Home


  • Namba Zetu Za Malipo

    Namba za malipo ya vitabu:

    Namba za lipa

    TIGO PESA: 19016638 Jina ni SONGAMBELE CONSULTANTS

    M-PESA: 5564517 jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

    Namba za kawaida

    AIRTEL MONEY: 0684408755
    TIGO PESA: 0655 848 392
    M-PESA: 0745 848 395

    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    NB: Kama namba ya malipo anatumiwa mtu ambaye yuko nje ya nchi. Iandikwe Kwa kuanza na +255

    Kwa hiyo namba zinazotumwa nje ya nchi zitakuwa
    Airtel money: +255 684 408 755
    TIGO PESA: +255 655 848 392
    M-PESA: +255 745 848 395

    KOTE Jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Kama malipo yatakuwa yanafanyika kupitia benki.

    Yafanyie kupitia

    1. CRDB BANK: 0150770710200
    2. NMB BANK: 22110047274

    Kote jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

  • Wasiliana na Godius Rweyongeza Sasa

    Habari yafuatayo ni mawasiliano Unayoweza kutumia kumpata GODIUS RWEYONGEZA

    Simu: +255 (0) 684408755

    Whatsap: +255 (0) 755848391

    Email: songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu vyake wasiliana Moja kwa Moja na +255 (0) 684408755 (more…)

  • Fursa Tano Ambazo Vijana Wa Siku Hizi Wanachezea (SEHEMU YA TATU)

    Kama hukusoma sehemu ya pili bonyeza HAPA

    3. Fursa ya kufanya kazi kwa bidii

    Kwani kufanya kazi kwa bidii ni fursa? 

    Na hapa ningependa nikurudishe tena nyuma mpaka miaka ya akina Napoleon Bonaparte. Umewahi kumsikia huyu mtu? Bonaparte alikuwa mbabe wa vita wa nyakati zake na pengine mbabe wa vita wa nyakati zote. Alipigana Sana vita na kushinda kwa kishindo kila mara. Ila moja ya kitu kilichokuwa kinamfanya Bonaparte kuwa wa tofauti, ni juhudi zake katika kazi. Alikuwa na juhudi kazini kuzidi juhudi zenyewe, hahaha.

    Unaambiwa alikuwa anafanya kazi kiasi kwamba hata kama angekuwa bafuni, mtu akaja na nakala ya kusaini, alikuwa anatoka bafuni na sabuni mwilini, kusaini hiyo nakala Kisha anarudi bafuni kuendelea kuoga.

    Siku hizi vijana ni kama tumepotea vile. Unakuta mtu anasafu mtandaoni asubuhi, mchana mpaka jioni, huku akiwa hazalishi chochote. 

    Namkumbuka rafiki yangu aliyekuwa ananiambia eti mimi ninataka kazi ya kuwa naweka saini tu! Loo!

    Hivi ni kweli yupo mtu ambaye kazi yake ni kuweka saini tu? Ebu kwa mfano tuseme yupo. Kama kweli yupo, Basi walau kuna vitu viwili ambavyo nitakuwa na uhakika navyo kuhusu yeye.

    Kwanza ni mchapakazi. Anachapa kazi kwa viwango vya juu sana, kiasi kwamba ameaminiwa na kupewa kazi ya kusaini tu. 

    Maana kazi ya kusaini tu inakuhitaji uwe mfuatiliaji ili kuhakikisha unachosaini kipo sawa. La sivyo unaweza kujikuta unasaini vitu visivyoeleweka ukapoteza kazi yako, cheo na kila kitu na hata kuwaharibia wengine.

    Kazi ni gharama ambayo unapaswa kuilipa na kazi huwa haiangushi mtu.

    Nimeandika kitabu kinachoitwa MAISHA NI FURSA;  ZITUMIE ZIKUBEBE. Kitabu hiki ninaenda kukizindua rasmi tarehe 1.10.2021.

    Ila habari njema ni kuwa leo hii unaweza kuweka oda ya kupata kitabu hiki. Na kwa atayaweka oda;
    Kwanza atapata kitabu kwa bei ya punguzo.
    Pili, nitampa vitabu vingine vya ziada kama zawadi; tena hivyo vitabu vingine vya zawadi nitavituma leo hii baada ya mtu huyo kuweka oda.

    Kuweka oda utalipia, elfu kumi tu (10,000/-) tu. Ila kwa kuwa utalipia elfu kumi leo hii, utpewa  vitabu vingine vitatu wakati ukiendelea kukisubiri kitabu cha maisha ni fursa, ZITUMIE ZIKUBEBE.
    Vitabu utatavyopewa kwa sasa ni
    1. KUTOKA SIFURI MPAKA KILELENI
    2. SEKTA 11 ZA KUTENGENEZA MAMILIONI YA FEDHA TANZANIA
    3. MAAJABU YA KUWEKA AKIBA.

    Rusha elfu kumi leo kwa namba 0755848391. Upate vitabu hivyo vitatu, na kitabu cha MAISHA NI FURSA, ZITUMIE ZIKUBEBE kitatumwa kwako tarehe 1.10.2021 bila wewe kuhitajika kuongeza senti ya ziada.

    Namba ya malipo ni

    MPESA 0755848391
    Airtel money: 0684 408 755
    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA.

    NAKUKUMBUSHA TU: Ukituma elfu kumi leo. Taarifa zako zitatunzwa vizuri, na tarehe 1.10.2021 utatumiwa kitabu cha MAISHA NI FURSA; ZITUMIE ZIKUBEBE bila kuongeza senti ya ziada, wala bila kutukumbusha tukutumie.

    Karibu.

    Vitabu vyote ni soft copy.

    Ni mimi
    GODIUS RWEYONGEZA
    +255755848391
    MOROGORO-TZ

    Hakikisha Umesubscribe kwenye Channel yangu ya youtube kwa KUBONYEZA HAPA

    Jiunge na mfumo wa kupokea makala maalumu kwa njia ya barua pepe kwa KUBONYEZA HAPA

    Jipatie nakala za vitabu vyangu vya kiswahili kwa KUBONYEZA HAPA

    Kama ungependa kujifunza kuhusu uandishi kutoka kwangu wasiliana nami kwa 0755848391

    kila la kheri

  • KITABU CHA SUGU: From The Streets To Parliament; MUZIKI NA MAISHA

    Leo wakati natembea hapa mtaani, nimekutana na mtu anauza vitabu kikiwemo hiki cha wasifu wa SUGU.

    Nilivyoambiwa bei ya kitabu tu, sikuchelewa kutoa fedha mfukoni kukichukua!
    Kinaeleza maisha yake kutoka mtaani mpaka kufika bungeni.

    Ndio naanza kukisoma hivyo maswali yako yote yatunze. Utaniuliza nikimaliza kukisoma.

    Kwa wale mnaopenda vitabu vyenye picha, hiki kinaweza kukufaa pia. Kina picha za hapa na pale kuanzia utotoni, harakati za mziki na hatimaye akiwa hungeni.

    Nimefanya uchambuzi wa kitabu hiki hapa. Naomba ubonyeze hapa ili uweze kujifunza yaliyomo kwenye hiki kitabu

    Godius Rweyongeza

    0755848391

    Morogoro-Tz

    Hakikisha Umesubscribe kwenye Channel yangu ya youtube kwaย KUBONYEZA HAPA

    Jiunge na mfumo wa kupokea makala maalumu kwa njia ya barua pepe kwaย KUBONYEZA HAPA

    Jipatie nakala za vitabu vyangu vya kiswahili kwaย KUBONYEZA HAPA

    Kama ungependa kujifunza kuhusu uandishi kutoka kwangu wasiliana nami kwa 0755848391

    kila la kheri

  • Fursa Tano Ambazo Vijana Wa Siku Hizi Wanachezea (SEHEMU YA PILI)

     

    Leo tutaendelea na sehemu ya pili. Kama hukusoma sehemu ya kwanza; BONYEZA HAPA kwanza.

    2. Fursa ya kujifunza
    Acha nikurudishe nyuma tena, mpaka miaka ya akina Benjamin Franklin. Miaka hiyo walikuwa wanafanya apprenticeship kwa miaka 7-9. Huo ni muda ambao mtoto au kijana alikuwa ananolewa chini ya mtaalamu bila malipo. Kama kijana alifuatilia vizuri masomo yake basi ilikuwa inategemewa kuwa baada ya muda huo kijana atakuwa amenolewa na kunoleka. Na baada ya miaka hiyo 7,8 au 9 alikuwa anaweza kufanya kitu alichokuwa anaandaliwa kukifanya. Akina Darwin, wote walipitia kwenye kipindi hiki cha kujifunza kwa vitendo.

    Na hiki ndicho kimekuja kuzalisha ile dhana ya saa elfu kumi kwenye ulimwengu wa hamasa.
    Unaifahamu dhana ya saa elfu 10? Dhana hii imepewa unaarufu sana na mwandishi Malcon Gladwell. Kwenye kitabu chake cha Outliers, mwandishi kaainisha kuwa inachukua saa elfu kumi kwa mtu kuwa mbobevu kwenye jambo fulani.

    Yaani, kuwa hizi ni saa elfu kumi mbapo mtu anaweka akili yake, nguvu zake na kila rasilimali aliyonayo katika kufanyia kazi kipaji, ujuzi au kitu fulani. Na baada ya huo muda kama kweli mtu huyo atakuwa amejitoa na kujifunza kwa kina basi atakuwa ameweza kufanikiwa kufikia utaalam au ubobevu.
    Mwandishi anatolea mfano wa Bendi maarufu ya The Beatles. Hii ilikuwa bendi maarufu sana miaka ya 60 huko Marekani. Ilifanya maonyesho kwa weredi mkubwa na iliuza albamu nyingi kwa enzi zake. Mpaka leo hii inaaminiwa kuwa ni bendi bora kuwahi kutokea. Kama huamini kamuulize Google.

    Sijui kwa hapa Tanzania bendi maarufu miaka hiyo ilikuwa ipi. Ngoja kwanza nimpigie baba yangu, bila shaka ataniambia. Si unajua mimi kijana wa kisasa najua tu mambo ya akina Diamond, Alikiba na Harmonize? Hahaha

    Achana na hayo tuendelee bwana, Japo dhana ya saa elfu kumi imekuja siku za hivi karibuni, ila ilikuwepo tokea enzi hizo. Ndiyo maana enzi za akina Benjamin Franklin vijana walisota hiyo miaka 7-9. Kipindi ambacho sasa hivi kinaaminika kuwa kinaendana na hizo saa elfu kumi.

    Hata Benjamin Franklin alisota miaka 9 chini ya kaka yake akijifunza uchapaji wa vitabu tu. Ila walikuwa wanazingua kweli, au wewe unasemaje. Eti jamaa miaka 9 alikuwa anajifunza kuchapa vitabu tu! Loo!

    Ila kwa miaka hiyo ilikuwa lazima. Maana upatikanaji wa taarifa ulikuwa adimu sana. Siku hizi vijana tuna raha zetu asikwambie mtu. Kitu chochote kile unachotaka, unaingia Google tu na kukipata ndani ya sekunde chache. Halafu ninavyokujua wewe ukimaliza hapa utaenda kumtafuta Benjamin Franklin Google ili uone ninayosema ni sahihi au namsingizia. Kama nakuona vile.

    Wanasema kwamba taarifa zinazopatikana sasa hivi ni nyingi sana kiasi kwamba hata mfalme wa karne ya 15 hakuwa na uwezo wa kuzipata. Kabisa.

    Sisi tunayo hazina kubwa. Tuna mitandao ya kufundisha kwa video Kama YouTube.
    Tuna mitandao ya kufundisha kwa njia ya sauti tu.
    Tuna vitabu, ambavyo aidha vinapatikana kwa bei rahisi sana au bure kabisa. Wakati babu zetu hawakuwa na uwezo wa kupata hivi vitu vyote, kitu kilichowafanya waendelee kubaki nyuma. Ila sisi tunavyo vyote tena kiganjani.

    Leo hii ukiamua kujifunza kilimo cha kitunguu ni rahisi sana ukilinganisha na babu yako miaka 60. Halafu wewe hii fursa unaichukulia poa.

    Sisi hivi vitu tunavichukulia poa kwa maana tunaona vipo tu, ila kama nilivyokwambia jana, kama babu yako angekuwa anafufuka leo hii. Angeweza kukuchapa viboko maana unachezea fursa ya kujifunza.

    Leo hii kuna watu wanasema kuwa ile dhana ya saa elfu kumi unaweza kuipunguza kutokana na wingi wa maarifa. Unaweza kujifunza kwa kina kitu fulani tena kwa gharama nzuri na kupunguza hizo saa.
    Kitakachokufanya upunguze hizo saa ni

    Moja, kujifunza kutoka kwenye makosa ya watu wengine. Wewe huhitaji kurudia makosa ambayo yamefanywa na wengine badala yake unajifunza  na kuyaepuka hayo.
    Pili, kujifunza Kutoka kwa mambo ambayo watu wengine wamefanya vizuri ili uyafanye vizuri zaidi. Ni ujinga kurudia makosa ambayo yamefanywa na watu karne ya 19 wakati wameshayaandika na unaweza kuyasoma.

    Labda unajiuliza nijifunze nini?
    Nimeshasema, ila nasisitiza tena.
    Soma vitabu,
    Jifunze kupitia mtandaoni (huko Kuna blogu na tovuti zenye mambo mengi ya kukufaa).
    Hudhuria semina.

    Kwa leo napenda kuhitimisha na nukuu kutoka Alvin Toffler. Kwenye kitabu chake cha The Future Shock anasema, mjinga wa karne ya 21 siyo yule ambaye hajui kusoma, bali anayejua kusoma ila hasomi.

    Kijana kama unajua kusoma ila husomi basi wewe ni….(mimi naishia hapo, usije ukanipiga mawe bure)
        

    Nimeandika kitabu kinachoitwa MAISHA NI FURSA;  ZITUMIE ZIKUBEBE. Kitabu hiki ninaenda kukizindua rasmi tarehe 1.10.2021.

    Ila habari njema ni kuwa leo hii unaweza kuweka oda ya kupata kitabu hiki. Na kwa atayaweka oda;
    Kwanza atapata kitabu kwa bei ya punguzo.
    Pili, nitampa vitabu vingine vya ziada kama zawadi; tena hivyo vitabu vingine vya zawadi nitavituma leo hii baada ya mtu huyo kuweka oda.

    Kuweka oda utalipia, elfu kumi tu (10,000/-) tu. Ila kwa kuwa utalipia elfu kumi leo hii, utpewa  vitabu vingine vitatu wakati ukiendelea kukisubiri kitabu cha maisha ni fursa, ZITUMIE ZIKUBEBE.
    Vitabu utatavyopewa kwa sasa ni
    1. KUTOKA SIFURI MPAKA KILELENI
    2. SEKTA 11 ZA KUTENGENEZA MAMILIONI YA FEDHA TANZANIA
    3. MAAJABU YA KUWEKA AKIBA.

    Rusha elfu kumi leo kwa namba 0755848391. Upate vitabu hivyo vitatu, na kitabu cha MAISHA NI FURSA, ZITUMIE ZIKUBEBE kitatumwa kwako tarehe 1.10.2021 bila wewe kuhitajika kuongeza senti ya ziada.

    Namba ya malipo ni

    MPESA 0755848391
    Airtel money: 0684 408 755
    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA.

    NAKUKUMBUSHA TU: Ukituma elfu kumi leo. Taarifa zako zitatunzwa vizuri, na tarehe 1.10.2021 utatumiwa kitabu cha MAISHA NI FURSA; ZITUMIE ZIKUBEBE bila kuongeza senti ya ziada, wala bila kutukumbusha tukutumie.

    Karibu.

    Vitabu vyote ni soft copy.

    Ni mimi
    GODIUS RWEYONGEZA
    +255755848391
    MOROGORO-TZ

  • Fursa Tano Ambazo Vijana Wa Siku Hizi Wanachezea

    Ngoja kwanza, kwani fursa ni nini? Unafanyaje ili kujua kuwa kitu fulani ni fursa na kingine siyo fursa. Kwani fursa huwa zinavaa vazi gani haswa?

    Enewei, tuachane kwanza na maswali hayo japo nitayajibu mwishoni mwa makala haya, ila kwa sasa acha kwanza tuone fursa tano ambazo vijana wanachezea.  Hizi fursa, japo zinachezewa sasa hivi, hazikuwahi kuwepo miaka nyuma, ila zimejitokeza kwenye zama hizi na bado zinachezewa. Mababu zako wangekuwa wanafufuka na kuona jinsi unavyochezea fursa hizi, wangeweza hata kukupiga viboko! Hahaha, natania tu!

    Kwa kila fursa nitakueleza jinsi hali ilivyokuwa zamani, na jinsi hali ilivyo sasa hivi na mwisho kabisa, nitakueleza nini unaweza kufanya ili kuitumia fursa husika. Ngoja sasa tuanze.

    1. Fursa ya kunoa kipaji chako na kukitangaza kwa  gharama nafuu au bure kabisa

    Ngoja turudi nyuma mpaka karne ya 15,16,17, 18…mpaka karne ya 20. Hapa tunakutana na wanasayansi maarufu wa nyakati hizo, akina Isaac Newton, akina Michael Faraday, akina Einstein na wengineo. Pia tunakutana na wagunduzi wa nyakati hizo; akina Henry Ford, Thomas Edison na wengineo. Bila kusahau waandishi,wachoraji na wasanii wote wa zama hizo. Hao niliowataja hapo walikuwa maarufu au walau walifanya kazi zilizogusa jamii ya kipindi hicho, na nyingine bado zina msaada mkubwa mpaka leo hii. Kazi za watu kama Picasso, Leonard Da Vinci, Shakespeare na wengineo.

    Wakati hawa wanakuwa maarufu kwa gunduzi zao, maandishi ya ubunifu wao miaka hiyo, kuna wengine wengi walishindwa kutoboa kwa sababu ya kukosa namna ya kuwafikia watu sahihi ambao wangeweza kuwapa msaada wa kifedha kuwawezesha kunoa na kuinua vipaji vyao. Wengine walikosa nafasi kwenye majukwaa ili kuonesha kazi zao. Miaka hiyo kulikuwa na majarida na baadhi ya majarida, usingeweza kutoa chapisho lako kama wewe hukuwa mtu wa viwango fulani. Au kama hukuwa na konekisheni na mtu fulani.

    Mfano mzuri ni Michael Faraday, huyu alizaliwa kwenye familia ya kimasikini, kipindi hicho Uingereza ilikuwa imewatenga watu kwenye kundi la wenye nacho (royal class) na wasiokuwa nacho (servant class). Na Faraday alikuwa kwenye kundi la pili. Kumbe hakuwa na ruksa ya kuchapa kwenye jarida kutokana na kundi alilokuwemo. Stori yake nitaieleza siku nyingine, ila fahamu kuwa  jinsi alivyoweza kufikia viwango hivyo vikubwa mpaka kuwa mwanasansi mkubwa wa nyakati hizo, ilikuwa ni baraka kubwa sana kwake. 

    Kuna watu wengi enzi hizo walikuwa na vipaji hata kuwazidi wachoraji na wanasayansi wakubwa wa miaka hiyo. Ila hawakuweza kutoboa kwa sababu hawakuwa na konekisheni au fedha za kutosha. 

    Hiki kitu kwenye zama hizi kimepatiwa ufumbuzi kwa zaidi ya asilimia 80 Kama siyo 100 zote, hahaha. 

    Siku hizi ni rahisi sana kuanza kunoa kipaji chako hata kama huna konekisheni. 

    Kwa mfano ebu tuangalie miaka ya 1960. Kama wewe ungependa kuwa msanii na kutoa kazi yako, kulikuwa na mlolongo mrefu. Studio tu kurekodi wimbo wako ilikuwa mbinde. Na hapo hujaingia kwenye kuutangaza redioni, magazetini na kwenye runinga.

    Ila sasa tuangalie kinyume chake. Siku hizi ni rahisi sana. Kwanza, ukiwa na kipaji cha kuimba tu, utatunga wimbo. Utaenda studio na kurekodi wimbo wako bila shida yotote ile. Baada ya hapo unaweza kuanza kuusambaza kwa ndugu zako, marafiki zako wa karibu na watu wengine unaoweza kuwafikia. Badala ya kuutambulisha wimbo wako redioni, unaweza kuutambulisha wimbo wako mtandaoni na watu wakausikiliza. Wakiupenda watawatumia wengine pia. Na hao wengine watawatumia wengine zaidi. Unaweza kujikuta kipaji chako kinakufanya uwe maarufu ndani ya muda mfupi sana. 

    Lakini je, ni vijana wangapi wanatumia hiyo fursa?

    Ebu kwa mfano ona mambo yalivyokuwa kwa mwandishi. Kabla ya kuandika kitabu, ulipaswa kupata ruhusa kutoka kwa wachapaji wa vitabu iliyokuwa inasema, andika kitbu chako. Hapo ndio ulianza kuandika  kitabu chako, kisha baada ya hapo,  ulikipeleka kwa wachapishaji waliokupa ruhusa kukiandika ili wakisome. Kama wangekipenda, basi ulikuwa unapewa ruhusa ya kukichapa, ila kama hawakukipenda, uandishi wako ulikuwa unaishia hapo.  Kipindi hicho kuna waandishi wengi kweli walishindwa kutoboa. Pengine hata babu yako alishindwa kuandika kitabu kwa sababu hiyo. Hahaha, hapo nimechomekea tu.

    Ila sasa hivi mambo yamebadilika. Unaweza kuandika, kuchapa na kuuza kitabu chako ukiwa chumbani kwako. Unapata wazo na kuanza kuliandikia na baadaye unachapa na kuuza kitabu chako kwa njia ya mtandao. Unatengeneza fedha. 

    Siyo hivyo tu, nadhani siku za nyuma utakuwa ulisikia sana watu wanazungumzia bifu za wasanii na wamiliki wa vyombo habari na wasanii kutonufaika na kazi zao. Kama vyombo vya habari havikupenda kazi yako, basi 

     kiufupi hapo ulikuwa huwezi kusambaza kazi yako. Ila leo hii tunaye YouTube, habagui kazi za watu, wala hapendelei watu.

    Tunayo majukwaa mengi ya kuonesha kazi zetu kama mtandao wa Amazon ambapo unaweza kuuza vitabu na bidhaa zako nyingine. Mtandao huu wenyewe haubagui bidhaa yako. Wewe kama unayo bidhaa yako unaweza kuuza, na ukiweza kutengeneza bidhaa nzuri, soko litakukubali na kuipokea kwa mikono miwili. Kitu hiki babu yako asingeweza kukifanya miaka ya 1920. 

    Kumbe zama zimebadilika. Maisha yamebadilika na mtandao wa intaneti unaleta fursa nyingi kweli kwelikweli. Kazi ni kwako kuzitumia. 

    Kwa leo naishia hapa, ili nikuachie nafasi ya kutafakari ulichojifunza mpaka hapa. Kesho tutaendelea na fursa namba 2 inayochezewa na vijana kwenye zama hizi.

    Ila kuna kitu kimoja nimekumbuka, mwanzoni mwa makala hii, nilianza kwa kukuuliza, kwani fursa ni nini?

    Unafanyaje ili kujua kuwa kitu fulani ni fursa na kingine siyo fursa. Kwani fursa huwa zinavaa vazi gani haswa?

    Kujibu maswali hayo na mengine, nimeandika kitabu kinachoitwa MAISHA NI FURSA;  ZITUMIE ZIKUBEBE. Kitabu hiki ninaenda kukizindua rasmi tarehe 1.10.2021.

    Ila habari njema ni kuwa leo hii unaweza kuweka oda ya kupata kitabu hiki. Na kwa atayaweka oda; 

    Kwanza atapata kitabu kwa bei ya punguzo. 

    Pili, nitampa vitabu vingine vya ziada kama zawadi; tena hivyo vitabu vingine vya zawadi nitavituma leo hii baada ya mtu huyo kuweka oda.

    Kuweka oda utalipia, elfu kumi tu (10,000/-) tu. Ila kwa kuwa utalipia elfu kumi leo hii, utpewa  vitabu vingine vitatu wakati ukiendelea kukisubiri kitabu cha maisha ni fursa, ZITUMIE ZIKUBEBE.

    Vitabu utatavyopewa kwa sasa ni 

    1. KUTOKA SIFURI MPAKA KILELENI

    2. SEKTA 11 ZA KUTENGENEZA MAMILIONI YA FEDHA TANZANIA

    3. MAAJABU YA KUWEKA AKIBA.

    Rusha elfu kumi leo kwa namba 0755848391. Upate vitabu hivyo vitatu, na kitabu cha MAISHA NI FURSA, ZITUMIE ZIKUBEBE kitatumwa kwako tarehe 1.10.2021 bila wewe kuhitajika kuongeza senti ya ziada.

    Namba ya malipo ni 

    MPESA 0755848391

    Airtel money: 0684 408 755

     Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA.

    NAKUKUMBUSHA TU: Ukituma elfu kumi leo. Taarifa zako zitatunzwa vizuri, na tarehe 1.10.2021 utatumiwa kitabu cha MAISHA NI FURSA; ZITUMIE ZIKUBEBE bila kuongeza senti ya ziada, wala bila kutukumbusha tukutumie.

    Endelea na SEHEMU YA PILI KWA KUBONYEZA HAPA

    Karibu.

    Vitabu vyote ni soft copy.

    Ni mimi

    GODIUS RWEYONGEZA

    0755848391

    MOROGORO-TZ

  • Vitu Vitano Ambavyo Havitabadilika Miaka Kumi Ijayo

     

    Vimeandikwa vitabu vingi sana kuhusu mabadiliko. Vinaeleza kuwa unapaswa kubadilika maana mambo yanabadilika. Mimi pia nimekuwa nikiandika kuhusu mabadiliko ila leo ninataka kukwambia vitu vitano ambavyo havitabadilika miaka 10 ijayo.

    Ubora ni kuwa ukivijua vitu ambavyo havitabadilika, unaweza kuvitumia kwa manufaa na kuvifanya kuwa fursa. Hivyo, hivi hapa ndivyo vitu ambavyo havitabadilika ndani ya miaka 10 ijayo;

    1. Watu kupenda vitu vizuri kwa bei rahisi

    Hiki ni kitu ambacho kitaendelea kuwa kipaumbele kwa watu. Watu wataendelea kupendelea kupata vitu vizuri kwa tena kwa bei rahisi sana. Na hii ishara kuwa hii inaweza kuwa fursa nzuri kwako. Ni fursa kwako kuanzisha biashara katika msingi ambao utakuwa ukiwasaidia watu kupata huduma nzuri, tena kwa bei nafuu.

    2. Watu wataendelea kupenda kupata huduma kwa haraka

    Sasa hivi tupo katika kipindi ambapo watu wanapenda kupata huduma nyingi kwa haraka kweli. Ndio maana siku hizi utasikia kuna magari ya mwendokasi, mitandao ya simu inajinadi kwa intaneti  yenye kasi, kuna migahawa inayotoa chakula cha haraka (fast food), hii yote ni kuonesha kuwa vitu vya haraka vinahitajika sasa hivi na vitaendelea kuhitajika kwa siku nyingi zijazo. Huduma  za kutuma fedha kwa haraka kama mpesa na tigo pesa zimekuwa maarufu, kwa sababu zinatoa nafasi ya kupata huduma ya kifedha kwa usalama, uhakika na haraka.

    Hii nayo ni fursa unayopaswa kuangalia namna ya kuitumia.

    3. Kula chakula

    Ndio, watu wataendelea kula na kunywa ndani ya miaka 10 ijayo. Hawataacha kula wala kunywa. Hii nayo ni fursa ambayo unaweza kuitumia kwa manufaa yako. Unaweza kwa mfano kuanzisha mgahawa kwa ajili ya kuwapatia watu chakula, unaweza kuongeza thamani ya vyakula, unaweza kuingia sahambani kulima, unaweza kuwa msambazaji wa chakula n.k. hapa napo fursa ni nyingi.

    4. Saa 24 kwa siku

    Sidhani kama kitagunduliwa kifaa cha kuongeza muda ndani ya miaka kumi ijayo. Hivyo, muda utabaki kuwa saa 24 kwa siku. Hii nayo ni fursa, japo saa zitabaki kuwa 24 ndani ya muda huu ila majukumu  ya watu yataongezeka na wewe unaweza kuwa mtu utakayewasaidia hawa watu kwa kurahisisha au hata kufanya majukumu yao yaliyoongezeka. 

    Angalia kitu ambacho unachoweza kurahisisha na jikite hapo.

    5. Watu wataendelea kupenda kupata uhakika wa huduma wanazopata. Watu watahitaji uhakika. Uhakika kuwa wanatumia fedha zao sehemu sahihi, uhakika kuwa wewe ni mtu sahihi, uhakika kuwa bidhaa zako ni bora kuliko nyingine, n.k.

    Na wewe unapaswa kuwapa uhakika watu hao. Ndio maana siku hizi, utaona watu wanatoa bidhaa na guarantee. Hii yote ni kwa ajili ya kuwapatia uhakika wateja.

    Kwa Leo naishia hapo.

    Hayo ndiyo mambo matano ambayo hayatabadilika ndani ya miaka 10 ijayo. Hivyo, kama upo makini,  unaweza kuchagua eneo moja na kuligeuza kuwa fursa ambayo wewe utachangamkia.

    Nimeandika kitabu, kinaitwa MAISHA NI FURSA, ZITUMIE ZIKUBEBE. Kitabu hiki kimezungumzia sana juu ya suala zima la fursa, jinsi ya kuziona na kuzitumia kwenye maisha. Na kitabu hiki kitazinduliwa rasmi tarehe 1.10.2021.

    Ila habari njema ni kuwa leo hii unaweza kuweka oda ya kupata kitabu hiki. Na atayaweka oda; kwanza atapata kitabu kwa bei ya punguzo. Pili, nitampa vitabu vingine vya ziada kama zawadi; tena hivyo vitabu vingine vya zawadi nitavituma leo hii baada ya mtu huyo kuweka oda.

    Kuweka oda utalipia, elfu kumi tu (10,000/-) tu. Ila kwa kuwa utalipia elfu kumi leo hii, utpewa  vitabu vingine vitatu wakati ukiendelea kukisubiri kitabu Cha maisha ni fursa, ZITUMIE ZIKUBEBE.

    Vitabu utkavyopewa kwa sasa ni 

    1. KUTOKA SIFURI MPAKA KILELENI

    2. SEKTA 11 ZA KUTENGENEZA MAMILIONI YA FEDHA TANZANIA

    3. MAAJABU YA KUWEKA AKIBA.

    Rusha elfu kumi leo kwa namba 0755848391. Upate vitabu hivyo vitatu, na kitabu cha MAISHA NI FURSA, ZITUMIE ZIKUBEBE kitatumwa kwako tarehe 1.10.2021 bila wewe kuhitajika kuongeza senti ya ziada.

    Namba ya malipo ni 

    MPESA 0755848391

    Airtel money: 0684 408 755

     Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA.

    NAKUKUMBUSHA TU: Ukituma elfu kumi leo. Taarifa zako zitatunzwa vizuri, na tarehe 1.10.2021 utatumiwa kitabu cha MAISHA NI FURSA; ZITUMIE ZIKUBEBE bila kuongeza senti ya ziada, wala bila kutukumbusha tukutumie.

    Karibu.

    Vitabu vyote ni soft copy.

    Ni mimi

    GODIUS RWEYONGEZA

    0755848391

    MOROGORO-TZ

  • Waafrika Tuutafute Ukweli Wetu; Wazungu Wamedanganya Vyakutosha Sasa

     

    Waafrika tukiujua ukweli kuhusu sisi utatusaidia kufanya makubwa zaidi.

    Kuna ukweli mwingi umefichwa.

    Vitabu vya historia vyenyewe vimeandika historia feki.

    Vyombo vya habari vikubwa, vinatoa habari zisizokuwa za kweli. Vinatoa habari kwa maslahi ya wamiliki wa vyombo hivyo.

    Kitu kinachotufanya tuendelee kuamini uongo kama ukweli. 

    Najisikia kusema kitu kuhusu Afrika na uongo mwingi uliosemwa/unaosemwa kuhusu Afrika. Na nitakuwa nikusema Mara kwa mara kupitia blogu hi hapa.

    Rise Afrika.

  • Mambo 100 Ya Kujifunza Kutoka Kwenye Kitabu Cha Rich Dad Poor Dad

    Kitabu: RICH DAD POOR DAD
    Mwandishi: Robert Kiyosaki
    Mchambuzi: Hillary Mrosso
    Simu: +255 683 862 481

    UTANGULIZI

    RICH DAD POOR DAD, ni kitabu cha ajabu sana, tangu kiandikwe zaidi ya miaka 25 iliyopita kimeleta mageuzi makubwa sana kwenye maisha ya watu, makampuni, biashara, fedha, uwekezaji, uongozi, ujasiriamali na utajiri. Ni kitabu ambacho kinaelezea mifumo ya maisha na vipaumbele vya wazazi wawili ambao mmoja ni tajiri na mwingine ni masikini. Kila mmoja alikuwa na mitazamo yake yanapokuja masuala ya kifedha, utajiri, uwekezaji, biashara, elimu na hata malezi ya watoto. Katika uchambuzi wa kitabu hiki nitaelezea kwa kina mambo haya. Ninaweza kuungana na watu wengine mashughuri waliosema hiki ndio moja ya kitabu bora sana kuwahi kuandikwa katika karne hii kuhusu masuala yote muhimu ya kifedha uwekezaji. Nakukaribuisha katika uchambuzi wa kitabu hiki tujifunze kwa kina mambo 100 niliyoyaona katika kitabu hiki cha RICH DAD POOR DAD.

    1. Kati ya vitu alivyosisitiza sana mwandishi wa kitabu hiki ni jinsi elimu ya fedha ilivyo muhimu kwenye maisha yetu ya kila siku. Mwandishi ametilia sana mkazo katika kupata maarifa sahihi ya fedha yatakayotutoa kwenye umasikini wa kipato na kutufanya kuwa matajiri.

    2. Mfumo wetu wa elimu ulivyoshindwa kutuandaa katika maisha halisi ya duniani yanayohusu fedha na uwekezaji. Badala yake mfumo umejikita kutuandaa kuwa wataalamu wa kuifanyia pesa kazi ili tupate utajiri.

    3. Mfumo wetu wa elimu hautoi elimu ya msingi ya kupata fedha, kutengeneza fedha, kutunza fedha na kuzalisha fedha.

    4. Hata familia zetu zimejikuta zikiishi mfumo huo wa elimu na kukosa kabisa somo la fedha, na wazazi wetu hawajui hilo, ndio maana wanawekeza nguvu sana kwenye kupata elimu ya chuo pekee.

    5. Tunatakiwa kubadilika haraka na kuacha kufikiri elimu ya chuo pekee ndio itatutoa kwenye umasikini.

    6. Elimu ya chuo tunayoipata ina mapungufu mengi hasa kwenye kipengele cha fedha, haituandai jinsi ya kutatua changamoto za kifedha.

    7. Nadharia ya kusoma kwa bidi, upate maksi kubwa, ili uje kupata kazi nzuri na salama inayolipa, inaweza kuwa sio ushauri mzuri sana kwa zama hizi.

    8. Kama unataka kuwa tajiri, jua kuwa unahitaji sana kuielewa fedha kiundani nasio kujua kufanya kazi kwa bidii pekee.

    9. Ni ngumu sana na hutaweza kuwa tajiri kwa kutegemea ajira pekee, jifunze namna ya kuzalisha fedha jitaidi kuwekeza kwenye vitu vinavyokuingizia fedha.

    10. Kazi kubwa ya kufanya kama unataka kufikia utajiri na kuwa na uhuru wa kifedha ni kujielimisha kila wakati kuhusu mambo ya kifedha.

    11. Mengi tunayojifunza ni namna ya kutumia pesa kwenye mambo yasiyozalisha fedha, na hapo ndio changamoto kubwa huanzia. Mfano kununua vitu vingi visivyokuingizia fedha.

    12. Mwandishi ameonyesha sehemu kubwa ya maisha yetu tunajua kutumia tu vifedha kidogo tunavyopata, na huvitumia katika kununua vitu visivyozalisha (liability) badala ya kununua vitu vinavyozalisha fedha (asset).

    13. Mwandishi anashauri sana tutafute progamu na mafunzo ya kutuelimisha kuhusu fedha, ni somo muhimu sana kwenye zama hizi.

    14. Mwandishi anapendelea kila mtu kujua kuhusu uhasibu na uwekezaji maana huko ndio msingi wa fedha na usimamizi wake huanzia.

    15. Tunashauriwa kujitoa kwenye mbio za panya, ambazo ni mzunguko wa maisha unaojirudia rudia na hauna tija wala machango katika safari ya kukufanya kuwa tajiri na kuwa huru kifedha.

    16. Tunatakiwa kubadili mbinu katika mchezo, maana hatuwezi tena kuendelea na mbinu za zamani ambazo haziwezi kutatua changamoto za kifedha tulizonazo.

    17. Kumbuka mitaala mingi ya elimu imeandaliwa kutufanya wafanyakazi, wanaoifanyia kazi pesa, kwa malipo kidogo.

    18. Pia kupitia uzoefu wake akiwa nyumbani anasema somo la fedha ni gumu zaidi kufundishwa nyumbani kuliko vyuoni. Hii ni kutokana na mfumo wa elimu na namna watu na wazazi wetu walivyoaminishwa kuhusu fedha.

    19. Wazazi wengine huwaambia watoto wao kuwa fedha sio nzuri, na watu wanaopenda fedha wana roho mbaya, ni watu wenye tamaa na wasiojali wenzao. Mambo kama haya mtoto anakuwa akijua fedha sio nzuri na hana haja ya kuipa kipaumbele kama sehemu muhumu ya maisha.

    20. Tofauti na matajiri, wao hufundisha watoto wao misingi ya kupata fedha, kutunza fedha, kuzalisha fedha na huwafundisha watoto wao namna ya kutoa fedha na kuwasaidia wengine.

    21. Ujinga mwingi tulio nao kwenye mambo ya fedha ndio hutuletea changamoto za kifedha za kila siku.

    22. Tunatakiwa kuziruhusu akili zetu zifanye kazi inapokuja suala la fedha, na sio kuzizuia kama wengi wanavyofanya, ipe akili yako majukumu ili ihangaike kukutafutia suluhisho la changamoto za kifedha.

    23. Husisha na tumia akili zaidi linapokuja suala nyeti kama la fedha, tumia akili zaidi kuliko hisia. Hii ndio njia ya kulinda matumizi mabaya kwenye fedha zako.

    24. Ruhusu changamoto za maisha zishughulishe akili zako ili kukupatia suluhisho kwenye changamoto za kifedha unazokutana nazo.

    25. Kamwe usikubali wala kuruhusu changamoto za maisha zikufanye ushindwe na kuwa mnyonge au zikuharibu, zitumie kwa faida yako maana ndio mwalimu mzuri.

    26. Utajua una uwezo mkubwa kiakili pale unapoipa akili yako majukumu ya kufikiri kila wakati, usizimishe uwezo huo ambao umepewa na Mungu, kila mtu ana uwezo huo, uache utokee na ukusaidie kifedha.

    27. Jitahidi sana kutokuogopa, ondoa hofu zinazokupeleka kwenye umasikini wa kipato, dhibiti kabisa na uwe tayari kuchukua hatua za kijasiri ili utoke kwenye umasikini.

    28. Inahitaji ujasiri na moyo mkuu kuamua kutoka kwenye mazoa na tabia zinazokurudisha nyuma kifedha, amua kwa dhati inapofikia unataka kubadilika na kuwa tajiri, sio safari nyepesi.

    29. Usiruhusu hofu ikutawale maana utashindwa kuchukua hatua za kijasiri kujitoa kwenye umasikini na madeni, hofu inakufanya unakuwa mtumwa wa fedha.

    30. Kumbuka siku zote serikali huwa ndio ya kwanza kuchukua fedha zako kama kodi, na watakata kodi unapopata fedha zako, watakata kodi unapozitumia, watakata kodi unapozihifadhi, wanakata kodi hata utakapokufa.

    31. Wanaolipa kodi nyingi ni watu masikini na watu wa kati walioajiriwa, matajiri hawateseki na kodi kama masikini.

    32. Waajiriwa wengi wanawalaumu sana mabosi wao kwa matatizo waliyonayo wao wenyewe.

    33. Mfumo wa maisha ya wengi ni kama vile wamezaliwa kuja kufanyia kazi watu wengine na kisha wakipata fedha wakalipe kodi wanazodaiwa.

    34. Pesa ina nguvu sana, jitahidi kutumia hiyo nguvu kukufanikisha kwenye maisha na sio hiyo ngumu iwe kinyume chako.

    35. Dhibiti kabisa hisia na tamaa zako linapkuja swala la fedha maana usipofanya hivyo utaishi kwa hofu na kamwe hutaweza kuwa tajiri.

    36. Kwa kiasi kikubwa umasikini na changamoto nyingi hunasababishwa na ujinga kwenye masuala ya kifedha.

    37. Hakuna kuhitimu chochote kwenye maisha, usihitimishe elimu yako, jifunze kila siku hata kama umefikia hatua kubwa kwenye maisha.

    38. Wengine wakimaliza chuo ndio basi tena hakuna cha kujifunza tena, na hapo ndio kiburi huzaliwa na kuwazuia wasijifunze chochote maana huona wanajua kila kitu.

    39. Tumia hisia zako kufikiri na sio kufikiri kwa kutumia hisia hasa kwenye mambo ya fedha.

    40. Mara nyingi sio kazi rahisi kuwapata wafanyakazi au wasimamizi waaminifu na wazuiri, ni kazi sana kuwapata, jua hilo siku zote.

    41. Pesa bila kuwa na akili ni sawa na kupoteza tu.

    42. Muhimu kwenye fedha sio kujua tarakimu tu, bali kujua maana na hizo tarakimu zinaashiria kitu gani.

    43. Ni muhumu kuelewa ujumbe ambao unaupata hasa kwenye masula ya fedha na uwekezaji, elewa maana ya ujumbe huo kwa kina.

    44. Jifunze kusoma taarifa za kifedha na kuzielewa, ili uboreshe biashara yako.

    45. Pambana uwezavyo kuondoa kabisa ujinga hasa kwenye masula ya fedha, pata kila elimu kuhusu fedha jinsi inavyofanya kazi na jinsi inavyoweza kukufanyia kazi.

    46. Elewa kwa undani kuhusu asset na liability, kamwe usichanganye, maana ndio zitaamua uhuru wako wa fedha kwa siku zijazo.

    47. Asset ni vitu ambavyo vinakuingizia fedha, au vitu ambavyo vinaweka fedha mfukoni mwako.

    48. Liability ni vitu ambavyo hutoa fedha mifukoni mwako, yani vitu ambavyo havikuingizii fedha.

    49. Kama unataka kuwa tajiri mapema zinagatia sana katika kuwekeza kwenye asset na sio liability.

    50. Kama huna matumizi mazuri ya fedha, hata ukiongezewa fedha nyingi pia hutakuwa na matumizi mazuri, zaidi utazidisha matumizi mabaya ya fadha zako.

    51. Changamoto nyingi za kifedha tunazopitia ni kutokana na kufuata mkumbo na kununua vitu ili kuwafurahisha wengine.

    52. Watu wenye akili huajiri na hufanya kazi na watu wenye akili zaidi ili wazidi kufaninkiwa
    53. Ukizidisha hisia sana inaweza kuathiri hata uwezo wako wa kifedha unashuka.

    54. Moja ya maana ya utajiri ni kuwa na uwezo wa kuishi siku nyingi zaidi bila kufanya kazi yoyote na kuweza kumudu gharama zote za maisha.

    55. Utajiri unapimwa kuwa na mzunguko mkubwa wa fedha kwenye asset zako.

    56. Matajiri mara azote hununua asset au vitu vitakavyowaingizia fedha zaidi, masikini na watu wa kati wenyewe hupenda matumizi na kununua vitu visivyowaingizia fedha.

    57. Matajiri wataendelea kuwa matajiri na masikini watendelea kuwa masikini kwasababu wanatofautiana sana katika matumizi yao ya fedha.

    58. Changamoto nyingi za kifedha huwa zinatokana na watu kutumia muda mwingi wa maisha yao kuwafanyia wengine kazi, au kuajiriwa au kukaa katika ajira.

    59. Hatari au risk inapungua pale unapopenda kuwekeza na kuelewa uwekezaji kwa ujumla, uelewa hupunguza hatari.

    60. Kila fedha inayongia kwenye uwekezaji wako, ifanye ikufanyie kazi kama mtumwa wako.

    61. Tumia uwezo wako wa kiakili kifedha ili kupata vitu unavyovitamani katika maisha yako.

    62. Kama unaifanyia kazi fedha, pesa itakutesa, pesa itakunyanyasa, na siku zote hutakuwa na sauti kwa mwajiri wako. Pesa inatakiwa ikufanyie wewe kazi.

    63. Jitahidi kutengeneza sauti yako, kwa kuwekeza na kujizoeza kujifunza masula ya kifedha kwa undani ili uimiliki fedha, na sio fedha ndio ikupelekeshe.

    64. Pambana kutafuta uhuru wako kifedha, jitie bidii kujitoa kwenye umasikini kwa kujifuza kuhusu fedha.

    65. Moja ya sifa kuu za kitajiri ni kuwa na uweza wa kusoma taarifa za kifedha na kuzielewa barabara.

    66. Misingi mikuu ya kuwa na uwezo wa kiakili kifedha ni kuelewa mahesabu ya fedha (accounting), uwekezaji, masoko na masuala ya kisheria.

    67. Ni muhimu kuwa na shirika au kampuni yako katika safari za kusaka utajiri.

    68. Kwenye safari ya kuwa tajiri na kufikia uhuru wa kifedha wengi wanarudishwa nyuma na hofu zao wenyewe, kutokujiamini.

    69. Hofu na kutojiamini kunaondoa na kudumaza uwezo wako wa akili kwenye mambo ya fedha.

    70. Safari ya kuwa tajiri inahitaji akili na ujasiri mkubwa maana changamoto ni nyingi.

    71. Watu wengi linapokuja suala la hela wanachojua na ujuzi walionao ni kufanya kazi kwa bidii tu.

    72. Tunashauriwa tusifanyekazi tu kwasababu tunalipwa,bali tufanye kwasababu tutanajifunza.

    73. Ifanye pesa iwe mtumwa wako, pesa ikufanyie kazi na sio vinginevyo.

    74. Muhimu kuwa na ujuzi katika haya; Usimamizi wa mzunguko wa fedha, usimamizi wa mifumo muhimu kama familia, muda, usimamizi wa watu.

    75. Watu wengi walio bize ni wavivu kufuatilia masula muhimu kama masuala ya fedha.

    76. Wengi wanatumia kiburi kuficha ujinga wao maana hawapo tayari kujifunza.

    77. Kila kipato unachopata kwenye maisha yako, jilipe mwenyewe kwanza.

    78. Tengeneza nidhamu ya juu sana kuhakikisha kila kipato unachpata unajilipa mwenyewe kwanza, kisha ndio ulipe mambo mengine kama vile kodi.

    79. Tumia pressure ya wanaokudai kutengeneza njia nyingine za kukuinginzia kipato ili uweze kuwalipa.

    80. Kuwa mtoaji, unapofanikiwa kifedha na unapopungukiwa kifedha jambo muhimu la kufanya ni kuwa mtoaji.

    81. Walipe vizuri wafanyakazi wako, maana hao ndio wanakusaidia mambo mengi kwenye biashara yako.

    82. Elewa kuwa asset ndio hununua vitu vya anasa au luxuries.

    83. Kopa pesa ili uzalishe pesa na sio vinginevyo.

    84. Kuwa na mtu unayemwangalia kama model au shujaa wako kwenye safari yako ya utajiri, angalia waliofanikiwa na wanaofanya unachotaka kufanya.

    85. Wafundishe wengine mambo unayoyajua kuhusu maisha na fedha, kwa kufanya hivyo utapokea mara nyingi zaidi ya kile ulichotoa.

    86. Ni vizuri sana kama hutoingia au kuwa na madeni kwenye maisha yako.

    87. Kanuni ya maisha kama unataka chochote, basi jufunze kutoa kwanza na sio tofauti na
    hapo.

    88. Kama kuna kitu chochote unakitaka kwenye maisha, toa kwanza kile ulicho nacho, ndio utapata unachokitaka.

    89. Masikini wengi ni wachoyo na wana roho mbaya, wanasubiri wafanyiwe kitu kwanza ndio na wao wafanye, yani wapokee kwanza ndio nao wawe watoaji.

    90. Acha kufanya unachofanya, chunguza na pitia maisha yako kwanza angalia vinavyofanya kazi na vinavyokupotezea muda.

    91. Chukua Jukumu la kushughulikia masuala yako ya kifedha, usimuachie mtu mwingine.

    92. Jifunze sayansi ya kutengeneza fedha.

    93. Tafuta mawazo tofauti, katika uwekezaji, kisha chukua hatua mara moja.

    94. Tafuta aliyefanya uanachofanya.

    95. Tafuta mafunzo na madarasa ya kujifunza, nunua mafundisho.

    96. Tangeneza offa.

    97. Tembea maeneo tofauti ujifunze.

    98. Angalia sehemu sahihi

    99. Chukua hatua

    100. Anza mapema uwezavyo.

  • Uoga wako ndio umasikini wako

    Watalaam wa Biblia wanasema kwamba kwenye Biblia kuna usiogope 365. Maana yake kila siku ukiamka unaambiwa usiogope.

    Usiogope maana uoga wako ndio utakufanya uendelee kuishi maisha yaleyale kila siku bila kufanya kitu Cha tofauti ambacho kinaweza kuleta mabadiliko makubwa maishani mwako. Usiogope maana uoga wako ndio umasikini wako. Ukiogopa, hutachukua hatua yotote, kitu ambacho kitakufanya ushindwe hata kufanya vitu ambavyo vingekuletea maendeleo.

    Ukiendelea kuogopa na kufikiri kuwa watu watanionaje. Utashindwa kufanya kitu chochote cha maana.

    Unapaswa kuipiga chini, misuli ya uoga ili uweze kufanya vitu vinavyoeleweka.

    Neno uoga kwa kiingereza linaitwa FEAR. Kirefu chake ni False Evidence Appearing Real.

    Hii ndio kusema kuwa vitu vingi unavyoviogopa siyo sahihi na asilimia kubwa havitakuja kukutokea kama unavyodhani. Na vitakavyokutokea havitakuwa na madhara kama unavyodhani.

    Uoga una madhara mengi sana, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kukuua. Hivyo, achana na uoga vaa vazi la ujasiri.
    Muda ambao utaanza kujiambia kuwa ngoja niache, nisifanye kitu fulani kwa uoga. Amua ukifanye. Utanufaika zaidi kwa kukifanya hicho kitu kuliko kuendelea kuogopa.

    Kila la kheri.

    Soma zaidi:  Ijue maana nzuri ya MASIKINI

    Umekuwa nami,

    GODIUS RWEYONGEZA

    Hakikisha Umesubscribe kwenye Channel yangu ya youtube kwa KUBONYEZA HAPA

    Jiunge na mfumo wa kupokea makala maalumu kwa njia ya barua pepe kwa KUBONYEZA HAPA

    Jipatie nakala za vitabu vyangu vya kiswahili kwa KUBONYEZA HAPA

    Kama ungependa kujifunza kuhusu uandishi kutoka kwangu wasiliana nami kwa 0755848391

    kila la kheri

  • Jinsi ya kuwa na fedha kama serikali

    Bila shaka umewahi kusikia watu wanasema serikali ina fedha nyingi, au pengine wewe mwenyewe ndiye huwa unasema hivyo.

    Sasa leo ni zamu yako wewe kuwa na fedha kama serikali. Na utaweza hili kwa kuwa na vyanzo vingi vya kipato. Wanasema serikali ina mkono mrefu. Na fedha yake inapata kutoka sehemu nyingi.
    Kwanza ina una uwezo wa kuchapa fedha zake yenyewe. Na wewe unaweza kuchapa za kwako kama utafuata utaratibu nilioeleza kwenye makala hii.

    Pili, serikali inakusanya kodi kutoka maeneo mengi kwa wakati mmoja. Wewe pia unaweza kukusanya faida kutoka vyanzo vingi ambavyo vitakunufaisha wewe.
    Vyanzo kama, biashara zako, uwekezaji wako n.k.

    Rafiki yangu, kuanzia leo, anza kutengeneza mfumo utaokuwa unafanya kazi kwa manufaa yako ili kukunufaisha wewe na kukuongezea kipato. Na hili linawezekana sana kwenye zama hizi za ubepari. Wewe mwenyewe kuwa bepari.

    Soma zaidi: UCHAMBUZI WA KITABU CHA WEALTH OF NATIONS-8

    Umekuwa nami,

    GODIUS RWEYONGEZA

    Hakikisha Umesubscribe kwenye Channel yangu ya youtube kwa KUBONYEZA HAPA

    Jiunge na mfumo wa kupokea makala maalumu kwa njia ya barua pepe kwa KUBONYEZA HAPA

    Jipatie nakala za vitabu vyangu vya kiswahili kwa KUBONYEZA HAPA

    Kama ungependa kujifunza kuhusu uandishi kutoka kwangu wasiliana nami kwa 0755848391

    kila la kheri

  • USHAURI: Jinsi Ya Kuanzisha Biashara Ukiwa Umeajiriwa Bila Bosi Wako Kujua

     Ok vizuri.

    Inawezekana kuanzisha biashara ukiwa umeajiriwa. 

    Kwanza, unapaswa kujua aina ya biashara ambayo ungepsnda kuanzisha.

    Pili, unapaswa kujua na ratiba yako ya kazi. Hii itakusaidia kupangilia muda wa mwajiriwa wako na muda wa kufanya biashara yako. 

    Tatu, unapaswa kuhakikisha kwamba unafanya kazi zako kuajiriwa kwa nguvu na weredi mkubwa. Usifanye kazi ya ajira hovyo, muda wa kazi ya ajira utumie kuifanya.

    Nne, fahamu unapoamua kuanzisha biashara ukiwa umeajiriwa unapaswa kujitoa sana. Inahitaji ujitoe na upate muda wa kufanya kazi yako ya ajira na biashara yako. Nyakati nyingine utakuwa umechoka ila UTAPASWA kujilazimiaha. Utajikosesha raha na starehe nyingi ulizokuwa unapata. Hayo yote kwa ajili ya biashara yako.

    Muhimu sana katika kuifanya biashara yako isijulikane ni kutoanzisha biashara ambayo utakuwa unaifanyia ofisini kwa bosi wako; kama kuuza vitu kwa wafanyakazi wenzako. Ikiwezekana, hata wafanyakazi wenzako wasijue kuwa umeanzisha biashara maana wanaweza kuwa watu wa kwanza kukuchongea. Unaweza kuanzisha biashara mbali kidogo na ajira yako ilipo, ila unapoweza kufika kwa haraka.

    Kila la kheri

X