Category: Uncategorized

  • Maeneo Mawili (02) Ambayo Hayahitaji Bajeti

    Katika maisha ya kila siku mambo yetu mambo mengi sana yanakwenda kwa bajeti. Ukipata mshahara au kipato chako kikiingia kitu cha kwanza unachokifanya ni kuweka bajeti.Hii inakuhakikishia kwamba umeitumia vizuri kila senti inayoingia kwenye mfuko wako Ukinunua chakula chako unakiwekea bajeti kwa kuhakikisha kwamba chakula Fulani kitatumika siku fulani na kingine siku nyingine. Unakuwa una uhakika…

  • Acha Kulalamika, Anza Kuishi

    Acha kulalamika kwamba hauna muda wa kutosha kwa ajili ya wewe kufanya mambo fulani. Acha kulalamika kwamba kuna watu wanatumia uchawi kufikia mafanikio. Acha kulalamika kwamba wewe umezaliwa kwenye familia maskini Acha kulalamika kwamba serikali haijafanya kitu kwa ajili yako. Chukua hatua hakuna kitu ambacho hakipo ndani ya uwezo wako, hakuna ambacho huwezi kukifanya wewe…

  • KONA YA SONGA MBELE; Zaeni Mkaongezeke.

    Sasa tuangalie leo kwenye kona ya songa mbele kuna nini?.Zaeni muongezeke mkaijaze nchi.Baada ya Mungu kumuumba mwanadamu alimwambia maneno hayo. Maneno ambayo Mungu alilenga juu ya suala zima la kuendeleza kizazi. Katika suala zima la kuzaa na kuongezeka naweza kusema binadamu amefaulu kwa maksi za juu sana mpaka sasa hivi ninapoandika makala hii. Lakini tatizo…

  • Jifunze Kutoka Matukio Ya Zamani

    “experience is a best teacher“Uzoefu ni mwalimu mzuri huu ni msemo wa kiingereza ambao binafsi huwa napenda kuutumia. Huwa unanipa nguvu ya kujifunza kutoka kwenye makosa yangu ya zamani, kuyafanyia marekebisho na kuja na kitu kipya Kizuri na bora zaidi. Usiweke nguvu kubwa sana kwenye makosa yako ya zamani au matatatizo yako ya zamani na…

  • Unayofikria Hayawezekani Yanawezekana

    Je, unaamini katika miujiza? Je, unaamini kwamba mambo ambavyo unafikiri au watu wengine wanafikiri hayawezekani yanawezekana?mimi naamini hivyo? Yasiyowezekana yanawezekana. Hivi ushawahi kujiuliza ni kitu gani kinafanya watu zaidi ya 1000 wanaingia kwenye ndege na kupaa? Au kwamba upo nyumbani kwako umekaa na unamtumia mtu meseji aliye mamilioni ya kilomita kutoka ulipo na inamfikia? Yasiyowezekana…

  • Hili Ni Jambo Linaloendelea kukuweka Hapo Ulipo.

    Vitu vyote duniani havibaki kama vilivyo bali vinabadilika kadri ya mazingira na maeneo. Binadamu pia hajaachwa nyuma katika mabadiliko haya. Na ni mtu ambaye anabadilika kila siku katika utendaji, ukuaji na kufikiri. Hii ni sheria ya asili yaani, kama ambavyo mti unapandwa ukiwa mbegu vivyo hivyo binadamu anahitaji kubadilika hili kuendana na mazingira. Mabadiliko yana…

  • Jifunze Kuvua

    Kumfundisha mtu kuvua ni njia nzuri ya kumwondoa kwenye kuomba samaki maisha yake yote.” Askofu Oyedepo Kuna mtu aliwahi kusema kwamba “Afrika ni nchi pekee duniani ambapo mtu unaweza kuokota pesa njiani wakati wananchi wake hawajaiona.” Kuonesha kwamba wingi, uzuri, ubora wa  raslimali zilizopo mtu anaweza kuzitumia raslimali hizi kusonga mbele. Hakuna kitu chochote kinachotokea…

  • Kioo Hakidanganyi

    Tunapoangalia kwenye kioo tunajiona sisi wenyewe. Itaonekana ajabu pale utakalalamika kwamba juu ya kile unachokiona kwenye kioo. Ni ajabu pia kubadili kioo ili upate picha ya tofauti. Kama tunataka kubadili picha ya kweye kioo lazima tujibadili sisi wenyewe. Kwa maneno mengine ni kwamba kama hutaki matokeo ya kile unachopata kwenye maisha basi unahitaji unahitaji kujibadili…

  • Usijilinganishe Na Wengine

    Moja kati ya vitu ambavyo vimekuwa vinaharibu maendeleo na mafanikio ya watu ni kujilinganisha. Hili suala naweza kusema ni tabia moja ambayo binadamu anayo na inamrudisha nyuma. Kujilinganisha na watu sio kubaya ila  ubaya unakuja pale unapokufanya kuwa kipimo  cha maisha yako. Pale kujilinganisha kunapokufanya kuwa mvivu wa kufikiri na  kuacha kufanya kwa kujiona wewe…

  • Miaka 20 Iliyopita Miaka 20 Ijayo

    Tupo katika dunia ambayo mambo yake yanabadilika kila siku asubuhi mchana na jioni. Kutokana na  mabadiliko hayo basi sisi wenyewe tunahitaji kubadilika. Maana ni asili kwamba vitu lazima vibadilike. Miaka 20 iliyopita intaneti ilitumika kwa ajili ya kutuma na kupokea e-mail lakini leo mambo yamebadilika. Miaka 20 kujifunza ilikulazimu uende darasani ukamsikilize mwalimu, leo hii…

  • Ifahamu Tofauti Kati Ya Kupenda Na Kupata

    Habari za leo na ndugu msomaji wa blogu ya songa mbele karibu sana katika makala ya leo ili tupate kujifunza kitu kipya cha kutufanya tusonge mbele Mara nyingi watu wanachanganya kati ya kupenda na kupata kitu. Kupenda kitu ni tofauti sana na kupata. Mfano mtu akisema napenda kupata gari ni tofauti kabisa na kupata gari…

  • Vunja Pingu Hizi

    Watu wengi wanatumia muda mwingi sana katika mitandao ya kijamii. Kati ya masaa nane ya kazi basi unakuta anatumia masaa matatu mpaka manne kwenye facebook.Kati ya masaaa kumi ya kuwa darasani ya mwanafunzi wa chuo basi matano anayatumia katika mtandao. Baada ya hapo mtu anatumia muda uliobaki katika kuangalia tv na kuangalia filamu. Wanavutiwa sana…

  • Kuwa Na Sababu

    Kila kitu ambacho kipo lazima kuna sababu ya kitu kile kuwepo na kitu chochote ambacho kinafanyika lazima kuna sababu ya kitu kile kufanyika. Lazima kuna sababu ya wewe kufanya kitu kile ambacho unafanya sasa hivi. Kama unanona unafanya kitu bila ya kuwa na sababu basi nakushauri acha kufanya sasa na anza tena Acha ili uweke…

  • Watu Sita Waliokuzunguka

    Wewe ni tofauti na mtu mwingine yule kwa wastani wa watu sita waliokuzunguka.  Kwa lugha nyingine naweza kusema kwamba maisha yako ni wastani wa maisha ya watu sita waliokuzunguka. Tabia zako, kipato chako, na matendo yako yote ni sawa na kuchukua wastani wa wa tabia, matendo, na kipato cha watu sita waliokuzunguka. Kumbe kama umezungukwa…

  • Yaboreshe Mazingira Yako Fanya zaidi.

    Habari za leo rafiki na ndugu msomaji wa blogu ya songa mbele. Karibu sana katika makala ya leo. Kila mtu kakulia katika mazingira tofauti  na ya mwenzake. Mazingira haya ni kuanzia nyumbani, shuleni na jamii kwa ujumla. Kama umekulia kwenye mazingira linapotumika jembe la mkono basi utakuwa na utaalamu na ujuzi wa kulitumia jembe la…

  • Wiki Moja Bila Habari

    Tupo katika ulimwengu ambapo habari zinasambaa kwa kasi kubwa sana. Tupo katika ulimwengu ambapo habari inaweza kuizunguka dunia nzima ndani ya dakika tano jambo ambalo halikuwahi kutokea miaka ishirini iliyopita. Gazeti lenye habari hasi linauza sana kuliko gazeti lenye habari chanya, au gazeti lenye historia ya mtu maarufu sana Gazeti lenye habari inayoeleza janga fulani…

  • Hili Hapa Jambo La kuogopa

    Muda  ambao mtu anaupoteza akiwa na hasira,Nguvu ambayo mtu anaipoteza akiwa na hasira, kupiga majungu na kuwachukia watu unatosha sana kumfanya kuwa tajiri katika maisha yake yote. Nwanadamu anapoteza robo tatu ya maisha yake yote bila kufanya kitu.Napolleon HillKatika maisha yangu sijawahi kusikia kwamba mtu kafaidika kutokana na hasira. Sijawahi kusikia kwamba hasira imezalisha kitu…

  • Vutia Kwako Tabia Hizi.

    Habari za leo rafiki na ndugu yanguKaribu sana katika makala ya leo. Ili kufikia mafanikio na kufikia sehemu ambayo inaonekana iko juu sana katika ulimwengu wa mafaniko unahitaji kuwekeza sana kwa kuweka nguvu, muda, lakini pia kutafuta watu sahihi wa kwenda nao kwenda kwenye mafanikio na kuhakikisha wamekufikisha kule ambapo wewe unataka kufika. Huwezi kutoka…

  • Utumie muda wako wa safari vizuri

    Habari za leo rafiki na ndugu msomaji wa makala za SONGA MBELE karibu sana katika makala ya leo ambapo tunaenda kujifunza kitu kipya ambacho kitabadilisha mtazamo wako na mwelekeo wako kiujumla na kukufanya kuwa mtu mpya kabisa. Kitu ambacho kitakusogeza sana karibu sana na mafanikio. Kujifunza kila siku ni njia nzuri ya kukufanya uzidi kusonga…

  • Ubongo Ni Bustani

    Habari za leo rafiki yangu na msomaji wa makala kutoka SONGA MBELE BLOG. Matumaini yangu unaendelea vyema na hatua kuelekea mafanikio ndani ya mwaka wetu huu mpya wa 2017. Karibu sana katika makala ya leo, ili tuendelee kujifunza maana hakuna sherehe kwa mwanamafanikio katika kujifunza. Kujifunza kunakufanya unakuwa kijana hata kama una miaka themanini (80) lakini…

X