocacola pia siyo kwamba lilikuwa ni wazo bora, ni mpaka pale lilipofanyiwa kazi. Sasa wewe kama huwezi kufanyia kazi wazo lako kwa siku 365 zijazo tu.

    Linaweza lisije kuleta manufaa yoyote maishani. Utaaishia kufa nalo na kwenda kujaza makaburi na wazo lako zuri. Kitu kikubwa cha kuondoka nacho kwenye kipengele hiki ni kwamba unapaswa kuanza kufanyia kazi wazo lako, tena unapaswa kuanza kulifanyia kazi leo hii. Kila la kheri

  • Hivi Ndivyo Unaweza Kutenda Miujiza Maishani Mwako

    Ninaandika hii makala tukiwa kwenye mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan kwa waislam.

    Kwa kawaida baada ya mfungo wa Ramadhan ndio huwa zinafuata sherehe za Idd. Hakuna mwaka hata mmoja nimewahi kusikia waislam wamesherehekea Idd bila ya kufunga kwanza. Haijawahi kutokea na wala haitakuja kutokea.

    Kwa kawaida siku ya Idd huwa ni sikukuu kubwa, ambayo inatanguliwa na siku 30 za kufunga kwanza.
    Hiki kitu kinanifunza kuwa hakuna zuri ambalo huwa linatokea tu hivihivi bila ya kuandaliwa. Badala yake kila zuri huwa linaandaliwa tena siyo kwa siku moja, huwa linaandaliwa kidogokidogo.

    Hakuna mtu AMBAYE anaweza kususa kufunga, halafu akasubiri siku moja kabla ya Idd na akafunga kwa ajili ya siku zote za nyuma ambazo hakufunga. Badala yake unapaswa kufunga kila siku kwa siku 30 mfululizo. Hiki kitu kinanifundiaha kuwa fanya ufanyavyo, kwa majukumu ambayo unapaswa kuyafanyia kila siku, usikose kuyafanya.

    Hiki kitu pia kinatumika kwenye maisha ya kawaida. Huwezi kwa mfano kuweka malengo yako ya mwaka. Na kukaa chini ukisubiri uje kuyafanyia kazi mwishoni mwa mwaka. Ni lazima kila siku ufanye kitu kuelekea kwenye malengo yako. Ule muunganiko wa vitu vidogo unavyofanya kila siku, ndio mwisho wa siku unakuwezesha wewe kufikia malengo yako.

    Kwa hiyo kwa kitu chochote kikubwa ambacho unataka kufanya, fikiria namna ambavyo unaweza kuanza kukifanya kwa kuanza kidogo, Kisha ukakiendeleza zaidi na zaidi ya hapo.

    utani tu!!

    Vitu vyote vikubwa Kuna wakati vilikuwa vidogo. Walau mfano mzuri tu ambao watu huwa wanatokea ni mfano wa Mbuyu, kuwa ulianza kama mchicha.

    Kikawaida Mbuyu ni mkubwa, Ila huwa hauoti kwa siku moja tu. Unaota kwa siku nyingi sana. Hakuna siku moja kwenye ukuaji wa Mbuyu ambayo inaweza kujigamba kuwa yenyewe ndiye ilifanya mti ukue. Maana uwepo wa siku moja ndio chanzo Cha uwepo wa siku nyingine na ndio ukuaji wake unaendelea.

    Kuna watu wamekuwa wanabeza suala zima la kuanza kidogo kwa kutaka waanzie juu. Na wengine kwa kutaka wafanye makubwa kimiujiza. Kama kuna muujiza unauhitaji kwenye maisha yako, Basi Ni muujiza wa kutumia vizuri siku moja moja unayokutana nayo maishani mwako.

    Kila siku weka akiba hata Kama ni kidogo. Baada ya muda hicho kidogo litakuwa kikubwa
    Kila siku soma kitabu hata Kama ni kurasa kidogo, baada ya muda hizo kurasa chache zitakuwa nyingi na zitakuongea maarifa ya kutosha. Nashauri uanze kwa Kusoma kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO. Kutakusaidia sana kufanya makubwa.

    Ni Mimi rafiki yako
    Godius Rweyongeza kutoka SONGAMBELE
    Tuwasiliane kwa 0755848391
    Morogoro-Tz

  • Kwa Nini Unasherehekea Mabadiliko Yaliyo Nje Ya Uwezo Wako Pekee?

    Kuna watu vitu ambavyo huwa wanasherehekea kama mafanikio yao ni vile vitu vilivyo nje ya uwezo wao. Yaani, watu wanasherehekea sherehe kama pasaka, idi, siku za kuzaliwa,…

    Haya yote ni mabadiliko ambayo yanatokea kila mwaka, ila mabadiliko haya yapo nje ya uwezo wako. Wewe siyo unayesabisha mabadiliko haya, badala yake kalenda iko hivyo. Kwa mfano, wewe huwezi kuamua kwamba mwaka huu sikukuu ya uhuru isherehekewe siku nyingine tofauti na ile iliyozoeleka. Hata hivyo, kuna mabadiliko ambayo unaweza kufanya kwenye maisha yako. Na mabadiliko haya yanaweza kuleta utofauti.

    Kuanzia mwaka huu unapaswa sasa kuamua kwamba wewe huendi kusherehekea mabadiliko ambayo ni ya kalenda tu. badaa yake unaenda kufanya mambo ya tofauti yatakayokupelekea wewe kupata matokeo ya tofauti. Na hivyo, kukuwezesha kusherehekea mafanikio yaliyotokana na juhudi zako pia

X