-
Jinsi Ya Kuanza Biashara Na Mtaji Kidogo Mpaka Kuikuza Kuwa Bisshara Kubwa
Siku moja nilikuwa naangalia mtandaoni, nlikutana na picha iliyokuwa inaonesha kampuni ya azam ilivyoanza kama mgahawa, ambao ulikuwa unahudumia katika mkoa wa Dar Es Salaam. Ambapo walikuwa wanafanya huduma za Catering na huduma nyingine zinahousisha hilo.
Picha hiyo ilikuwa ni picha ya tangazo ambalo walifanya mwaka huo. Kama sijakosea ule mwaka uliooneshwa kwenye ile picha ulikuwa ni 1984. Sijaweza kupata tena ile picha wakati naandika makala hii hapa, lakini endapo utaipata unaweza kuituma kwangu kupitia whatsap 0755848391 au godiusrweyongeza1@gmail.com
Sasa leo hii nataka niongelee jinsi na wewe unavyoweza kuanza bishara na mtaji kidogo na kuikuza kuwa biashara kubwa
Kwa wenginen wanaweza kuona hili kama ndoto fulani ya Habunwasi …
Wanaweza kuonakama vile ni kitu ambacho hakiwezekani. Yaani, kwa wengine hata ufanyeje, mafanikio yamewekwa kwa ajili ya watu wachache na wengine wapo hapa duniani kuhangaika.
Kitu hiki siyo kweli hata kidogo, wewe mwenyewe unaweza kuanzisha biashara hata kama utaanza nayo kidogokidogo, lakini bado ukaweza kuifikisha kwenye viwango vikubwa. zifuatazo ni hatua ambazo unapaswa kufuata kwenye hili hapa.
KUWA NA NDOTO KUBWA
Ili biashara ndogo iweze kufikia kuwa biashara kubwa unapaswa kuwa na ndoto kubwa kwanza. Watu wengi hawawezi kukuza biashara zao kwa sababu tu wanakuwa hawana maono makubwa tangu wanapoanzisha biashara. Wengi wa watu ambao unaona kwamba biashara zao ni za kawaida miaka nenda miaka rudi ni kwa sababu tu wanakuwa hawana ndoto kubwa tangu wanaanzisha biashara hizo.
Unakuta mtu anaanzisha biashar kwa ajili tu ya kupata hela ya kula na kutunza familia yake. Biashara ya aina hii ni ukweli kwamba usitegemee itafika mbali. Badala yake itaendelea kuwa biashara ya kawaida kila wakati.
Na muda mwingine hata itakuwa inafilisika na mwenye biashara anatakiw kuanza upya kwa kuingia mfukoni kutoa hela ili kuiamusha tena. Sisemi kwamba ukiwa na ndoto kubwa kitu kama hiki hatitatokea, ila ninachotaka ufahamu ni kwamba, usipokuwa na ndoto kubwa, kila kitu ambacho utafanya kitakuwa ni cha kawaida kwa sababu tu huna ndoto kubwa.
KUANZA KIDOGO
Ndio unapaswa kuwa na ndoto kubwa, ila ndoto kubwa peke yake tu haitoshi. Ndoto inapaswa kuwekwa kwenye vitendo kwa kufanyiwa kazi.
Kuwa na ndoto kubwa kuhusu biashara yako, ila anza kuifanyia kazi kidogo kidogo kadiri unavyokuwa unaenda.
TUNZA HESABU ZA BIASHARA YAKO
Mali bila kalamu huisha bila habari. Hiki ni kitu kikubwa ambacho huwa kinawafanya wafanyabiashara wengi waendelee kufanya biashara zao kwa namna ambayo ni ya kawaida sana kwa siku nyingi kiasi kwamba wanakuwa hawapati matokeo ambayo wanatakiwa kupata.
Biashara ni hesabu. Mara zote na muda wote tunza hesabu za biashara yako.
Kama unakwama na unajiuliza wapi unaweza kuanzia kwenye kutunza hesabu za biasahara yako, anza na kutunza hesabu za mapato na matumizi. Kiasi ambacho unaingiza na kiasi ambacho kinatoka, hivyo tu. Fanya hiki kwa mwezi mmoja, utakuwa tayari umeshakuwa mtaalamu wa biashara yako.
Tayari utakuwa unajua fedha inayoingia na fedha ambayo inatoka kwenye biashara yako. Na hicho ndiyo kitu kikubwa ambacho unahitaji walau kwa kuanzia.
FANYA BIASHARA KWA UTOFAUTI NA WASHINDANI WAKO WANAVYOFANYA
Angalia vitu ambavyo washindani wako wanafanya kwa namna ambayo ni ya kawaida, kisha wewe anza kuvifanya kwa namna ambayo ni ya tofauti kidogo. Kwa mfano, suala la kutunza mawasiliano ya wateja wako na kuwasiliana nao mara kwa mara linaweza kuleta matokeo na utofauti mkubwa kwenye biashara yako.
Lakini pia kama washindani wako wanachelewa kufungua na kuwahi kufunga, wewe kwako hili linaweza kuwa jambo la faida pia. Unaweza kuitumia nafasi hiyo kuanza kufungua mapema na kuchelewa kufunga kidogo ili kuwanasa wateja wanaokuwa wanadamka au wale wateja wanaofanya manunuzi wakiwa wamechelewa.
JIFUNZE KWENYE BIASHARA NYINGINE
Maisha yetu ya kila siku yanatufanya twende kwenye biashara nyingi sana. unapopanda daladala ujue kwamba unakuwa umepanda biashara ya mtu. Na hapo unaweza kujifunza kwa konda ambaye kwake kila mtu anayemuona ni mteja wake. anamkaribisha kwenye gari ili waondoke. Utasikia kondakta anasema unaenda dada, au kaka au mjomba…
Muda mwingine unaweza kushuka kwenye gari na bado konda akakukaribisha tena upande ili mwende ruti nyingne. Wewe pia, kuwa mtu wa kuwakaribisha watu.
Jifunze kwa mtu wa mapokezi kwenye ofisi yoyote utakayoingia.
Ukienda kwa mama ntilie akakuwekea chakula kingi, jifunze kwake pia huku ukijua kwamba kwenye hoteli kwa hela hiyohiyo usingeweza kupata chakula kingi kama hicho.
Ukienda sehemu ukapata huduma nzuri, jifunze na wewe unaweza kuitumia kwenye biashara yako pia.
Ukienda sehemu ukapata huduma mpya mpaka ukachoka, jifunze hapo pia na lifanyie kazi hilo ili lisije kujitokeza tena kwenye biasahara yako.
Na kwa hapa kwetu Tanzania biashara zenye huduma mbaya ni nyingi, hivyo ukijifunza kutokana na mabaya ambayo biashara nyingine zinafanya na kuyafanya kuwa mazuri kwenye biasahra yako, utaweza kufika mbali sana.
IWEKE BIASHARA YAKO MTANDAONI
Tunaishi kwenye ulimwengu ambapo karibia kila biashara inapaswa kuhamia mtandaoni. Hii ni kutokana na ukweli kwamba watu sasa hivi wakitaka kitu, sehemu ya kwanza kabisa ambapo wao wanakimbilia ili kupata taarifa ni mtandaoni
Wewe kwa sasa unaweza kuona kwamba biashara yako haistahili kuingia mtandaoni, ila siyo kweli. Ndio maana kitu cha kwaza kabisa unapaswa kuanza na maono, hivyo kitu kikubwa tunachokiangalia, siyo biashara yako ya sasa hivi, ila biashara ya miaka kumi ijayo. Ndio maana tumesema uwe na maono makubwa.
SOMA ZAIDI:
KUZA BIASHARA YAKO KWA ASILIMIA MOJA KILA SIKU
Ukifuatilia kampuni kubwa, utagundua kwamba huwa zinatoa ripoti ya mwenendo wake kila baada ya miezi mitatu. Wewe pia unapaswa kufanya hivi.
Ndio maana nimekwambia kwamba unapaswa kutunza hesabu za biashara yako. Huo utakuwa ni mwanzo wa wewe kuona hatua unazopiga.
Lakini pia jenga utaratibu wa kujiwekea malengo ya utakayofanyia kazi ndani ya miezi mitatu ijayo.
Weka malengo ya kufanyia kazi ndani ya mwezi ujao na wiki moja ijayo.
Usisahau kuweka malengo ya kila siku.
Ukiwa na malengo, lazima tu utafika mbali, ila usipokuwa na malengo, jua kwamba kila kitu unaenda kukifanya kwa namna ya ukawaida, na hapo utakwama kwenya safari yako na hutafika mbali.
KUWA MTU WA KUJIFUNZA NA KUTUMIA MAARIFA UNAYOPATA
Biashara yako itaweza kukua kulingana na kiwango cha maarifa uliyonayo. Hivyo penda sana kujifunza mara kwa mara. Soma vitabu, vitakuwezesha wewe kupata maarifa utakayoweza kutumia kwenye biashara yako.
Mkurugezi wa kawaida anakadiriwa kusoma vitabu 52 kwa mwaka. Sasa jiulize wewe unasoma vitabu vingapi kwa mwaka?
Anza na kusoma kitabu hiki cha BURE HAPA
Rafiki yangu, hivi ni baadhi ya vitu kidogo vinavyoweza kukusaidia wewe kukuza biashara yako na kuifanya kuwa kubwa. unaweza kuviona vya kipuuzi hivi, ila ni hivi hivi vinavyotofautisha kati ya wafanyabiashara wanaokuza biashara zao na wale ambao wanazidi kubaki pale pale mwaka hadi mwaka.
Ebu nenda uvijaribu kwenye biashara walau kwa mwezi mmoja tu, halafu uje hapa kutupa mrejesho.
Bila kuongeza la ziada, napenda kukushukuru sana kwa wakati wako. Nakushauri sana usome kitabu cha MAMBO 55 YA KUZINGATIA KABLA YA KUANZISHA BIASHARA, KUTOKA SIFURI MPAKA KILELENI pamoja na kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO.
Mimi ni Godius Rweyongeza
0755848391
Morogoro-Tz
-
Uchambuzi wa Kitabu: The Psychology of Money: Mambo 94 niliyojifunza katika kitabu hiki.
Mwandishi : Morgan Housel

Karibu katika uchambuzi wa kitabu hiki muhimu sana kuhusu masuala ya fedha, tamaa, na tabia za watu wanazozionyesha wanapokuwa na fedha, kwenye uchambuzi huu utaelewa kwa kina kwanini tabia zina mchango mkubwa kukufanya kuwa tajiri au kuwa masikini. Yote haya tutajifunza katika uchambuzi wa kitabu hiki. Karibu!
- Linapokuja suala la fedha hapo ndipo tunapoanza kutofautiana, maana fedha inahusisha sana tabia na tabia ndio huleta utofauti na utofauti huo ndio hufanya wengine kuwa matajiri na wengine kuwa masikini.
- Kufanya vizuri kifedha hakuhusiani na kuwa na uwezo mkubwa kiakili bali kunahusisha zaidi tabia za mtu na hulka.
- Tabia ndio huamua matumizi mazuri na mabaya ya kifedha na sio uwezo wake wa kiakili, ndio maana tabia ni ngumu kuifundisha hata kwa watu wenye uwezo mkubwa kiakili.
- Matumizi mabaya ya fedha huchangiwa sana na mtu kushindwa kuzuia hisia zake ambazo huathiriwa na tabia alizonazo.
- Mtu wa kawaida mwenye elimu ya kifedha anaweza kuwa tajiri endapo atakuwa na udhibiti mzuri wa tabia zake linapokuja suala la fedha.
- Kufanikiwa kifedha sio kujua mahesabu mengi ya kifedha, uhasibu na uchumi, inahusisha zaidi tabia za kila siku za mtu.
- Jinsi ninavyoamua kifedha inaweza isiwe na maana kwa upande wako, lakini ikawa na maana upande wangu.
- Ukitaka kujifunza na kuelewa kwanini watu wanaingia kwenye madeni, huitaji kujufunza kuhusu riba, unahitaji kujifunza kuhusu historia ya binadamu.
- Mara zote historia huwa haijirudii, watu ndio hurudia historia, na hii inaenda hadi katika masuala ya kifedha tunaona yanavyojirudia mara kwa mara.
- Kinachoonekana cha ajabu kwako kwangu kinaleta maana. Hii ni kutokana na kuwa tuna maisha yaliyopitia vitu tofauti ambayo vinatufanya tuamue tofauti kwenye masuala ya fedha.
- Uzoefu unaonyesha hatuwezi kuwa sawa katika masuala ya kifedha, utofauti wa malezi, makuzi na maamuzi ya watu kuhusu fedha yanatofautiana sana.
- Mfano, mtu aliyekulia na kuishi kwenye umasikini atafikiri zaidi kuhusu hatari na zawadi tofauti na mtoto aliyekulia katika utajiri.
- Utofauti tulionao ndio hutufanya tuione dunia katika mtazamo tofauti, na lipapokuja suala la fedha hutazamwa hivyo pia.
- Wakati mwingine tunaposoma historia tunadhani tumeelewa kila kitu, ukweli ni kwamba hatujaelewa kila kitu kwa sababu hatukuwepo na hatukuhusika katika matukio hayo tunayoyasoma, kwa sababu hiyo hatuwezi kupata maelezo mazuri ya kutufanya tubadili baadhi ya tabia zetu kuhusu fedha.
- Kwenye maisha kuna baadhi ya vitu inabidi tukutane navyo na tuviishi ili tuvielewe zaidi, sio kila kitu tutakielewa kwa kusoma historia yake.
- Uzoefu unaonyesha uwezo wa mtu kustahimili hatari unatokana na aliyoyapitia katika maisha yake binafsi.
- Wakati mwingine mafainikio hayahusishi uwezo mkubwa wa kiakili, wala elimu, wala ujuzi na teknolojia, bali inaweza kuwa ni bahati na mahali mtu alipozaliwa.Maamuzi yote wanayayafanya watu kuhusu fedha yanatokana na taarifa walizonazo na wanazozipokea kila siku kuhusu fedha, taarafa hizo ndio hujenga mitazamo tofauti kwa kila mtu.
- Hakuna kitu kizuri sana kama unavyodhani wala hakuna kitu kibaya kama unavyofikiri na kutazama, ni kwa vile umeona sehemu moja tu ya shilingi.
- Tuwe makini na watu ambao tunawasifia na kutamani kuwa kama wao, lakini pia tuwe makini na watu ambao tunawachukulia poa na hatutamani kabisa kuwa kama wao, kasababu hujaona kila kitu.
- Punguza kuangalia mtu mmoja kama ndio aliyekamilika, jifunze kwa mapana na jipe nafasi ya kuelewa mambo kwa upeo mkubwa, watu wanapitia mengi sana ambayo hayaonyeshwi.
- Tuelewe kabisa kwenye fahamu zetu, kuwa sio mafanikio yote yanatokana na kufanya kazi kwa bidi, na pia sio kila umasikini unatokana na uvivu. Tuepuke kutoa hukumu haraka.
- Tunapokubali kuwa bahati hutokea kwenye mafanikio, pia tukubali nafasi ya hatari kama kitu kinachoweza kutokea kwenye safari ya mafanikio, hii itatupa mtazamo tofauti tunaposhindwa kufikia malengo tuliyojiwekea.
- Tunapotoa nafasi kwa bahati na hatari kama vitu vinavyoweza kumtokea mtu yeyote katika safari yake ya mafanikio, itatupa nafasi ya kujisamehe pale tunaposhindwa kufikia mafanikio, na kutufanya tuhukumu bila lawama.
- Kamwe epuka maisha ya kujilinganisha, hutaweza kuridhisha kila mtu kweye jamii yako, na gharama ya kuingia kwenye kujilinganisha na wengine ni kubwa, na sio rahisi kufikiwa.
- Kuridhika ni kutambua kuwa kuendekeza tamaa zisizo na kiasi zinaweza kukupelekea kwenye majuto.
- Kuna watu walikuwa ni matajiri na waliweza kumudu mambo mengi sana kwenye maisha yao kutokana na fedha nyingi walizokuwa nazo, lakini tamaa ya kupata fedha zaidi iliwafanya waingie kwenye biashara haramu, kamari, utapeli ambao ulipotezea fedha zao na kuingia katika mikono ya sharia na kufilisiwa kila kitu.
- Usiingize fedha safi kwenye biashara zinazozalisha fedha chafu kwa kigezo cha kupata fedha zaidi, uzoefu na historia inaonyesha waliofanya mambo ya aina hii waliishia jela na majuto makubwa.
- Tabia walizonazo watu wanapokuwa na fedha ndio hupelekea kupoteza fedha na kutoridhika hata kama wanapata fedha nyingi kwa njia nzuri.
- Kupata fedha na kuzitunza fedha ni vitu viwili tofauti vinavyohitaji ujuzi tofauti, ndio maana ubepari ni mgumu sana.
- Uwezo wa kuwa king’ang’anizi kwa muda mrefu, kutokatishwa tamaa, ndio huleta utafauti, uwezo wa kuvumilia hayo yote ndio unatakiwa kuwa ndio nguzo kuu kwenye mikakati yako yote ya uwekezaji, biashara, na kwenye kazi zako.
- Kwenye biashara, uchumi, uwekezaji na kazi, wanaofanikiwa na kupata faida ni wale wanaovumilia na kustahimili mikiki mikiki wanayokutana nayo kwenye safari ya mafanikio.
- Kuwa na mpago wa mafanikio ni muhimu sana, lakini sehemu moja muhimu katika mpango wowote ni kupanga pale ambapo mpango ulioupanga hautaenda sawa na mpango wako wa mafanikio.
- Mwandishi anasema moja wapo ya aina ya juu ya utajiri ni kuamka kila siku asubuhi na kufanya chochote unachokitaka.
- Uwezo wa kufanya kile unachokipenda, kwa wakati unaoutaka, na mtu unayemtaka, na kwa jinsi unavyotaka, ni zaidi ya fedha na dhahabu.
- Binadamu yoyote hakuna kitu kitamfanya ajisikie vizuri na mwenye nguvu zaidi kama anapokuwa na hisia za umiliki na kudhibiti mambo kwenye maisha yake. Hakuna hisia nzuri kama hizi kwenye maisha na ndio huleta furaha ya kudumu.
- Kwa asili binadamu wote tunapenda kuendesha maisha yetu wenyewe, tunataka tuwe waamuzi kwenye maisha yetu, tunataka tuamue vitu kwenye maisha yetu. Hakuna binadamu anayetaka kuendeshwa na kupelekeshwa kwenye maisha yake.
- Kutawala na kuutumia muda wako vizuri ni zaidi ya jinsi fedha inaweza kukulipa, ni uhuru mkubwa sana.
- Wahenga wanasema, sikiliza zaidi, kuwa na muda mwingi wa kuchakata mambo katika ubongo wako, kwa kufanya hivyo utapata nafasi ya kuanzisha jambo lako kwa mafanikio.
- Watu wanadhani wanahitaji magari ya gharama, kuvaa saa za gharama, mavazi ya gharama au kuwa na nyumba kubwa ya gharama, ukweli ni kwamba hawahitaji vitu hivyo, watu wanahitaji heshima na kupendwa na watu wengine.
- Wengi hudhani kuwa na vitu vya gharama wataheshimika na kupendwa na watu wengine. Pia watu wengi hudhani watu wenye mali na wenye vitu vya gharama wanaheshimika na kufurahiwa zaidi yao.
- Watu wanatafuta utajiri na kumiliki vitu vya gharama ili wapendwe, haitakuwa hivyo mara zote, badilisha mtazamo wako.
- Kama unatafuta kuheshimika na kupendwa kwa kuwa una vaa au unamiliki vitu vya gharama fikiri tena, heshima haitafutwi hivyo njia hii, itakugharimu sana. Heshima, ubinadamu, na kusaidia wengine ndio vinaleta heshima kwako kuliko nguvu nyingi unazotumia kununua na kumiliki vitu vya gharama kubwa ili uheshimike na kupendwa.
- Kumbuka siku zote, utajiri wa mtu sio vile unavyomuona navyo, utajiri halisi wa mtu hauwezi kuuona kirahisi.
- Mara nyingi tumekuwa tunatumia taarifa tunazoziona kwa nje na kufikiri mtu huyu ni matajiri au masikini. mfano, magari, picha za mitandaoni, mwonekano, mavazi anayovaa nk.
- Vitu ambavyo hatuvijui au kuviona kwa mtu ndio utajiri wenyewe, kama vile kiasi cha fedha katika akaunti yake ya benki, uwekezaji wake, nk.
- Dunia ya sasa ina waigizaji wengi sana wanaoonekana ni matajiri kumbe hawana kitu, ni rahisi kuigiza na kunekana mtu tajiri hata mitandao ya kijamii inaweza kukusaidia kufanya hivyo, hivyo basi punguza kuhukumu na kufikiri taarifa za nje pekee zinaweza kukuamulia kuwa mtu fulani ni tajiri au masikini.
- Utajiri ni gari zuri ambalo halijanunuliwa, almasi ambayo haijanunuliwa, saa ya gharama ambayo haijanunuliwa, nguo za gharama ambazo hazinanunuliwa, na vitu vingine vya gharama kubwa ambavyo havijanunuliwa.
- Hivyo utajiri ni asseti za kifedha ambazo hazijabadilishwa kuwa vitu vinavyoonekana.
- Siku zote tukumbuke, endapo tutamia hela kununua vitu, tutaishia kuwa na vitu hivyo bila kuwa na fedha.
- Wengi wanadhani kuwa milionea ni kutumia mamilioni, kitu ambacho ni tofauti kabisa na kuwa milionea. Unaweza kutumia mamilioni ya fedha kununua vitu lakini haimaanishi wewe ni milionea, umilionea haupo kwenye matumizi.
- Shida kubwa ipo watu wanataka kuonekana matajiri kwa kutumia pesa, utajiri wa kweli haupo kwenye muonekano wa nje, utajiri wa kweli upo kwenye vitu usivyoviona.
- Watu wengi hujiona na kujisikia ni matajiri kwa kutumia fedha nyingi kununua vitu vizuri.
- Sio kazi kuwaona watu waliojifanya matajiri, kwasababu kuna wengi wanafanya hivyo ili waonekane na watu.
- Tunashindwa kuwaona matajiri wa kweli kwasababu wengi wanajifanyisha matajiri kwa nje hivyo inatuwia vigumu kutambua haraka na kupata watu sahihi wa kutuongoza.
- Ni ngumu kujifunza kwa vitu usivyoviona, na utajiri wa kweli hauonekani, maana vinavyoonekana sio halisi.
- Mwandishi wa kitabu hiki anasema utajiri unatengenezwa kwa kuweka akiba na sio kwenye matumizi.
- Utajiri ni malimbikizo ya muda mrefu ya mali na fedha ulizobakiza baada ya matumizi yako, na kama ilivyo huwezi kujenga utajiri bila kuwa na mapato mengi basi hutaweza kuwa tajiri bila kuwa na uwekezaji mkubwa.
- Kama unataka kukuza uwekezaji wako, unatakiwa pia kukuza na kuongeza uvumilivu wako, maana utajiri na mafanikio yanahitaji muda.
- Kuweka akiba ni jambo lililopo ndani ya uwezo wa kila mtu, na huhitaji sababu nzuri kwanini usiweke akiba, huhitaji kuwa hata na sababu kwanini unahitaji kuweka akiba, wewe weka akiba.
- Akiba inaweza kutengenezwa kwa kuwa na matumizi kidogo, au kudhibiti matumizi yako ya fedha, na unaweza kudhibiti matumizi endapo tutapunguza tamaa, na tamaa itapungua endapo hatutajali sana wanachofikiri watu wengine kuhusu sisi.
SOMA ZAIDI: Fursa Tano Ambazo Vijana Wa Siku Hizi Wanachezea (SEHEMU YA TATU)
- Dunia inabadilika kwa kasi sana, baadhi ya mambo yanatuacha na mshangao, kwasababu hiyo tunasafari ndefu hapa duniai ya kuona mambo mengi ambayo hatujayatarajia.
- Mambo mengi yanatokea hapa duniani bila hata sisi kujiandaa, dunia haitabiriki nini kinaweza kutokea kesho, hivyo basi tunatakiwa kuwa na fedha nyingi za kuweza kuhimili hali zozote mbaya zinazoweza kutokea baadaye.
- Kama kuna jambo tunatakiwa kulielewa katika maisha yetu ni kwamba makossa hutokea na tunatakiwa kutoa nafasi ya kukosea kama sehemu ya maisha.
- Sio kila kitu tutapanga kitaenda kama kilivyopangwa kwa asilimia 100, kuna mengi yasiyotarajiwa huweza kutokea katika mipango yetu, kwa kutambua hilo tunatakiwa kutoa nafasi hiyo ya makosa kutokea.
- Tukitambua kuwa makossa huweza kutokea licha ya kuwa na mipango mizuri itatusaidia kustahimili misuko suko mingi ya maisha na kutupunguzia majuto.
- Mambo yasiyotarajiwa yanaweza kutokea wakati wowote katika safari ya mafanikio, hivyo tunaposimama na kuiangalia dunia hatutakiwi kuiangalia kwa mstari mnyoofu wa nyusi na nyeupe.
- Matarajio yako yasiwe makubwa sana kwasababu ya mipango yako, kuna mengi huyajui yanaweza kutokea kwenye safari yako na kuharibu kabisa au kubali kabisa mipango yako, kuwa tayari kwa hilo.
- Kila kitu kina gharama yake, hivyo hata kwenye masula ya kifedha, tambua gharama unayotakiwa kuilipa na ulipe ili kufikia ndoto zako.
- Gharama ya kitu au kufikia ndoto zako inaweza isiwe sawa na ulivyohadithiwa, ukiingia na kuanza utekelezaji wa malengo yako ndio utaona gharama halisi uliyotakiwa kulipa au ya kitu hicho.
- Kila kazi inaonekana ni rahisi kwasababu hujaingia kuifanya, ukiifanya ndio utajua gharama yake ambayo wengi hatuioni.
- Ugumu wa kitu upo kwenye kukifanyia kazi, na sio kwenye maneno tu ya mdomoni. Ndivyo ilivyo hata kwenye uwekezaji, ni rahisi sana kuzungumza uwekezaji na faida zake na hasara zake, lakini gharama na ugumu wake upo katika utekelezaji.
- Usidhani dunia ni nzuri kama unavyofikiria, hakuna kitu cha bure, kila kitu kizuri utakilipia, hakuna cha bure dunia hii ndugu yangu.
- Hakuna atakaye kupa zawadi ya bure, hakuna hata miungu itayokuja kukupa kitu cha bure hapa duniani, Mungu na malaika, na asili yote inaangalia wanaojitoa na wanaofanya kazi ili wawabariki. Kuna gharama za kulipa ili upate baraka…hakuna baraka za bure.
- Namna nyingine nzuri ya kutusaidia katika kuweka akiba ni kufikiria akiba kama ada unayotakiwa kuilipa ili upate kitu fulani cha thamani, na sio kama faini ambayo unatakiwa kuikwepa.
- Suala la kuweka akiba ni juu yako kujishawishi vya kutosha kuwa, kuweka akiba itakusaidia na ni muhimu kama sehemu yoyote ya mwili wako.
- Dhibiti kabisa matumizi yako ya fedha, matumizi yako ya fedha yasiingiliwe na ushawishi wa watu wanaokuzunguka, amua kutumia pesa zako kwa matumizi muhimu tu.
- Jamii ina watu wanacheza michezo ambayo huijui na fedha zao, kamwe usishawishike ukaamua kuwa mjinga kutumia fedha zako kawaababu ya ushawishi wao.
- Cheza mchezo wako mwenyewe na fedha zako kwa faida yako, usiingiliwe na kushawishika kufanya mambo mabaya na fedha zako ikaja kukugharimu.
- Dunia ina kamchezo cha kuamini na kuzipa umakini mkubwa habari mbaya au hasi kuliko habari nzuri.
- Habari za kuogofya, habari za vita, mauaji na majanga ndio huteka umakini wa watu zaidi kuliko habari njema za matumaini.
- Mfano mzuri mwambie mtu mambo yatakuwa mazuri na hali itakuwa shwari hatakusikiliza kiviile, ila mwambie kuhusu hatari, vifo, mambo ya kutisha yatakayokuja, nakwambia atakusikiliza kwa makini sana, na hivyo ndivyo ilivyo duniani kote, habari mbaya huenezwa na hununuliwa na watu hulipwa kuja kuelezea vizuri kuhusu habari mbaya.
- Watu wenye habari mbaya ndio hutafutwa, hupewa nafasi kwenye radio, TV magazeti na ndio wanaosikilizwa zaidi. Ukiwa na habari nzuri hakuna atakayekutafuta wala kukusikiliza, watu wanapenda kusikia habari hasi zaidi kukiko habari chanya.
- Angali mafanikio yaliyofikiwa kwenye sekta za uchumi, afya, miundombinu, biashara, masoko na uwekezaji lakini hizi sio habari za kugonga vichwa vya habari, watu wanataka kusikia milipuko ya moto, vita, mabomu, tetemeko la ardhi, vifo, ajali, magonjwa kama corona, na majanga mengine ya kutisha.
- Habari mbaya na hasi ndio huuza zaidi, habari njema na chanya hazina soko. Kuwa makini na taarifa zinazovuma sana, maana zinaweza siziwe na uhalisia wote.
- Ndio maana mara nyingi habari za moto moto ni zile zinazoelezea kuyumba kwa uchumi, kushuka kwa uchumi, na sio kupanda kwa uchumi, wataalamu wengi wanapenda kueleza kushuka kwa uchumi kuliko kupanda kwa uchumi.
- Ni rahisi kuelezea kushuka kwa uchumi, kutengeneza hofu, na kutenegeneza stori nyingi kuhusu kushuka kwa kuchumi kuliko kupanda kwa uchumi.
- Wengi hupenda kutabiri anguko la uchumi, na majanga mengine yanayoweza kutokea baadaye, lakini imekuwa ngumu sana kutabiri mafanikio na kukua kwa uchumi. Hii ni kwabababu ukuaji wa uchumi hufanyika taratibu na hauonekani kirahisi, ila anguko ni rahisi kuonekana na wengi hupenda kutolea maelezo.
- Ukweli ni kwamba kuna majanga mengi yanaweza kutokea kwa muda mfupi na kwa haraka, lakini sio hivyo kwa miujiza na mafanikio yanachelewa na kukawia.
- Lazima tuufikie ukweli kwamba vinatokea vitu vingi hapa duniai ambavyo hatutakuwa na uwezo navyo wa kuvidhibiti, kuna vitu tutaacha tu vitokee maana hatuwezi kuviathiri kwa vyoyote.
- Hatari ndio kitu pekee hubakia baada ya kufikiria umepanga kila kitu na kila kitu kipo kwenye mstari sahihi. Hii inamaana hata kama una mipango mizuri kiasi gani, bado inaweza kuathiriwa na hatari usizoziona wala kuzijua.
- Sayansi ya kurusha ndege na roketi ni tofauti sana na sayansi ya uchumi, uwekezaji na biashara. Kwenye sayansi ya kurusha roketi kuna fomula ambazo zimetenezwa, na wanatumia mahesabu na kanuni kufanikisha mambo yao, ni eneo ambalo hisia hukaa pembeni kabisa tofauti na maswala ya fedha, uchumi, biashara na uwekezaji, ambayo huingiliwa na hisia na mitazamo ya watu wenye tabia zinazotofautiana.
- Kuwa msimamizi mzuri wa fedha zako kwa namna ambayo itakufanya utalala usingizi mzuri usiku. Weka akiba ya kutosha.
- Sio kila kinachoshuriwa kufanyika kinafanyika kama kilivyoshauriwa, sio kila kilichoandikwa kinafanyika kama kilivyoandikwa. Mambo ni mengi sana hii dunia, tafuta pa kushika na usiache kujifunza kila siku.
- SOMA ZAIDI: Kwa Nini Wanafunzi Wanaopata “A” Wanawafanyia Kazi Wanafunzi Wanaopata ‘C’, Na kwa Nini Wanafunzi Wanaopata “B” Wanaifanyia Kazi Serikali
Ahsante kwa kusoma uchambuzi wa kitabu hiki, karibu na endelea kufuatilia chambuzi nyingine za vitabu hapa hapa.
Mchambuzi: Hillary Mrosso
Mawasiliano: +255 683 862 481
Tarehe: 01.03.2022
-
Jinsi Ya Kupata Mtaji Wa Biashara

Tree growing on money coins arranged as a graph on wooden table with natural bokeh background, concept of business growth and saving money Siku ya leo tunaenda kuona ni kwa namna gani unaweza kupata mtaji wa biashara. Mtaji wa biashara kimekuwa ni kitu ambacho vijana wengi wanahangaika nacho. Wengi sana wamekuwawanauliza ni kwa jinsi gani naweza kupata mtaji wa kuanzia biashara.
Tayari nimeshaandika ebook inayoeleza mitaji 8 iliyokuzunguka na jinsi ambavyo unaweza kuitumia hiyo mitaji.
Lakini siku ya leo nataka tujikite hasa kwenye mtaji fedha. Mtaji fedha unaipataje? Unapataje fedha za kuanzisha biashara? Kujibu hilo swali, acha tufuatilie haya mafunzo ya youtube maana yana kila kitu unachohitaji kujua kuhusu MTAJI FEDHA.
- SOMA ZAIDI: Kwa Nini Mpaka Sasa hivi huanzishi biashara yako?
- Hivi Ndivyo Unaweza Kupata Mtaji Wa Biashara Ukiwa Bado chuo
- Maeneo Matatu Unayoweza Kuwekeza Kama Hauna Pesa/Mtaji
Umekuwa nami
Godius Rweyongeza
0755848391
Morogoro-Tz -
Inawezekana
Ndio, inawezekana kwako wewe kufanya na kufanikisha kitu chochote kile utakachotaka kwenye maisha.
inawezekana wewe kufikia ndoto zako.
inawezekana wewe kuwa utajiri na kuagana na umasikini
kiufupi inawezekana wewe kufanya kitu chochote na kukifanikisha.
-
Umeshapata ebook ya kipaji ni dhahabu? hivi ndivyo unaweza kuipata
Juzi nilizindua ebook ya KIPAJI NI DHAHABU.
Ebook hii imeeleza kwa kina mambo yote unayohitaji kujua kuhusu kipaji.
Ndani yake Utajifunza kipaji ni Nini?
Namna ya kugundua kipaji chako
Namna ya kukiendeleza.
Jinsi ya kutengeneza fedha kwa kutumia kipaji chako.
Kipaji katika karne ya 21. Jinsi ya kutumia mtandao wa intaneti kwa manufaa na namna ya kuweka kipaji chako mtandaoni.
Mwisho kabisa nimeeleza kipaji na elimu.
Rafiki yangu, ebook hii imesheheni madini.
Halafu nilitaka kusahau kitu kimoja cha muhimu sana kwenye ebook hii. Kitu hiki ni kwamba nimeeleza namna ya kugundua kipaji cha mwanao.
Ewaaa! Yote haya na zaidi yapo kwenye e-book ya KIPAJI NI DHAHABU.
E-book hii inapatikana kwa elfu 5 tu. Tuma fedha kwenda 0684 408 755. Jina litatokea GODIUS RWEYONGEZA.
Ukishatuma, utanitaarifu kwa ujumbe mfupi ilu nikutumie e-book hii ya kipekee.
Karibu.
Umekuwa nami
Godius Rweyongeza
0755848391
Morogoro-Tz -
Kitu hiki tu kinakwamisha watu wengi Sana
Moja ya kitu ambacho kinakwamisha watu wengi kwenye kufanyia kazi malengo ni kutojiwekea viwango.
Unapaswa kuishi kwa viwango.
Kampuni huwa zinajiwekea viwango vya uzalishaji wa bidhaa zake. Na muda mwingine viwango hivi huwa vinaangaliwa na watu wa ndani ya kampuni na nje ya kampuni.
Kwenye kampuni unakuta kuna mkurugenzi anayehakikisha bidhaa zinazozalishwa ni bora. Wengine watamwita quality manager au majina mengine ila kazi ni yake ni kuhakikisha kazi ya mwisho inayozalishwa ni kazi ya viwango.
Huyu ni lazima tu atahakikisha kweli kila kitu kinazalishwa kwa ubora kwa sababu kuu zifuatazo.
Moja, bidhaa ikizalishwa kawaida, bosi wake akaigundua anaweza kumwachisha kazi.
Au la bidhaa imezalishwa kwa viwango vya kawaida imeenda kwa walaji wakalalamika, bosi atafuatilia na akagundua kuna uzembe ulifanyika, atamwachisha kazi.
Kwa hiyo huyu mkurugenzi lazima awe makini mara zote kuhakikisha bidhaa zinazozalishwa ni za viwango Kama inavyotakiwa.
Na kitu kingine kinachoongeza umakini kwenye kazi hasa ni pale ambapo kunakuwa na wakaguzi kutoka nje.
Hiki Kitu kinamsukuma zaidi mkurugenzi husika na kampuni nzima kiujumla kuhakikisha kwamba wanazalisha bidhaa za viwango.
Wewe pia unapaswa kujiwekea viwango.
Unaweza usiwe na mkurugenzi wa kukufuatilia kuona kama viwango vimefikiwa au la! Ila sasa hiyo kazi unapaswa kujipa mwenyewe. Wewe mwenyewe unapaswa kuwa mkurugenzi wa ubora (quality manager) wa maisha yako.
Jiwekee viwango, kisha vifuate. Kama huwezi, tafufa mtu wa kukushikiria. Ambaye utaripoti kwake mara kwa mara, na yeye atakusaidia kuona Kama kweli umeweza kukidhi viwango au la!
Mimi naweza kukusaidia kwenye hilo.
Siku siyo nyingi nilijiwekea viwango vya kuandika makala mbili kila siku. Na viwango hivi nimeshaanza kuvifanyia kazi kwa zaidi ya wiki na nusu na nitaendelea kuvifanyia kazi kila iitwayo leo bila kuchoka.
Ila sasa nimekaa chini na kugundua kuwa napaswa kujiwekea viwango vipya na vya juu kuliko nilivyozoea kwenye kila eneo la maisha. Hivyo, leo nimejiwekwa viwango vingine kwenye maeneo mengine.
Nakusihi na wewe ujifanyie tathimini na kujiwekea viwango utakavyokuwa unafuata.
Unaenda kujiwekea viwango kwenye eneo gani la maisha?
Tutawasiliana
Godius Rweyongeza
0755848391
Morogoro-Tz -
Watu ambao wanapata wazo bora la biashara huwa wafanya hivi
Usije ukafanya kosa la kukaa chini, na kuanza kusubiri upate wazo bora. Wazo bora halipatikani kwa kukaa chini n akuumiza kichwa.
Muda mwingine wazo bora linapatikana kwa kufanya kazi.
Ebu kwa mfano, hakuna mtu ambaye alikaa na kuumiza kichwa ili aje na wazo la tairi. Ugunduzi wa taili ulikuwa ni miongoni mwa mapinduzi makubwa, ambayo yalifanyika kwa wakati huo,mpaka sasa hivi. ila hakuna mtu alikaa chini na kuumiza kichwa, kisha akatengeneza taili.
Watu walipata wazo la taili katika kufanya kazi. kadiri walivyokuwa wanafanya kazi na kufeli na kuinuka ndivyo walikuwa wanakuja na wazo bora zaidi. inawezekana labda taili la kwanza lilikuwa ni la pembe nne.
Au fikiri kuhusu wazo la uchapaji wa vitabu. Hakuna ambaye alikuja na wazo bora lililokamilika la kuchapa vitabu. sote tunajua kwamba uchapaji wa vitabu wa zamani na wa sasa hivi ni tofauti. Ila haya maboresho tunayoyaona sasa hivi ni kutokana na watu waliokuwa tayari kufanyia kazi kile walichokuwa wanafikiri mwanzoni, wakakiboresha kadiri walivyokuwa wanaendelea mpaka wwe unalifahamu kama lilivyo. Hivyo, basi, usije ukakaa na kusubiri upate wazo bora na la kipekee ambalo halijawahi kutokea hapa duniani.
Leo hii Thomas Edison anapewa sifa nyingi sana kwenye ulimwengu wa uzinduzi wake wa taa. Ukisoma wasifu wake utagundua kwamba Thomas Edison hakuwa na wazo lililokamilika tangu mwanzo. Ila kadiri alivyokuwa analifanyia kazi ndivyo ambavyo wazo lake lilikuwa linazidi kuwa bora na kuimarika. Alijaribu mara elfu moja kabla hajapata kitu ambacho kilikuwa kinafanya kazi kwa asilimia 100.
Na wewe usije ukakaa na kuanza kusubiri wazo lako liwe bora. Anza kulifanyia kazi. utariboresha kadiri utakavyokuwa unaendelea
Ndio maana hata ukiangalia watengezaji wa simu hawatengezi simu moja na kutulia. Wanaziboresha simu kila siku, hii ndio kusema wazo la awali linaboreshwa na kufanywa kuwa imara zaidi.s
-
Kwa Nini Watu Wengi Na Hasa Vijana Wanashindwa Kuzifikia Ndoto Zao
Juzi niliomba watu wapendekeze mada ambazo nitaandikia kwenye blogu yangu kupitia status yangu ya whatsap. Nilipokea maombi kadha wa kadha ambayo nitakuwa nayafanyia kazi moja baada ya jingine. Ombi mojawapo lilikuwa ni kuandika makala maalumu kueleza kwa nini watu wanashindwa kufikia NDOTO zao.
Kabla sijaenda mbali nataka ufahamu kuwa tayari nimeandaa makala nyingi kuhusu ndoto na jinsi unavyoweza kufikia NDOTO zako. Makala zote hizo nitajidi kuzihusisha kwenye makala ya leo ili uweze kurejea na kuzisoma.
Lakini pia nimeandika kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO. Unaweza kupata kitabu hiki kwa kuwasiliana na 0755848391 utatumiwa popote ulipo duniani.
Natamani sana siku moja nikuone ukiwa umeweza KUFIKIA NDOTO ZAKO KUBWA- SOMA ZAIDI: Vikwazo vitano vitakavyokuzuia KUFIKIA NDOTO ZAKO ndani ya 2021
- Vitu vitano vinavyofanya watu waue ndoto zao na hivyo kushindwa kuzifikia

kupata kitabu hiki wasiliana na 0755848391. Utatumiwa popote ulipo duniani 1. KINACHOKUKWAMISHA kufikia ndoto zako ni kuchelewa kuchukua baadhi ya hatua.
Ulipaswa kuwa umechukua hatua fulani ila sasa unachelewa aidha kwa kutoelewa au kwa kuelewa na kupuuza, au kwa uoga.
Mfano, kwenye ulimwengu wa sasa ulipaswa kuwa umeweka biashara yako au kipaji chako mtandaoni, ila hujafanya hivyo.
Na haikugharimu chochote. Kwa bando lako tu unafungua na kuendesha blogu yako, unatengeneza akaunti za biashara kwenye mitandao ya kijamii na mengine mengi.
Ulipaswa kuwa unatunza kumbukumbu za hesabu za mapato na matumizi ya biashara yako, ila hufanyi hivyo, halafu ukija unasema kwamba biashara ni mbaya.
Kwani inakugharimu wewe shilingi ngapi kufanya kitu kama hiki.Kuna baadhi ya hatua unachelewa kuzichukua, na hapo unakuwa unakwama kufikia ndoto zako.
- SOMA ZAIDI: Kinachotokea Unapokuwa Na Ndoto Kubwa
- Kitu cha kufanya pale unapokuwa na ndoto kubwa inayohitaji pesa na wewe hauna pesa.
2. Kutaka kuishi maisha kama ya wengine wakati una ndoto kubwa
Unapokuwa na ndoto kubwa matumizi yako, mwenendo wako, ulaji wako na mambo mengine yote yanabadilika.
Huwezi kuwa na ndoto ya kuwa mkimbiaji wa Marathon ukawa hufanyi mazoezi huku ukila chipsi kila siku. Vitendo vyako vinapaswa kuendana na ndoto yako.
Kuna vitu bila kulazimishwa wala kuambiwa na mtu yeyote utapaswa kuachana navyo, sio kwa sababu ni vibaya ila tu kwa sababu havieneani na ndoto zako kubwa.
Huwezi kuwa na ndoto za kuwa bilionea huku ukiwa unataka kumhonga kila binti anayepita mbele yako.
- SOMA ZAIDI: Nukuu Tano Zilizokonga Nyoyo Za Watu Kutoka Kwenye Kitabu Cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO
- Edius Katamugora Afunguka Mazito Kuhusu Kitabu Cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO
3. Hujafanya uamuzi wa dhati wa kuzifikia NDOTO ZAKO.Ngoja nikwambie kitu, kuna uamuzi unapaswa kuufanya kwenye maisha yako. Na uamuzi huu ni au utazifikia ndoto zako au utakufa ukiwa ukiwa unazipambania au hutazifanyia kazi kabisa ndoto zako.
Hapo unapaswa KUCHAGUA maana maisha ni kuchagua.
Ukichagua kuzifanyia kazi ndoto, fahamu kuwa umechagua kitu kigumu ila kinachowezekana.Kama ndoto ingekuwa ni barabara basi ni sawa na kuchagua barabara mbaya, yenye makorongo ila inayokufikisha ikulu.
Nadhani umewahi kusikia kuwa mlango wa kuingia mbinguni ni mwembamba, hivyohivyo mlango wa kufikia ndoto zako. Haupitiki mara kwa mara ndio maana watu wengi kwenye jamii yako wameamua kuishi maisha ya kawaida.Mwaka 1968 kwenye mbio za marathon; mshiriki mmojawapo alikuwa ni Mtanzania John Stephen Akhwari

Mtanzania John Stephen Akhwari kwenye mbio za marathon mwaka 1968. Mtanzania huyu naweza kusema siku hiyo alikuwa miongoni mwa watu waliotegemewa kushinda. Hii ni kutokana na rekodi yake ya mashindano ya nyuma likiwemo moja la olimpiki na jingine la jumuia ya madola ambayo alikuwa amefanya vizuri sana.
Sijui kama kubeti kulokuwepo miaka hiyo, ila kama vijana wa siku hizo wangekuwa wa kubeti, basi siku hiyo wangempa ushindi wote JOHN STEPHEN AKHWARI.
Alianza mbio kama ambavyo watu wengine walikuwa wameanza. Baada ya kufikia kilomita kama thelathini hivi, aliumia na kupata maumivu ambayo kwa mtu wa kawaida yalitosha tu kumfanya asiendelee na mbio. Ila hali haikuwa hivyo kwa Bwana John Stephen Akhwari.
Alitulia pembeni kwanza. Alipewa huduma ya kwanza, kisha baada ya hapo akaendelea kusonga mbele. Zamu hii akiwa anajikongoja. Gari la kumbeba lililetwa ila alikataa kulipanda.
Wale ambao hawakuumia walimaliza mbio mapema na Mwethiopia siku hiyo ndiye alishindwa
Saa moja baada ya mashindano kuwa yamekamilika na watu wameanza kuondoka uwanjani pale, ndipo vyombo vya habari vilipata taarifa kuwa kuna mtu bado anakimbia.
KUMBUKA hapa watazamaji wengine wameshaondoka uwanjani na tuzo zilishatolewa. John Stephen Akhwari ambaye aliumia ndipo alikuwa anaingia.
Vyombo vya habari vilituma watu wao ili warekodi kinachoendelea. Walimwona John Stephen Akhwari alivyokuwa anachechemea ila akipambama kumaliza mbio. Na mwisho alimaliza huku akipigiwa makofi ma watazamaji wachache waliokuwepo pale uwanjani.
Alipoulizwa kwa nini uliendelea kukimbia wakati ulikuwa umeumia, alisema. Nchi yangu haikunituma maili elfu tano ili nianze mbio bali nimalize mbio.
Tokea hapo kauli hiyo imekuwa kauli inayotumika sana kwenye ulimwengu wa michezo kuwahamasisha wachezaji.Ninachotaka utoke nacho hapa Ni kwamba, unapaswa kuamua kwa DHATI kuifanyia kazi ndoto yako au kutoifanyoa kazi kabisa. Ila hakuna kitu cha katikati
- SOMA ZAIDI: Mwalimu Mazumila Asema Kitabu Cha Jinsi Ya Kufikia Ndoto Zako Kimegeuka Kuwa Baraka Kwake
- Maswali Muhimu Unayopaswa Kujiuliza Kabla Ya Kuachana Na Ndoto Yako
Kwa Leo naishia hapo. Kuna makala nyingi za nyuma ambazo nimewahi kuandika kuhusu mada hii. Nimeziunganisha kwenye makala ya leo. Naomba UBONYEZE viunzi husika ili uweze kuzisoma.
Mimi naitwa
GODIUS RWEYONGEZA
0755848391
MOROGORO -
Chukua Mambo Haya 10 Kuhusu Namna Ya Kuanza Kidogo Na Kufikia Pakubwa

1. Mti wowote ule mkubwa haukuanza ukiwa hivyo, ulikua taratibu mpaka kufikia ulipofikia.
Wewe pia kuwa tayari kuanza kidogo na kuendelea mbele zaidi.
2. Ukitaka kupanda ghorofa kuna njia mbili. Unaweza kupanda ngazi moja baada ya nyingine au unaweza kupanda lift.
Ila fahamu kuwa njia ya kwanza itakuimarisha na kukufanya uwe bora zaidi.
3. Ukianza kupita eneo mara ya kwanza, nyayo zako hazitaonekana. Ila ukiendelea kupita mara kwa mara njia itatengenezeka.
4. Njiti ndogo tu ya kiberiti ina uwezo wa kuwasha moto wa kuunguza msitu mkubwa. Usidharau kitu kwa udogo wake.
5. Safari ndefu ya maili elfu moja, huanza na hatua moja.
6. Ukikata mti kwa shoka, haukatiki kwa shoka la kwanza bali kwa muunganiko wa mashoka mengi unayopiga.
7. Ukitaka kuhamisha mlima, Anza kwa kuondoa jiwe moja.
8. Ukitaka kujenga ghorofa, anza kuweka jiwe moja.
9. Kuna vitu katika maisha havihitaji haraka. Huwezi kupata mtoto ndani ya mwezi mmoja kwa kuwapa mimba wanawake tisa.
10. Katika maisha, hakikisha una ndoto kubwa. Zifanyie kazi kila siku.
-
KUWA MABADILIKO UNAYOTAKA KUYAONA

Kama kuna mabadiliko unataka kuyaona kwenye jamii yako wewe kuwa wa kwanza kuonesha njia.
Badala ya kukaa na kulalamika kwamba unataka ufanyiwe kitu fulani. Onyesha njia. Fanya unachotaka kuona.
Mabadiliko yanaanza na mimi na wewe.
Ni mabadiliko gani unayotaka kuona?
Picha hiyo hapo juu inaonesha kijana aliyetaka kufanya mabadiliko kwenye jamii yake kwa kuwasaidia kusoma vitabu. Aliweka maktaba kwenye saloon yake badala ya TV na kila mtu aliyesoma kitabu alipewa punguzo wakati wa kunyolewa.
Wewe ni mabadiliko gani unataka uyaone kwenye jamii yako. Utachukua hatua gani ndogo kuhakikisha na wewe unakuwa sehemu ya hayo mabadiliko?
Nishirikishe kupitia godiusrweyongeza1@gmail.com
SOMA ZAIDI: TATIZO LAKO WEWE
Hapa Ndipo Mabadiliko Makubwa Huanzia
Kama Unataka Kubadili Dunia Fanya Haya Hapa
Ni mimi
Godius Rweyongeza
0755848391
Morogoro-Tz.