Author: Godius Rweyongeza

  • Ushauri Kwa Kijana Ambaye Anaanza Maisha Na Angependa Kufanya Kitu Anachopenda Ila Hajui Pa Kuanzia

      Mara nyingi huwa unakuta kwamba, kijana anapoenda kusoma chuo,  anasoma kitu ambacho wazazi wake au walezi wake wameona kwamba kinafaa kwake. Hivyo, hata anapoenda kufanya kazi, anaenda kufanya kazi ambayo haitaki.   Lakini kwenye zama hizi hapa, ni rahisi sana kwa kijana kufanya kazi ambayo anataka hata kama chuo kasomea kitu ambacho walikuwa hataki.…

  • Hizi hapa ni kazi nne za fedha

    Moja ya kitu ambacho watu wengi wamekuwa hawajui ni  kazi za fedha. Wengi wamekuwa wanafikiri kwamba fedha ina kazi mbili. huku wachache wakifikiri kwamba fedha ina kazi tatu na ni wachache zaidi ambao wanafikiri kwamba fedha ina kazi nne.  Hivyo leo nimeona nikuweke kwenye kundi la wachache zaidi ambao wanafahamu wazi kwamba fedha ina kazi…

  • Mafunzo Saba (07) Muhimu Kutoka Kwa Wajasiliamali Saba Waliofanikiwa Kibiashara Kwenye Karne Ya 19

    Siku ya leo ninaenda kukuletea masomo saba muhimu kutoka kwa wajasiliamali na wagunduzi bora a karne ya 19. Kutoka kwa watu hawa utaweza kujifunza mengi ambayo unaweza kuchukua hatua. Ujue ipo hivi rafiki yangu. Kwenye maisha unaweza kuamua kujifunza kutoka kwa watu waliofanikiwa au unaweza kuamua kujifunza ambao hawajafanikiwa. ubora wa kujifunza kwa watu waliofanikiwa…

  • Jifunze Ujuzi Huu Mmoja Tu, Utakufaa Maisha Yako Yote

    Ebu fikiria kama ndani ukijifunza ujuzi wako mmoja tu ambao hakuna mtu mwingine ataweza kukuibia ujuzi huu  maisha yako yote. Ujuzi ambao utaweza kuendelea kuwa nao utakusaidia miaka na miaka. Ujuzi ambao utakuwa nao nyakati zote bila kujali hali ya hewa au mazingira. Ebu fikiria ujifunze ujuzi huu sasa hivi ikiwa ni mwishoni mwa mwezi…

  • Hivi Ndivyo Unaweza Kusoma Vitabu Vingi Kwa Muda Mchache

    Siku si nyingi sana niliandika makala iliyokuwa inaeleza jinsi ambavyo nimeweza kusoma vitabu tisa kwa kipindi cha wiki moja na nusu.  Moja ya swali ambalo watu waliniuliza ni swali la je, nimewezaje kusoma vitabu vy te hivyo kwa kipindi kifupi hivyo?  Inawezekana wewe pia ukawa unajiuliza swali hili hapa. hivi inawezekanaje kusoma vitabu vingi kwa…

  • Vikwazo Kama Hiki Hapa Huwa Vinatokea Kukuimarisha Sio Kukuangusha

    Moja ya kitu ambacho ambacho kimekuwa gumzo na bado kinaendelea kuwa gumzo ni virusi vya korona. Kila mtu amekuwa kila mtu amekuwa akiongea na kutazama  kwa jicho la tofauti na huku wengi wakifikiri kwamba uwepo wa virusi hivi ndio mwisho wa dunia. Siku ya leo nataka niokuoneshe jinsi vikwazo kama Corona ambavyo vipo kukuimarisha wewe…

  • Salaam Zangu Kwako. Nimekuwa Kimya Kwa Muda Sasa Haya Hapa Ndio Niliyogundua

    Unaedeleaje rafiki yangu, ni takribani wiki sasa nikiwa sijakutumia ujumbe wa moja kwa moja  na wala nikiwa sijaandika na kuweka makala kwenye blogu ya SONGA MBELE. Pole sana rafiki yangu kwa mimi kupotea ghafla bila kutoa taarifa. Ila nipende tu kukwambia kuwa kama wahenga wanavyosema. Kimya kikuu kina mshindo mkuu. Kwa upane wangu mambo yako…

  • KANYAGA MAPIGO YOTE YA KUITWA MTU WA KAWAIDA

    Moja ya kitu ambacho jamii imekuwa inakutega wewe hapo, ni kukuweka kwenye kundi la WATU WA KAWAIDA. Utasikia watu wanasema, sasa mtuangalie na sisi watu wa kawaida. mwingine atasema, sasa sisi watu wa kawaida hii itatusaidiaje. Leo hii nataka nikwambie hivi, kanyaga mapigo yote ya kuwa mtu wa kawaida. Ukiendelea kujiita mtu wa kawaida maana…

  • Kitu kimoja Ambacho Watu Hawajui Kuhusu Biashara Zao

    Kitu kimoja ambacho hawajui watu kwenye biashara wanazofanya ni kuwa na wao ni wateja wa biashara zao.  Kitu hiki kinawafanya watu hawa kutoa bidhaa kwenye biashara bila mpangilio maalumu kwa sababu tu wao ni wamiliki wa biashara hizo.  Rafiki yangu, hili ni kosa kubwa ambalo hupaswi kufanya. Kuna wakati wewe unapaswa kuwa mteja kwenye biashara…

  • The Mamba Mentality

    Huwezi kupenda kuufikia ukuu wakati bado unaendelea kutembea kwenye mstari mnyoofu.  Kama unapemda kufikia mafanikio basi ni wazi kwamba utapaswa kunyanyuka hapo ulipo. kuchukua hatua za ziada na kusongambele. Kuwa tayati kuchukua hatua amabazo hujawahi kuchukua.Kuwa tayari kujaribu vitu hata kama wengine wataona havifai.kuwa tayari kuipigania ndoto yako. Ukuu hauji kizembe kizembe. Ni mchakato. Nakutakia…

  • Kama Huwezi Kuwa Kichaa Wa Ndoto Yako, Basi Isahau

    Moja ya kitu kinachowafanya watu wengi washindwe kutimiza ndoto zao ni kwa sababu tu ya hawataki kuonekana vichaa miongoni mwa watu. kwa nini? Kwa sababu siku zote ndoto huwa ni kubwa kiasi kwamba mtu akianza kuisema mbele za watu basi ataonekana kama kichaa vile. Una ndoto yako kubwa kwa jamii unakuwa kama muasi. Maana jamii…

  • Maeneo Matatu (03) Ya Kutembelea Unapokuwa Mtandaoni

    Usikose kutembelea maeneo haya matatu kila unapoingia mtandaoni kila siku. Ujue watu huwa wanaingia mtandaoni kwa kusukumwa na vitu mbalimbali. ila kwa jinsi ambavyo ninakufahamu wewe moja ya kitu ambacho kinakukfanya uingie mtandaoni ni kujifunza. si ndio? Kama ndio hivyo, basi hapa nina kuletea maeneo mawili muhimu ambayo hupaswi kukosa kutembelea kila siku unapoingia mtandaoni.…

  • KITABU NI LENZI

    Siku zote kuwa unasona kitabu, maana kitabu ni lenzi ya kuiona dunia vizuri. Kama kuna kitu ambacho hukielewi, chukua kitabu usome.Ukikwama, chukua kitabu usome.ukiwa hauna cha kufanya, chukua kitabu usome.ukiwa na fikra hasi, chukua kitabu usome. ila ukweli ubaki kuwa siku zote kuwa unasona kitabu  Maana kitabu ni lenzi ya kuona dunia vizuri. kazi ya…

  • Washindi Huwa Wanafanya Hivi Baada Ya Changamoto

    Mara nyingi unapoanza kufanya kitu mwanzoni matokeo mrejesho wake huwa ni mdogo sana. Kwa mfano unaweza kuanzisha biashara ukiwa na timu kubwa ya watu ambao wako nyuma yako na wanakuahidi kununua ila baada ya kuanzisha biashara ukawa huwaoni watu hao kwenye biashara. Au pengine unaweza kuanzisha biashara ukitemgemea kupata mwitikio mkubwa wa wateja kuanzia siku…

  • Ebu Jionee Jinsi Tone La Wino Linavyoweza Kubadili maisha Yako

    Moja kati ya usemi maarufu sana wa Lord Bryon ni ule aliosema kuwa tone la wino, linaweza kuwafnya mamilioni ya watu kufikiri. Na hii ni kweli kwa asilimia zote. Ukitaka kunielewa kwenye hili napenda nikupe mfano wa karatasi nyeupe ambayo imewekwa nukta moja tu katikati. ukiwaita watu wakuambie wanaona nini kwenye hiyo karatasi wapo watakaokwambia, …

  • Kama Unataka Kuhamisha Mlima Basi Anza Kutoa Jiwe Moja Leo

    Rafiki yangu, ni wazi kuwa kila mtu ana ndoto ya kufikia mambo makubwa sana maishani mwake. Kila mtu angependa kile kilicho kwenye akili yake kinatimia. Lakini sasa tatizo la watu wengi ni kutochukua hatua ya kwanza. Siku ya leo nimeona waziwazi kwamba niongee na wewe moja kwa moja kuwa kama una ndoto ya kuhamisha mlima…

  • Hivi Ndivyo Unaweza Kufanya Makubwa Mpaka Kumzidi Mwenye Kipaji

    Rafiki yangu kuna vitu sita ambavyo unaweza kuvitumia kumpita mwenye kipaji na wewe ukaweza kufanya makubwa hata zaidi ya yeye. Kitu cha kwanza ni kuchagua eneo ambalo unaweza kuwekeza nguvu zako. pili ni kuamua kuwa hapa kufa na kupona mpaka kieleweke. Siachi kufanya hiki kitu mpaka nipate mafanikio. Tatu, ni kufanya kazi kwa bidii. Ukifanya…

  • Maisha Yangekuwa Rahisi Kama Kungekuwa Na Kitu Hiki

    maisha yangekuwa rahisi sana, kama kungekuwa na kibao cha mabadiliko kwenye safari ya maisha. Yaani kwamba ukikifikia kibao hicho unajua kwamba kuna mabadiliko mbele yatatokea baada ya mita mia, hivyo na wewe utapaswa kubadilika. Lakini ukweli ni kwamba mabadiliko hayatokei kwa kelele kubwa. Ndio maana baadhi ya watu huyapokea na wengine huyapuuza. kama kila mtu…

  • Hivi Ndivyo Unaweza Kupata Kitu Cha Kuandika

    Habari ya siku hii njema sana rafiki yangu. Bila shaka siku ya leo imeanza vyema kabisa rafiki yangu. Siku ya leo, nataka nikwambie kitu kimoja muhimu sana  kuhusu uandishi. Ujue rafiki yangu moja ya  swali ambalo watu huwa wanauliza mara nyingi sana linapokuja suala la unandishi ni swali la je, mimi ninandike kitu gani. Ukweli…

  • Ushauri muhimu kwa mtu anayetaka Kubobea kwenye Uandishi

    Rafiki yangu hongera sana kwa siku hii ya kipekee sana. Siku ya leo, nimekuja na ushauri kwako wewe ambaye ungependa kubobea kwenye uandishi. Kuna namna mbili za wewe kuweza kuwa mwandisho bora. Kwanza ni kuhakikisha kamba unaandika mara kwa mara. Kitu hiki kitakufanya uwe unaboresha uandishi wako kila unapoandika na hivyo kukufanya uwe mbobezi baada…

X