Category: A NOTE FROM SONGAMBELE

  • Jinsi Ya Kuweka Oda ya Kitabu Cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO

    Hello! Bila shaka unaendelea vyema. Kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO (hardccopy) kitatoka rasmi tarehe 20.5.2022 Hili ni toleo la pili la kitabu hiki cha kipekee. Karibu uwe miongoni mwa watu ambao watapata nakala ya kitabu hiki. Kwa wakazi wa mikoa ya Dar, Pwani na Morogoro mtafikishiwa nakala popote pale mlipo. Kama upo nje…

  • Usiweke bajeti kwenye AKILI yako.

    Kama umeanza kufanya hivyo, basi kuanzia leo iondoe bajeti hiyo maana ni kikwazo kikubwa sana. Akili yako itumie kubuni vitu vipya, itumie kufikiria mbinu mpya za kutatua matatizo, itumie kuongeza MAUZO kwenye biashara. Tafiti nyingi zimefanyika na tafiti hizi mara zote zimekuja na jibu moja kuwa watu wengi wanatumia chini asilimia kumi ya uwezo wao.…

  • Kuna Nini Kwenye Toleo La Pili La Kitabu Cha Jinsi Ya Kufikia Ndoto Zako

    Jana nilitangaza kuwa tarehe 20 Mei toleo la pili la kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO litakuwa tayari. Nakala zitafikishwa mpaka nyumbani kwako au ofisini kwako kwa wakazi mikoa ya Dar, Pwani na Morogoro. Hata hivyo, kama upo nje ya hii, mikoa, nakala zitatumwa na utazipokea vizuri tu. Nakala moja ni 20,000/- . hata…

  • Kama Unataka Mali: Maeneo Matano Unapoweza Kupata Mali Halali…

    Unalikumbuka lile shairi la kama mnataka mali mtaipata shambani? Ila shairi hili…walilisoma baba zetu, sisi tumelisoma na sasa watoto wetu wanaenda kulisoma pia. Hahah Kitu kikubwa kwenye hili shairi ni kwamba kama unataka mali utaipata shambani. Leo hii nilikuwa nafiria hivi kwamba huyu mwandishi wa hili shairi angekuwa analiandika sasa hivi, hivi kweli bado angeendelea…

  • YAH: UJIO WA TOLEO LA PILI LA KITABU CHA JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO

    Hello upande wa huko, siku ya leo nina furaha kubwa sana. na ninapenda kukujulisha kuwa nakala za kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO toleo la pili, zinaenda kuanza kupatikana kuanzia tarehe 20 Mei 2022. Kwa mara ya kwanza kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO nilikizundua mwaka 2020 mwishoni, na sasa mwaka huu 2022…

  • Unajua kwa nini mpaka sasa hivi hufanikiwi?

    Enheee! Leo bwana, nataka nikuchokonoe kidogo. halafu baada ya kuwa nimekuchokonoa nitakwambia ni kitu unapaswa kufanya ili uweze kufika kule unapotaka kufika. Au basi! Ninajua, kwamba wewe una ndoto kubwa, una ndoto za kufika mbali na ndoto za kufanya makubwa kwenye maisha yako. Si ndio. Na kwa siku nyingi sana umekuwa unapambana ili kuweza kufikia…

  • Mazoezi Ndio Kila Kitu

    Leo nimekumbuka msemo mmoja wa kilatini. Unasema repetitio est mater studiorum .Ukimaanisha repetition is the mother of study. Tukiwa o-level walimu wetu walipenda kuutumia sana kutuhamasiaha ili tusome kwa bidii na kwa kurudia mara kwa Mara kile tunachosoma. Kadiri unavyofanya mazoezi na Tena kwa marudio, ndivyo unakuwa unaelekewa kwenye ubobevu Kumbuka repetitio est mater studiorum.…

  • Hakuna mtu Ambaye Anaenda Kupiga Kazi Kwa Ajili Yako

    Ngoja nikwambie kitu, hakuna namna ambavyo wewe unaweza Kuepuka kazi katika suala zima la kufanikiwa. Kama unataka kufanikiwa sharti uwe tayari kuweka kazi itakayokufikisha kule unapotaka kufika. Usije unategemea kwamba MTU yeyote atafanya kazi kwa ajili yako. Nakumbuka siku za nyuma niliwahi kuandika Makala hapa nikasema kwamba hakuna MTU ambaye anaweza kupiga Push-Up kwa ajili…

  • Siku 30 Za Kushinda Kwa Kishindo (Juzuu 1)

    Katika moja ya semina ambazo Zig Ziglar alikuwa anatoa kuna mtu mmoja ambaye alihamaki siku moja na kumwuliza, “hivi kwa nini hizi hamasa zenu huwa hazidumu?” Huku akiwa ametulia, Zig Ziglar alijibu kwa kusema kuwa hamasa ni kama kuoga, ukioga leo unapaswa kuoga na kesho. Tena wakati mwingine ukioga asubuhi utapaswa kuoga mchana na jioni…

  • Utapata Kile Unachotaka Kama Utawasaidia Watu Kiasi Cha Kutosha

    Utapata kile unachotaka kama utawasaidia watu kiasi cha kutosha kupata kile wanachotaka-Zig Ziglar. Ili wewe kupata kile ambacho unataka maishani unapaswa kuwa tayari kuwasaidia watu kupata kile wanachotaka wao. Kadiri unavyowasaidia watu kupata kile wanachotaka, ndivyo na wewe unakuwa kwenye njia ya kupata kile unachotaka. Kwa hiyo, kazi yako kubwa unayopaswa kufanya ni kutafuta kujua…

  • Jinsi Ya Kufanyia Kazi Ndoto Zako Wazazi Wanapokuwa Wanakupinga

    Karibia kila wiki huwa naandika makala moja inayohusu ndoto na jinsi ambavyo unaweza kufiki andoto zako kubwa ulizojiwekea maishani. Kwenye makala ya jumapili ya leo ninaenda kuandika kuhusu tena kuhusu hii mada ya kipekee. Ambayo kila nikishika kalamu kuandika basi najikuta nahamasika zaidi kufanyia kazi ndoto zangu mwenyewe. Halafu eti nikishika kalamu wakati natumia kibodi…

  • Historia ya Kiswahili

     Ukisoma historia ya Kiswahili  unaona kwamba kilianza kimasihala tu. Kilianza kutumiwa maeneo ya Pwani na baadaye kikasambaa kuja bara na mpaka leo hii, kina wazungumzaji zaidi ya milioni 150. Ni lugha pekee barani afrika ambayo siyo ya kigeni ila watumiaji wengi. Ninataka kusema nini sasa hapa.Ninataka niseme kwamba, kitu chochote kikubwa huwa hakianzi kwa ukubwa wake.Mbuyu…

  • IJUE NJIA YA KUFUATA

    Kama haujui njia ambayo unapaswa kuchukua basi njia yoyote ile itkupeleka Ebu fikiria kitu kama hiki hapa, umeenda stendi ili kukata tiketi, halafu unampa mkata tiketi pesa yako. Na unamwambia kwamba unaomba akupe tiketi unadhani atakuwambiaje? Au au nadhani swali gani atakuuliza? Unaelekwa wapi?  Ebu fikiria unamjibu kwamba sijui. Atakwambia kwamba kama haujui basi rudi…

  • Matendo yako, Ndio matendo yako

    Miongoni mwa ukweli ambao unapaswa kuufahamu ni kwamba matendo ndiyo yanapaswa kutangulia matokeo na siyo matokeo yatangulie matendo.Yaani, huwezi kuwa na afya njema kwanza, halafu eti ndio ukaja kuanza kula vizuri. HapanaUnakula vizuri ndio maana una afya njema.Unafanya mazoezi ndio maana una afya njema.Unaweka akiba benki ndiyo maana una fedha ya kutosha.Unawekeza ndio maana utajiri…

  • Nyakati Ngumu Hazina Ukomo

    Leo nimekumbuka mwaka 2018 na 2019 jinsi watu walivyokuwa wanalalamika kwamba vyuma vimekaza. Kuna watu wengi walikuwa wanasema kwamba hawawezi kufanyia kazi malengo yao kwa sababu tu vyuma vimekaza. Nakumbuka kila nilipokuwa nikiongea na watu, kitu muhimu nilichokuwa nikiwasisitiza kilikuwa ni kwamba, USISUBIRI VYUMA VILEGEE. Badala yake katika kukaza hukohuko, wewe mwenyewe pambana kuhakikisha kwamba…

  • Je, Kuna Namna Na Kutengeneza Fedha Kupitia Affiliate Marketing Ukiwa Nchini Tanzania?

    Habari ya huko upande wa pili. Mimi kutokea hapa mkoani Morogoro naendelea vizuri tu. Siku ya leo napenda kujibu swali la mmoja wetu hapa kwenye jukwaa ambaye ameniuliza kama kuna namna ya kutengeneza fedha kupitia affiliate marketing ukiwa hapa nchini Tanzania. Na mimi kwa ufupi napenda kusema kwamba INAWEZEKANA. Ila naomba usome ujumbe huu mpaka…

  • Songambele

     Rafiki yangu, muda wote na mara zote unapaswa kuwa mtu wa kusonga mbele. Usikubali kukwama na wala kubaki eneo lile bila ya kusongambele. Vitu ambavyo vinakaa sehemu moja bila ya kusongambele huwa vina sifa mbaya kweli.Maji yaliyotuama, ndio huwa yanazalisha mbu wa malaria. Hata mdomo wako ukiufunga bila kuongea kwa muda mrefu unatoa harufu mbaya.…

  • Fedha Chanzo Chake Ni Thamani

    Wachezaji Lionel Messi na Ronaldo wanacheza dakika 90 uwanjani na wanalipwa kiasi kikubwa Cha fedha kuliko wachezaji wengine. Unadhani kwa nini wanalipwaa kiasi kikubwa hivyo? Ni kwa sababu ya thamani yao wanayotoa. Kitu chenye thamani kubwa kinauzwa kwa bei kubwa ukilinganisha na kitu chenye thamani ya ndogo. Kama unataka kupata fedha basi unapaswa kuwa tayari…

  • Fanya Yafuatayo Kuepuka Kuwa Miongoni mwa Walalamikaji

    Moja ya kitu rahisi sana ni kulalamika. Kila mtu anaweza kukifanya. Lakini kitu kigumu kufanya ni vitendo na kuonesha matokeo. Sasa siku ya leo, nataka uepukane na malalamishi ili mwisho wa siku uwe mtu wa kuleta matokeo ambayo wewe mwenyewe unayatamani Unajua kwa Nini Watu wanalalamika? Kwa sababu kuna matokeo mazuri wanayataka ila  wanataka mtu…

  • Usikubali Kuendelea Kubaki Hivyo hivyo

    Kuna mtu mwaka 2010 alikuwa analalamika kuwa hana mtaji, mwaka 2015 alikuwa bado analalamika kwamba hana mtaji, mwaka 2020 bado analalamika kwamba hana mtaji. Na cha kushangaza zaidi ni kwamba mwaka 2025 atakuwa bado analalamika kwamba hana mtaji. Hivi ni kweli kwamba huyu hana mtaji au hayuko makini? Leo ninachotaka kuongea na wewe ni kwamba usikubali kubaki hivyohiyo.…

X